20 Aug 2011




Thank you so much from the bottom of my heart to all my fans.

LAST NIGHT THE SPORAH SHOW WON AN AWARDS FOR THE FACE OF 2012  SPECIAL RECOGNITION AWARDS ON WORLD HUMANITARIAN DAY 19TH AUGUST 2011 AT  THE ROYAL BOROUGH OF KENSINGTON & CHELSEA.

Sporah Sporah in the building.


The World Humanitarian Day is a celebration of people helping people. Every day humanitarian aid workers help millions of people around the world no matter who they are or where they are. The day recognizes the sacrifices and contributions of those who risk their lives to give others help and hope.


 WALKING THE ROOM..!


YES! WE WON IT..!

Sporah Accepting The Award from Dorothy.!

 All thanks goes to our adoring fans who watch The Sporah Show on TV, follow us on Twitter, Facebook, Blog etc day in and day out.

Special thanks goes to all my entire team who work tirelessly on this production.


RECOGNITION IS GREAT WHEN IT COMES FROM ANYONE.!



 SPORAH ON INTERVIEW WITH OTHER PRESS AFTER RECEIVING THE AWARD.!

 The Sporah show would like to thank Dorothy and the Team for Organising the Awards, and of course to YOU, You Guys make The Sporah Show What It Is..! Thanks for your continuing support, we could't have done this without you..!  

