29 Nov 2009



In 2002, one in every 109 £1 coins was a fake. Today it's one in 40. A former counterfeiter reveals how to spot the fake in your pocket... and asks the question: bearing in mind you can't swap one for legal tender, would you throw yours in the bin?



28 Nov 2009



KINGSTON, Jamaica

RAIS Jakaya Kikwete ametaka ushirikiano zaidi kati ya Jamaica na Tanzania katika nyanja za muziki na michezo.

"Jamaica ina wanariadha wenye kasi zaidi duniani kwa sasa," alisema kwa kusifia.

Alisema kuwa muziki wa rege ni maarufu zaidi nchini Tanzania, huku akimtaja nyota wa muziki huo, Bob Marley kuwa ni maarufu zaidi nchini mwake.

Kikwete aliiomba Jamaica kuisaidia nchi yake kwa kuwapatia kocha wa ajili ya kuendeleza mchezo wa riadha.

Kiongozi wa Upinzani, Portia Simpson Miller alimweleza Kikwete kuwa wanachama wa chama chake, People's National Party nao wako tayar kushirikiana na Tanzania.

CHANZO: Mwananchi

Alimshauri rais aanzishe ofisi nchini kuratibu shughuli za ushirikiano katika ukanda wa Karibiani.

27 Nov 2009


Uwajibikaji uliotukuka au kupitiliza majukumu?Who cares as long as we are kept safe.Katika magazeti mbalimbali ya hapa Uingereza kuna habari kwamba Waziri wa Usalama,Lord West,amehenyeshwa na askari baada ya kusimamishwa na kusachiwa (stop and search) kwa mujibu wa sheria za kuzuia ugaidi.Uzuri wa hawa wenzetu ni ile tabia ya "hapendwi mtu",yaani kutekeleza majukumu kwa maadili badala ya kuangalia urembo au haiba.

Sidhani kama kuna haja ya kuwakumbusha madudu ya Waziri wetu mwenye jukumu la utawala bora (which includes mapambano dhidi ya ufisadi) alivyojitokeza kuwa mama mlezi wa mafisadi.Ni katika tawala ambazo mtu anaweza kuropoka chochote na akaendelea kuitwa mheshimiwa ndipo hadi muda huu Sophia Simba anaendelea na wadhifa unaohitaji uadilifu wa hali ya juu,including umakini katika kauli.

Sasa kama askari wanaweza kudili na bosi wao kama raia mwingine iweje basi waziri wetu mwenye dhamana ya kuhakikisha mafisadi "wananyea ndoo" gerezani awe mtetezi wao mkubwa?Jibu jepesi ni kwamba Waziri Simba anapata jeuri hiyo kutoka mahala flani.Na si yeye tu bali viongozi wetu wengi wametokea kuwa na jeuri ya ajabu kwa vile wanafahamu fika hakuna wa kuwaadhibu.Kama aliyekuteua haonekani kuerwa na madudu yako why would you care kurekebisha madudu hayo?

Unfortunately,lawama nyingi zimekuwa zikielekezwa kwa watendaji wabovu badala ya kumkalia kooni aliyewapa fursa ya kuweka hadharani udhaifu wao.Ni kama katika futiboli;kocha akipanga kikosi kibovu basi lawama zaidi zitaelekezwa kwake kwa vile kikosi alichopanga hakijichagua chenyewe.Na ndio maana hivi majuzi kocha wa timu ya taifa ya Scotland alijikuta akifungashiwa virago vyake baada ya timu hiyo kufanya vibaya kwenye kampeni yake ya kushiriki Kombe la Dunia hapo mwakani.

Na ukidhani mie ni malalamishi nisiye na hoja basi SOMA HAPA uelewe chanzo cha tatizo kiko wapi.

22 Nov 2009


Happy birthday to the best dad I know,

A father I love and respect,

A dad who fulfills all his duties

To teach, to guide, to protect.

If everyone had such a father,

A really good dad like mine,

The world would be so much better,

It would look like God’s own design.

