23 Nov 2008
23.11.08
Evarist Chahali
BORIS JOHNSON, IMMIGRATION
No comments

Boris Johnson, the mayor of London, has broken ranks with David Cameron and the Conservative party by announcing plans to study the potential benefits of an amnesty for illegal immigrants.
Johnson said this would lead to increased tax revenues, adding that mass deportation was impractical and too expensive.
“What I want is to lead a debate about how sensibly to deal with the 400,000 people who are living here [in London] and working here illegally,” he said.
The plans were condemned by the Conservative and Labour party. Cameron, the Tory leader, immediately distanced the party from Johnson’s stance. “The problem with amnesties is that they just store up another for the future, as people expect another one,” he said.
Phil Woolas, the immigration minister, called Johnson “naive”. He added: “His comments might start with the best of intentions but will lead to more people traffickers making more money and exploiting more vulnerable individuals.”
Johnson first raised the idea of an amnesty during his mayoral campaign in April, when he openly clashed with Cameron. It was assumed that the plan had been shelved.
Last Friday, however, Johnson reopened the rift by announcing the study, which will be conducted by his economics team.
His idea is that immigrants would be allowed to stay only if they had been resident in Britain for five years, did not have a criminal record and had passed a citizenship test.
SOURCE: The Times
23.11.08
Evarist Chahali
BONGOLAND, KIBIRA, SWAHILI FILMS
No comments
Juzi nilipata kijiparaseli (hili neno nililiskia mara ya kwanza Tanga) changu kutoka Amerika,kikiwa kimesheheni dvd ya Bongoland 2.Nilivutiwa sana na Bongoland 1 na nilitarajia sehemu hii ya pili itakuwa moto vilevile.Awali ya yote,mimi sio mchambuzi wa filamu na nitachoandika hapa ni mtizamo wangu wa ki-novice katika fani hiyo.Lakini la muhimu zaidi ni pongezi kwa wote walioshiriki kutuletea burudani hiyo.I just wish tungepata Watanzania wengi zaidi wanaoweza kutonyesha taswira za popote walipo duniani kwa njia mbalimbali,kama filamu,katuni,maandishi,picha,nk.Ndugu yetu Kibira ameonyesha njia.
Sio siri,nilipoangalia Bongoland 1,nilijikuta nimekuwa Juma (mmoja wa wahusika wakuu wa filamu hiyo) tangu mwanzo hadi mwisho.Kwa kweli filamu ile ni nzuri na inakuacha mtazamaji ukijiuliza nini kinafuata.
Katika Bongoland 2,moja ya yaliyoniangusha ni kukutana na Juma "mwingine".Kwa akina sie tuliokwishamzowea yule Juma wa mwanzo hapo tumeangushwa kidogo.Nadhani katika kuleta mtiririko mzuri,jitihada zingefanyika za kuendelea na Juma yule wa mwanzo,japo hiyo haimaanishikwamba huyo "mpya" hakuimudu role yake vyema.Nadhani kaka Kibira alikuwa na wazo hilo lakini nahisi huenda "Juma orijino" hakuweza kujumuishwa kwa sababu zilizokuwa nje ya waandaaji wa filamu hiyo.
Pia nilitarajia kwamba baada ya Juma "kubwaga manyanga" ya maisha ya Amerika,angefika bongo na kukutana na hali halisi ya bongo.Ukiachia sekeseke za hapa na pale kati ya Juma "mpya" na mama mwenye nyumba,siri iliyofichuka ndani ya familia,mbinde za hapa na pale na bosi kazini pamoja na nyodo za Tatu,Juma hakuonekana kukutana na kile kinachoifanya bongo iitwe bongo.Kwa vile siwezi kujua lililokuwa kichwani mwa kaka Kibira,ni vigumu kufanya matarajio yangu yawe halisi.Lakini pengine ingependeza zaidi iwapo mara baada ya kuamua kuondoka Amerika na kurejea nyumbani,Juma angekutana na kile ambacho wengi wetu hutufanya tuhitimishe kwamba AHERA HAKUENDEKI DUNIANI HAKUKALIKI,yaani tunachukizwa na baadhi ya mambo yanayotusibu huku ugenini lakini tunajipa moyo kwamba "ahh haya yana mwisho pindi nikirejea nyumbani",only to get back home na kukutana na mambo kinyume kabisa na matarajio yetu.
