22 Oct 2008


Na Hilary Komba 

WATANZANIA Bara hawawezi kulazimika kuingia Zanzibar kwa pasipoti kutokana na sheria ya uraia kukataza utaratibu huo ndani ya Jamhuri moja. 

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Naibu Kamishina wa Uhamiaji, Wizara ya Mambo ya Ndani Bw. Abdi Ijimbo, wakati akizungumza na Majira kuhusu hoja zilizoripotiwa na vyombo vya habari hivi karibuni, vikiwanukuu baadhi ya watu wakisema ni vyema Watanzania Bara waingie Zanzibar kwa pasipoti. 

Bw. Ijimbo alisema sheria za Uhamiaji zinaruhusu Mtanzania anayetaka kutoka nje ya nchi kuwa na pasipoti, ili ajulikane kuwa ni Mtanzania aliyefuata taratibu ambazo zipo duniani kote. 

"Hadi sasa Serikali haina sababu ya kuanzisha pasipoti kuingia Zanzibar, kwa vile hakuna sheria inayosema hivyo na Zanzibar ipo katika Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, ndiyo maana hata huko nyuma hati ya kuingilia Zanzibar ilifutwa," alisema. 

Bw. Ijimbo aliongeza kuwa katika Serikali ya Awamu ya Pili, Watanzania Bara walikuwa wanaingia Zanzibar kwa hati ambayo ilikuwa pia haina hadhi ya pasipoti, bali ulikuwa ni utaratibu fulani tu uliowekwa na baadaye kuonekana hauna sababu ya kuendelea kuwapo. 

Alisema anashangaa kuona baadhi ya Watanzania wanazungumzia jambo hilo ndani ya nchi zilizoungana na kuwa kwenye Jamhuri ya Muungano. 

Nayo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imesisitiza kwamba vitambulisho vinavyotolewa vya Mzanzibari mkazi ni kwa wale tu wanaoishi visiwani humo, anaripoti Ali Suleiman. 

SMZ imesema Watanzania kutoka Bara wataweza kutambuliwa kwa vitambulisho hivyo, baada ya kutimiza masharti yaliyopo. 

Imesema vitambulisho hivyo havina malengo ya kisiasa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kwamba ni mikakati ya CCM kushinda katika uchaguzi mkuu ujao. 

Akitoa juzi majumuisho ya mjadala wa sera ya vitambulisho vya Mzanzibari, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali Zanzibar, Bw. Suleiman Othman Nyanga, alisema Zanzibar haiwezi kutoa vitambulisho vya uraia kwani yenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Serikali ya Muungano. 

Alisema sera iliyoandaliwa ni ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na si ya vitambulisho vya Mzanzibari. 

“Mheshimiwa Spika ni vyema kutambua kuwa hii sera ni ya vitambulisho vya Mzanzibari kwa sababu michango mingi iliyotolewa, imezungumzia suala la Mzanzibari, lakini hapa tunasema ni sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi kwa sababu Mzanzibari tunayetaka kumpa kitambulisho ni yule ambaye anakaa Zanzibar,” alisema Waziri huyo. 

Waziri Nyanga alisisitiza, kwamba vitambulisho hivyo hatapewa Mzanzibari anayekaa nje ya visiwa hata kama anakaa Dar es Salaam, lakini ikiwa si mkazi, hatakuwa na halali ya kupata kitambulisho hicho, ambacho ni kwa ajili ya Wazanzibari wanaoishi Unguja na Pemba. 

“Tunayemsema sisi hapa ni Mzanzibari mkazi ndiye tutakayempa kitambulisho, kama anakaa Dar es Salaam maadam si mkazi yeye hahusiki na kitambulisho hiki cha sera hii, ambayo tunataka kuipitisha,” alisema. 

Waziri huyo alisema SMZ haitatoa vitambulisho vya uraia kwa sababu suala hilo ni la Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hata Rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Amaan Karume alitoa vitambulisho vya uraia kwa Zanzibar. 

“Wakati huo vitambulisho kweli vilitolewa na viliitwa pasi ya uraia iliyotolewa wakati huo na kwa kuwa kuna neno uraia, na uraia kwa Tanzania ni mmoja, kwa hivyo vitambulisho hivyo kama utavitazama vitakuwa vimeandikwa pasi ya uraia na vimeandikwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Zanzibar ... haikuwa pasi ya uraia ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,” alisema. 