I LOVE YOU, I LOVE YOU, I LOVE YOU ALL XOXO



19 Aug 2011




Raia Mwema Ughaibuni
Walalahoi Uingereza, sawa na wa Tanzania, ni ‘bomu’
Evarist Chahali
Uskochi
17 Aug 2011
Toleo na 199
  • Lisipoteguliwa na watawala hulipuka
  • Ghasia za Tottenham ni kengele ya uamsho
KATIKA makala ya wiki iliyopita, nilizungumzia vurugu zilizotokea katika kitongoji cha Tottenham, jijini London, hapa Uingereza. Kadhalika nilijaribu kuzihusisha vurugu hizo na mazingira yalivyo sasa huko nyumbani na kutoa wito kwa watawala wetu kufanya kila wawezalo kutatua matatizo yanayowakabili Watanzania ambayo yanaweza kusababisha vurugu kama hizo.
Hata hivyo, wakati naandaa makala hiyo vurugu hizo zilikuwa zimetawala Tottenham pekee. Lakini kwa takriban siku tano tangu zianze, ziliweza kusambaa maeneo mbalimbali ya London na hatimaye kuvuka mipaka hadi miji ya Liverpool, Birmingham, Manchester na mingineyo.
Kwa bahati nzuri sie huku Scotland tumenusurika. Na katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama uhusiano wa ‘paka na panya’ kati ya Scotland na England, Waziri Mkuu (First Minister) Alex Salmond, alitahadharisha watu walioziita vurugu hizo ‘za Uingereza’ (UK riots) na kuwakumbusha kuwa hazijaigusa Scotland, Wales au Ireland ya Kaskazini; bali England pekee. Kwa hiyo, Salmond alitaka vurugu hizo ziitwe ‘za England’ (English riots).
Baada ya takriban siku tano zilizoshuhudia uharibifu mkubwa na vifo vya angalau watu watano, hatimaye polisi walifanikiwa kuzizima japokuwa hadi sasa bado hali haijarejea kuwa shwari kabisa.
Zaidi ya watu 1,000 wameshafikishwa mahakamani na wengine kuhukumiwa. Mahakama zinazoendesha kesi dhidi ya washiriki wa vurugu hizo zimelazimika kufanya kazi hadi usiku kukabiliana na msongamano wa watuhumiwa.
Waziri Mkuu wa Uingereza (nzima), David Cameron, alilazimika kukatisha likizo yake ili kutoa tamko na kuendesha mjadala Bungeni kuhusu vurugu hizo. Takriban kila mwanasiasa aliyezungumzia vurugu hizo aliwalaani wahusika na kuhitimisha kuwa hakuna maelezo mengine zaidi ya uhalifu mtupu (sheer criminality).
Licha ya Kamisheni Huru ya Malalamiko dhidi ya Polisi (Independent Police Complaint Commission) kukiri bayana kuwa taarifa za awali kwamba kulikuwa na kurushiana risasi kati ya Mark Duggan (Mwingereza Mweusi aliyeuawa na polisi kwa risasi na hatimaye kusababisha vurugu hizo) na polisi si sahihi (marehemu alikutwa na silaha lakini hakuwafyatulia risasi polisi), ‘makosa’ hayo ya polisi yalifunikwa na shutuma na laana zilizoelekezwa kwa waliohusika kwenye vurugu hizo.
Kimsingi, vurugu hizo zilipoanza katika kitongoji cha Tottenham zilihusisha zaidi Weusi. Na hata ziliposambaa kwenye maeneo mengine ya jiji hilo bado wahusika wengi walikuwa Weusi. Hata hivyo, kadri zilivyosambaa ndivyo tulivyozidi kushuhudia picha kwenye vyombo vya habari zikiwaonyesha Weupe kadhaa wakishiriki kwenye uporaji ulioambatana na vurugu hizo.
Kwa baadhi yetu, licha ya kutopendezwa na vurugu hizo, uwepo wa Weupe ulileta ahueni kidogo; kwani ni siri iliyo wazi kwamba kila baya linalofanywa na asiye Mweupe (Non-Whites) ‘linaongeza shehena ya silaha kwenye ghala la chuki dhidi ya kila asiye Mweupe.’ Mifano ni mingi lakini hapa nitaonyesha machache.
Kwa mfano, huko Marekani ambapo mtikisiko wa uchumi unaisumbua nchi hiyo vilivyo, kuna wanaoamini kuwa tatizo ni rais Mweusi, Barack Obama. Lakini ukweli ni kwamba matatizo ya kiuchumi ya nchi hiyo yalianza zama za mtangulizi wa Obama; yaani ‘Mweupe’ George W. Bush.
Na mfano unaoweza kutoa picha halisi ya double standards (viwango vinavyokinzana) ni tukio la kinyama kabisa la kigaidi lililotokea mwezi uliopita nchini Norway ambapo mhusika, ‘Mweupe’ Anders Behring Breivik, aliwaua kinyama zaidi ya watu 70. Mara baada ya kupatikana kwa habari za kusikitisha kuhusu tukio hilo, wachambuzi walikurupuka na kubashiri kuwa wahusika wangekuwa “Waislamu wenye msimamo mkali.”
Wachambuzi hao wakajitahidi kadri wawezavyo kubainisha sababu mbalimbali zinazowafanya kuamini kuwa kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa wahusika ni “magaidi wa Kiislamu.”
Wakajaribu kuhusisha hasira za Waislamu dhidi ya mchora katuni wa Kidenishi aliyechora kikaragosi cha kumkashifu Mtume Muhammad S.W.A na kusababisha maandamano sehemu mbalimbali duniani. Kwa nini tukio lililotokea Udenishi lisababishe shambulizi ‘la kigaidi’ Norway? Jibu wanalo wachambuzi hao.
Wakajaribu pia kuhusisha uwepo wa majeshi ya nchi za Magharibi huko Afghanistan, na sababu nyingine kadha wa kadha; alimradi kuongeza nguvu kwenye ubashiri wao.