Juma aliweza kupata nyumba ya kupanga kirahisi pasipo kukutana na ujanja ujanja wa madalali,au utapeli uliokubuhu katika biashara ya kupanga nyumba.Juma hakupelekeshwa vya kutosha pale ofisini kama ambavyo baadhi ya wenzetu wanavyoshuhudia "laana ya kutoka ng'ambo".Ukifanya hiki utaambiwa "aah usituletee mambo yako ya Ulaya/Amerika hapa..." Ukitaka kuleta mijadala ya msingi ya kuchochea maendeleo unaambiwa "hayo ni hukohuko kwa wazungu...." na pengine Juma angeweza kuonyeshwa akihaha huku na kule kutafuta ATM yenye hela (hususan Ijumaa jioni hadi Jumapili) maana hizo ni miongoni mwa mbinde za bongoland.Pia Juma ana bahati ya kutokutana na mbinde za daladala,"kupigwa mizinga" au hata kumendewa na akina dada walio "ready made" kwa "wachumba kutoka ng'ambo".
Inawezekana kabisa kwamba kuna Bongoland 3,na huenda baadhi ya haya niliyotamani kuyaona katika filamu hii yatakuwa katika filamu ijayo.Hata hivyo,hayo ni maamuzi ya kaka Kibira na timu yake.Who knows,pengine katika sehemu ijayo tutaonyeshwa namna Juma anavyoonja machungu ya ufisadi....maana ni vigumu kwa hali ya sasa kutokutana na jinamizi hilo.
Pamoja na hayo niliyoeleza (yanayoweza kutafsiriwa kama criticism japo sio dhamira yangu) Bongoland imeendelea kuwa kioo kizuri kwa Mtanzania alie ng'ambo kwani imejaribu kutoa picha ya namna mambo yalivyo huko nyumbani.Katika filamu hiyo kuna matukio kadhaa yanayoweza kukufanya utafakari mambo mbalimbali tunayokumbana nayo huku ng'ambo na jinsi yalivyo huko nyumbani.Again,kaka Kibira na timu yake wanastahili pongezi kubwa kwa ubunifu na jitihada zao za sio tu kutuburudisha bali pia kutuelimisha kwa njia ya filamu.
Mwisho,natarajia kitu kingine kikali cha mfanano wa NISAMEHE,filamu ambayo almanusura initoe machozi.
22 Nov 2008
21 Nov 2008
21.11.08
Evarist Chahali
AMANI TANZANIA, JOSEPH WARIOBA, MIGOMO, UFISADI
No comments
Asema viongozi wanakumbatia matajiri, nchi inahitaji maadili mapya ya viongozi
Na Ramadhan Semtawa
WAZIRI MKUU mstaafu, Jaji Joseph Warioba, ameonya kuwa iwapo hali ilivyo sasa nchini ikiachiwa iendelee kama ilivyo, amani, umoja na utulivu vitatoweka.
Kauli ya Jaji Warioba ambaye anaheshimika kutokana na maono yake ya mara kwa mara kuhusu mwelekeo wa nchi, imekuja wakati nchi inakabiliwa na tatizo la ufisadi na migomo kutoka kwa makundi mbalimbali ya jamii.
Huku akichambua nchi ilikotoka, ilipo na inakoelekea, Jaji Warioba alionya jijini Dar es Salaam jana kwamba, hakuna tena sera ya kujitegemea bali msingi wa maendeleo ni fedha, huku utu ukitoweka kwa kasi kubwa na kwamba, hali hiyo imeibuka zaidi baada ya kuvunjwa Azimio la Arusha visiwani Zanzibar mwaka 1990.
Jaji Warioba alisema kuvunjwa kwa Azimio la Arusha kumeivuruga nchi na kutaka ifanyike tathimini ya kuunda azimio jipya ambalo litaweka miiko ya uongozi, kwani sasa nchi iko katika hali ngumu.
Akionyesha jinsi mfumo wa uongozi wa nchi ulivyovurugika baada ya kuvunjwa azimio hilo la mwaka 1967 na kuundwa Azimio la Zanzibar, alisema viongozi badala ya kuangalia wananchi wa kawaida, huamua kukumbatia matajiri na wafadhili ili waendelee kuwepo madarakani.