Alisema watakaopaswa kupewa vitambulisho ni wale walioamua kuwa wakazi wa Zanzibar, ambao watakuwa na makazi yao ya kudumu na watakuwa wanahitaji huduma za kila siku za Serikali ambao takwimu zao zitasaidia kupanga mipango ya maendeleo ya visiwa vya Unguja na Pemba. 

Hata hivyo, Waziri Nyanga alisema Mzanzibari yeyote anayeishi nje ya Zanzibar anapoamua kurudi Zanzibar, basi ana haki ya kuomba kitambulisho na atapewa baada ya kuthibitisha kuwa na sifa zinazohitajika. 

“Kwa hiyo akiweza kuthibitisha sifa zilizotajwa, atapewa vitambulisho ingawa wengine walitoa maoni kwamba vielezwe kuwa ni vitambulisho vya uraia kwa kuwa suala la uraia ni la Jamhuri ya Muungano na hakuna raia wa Zanzibar, kwa hiyo vitambulisho hivi vitakuwa bado ni vya Mzanzibari mkazi na si vitambulisho vya uraia wa Zanzibar," alisema. 

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha sera ya vitambulisho vya ukazi vya Zanzibar, hatua ambayo itasaidia kuweka kumbukumbu na kusaidia takwimu za nchi katika maendeleo.

CHANZO: Majira

21 Oct 2008

Albino Girl Killed For Witchcraft
Tuesday, October 21 02:52 pm
Sky News
A gang murdered and mutilated a 10-year-old albino girl in Tanzania - because they wanted to sell her body parts to witch doctors. Skip related content

Esther Charles was killed in Shilela in the western region of the African country on Sunday.

She died just hours after President Jakaya Kikwete called for a crackdown on gangs, saying the killing of albinos has "stained the country's good image".

At least 26 other albinos, mostly women and children, have been killed in different parts of the east African country over the past year.

Albinos lack melanin pigment in the skin, eyes and hair, which protects from the sun's ultraviolet rays.

But witch doctors believe they have magical powers to bring fortune, and discrimination against albinos is rife across sub-Saharan Africa.

In 2007, police in Tanzania reported several cases of people digging up the bodies of children to remove organs, in many cases the genitals and eyes, to make potions used in rituals.

Shilela councillor Joseph Manyara told a rally organised by the Tanzania Albino Society (TAS): "It is utterly stupid for some people to believe that albinos have magic powers and their parts can make them rich.

"People should be provided with education to understand that it is only through hard working that they can prosper in life and not through selling albinos' body parts."

Police said they have arrested 47 people suspected to be involved in the killings this year.

But TAS chairman Ernest Kimaya blasted authorities over the speed at which the murders were solved.

He said: "We are yet to witness any convictions and incidents of the murder of albinos are on the rise."

There are about 150,000 albinos in the country, and more than 8,000 of them are registered with the TAS.

Some families kill albino babies upon birth, Tanzanian authorities say.

And authorities in Kenya and Burundi, where albino killings have also been reported in recent months, have started to give added protection.

Some reports say albino skin is prized in the Democratic Republic of Congo, another troubled African nation where superstition is high.

SOURCE: Sky News


BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamepinga sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na kusema suala hilo linafanywa zaidi kisiasa na kutaka kurudishwa kwa hati ya kusafiri kati ya Tanzania Bara na Zanzibar ambayo iliondoshwa mwaka 1995. 

Hayo yalisemwa jana na Waziri Kivuli Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Bw. Abdalla Juma, wakati akisoma maoni ya kambi ya upinzani katika suala la sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi. 

Alisema haiwezekani Wazanzibari kuitwa wakazi katika nchi yao na kuongeza kwamba vitambulisho hivyo havifai. 

"Vitambulisho hivi kwa kweli havifai, sera hii haifai isipitishwe, kwa sababu inaonekana wazi kuwadhalilisha Wazanzibari katika nchi yao," alisema Bw. Abdalla. 

Wajumbe wengine wa Baraza walitaka kurudishwa kwa utaratibu wa zamani wa kuwapo hati za usafiri wakati wa kuingia katika visiwa vya Unguja na Pemba. 

