7 Sept 2009


Unaweza kupatwa na hasira nikikuambia kuwa wewe (na mie) kwa namna flani tunahusika na kushamiri kwa biashara ya filamu za ngono, au kwa lugha mwafaka sekta ya filamu za ngono.” Najua utakuwa tayari kushika kitabu kitakatifu kuapa kwamba kamwe hujawahi kujihusisha na “uchafu wa aina hiyo.”

Katika sehemu ya pili ya kipindi cha BBC2 nilichokizungumzia wiki iliyopita kuhusu Utandawazi na Filamu za Ngono kumebainishwa mambo ambayo kwa hakika yanatuhisisha wengi wetu na kukua kwa sekta ya filamu za ngono. Tukiweka kando namna tunavyohusishwa kwa kuwa wateja wa makampuni yanayonufaika kwa ushiriki wao katika sekta hiyo (kwa mfano makampuni ya simu za mikononi, vituo vya runinga vyenye idhaa za filamu za ngono, mahoteli yanayotoa huduma ya “luku” ya filamu za ngono, nk) kuna uthibitisho kuwa baadhi ya taasisi za dini, hususan za Kikristo, zinawekeza fedha zao katika sekta ya ngono, japo sio moja kwa moja (directly).

Tunafahamu kuwa makanisa mengi yanategemea ufadhili kutoka mashirika mbalimbali ya kidini hapa Ulaya na huko Amerika.Lakini ili wafadhili hao waweze kuendelea na usamaria wema huo ni lazima wawekeze fedha zao katika mifuko au makampuni katika mfumo wa hisa.Mfano hai ulioonyeshwa katika kipindi hicho ni namna shirika moja kubwa la kidini huko Marekani lilivyowekeza mamilioni ya dola kwa mfumo wa hisa katika kampuni moja maarufu ya simu za mikononi, ambayo kama zilivyo kampuni nyingi za aina hiyo, hufanya biashara ya kuonyesha filamu za ngono kwa mfumo wa kulipia premium content.

Kwa lugha nyingine, misaada inayotolewa na shirika hilo inatokana na sehemu ya faida iliyopatikana kwa kuwekeza kwenye kampuni ya simu inayotengeneza sehemu ya faida yake kwa kuonyesha filamu za ngono. Naamini kwamba hadi hapo si vigumu kwako msomaji kuona uhusiano kati ya shirika hilo la kidini na filamu za ngono.

Lakini kuna namna nyingine ambavyo wengi wetu tunahusishwa na ustawi wa sekta ya filamu za ngono pasipo kuelewa waziwazi.Chukulia mfano huu mwepesi wa huko nyumbani. Vyama vingi vya kuweka na kukopa (Saccos) huzalisha faida zao kwa kuwekeza hisa kwenye mabenki, mifuko ya jamii (kama NSSF) au makampuni yaliyoandikishwa kwenye soko letu la “kichovu” la hisa.Kadhalika, Saccos hizo huwa na akaunti katika mabenki mbalimbali kwa vile sote tunafahamu kuwa kulaza mamilioni katika ofisi ya Saccos ni mithili ya kutangaza tenda ya kuvamiwa na majambazi.

Sote tunafahamu katika kutoa mikopo, mabenki mengi hayajihangaishi na maadili ya biashara ya mkopaji as long as ametimiza masharti ya kupata na kurejesha mkopo.Na hapo ndipo fedha zako kule Saccos zinapoweza kujikuta zikiishia kwenye akaunti ya mkopaji anayejishughulisha na filamu za ngono.

Lakini mfano mwepesi zaidi kwa mabenki ni akaunti zetu. Fedha tunazoweka katika akaunti hizo hazikai kama matangazo huko benki bali hutumika kibiashara aidha kwa kuwekeza au kukopesha.Na miongoni mwa wakopeshwaji hao ni haohao wanaojihusisha na filamu za ngono. Kwa huko nyumbani, fedha zako unazoweka benki zinaweza kabisa kuishia kwenye akaunti ya mkopaji mwenye gesti bubu wanakotengeza filamu za ngono kama sio gesti hiyo sio danguro bubu.

Njia nyepesi ya “kuua” makampuni ya filamu za ngono ni aidha kususia bidhaa zao (jambo ambalo ni rahisi kufikirika lakini almost impossible kutekelezeka kwa vile kilicho haramu kwako na kitakatifu kwa mwenzako) au kuyakatia mirija ya fedha, yaani kwa mfano kwa mabenki kukataa kutoa mikopo au kwa makampuni yanayowekeza huko kuacha kufanya hivyo au kwa biashara zinazotumia huduma za makampuni ya filamu za ngono kuachana na mtindo huo.

Ili hayo mawili ya mwisho yawezekane kunahitajika kitu kiitwacho uwekezaji wa kimaadili (ethical investment).Lakini hilo si rahisi kwa vile lengo kuu la uwekezaji, kama yalivyo maudhui ya ubepari, ni kutengeneza faida.Ni dhahiri basi kuzingatia maadili kutakwaza upatikanaji wa faida “rahisi” kama hiyo inayopatikana katika mahusiano ya kibiashara na makampuni ya ngono.

Na kwa masikini kama sie tunaotarajia misaada katika ustawi wa takriban kila sekta ya maisha yetu, ni dhahiri hatuna jeuri ya kuhoji msaada tuliopewa umepatikana kutokana na fedha za baishara ya filamu ya ngono au la.

3 Sept 2009


Kikwete awapa mafisadi ahueni

Asaini marekebisho yaliyopitishwa na Bunge kimya kimya

Ufisadi sasa si uhujumu uchumi

Kesi za ufisadi kuwa kiini macho?