"Hata ukiangalia huo mfumo wa uwakilishi wa uwiano, badala ya watu kukaa na kujadili namna bora ya kufanikisha mfumo huo, kinachoonekana ni watu kutaka kuzidi kukaa katika madaraka wakifikiri majimbo ni yao," alionya.
Waziri Mkuu huyo mstaafu, alisema mbali ya kukumbatia matajiri, lakini hata maisha ya baadhi ya viongozi wa sasa na watumishi wa umma yako juu yakilinganishwa na viongozi wa zamani ambao walifanya kazi chini ya misingi na miiko ya uongozi ikiwemo ya Azimio la Arusha.
Huku akionyesha msisitizo wa hilo, Jaji Warioba ambaye alizungumza mbele ya viongozi wa vyama 17 vya siasa nchini na wawakilishi wa serikali kutoka Idara ya Utawala Bora Ikulu, katika kongamano hilo lililoandaliwa na Kituo cha Demokrasia (TCD), alimtolea mfano mzee Rashid Kawawa, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15 kutoka mwaka 1962 hadi 1977, lakini maisha yake ni ya kawaida.
"Mzee Kawawa alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15, kutoka 1962 hadi 1977, tena Waziri Mkuu Mtendaji mwenye madaraka kweli si kama Waziri Mkuu wa sasa hivi, lakini hebu nenda katafute mali zake, kaangalie nyumba yake ya Madale ni ya kawaida tu, utajiuliza hivi yale ni maisha ya mtu aliyekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15?" alihoji na kuongeza:
"Leo hii nyumba za serikali zilizouzwa kwetu sisi viongozi, zimekarabatiwa na zinapendeza kweli, wengine wamezivunja na kujenga upya, angalia haya maisha, hata tupige kelele za ufisadi bado haya ni matokeo madogo, tuko katika hali ngumu sana."
Akichambua kipengele kimoja baada ya kingine katika Azimio la Arusha na athari zake kwa sasa baada ya kuvunjwa, alisema wakati siku za nyuma ilikuwa ni mwiko watumishi wa umma kuwa na mishahara miwili, leo hii baadhi yao wanapokea mishahara zaidi ya mmoja na pia ilikuwa ni mwiko kwa watumishi kuwa wakurugenzi au kuwa na hisa, leo wapo wanaomiliki makampuni.
Kwa msisitizo, alisema watu wanapata mishahara miwili, wapo baadhi ya watendaji serikalini wakiwemo mawaziri hawaendi kufungua semina kama hazina maslahi ya posho kubwa.
Alisema posho hizo wakati mwingine ni kubwa kuliko mishahara na kibaya zaidi ni kwamba, haikatwi kodi kama inavyofanyika katika mshahara.
Licha ya kumulika baadhi ya viongozi walio katika utumishi wa umma, Jaji Warioba alisema hata baadhi ya wabunge hupenda kuhudhuria semina ambazo zina posho huku wakilalamikia maslahi duni wakijilinganisha na wenzao wa Kenya.
"Wakati mwingine hata baadhi ya wabunge hutaka kwenda sehemu zenye posho, pia hulalamikia maslahi duni, ni kweli mkijiangalia na wenzenu wa Kenya wao wako juu sana, lakini nanyi msiangalie wale angalieni watu wa chini," alisisitiza.
Huku akiangalia zaidi athari za kuvunjwa azimio hilo kwa nchi, alisema sasa wakati kipindi cha nyuma uongozi wa nchi ulikuwa ni kwa wakulima na wafanyakazi, leo hii hakuna tena nafasi kwa watu wa kada hiyo kushika nafasi.
Alisema hata mfanyakazi au mkulima awe na uwezo mkubwa kiasi gani bado ni nadra kuweza kupata nafasi ya kuongoza kutokana na kuwepo tabaka la wafanyabiashara wenye pesa, ambalo limewatenga na kuwafanya duni watu wa chini.
Jaji Warioba alisema ni kujidanganya kufikiri kunaweza kuwepo Sheria ya Maadili, akitoa mfano kwamba Azimio la Arusha halikuwa sheria, lakini watu waliheshimu na ambao walishindwa kutii walijiondoa wenyewe kabla ya kufikishwa mahakamani.