Mwakilishi wa Magomeni, Bw. Salmin Awadh, alitaka kurudishwa kwa hati za usafiri na kusema kuondoshwa kwake kwa kiasi kikubwa kumesababisha kasi ya ujambazi na uhalifu. 

"Tunataka kurudishwa kwa hati za usafiri kati ya Zanzibar na Tanzania Bara...tunataka kuwepo kwa udhibiti katika eneo la bandari pamoja na uwanja wa ndege'alisema Awadh. 

awadh alisema sera ya vitambulisho vya uzanzibari ukazi lengo lake ni ulinzi kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba na kuweza kuwatambuwa hasa Wazanzibari na wageni. 

mwakilishi wa viti maalumu kutoka katika chama cha wananchi CUF Zakia Omar naye alitaka kurudishwa kwa utaratibu huo ambao alisema ulisaidia sana kudhibiti vitendo vya uhalifu. 

alisema kuondoshwa kwa hati za kusafiria kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kiasi kikubwa kumerudisha wimbi la vitendo vya uhalifu. 

hati ya kusafiri kati ya Tazania Bara na Zanzibar pasipoti iliondolewa katika miaka ya 1995,baada ya kubainika kuwepo kwa vikwazo vya usafiri katika nchi moja ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na kuonekana kwenda kinyume na katiba
.

CHANZO: Majira

20 Oct 2008


Now you will need a passport to buy a mobile phone under 'Big Brother' style scheme

Anyone buying a mobile phone could be forced to produce their passport as part of the plan for a huge surveillance database. 

Security chiefs want a national register of all 72million mobile phone users in the UK to help track terror plots or crime networks. 

Customers can currently buy prepaid mobile phones with cash, without providing personal details. 

There are some 40 million prepaid and unregistered mobile phones in Britain. 

Opponents claim determined terrorists or criminals will find it easy to sidestep the database by using foreign-registered mobile or satellite phones. 

The phone database will form part of a surveillance system proposed in the Communications Data Bill, unveiled by Home Secretary Jacqui Smith last week. 

It includes plans to log and store details of every phone call, email, text message and internet visit in Britain - including websites such as Facebook and eBay. 

A spokesman for Information Commissioner Richard Thomas said: 'We would expect that this information would be included in the database proposed in the draft Bill.'

SOURCE: Daily Mail

19 Oct 2008






CLICK HERE to read the story

18 Oct 2008

Wanafunzi 5,300 na wahadhiri wao zaidi ya 100 wa Chuo Kikuu cha Dodoma, wameanza mgomo usio na ukomo wakishinikiza uongozi wa chuo hicho kuwalipa stahili zao mbalimbali.Wanafunzi hao walikuwa wamebeba mabango mbalimbali yenye ujumbe wa kumtaka Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Shabani Mlacha, kujiuzulu kwa madai kuwa ndiye kikwazo. 

Pia walikuwa wakiimba nyimbo za kuhamasisha mshikamano huku wakimtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwenda chuoni hapo kuwasikiliza. 

Askari Polisi wakiwa kwenye magari walikuwa pembeni ya wanafunzi hao wakiwa tayari kupambana na wanafunzi hao kama wangefanya fujo hivyo kusababisha uvunjifu wa amani chuoni hapo. 

Hata hivyo, polisi hao walijikuta hawana kazi ya kufanya kwani hakukuwa na hali yoyote ya uvunjifu wa amani na wanafunzi hao walionekana kuwa watulivu wakati wote wa kuimba nyimbo zao. 

Katika mgomo huo ulioanza jana, wanafunzi hao wanalalamikia uhaba wa malazi kwa madai kuwa wanachangia Sh. 500 kila siku, lakini baadhi yao wanalala kwenye nyumba za kulala wageni na wengine wakilazimika kulala kwenye chumba kimoja watu wanne. 

Akizungumzia mgomo huo, Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho, Malimi Joramu, alisema sababu nyingine ni uongozi wa chuo hicho kuwatoza wanafunzi Sh. 100,000 kama gharama za matibabu kwa miaka mitatu. 

Alisema malalamiko yao yapo upande wa wanafunzi ambao ni watumishi wa umma ambao hulazimika kuchangia gharama hizo kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, lakini uongozi wa chuo umewataka wote kulipia gharama hizo bila kujali ni mtumishi wa umma au la. 