RAIS Jakaya Kikwete amesaini kuridhia mabadiliko ya sheria zinazohusu rushwa na uhujumu uchumi, hatua ambayo wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi nchini wanaitafsiri kwamba ina lengo la kupunguza makali kesi za uhujumu uchumi na rushwa zinazowakabili baadhi ya vigogo nchini, RAIA MWEMA limeambiwa.

Katika hatua hiyo, inayoashiria kupunguza makali ya sheria zinazotumika kuendesha kesi za uhujumu uchumi na rushwa nchini, kesi ambazo baadhi zinaendelea kusikilizwa mahakamani zikiwahusisha waliowahi kuwa viongozi wa kitaifa, Rais Kikwete, Machi, mwaka huu, alisaini marekebisho hayo ya sheria yaliyopitishwa na Bunge katika kikao chake cha Januari mwaka huu.

Hatua hiyo inatokana na kuwasilishwa bungeni kwa Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali, ndani yake kikiwamo kipengele kinachoingiza makosa ya rushwa katika Sheria namba 200 ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2002 (Economic and Organized Crime Act Cap 200 R.E. 2002).

Kwa kutia saini kwa Rais Kikwete kuridhia marekebisho hayo, rushwa sasa si kosa la kuhujumu uchumi.

Raia Mwema imefahamishwa kwamba mabadiliko hayo ya sheria yaliyopitishwa na Bunge Januari, yalisainiwa na Rais Jakaya Kikwete, Machi 12, mwaka huu na kutangazwa katika Gazeti la Serikali Machi 20, 2009. Habari kwamba Rais ameridhia marekebisho hayo kwa kutia saini zilifahamika hivi karibuni tu kwa wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi nchini.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kwamba Mabadiliko hayo ya Sheria hiyo yamewashitua wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi ambao wanasema wakati sheria hiyo inapitishwa walipata nafasi ya kuchangia maoni, hali ambayo haikujirudia wakati wa kuifanyia mabadiliko.

“Tulikuwa tunafikiria Serikali iongeze makali katika sheria ili tuweze kuwadhibiti zaidi mafisadi na wahujumu uchumi, badala yake sasa tunalegeza sheria ili kuwasaidia, ” alihoji mdau wa mapambano dhidi ya ufisadi aliyeko serikalini ambaye anasema ameshitushwa na mabadiliko ya sheria hiyo.

Mabadiliko hayo yamo katika kifungu cha 38 na 39 cha Sheria namba 3 ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali ya mwaka 2009, kifungu kinachofuta kifungu cha kwanza na cha pili katika jedwali la kwanza la makosa ya uhujumu uchumi kinachoingiza makosa ya rushwa na ufisadi.

Vifungu vilivyofutwa vilikuwa vinasomeka hivi:“Mtu yeyote atakuwa ametenda kosa (la uhujumu uchumi) ikiwa atakuwa ametenda kosa chini ya Sheria ya Kuzuia Rushwa” na “atakuwa ametenda kosa (la uhujumu uchumi) ikiwa atakuwa ametenda kosa la rushwa zaidi ya makosa yanayotajwa katika kifungu cha nne cha Sheria ya Kuzuia Rushwa.”

Kuondolewa kwa vifungu hivyo kunatoa nafuu kubwa kwa watu ambao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ufisadi, lakini pia mabadiliko hayo yanawavunja nguvu wapambanaji wa ufisadi ikiwa ni pamoja na vyombo vya dola vikiongozwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Habari za ndani ya Serikali zinaeleza kwamba hakuna uhakika wa moja kwa moja kwamba TAKUKURU ilishirikishwa katika mchakato wa kuifanyia mabadiliko sheria hiyo ambayo ndiyo imekuwa kwa muda mrefu msingi wa mashauri mengi inayopeleka mahakamani na kwa ajili hiyo marekebisho hayo yanagusa moja kwa moja utendaji kazi wa kila siku wa taasisi hiyo inayopigana dhidi ya rushwa nchini.

“Kama TAKUKURU wameshirikishwa basi itakuwa ni juu juu sana, lakini ninavyofahamu ni kwamba hawajashirikishwa katika hili bali Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliandaa muswada na kuupeleka bungeni kimya na wabunge wetu bahati mbaya sana hawakugundua hilo,” ameeleza mdau mmoja muhimu wa mapambano dhidi ya rushwa.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea, hakuweza kupatikana kuzungumzia Mabadiliko hayo ya Sheria yanayoipunguzia ofisi yake ‘makali’ kutokana na kile Raia Mwema ilichoambiwa ya kuwa amekuwa na vikao na kufanya kazi za nje ya ofisi.

Mabadiliko hayo ya Sheria ndogo ndogo yaliwasilishwa bungeni yakiwa na marekebisho katika sheria mbalimbali 11 ikiwamo hiyo ya uhujumu uchumi na inawezekana kwamba wabunge wengi walikosa nafasi ya kupitia sheria zote zilizoguswa na mabadiliko hayo.

Sheria nyingine zilizounganishwa katika muswada huo ambao tayari umekuwa sheria ni pamoja na ya Administrator-General (Powers and Function) Act, ya Usajili wa Vizazi na Vifo, ya Chuo cha Sheria (Law School of Tanzania), Utumishi wa Umma, Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Afya, National Prosecution Service Act, Sheria ya Uchawi, Penal Code, Sheria ya Leseni za Usafirishaji na Sheria ya Ardhi.

Madhumuni ya awali ya kutungwa kwa sheria ya rushwa yalikuwa ni pamoja na kukuza na kuchochea utawala bora na kutokomeza rushwa na ufisadi kwa kutoa msingi wa kitaasisi na kisheria ambao ni muhimu katika mapambano hayo.