Alisema sasa hivi maisha ya tabaka la chini yanazidi kuwa magumu hasa kwa wafanyakazi katika sekta ya umma kuwa na mishahara midogo, lakini wakubwa wakizidi kujiongezea posho na mishahara huku tabaka hilo la chini likiona, kitu alichoonya kwamba ni cha hatari.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema uamuzi wa kuandaa kongamano lenye mada hiyo linalenga kukumbusha maadili katika utumishi wa umma.
Profesa Lipumba ambaye ni msomi mwenye kuheshimika katika taaluma ya uchumi, alisema utumishi wa umma unapaswa kuegemea katika msingi wa kuangalia maslahi ya umma.
"Tumeamua kuangalia hili ili kukumbusha maadili katika utumishi wa umma, hali ni mbaya na nchi inaweza kuvurugika kama hali itakwenda kama ilivyo sasa," alionya.
Profesa Lipumba alisisitiza kwamba, kama matabaka yataendelea kwa watumishi wa chini kuishi kwa mishahara midogo huku viongozi wa juu wakijiongezea posho na mishahara mikubwa, hali itakuwa mbaya.
Kongamano hilo ambalo linamalizika leo, pamoja na mambo mengine limejikita katika kujadili maadili katika utumishi wa umma na namna bora ya kupata viongozi wa dola.
CHANZO: Mwananchi
19 Nov 2008

US president-elect Barack Obama has named longtime lawyer Eric Holder to be attorney general, which if confirmed would make him the first African-American ever to hold the post, US media said. Skip related content
Holder, who served as deputy attorney general under former president Bill Clinton, has accepted Obama's invitation to head the Justice Department, Newsweek magazine said, citing legal sources close to the presidential transition.
Obama's transition team did not immediately comment on the report, which was later confirmed by NBC news.
"Obama offered Holder the job and he accepted," Newsweek said, adding that "the announcement is not likely until after Obama announces his choices to lead the Treasury and State departments."
Holder would face Senate confirmation hearings in order to officially take on the post, which would put him at the head of the Justice Department as the US government's chief law enforcement officer.
Holder was co-chief along with Caroline Kennedy of Obama's vice-presidential selection process and, like Obama, is a fellow alumnus of Columbia University in New York.
"He was on the short list from the beginning and obvious choice," Newsweek reporter Michael Isikoff told CNN.
"Also, a symbolic choice. This will be the first, he will be the first African-American to head the Justice Department, and that's a pretty big deal in its own right."
Holder 57, is a partner in the Washington law firm of Covington and Burling. He has served as a superior court judge in the nation's capital and was named the capital's US attorney by former president Clinton before taking the post of deputy attorney general under Janet Reno in 1997.
Isikoff, who broke the story, said that the Obama team likely chose Holder because of his experience in the Justice Department and viewed him as a stark contrast to those who served under President George W. Bush.
Holder "lives and breathes the culture of the Justice Department. He served for years in the public integrity section of the Justice Department, and prosecuting political corruption, Republicans and Democrats," said Isikoff.
"One of the big criticisms of the Bush team both in the first term and the second term is that ... they weren't a part of the Justice Department, and they didn't quite understand the very unique culture at Justice. Eric Holder does."
The current US attorney general is Michael Mukasey. During his eight years in office, Bush has previously named Alberto Gonzalez and John Ashcroft to the post.
Gonzalez resigned in 2007 amid controversy over his role in and tstimony he gave to lawmakers about the firings of US prosecutors.
Ashcroft, who oversaw a series of anti-terror regulations in the aftermath of the Spetember 11, 2001 attacks, resigned after Bush's first term ended.
According to reports, Obama's vetting team wanted to make sure that controversy over Holder's role in the presidential pardon of fugitive financier Marc Rich at the end of the Clinton administration would not prevent his confirmation.
When the Clinton White House asked Holder for his view on the potential pardon of commodities trader Rich in January 2001, Holder gave it a "neutral leaning towards favorable."
Clinton pardoned Rich. Critics said the move showed that Rich had bought his freedom, because Rich's wife had donated amply to Clinton's campaign.
