31 May 2010


Ukisoma habari zifuatazo unaweza kukubaliana nami kuwa AKUTUKANAE HAKUCHAGULII TUSI.Katika habari ya kwanza tunashuhudia Waziri wetu wa Fedha akiongea vitu ambavyo vinaleta maana tu vikiangaliwa kwa maadnishi lakini sio mtaani.Na katika habari ya pili,tunashuhudia uzembe uliozoeleka wa kitokee kwanza kisha tufanye kitu flani.Yaani siku zote hizi mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kuongoza Jeshi la Polisi alikuwa hafahamu kuwa kituo cha polisi kisicho na silaha hakina tofauti simba wa karatasi!
Hebu soma habari husika hapa chini
Mkulo: Uchumi unazidi kukua 

Saturday, 29 May 2010 09:22

Exuper Kachenje

SERIKALI imesema kuwa ukuaji wa pato la taifa katika unakadiriwa kuongezeka na kwamba pato halisi litakua kwa asilimia 7 katika mwaka 2010.

Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2009 na mwelekeo katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2013 mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema kuna matarajio makubwa uchumi kuendelea kukua.

Huku akiwaomba radhi wabunge kwa kuchelewa kuwapa nakala ya taarifa hiyo, Mkulo alisema maelezo hayo yalipitishwa juzi asubuhi na Baraza la Mawaziri.

"Naomba radhi waheshimiwa kwa kuchelewa kuwapatia nakala ya taarifa hii kwa kuwa imepitishwa jana asubuhi (juzi) na Baraza la Mawaziri hivyo imechelewa kuchapwa," Mkulo alisema.

Mkulo alisema kuwa katika mwaka 2011, pato halisi la uchumi litakuwa kwa asilimia 7.1, mwaka 2012 asilimia 7.4 na hadi kufikia mwaka 2013 pato halisi la taifa litafikia asilimia 7.8.

“Kama ilivyotarajiwa athari za msukosuko wa uchumi zilikuwa za mpito, hivyo ukuaji wa pato la taifa unakadiriwa kuanza kuongezeka. Pato halisi litakua kwa asilimia 7.0 mwaka 2010, asilimia 7.1 mwaka 2011, asilimia 7.4 mwaka 2012 na kuendelea kuongezeka hadi asilimia 7.8 mwaka 2013,” alisema Mkulo.

Alifafanua kuwa malengo hayo yanatarajiwa kufikiwa kwa kutekeleza sera na misingi ya uchumi kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwemo mwenendo wa uchumi wa dunia na hitaji la kujenga uwezo kukabiliana na athari za msukosuko wa uchumi wa dunia.

Alitaja misingi mingine kuwa ni kuendelea kutengemaza vigezo muhimu vya uchumi jumla na maendeleo ya jamii hasa mfumuko wa bei, kuweka msukumo katika utekelezaji Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mkukuta awamu ya pili, Kilimo Kwanza na kuelekeza rasilimali kwenye maeneo chochezi ya uchumi kwa haraka zaidi.

Kwa mujibu wa Mkulo katika kipindi hicho miradi inayopewa kipaumbele katika mwongozo huo wa bajeti itakuwa ni pamoja na miundombinu, uendelezaji ardhi na makazi pamoja na vitambulisho vya taifa.

Vingine ni nishati, viwanda, sekta ya fedha na pia kutaja uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba mwaka huu kuwa ni kipaumbele cha kipekee kwa serikali katika mwaka huu kwa lengo la kuhakikisha unafanyika kama ilivyopangwa.
Waziri huyo alisema katika muda huo kasi ya upandaji wa bei inakisiwa kupungua hadi asilimia 8.0 kufikia mwezi Juni mwaka huu na kupungua zaidi hadi asilimia tano ifikapo Juni 2011.