Bahati nzuri, kama wasemavyo Waswahili, Mungu hamfichi mnafiki. Baada ya muda si mrefu ikafahamika kuwa mhusika wa ugaidi huo alikuwa sio tu Mnorway; bali pia ni Mweupe, na tena ni muumini wa Ukristo wenye mrengo mkali (Christian Fundamentalism) na mfuasi wa siasa za mrengo mkali wa kulia (far-right politics).
Pamoja na majonzi yaliyowakumba wengi kutokana na mauaji hayo ya watu wasio na hatia, lakini taarifa kwamba mhusika hakuwa Muislamu zilileta ahueni kubwa.
Lakini kama ilivyo katika matukio mengine ya kigaidi yaliyofanywa na Weupe, ukajitokeza ‘utetezi’ kuwa Breivik (muuaji) “alikuwa ni chizi tu, na wala hakusukumwa na Ukristo wake wala itikadi yake ya siasa za chuki dhidi ya wageni na Waislamu.”
Licha ya gaidi huyo kuchapisha mtandaoni ‘ilani’ yake yenye kurasa 1,500 (siku chache kabla ya mashambulizi yake ya kigaidi) ambapo alibainisha chuki aliyonayo dhidi ya wageni na Waislamu na kuweka wazi kuwa ‘angefanya kitu fulani kikubwa kuleta ufumbuzi’, bado watetezi wake wameendelea kumtenganisha na siasa za mrengo mkali wa kulia na Ukristo wa msimamo mkali.
Tukirejea kwenye vurugu za Uingereza, tayari dalili zimeanza kujitokeza kuwa wa ubaguzi wa rangi watafanya kila wawezalo kumhusisha mtu Mweusi na vurugu hizo.
Ni kweli kuwa vurugu zilichipuka kutoka katika maandamano ya amani ya baadhi ya watu kwenye Jumuiya ya Weusi katika baadhi ya vitongoji vya London. Lakini kila aliyeshuhudia vurugu hizo zikipamba moto aliona wahusika wa rangi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Weupe.
Majuzi, mwanahistoria maarufu wa hapa, David Starkey, aliwachefua watu wengi alipodai kuwa vurugu hizo ni matokeo ya ‘Weupe kugeuka Weusi.’ Kimsingi, hoja yake ni kwamba vurugu ni kasumba ya mtu Mweusi, na Weupe wanaojihusisha na vurugu ni matokeo ya ‘maambukizo’ ya kasumba hiyo kutokana na mwingiliano wa kijamii kati ya Weusi na Weupe. Inachefua!
Kwa upande mwingine, ‘majibu’ ya watawala wa hapa wakiongozwa na Waziri Mkuu Cameron yanaonekana kuelemea zaidi kwenye kukabiliana na matokeo badala ya chanzo. Cameron amekuwa akizungumza kwa ukali dhidi ya ‘wahalifu’ waliosababisha vurugu hizo; huku akinuia kupambana nao kwa nguvu zote.
Lakini Profesa wa Historia ya Wakati Huu (Modern History), Robert Gildea wa Chuo Kikuu cha Oxford anabainisha kuwa “wanasiasa na vyombo vya habari wameongoza msafara wa kulaani walioshiriki vurugu kama wahalifu, wendawazimu na wasio na maadili. Hii ni lugha ya matabaka tawala yanapokabiliwa na vurugu za kijamii, kuwaharamisha wanaonyanyaswa kama wahalifu wa anasa dhidi ya jamii yenye amani, lengo likiwa kuwaadhibu wanyanyaswa hao na kuwatenga zaidi.
Cameron na Wahafidhina wenzake wana kila sababu ya kuwabebesha lawama ‘wahalifu’ hao; kwani baadhi ya wachambuzi wanazihusisha vurugu hizo na hatua ya serikali kubana matumizi kutokana na mtikisiko wa uchumi wa dunia, ambapo wahanga wakubwa wameendelea kuwa tabaka la walalahoi.
Kwa kuaminisha umma kuwa vurugu hizo ni uhalifu tu, Cameron na serikali yake atakuwa amefanikiwa kuepusha lawama dhidi ya hatua zinazochukuliwa na serikali yake kubana matumizi na madhara yake kwa jamii.
Kadhalika, kwa bahati mbaya au makusudi watawala wameamua kufumbia macho tatizo la ubaguzi wa rangi ambalo ndio kilio kikubwa cha jamii za Wasio Weupe, na kwa wengi ni sababu kuu ya kuibuka kwa vurugu hizo.
Vilevile, uwezekano kwamba baadhi ya walalahoi wa Uingereza wanaona kama wamesahauliwa na tabaka tawala, na hivyo kusubiri kwa hamu fursa za kuonyesha hasira zao, pia unaelekea kupuuzwa.
Kama nilivyoeleza wiki iliyopita, kuna mengi ambayo watawala wetu huko nyumbani wanaweza kujifunza kutoka kwenye vurugu hizi na jinsi watawala walivyozishughulikia.
Historia inatufundisha kuwa amani inayotawala licha ya uwepo wa lindi la ubaguzi, ukandamizwaji na umasikini, ni sawa na bomu la muda linalosubiri tu wakati lilipuke. Kama tabaka tawala Uingereza litapuuzia vyanzo halisi vya vurugu hizo (ubaguzi, umasikini, nk), basi, ni suala la muda tu kabla hatujashuhudia vurugu nyingine.
Katika mtizamo huo huo, iwapo watawala wetu huko nyumbani wataendelea kuamini katika amani ya kukosekana vurugu; ilhali kuna mamilioni ya Watanzania wasio na amani matumboni na mifukoni mwao (kutokana na umasikini), basi, nasi tunaweza kujikuta katika hali mbaya kama hii iliyojiri hapa.
Tunaweza kusema ‘Mungu aepushie mbali’, lakini tukumbuke kuwa mara nyingi Mungu huwasaidia wale wanaojisaidia wenyewe kwanza.


