Showing posts with label KANYE WEST. Show all posts
Showing posts with label KANYE WEST. Show all posts

26 Feb 2012


Kwa Waafrika wengi,na pengine kwingineko ulimwenguni,Wanigeria wanatamba kwa sifa kuu mbili;moja mbaya  na nyingine nzuri.Mbaya ni tabia yao ya utapeli ambapo ni bora kulala na chatu mwinye njaa kuliko kumwamini Mpopo.Wenye uzoefu nao wanajua ninamaanisha nini.Sifa yao nzuri-hasa kwa wanaume ni kutamba katika soka takriban kila kona ya dunia.Inayoambatana na hiyo ni mfaniko makubwa waliyonayo wengi wao-hasa nje ya nchi (usiulize wameyapataje).

Katika hili la mafanikio,juzi juzi tu tumesikia wanamuziki kadhaa wa Kipopo wakivamia anga za muziki nchini Marekani ambapo tayari majina makubwa kama Snoop Dogg na Akon wameshafanya kazi nao.D'Banj kwa sasa anafanya kazi kwenye lebo ya G.O.O.D Music ya Kanye West



Kwa upande mwingine,wanamuziki maarufu wa Kinigeria P.Square, 2Face Idibia na Whizkid wamesaini kwenye lebo ya Konvict ya Akon.



Na wiki hii,gazeti maarufu la nchini Marekani la New York Times lina makala ndefu kuhusu kiwanda cha filamu za Nigeria kinachojulikana kama Nollywood.Unaweza kusoma makala hiyo ndefu HAPA.

Maendeleo haya ya wasanii wa kipopo yanaweza kuwa changamoto kubwa kwa wasanii wetu huko nyumbani.Japo kuna dalili kidogo za kutia matumaini baada ya wasanii AY na Jay Mo kushirikiana na wasanii wa kimataifa,kimsingi wengi wa wasanii wetu wanaendelea kutafsiri mafanikio kwa kigezo cha umaarufu ndani ya Tanzania (na kidogo kwa Afika Mashariki) na kuendekeza zaidi shoo za hapa na pale.




14 Nov 2008


Kanye West’s famous temper is under the spotlight again after Northumberland police arrested the hip-hop heavyweight on suspicion of assault in the early hours of this morning.

The 31-year-old rapper and producer, currently touring the UK, reportedly attacked a paparazzi photographer as he left Newcastle nightclub Tup Tup Palace.

Terry Blackburn alleges he suffered a cut face and bruising after the chart-topper pushed his camera into his face and shouted: “Get the f***ing camera off him!”

A Northumberland police spokesman told Times Online: “We arrested a 31-year-old man on suspicion of assault.

“He was released without charge and there will be no further police action taken.”

It is the second time in as many months that the rapper has been taken into custody after clashes with the paparazzi.

In September, West was arrested at Los Angeles International Airport after allegedly smashing a photographer’s camera. Part of the incident was caught on video by another member of the press and showed the rapper throwing a piece of camera equipment to the ground.

He became known for his quick temper in 2006 when he failed to win the best video gong at the MTV Europe Music Awards. West took to the stage and ranted to the audience that he should have won.

But this year, after winning the Ultimate Urban Award, he publicly criticised the awards again, accusing organisers of giving him the prize because he attended the ceremony. The rapper said it should have gone to Lil Wayne.

West has impressed fans and garnered critical praise for his high-tech Glow In The Dark tour, which features a moving stage, explosions and even waterfalls. But earlier this week, the rapper said he was struggling with life in the spotlight and grief over the first anniversary of his mother's death. Donda West died suddenly last year following cosmetic surgery.

"I'm just going through balancing that. And I always used to have that support system, you know. My mom would be there; no matter what, she was there before everything."

"We were together for like 30 years. And you know now when I'm on that stage and I look out and I say, 'What am I going to do with the rest of my life?' Like when does a real life start?' Because I have sacrificed real life to be a celebrity and to give this art to people, which is great. It is great that I was able to do that, I'm not trying to shun that in any way, but it's definitely a Catch-22 and it's bittersweet."

A wave of sympathy followed, but a few days later he came in for ridicule after claiming to be the voice of his generation.

West declared: “I realise that my place and position in history is that I will go down as the voice of this generation, of this decade, I will be the loudest voice."

ANYWAY,BELOW ARE SOME OF KANYE'S GREATS HITS (I SAID SOME COZ SEEMS LIKE ALL OF HIS HITS ARE GREAT)




11 Sept 2008

Sidhani kama kuna ubishi kwamba Kanye West ana kipaji cha hali ya juu katika muziki,both as a rapper and a producer.Sasa sijui ni yale ya mgema akisifiwa tembo hulitia maji au ni matokeo ya ile ajali ambayo almanusura ichukue uhai wake,lakini something is wrong with Kanye.Hebu angalia HAPA kasheshe aliyoizua leo huko Los Angeles Airport.

Hapa chini kuna kazi mbili za msanii huyo.Ya kwanza ni wimbo wake mwenyewe wa Through The Wire na ya pili ya ni production yake kwa The Game katika wimbo Dreams.




23 Jan 2008

Rafiki yangu mmoja amenitumia barua-pepe muda mfupi uliopita baada ya kusoma makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Hakuwa na pongezi wala malalamiko bali alidai kwamba wakati anasoma makala hiyo alijiskia kama anaongea nami uso kwa uso japo tuko umbali wa maili elfu kadhaa.Ni kweli,napoandika makala huwa najitahidi kadri ya uwezo wangu kuiwasilishalisha kwa kutumia staili ya mazungumzo (conversational style).Lakini sio mazungumzo kama ndani ya semina-elekezi,warsha,kongamano au semina bali yale yanayoweza kuwa yanafanyika mahala ambapo "tunaongea kwa kijinafasi" (comfortably).

Tukiachana na hilo,makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inagusia michuano ya soka ya Mataifa ya Afrika huko Ghana,na kuielezea kwamba ni moja ya habari njema chache kutoka bara hilo,hasa kwa vile kwa takriban mwezi sasa habari zinazotawala kutoka huko ni kuhusu vurugu zinazoendelea Kenya zilizotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo.Kwa kutumia mfano hai,makala hii pia inaelezea ugumu anaoweza kukabiliwa nao Mtanzania pindi akidadisiwa chanzo cha umasikini wa nchi yetu,kabla ya kuwachambua mafisadi wa fedha na wale wa mawazo.Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule katika jarida hilo la Raia Mwema,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

Ukimaliza kusoma makala hiyo,unaweza kuangalia clips hizi za versions mbili za Jesus Walks ya Kanye West.Naamini nasi tunahitaji nguvu za kiroho kukomesha ufisadi huko nyumbani.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.