Uchambuzi wangu wa kiintelijesnia kuhusu shambulio la kigaidi lililotokea jana usiku katika jiji la Nice, nchini Ufaransa ambapo hadi sasa watu 84 wameuawa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa baada ya gaidi mmoja kuliingiza lori kwenye kundi la watu waliokuwa wakisherehekea siku ya kitaifa nchini humo. Bonyeza hapo chini kusikiliza uchambuzi huo
Showing posts with label TERRORISM. Show all posts
Showing posts with label TERRORISM. Show all posts
15 Jul 2016
24 Sept 2013
H.E. Uhuru Kenyatta,
President of the Republic of Kenya,
NAIROBI.
I
have received with shock and anger the devastating news of tragic terrorist
attack at the Westgate Shopping Centre in Westlands, Nairobi, on 21st
September, 2013 and claimed 59 innocent lives, more than 175 injured and many
more in traumatic condition.
During
this time of grief, I wish, on behalf of the Government and people of the
United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, to convey our deepest
condolences to you and through you to the Government and People of the Republic
of Kenya as well as bereave families who have been robbed of their loved ones
by this heinous attack. I also send our prayer and sympathy for the speed
recovery, comfort, courage and consolation of all those affected by this
horrendous attack.
This
attack not only aimed at bringing fear and hatred among Kenyans, but also to deviate
the Government of Kenya from fulfilling its international obligation to support
peace processes on the continent. In this respect, this cowardly and senseless attack
on innocent people must be condemned by all peace loving people in no an
uncertain terms.
We
are convinced that under your able leadership, the Government of Kenya will
leave no stone unturned and bring the perpetrators to justice as it has been
done before. The Government and people of the United Republic of Tanzania stand
together with the people of Kenya during this trying moment. My Government
pledge our unreserved support to the Kenyan Government in working together to fight
the scourge of terrorism in all its forms.
Please
accept, Your Excellency the assurances of my highest consideration.
Jakay Mrisho Kikwete
PRESIDENT
OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
23 Sept 2013
Nadhani utakuwa umemuona huyu jamaa (kushoto) kwenye picha za TV zinazoeleza kilichotokea na kinachoendelea katika tukio la kigaidi kwenye Mall ya Westgate , jijini Nairobi nchini Kenya. Kwa hakika ninamuona kama mmoja wa mashujaa wakubwa katika harakati za kukabiliana na magaidi na kuokoa maisha ya wahanga wa tukio hilo.Sina hakika kama ni polisi au shushushu lakini picha mbalimbali zinazomwonyesha, zinathibitisha kuwa ni mmoja wa mashujaa wanaoweza kuingia kwenye kumbukumbu za muda mrefu kuhusu tukio hili la kusikitisha. Anaglia baadhi ya picha zinazomhusu.
Balozi wa Uingereza nchini Kenya, Christian Turner, alikuwa miongoni mwa waliojitolea damu kuokoa maisha ya majeruhi wa tukio hilo. Huu ni mfano wa kuigwa.
BOTTOM LINE IS, tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu Wakenya na katika tukio hili kwa ujumla.