Your #1 classified AD listing site
Copyright © 2011 ADVERTISING DAR, All rights reserved. 
 

18 Aug 2011



 Mimi ni Mtanzania halisi niliyezaliwa miaka 38 iliyopita jijini Arusha maeneo ya Sanawari. Niliamia hapamiaka 5 iliyopita baada ya kuonana na mme wangu kupitia njia kama hii (Cyber-love). Nina motto 1 na ninaishi maisha tu ingawa ni ya kawaida. Hivyo nimeona ni vyema nikatoa nafasi kama kwa watanzania wengine ambao wangependa vilevile kuonana na marafiki wengine popote duniani kupitia blog hii ya WabongoMeet.

Wabongomeet ni blog ya Kitanzania inayotoa mwanya kwa watanzania mahali popopo kujitafutia marafiki, wachumba mume/mke ulimwenguni kote. Mnakaribishwa bila ubaguzi wowote. 

AKINA DADA MNAKARIBISHWA NAWAPA MOYO ZAIDI KUTEMBELEA HAPA http://wabongomeet.blogspot.com
Kwa wale wote ambao watapenda kuweka picha pamoja na info zao tafadhali tuma kwa kupitia email [email protected], Pia nakaribisha maoni yenu.



 
By Georgina Littlejohn
Last updated at 4:56 PM on 17th August 2011


He's managed to transform Valletta and Falmouth into a world dealing with the aftermath of a global zombie war.

And this week the post-apocalyptic scenes witnessed in by locals in Malta and Cornwall have now come to Glasgow, as Brad Pitt and his crew bring the living dead to the Scottish city.

The city centre has been transformed into Philadelphia for scenes for the actor's upcoming movie World War Z.
It's looking good, everyone! Brad Pitt talks to crew members as he arrives on set in Glasgow to start filming scenes for World War Z
It's looking good, everyone! Brad Pitt talks to crew members as he arrives on set in Glasgow to start filming scenes for World War Z

And Brad, 47, was right in the thick of it all as he chatted to his crew and watched as the streets were turned into the US city.

Cochrane Street has been renamed John F Kennedy Boulevard and American road signs and street names were put up while yellow taxi cabs and white police cars lined the streets as Philadelphia came to life.
Keep up the good work: Brad looked happy with the set as he chatted to crew members
Keep up the good work: Brad looked happy with the set as he chatted to crew members

Working hard: Crew members line the street and get the lighting and the cameras ready
Working hard: Crew members line the street and get the lighting and the cameras ready

Glasgow was chosen to double as the Pennsylvanian city because of the huge similarities between them including the architecture, wide roads and grid layout of the cities.