Mabadiliko haya yamekuja baada ya hatua kadhaa za Serikali ya Awamu ya Nne iliyofungua, baada ya muda mrefu, kesi kadhaa, zikiwagusa vigogo mbalimbali, karibu zote zikitumia kipengele cha makosa ya uhujumu uchumi ambacho kilisababisha wengi wao kukwama kupata dhamana.

Miongoni mwa walioshitakiwa kwa makosa hayo ni pamoja na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, mawaziri wa zamani, Daniel Yona na Basil Mramba na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha kwa muda mrefu, Gray Mgonja.

Mbali ya viongozi hao waandamizi, kuna mlolongo wa watuhumiwa wengine wa ufisadi ambao TAKUKURU imewashitaki kwa kutumia Sheria ya Uhujumu Uchumi, wakiwamo watuhumiwa wa EPA na ujenzi wa majengo pacha ya BoT, wote wakibanwa na sheria hiyo katika kupatiwa dhamana.

Wakati kesi hizo zikifunguliwa hasa baada ya vigogo kuanza kupandishwa kizimbani, baadhi ya watu walisema kwamba kesi hizo zimefikishwa mahakamani kama njia ya kufunika baadhi ya mambo ya ndani ya serikali.

Japo baadhi ya Watanzania walifurahia hatua hiyo ya Serikali kufikisha mahakamani baadhi ya vigogo, kumekuwa na maoni kwamba hakukuwa na mantiki ya kuwatia nguvuni watu ambao maamuzi yao yalikuwa ni ya kimchakato na kwamba kesi hizo zilikuwa ni kama mzaha katika utendaji kazi wa serikali.

“Nashangaa ninyi mnafurahia (vyombo vya habari).. Tena inaelekea kila mara wanapopelekwa mahakamani mlikuwa mnajulishwa mapema. Huu ni mzaha. Ni masuala ya kisiasa. Ni kesi zilizojaa siasa. Ukitaka kuwashitaki watu kama hawa basi itabidi ama ushitaki baraza la mawaziri au kundi zima la makatibu wakuu wa wakati huo,” alisema msomaji mmoja wa Raia Mwema.

Aliongeza: “ Haya ni matumizi mabaya ya sheria kwa maslahi ya kisiasa. Nadhani hizi ni jitihada za kufunika kesi nyingine nyeti. Nia ni wananchi wazisahau hizo.

Mramba, Yona na Mgonja, walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu wakishtakiwa kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh 11,752,350,148 kutokana na kile kilichodaiwa mahakamani kwamba walitumia madaraka vibaya kwa kusababisha kusamehewa kodi Kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayer) Government Business Corporation.

Makosa yote hayo yaliegemea zaidi katika Notisi za Serikali (GN) zilizotangazwa kati ya mwaka 2003 na 2005, notisi ambazo ndizo zilihalalisha msamaha wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayer) Government Business Corporation.

CHANZO: Raia Mwema

1 Sept 2009




Jana nilibahatika kuangalia kipindi flani cha kuvutia katika kituo cha runinga cha BBC2.Mada kuu ilikuwa ni namna makampuni makubwa, katika jina la utandawazi, yanavyosaka faida kupitia biashara ya ngono.Tangu mwanzo wa kipindi hicho ilionekana bayana kwamba kuna mahusiano ya karibu, japo yasiyo waziwazi, kati ya makampuni yanayotengetengeneza filamu za ngono na makampuni ya biashara nyingine katika nyanja zisizohusiana na ngono.

Kwa mfano, hoteli nyingi zina huduma ya idhaa (channels) za kulipia kadri inavyoangalia zinazoonyesha ngono kwa wateja wanaohitaji.Kwa namna utaratibu huo ulivyosambaa sehemu nyingi ulimwenguni ni dhahiri biashara hiyo ina faida nono.

Mfano mwingine ni kwa makampuni ya simu za mikononi.Japo jambo hilo linaweza kuonekana geni huko nyumbani, takriban makampuni yote makubwa ya simu za mikononi yana huduma zinazomwezesha mteja kuchungulia kile kinachojulikana kama ngono nyepesi (soft-core porn).

Lakini kama kuna mahala ambapo biashara ya filamu za ngono imeshamiri vilivyo basi ni kwenye mtandao wa kompyuta yaani intaneti.Ni kutokana na kushamiri kwa filamu za ngono kwenye intaneti, hususan huduma zinazowezesha watumiaji kuweka filamu (uploading) wao wenyewe,kumekuwapo hisia kwamba intaneti “itaua” makampuni ya filamu za ngono.

Watetezi wa hoja hiyo wanadai kuwa urahisi, kwa maana ya gharama na access, wa kuona filamu za ngono kwenye intaneti unaweza kabisa kupelekea wateja wazoefu wa filamu za ngono kuacha kununua filamu hizo madukani kwa vile zinapatikana (mara nyingi pasipo kulipia senti moja) mtandaoni.

Wapinzani wa hoja hiyo wanadai kuwa kama ambavyo watu hawaachi kwenda hotelini au migahawani kwa vile tu wanaweza kujipikia nyumbani ndivyo ambavyo filamu “halisi” za ngono madukani zitakavyoendelea kuvutia wateja licha ya upatikanaji wake kirahisi mtandaoni.

