Showing posts with label PRO-UFISADI ALLIANCE. Show all posts
Showing posts with label PRO-UFISADI ALLIANCE. Show all posts

2 Jun 2010

Kwa mujibu wa imani zetu za Kiswahili,aliyekuroga akifariki basi uwezekano wa kupona nao unakuwa kama umefariki.Na msemo huu unaonekana kurandana na hali halisi ya baadhi ya matendo yetu viumbe tunaojulikana kama Watanzania.Nafahamu kuwa si wote "tuliorogwa" lakini hiyo si sababu ya "kutowatolea macho" wenzetu "waliorogwa kisha aliyewaroga akafariki".

Mwishoni mwa wiki hii,timu yetu ya taifa inakabiliwa na mpambano muhimu dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda katika kusaka nafasi ya kushiriki kwenye michuano ya CHAN.Taifa Stars inatarajiwa kucheza siku ya Jumapili kisha Jumatatu wanatarajiwa kuingia tena uwanjani kupambana na timu ya Taifa ya Brazil katika pambano lililonunuliwa kwa mamilioni ya dola na chama chetu cha soka.

Na kwa takriban wiki nzima sasa,uongozi wa FA umekuwa bize zaidi na maandalizi ya pambano hilo walilonunua kuliko kuelekeza akili zao kwa mpambano dhidi ya Rwanda.Japo natambua kuwa kila mpenzi wa soka duniani angependa kuiona Brazil ikicheza uwanjani lakini sio kwa kununua mechi ya mamilioni ya fedha ambazo hakuna uhakika kama zitarudi.FA hawajaweka bayana gharama za kununua mechi hiyo lakini taarifa zinasema wamelipa dola za kimarekani milioni mbili unusu  (zaidi ya shilingi bilioni 3 unusu).Na hiyo ni ada (fee) tu lakini kuna uwezekano wa kiwango hicho kuwa kikubwa zaidi tukichanganya na gharama za kumudu ziara hiyo.

Kuna hoja kuwa ziara hiyo itasaidia kutangaza utalii.Well,lakini tuwe wakweli,yaani kutangaza utalii kwa dakika tisini kwa gharama ya shilingi bilioni tatu!?Na kama tujuavyo tatizo sugu la wizi wa mapato kuanzia TRA hadi kwa watendaji ngazi ya kata,si ajabu muda huu mafisadi wameshapiga mahesabu ya pasenti ngapi watakwiba kwenye chochote kitakachpatikana kwenye mechi hiyo.

Na kuna hoja ya rankings za FIFA.Hivi mechi moja ya kununua kwa mabilioni itatupandisha kwa kiwango gani ukilinganisha na menchi dhidi ya Rwanda ambayo kama "tukikaza misuli" na kufanikiwa kucheza CHAN tutapata nafasi kubwa zaidi ya kupandisha ranking yetu huko FIFA?

Ukitaka kufahamu namna ubabaishaji na ufisadi unavyozidi kutafuna mfumo wa jamii yetu subiri mechi iishe kisha vianze visingizio vya namna FA walivyoshindwa kufikia lengo la mapato.Binafsi nisingekuwa na tatizo laiti FA wangeafikiana na wenzao wa Brazil kisha kuuza tiketi kabla ya mechi na hivyo kufahamu faida au hasara itakayopatikana.Lakini kwa hali yasasa ni sawa na kucheza bahati nasibu.Na si ajabu visingizio vimeshaandaliwa as to kwanini "mechi hiyo haikuweza kurejesha faida iliyotarajiwa".

Ndio maana nashawishika kusema kuwa inawezekana ALIYETUROGA KESHAFARIKI.