Local people have been recruited as zombie extras and Glasgow City Council said the production will involve almost 1,200 people and the impact on local economy is expected to be more than £2 million.
Ready for your close-up, Mr Pitt? Brad is directed as he prepares for what could be a car chase scene
Ready for your close-up, Mr Pitt? Brad is directed as he prepares for what could be a car chase scene

Buckle up: Brad gives one last look out of the car door before shooting the scene
Buckle up: Brad gives one last look out of the car door before shooting the scene

The film Brad's latest film is a post-apocalyptic horror film based on the novel of the same name by Max Brooks.

Brad plays Brooks who scours the world collecting the stories and experiences of those who have survived ten years after the human victory over the world wide zombie epidemic.
Read all about it: Crew members carry American newspaper boxes on to the set
Read all about it: Crew members carry American newspaper boxes on to the set

The means streets of Philadelphia: Glasgow is unrecognisable as yellow taxis and American cars line the city's roads
The means streets of Philadelphia: Glasgow is unrecognisable as yellow taxis and American cars line the city's roads

Reclaiming the streets: Crew members climb aboard a cherry picker to put up American road signs
Reclaiming the streets: Crew members climb aboard a cherry picker to put up American road signs

Marc Forster, who directed Bond classic Quantum Of Solace, is the man behind the lens, while Mireille Enos, who plays leading lady Sarah Linden in The Killing, will play Brad's wife.
Brad arrived in the city yesterday with partner Angelina Jolie and their six children - Maddox, 10, Pax, seven, Zahara, six, Siloh, five and three-year-old twins Vivienne and Knox - having chartered a Virgin train from London.
Forces united: A Glaswegian police officer looks inside a white Philadelphia police car
Forces united: A Glaswegian police officer looks inside a white Philadelphia police car

Coming through: An actor playing an American traffic cop weaves his way through the taxis
Coming through: An actor playing an American traffic cop weaves his way through the taxis

The A-list couple and their six children were snapped arriving at Euston station this morning in a large black people carrier and surrounded by bodyguards and members of their entourage.
When they arrived in Glasgow at 2.30pm, silver vehicles with tinted glass were allowed onto platform 11 to whisk them away from a waiting crowd.
And action! Actors and extras take their positions
And action! Actors and extras take their positions

In character: Actors dressed as a policeman and a homeless man get ready for their scenes
In character: Actors dressed as a policeman and a homeless man get ready for their scenes
In character: Actors dressed as a policeman and a homeless man get ready for their scenes

Who ordered the meat? Locals stand around and watch the action as a delivery truck arrives on set
Who ordered the meat? Locals stand around and watch the action as a delivery truck arrives on set

Speaking to the Scottish Sun, a fan who had been waiting for them to arrive said: 'There were dozens of screaming fans waiting patiently for a glimpse. After all, it's not every day you can say you've seen a Hollywood movie star in Glasgow Central Station.

'But a glimpse was about all people were going to get because no sooner were they off the train than they were straight into some fancy people carriers and off.
You'll need another coat: Rain washes away newly painted crossing lines
You'll need another coat: Rain washes away newly painted crossing lines

Landmark: Workers put up signs for Philadelphia's famous suspension bridge
Landmark: Workers put up signs for Philadelphia's famous suspension bridge
'Cops and security were trying their best to keep the crowds at bay and it would have been nice if the couple had just waved or something. But even the kids had their heads down.'
The couple are believed to be staying the Carnell Estate Mansion near Kilmarnock and will make the 16th century home theirs for their next few weeks.
Famous commuters: Angelina Jolie walks down the platform with daughter Shiloh while Brad carries his youngest daughter Vivienne
Famous commuters: Angelina Jolie walks down the platform with daughter Shiloh while Brad carries his youngest daughter Vivienne
Famous commuters: Angelina Jolie walks down the platform with daughter Shiloh while Brad carries his youngest daughter Vivienne


Sosthenes Nyoni
SIMBA, Simba ndio ulikuwa wimbo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada vijana hao wa mtaa wa Msimbazi kulipinza kisasi kwa ukifunga Yanga mabao 2-0 kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.