Holder later came under fire for not raising enough questions about whether or not Rich should have been pardoned, but was not implicated of any wrongdoing.
"After reviewing the evidence in the case, and checking with staffers on the Senate Judiciary Committee, Obama aides and Holder both decided the issue was highly unlikely to prove an obstacle to his confirmation," Newsweek said, citing one source close to the process.
Holder has said he met Obama at a dinner party in 2004 and was energized by the Illinois senator's campaign to become America's first black president.
"I think we share a world view," Holder told American Lawyer magazine in a June profile.
Obama "is not defined by his race. He's proud of it, cognizant of the pernicious effect that race has had in our history but not defined by it."
Holder was born in New York City. His father was an immigrant from Barbados who came to the United States when he was a teenager.
Holder majored in American history at Columbia College before earning his law degree from Columbia Law School in 1976.
He currently lives in Washington with his wife Sharon, who works as an obstetrician, and their three children.
SOURCE: AFP


Kwa mujibu wa gazeti la kila wiki la Changamoto,toleo la wiki hii,mahusiano ya kikazi kati ya Waziri wa Maliasili na Utalii Bi Shamsa Mwangunga na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi Blandina Nyoni ni mabovu kiasi kwamba hawapiti mlango mmoja wa kuingilia na kutokea ofisini.
Kwa mujibu wa gazeti hilo,inasemekana chanzo cha uhasama huo ni tofauti za kimtazamo katika utendaji kazi ambapo mmoja wao anadaiwa kuzingatia taratibu na sheria katika utekelezaji wa majukumu yake huku mwenzie akitaka kupindisha kwa sababu anazojua yeye.
Uhasama kati ya vigogo hao unadaiwa kuanza nyuma kabla ya sasa kwani wakati flani wote walikuwa viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Maji Taka (DAWASCO).Inaelezwa pia kuwa uhasama huo umepelekea mmoja wao kuwa "anaingizwa mkenge" kwa kupewa taarifa feki za kuwapo kwa nyara za serikali na hivyo kulazimika kulipa dola 70 baada ya kukagua kontena na kugundulika kuwa halikuwa na nyara zozote.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Wizara hii imekuwa na desturi za migogoro baina ya watendaji wake wakuu ambapo ilisharipotiwa huko nyuma kuhusu mgogoro kati ya aliyekuwa Waziri wakati huo,Anthony Diallo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Wanyamapori,Bw Severe,kisha "bifu" kati ya aliyekuwa Waziri,Prof Jumanne Maghembe na aliyekuwa Katibu Mkuu,Salehe Pamba.
SWALI LA KUJIULIZA,MIGOGORO HII SIO DALILI ZA MGONGANO KATI YA WAPINGA UFISADI NA WALEA UFISADI?JEURI YA WALEA UFISADI INATOKA WAPI?UFANISI UTAPATIKANA VIPI IWAPO WATENDAJI WAKUU WANAWINDANA KAMA PANYA NA PAKA?KWA STAILI HII MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YATAWEZEKANA KWELI?
19.11.08
Evarist Chahali
MAUAJI YA ALBINO
No comments

Picha kwa hisani ya LUKWANGULE
Albino anusurika kunyofolewa mkono (Majira Novemba 16,2008)
*Mnyofoaji alimrubuni kuwa anataka kumwoaNa Benedict Kaguo, TangaWIMBI la mauaji ya albino limechukua sura mpya mkoani Tanga baada ya Bibi Aisha Yusuph mwenye ulemavu huo kunusurika kuuawa kikatili.Imedaiwa Bibi Aisha alinusurika kuuawa na Bw. Mohamed Athuman baada ya kutaka kumkata mkono ili kwenda kuuza.Polisi mkoani hapa tayari imemkamata Bw. Athuman ambaye ni mkazi wa kijiji cha Dindira, Korogwe kwa tuhuma za kutaka kumuua Bi Aisha.Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Bw. Anthony Rutta, alisema mtuhumiwa huyo alitaka kutenda kosa hilo kwa kujifanya anataka kumchumbia Aisha.Tukio hilo lilitokea Novemba 13 mwaka huu saa 12 jioni katika kijiji chaDindira.Bw. Athuman amelazwa katika Hospitali ya wilaya Korogwe Magunga kutokana na kipigo cha wananchi wenye hasira baada ya kubainika kutaka kumuua albino huyo.Polisi Tanga inawashikilia watu wawili kuhusu tukio hilo ambao ni Bw. Eliaza Seif na Bw. Shaaban Ramadhan wote wakazi wa Dindira.Watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili baada ya upelelezi kukamilika.