``Tulishakubaliana na Uongozi wa Chuo mwaka jana kuwa wanafunzi hao wasichangie gharama hizo na wale waliokwisha changia warudishiwe gharama zao, lakini tumeshangaa kwa wanafunzi wa mwaka huu, gharama hizo zimerudishwa tena na wale waliorudishiwa fedha zao, wametakiwa kurudisha gharama hizo,`` alisema Rais huyo. 

Madai mengine alisema ni pamoja na Uongozi wa Chuo kuweka muda mfupi wa usajili wa wanafunzi, ambapo chuo hicho kimetangaza kwamba jana ndiyo mwisho na wale ambao watakuwa hawajajisajiliwa, Chuo hicho hakitawatambua. 

Rais huyo anadai kuwa, muda huo ni mfupi mno ukilinganisha kuwa wanafunzi wengi wanaosoma chuoni hapo wanatoka katika familia maskini na hata walipouomba uongozi wa chuo kuwaongezea muda, ulikataa kufanya hivyo na kushikilia msimamo wake wa kuwafukuza. 

``Tunajiuliza hivi iweje mafisadi wa EPA ambao ni wezi wameongezewa muda wa kulipa fedha walizoiba, sisi ambao ni wanafunzi na tunatoka kwenye familia maskini tunakataliwa kuongezewa muda hata wa mwezi mmoja tu, hii sio haki kabisa,`` alilalamika Joramu. 

Kwa upande wa wahadhiri wa chuo hicho, wao wanadai kutolipwa posho ya kujikimu ya wiki moja ya kuripoti chuoni hapo pamoja na fedha za uhamisho kwa baadhi ya wahadhiri. 

Wengine wamedai hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita hali inayowafanya waishi maisha ya kuombaomba, hasa kutokana makali ya maisha kupanda. 

Wahadhiri hao wanaokadiriwa kupita 100, wamegoma kuingia madarasani wakishinikiza kulipwa posho hizo, pamoja na mishahara yao na ikiwa ni vinginevyo, mgomo huo hautakuwa na ukomo. 

Akijibu tuhuma za wanafunzi, Profesa Mlacha alisema gharama za malazi wanazolipia wanafunzi hao, zimepunguzwa kutoka shilingi 700 kwa siku mwaka jana, hadi kufikia Sh. 500 mwaka huu. 

Alisema sababu za kupunguza gharama hizo ni malalamiko ya wanafunzi hao wakidai kuwa ni kubwa na wazazi wao wanashindwa kumudu kulipa. 

``Kutoka na hali halisi ya maisha, tuliwaelewa na tukaamua kushusha hadi kufikia Sh. 500, lakini pamoja na kushusha huko, bado baadhi yao wanaendelea kulalamika kuwa gharama hizo ni kubwa,`` alisema. 

Hata hivyo, Profesa Mlacha alisema chuo hicho kina malazi ya kutosha na kila chumba wanalala wanafunzi wanne kutokana na ukubwa wa vyumba hivyo, kwa kuwa kila mwanafunzi ana kitanda chake. 

Alisema hivi sasa kuna vitanda na magodoro zaidi ya 1,000 ambayo hayajalaliwa na wanafunzi kutokana na wengi wao kuwa hawajaripoti chuoni hapo hadi sasa na kushangazwa na malalamiko ya wanafunzi ambayo aliyaita kuwa ni ya uzushi. 

Kwa upande wa malipo ya matibabu alisema, chuo hicho kilikutana na watendaji wa Mfuko wa Bima ya Afya na kuzungumza nao kuangalia utaratibu wa matibabu ambapo walibaini kuwa, kuna baadhi ya magonjwa ambayo mfuko huo hauyalipii. 

Kuhusu madai ya usajili alisema, hizo ni sheria za chuo kwamba mwanafunzi ambaye hajasajiliwa na chuo, hatambuliki kama ni mwanafunzi. 

``Tangu siku ya kwanza ya mwanafunzi kupata barua ya kuitwa chuoni, anaorodhoshwewa mahitaji yote anayotakiwa kuja nayo, sasa iweje mwanafunzi aje shuleni akiwa hana fedha hata nusu ya gharama hizo, chuo hakitakubali hata kidogo kumsajili mwanafunzi ambaye hajalipa hata nusu ya gharama zinazohitajika,`` alisisitiza. 