21 Nov 2009



AND LISTEN TO THIS SERIAL MASTURBATER



THE JACKO REINCARNATED


19 Nov 2009



Associated Press
guardian.co.uk,
Friday 30 October 2009 18.09 GMT

Barack Obama said today that a US travel ban against people infected with the HIV virus will be overturned early next year.

The order will be completed on Monday, Obama said, finishing a process begun during the administration of George Bush.

The United States is one of about a dozen countries that bar entry to travellers based on their HIV status. The ban has been in place for more than 20 years. Obama said it will be lifted just after the new year, after a waiting period of about 60 days.

"If we want to be a global leader in combating HIV/Aids, we need to act like it," Obama said at the White House before signing a bill to extend the Ryan White HIV/Aids programme. Begun in 1990, the program provides medical care, medication and support services to about half a million Americans with HIV or Aids, mostly low-income people...
READ MORE

16 Nov 2009


BUSARA ZINAELEKEA KUSHINDWA KUFANYA KAZI KATIKA TANZANIA YA SASA.BUSARA ZIMEKUWA ZIKITUFUNDISHA KUWA UTU UZIMA DAWA LAKINI TUKIANGALIA JINSI MAMBO YALIVYO SHAGHALA BAGHALA LICHA YA KUWEPO KWA WAZEE-KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU-WENYE NGUVU KATIKA ULINGO WA SIASA NI DHAHIRI UTU UZIMA UMESHINDWA KUJIDHIHIRISHA KUWA NI AMANA KATIKA UONGOZI.

PIA KUNA SUALA LA ELIMU.WENGI TUNAAMINI KUWA DALILI ZA KUELIMIKA NI PAMOJA NA KUFANYA YANAYOTARAJIWA NA JAMAA,NA PENGINE KWA NIABA YA JAMII HUSIKA.YAYUMKINIKA KUSEMA KWAMBA KATIKA TANGU NCHI YETU IPATE UHURU HAIJAWAHI KUSHUHUDIA WINGI WA WASOMI KATIKA NYADHIFA MBALIMBALI ZA KISIASA NA KITAALAMU.UNGETARAJI WINGI HUO WA WASOMI UNGEIWEZESHA TANZANIA KUWA KATIKA MAHALA INAPOSTAHILI (YAANI TANZANIA YENYE MAISHA BORA YANAYOENDANA NA UTAJIRI WA RASLIMALI ULIOPO).LAKINI LICHA YA UTITIRI HUO WA WASOMI TUMEZIDI KUSHUHUDIA NCHI IKIGEUZWA SHAMBA LA BIBI HUKU UTAJIRI WETU UKITAFUNWA KANA KWAMBA KUNA MASHINDANO YA KUUMALIZA.

KWA VILE HUKO NYUMA TULIELEZWA KWAMBA ILI TUENDELEE TUNAHITAJI WATU,ARDHI,SIASA SAFI NA UONGOZI BORA,NA KWA VILE ARDHI IPO BWERERE HADI TUNAALIKA WAWEKEZAJI,NA WATU TUPO ZAIDI YA MILIONI 40,BASI NI DHAHIRI KUSUASUA KWA MAENDELEO YETU NI MATOKEO YA SIASA MUFILISI NA VIONGOZI WASIOFAA.

NI KATIKA MINAJILI HIYO NAONA UMUHIMU WA KUHOJI BUSARA ZILIZOMO KATIKA HABARI IFUATAYO



Rais Kikwete Aota kujenga safu ya vijana katika uongozi wa kitaifa
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuwa kama akijaliwa kupata kipindi cha pili cha kuliongoza taifa la Tanzania, atafanya jitihada kubwa kuubadilisha uongozi wa Tanzania kuwa uongozi wa vijana.

Rais Kikwete akizungumza juzi, mjini Dar es Salaam na vijana kutoka nchi mbali mbali za Afrika wanaoshiriki katika Mpango wa Kulea Uongozi wa Afrika wa African Leadership Initiative, Rais Kikwete alisema kuwa anauthamini Mpango huo.

