6 Feb 2009

Zaidi,soma HAPA.

5 Feb 2009

Habari HII ni kwa mujibu wa toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema.Bingirika nalo kwa habari za uhakika sambamba na makala zilizokwenda shule.

Picha kwa hisani ya rasodo.wordpress.com
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi mjini hapa, imewahukumu vijana watano wa kiume wakazi wa kijiji cha Uhamaka manispaa ya Singida faini ya Sh250,000 baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la kukaidi kushiriki mafunzo ya mgambo. Vijana hao ni Khalid Hassan,Yahaya Jumanne, Issa Jumanne, Mohamed Omari na Mohamed Omari Salumu.

Awali, mwendesha mashitaka inspekta wa polisi Joseph Bukombe alidai mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Ruth Massamu kuwa mnamo Juni 22 mwaka 2006 washitakiwa wote kwa pamoja walikaidi kwa makusudi kuhudhuria mazoezi ya mafunzo ya mgambo. Bukombe alisema washitakiwa walikaidi maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Singida katika barua yake ya Mei 28 mwaka 2006 iliyowataka vijana wote wenye sifa ya kuhudhuria mafunzo ya mgambo, wakahudhurie bila kukosa.

Kabla ya kutolewa adhabu hiyo,kila mshitakiwa kwa wakati wake, aliiomba mahakama hiyo kumpa adhabu nafuu kwa vile, hilo ni kosa la kwanza na kwamba hawatarudia tena kutenda kosa hilo. Akitoa hukumu hiyo, hakimu Massamu, alisema upande wa mashitaka umethibitisha bila kuacha shaka kuwa washitakiwa wanayo hatia kama walivyoshitakiwa.

"Kwa hiyo, mahakama hii inawahukumu kila moja kulipa faini ya Sh50,000 na atakayeshindwa kulipa faini hiyo, atakwenda jela mwaka moja",alisema Massamu. Washitakiwa wote walilipa faini na kuachiwa huru.

4 Feb 2009


Wafanyakazi wote wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) wameachishwa kazi na kulipwa mafao yao kuanzia jana ili kupisha mpango wa kuliboresha shirika hilo litoe huduma kwa ufanisi.

Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya NIC, Dk. Hamis Kibola jana, ilisema kuwa shirika hilo litaajiri wafanyakazi wapya kulingana na mahitaji ya shirika. Dk. Kibola alisema leo na kesho shirika hilo halitatoa huduma ili kupisha kazi ya kuajiri upya na huduma itarejea tena Jumatatu ijayo wakati mchakato wa kuajiri utakapokuwa umekamilika.

Inakadiriwa wafanyakazi 500 wataachishwa kazi na shirika hilo litaajiri wafanyakazi wachache wenye ufanisi na wanaoweza kuleta changamoto mpya ya kulifanya shirika hilo liwe na tija na kuhimili ushindani wa biashara ya bima.

Dk. Kibola alisema mpango huo wa kuwaachisha kazi ni kwa mujibu wa makubaliano kati ya wafanyakazi kupitia chama chao TUICO –NIC, Serikali na Shirika la Kusimamia Mali za Serikali (CHC).

Alisema hadi jana taratibu za kuajiri upya zilikuwa zimekamilika, lakini hakusema ni kiasi gani kilichotumika kuwalipa wafanyakazi, lakini taarifa za NIC kwa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi mwaka jana zilionyesha shirika hilo limetenga Sh bilioni 5.2 kwa ajili ya malipo ya wafanyakazi. Mwaka jana, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema serikali itauza hisa nyingi za NIC kwa wananchi pindi shirika hilo litakapoweza kusimama lenyewe miaka michache ijayo.

Akizungumza baada ya mkutano wa 12 wa Siku ya Bima, Novemba mwaka jana, Mkulo alisema serikali itapeleka bungeni mabadiliko ya sheria mbalimbali ili kuibadilisha NIC kutoka kwenye shirika kuwa kampuni na serikali iongeze fedha zaidi kuliokoa ili baadaye hisa zake ziuzwe kwa wananchi na lijiendeshe kwa faida. “Tayari mchakato wote umeshakamilika wa kuliboresha shirika hili ambapo lengo la serikali si kuliuza, bali kuliendeleza,” alisema Mkulo.

3 Feb 2009

CLICK HERE for full story.

2 Feb 2009

















30 Jan 2009

29 Jan 2009


BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo na nyinginezo,pamoja na makala motomoto.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.