Akijibu malalamiko ya wahadhiri, Profesa Mlacha alisema sheria iliyokuwa ikitaka wahadhari hao kulipwa posho hiyo imefutwa, lakini hata hivyo, chuo hicho kimetumia busara ya kuwaombea fedha hizo serikalini na taratibu hizo zilikuwa zinaendelea. 

Hata hivyo, alisema pamoja na kwamba asilimia 80 ya walimu hao hawana sifa za kulipiwa gharama za malazi na chuo, chuo hicho kimejitahidi kuwapatia nyumba ambazo zina kila kitu na kwamba hakuna mhadhiri anayekaa kwenye nyumba za kulala wageni. 

``Wahadhiri hao nao wametufikisha mahali ambapo tunashangaa, mwaka jana tuliwalipa, lakini kutokana na sheria hiyo kufutwa bado tukatumia ubinadamu wa kuwaombea fedha hizo serikalini, lakini wakati suala hilo likishughulikiwa tunashangaa nao wanagoma, chuo hakielewi nia yao ni nini,`` alihoji Prof. Mlacha. 

Aidha, Profesa Mlacha alisema, uchunguzi wa chuo hicho umebaini kuwa, wapo wahadhiri wachache wanaojifanya wanazijua siasa au wanataka kutumia chuo hicho kujifunza siasa. 

``Tumebaini wahadhiri hao ndiyo walioshinikiza mgomo huu, inawezekana wanajifunza siasa ndani ya chuo hiki, lakini tunawaeleza kuwa, hiki sio chuo cha siasa na kama wanataka siasa waende kwenye vyama vya siasa kuonyesha uwezo wao wa kujua siasa,`` alisema Profesa Mlacha. 

Hadi mwandishi wa habari hizi anaondoka eneo la chuo hicho bado wanafunzi hao walikuwa wakiendelea na mgomo wao.

CHANZO: Nipashe









17 Oct 2008

2008-10-17 10:38:12 
Na Simon Mhina

Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustino Ramadhani, ametoboa siri ya ufisadi unaokua kila kukicha nchini kwamba unatokana na uchaguzi. 

Ameonya kama rushwa kwenye uchaguzi haitadhibitiwa basi ufisadi ambao umekithiri kila eneo utaendelea kuitafuna nchi. 

Alisema rushwa na ufisadi katika nchi ni sawa na watoto mapacha, na mama yao ni uchaguzi. 

Jaji Mkuu alisema hayo jana wakati akitoa mada katika kongamano la siku mbili la kujadili rushwa katika siasa na ugharimiaji wa shughuli za kisiasa katika vyama. 

Katika hutuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Msajili wa Mahakama Kuu, Ferdinand Wambali, Jaji Mkuu alisisitiza kuwa bila kudhibiti rushwa kwenye uchaguzi, uovu huo utaendelea hata katika vyombo vya kutunga sheria na vile vya utoaji haki kama mahakama. 

``Ukimpitisha mgombea kwa misingi ya rushwa, ujue kiongozi huyo ndiye utakayekutana naye mbele ya safari katika kukuhudumia. Mtu aliyetokana na rushwa kwake ni vigumu kukemea rushwa hata kama imemzunguka,`` alisema. 

Naye Jaji Kiongozi Mstaafu, Amir Manento, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, alisema umefika wakati sasa kumpa nafasi Rais kuteua mawaziri nje ya wabunge kwa kuwa wengi wao wamepata nafasi hizo kwa kutoa rushwa. 

Alisema wabunge ambao huingia bungeni kwa njia ya rushwa, wanapoteuliwa kuwa mawaziri hutumia fursa hiyo kurudisha fadhila kwa wale waliowakopesha takrima. 

Alionya kwamba hakuna mfadhili yeyote ambaye anaweza kutoa fedha zake bure bila kuwa na lengo ya kupata faida baadaye. 

Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema chanzo cha rushwa, ufisadi na aina zote za ubadhirifu wa mali ya umma, ambavyo vimeshamiri nchini vinatokana na viongozi kuingia madarakani kwa njia ya rushwa. 

Aidha, alisema bila kukomesha rushwa katika uchaguzi, itakuwa vigumu kukomesha ufisadi nchini, kwa vile viongozi wengi wameogolea katika rushwa hadi kufikia katika ngazi walizo nazo. 

Kutokana na sababu hizo, Warioba aliona kwamba ni vigumu kwa viongozi waliochaguliwa kwa rushwa kuweza kupambana na janga hilo. 

