Showing posts with label JOHN TENDWA. Show all posts
Showing posts with label JOHN TENDWA. Show all posts

4 Sept 2010

Kwa mujibu wa blogu ya Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua (mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo),Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alionekana Ikulu siku ya Alhamisi majira ya saa 9 alasiri ambapo inaelezwa alikutana na Rais Jakaya Kikwete,mgombea wa CCM ambaye amelalamikiwa na Chadema kwa kukiuka Sheria y Gharama za Uchaguzi.Awali,Tendwa alisema kuwa angetoa "hukumu" keshokutwa (Jumatatu).

Kwa hakika,haihitaji utaalam wowote kuhusisha tukio hilo (la Tendwa kukutana na Kikwete) na pingamiz la Chadema.Na haihitaji ujuzi wa sheria kubashiri matokeo ya "hakimu kukutana faragha na mshtakiwa" siku chache kabla ya hukumu.

Wengi wetu tunafahamu Tendwa atasema nini hiyo Jumatatu.Most likely,ameshafanya maamuzi ila kinachoshughulikiwa sasa ni usanii wa lugha ya utoaji wa maamuzi hayo.Na ni katika hilo ndio maana inamlazimu awasiliane na JK ili "ajenge mazingira ya hukumu ya haki".Katika mazingira tuliyonayo ambapo Msajili wa vyama vya siasa ni kama kibaraka wa CCM,haiwezekani kabisa kiongozi huyo kutoa maamuzi ya haki yatakayokiathiri chama hicho.

Na dalili za "usanii" zimeonekana tangu Chadema wawasilishe malalamiko yao.Hivi Tendwa anaweza kuwaambia Watanzania kwanini imchukue takriban wiki nzima kutoa maamuzi kuhusu malalamiko ya Chadema?Je hiyo pekee sio dalili ya uzembe na kutowajibika ipasavyo?Awali aliwaeleza waandishi wa habari kuwa angetoa maamuzi Jumatatu lakini hakueleza kwanini itachukua muda wote huo kutoa maamuzi hayo muhimu kwa mustakabali wa demokrasia nchini mwetu.Jibu jepesi ni kwamba hana ubavu wa kutoa maamuzi kabla ya kupata ridhaa ya CCM.Na kwa vile CCM ndio watuhumiwa,ni dhahiri maamuzi ya Tendwa yataelemea kuipendelea CCM.

Nafahamu kuna wataosema "aah,sasa kelele za nini wakati maamuzi hayajatolewa?" Wana haki ya kusema hivyo lakini wanapaswa pia kutambua vema mapungufu ya Katiba yetu yanayomfanya mgombea wa chama tawala kuwa na advantage kubwa dhidi ya wagombea wengine kutokana na ukweli kwamba Katiba inampa rais nguvu kubwa mno.

Kikwete ameendelea kupuuza malalamiko ya Chadema kwa kuzidi kutoa rushwa ya ahadi katika mikutano yake ya kampeni.Sote tumemsikia akiwazuga wapigakura huko Mbagala kuhusu daraja la Kigamboni na ahadi nyingine hewa ya huduma ya uhakika kwa maji jijini Dar es Salaam.Huyu mtu hana aibu kwa sababu ahadi anazotoa sasa zinatoa picha ya mgombea anayeomba idhini ya kuingia madarakani kwa mara ya kwanza na sio aliyekuwa rais wetu kwa miaka mitano iliyopita.Kama tangu 2005 hadi leo ameshindwa kuwezesha ujenzi wa daraja hilo la Kigamboni,kwanini tumwamini kuwa ataweza katika mhula wake wa mwisho (2010-2015) hasa ikizingatiwa kuwa kipindi hicho cha pili kitatumika zaidi kwa yeye kujitengenezea mazingira ya "kustaafu kwa amani"?

Jeuri ya Kikwete inasababishwa na ufahamu kuwa Chadema,na vyama vingine vya upinzani,havina mahala pa kukimbilia pindi wasiporidhishwa na mwenendo wa kampeni za Kikwete na CCM kwa ujumla.Anafahamu kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Mahakama na taasisi nyingine za kusimamia uchaguzi na sheria nza nchi kwa ujumla,ziko mikononi mwa CCM.Hata hivyo,wapinzani hawapaswi kukata tamaa kwa vile nchi yetu kama masikini wa kutupwa inategemea sana misaada ya wafadhili.Japo kuwapigia magoti wafadhili kunaweza kutafsiriwa kama "kuegemea kwenye ukoloni" lakini tufanyeje kama nchi yetu inaendeshwa kiholela.Binafsi,nina matumaini makubwa kuwa nchi wafadhili zinafuatilia kwa karibu mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa nchini na hazitasita kuchukua hatua mwafaka pale CCM itakapotumia ubabe wake kulazimisha ushindi.