Kuna hoja ya ziada kwamba wakati filamu “halisi” za ngono hutengeneza kwa kuzingatia ubora wa hali ya juu katika studio zilizo tayari kwa shughuli ya aina hiyo, nyingi ya filamu za “ridhaa” kama hizo zilizotapakaa mtandaoni zina ubora duni. Lakini hoja hiyo inavutia upinzani mwingine (kutoka kwa watetezi) kwamba nyingi ya filamu za “ridhaa” mtandaoni zina uhalisia zaidi, kwa mfano pale wapenzi wanapoamua “kuweka mambo yao binafsi hadharani” mtandaoni. Watetezi hao wanakwenda mbali zaidi na kudai kuwa filamu za “ridhaa” mtandaoni zina ladha mithili ya “kupiga kozi” (u-peeping tom).

Mfano mwingine ulioonyeshwa kwenye kipindi hicho ni namna makampuni makubwa ya ku-process malipo ynanavyorahisisha upatikanaji wa huduma ya filamu za ngono.Na hili ni maarufu zaidi kwenye tovuti za ngono mtandaoni. Mara nyingi, ili mtumiaji aweze kulipia huduma hiyo analazimika kutumia credit au debit card yake katika tovuti maalumu za ku-process malipo. Kwa mara nyingine, ni dhahiri kwamba kushamiri kwa makampuni ya aina hiyo kunaashiria faida nono kwao kwani kinyume chake yasingekubali “fedha chafu”.

Kilichonigusa zaidi katika kipindi hicho ni namna filamu za ngono, whether zile halisi kutoka studio au hizo za “ridhaa” mtandaoni zinavyochangia kubadili sexual behaviours sehemu mbalimbali duniani.Na pasipo kutarajia, mtangazaji alitoa mfano wa athari za filamu hizo kwa sexual behaviours huko nyumbani. Guess what? Ni kile ambacho wengi wanakihusisha na u-Magharibi: tendo la ndoa kinyume cha maumbile! Kwa mujibu wa kipindi hicho, wataalam wetu wa sexual behaviours huko nyumbani wanaamini kwamba filamu za ngono zimechangia sana kulifanya tendo la ndoa kinyume cha maumbile kuwa mithili ya jambo la kawaida (mainstream).


Binafsi nadhani moja ya eneo lililopewa attention pungufu tunapoangalia athari za mageuzi mbalimbali yaliyojitokeza miaka ya 80 (1980s) ni mageuzi katika tabia za kujamiiana.Hivi ni mie pekee ninayeshtushwa na kukua “kwa ghafla” kwa interest kwenye umbile halisi la mwanamke wa Kiafrika? Na swali la nyongeza, je kwanini “ghafla”, ashakum si matusi, makalio ya mwanamke wa Kiafrika yaonekane kuwa na umuhimu wa kipekee katika ku-describe shepu yake? Wapo wanaohusisha interest hiyo na kukua kwa interest kwenye tendo la ndoa kinyume cha maumbile.

La kusikitisha ni kwamba hakuna namna tunavyoweza kukabiliana na nguvu kubwa ya utandawazi. Filamu za ngono zinazoendelea kuonyeshwa katika “Drive-Inn, Avalon na Empress za uswahilini” zinazidi kusambaza tabia ambazo kimsingi zinakinzana na maadili yetu. Kipindi nachokizungumzia kilionyesha namna vijana flani huko Ghana walivyoishia kuambukizwa ukimwi baada ya kujifunza “mbinu za kisasa za kufanya tendo la ndoa” mtandaoni.Ni dhahiri pia kuwa filamu za ngono zinazoonyeshwa kwenye “majumba yasiyo rasmi ya filamu za ngono” (tukiweka kando mfumuko wa kasi wa madanguro bubu) unazidi sio tu kubomoa mila na desturi zetu bali pia kutapakaza maambukizo ya gonjwa la ukimwi.

Pengine mahala mwafaka kubaini kuwa tendo la ngono kinyume cha maumbile limekamata kasi katika jamii yetu ni pale kwa Dada Dina.Lakini hiyo si kusema kwamba suala hili linajadiliwa kwa uwazi zaidi. Kama kawaida yetu, baadhi ya mambo yanaonekana kama mwiko kuyajadili hata kama yanaathiri jamii yetu. Yayumkinika kuhitimisha kuwa unafiki ni kikwazo kikubwa kwa mijadala ya aina hiyo. Wapo “waliobobea” kwenye matendo kama hayo lakini aidha wanakwazwa na “kuonekana wa ajabu” iwapo watadiriki kuzungumzia ishu ya namna hiyo au “wanaruka kimanga” pale wanapoulizwa licha ya umahiri wao.

TAFAKARI!

28 Aug 2009


Pengine ushasikia kuhusu Perfect Storm.Sijui tunaweza kuiitaje kwa Kiswahili lakini kwa kifupi ni hivi: kadri idadi ya watu inavyoongezeka duniani,mahitaji ya chakula,maji na nishati nayo yanaoongezeka.Pasipo jitihada za makusudi na za haraka kufanyika,inatarajiwa kufikia wakati flani bei za vyakula zitakuwa hazikamatiki,watu lukuki watakabiliwa na njaa kutokana na uhaba wa chakula,na idadi wa "wakimbizi" kuongezeka kutoka mahala kwenye uhaba kuelekea kwenye nafuu (ambayo itapelekea sehemu hizo zenye nafuu nazo kujikuta zikishindwa kuhimili mahitaji ya "wakimbizi" hao).


Kwa mujibu wa takwimu zilizopo,inatarajiwa kwamba kufikia mwaka 2030 idadi ya watu duniani itafikia bilioni 8 kutoka bilioni 6 ya sasa,mahitaji ya chakula yatapanda kwa asilimia 50,mahitaji ya maji yatapanda kwa asilimia 30 na ya nishati nayo asilimia 50.