28 Mar 2010


Kwa mara nyingine,baadhi ya Watanzania waishio Uingereza walipata nafasi ya kuhudhuria mkutano uliobeba jina la Diaspora Forum 2.Binafsi sikuhudhuria,sio kwa vile sikuona umuhimu wa kufanya hivyo bali nilitingwa na majukumu binafsi.Hata hivyo,laiti ningehudhuria ningejaribu kutoa mchango wa kwanini uhamasishaji kwa Watanzania walio nje kurejea nyumbani au kuchangia maendeleo ya taifa unaweza kuendelea milele pasipo kupatikana mafanikio yanayokusudiwa. Pamoja na nia nzuri ya kuwepo forums kama hiyo ya Diaspora,lakini ni muhimu kutambua kuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu kama taifa hakijawahi kuwa kwenye mipango mizuri.Tanzania tumebahatika kuwa na viongozi wenye uwezo wa hali ya juu katika kuongea na kubuni mipango mizuri.Lakini,kwa bahati mbaya au makusudi,wengi wa viongozi hao ni wazembe wa daraja la kwanza linapokuja suala la utekelezaji mipango including waliyoibuni wao wenyewe.Unajua kuna tofauti kati ya uzembe katika kutekeleza mawazo ya mwenzako na uzembe katika kutekeleza mawazo yako binafsi.Kwa mfano,hakuna mtu aliyeishauri CCM kuja na kauli-mbiu ya "ARI MPYA,KASI MPYA NA NGUVU MPYA" au ile ya "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA".Uamuzi wa kuja na kauli-mbiu hiyo ulikuwa wa CCM binafsi pasipo shinikizo kutoka kwa wafadhili,viongozi wa dini,wananchi au kikundi chochote kile.Nafahamu wapo watakaobisha kuwa kauli-mbiu zote hizo zimeishia kuwa kauli-mbiu tu pasipo matokeo kuonekana,lakini ukweli ndio huo,na shurti uwekwe wazi.

Back to the Diaspora thing.Kwanza,katika mazingira ya kawaida,haihitajiki kumhamasisha mwananchi kurudi nyumbani kwake au kuchangia maendeleo ya alikotoka.Wengi wa Watanzania walioko ughaibuni hawahamasishwi kusaidia ndugu na jamaa zao walio Tanzania bali wanafanya hivyo kwa vile wanatambua kuwa ni wajibu wao.Naamini kuwa wengi wa wanaokumbuka ndugu na jamaa nyumbani wanasukumwa zaidi na namna misaada yao inavyosaidia walengwa huko nyumbani.Sidhani kama kuna mtu ambaye kila wiki au mwezi anakwenda Western Union,Moneygram au "Kwa Wapemba" kutuma pauni zake alizopata "kwa mbinde" only for watumiwa huko Tanzania kuendeleza libeneke la anasa.

Ninajaribu kutumia mfano wa ndugu na jamaa kama mahala pa kuanzia kabla ya kuangalia namna Watanzania walio nje wanavyoweza kufanya the same kwa nchi yao.Kwa bahati mbaya,forums kama Diapora 2 hazitoi sura ya pili ya hali ilivyo huko nyumbani.I wish miongoni mwa waalikwa wangekuwa taasisi zinazohamasisha Watanzania walio nje kuchangia kuleta mabadiliko ya haraka kwenye mwendendo na hatma ya taifa letu.Yah,Diaspora forums zinaweza kuhamasisha Watanzania wote walio ughaibuni kurejea nyumbani au kuchangia asilimia kadhaa ya vipato vya kujenga taifa letu "changa" (sijui lini litakua),lakini kwa hali ilivyo sasa,watakaoendelea kunufaika ni wateule wachache wafahamikao kama MAFISADI.

Na tatizo jingine linalotukabili Watanzania wengi ni usikivu uliotukuka pasipo udadisi.I hoped mshiriki mmoja angemuuliza Waziri Membe kuhusu commitment ya watwala wetu katika kupambana na ufisadi underlining mifano kama dilly-dallying za kuwachukulia hatua majambazi wa Kagoda au hili skandali jipya la trilioni za stimulus package ambapo tunaambiwa kuwa mafisadi came up with some phony companies to create another EPA-like swindle.

Binafsi napenda kuamini kuwa moja ya negative legacy za itikadi ya Ujamaa ni kwa wananchi kupenda kunyenyekea viongozi "kikasuku".Utaona wananchi wakihangaika kupata nafasi za kupiga picha na kiongozi badala ya kumkalia kooni kumuuliza kwanini mamabo yanaenda mrama.Unadhani laiti Mugabe au Waziri wake akija UK na kukutana na Wazimbabwe waishio hapa "patatosha"?And I don't mean kufanyiwa vurugu bali kubanwa na mwaswali ya msingi kwanini mambo yanakwenda mrama.Lakini kwa akina sie,mdau akishapata picha na kigogo kisha akaipenyeza bloguni basi anakuwa ame-achive lengo kubwa kabisa.