Hata hivyo,wakati we keep on hoping for the best and expecting the worst,Tendwa afahamu kuwa he wont get away with this issue as easily as he might think.Blogu hii inaamini kuwa Chadema ni chama makini na chenye rekodi nzuri ya ufuatiliaji mambo.Ni katika mantiki hiyo basi blogu hii inatarajia kuwa Chadema hawatamruhusu Tendwa kufanya uhuni wa aina yoyote ile katika maamuzi yake.Ni heri uchaguzi uvurugike lakini haki ipatikane.Kutoa fursa ya sheria za nchi kupindishwa kwa namna watawala wanavyotaka ni hatari sana hasa tukizingatia ulevi wa madaraka unaowakabili viongozi wengi wa "dunia ya tatu".

Kama alivyoandika Ngurumo katika blogu yake,nami narejea kumkumbusha Tendwa kuwa HATUDANGANYIKI!

18 May 2010

Ofkoz,Mtukufu Rais Jakaya Kikwete alikuwa anatania alipotetea rushwa hadharani kwa kudai takrima haikwepeki.Ndio,Rais alikuwa anatania,na ndo maana,Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa amekaririwa na magazeti kadhaa akimtetea JK kuwa "kauli yake (JK) kuhusu takrima (rushwa) ilikuwa utani tu".Pengine neno 'utani' kwa mujibu Tendwa linaweza kuwa na maana kubwa zaidi tukilitafsiri katika informal English.Kwenye kamusi,'joke' (informal) inamaanisha An object of amusement or laughter; a laughingstock.Kwa Kiswahili,ni 'kituko', 'kioja' au 'kitu cha kuchekwa'.

Lakini kwa namna siasa zetu zilizvyojaa vituko (jokes) si ajabu Tendwa alikuwa serious kumtetea bosi wake JK.Na inawezekana kabisa Msajili huyo wa Vyma vya Siasa anayepaswa kufanya kazi bila upendeleo anaamini kwa dhati kuwa rais wetu alikuwa anataniana tu na viongozi wa dini.Kama ni hivyo,basi nae ni kituko pia.Haiingii akilini kwa kiongozi wa nchi kukutana na watu muhimu katika jamii yetu (viongozi wa dini) na kufanya 'utani mbaya' kama huo.Kulikuwa na umuhimu gani basi wa rais kuhudhuria mkutano huo kama lengo lilikuwa kutoa utani tu?Si angeweza kuwapigia simu kwa wakati wake kisha akawarushia utani huo!

Kwa bahati mbaya,au makusudi,'utani huo mbaya' ushaanza kusahaulika miongoni mwa Watanzania wengi.Siwezi kuwalaumu walalahoi ambao wako bize na kuhakikisha mkono unaenda kinywani,lakini nashindwa kujizuia kuwashangaa Watanzania wenzetu walio katika 'tabaka la kati' (middle class) kwa kuweka umuhimu zaidi kwenye ishu kama tuzo za Kili,ujio wa Sean Kingston,'kujirusha',nk ilhali tabaka la chini linalohitaji sapoti yao likizidi kuangamia.Wengi wa walio katika tabaka la kati wako bize zaidi 'kuishi kama tabaka tawala' (hata kama hiyo itamaanisha wakope kwa ndugu na marafiki au wajihusishe na ufisadi) kuliko kupambana na 'tabaka tawala' (tabaka la juu) 'kusawazisha uwanja' (to level the ground) kwa minajili ya kujenga jamii yenye kukaribia usawa.


Sijui tunaelekea wapi,lakini lililo bayana ni kwamba hatma ya taifa letu iko mashakani.Ukiona mkuu wa nchi anaongea pasi hofu (na kicheko juu,kama kawaida yake) kuwa takrima (ambayo ni jina la kistaarab la rushwa) haikwepeki.Tafsiri pana ya kauli hiyo ya 'Chaguo la Mungu' ni mithili ya kuhalalisha uhalifu kwa vile rushwa ni kosa la jinai.Lakini binafsi sishangazwi sana na kauli hiyo ya 'mwenye nchi' kwa vile alishawahi kutamka bayana kuwa 'anajali haki za binadamu za mafisadi' alipohutubia Bunge Agosti mwaka 2008



Kusoma habari kamili kuhusu utetezi wa Tendwa kwa Kikwete BONYEZA HAPA na HAPA.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.