Aidha, alisema katika kipindi hicho mapato ya ndani ya taifa yatafikia uwiano wa asilimia 17.3 kwa mwaka 2010/11; asilimia 17.4 mwaka 2011/2012 na asilimia 17.6 ifikapo mwaka 2012/2013.

Alisema serikali pia inalenga kuwa na akiba ya fedha za kigeni itakayokidhi uagizaji bidhaa kutoka nje na huduma kwa kipindi kisichopungua miezi mitano; kuwa na viwango imara vya ubadilishaji wa fedha; kuboresha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara na kuedeleza kilimo na kupunguza viwango vya riba.
Kuhusu biashara, Mkulo alisema Tanzania imeshuka katika vigezo vya urahisi wa kufanya biashara kutoka nafasi ya 126 kati ya nchi 183 na kuwa ya 131 mwaka 2009.

Kuhusu mapato ya ndani, Waziri Mkulo alisema yaliongezeka kwa asilimia 18.1 kufikia Sh4,293.1 bilioni mwaka 2008/09; kutoka Sh3,634.6 bilioni mwaka 2007/08 na kwamba kiasi hicho ni pungufu ya asilimia 10 kwa mwaka 2008/09.

Kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi 2010, mapato ya ndani yalifikia Sh3,490.3 bilioni ikiwa chini ya asilimia 8.7 ya makisio ya Sh3,924.9 kwa kipindi hicho akieleza kuwa hali hiyo ilitokana na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia.

Mkulo alisema kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi mwaka huu matumizi ya serikali yamefikia Sh6,143.9 bilioni kati ya makisio ya Sh6,718.7 kwa kipindi hicho, ikiwa ni upungufu wa asilimia tisa uliotokana na upungufu wa mapato.

Wakichangia maelezo hayo wabunge walitaka serikali ieleze itafanya nini kuwezesha wananchi kumiliki uchumi badala ya kumiliki asilimia 10 pekee kama ilivyo sasa.

CHANZO: Mwananchi

IGP Mwema afuta vituo

na Sitta Tumma na Ali Lityawi
SIKU tatu baada ya wananchi wa Kata ya Mbarika, wilayani Misungwi, mkoani Mwanza kuvamia kituo cha polisi na kuua majambazi watatu, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema ameanza kulikarabati upya jeshi hilo.
Tanzania Daima imethibitishiwa hilo; ukarabati wa jeshi hilo umelenga kuvipunguza kwa kuvifutilia mbali baadhi ya vituo vidogo visivyokuwa na silaha wala askari wa kutosha.

Wakati IGP Mwema akipanga kuvifumua vituo hivyo, jeshi la polisi mkoani Mwanza halijamkamata mtu hata mmoja kuhusiana na tukio la kuvamia na kuvunja kituo cha polisi Mbalika na kuua watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.

Akithibitisha yote hayo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanmza, Simon Sirro (RPC), alisema IGP Mwema yupo katika mikakati ya kupunguza utitiri wa vituo vidogo vidogo vya polisi, kwani vimeonekana havina faida kwa wananchi.

“Unajua vituo hivi vidogo visivyokuwa na silaha havina faida kwa maana hiyo mkuu wa polisi kwa sasa yuko katika mpango wa kuvipunguza.

“Mkakati huu madhumuni yake ni kuwa na kituo kimoja kila kata chenye silaha na askari wa kutosha,” alisema Kamanda Sirro.

Mei 27 mwaka huu majira ya saa 1:30 jioni, wananchi wa Mbalika, wilayani Misungwi mkoani hapa, walivamia na kuvunja kituo cha Mbalika kisha kuua watuhumiwa.

Moja ya sababu za wananchi hao kuvamia na kufanya mauaji katika kituo hicho, inaonekana ni kutokuwa na silaha pamoja na askari wa kutosha kituoni hapo na kumshtua IGP Mwema.

Kamanda Sirro, alipoulizwa mikakati ya kupunguza vituo hivyo, alisema hana jibu anayepaswa kulizungumzia ni IGP Mwema pekee.