Naamini,hata kama ntapingwa,kuwa Watanzania walio nchi zinazojitahidi kuwatumikia wananchi kwa namna inavyostahili (kama hapa Uingereza,though it couldn't always be absolutely perfect) hawawezi kukwepa lawama za michango yao hafifu katika kuboresha hali ilivyo huko nyumbani.Siamini kama ni ubinafsi au imani kwamba "hata tukisema haitobadilisha kitu" bali ni kasumba ileile inayokwaza mabadiliko huko nyumbani kwamba kwa namna ya miujiza,watu walewale wanaokwaza maendeleo yetu wataamua kwa hiari yao kubadilika na kisha kuutumikia umma kwa ufanisi.Hivi,kwa Watanzania walio Uingereza,hatuoni namna Labour wanavyobanwa mbavu katika jitihada zao za kurejea madarakani?Na si kwamba wame-perform vibaya kihivyo-compared to our CCM-lakini taxpayers wa Uingereza wanaamini kuwa good is not good enough,they want better if not the best from Labour.

Juzijuzi,Makamu Mwenyekiti wa CCM,Pius Msekwa,alifanya ziara hapa UK lakini akanusurika pasipo kubanwa na wana-CCM wenzake kwamba,kwa mfano,kwanini chama hicho kinashindwa kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi.Mimi si mmoja wa wanaobeza uanachama wa CCM nje ya nchi kwa vile natambua kuwa hiyo ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania.By the way,kuna Democrats Abroad na Republicans Abroad which are more or less the same as na matawi ya CCM nje ya nchi.Nadhani wanaopinga uanzishwaji wa matawi ya CCM nje ya nchi au unachama wa matawi hayo wanasukumwa zaidi na ukweli kwamba kuna madudu mengi yanayolelewa na CCM huko nyumbani.Sasa inatarajiwa kuwa wana-CCM walio nje ya nchi wakisaidie chama hicho tawala kutambua kuwa mwenendo wake unawaangusha Watanzania.Na wanatarajiwa kufanya hivyo kwa vile wana advantage ya ku-compare and contrast as to kwanini,kwa mfano,Labour inaweza lakini CCM inashindwa.Yaani,kama Labour inaweza kuwakalia kooni wabunge wake kwenye expenses scandal kwanini basi CCM ishindwe kumbana mtu kama Mzee wa Vijisenti ambaye hadi muda huu ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ndani ya chama hicho?

Nimaelizie kwa kupongeza waandaaji wa Diaspora Forums kwani naamini kuwa wanachofanya kina umuhimu mkubwa.Hata hivyo,umuhimu huo unakwamishwa na ukweli kwamba mazingira ya nchi yetu kwa sasa yanakwaza wengi wa Watanzania walio nje kuchangia jitihada za ujenzi wa taifa.Hakuna anayetaka kuona fedha anazochuma kwa mbinde zinaishia kunufaisha nyumba ndogo za mafisadi huko nyumbani au kuongeza idadi ya mahekalu yao.Diaspora forums zinaweza kufanywa hata kila baada ya wiki lakini hazitazaa matunda yanayokusudiwa-au kubaki photo ops tu-laiti mwenendo wa mambo huko nyumbani hautarekebishwa.

14 Aug 2009


Kingunge Ngombale Mwiru ni mkingwe,kiumri,kisiasa na kimadaraka.Japo umri si kigezo muhimu cha kuwa na busara,ukongwe katika fani flani unatarajiwa kuambatana na busara.Lakini hali si hivyo kwa Kingunge.Kuna nyakati baada ya kifo cha Nyerere baadhi ya watu walitarajia kuwa Kingunge angefanikiwa kuendeleza mema ya Mwalimu hasa kwa vile tuliaminishwa kwamba mwanasiasa huyu (Kingunge) ana damu ya Ujamaa kiasi cha kuachana na mambo ya imani ya kidini.Tuliambiwa dini ya Kingunge ni Ujamaa.