Kama ilivyo kawaida ya majanga makubwa,nchi masikini huwa waathirika wakubwa zaidi kutokana na uwezo duni unaochangiwa pia na viongozi mafisadi walio maarufu zaidi kwa ngonjera kuliko vitendo.Kabla ya hiyo 2030,tayari kumeanza kujitokeza kinachoitwa "ukoloni mpya wa ardhi" ambapo baadhi ya makampuni ya katika nchi zilizoendelea yamekuwa yakinunua ardhi kwa kasi katika nchi masikini.Hali hiyo inajionyesha zaidi huko Ulaya Mashariki,lakini kuna kila dalili kuwa upepo unaelekea kwenye "shamba la bibi",yaani bara letu la Afrika.Urahisi wa Afrika unachagizwa zaidi na mitizamo mifupi ya baadhi ya viongozi wetu kuwa hatuwezi kuendelea pasipo ushiriki wa "wawekezaji" katika mipango yetu ya maendeleo (kana kwamba "wawekezaji" hao ni wazalendo wenzetu).

Itakumbukwa kuwa miezi michache iliyopita viongozi wetu waliwashawishi "masikini wa ardhi" kutoka Saudi Arabia kuja kuwekeza Tanzania huku wakihakikishiwa umilikishwaji ardhi wa muda mrefu.Nawaita Wasaudi "masikini wa ardhi" kwa vile asilimia kubwa ya nchi za Ghuba,Arabia na Mashariki ya Kati zina uhaba mkubwa wa ardhi ya kilimo (sehemu kubwa ni jangwa) japo wana utajiri wa mafuta.Tatizo sio kuwakaribisha Wasaudia au Makaburu,bali ni udhaifu sugu tulionao kwenye udhibiti wa raslimali zetu.Uzoefu tulionao katika namna madini yanavyokombwa kwa pupa na " wawekezaji" huku tukiambulia mrahaba " cha mtoto" ambao asilimia kubwa unaishia mifukoni mwa mafisadi,ni dhahiri kukodisha ardhi kwa wageni kutapelekea kuiweka rehani nchi yetu,achilia mbali wakulima kuporwa ardhi yao kama inavyoshuhudiwa kwenye maeneo yenye madini.

2005 CCM iliahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania,lakini kabla hatujapewa tathmini ya utekelezaji wa wimbo huo,kunakuja hadithi nyingine ya Kilimo Kwanza.Huu ni usanii wa kisiasa.Kilimo Kwanza mwaka mmoja kabla ya uchaguzi?Kwanini haikuwa kwenye Ilani ya 2005?Na kwa aliyepata muda wa kusoma kilichomo kwenye "kibwagizo" hicho cha Kilimo Kwanza atabaini kuwa ni muendelezo uleule wa kupiga risasi kisha kulenga (shooting then aiming).Yaani,watu wanakurupuka na mawazo ya ajabu ajabu,yanashindikana kisha zinaanza semina elekezi za kujadili kwanini mkakati ulishindwa.

And these people can't be serious kwa vile wakati wanakuja na Stimulus Package (sijui imeishia wapi) "walisahau" kuwa kilimo bado ni uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania,with exception of mafisadi ambao uti wa mgongo wa uchumi wao ni ufisadi.

Ni katika mazingira hayo tunalazimika kujiuliza itakuwaje hapo 2030 tunapotarajia hiyo Perfect Storm.Of course,sie tushazowea storms mbalimbali miaka nenda miaka rudi.Tunaambiwa taifa letu changa lakini tunamudu kuongeza maradufu mishahara ya wabunge huku walimu wakitishia kugoma kutokana na madai yao ya malimbikizo ya mishahara yao kiduchu.

Kitakachotunusuru ni kudra za Mwenyezi Mungu pekee kwa vile sote tunajua nini kitatukumba come hiyo Perfect Storm tukiwa na wababaishaji kama hawa waliopo sasa.

24 Aug 2009


EITHER ex-prime minister Edward Lowassa or ex-attorney general Andrew Chenge were on the short list to take over the Speaker’s seat in the National Assembly had the attempted ouster of incumbent Samwel Sitta succeeded last week, THISDAY can reveal today.

According to a senior Chama Cha Mapinduzi (CCM) official privy to details of the reported plotting and scheming during last week’s high-level CCM meetings in Dodoma, a good number of ruling party regional branch chairmen had been "compromised" to push for either of the two ex-government leaders to assume the Speakership after Sitta’s envisaged ejection.

It has been confirmed that the entire plan to remove Sitta and put in place a smooth replacement system was hatched and finalized during a series of secret meetings in Dodoma, Dar es Salaam and Mbeya ahead of the Dodoma meetings involving CCM’s central committee and national executive committee (NEC).

”The plotters not only sought Sitta’s removal as Speaker and expulsion from the party...they also took it a step further and earmarked who exactly should immediately replace him (as Speaker),
” the CCM official, also a NEC member, said.

He continued: ”The names that came up were Lowassa or Chenge. But would either of them have actually agreed to have their names nominated for election as Speaker, had the plot to remove Sitta succeeded? Of that I am not sure.”

It is also unclear if either Lowassa or Chenge were even aware that they were in line to replace Sitta at short notice, if it had come to that.

Lowassa was forced to resign from the post of prime minister in February last year, after being heavily implicated by a parliamentary team probing the infamous Richmond power generation scandal.

Hardly a couple of months later, Chenge - the country’s attorney-general for ten years until 2005, and thereafter a senior Cabinet minister - was similarly compelled to quit his government position after being named as an official suspect in the radar deal corruption investigation.

While both have yet to be formally charged with criminal wrongdoing, they remain active as members of both the parliamentary backbench and the various CCM caucuses.

Apart from Lowassa and Chenge, another name floated as a potential replacement for Sitta is the incumbent deputy Speaker of the National Assembly, Anna Makinda, who political insiders say is seen as more inclined to ”defend CCM interests” in parliament.