Tanzania Daima, ilipomtafuta IGP Mwema kwa ajili ya kupata ufafanuzi zaidi, simu yake ilipokelewa na msaidizi ambaye alidai yuko mkutanoni.

“Afande IGP yupo kikaoni huku Kilolo mkoani Iringa; atakuwa Dar es Salaam kesho (leo),” alisema msaidizi huyo.



Tawala,viongozi na wafanyakazi wa African Star,Afro Euro Events Management, Buzzie Production, Manamba Studio na Urban Pulse. Wanatoa shukurani zao za dhati kwa Watanzania wote waliojitokeza usiku wa jana 29/05/2010 kwenye onyesho maalum la ‘£OVELY GAMBLE’ kuchangia watoto wanaoishi na vijirusi vya UKIMWI nyumbani Tanzania. Watoto hawa wanaangaliwa na TANZANIA MITINDO HOUSE. Hakika ya kweli mmeoonyesha umoja ambao tunauthamini na hatutousahau.

Vilevile tungependa kuwatambua watu wafuatao, ambao kwa njia moja ama ingine    wmesaidia sana kufanikisha Onyesho hili maalum

UBALOZI WA TANZANIA  (mama Balozi na Maafisa wote wa Ubalozi)
TANZANIA ASSOCIATIONS zote Kitaifa na matawi  ya Reading, Birmingham na Soctland
BONGO FLAVOUR (Dixon na Flora)
TMH (Khadija Mwanamboka)
SWIFT FREIGHT (Abu Faraji)
SWAHILI TRAVEL AGENCY (Tino)
VINCENT BAR (Kalinga na Gado)
MAMA MAYOR (Mariam Nice)
NOCHA SEBE
MISS YVONNE
WITENGERE KITOJO 
TEGEME CHAMPANDA
FRANCIA CHENGULA
FREDDY MACHA
AYOUB MZEE
RASHIDI KAWAWA
ALLY MUHIDINI
GLOBAL PUBLISHER (Abdalah Mrisho)
BONGOSTARLINK (Dj Choka)
JIACHIE (Ahmad Michuzi)
KULIKONI UGHAIBUNI ( Evarist Chahali)
MISS JESTINA GEORGE (Tina George)
FASHION 8020 (Shamim Mwasha)
NURU THE LIGHT (Nuru)

Vyombo hivi na Watanzania hawa wamekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha Onyesho hili maaaluma la mchango wa kihiyari. Mungu awaongezee na tuendeleze umoja  huu.


            MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU WABARIKI WATANZANIA

29 May 2010

Mama Mpendwa,

Ilikuwa saa 4.30 usiku,tarehe 29 Mei 2008 ulipotutoka.Nakumbuka nilipopigiwa simu kufahamishwa kuwa Bwana Amekutwaa,nilidhani ni ndoto tu.Japo ulikuwa umepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu kabla ya kukumbwa na mauti sote tuliamini kuwa siku moja ungeamka ukiwa mzima.Mama,japo leo ni miaka miwili tangu ututoke,bado nahisi niko ndotoni na nimeshindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba haupo nasi.Mara kwa mara nakuona ndotoni,lakini napoamka nagundua ni ndoto tu,na hiyo inazidisha uchungu na majonzi.

Baba Mzee Chahali,uliyeishi nae katika ndoa kwa miaka 50,anaendelea kukukumbuka mno.Ni vigumu zaidi kwake kukabiliana na kututoka kwako kwa vile ulikuwa ni rafiki yake mkuu,mtu wake wa karibu kabisa na kila kitu kwake kama ilivyo kwetu.Mapacha, Kulwa (Peter) na Doto (Paul) nao wameendelea kuwa na wakati mgumu kwa vile wewe ulikuwa zaidi ya mama yao.Walikutania,walicheka nawe,walikusaidia kazi za nyumbani,walikwambia furaha na majonzi yao,na waliringa kuwa na mzazi mwenye upendo kama wewe.