Alisema kuwa vijana ndiyo Tanzania ya kesho, na kama Tanzania haikuwekeza vya kutosha katika vijana na maendeleo yao, basi itakuwa haiwekezi katika hali yake ya baadaye.

Aliwaambia vijana hao ambao wanashiriki katika Mpango huo unaodhaminiwa na Askofu Mkuu (mstaafu) wa Kanisa la Anglikan Desmond Tutu wa Afrika Kusini kuwa kwa kadri miaka inavyokwenda ni lazima rika la wazee lipishe lile la vijana....INAENDELEA

CHANZO: Mwananchi

JE WINGI WA VIJANA (NA NENO LENYEWE "KIJANA" NI TETE KATIKA ANGA ZA SIASA ZETU) UTAWEZA KUIFIKISHA TANZANIA INAPOSTAHILI KUWA?JE KIKWAZO CHA MAENDELEO YETU NI WINGI WA WAZEE,UPUNGUFU WA VIJANA AU UKOSEFU WA UZALENDO MIONGONI MWA TULIWAOWAPA DHAMANA YA KUTUONGOZA?

TWENDE MBALI ZAIDI.JE KIJANA KWA MUJIBU WA SIASA ZETU NI MTU WA AINA GANI?MWENYE CHINI YA MIAKA 30,40 AU 50?JE KUNA UHUSIANO WOWOTE KATI YA UJANA NA UONGOZI BORA?JE VIJANA TUOTAKA WASHIKE MADARAKA WATAWEZA KWELI KUTONGOZA WAKATI VIBABU VINATAKA KUFIA MADARAKANI NA HIVYO KUWANYIMA FURSA VIJANA YA KUPATA UZOEFU WA UONGOZI?

NA KWA VILE SIASA ZETU ZIMETAWALIWA NA FEDHA,JE VIJANA TUONATAKA WASHIKE MADARAKA HAWATAKUWA WAMEFADHILIWA NA MAFISADI ILI KUWATUMIKIA?NA VIJANA TUNAOWAZUNGUMZIA NI VIJANA WOTE AU WATOTO WA VIGOGO?

LILILO WAZI,KWA KUZINGATIA UZOEFU WA SIASA ZETU,SI KIGEZO CHA UJANA AU HAIBA KINACHOWEZA KUTUKWAMUA HAPA TULIPO BALI NI DOZI NZITO YA UZALENDO.NA JAPO SIWEZI KUJIPAMBANUA KAMA MCHAMBUZI NILIYOBOBEA KWENYE SIASA,SIJAWAHI KUONA MAHALA PANAPOTHIBITISHA KUWA UJANA NI SAWA NA UZALENDO.

LABDA NI MUHIMU PIA KUFAHAMU KUWA HATUWEZI KUENDELEA KWA KUTOA MAJIBU MEPESI TUNAPOKABILIWA NA MASWALI MAGUMU.NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA KWAMBA WENZETU WALIOENDELEA WANAFANYA KILA JITIHADA ZA KUPAMBANA NA UBAGUZI KWA VIGEZO VYA UMRI,JINSIA,RANGI,ASILI AU NAFASI YA MTU KATIKA JAMII.KWA MANTIKI HIYO,TUNAPOTAMANI VIJANA WARITHI WAZEE,HUKU TUKIWA HATUNA UTHIBITISHO KUWA UJANA NI TIBA YA MATATIZO YETU,TUNAWEZA KUKARIBISHA MANUNG'UNIKO KUTOKA KWA MAKUNDI MENGINE KATIKA JAMII HUKU TUKIENDELEA KUPIGA MARK TIME WAKATI TAIFA LETU LINAZIDI KUTAFUNWA KAMA MCHWA NA MAFISADI.