The Speakership of the National Assembly is seen as a powerful and pivotal post within the ruling party and the national political scenario as a whole.

As such, according to various CCM insiders, Sitta’s continued occupation of that post and anti-corruption stance represents a perceived large thorn in the flesh of a powerful group of corrupt politicians with vast personal business interests, who more or less control the party at will through its secretariat.

According to one ruling party insider speaking to THISDAY:"These politicians are now desperate to also control the parliament...and they regard the removal of Sitta as a key necessity towards that goal.”

The said group of politicians is believed to number about five or six, most of them incumbent members of parliament whose public images have in recent years become heavily tainted by serious allegations of grand corruption.

”They want to use the Bunge to clean up their own battered images, so that they emerge smelling like roses ahead of next year’s general elections,” said another CCM insider.

According to THISDAY findings, the plot to remove Sitta from the post of Speaker is understood to have involved large sums of money exchanging hands within the CCM-NEC ranks.

It is also understood that party leaders at various levels within mainland Tanzania were targeted to be roped in, while emissaries were also dispatched to Zanzibar to garner similar CCM grassroots leadership support for the plot over there.

Sources say some NEC members received between 3m/- and 5m/- "to ensure that the plan to get rid of Sitta succeeded."

Speaker Sitta was on Saturday accorded a hero’s welcome on returning to his Urambo parliamentary constituency in the wake of the failed plot to oust him. He vowed to soldier on with his work in the National Assembly, to ensure greater transparency and accountability in government.

SOURCE: ThisDay

20 Aug 2009


Labda CCM imekaa madarakani kwa muda mrefu mno hadi imefikia hatua ya kusahau wajibu wake. Pengine ni matokeo ya mafisadi kushika hatamu ndani ya chama hicho, au pengine ni CCM imesharidhika kwamba Watanzania wamezowea kunyanyaswa, kupuuzwa na kuchezewa kama watoto wadogo pasipo kuchukua hatua yoyote.

Najiuliza hivyo baada ya kusoma habari kwamba chama hicho tawala “kimechimba mkwara mzito” kwa baadhi ya viongozi na wanachama wake wanaodiriki kunyooshea vidole ufisadi na mafisadi.Ungetegemea CCM ingekuwa mstari wa mbele kuhamasisha mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi kwa vile so far ndio kikwazo kikubwa katika utekelezaji wa kauli-mbiu Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Lakini kwa vile mafisadi ni watu muhimu sana kwa chama hicho, jaribio lolote la kuwakemea ni sawa na kusigina katiba ya CCM.

Kana kwamba kushindwa ku-meet matarajio ya wapigakura (waliokipa dhamana chama hicho mwaka 2005 kututawala tena) sio jambo linaloinyima CCM usingizi, chama hicho kimeanza kuonyesha dalili za udikteta tukirejea kauli zake nzito za hivi karibuni. Siku chache zilizopita, kiongozi mkongwe na miongoni mwa waasisi wa CCM,Kingunge Ngombale Mwiru,aliwakemea viongozi wa Kanisa katika lugha inayoweza kutafsiriwa kuwa ni ya kidikteta,alipoonyesha dhahiri kukerwa na kitendo cha viongozi wa dini kutumia uhuru wao wa kikatiba kutoa maoni yao kuhusu hatma ya taifa letu.Na sasa tunaambiwa kwamba chama hicho kimeamua kuwafunga midomo wabunge wake wanaojaribu kuwakemea mafisadi, sambamba na kunyamazisha kelele dhidi ya tuhuma zinazomwandama Benjamin Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu.

CCM imefikia hatua ya kulitukana Bunge la Jamhuri ya Muungano na kulifananisha na kikundi cha vichekesho cha Ze Komedi.Jaribu ku-imagine kauli kama hiyo ingetoka kwa mtu kama Dkt Wilbroad Slaa au Zitto Kabwe! Ni dhahiri watu kama George Mkuchika, anayechanganya majukumu yake ya u-Katibu Mwenezi wa CCM na u-Waziri wa Habari, au Yusuph Makamba wangekurupuka na vitisho kuwa “wapinzani wanaikosea heshima Katiba ya Jamhuri.” Kulilinganisha Bunge na Ze Komedi kwa vile tu limejikongoja kuruhusu sauti zisizopendeza masikioni mwa mafisadi na watetezi wao ni kitendo kinachoashiria utovu wa nidhamu wa hali ya juu.

Bunge la Jamhuri ya Muungano ni taasisi nyeti na inayopaswa kuenziwa na kuheshimiwa na kila Mtanzania including hao wanaoifananisha na kikundi cha vichekesho. Kama unadhani kauli ya “Bunge ni mithili ya Ze Komedi” haina uzito, tafakari upya. Mtu anapokufananisha na mchekeshaji (comedian) anafikisha ujumbe kwamba hupaswi kuchukuliwa seriously. Kauli na matendo yake pia yanapaswa kuchukuliwa kama mambo yasiyopaswa kupewa umuhimu au kutekelezwa kwa vile ni ya “kusukuma muda” tu. Japo vichekesho vingi huwa na ujumbe uliofichika katika maneno au matendo ya kuchekesha, mara nyingi kauli au matendo hayo hayapaswi kuchuliwa seriously.