Japosiku zote  tangu ututoke tumekuwa na wakati mgumu sana,siku hii ya leo tunapoadhimisha miaka miwili ya kifo chako ni ngumu zaidi kwetu.Inaleta kumbukumbu zisizoelezeka na zisizostahimilika.

Kazi ya Mungu haina makosa.Tukijiuliza sana kwanini alikuchukua wakati bado tunakuhitaji sana tutakuwa tunakufuru.Tunajaribu kujifariji kwa kuamini kuwa alikuchukua kwa vile alikupenda zaidi yetu.Na tunajitahidi pia kujiridhisha kuwa huko ulipo unapata pumziko la amani na unaangaziwa mwanga wa milele ukistarehe kwa amani.Japo haupo nasi kimwili lakini siku zote tupo nawe kiroho.

Pumziko la Milele Akupe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Akuangazie Ustarehe Kwa Amani,Amen.


ONYESHO MAALUM LA FILAMU £OVELY GAMBLE 
TAREHE 29TH OF MAY 2010. 
 KARIBUNI KUCHANGIA YATIMA WALIOATHIRIKA NA UKIMWI TANZANIA NA JUMUIA YETU YA TANZANIA

VILEVILE KUTAKUWA NA CHAKULA, VINYWAJI, BURUDANI YA MIZIKI NA VICHEKESHO.
NYOTE MNAKARIBISHWA NA KUFIKA KWENU NDIO KUFANIKISHA SHUGHULI HII. TUNAWAOMBA MJE KUSAIDIA WATOTO HAWA NA JUMUIYA YETUWETU.

DRESS CODE: LADIES: DRESS GLAMOROUS AND ELEGANT  GENTS: SMART

MUSIC: LIVE MUSIC, AFRO BEAT, BONGO FLAVOR, HIP HOP, MDUARA AND RNB

WYCLIFFE VENUE 233 KINGS ROAD READING RG1 4LS. 6.30pm-11.30pm

TCKT IN ADVCE £10 FOR VIP’s SEATS AND £5 FOR STANDARD SEATS. (*VIP TCK HOLDERS GETS FREE AFTER PARTY PASS*)

TCKT ZA PAUNDI 5 ZINAMALIZIKA WAHI MAPEMA

‘£OVELY GAMBLE DVD AND SOUNDTRACK OUT NOW’

DVD MAALUM “DIRECTORS CUT” WITH BONUS MATERIAL
*FILMMAKERS
*HATAKAMA
*SEXY MAMA

WOTE MNAKARIBISHWA
---------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

27 May 2010


Baraka Baraka ndio mhariri (Editor) wa £ovely Gamble. Huyu Bwana ni Photograher, Director na Producer. Amesha fanya kazi kwenye uzalishaji wa vipindi vingi ambavyo vimeshaonyeshwa katikaTelavisheni tofauti Uingereza na Ulaya kama vile OBE TV, MATV na TVT (ZE COMEDY London Special). Baraka pia ni mkali wa na advertising shot films kama vile ‘KARMA’ na ‘The ONE’ vilevile amesha Direct documentary programmes za kisiasa kama ‘A PATH TO WAR’ na za kijamii kama IN A ‘FOREIGN LAND’

Kwenye upande wa Photography amebobea kwenye fani ya fashion and advertsing. Kijana huyu ana freelance na kampuni tofauti za media na advertising agencies ikiwa ni pamoja na prestigious PUBLIC LTD. Baraka ameshawahi kufanya maonyesho (Exihbition) ya kazi zake za Photohgraphy mara tatu sasa. Hivi sasa anajitayarisha kushoot shot film iitwayo ‘JIKO LA SAIDI’ . Pia anakuwa moja ya wamiliki wa URBAN PULSE CREATIVE ya hapa UK.

