Showing posts with label Michezo na Burudani. Show all posts
Showing posts with label Michezo na Burudani. Show all posts

6 Feb 2015

 YAMOTO BAND  COMFIRMED will performing all their major hits including NITAJUTA, NISEME, WAMBEA, NITAKUPWELEPWETA and many more @ The Royal Regency Banquet Hall, Sat 21 Feb 2015 From 8pm to 3:30am, there are limited VIP Tables available book yours now for ultimate VIP treatment or individual place your booking early to avoid disappointment. Table bookings please call 07405824696/ WhatsApp +447557304940
[email protected] or [email protected]
Ukumbi wa Royal Regency ndio sehemu pekee ambayo utawaona YAMOTO BAND kwenye jiji la LONDON usiku wa 21. Feb 2015

Usiku wa tarehe 21 February 2015 The Royal Regency patakuwa hapatoshi. Kwa kuondosha usumbufu wahi ticket yako mapema
 Kiingilio ni:
£25 kwa Ticket ya kawaida
£35 kwa VIP ticket
Kama Unahitaji VIP table for 10 people piga simu 07405824696 kwa maelezo zaidi au tuma email kwenda: [email protected] or [email protected]
YAMOTO BAND will be alongside supported artist such as Sultan King, OJ, Hyper hype And many more,why wait grab your ticket Now!!!! 
HOT LINE FOR TICKET 07853482158/07557304940

-- Regards, Jestina George 
Mobile +44 7557 304 940
website: www.jestina-george.com

4 Nov 2014

15 Oct 2014

Chris Brown is sharing his thoughts about Ebola. (Getty Images)
Dunia yetu imesheheni watu wanaoitwa 'conspiracy theorists,' Sina uhakika wa tasiri ya kiswahili ya neno hilo, lakini nadhani neno la karibu ni 'wazushi.' Hata hivyo, tofauti ya wazushi tuliowazowea ambao mara nyingi huzusha jambo kwa minajili ya kuzusha tu, kwa conspiracy theorist uzushi wao huambatana na 'ushahidi wa kimazingira,' japo si ajabu ushahidi huo nao kuelemea zaidi kwenye uzushi kuliko facts.

Sasa msanii maarufu wa Marekani, Chris Brown, nae ameingia katika kundi la conspiracy theorists baada ya kudai kuwa ugonjwa hatari wa Ebla ni moja ya mbinu za kudhibiti idadi ya watu duniani.

Msanii huyo ali-post mtizamo wake huo kwenye ukurasa wake wa Twitter, ambapo ana 'wafuasi' (followers) milioni 13.7. Hata hivyo, baadhi yao walipingana nae waziwazi

"Wajua mjadala kuhusu ugonjwa wa Ebola ulichokuwa unahitaji? Upuuzi zaidi. Hapa anaingia Chris Brown..." aliandika mmoja wa wafuasi wake.

"Chris Brwon anadai Ebola ni moja ya mbinu za kudhibiti idadi ya watu. Ajaribu ugonjwa." alitwiti mwingine  huo  akimaanisha msanii huyo ni miongoni mwa watu wanaohitaji kudhibitiwa.

"Chris Brown anadai kuwa Ebola ni njia ya kudhibiti widadi ya watu. Kwa hakika hiyo si kweli, na laiti ingekuwa kweli basi tungempa ugonjwa huo yeye kwanza," aliandika mwingine.

Brown ambaye hivi karibuni alitumikia kifungo cha siku 108 jela kwa kukiuka taratibu za uangalizi wa kimahakama (probation) kufuatia kosa la kumpiga mpenzi wake wa zamani, msanii Rihanna, baadaye alionekana kutafakari upya kauli yake, na kutanabaisha kuwa 'anafunga mdomo wake,' japo si kwa maneno ya kistaarabu.

Lakini muda mfupi baadae 'alipandisha mzuka' na kuwashambulia waliopingana na mtizamo wake huo, na kutwiti maneno makali: "naandika ninachotaka. Kama hutaki nyonya %$*£$ yangu (tusi)

Hata hivyo, licha ya baadhi ya watu kupingana na conspiracy theory hiyo ya msanii huyo, watu kadhaa katika mtandao huo wa Twitter walionekana kuafikiana nae kwa tweet hiyo kupata takriban  'Retweets' 30,000 na 'Favourites' 22,000.