9 May 2011
Baada ya kifo cha Osama bin Laden,nani anaweza kuchukua nafasi yake?Tuangalie historia na tabia za warithi watarajiwa wa uongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda
Ayman al-Zawahiri
Cheo: "Naibu" wa Osama
Wasifu: Daktari wa macho
Sifa Maalum: Msemaji mahiri wa Al-Qaeda
Maficho: Mara ya mwisho alionekana Khost, Afghanistan, mwaka 2001
Wasifu: "Kichwa" kilichoandaa Mashambulizi ya September 11,2001 nchini Marekani
Anafahamika zaidi kwa: Ushiriki wake katika mashambulizi ya mabomu kwa balozi za Marekani mwaka 1998
"Nembo" (trademark): Miwani ya njano
Saif al-Adel
Cheo: Mwandaaji wa operesheni za kigaidi kimataifa
Asili: Vikosi Maalum (special forces) vya Jeshi la Misri
Sifa maalum: "Bwana mipango"
Maficho: Waziristan, kwa mujibu wa ripoti
Wasifu: Aliwekwa kizuizini kwa miaka minane nchini Iran
Anafahamika kwa: Mashambulizi ya mabomu mwaka 1998
"Nembo": Vijinywele kwenye kidevu
Abu Yahya al-Libi
Cheo: Mwanateolojia
Asili: Mshairi na mwanazuoni
Sifa Maalum: Mwanapropaganda wa Al Qaeda
Maficho: Afghanistan au Pakistan
Wasifu: Alitoroka jula ya Wamarekani huko Bagram, Afghanistan
Anafahamika kwa: kujaribu kumuua Muammar Gaddafi
"Nembo": Hotuba kali
Nasser al-Wuhayshi
Cheo: Kiongozi Peninsula ya Rabia
Asili: Katibu muhtasi wa Osama
Sifa maalum: Alitoroka gerezani Sanaa, Yemen, mwaka 2006
Maficho: Yemen
Wasifu: Alishirikiana bega kwa bega na Osama katika mapambano huko Tora Bora, Afghanistan
Anafahamika zaidi kwa: Kutoroka jela huko Yemen
"Nembo": "Andunje": ni mfupi wa chini ya futi tano
Adam Gadahn
Cheo: Msemaji
Asili: Anapenda miziki ya sauti kali yenye ujumbe wa kifo
Sifa maalum: Anamudu kiingereza vizuri,mjuzi wa teknolojia
Maficho: Alihamia Pakistan mwaka 1998, ameoa mkimbizi wa Kiafghanistani
Wasifu: Aliwahi kufungwa kwa kumpa kipigo mwenyekiti wa msikiti aliokuwa akiswali
Anafahamika zaidi kwa: Kumpa elimu Osama kuhusu mtikisiko kwenye sekta ya dhamana ya majengo (mortgage crisis)
"Nembo": Mjukuu wa mtaalam wa Kiyahudi wa elimu ya mkojo (urology)
Adnan el-Shukrijumah
Cheo: Afisa mipango ya nje
Asili: alisoma Kemia
Sifa maalum: Aliishi Marekani kwa miaka 15
Maficho: inadhaniwa kuwa Pakistan
Wasifu: Mrithi wa Khalid Sheikh Mohammed
Anafahamika zaidi kwa: Kupanga shambulio lililofeli la mabomu kwenye mfumo wa reli ya chini ya ardhi nchini Marekani mwaka 2009
"Nembo": Kushirikiana na magenge ya majahili wa Honduras
Fahd al-Quso
Cheo: Kamanda wa operesheni za mashambulizi
Asili: Mbeba mabegi ya bin Laden
Sifa maalum: Kulala fofofo: "alilewa" usingizi hadi akachelewa kazi ya kurekodi shambulio la kigaidi kwa manowari ya USS Cole.
Maficho: Kaskazini mwa Waziristan
Wasifu: Kuandaa shambulizi la mabomu kwa manowari ya USS Cole.
Anafahamika zaidi kwa : Aliwatambua kwa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) magaidi wawili waliohusika na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11,2001 nchini Marekani
"Nembo": Nywele zake kwenye paji lake zimekaa kama herufi V iliyogeuzwa
Abdelmalek Droukdel
Cheo: Kiongozi wa Islamic Maghreb
Asili: mwanafunzi wa sayansi
Sifa maalum: Mtaalam wa milipuko
Maficho: Aljeria
Wasifu: Idara ya Hazina ya Marekani ilitaifisha mali zake mwaka 2007
Anafahamika zaidi kwa: Kuua watu 70 kwenye kwa shambulizi za bomu jijini Algiers,Aljeria
Trademark: Tambara la kijana kama yale ya mabaniani
Imetafsiriwa (isivyo rasmi) kutoka jarida la Newsweek
Subscribe to:
Posts (Atom)