Showing posts with label HUFFINGTON POST. Show all posts
Showing posts with label HUFFINGTON POST. Show all posts

18 Sept 2008









Picha ya hapo juu inafurahisha.Ndio namna jamaa wa The Huffington Post wanavyo-summarize masahibu yanayomkumba John McCain.Kwa mujibu wa Gallup polls,Barack Obama amefanikiwa kumwengua McCain kwenye kura za maoni ikiwa ni mara ya kwanza tangu mgombea huyo wa Republicans apande chati kufuatia convention ya chama hicho hivi karibuni.Zaidi,angalia video hii hapa chini


11 Mar 2008























Kufuatia Gavana wa New York,Elliot Spitzer,au "Client 9", kukumbwa na skandali la kujihusisha na makahaba,The Huffington Post wametoa wanachokiita (kwa tafsiri yangu) Mwongozo wa Kutumia Huduma ya Makahaba (Prostitution:A User's Manual).Soma Mwongozo huo HAPA (you never know when it might become handy!)

7 Jan 2008


Kuna mengi yanasemwa kuhusu mwelekeo mzuri wa Barack Obama katika harakati zake za kuingia Ikulu ya Marekani baadaye mwaka huu.Lakini,je mafanikio ya Obama yanamaanisha kukubalika kwa asilimia 100 kwa mtu mweusi katika jamii ya Waamerika au ni matokeo ya kukwepa kile "weusi wenzie" kama Jesse Jackson na Al Sharpton wamekuwa wakikipigia kelele?
Nimekutana na makala hii katika toleo la leo la gazeti la Guardian la hapa Uingereza na nimeona ni vema nikakupa nafasi msomaji mpendwa wa blogu hii nafasi ya kuisoma na kutoa hukumu yako wewe mwenyewe.

Binafsi napenda kumuona mtu mweusi (au hata half-caste) akiwa White House,na kwa maana hiyo ingependeza endapo Januari mwakani Bush angempokea Obama kama "mkazi mpya" katika jumba hilo maarufu hapo 1600 Pennsylvania Avenue NW.Lakini sioni dalili ya hilo kutokea.Na kumbe siko peke yangu mwenye mtazamo wa namna hiyo.Naendelea kuamini kuwa White America bado haiko tayari kumuona mtu mweusi akiwa Rais wa Taifa hilo.Na pengine ndio sababu muhimu ya Republicans "kusherehekea" mafanikio ya Obama (wahenga wanatuonya kwamba ukiona adui yako anasherehekea ushindi wako basi ujue ushindi huo utamnufaisha).Wana sababu kuu mbili,moja,wanafahamu ugumu wa kumzuia Hillary Clinton kuingia Ikulu,na pili,wanafahamu wepesi wa kumwangusha Obama pindi akipitishwa kuwa mgombea wa Democrats.Niite prophet of doom lakini amin nakuambia,pindi Obama akishinda kuwa mgombea,basi shehena zote za White America za kumbomoa mwanasiasa zitaelekezwa kwake.Na atakuwa target rahisi kwao:watapigia mstari jina lake la kati la Hussein na kulikuza utadhani linamaanisha ugaidi (baadhi yao walishajifanya kuteleza ulimi na kumwita Barack Osama),watakumbushia confession yake kwamba zamani hizo alishawahi kubwia unga na kuvuta bangi.Anyway,ndani ya The Huffington Post kuna makala inayoelekea kurandana na mtizamo wangu kuhusu Obama.

Ukimaliza kusoma jipoze na clip hii ya Common featuring Dwelle iendayo kwa jina The People

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.