Waua albino na kutoweka na miguu yake (Majira Julai 1,2008)
Na Mary Ng'oboko, MwanzaJESHI la Polisi mkoa wa Mwanza, linawatafuta watu wanne kwa tuhuma za kumkatakata na mapanga hadi kumuua albino na kutoweka na miguu yake.Akizungumza jana, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Khamis Bhai, alisema watu hao walifika nyumbani kwa albino huyo wakiwa na mapanga na wamevaa makoti meusi.Kamanda Bhai alimtaja marehemu kuwa ni Bw. Nyerere Ludaila (50) ambaye ni mkazi wa eneo la Usagara wilayani Misungwi mkoani hapa.Alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.30 usiku katika kijiji cha Nyaligwe, Usagara.Kamanda Bhai alisema inasemekana albino huyo alikuwa ni mganga wa kienyeji na kwamba wiki mbili kabla ya tukio, alikuwa na ugomvi na mtoto wake mkubwa uliosababishwa na mtoto huyo kudai urithi wa mali kutoka kwa baba yake, huku angali hai, lakini baba yake hakuwa tayari kutoa urithi huo."Baada ya tukio la mauaji, mtoto huyo wa albino ambaye hatujaweza kupata jina lake, alikimbia na hajaonekana nyumbani hadi sasa, nasi tunaendelea kumtafuta tukishirikiana na wananchi," alisema Kaimu Kamanda Bhai.Alisema hadi sasa hakuna aliyekamatwa kuhusiana na mauaji hayo na kwamba polisi wanaendeleza juhudi za kuwatafuta wahusika ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Wafukua kaburi wakidhani la albino, watoweka na mifupa (Majira Agosti 6,2008)
Na Theonestina Juma, BukobaWATU wasiojulikana wamefukua kaburi la mtu waliyedhani ni albino aliyefariki dunia miaka 18 iliyopita na kutokomea na mifupa yake yote.Habari kutoka eneo la tukio zilizothibitishwa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Bw. Henry Salewi, zilisema tukio hilo lilitokea Julai 30 mwaka huu usiku, katika kitongoji cha Igabilo kijiji cha Ihangiro kata ya Nshamba wilayani Muleba.Ilielezwa kuwa watu hao wasiojulikana walifukua kaburi la albino aliyejulikana kwa jina la Bibi Hilda Angelo (60) aliyefariki dunia Februari 6, 2001 kwa lengo la kuchukua mifupa yake inayoaminika kutumika kwa masuala ya kishirikina.Hata hivyo, inadaiwa kuwa watu hao hawakulenga kaburi la albino huyo kutokana na la mumewe Bw. Mkalimo Rufurani aliyefariki dunia mwaka 1990 kuwa karibu nalo.Ilielezwa kuwa makaburi ya wanandoa hao yalipangwa sehemu moja na hivyo watu hao walipofika walifukua kaburi la mume badala ya mke aliyekuwa albino na kuondoka na mifupa.Habari zaidi zilieleza kuwa watu wa familia hiyo walipoamka walikuta kaburi likiwa wazi huku mifupa yote ikiwa imechukuliwa na watu wasiojuliakana.Novemba 26 mwaka jana, katika kitongoji cha Nyakashenye kijiji na kata ya Rushwa, Muleba, watu wasiojulikana walifukua kaburi la Zeuria Yustance aliyefariki dunia Oktoba 29, 2006 wakati akijifungua na kuchukua masalia ya mifupa yake yote na kutokomea nayo.Hili ni tukio la pili kutokea wilayani humo ya watu wasiojulikana kufukua makaburi ya maalbino kwa lengo la kuchukua mifupa.Katika tukio lingine katika kijiji cha Nyambogo kata ya Ilememleza wilayani Chato, umeokotwa mwili wa mwanaume ukiwa umecharangwa mapanga na kisha kuteketezwa kwa moto na watu wasiojulikana.Hata hivyo haijajulikana mtu huyo alikuwa akituhumiwa kwa kosa gani hadi kufikia hatua ya watu hao wasiojulikana kumteketeza kwa moto.Uchunguzi zaidi unafanywa na Jeshi la Polisi Wilayani humo ikiwa ni pamoja na kuwasaka watu waliojulikana katika mauaji hayo ya kikatili.