Kwa CCM kulifananisha Bunge na Ze Komedi inatueleza kwamba taasisi hiyo yenye jukumu la kutunga sheria za nchi haistahili kuchukuliwa serious katika kauli, maamuzi na matendo yake. Lakini hilo si geni kwa vile hata maamuzi ya baadhi ya kamati za Bunge, kama ile ya Mwakyembe, yameendelea kupuuzwa katika kile kinachothibitisha kuwa CCM imekuwa ikiliona Bunge kama genge la wachekeshaji,with exception of wabunge kama Kingunge,Serukamba,Mkuchika ,Lowassa,Rostam,Karamagi,Chenge na “wateule wengine wachache” wenye umuhimu wa kipekee kwa chama hicho.

La kusikitisha ni kwamba bado mamilioni ya Watanzania wenye akili zao timamu wataipigia kura CCM hapo mwakani irejee madarakani kuendeleza nyodo kama hizi.Na hicho ndicho kinawapa jeuri watu kama Mkuchika kusema lolote pasi hofu ya kukigharimu chama hicho ushindi hapo mwakani.CCM inajivunia knowledge yake kuhusu Watanzania kwamba ni kama wamezowea kupuuzwa (wao na baadhi ya wawakilishi wao wachache wanaopiga kelele Bungeni kutetea maslahi ya walalahoi),kunyanyaswa,kuburuzwa na kudanganywa kama watoto wadogo.

La kusikitisha zaidi ni namna uongozi wa juu (with exception of Makamba na Mkuchika wanaofahamika bayana wanaoelemea upande gani kati ya watetezi na wapinzani wa ufisadi) walivyo kimya japo kila siku wanasikika majukwaani wakiahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Taarifa za vyombo vya habari kuhusu yaliyojiri kwenye vikao vya juu vya chama hicho zinatuthibitishia bayana kuwa uongozi wa juu wa CCM hauna dhamira ya dhati ya kukomesha ufisadi kwa vile badala ya kuwakemea wanaowakwaza wapambanaji dhidi ya ufisadi wanadaiwa kuleta ngonjera za “kujadili mambo ndani ya chama.”Yaani wanataka kutuambia hawajui kuwa ndani ya chama kuna watu kama Lowassa, Rostam, Chenge na wengineo ambao kwa namna yoyote hawako tayari kuruhusu mjadala huru dhidi ya ufisadi kwa vile wao ni watuhumiwa?

Ungetarajia busara za watu kama Mzee Ali Hassan Mwinyi ziwafumbue macho CCM kwamba kuzuia demokrasia katika kujadili mambo yanayowakera na kuwaumiza Watanzania kutapelekea kifo cha mende kwa chama hicho. Lakini pengine wanafahamu nguvu za mafisadi ndani ya chama hicho, na hivyo kuhofia kuwaudhi katika kipindi hiki ambacho CCM inawahitaji mafisadi more than ever ili iendelee kututawala.Wanatupuuza kwa vile wanajua hatuna jeuri ya kuwaadhibu kwa madhambi yao.

They could be right, though! However, they fooled us in 2005.They possibly will fool us again in 2010, but let them rest assured that they will never fool us forever. They are simply buying time to finish digging their own graves.


14 Aug 2009


Kingunge Ngombale Mwiru ni mkingwe,kiumri,kisiasa na kimadaraka.Japo umri si kigezo muhimu cha kuwa na busara,ukongwe katika fani flani unatarajiwa kuambatana na busara.Lakini hali si hivyo kwa Kingunge.Kuna nyakati baada ya kifo cha Nyerere baadhi ya watu walitarajia kuwa Kingunge angefanikiwa kuendeleza mema ya Mwalimu hasa kwa vile tuliaminishwa kwamba mwanasiasa huyu (Kingunge) ana damu ya Ujamaa kiasi cha kuachana na mambo ya imani ya kidini.Tuliambiwa dini ya Kingunge ni Ujamaa.

Pamoja na mapungufu ya hapa na pale,Nyerere anaendelea kukumbukwa kwa jitihada zake za kujenga jamii yenye kukaribia usawa na kuchukia unyonyaji.Sijui Kingunge akifa tutamkumbuka kwa lipi zaidi ya kuzeekea kwake kwenye siasa pasipo tija na hili jukumu jipya alilojipachika la u-Baba wa Taifa wa Mafisadi.Kingunge ni mnafiki mkubwa kwa vile wakati anadai kuwa viongozi wa kanisa "wangeufyata" laiti Mwalimu angekuwa hai,sijui yeye Kingunge angemwambia nini anaposimama kidete kutetea mafisadi.

Haya ndio madhara ya kuviacha vikongwe madarakani hadi vinapoteza uwezo wa kufikiri.Na huyu ni mshauri wa kiongozi wa nchi!Kama uwezo wake binafsi wa kufikiri umefikia kikomo atawezaje kumshauri mtu mwingine,achilia mbali kiongozi wa nchi?

Kwanini adai waraka wa kanisa utawagawa Watanzania lakini akae kimya pale chama chake cha CCM kilipocheza karata-tatu ya kisiasa kilipoahidi (katika manifesto yake ya uchaguzi 2005) uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa Waislam?Binafsi,sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya kadhi iwapo mambo flani muhimu yatazingatiwa,lakini kwa uendeshaji wa mambo kwa mtindo wa zima moto,au pata potea,ni dhahiri uamuzi huo wa mahakama ya kadhi unaweza kulipeleka pabaya taifa.Narudia,tatizo sio uanzishwaji au kuwepo kwa mahakama hiyo,bali ni ubabaishaji wa viongozi wetu katika kushughulikia uanzishwaji na uwepo wake pasipo kuathiri umoja wa kitaifa.

Na kikongwe huyu (Kingunge) mbona yuko kimya hadi leo baada ya chama chake kusuasua katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya uanzishwaji wa mahakama ya kadhi?Kama uamuzi wa CCM kutaja katika manifesto yake juu ya suala hilo ulikuwa hatari (kwa mujibu wa wanaodhani hivyo),kitendo cha chama hicho kurushiana mpira kila kinapoulizwa na waahidiwa (Waislam) kuhusu utekelezaji ni cha hatari zaidi.