Mahojiano haya (hapo juu) yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK. Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gambl kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU
WYCLIFF
233 KINGSROAD,
READING, RG1 4LS


TANGAZO MAALUM
KWA WAKAZI WA WA UGHAIBUNI
KUTOKA URBAN PULSE NA BUZZIE  PRODUCTION
Mashabiki na Wapenzi wa filamu wa Kitanzania tunapenda kuwataarifu kuwa tumepokea malalamiko yenu kuhusu ubora DVD za filamu ya £ovely Gamble.  Kwamba zina  giza na sauti  si bora  na picha zinacheza. Hili tumelichunguza na kugundua ya kuwa  linasababishwa na DVD HARAMIA (PIRATE COPIES) zinazouzwa kinyume ya sheria.

Tunaelewa tatizo hili ni sugu dunia nzima na  linawanyima thamani ya utamu wa filamu.  Vilevile lina changia kudumisha kiwanda cha uzallishaji wa filamu. Kuepukana na adha hii ,Wazalishaji wa £ovely Gamble wanawaomba na kuwashauri kununua  filamu hii kutoka kwa DVD za halali zitakazopatikana kuanzia Jumamosi ya tarehe  29-10-2010 kwenye  uzinduzi maaluma wa kuchangia yatima wanao ishi na vijirusi wa UKIMWI  nyumbani TANZANIA  na kwa wakala maalumu  watakao tangazwa rasmi   siku hiyo

DVD MAALUM “DIRECTOR'S CUT”  WITH BONUS MATERIAL
*FILMMAKERS
*HATAKAMA
*SEXY MAMA

                    WYCLIFFE VENUE                                                                                                           
233 KINGS ROAD                                                                                              
        READING RG1 4LS.                                                                                                       
 6.30pm-11.30pm
TCKT IN ADVCE £10 FOR VIP’s SEATS AND £5 FOR STANDARD SEATS. (*VIP TCK HOLDERS GETS FREE AFTER PARTY PASS*)
WOTE MNAKARIBISHWA


26 May 2010


Rennison Okenwa ndio kichwa kilicho Direct movie £ovely Gamble. Rennison-au maarufu kama 'Renny'- ni ndugu yetu kutoka Kenya. Huyu jamaa ndio aliyekuja na wazo la kue-xperiment namna ya kutumia picha na muziki kuelezea hadithi. Renny ni msomi wa uzalishaji wa vipindi vya television aliyehitimu katika chuo kikuu cha Thames Valley. Renny ameshatengeneza documentary programmes mbili kuhusu vifaa vya hospitali na kuhusu matatizo ya magonjwa ya akili. Kwa sasa ana shoot documentary kuhusu wazazi watoto 'Young Mums'

Mahojiano haya yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK.

Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gamble kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU Usiku.
WYCLIFFE VENUE,
233 KINGS ROAD,
READING, RG1 4LS

WATANZANIA WOTE WA UK MNAKARIBISHWA
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

Tanzania imeshuhudia vituko vingi mwezi huu wa Mei,kutoka Rais Kikwete kutetea takrima  hadi mtumishi wa Bwana Askofu Kilaini kudai kuwa Kikwete bado ni chaguo la Mungu,kutoka sakata la Masauni kufoji umri (oh Mungu, inawezekanaje?) hadi kifungo cha Liyumba (wengine wanadai alistahili kunyongwa kabisa).Na kutoka kauli ya Waziri Kombani kuwa daraja la mto Kilombero litajengwa katika awamu ya pili ya Kikwete (as if JK ameshashinda uchaguzi) hadi ajali ya gari la msafara wa JK.Makala hii inajaribu kuibua maswali kuhusu hili la mwisho,yaani ajali hiyo.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari,uchunguzi mkali unaendelea ku-establish chanzo cha ajali hiyo.Lakini wakati uchunguzi huo ukiendelea tayari kuna wingu limeigubika ajali hiyo huku kukiwa na maswali kama ilitokana na hujuma,au uzembe au ni bahati mbaya tu.