15 Nov 2009


13 Nov 2009


Baraza la Mawaziri la Kikwete lagawanyika

Godfrey Dilunga

Novemba 11, 2009

Mawaziri kumi wataka watuhumiwa waadhibiwe

Wanane wanawatetea, waliosalia hawana msimamo

Sophia Simba asonywa na wenzake

BAADA ya Kamati inayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuzungumza na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi na kuibuka malumbano, kejeli na matusi kwenye mkutano huo, imebainika kuwa sasa mpasuko si tu miongoni mwa wabunge; bali umesogea hadi kwenye Baraza la Mawaziri na kugawa mawaziri hao.

Uchunguzi wa Raia Mwema, ukihusisha mazungumzo na baadhi ya wabunge na mawaziri, umebaini kuwa mpasuko katika baraza la mawaziri kwa kiasi fulani umechukua sura tofauti na ule wa wabunge wa CCM.

Katika Baraza la Mawaziri, hali ni tofauti. Siku kadhaa mara baada ya mkutano wa Mwinyi, Dodoma, wapo mawaziri walioanza kuwapuuza manaibu mawaziri wao, lakini pia wapo manaibu mawaziri walioanza kuwapuuza mawaziri wao, hali inayotajwa kuwa huenda ikasogea hadi kwa watendaji wa chini kwenye wizara na hatimaye kugawa watendaji wote.

Lakini pia katika mazungumzo hayo ya Raia Mwema, pia imebainika kuwa kuna baadhi ya wizara zenye mawaziri wanaofanana kimtazamo wakiwa kundi moja kwenye mpasuko huo; hali inayotajwa kuwa huenda ikazua mvutano kama watendaji wengine waandamizi wizarani watakuwa na misimamo pinzani.

Mpasuko huo chanzo chake kinatajwa kuwa kashfa ya Richmond, na hususan kuhusika kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kwenye sakata hilo ambapo mawaziri na manaibu mawaziri wanaodaiwa kuwa karibu naye wameendelea kumtetea kwa siri na hadharani; huku wengine wakitafsiri hatua hiyo kuwa ni upuuzi na hata kuwaona wenzao wanaoendesha harakati hizo ni wapuuzi.

Mmoja wa mawaziri hao ni Sophia Simba, ambaye sasa si tu imedaiwa anatazamwa kwa jicho tofauti na baadhi ya mawaziri wenzake, lakini pia CCM imeanza kukana baadhi ya shutuma alizotoa kwa baadhi ya watu katika juhudi zake za kutetea watuhumiwa wa kashfa mbalimbali. Simba anadaiwa kueleza kuwa Mfanyabiashara Reginald Mengi, si mwanachama wa chama hicho.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kati ya mawaziri 26 waliopo ukimwondoa Waziri Mkuu, 10 wamedaiwa kuwa na msimamo unaofanana na baadhi ya wabunge wapambanaji wa ufisadi wakiwa na msimamo watuhumiwa wa ufisadi waadhibiwe, wakati mawaziri wengine wanane wakiwa katika kundi la utetezi.

Mawaziri wanaodaiwa kuwa na msimamo wa kupinga ufisadi ukiwamo wa Richmond ni pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Uvuvi, John Magufuli, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Mary Nagu, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Bunge, Philip Marmo.

Wengine ni Waziri wa Afya, Profesa David Mwakyusa ambaye anatajwa kuwa na msimamo wa chini chini, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Celina Kombani, Waziri wa Afrika Mashariki, Diodorous Kamala na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Margaret Sitta.

Mawaziri wanaodaiwa kuwa msimamo wao haueleweki katika sakata la Richmond ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, dk. Hussein Mwinyi, Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na Waziri wa Kilimo, Stephen Wasira.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa kundi la mawaziri wenye msimamo mkali wanaotaka hatua kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa, wengi wao wamekuwa na rekodi nzuri kiutendaji ikilinganishwa na wale watetezi wa watuhumiwa.

Baadhi ya wabunge waliozungumza na Raia Mwema wamedai kuwa mawaziri wengine wanane msimamo wao umeshindwa kubainika moja kwa moja kutokana na kuwapo katika kila kundi.