Tatizo la Kingunge kuhusu waraka wa kanisa haliko kwenye kile anachodai "kuijua vizuri nchi yetu" bali wasiwasi wake kwamba pindi waraka huo ukitekelezwa kwa vitendo basi yeye na mafisadi anaowatetea watakuwa katika wakati mgumu.Kwa lugha nyingine,Kingunge anatetea maslahi ya tabaka alilomo na analoliwakilisha (mafisadi).

Hivi ni lini umewahi kumsikia Kingunge akikemea ufisadi?Hivi Kanisa lingetoa wapi wazo la kujana waraka huo laiti kikongwe hiki cha siasa kingesimama kidete kuendeleza harakati za Mwalimu kupambana na unyonyaji?Badala ya kutueleza yeye anafanya nini kuhakikisha nchi inakwenda vizuri anakimbil;ia kukosoa wengine kuwa wanataka kuipeleka nchi pabaya.

Halafu inakera zaidi kumskikia babu huyu akijifanya kama yeye ndio mwenye hatimili ya historia,mwelekeo na chochote kuhusu Tanzania.Eti anakemea wenzake "wanaodakia hoja pasipo kujua vema tumefikaje hapa..."Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya watu kama Kingunge,wanafiki waliojifika kwenye ngozi wa kondoo wakati wa Mwalimu kumbe ni mbwa mwitu wa kifisadi waliokuwa wakisubiri Mwalimu aondoke kwenye ulingo wa siasa kisha watufisadi.

Kingunge ni mtu hatari sana,na asipodhibitiwa ataiingiza nchi katika machafuko.Kishajizeekea,hajali litakalotukumba kwa vile ashachuma vya kutosha na anamsubiri Muumba amrejeshe mbele ya haki (na huko atakuwa na maswali lukuki ya kujibu atapokutana na Mwalimu).Ni muhimu kwa wanaomlea kikongwe huyu wakamhurumia kwa kumpatia pumziko haraka,la sivyo "atazidi kulikoroga".

Mungu ibariki Tanzania na waangamize mafisadi na watetezi wao,hususan wale wanaotaka ligi
na wachunga kondoo wako.

11 Aug 2009


Kuna tamasha kubwa la kimataifa linaloendelea jijini Glasgow.Wenyewe wanaliita World Pipe Band Championships.Ni mashindano ya bendi za kupuliza filimbi kama zile za brass band (pipes).Kumejitokeza mgogoro wa kiplomasia baada ya Wakala ya Mipaka ya Uingereza (UK Border Agency) kuwanyima viza wanabendi ya kupuliza filimbi kutoka Pakistan.Licha ya bendi hiyo inayojulikana kama Lahore Piping Band,msafara wa wafanyabiashara kutoka Pakistan nao umenyimwa viza.Kinachochochea zaidi songombingo hilo ni ukweli kwamba Glasgow na Lahore ni miji pacha (twin cities).

7 Aug 2009



Kwa mfumo wa tarehe za "kwetu" tunaanza na tarehe kisha mwezi,tofauti na wenzetu wa kwa Obama ambao wanaanza na mwenzi kisha tarehe.Yaani,kwa hapa,na kama ilivyo huko nyumbani TZ,ni tarehe 07/08/09 japo kwa wenzetu wa US itaandikwa 08/07/09.Basi,leo mchana kulikuwa na tukio adimu katika uhai wa wengi.Kama inavyoonekana pichani juu,kuna muda saa na kaelnda ilisomeka 1-2-3-4-5-6-7-8-9,yaani saa 12 na dk 34 na sekunde 56 tarehe 7 mwezi wa nane mwaka 2009 (12:34:56 7/8/9).Ulikumbuka kuhusu tukio hili?

MHAMASISHA VITA DHIDI YA MAFUA YA NGURUWE NAYE AAMBUKIZWA....


Na the funny side ya "maadhimisho" hayo ni habari hapa Uingereza kwamba jamaa aliyetumika katika tangazo la "Wizara" ya Afya katika runinga kuhamasisha jamii dhidi ya mafua ya nguruwe (swine flu) nae ameambukizwa ugonjwa huo.Msanii Davidi McCusker (pichani juu).Hata hivyo,lililo dhahiri ni kwamba maambukizo hayo hayana mahusiano na ushiriki wa msaanii huyo David McCusker katika tangazo hilo.

6 Aug 2009


IMMIGRANTS who come to live and work in Scotland could have a better chance of earning full UK citizenship, it was revealed yesterday.

The Home Office unveiled plans for an Australian-style points systems for foreigners who want to settle in Britain.

Workers from overseas will receive extra points based on their skills and qualifications. Once they have enough points, they will be able to move to Britain permanently.

It also emerged yesterday that extra points will be given to migrants who settle in parts of the UK where population is set to fall - such as Scotland.

The move would build on the Fresh Talent Initiative, set up by former first minister Jack McConnell to let foreign students stay after graduation.

A Home Office spokesman said: "There are parts of the country where spaces in the workforce aren't being filled by UK residents and could very easily be filled by hard-working migrants."

Scottish Secretary Jim Murphy last night said he was "pleased" at the move.

He added:"Our need for a growing population is ranked alongside the need to recruit to occupations where we have a shortage."

SNP MP Pete Wishart gave the plans a cautious welcome. He said:"The Home Office must demonstrate the new points based immigration system is fit for Scottish purpose.

"Scotland's population and immigration requirements are completely different from the rest of the UK and this has to be recognised when points are added up."


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.