BAHATI MBAYA: Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi,ajali hiyo ni bahati mbaya.Gazeti la Tanzania Daima limemnukuu Msika akisema, “Tunaamini ni ajali ya bahati mbaya ambayo ilisababishwa na matatizo ya kiufundi, lakini jambo la kushukuru kiongozi wetu hakupata madhara kwa matukio yote mawili.” Yah,inawezekana ni bahati mbaya.Lakini kichekeksho ni pale Msika kutoa kauli hiyo kabla ya uchunguzi.Majibu rahisi katika maswali magumu?Well,hiyo ndio Bongo yetu.Kauli hiyo ya Msika inaweza kupewa nguvu na kauli nyingine iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Salva Rweyemamu,aliyenukuliwa na gazeti hilohilo la Tanzania Daima (toleo la Jumapili) akisema "hitilifu za magari alizokabiliana nazo Rais Kikwete zilikuwa ni za kawaida".Again,tunashuhudia watu walokabidhiwa dhamana muhimu wakikurupuka kutoa majibu mepesi hata kwenye masuala nyeti.Yani kuchomoka tairi ya gari la kiongozi wa nchi ni kitu cha kawaida!Au ni kwa vile ajali kubwa zimezoeleka sana kiasi kwamba hiyo ya msafara wa JK inaonekana 'cha mtoto'?

HUJUMA: Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,kamanda Msika haamini kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hujuma.Anasema, "Nasisitiza hatuamini kama kulikuwa na hujuma na ndiyo maana hatutafanya uchunguzi kuhusu matukio yote mawili, lakini kwa suala kama kulikuwa na uzembe wa ukaguzi wa gari, mtafute Salva (Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu), ndiye anaweza kulizungumzia.” Kwa mara nyingine tena tunashuhudia Msika akitoa majibu ya hisia zake (na pengine Jeshi analoongoza) badala ya kusubiri matokeo ya uchunguzi wa kitaalam.Hivi kulikuwa na ugumu gani kwa Msemaji huyo wa jeshi la polisi kutoa jibu lenye mantiki kwamba 'tusubiri matokeo ya uchunguzi badala ya kufanya guesswork'?
Tanzania Daima linakwenda mbali zaidi na kuihusisha ajali hiyo na matukio ya mbalimbali ambapo Rais amekuwa akipewa taarifa potofu (rejea Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na taarifa za vikao kati ya TUCTA na Serikali).Kwa mtizamo mpana,gazeti hilo linajaribu kueleza kuwa yayumkinika kuhisi kuwa ajali hiyo ni muendelezo wa 'hujuma' zinazofanywa dhidi ya Rais Kikwete.

Kwa bahati mbaya (au kwa makusudi) Watanzania hawatapata fursa ya kujua ukweli kuhusu tukio hilo.Kwanini nahitimisha hivyo?Well,labda mwenzangu umeshasahau kuhusu ripoti ya chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala.Najua kwa wengine,nikitaja Mbagala wanakumbuka zaidi kuhusu mwana-Bongofleva Diamond kuliko ukweli kwamba kuna wenzetu walipoteza maisha yao,tukaambiwa tume imeundwa kuchunguza milipuko hiyo,tukaonyeshwa picha ripoti ikikabidhiwa kwa waziri husika,na hadithi ikaishia hapo.Na kama hufahamu,tume iliyoundwa kuchunguza milipuko hiyo ilitumia fedha za walipa kodi.Sasa sijui wana-tume waliamua kufanya uchunguzi wao baa kisha 'kutokana na kilevi' wkaafikiana kuwa hakuna haja ya kuweka hadharani ripoti hiyo.