'Biashara ya viungo vya albino vigogo wanahusika' (Majira Oktoba 16,2008)
*Yahofiwa kuongezeka katika uchaguzi 2010Na Gladness MbomaSIRI nzito juu ya mauaji ya albino yanayoendelea kutokea sehemu mbalimbali nchini imefichuliwa kufuatia utafiti wa kina uliofanywa na albino wenyewe na sasa wameamua kukifikisha kilio chao kwa Rais Jakaya Kikwete.Kwa mujibu wa utafiti huo, imebainika kuwa watu wanaotumwa kukata viungo hivyo na kuua albino wanapewa fedha nyingi na vigogo ambao huvitumia kishirikina.Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania, Bw. Ernest Kumaya, wakati akizungumzia maandamano ya amani ya kupinga na kulaani mauaji yanayoendelea dhidi yao nchini."Tunaamini kabisa watu wanaonunua viungo hivi vya albino ni watu matajiri na wenye madaraka makubwa katika maeneo malimbali ikiwamo serikalini."Mtu maskini hana uwezo na hawezi kununua kiungo kimoja kinachouzwa sh. milioni 13 hadi 14 ni matajiri ndio wenye uwezo wa kununua," alisisitiza Bw. Kumaya akibainisha waliyoyagundua.Alisema kutokana na hali hiyo wana hofu kubwa katika uchaguzi mkuu wa 2010 viungo vyao vitazidi kuongezeka kwani kipindi hicho cha kuelekea uchaguzi mbalimbali nchini vitendo vya kishirikina pia huongezeka."Wakati huo kila kiongozi atataka kuhakikisha anashinda, hivyo kwa kuwa viungo vyetu ni biashara, vitendo vya kishirikina vya mauaji ya albino kwa ajili ya kuchukua viungo vyetu vitaendelea kutawala," alisema.Alisema katika uchunguzi wao wa Septemba mwaka huu albino waligundua pia kuwapo kwa kikundi cha watu wasiozidi 10 wakiwamo wanawake ambao wamekuwa wakifanya mauaji hayo.Bw. Kumaya alisema kikundi hicho ambacho kilikuwa kipo Kanda ya Ziwa hasa Mwanza kimehamia Bukoba na baadaye wanahofia kwamba kitahamia Dar es Salaam.Akigusia maandamano waliyopanga kuyafanya Oktoba 19 mwaka huu na Rais Kikwete kutarajiwa kuwa mgeni rasmi, Bw. Kumaya alisema msukumo uliowafanya waandae maandamano ni kutoona juhudi hasa za kumaliza tatizo la mauaji dhidi ya albino, ambapo yanazidi kuongezeka huku viongozi wakuu na watoa uamuzi wakiendelea kukaa kimya.Maandamano hayo yanatarajiwa kuanzia kwenye viwanja vya Shule ya Walemavu ya Uhuru Mchanganyiko na kuishia viwanja vya Karimjee."Kutolipa kipaumbele suala la mauaji ya albino kitaifa, mfano vifo vinavyotokea katika migodi ya madini ya Mererani viliundiwa Tume na kushughulikiwa maafa hayo ni mambo yaliyotufanya tuandamane."Vifo vya watoto vilivyotokea wakati wa Sikukuu ya Idd mkoani Tabora, Serikali imetia mkono wake kwa kutoa pole kwa wafiwa yakiwamo mashirika kutoa rambirambi zao kuonesha kuguswa na janga hilo, lakini suala la mauaji ya albino nchini viongozi hawajaweza kuchukua hatua madhubuti zenye kuonesha mwelekeo," alidai.
NILIWAHI KUANDIKA MAKALA KATIKA GAZETI LA RAIA MWEMA KUHUSIANA NA SUALA HILI.UNAWEZA KUJIKUMBUSHA NILIYOJADILI HUMO KWA KUBONYEZA HAPA
Subscribe to:
Comments (Atom)