Mlipuko wa ugonjwa wa Ebola umeshasababisha vifo zaidi ya 4000 huku Afrika ya Magharibi ikiwa ni eneo lililoathirika vibaya zaidi japo tayari kuna wagonjwa wachache waliokumbwa na maradhi hayo huko Hispania na Marekani.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka mtandaoni



24 Aug 2014

Leaving: Brown is seen walking to his Lamborghini after the drama at 1Oak in Los Angeles
Chris Brown akielekea kwenye Lamborghini lake kuondoka katika klabu ya usiku palipotokea shambulio la risasi
Prodyuza Marion Suge Knight (pichani chini) amejeruhiwa kwa risasi amejeruhiwa kwa risasi katika shambuli lililotokea katika pati iliyokuwa ikiendeshwa na msanii Chris Brown.
Music producer Suge Knight has been injured during a shooting at an awards show party at a Los Angeles nightclub hosted by singer Chris Brown, it has been reported
Mashuhuda wanaeleza kuwa msanii huyo ambaye bado yupo katika msamaha wa uchungu (parole) baada ya kutoka jela hivi karibuni ndiye alikuwa mlengwa wa shambulio hilo, ambapo alikuwa MC wa pati ya utangulizi wa Tuzo za Video za Muziki (MVA) zitakazofanyika leo usiku (kwa saa za Marekani).
OK now: Brown smiled as he left the nightclub where he was reportedly targeted by a gunman
Inadhaniwa kuwa Chris hakuumia katika shambulio hilo, lakini watu wengine watatu, akiwemo Suge Knight, mwanzilishi wa lebo ya muziki ya Death Row Records iliyokuwa ikitumiwa na msanii mwingine maarufu wa nchi hiyo, Marehemu Tupac Shakur, walijeruhiwa na kupelekwa hospitali ya Cedar's Sinai. Inaelezwa kuwa mmoja wa majeruhi hao yupo taabani.
Witnesses: Partygoers talk to emergency personnel after the shooting 
Mwanamitindo na mcheza filamu Tyson Beckford na memba wa kundi la Black Eyees Peas Apple De Ap walikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, na walieleza kuwa walisikia sauti nne za risasi mida ya saa 7.30 alfajiri ya kuamkia leo.
Treatment: Another victim is fitted with a neck brace following the dramatic shooting
Majeruhi akitibiwa
Suge Knight ambaye kwa sasa anamiliki kampuni ya muziki ya Black Kapital Records alionekana na polisi  nje ya ukumbi baada ya shambulio hilo na akachukuliwa katika gari la kubeba wagonjwa. Inaelezwa kuwa alipigwa risasi mbili, na kujeruhiwa tumboni na mkononi na sasa anafanyiwa upasuaji.
Host: Brown enjoys the party before the alleged shooting took place
Chris Brown 'akijirusha' kabla ya shambulio
Waliofanya shambulio hilo walikamatwa na polisi ambao sasa wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Mastaa wengine waliokuwa kwenye pati hiyo ni pamoja na Justin Beiber na rapa The Game.
Guests: Justin Bieber (right) was among the guests at the VMA Pre-Party hosted by  Brown
Justin Beiber alikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, kama ilivyokuwa kwa rapa The Game (pichani chini)

Jayceon Terrell Taylor, aka The Game attends a VMA Pre-Party hosted by Chris Brown and Pia Mia
Iliposikika milio ya risasi hizo, Chris Brown alionekana akiruka kuelekea kwenye eneo la baa katika klabu hiyo ya usiku (nightclub), huku kwa hasira akiwaagiza watu wengine kujikinga.
Aftermath: Brown jumped on a table after the shooting, apparently furious at what had taken place
Chrsi Brown akiruka kuelekea eneo la baa baada ya milio ya risasi
Saa 12 kasorobo asubuhi ya leo, msanii huyo alitwiti


Akimaanisha 'Jamii haiwezi kustarehe au kuburudika pasipo mikwaruzo.'
Injured: Another victim is transferred into an ambulance in a stretcher
Majeruhi wakiingizwa kwenye gari la kubebea wagonjwa
Angry: Brown at first appeared to still be furious when he made his way from the West Hollywood club
Chris Brown akiwa ametahayari baada ya shambulio hilo



CHANZO : The Mail Online




9 Aug 2014

Klabu Bingwa ya Soka hapa Scotland, imepewa ushindi wa bure katika hatua ya awali kuelekea michuano ya soka Ligi ya Mabingwa (Champions League) barani Ulaya, licha ya kutwangwa bao 6-1 na Legia Warsaw ya Poland.

Celtic walifungwa mabao 4-1 katika mechi ya kwanza iliyofanyika Warsaw, Poland, kabla ya kupewa kipigo kingine cha mabao 2-0 katika mchezo wa marudiano uliofanyika Edinburgh hapa Scotland.

Hata hivyo, timu hiyo ya Poland imeadhibiwa na Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA) kwa kunyang'anywa ushindi na kutolewa mashindanoni kwa kuchezesha mchezaji asiyestahili, na badala yake Celtic wamepewa ushindi wa mabo 3-0, na sasa watachuana na Maribor ya Slovenia.

Hii ni mara ya pili kwa mabingwa hao wa Scotland kuangukiwa na bahati kama hiyo. Mwaka 2011, timu hiyo ilirejeshwa katika Ligi ya Europa licha ya kutolewa kwa mabao 3-1 na timu ya Sion ya Uswisi. Kama ilivyotokea hivi, sasa, kosa la Sion lilikuwa kuchezesha wachezaji wasiostahili

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.