Kongamano hilo lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kushirikiana na Tasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) lilianza jana jijini Dar es Salaam na linamalizika leo. 

Jaji Warioba alisema hivi sasa Tanzania inaelekea kubaya kwani rushwa inaonekana kukubalika kabisa kuwa moja ya kigezo cha kumpima mgombea. 

``Hivi sasa hata kama utahubiri sera nzuri kiasi gani, hata kama mgombea anayo sifa kubwa kiasi gani, hawezi kupita bila kutoa rushwa, hizi ni dalili mbaya,``alisema. 

Jaji Warioba alisema kutokana na rushwa kushamiri, hivi sasa kampeni za mgombea kuomba kuteuliwa na chama chake zimekuwa nzito kuliko kampeni za ujumla za kiserikali. 

Alisema hata baada ya sheria ya takrima kufutwa bado wagombea wamekwa wakibuni mbinu mbalimbali za kugawa rushwa. 

Warioba alipinga vikali madai kwamba umasikini wa wananchi ndio unasababisha rushwa kushamiri. 

Alisema kwa maoni yake, rushwa inashamirishwa nchini na matajiri pamoja na viongozi ambao tayari wanazo pesa. 
Alisema hata hapa nchini, miaka ya nyuma watu walikuwa masikini wa kutupwa, lakini hapakuwa na rushwa katika uchaguzi. 

``Kwa hiyo si kweli kwamba umasikini ndio unasababisha rushwa katika uchaguzi, wanaosababisha rushwa na kuwafundisha watu waamini katika rushwa ni viongozi na matajiri,`` alisema. 

Jaji warioba alisema kunatokea matatizo makubwa wakati wa upigaji kura, kwani imebainika kwamba baadhi ya wasimamizi, wanapokea rushwa ili `kuvizima` vyama ambavyo hawavipendi. 

Alisema japokuwa wagombea huwaamini sana mawakala, lakini sio siri kwamba mawakala hao pia hutumiwa kuwahujumu baada ya kupewa rushwa. 

Alionya kuwa kutunga sheria nyingi za kuzuia rushwa hakusaidii kama jamii yenyewe haijaamua kupinga suala hilo. 

Vilevile, alisema daftari la kudumu la wapiga kura kimsingi sio mwarobaini wa matatizo ya uchaguzi nchini, kwani linaweza kuchezewa ili kuharibu kumbukumbu sahihi. 

Kuhusu mapato ya vyama, Warioba alisema kunahitajika uwazi kwa wale wanaofadhili vyama, ili kuviepusha vyama hivyo visigeuke kuwa vibaraka. 

Mathalan, alisema kuna uwezekano mkubwa wa viongozi kugeuka vibaraka wa mafisadi kama waliingia madarakani kwa kufadhiliwa kwa njia za rushwa. 

Alionya kuwa si sahihi kutoa ruzuku kwa vyama vyenye wabunge pekee, na kutaka utafutwe taratibu wa kuvipatia vyama vyote ruzuku ili kuweka uwiano. 

Vilevile, alisema si sahihi kuvifuta vyama vitakavyokosa kura kabisa, badala yake ameshauri viachwe kwani huenda kuna siku wananchi wakavihitaji. 

``Kanu kilikuwa chama kikubwa sana, lakini sasa ni kidogo na vile vidogo sasa vimekuwa vikubwa, hivyo tusifute chama eti kwa vile ni kidogo au hakikubaliki, kuna siku kitakubalika,`` alisema. 

Naye Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) akichangia katika kongamano hilo alisema kwamba ufisadi nchini unashamiri kutokana na matajiri na wanasiasa kuendeleza tabia hiyo na wala si umaskini kama wengi wanavyopotosha. 

Dk. Emmanuel Makaidi, Mwenyekiti wa National Legue for Democracy (NLD) alisema kwamba serikali ilifuta sheria ya takrima ambayo ilikuwa uchochoro wa kutoa rushwa, lakini inataka kuirudisha kwa njia nyingine ambayo ni mfuko wa jimbo. 

Pia alisema daftari la wapigakura linapaswa kuhakikiwa mara kwa mara kuepusha chama kimoja kutumia watendaji kufuta au kuongeza majina kwa manufaa ya chama chao.

CHANZO: Nipashe


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.