Katika mkutano uliopita wa Bunge, utekelezaji wa lala salama wa mazimio ya Bunge kuhusu Richmond ulipaswa kutolewa taarifa na serikali lakini haikuwa hivyo, bila kuelezwa sababu za wazi.

Uchunguzi huo wa muda mrefu wa Raia Mwema bungeni pia umebaini kuwa athari za makundi kwa kiasi fulani zimekuwa zikimgusa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye ndiye aliteuliwa na Rais baada ya Lowassa kujiuzulu.

Uchunguzi huo umebaini kuwa katika mkutano wa 16 wa Bunge na baadhi ya vikao vya mkutano wa 17 uliokwisha, hivi karibuni, wakati akitoa hoja au kujibu maswali ya papo kwa papo yenye utetezi wa Serikali ni sehemu ya mawaziri wachache tu wamekuwa wakimpongeza kwa kumpigia makofi na wengine wakibaki kuduwaa, wengine wakiwa katika mazungumzo yao.

Kutokana na hali hiyo, mmoja wa wabunge amedai kuwa wapo mawaziri wasiompa nafasi ya heshima na utiifu unaostahili Waziri Mkuu Pinda na kwamba, wameendelea kuwa watiifu zaidi kwa kundi lao kuliko kwa waziri mkuu.

Wizara ambazo zimejipambanua kuwa na waziri mwenye msimamo wa utetezi kwa Lowassa na watuhumiwa wengine ni Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Utawala Bora, inayoongozwa na Sophia Simba.

Wizara nyingine ambazo zimebainika kuwa na mawaziri wenye misimamo ya makundi ni pamoja na Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, inayoongozwa na Profesa Juma Kapuya, na Naibu wake Dk. Makongoro Mahanga.

Kapuya alitajwa na kundi mojawapo kwenye mpasuko huo kuwa ni kati ya watu wanaopaswa kuchukuliwa hatua akidaiwa kumtetea Lowassa kwa gharama za wanasiasa wengine akiwamo Spika wa Bunge, Samuel Sitta. Naibu wake, Makongoro naye pia alijipambunua kuwamo kwenye kundi la Lowassa, wakati wa mkutano wa Mwinyi.

Baadhi ya wabunge pia wanaitazama Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuwa inaongozwa na viongozi wenye mgongano wa makundi, japokuwa ikidaiwa kuwa Naibu Waziri Khamis Kagasheki, amejitahidi kwa muda mrefu kuficha hisia zake tofauti na Waziri wake, Lawrance Masha, anayedaiwa kuwa kundi la Lowassa.

Katika hatua nyingine, baadhi ya wabunge waliozungumza na Raia Mwema kutoka makundi yote wamebainisha matarajio yanayozidi kukinzana mara baada ya kukamilika kwa mkutano kati yao na Kamati ya Mwinyi.

Wakati upande mmoja ukiendelea kusisitiza kuwa watuhumiwa wenye nyadhifa katika chama hicho wang’olewe, wenzao wamekuwa na msimamo tofauti.

Hata hivyo, kundi la wabunge wanaotaka wenzao watuhumiwa watimuliwe ndilo linaonekena kuwa na nguvu zaidi hata mbele ya wananchi na taasisi nyeti zikiwamo za elimu ya juu nchini kama ambavyo imekuwa ikiandikwa na baadhi ya magazeti nchini.

Kwa upande mwingine, hali ya kuwapo kwa kile kinachoelezwa kuwa ni mvutano huenda ikaendelea. Kuwapo kwa dalili hizo kunatokana na kuendelea kukinzana kati ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta na baadhi ya wanasiasa wa kundi linalomwandama, akiwamo Kingunge Ngombale-Mwiru.