UZEMBE: Ni rahisi zaidi kuhisi kuwa ajali hiyo sio bahati mbaya au hujuma bali ni uzembe kwa kuangalia mlolongo wa matukio ya uzembe yanayojiri mara kwa mara.Kwa bahati mbaya,au makusudi,baadhi ya matukio hayo yanamhusisha Rais Kikwete moja kwa moja.Hebu angalia ishu ya Masauni,kwa mfano.Katika kudhibiti songombingo kati ya (Benno) Malisa na Bashe huko UVCCM,JK alionelea ni vema Mwenyekiti wa Umoja huo atoke Zanzibar.Na huyo ndiye Masauni.Kwa hiyo tunapozungumzia 'fojari' ya umri wa Masauni tunapaswa pia kukumbuka nani aliyemuibua.

Lakini tofauti na uzembe uliozoeleka katika shughuli mbalimbali za serikali,huu wa ajali ya gari la Rais hauwezi kuhusishwa na rushwa.Unajua,mara nyingi neno 'uzembe' linatumika kupunguza makali ya neno 'rushwa'.Yaani,utaskia mtu flani 'alifanya uzembe kusaini mkataba flani' lakini ukweli ni kwamba mtu huyo hakuwa mzembe bali alikuwa makini katika kuhakikisha teni pasenti inakwenda kwenye akaunti yake.

Kwanini ajali hii inaweza kuwa matokeo ya uzembe?Kwa wenye ufahamu wa usalama wa kiongozi kama rais,gari analotumia linapewa uangalizi wa hali ya juu kama ilivyo kwa afya,ustawi na usalama wake kwa ujumla.Kuna mlolongo wa watu (wanaolipwa vizuri tu) wanaowajibika kuhakikisha kuwa kila atakachotumia rais kipo katika hali nzuri (na ya juu kabisa).Sitaki kuingia kwa undani sana katika hili kwa sababu zangu binafsi,lakini nachoweza kusema hapa ni kuwa kuna wazembe flani ambao hawakutilia maanani hitilafu zilizojitokeza katika chombo cha usafiri wa rais.

Tatizo linaloweza kuwa limepelekea uzembe huo ni MAZOWEA.Nadhani kuna wanaokumbuka masahibu yalomkumba JK wakati wa kampeni yake huko Mwanza mwaka 2005.Naamini pia kuna wanaokumbuka balaa lilomkumba Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi pale aliponusurika kupigwa akiwa msikitini jijini Dar.Nahisi pia kuna wengi wanaokumbuka habari za msafara wa Kikwete kurushiwa mawe huko Mbeya.Matukio yote hayo yanaweza kuhusishwa na ajali hii ya gari la Rais,na yote yananyooshea kidole uzembe mahala flani.

Nihitimishe makala hii kwa kuusia kwamba matukio kama hilo la ajali ya gari la Rais yataendelea kutokea kama tutaendelea kukabidhiana majukumu kwa minajili ya urafiki (au kishkaji,kama wasemavyo mtaani.Tunapoweka kando professionalism na kuruhusu umimi tutambue kuwa tunajichimbia kaburi letu sie wenyewe.Ujuzi na uzoefu hauwezi kuwa replaced na udini,urafiki au kujuana.

Mwenye macho na asome,mwenye masikio na asikie.

You have been warned!

25 May 2010


Kijana ambaye yuko kwenye £ovely Gamble anaitwa Kisiri Elly anacheza part ya Frank. Huyu actor chipukizi wa Kitanzania ambaye ameingia katika fani ya usanii wa filamu. Kisiri amecheza filamu hii na staa za kitaaluma unaweza kufikiri ni mzoefu wa siku nyingi. Hivi tuzungumziavyo kesha tafutwa na Nollywood na ataanza production ya 'Man Alone' itakayotengenezewa Lagos na London shooting itaanza August mpaka September. Tumfagilie mbongo huyu ambaye anaanza career hii kwa kasi.

Mahojiano haya yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK.

Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gamble kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU Usiku.
WYCLIFFE VENUE,
233 KINGS ROAD,
READING, RG1 4LS

WATANZANIA WOTE WA UK MNAKARIBISHWA
-------------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.