Pamoja na mapungufu ya hapa na pale,Nyerere anaendelea kukumbukwa kwa jitihada zake za kujenga jamii yenye kukaribia usawa na kuchukia unyonyaji.Sijui Kingunge akifa tutamkumbuka kwa lipi zaidi ya kuzeekea kwake kwenye siasa pasipo tija na hili jukumu jipya alilojipachika la u-Baba wa Taifa wa Mafisadi.Kingunge ni mnafiki mkubwa kwa vile wakati anadai kuwa viongozi wa kanisa "wangeufyata" laiti Mwalimu angekuwa hai,sijui yeye Kingunge angemwambia nini anaposimama kidete kutetea mafisadi.

Haya ndio madhara ya kuviacha vikongwe madarakani hadi vinapoteza uwezo wa kufikiri.Na huyu ni mshauri wa kiongozi wa nchi!Kama uwezo wake binafsi wa kufikiri umefikia kikomo atawezaje kumshauri mtu mwingine,achilia mbali kiongozi wa nchi?

Kwanini adai waraka wa kanisa utawagawa Watanzania lakini akae kimya pale chama chake cha CCM kilipocheza karata-tatu ya kisiasa kilipoahidi (katika manifesto yake ya uchaguzi 2005) uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa Waislam?Binafsi,sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya kadhi iwapo mambo flani muhimu yatazingatiwa,lakini kwa uendeshaji wa mambo kwa mtindo wa zima moto,au pata potea,ni dhahiri uamuzi huo wa mahakama ya kadhi unaweza kulipeleka pabaya taifa.Narudia,tatizo sio uanzishwaji au kuwepo kwa mahakama hiyo,bali ni ubabaishaji wa viongozi wetu katika kushughulikia uanzishwaji na uwepo wake pasipo kuathiri umoja wa kitaifa.

Na kikongwe huyu (Kingunge) mbona yuko kimya hadi leo baada ya chama chake kusuasua katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya uanzishwaji wa mahakama ya kadhi?Kama uamuzi wa CCM kutaja katika manifesto yake juu ya suala hilo ulikuwa hatari (kwa mujibu wa wanaodhani hivyo),kitendo cha chama hicho kurushiana mpira kila kinapoulizwa na waahidiwa (Waislam) kuhusu utekelezaji ni cha hatari zaidi.

Tatizo la Kingunge kuhusu waraka wa kanisa haliko kwenye kile anachodai "kuijua vizuri nchi yetu" bali wasiwasi wake kwamba pindi waraka huo ukitekelezwa kwa vitendo basi yeye na mafisadi anaowatetea watakuwa katika wakati mgumu.Kwa lugha nyingine,Kingunge anatetea maslahi ya tabaka alilomo na analoliwakilisha (mafisadi).

Hivi ni lini umewahi kumsikia Kingunge akikemea ufisadi?Hivi Kanisa lingetoa wapi wazo la kujana waraka huo laiti kikongwe hiki cha siasa kingesimama kidete kuendeleza harakati za Mwalimu kupambana na unyonyaji?Badala ya kutueleza yeye anafanya nini kuhakikisha nchi inakwenda vizuri anakimbil;ia kukosoa wengine kuwa wanataka kuipeleka nchi pabaya.

Halafu inakera zaidi kumskikia babu huyu akijifanya kama yeye ndio mwenye hatimili ya historia,mwelekeo na chochote kuhusu Tanzania.Eti anakemea wenzake "wanaodakia hoja pasipo kujua vema tumefikaje hapa..."Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya watu kama Kingunge,wanafiki waliojifika kwenye ngozi wa kondoo wakati wa Mwalimu kumbe ni mbwa mwitu wa kifisadi waliokuwa wakisubiri Mwalimu aondoke kwenye ulingo wa siasa kisha watufisadi.

Kingunge ni mtu hatari sana,na asipodhibitiwa ataiingiza nchi katika machafuko.Kishajizeekea,hajali litakalotukumba kwa vile ashachuma vya kutosha na anamsubiri Muumba amrejeshe mbele ya haki (na huko atakuwa na maswali lukuki ya kujibu atapokutana na Mwalimu).Ni muhimu kwa wanaomlea kikongwe huyu wakamhurumia kwa kumpatia pumziko haraka,la sivyo "atazidi kulikoroga".

Mungu ibariki Tanzania na waangamize mafisadi na watetezi wao,hususan wale wanaotaka ligi
na wachunga kondoo wako.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.