Kingunge katika mkutano uliopita wa NEC-CCM Dodoma aliripotiwa kutaka Spika Sitta ang’olewe kwa kuwa anaendesha Bunge vibaya kwa kuruhusu mijadala ya ufisadi na hivyo kuhatarisha chama na serikali na kuimarisha hoja yake kwa kusema ubaya wa Spika unathibitishwa na hatua yake ya kuandika kitabu kinachoitwa “Bunge lenye Meno” akishirikiana na wabunge wengine machachari, akiwamo Dk. Harrison Mwakyembe.

Inaelezwa kuwa Kingunge alirejea msimamo wake huo katika mkutano wa Mwinyi lakini akionyesha kukejeli msimamo huo, Spika wa Bunge wakati akizungumza bungeni muda mfupi kabla ya kuahirishwa kwa Bunge, alijigamba kuwa Bunge lake bado lina meno.

Sitta alitamka; “Ni Bunge lenye meno” wakati akielezea uamuzi wa kuwatuma wabunge kwenda eneo la Loliondo lenye mgogoro kati ya wananchi na mwekezaji, mgogoro ambao serikali kupitia Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsha Mwangunga, iliwasilisha ripoti yake iliyotokana na kamati aliyounda kubaini kama kulikuwa na vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu.

Ripoti hiyo ya Mwangunga ilikataliwa na Bunge baada ya Waziri kueleza kuwa hapakuwa na haki za binadamu huku wananchi walioathirika wakieleza kuwa haki zao zilikiukwa, ikiwa ni pamoja na kuchomewa makazi na karaha nyingine zikiwamo za vitendo vya udhalilishaji wa wanawake.

Awali, kabla ya Spika kuingia bungeni kikao cha Bunge kilikuwa kikiongozwa na Mwenyekiti, Job Ndugai ambaye ni Mbunge wa Kongwa CCM, ambaye alionekana kutaka kuikubali ripoti hiyo ya Serikali kabla ya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka kusimama na kueleza Bunge kuwa kwa sehemu kubwa ripoti ya Waziri Mwangunga imejaa uongo na hivyo kuomba mwongozo wa Spika ili kutoa uamuzi utakaolinda maslahi ya wananchi.

Kutokana na uamuzi huo, Ndugai alikubali na kueleza kuwa atalifikisha suala hilo kwa Spika ambaye atatoa uamuzi na ilipofika kikao cha jioni siku hiyo, Spika akatoa msimamo kuwa atatuma timu ya wabunge kwenda Loliondo, hatua ambayo bila shaka mbele ya kina Kingunge itaendelea kumtafsiri Sitta kama kikwazo kwa mambo ya serikali kupita bila kujali yana maslahi ya wananchi au la.

Ripoti ya kamati ya Mwinyi inatarajiwa kuwasilishwa katika mkutano ujao wa NEC-CCM bila shaka baada ya kupitia mikononi mwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho.

Kwa muda mrefu kumekuwa na wito wa kutaka Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aenguliwe katika wadhifa huo kutokana na tuhuma mbalimbali zikiwamo za kuendelea siasa za makundi kwenye chama hicho. Kati ya matukio yanayomuhukumu Makamba ni kitendo chake cha kumlaani kada machachari wa CCM, Nape Nnauye, aliyejitokeza hadharani na kudai kuwa mkataba wa ujenzi katika jengo la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Upanga Dar es Salaam ni wa wizi na unaonyonya jumuiya hiyo.

Katika shutuma zake hizo, Nape alitaka baadhi ya viongozi wa Baraza la Wadhamini wa UVCCM akiwamo Edward Lowassa, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu na kujiuzulu kwa kashfa ya Richmond , awajibike. Makamba aliwatetea wadhamini hao akishirikiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Hata hivyo, suala hilo lilifikishwa kwenye NEC-CCM na uamuzi ulitolewa kuwa iundwe kamati kuchunguza na ikibidi kurekebisha mkataba huo. Kamati hiyo ilifanya marekebisho makubwa, uamuzi ambao kwa namna fulani unaathiri umakini wa Makamba katika utetezi wake kwa baadhi viongozi wanaodaiwa kuwamo katika kundi lake ndani ya CCM.

CHANZO: Raia Mwema

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.