Simba waliofungwa kwenye Kombe la Kagame na Ngao ya Jamii mwaka jana vijana hao wa Mganda Moses Basena walizinduka na kupata mabao ya mapema kupitia kiungo Haruna Moshi 'Boban' dakika 15 na penalti ya Felix Sunzu dakika 38.

Simba iliyoanza kwa kasi mchezo huo ilifanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia kwa Moshi 'Boban' aliyemalizia vizuri krosi ya kutoka upande wa kushoto iliyopigwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Sunzu aliyekuwa na ushirikiano mkubwa na Emmanuel Okwi.

Mshambuliaji Sunzu alifungia Simba bao la pili kwa mkwaju wa penalti baada ya Nadir Haroub kumchezea vibaya Moshi 'Boban', kwenye eneo la hatari dakika 35. Sunzu alilazimika kuonyesha ueledi wake pale alipotakiwa kurudia penalti hiyo baada ya mwamuzi Israel Mjuni kusema Kado alitokea kabla ya kupigwa kwa penalti ya kwanza pamoja na kuwa alikuwa amefunga.

Kocha Moses Basena aliyeonekana kujifunza kwa makosa alitumia mfumo wa 4:2:3:1 na kutoa nafasi kubwa kwa Okwi, Haruna na Sunzu kutawala sehemu kubwa ya kiungo tofauti na ilivyokuwa kwenye fainali ya Kombe la Kagame.

Okwi alifanya atakalo mbele ya mabeki wa Yanga walionekana kuwa kama watu waliozidiwa na mazoezi na kukosa unyumbulifu mchezoni, huku safu ya ulinzi wa Simba chini ya mkongwe Victor Costa aliweza kuwapoteza mchezoni kabisa mshambuliaji Keneth Asamoah na Jerry Tegete.

Kiungo Haruna Niyonzima alijitahidi kuonyesha uwezo mkubwa wa kutawala mpira na kujaribu kutafuta goli kwenye mechi yake ya kwanza ya watani wa jadi, lakini alikosa msahada kutoka kwa wenzake.

Simba ilianza mashambulizi kwa kasi na dakika kwanza Okwi alikosa bao baada ya shuti lake kumgonga Haroub na kupaa juu ya goli.

Okwi alipoteza nafasi nyingine dakika 8 baada ya kuwalamba chenga mabeki wa Yanga, lakini aliugonga mpira mbele zaidi na kipa Shaaban Kado akauwahi.

Beki wa Yanga, Chacha Marwa, nahodha Shadrack Nsajigwa alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Okwi. Naye Juma Nyoso wa Simba alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Asamoah.

Haruna Niyonzima alipiga shuti la umbali wa mita 25 baada ya kumchungulia Juma Kaseja kwa bahati mpira huo ulipaa juu ya goli.

Kipindi cha pili Yanga iliamka baada ya kuingia Hamisi Kiiza na Rashid Gumbo lakini walishindwa kuipenya ngome ya Simba.

Yanga waliendeleza sera yao ya kugomea jezi za wadhamini wa ligi Vodacom zenye nembo nyekundu kwa kuvaaa jezi za mdhamini wao TBL tofauti na Simba wenyewe walivaa zile walizopewa na Vodacom

Vikosi Yanga; Shaaban Kado, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Chacha Marwa, Juma Seif, Godfey Taita, Haruna Niyonzima, Keneth Asamoah/ Gumbo, Jerry Tegete, Kigi Makasi/ Kiiza.

Simba: Juma Kaseja, Said Nasoro, Amir Maftah, Juma Nyoso, Victor Costa, Partick Mafisango, Salum Machaku/ Kiemba, Jerry Santo, Felix Sunzu, Haruna Moshi/ Gervais Kago, Emmanuel Okwi/ Kapombe.

CHANZO: Mwananchi

17 Aug 2011

Taxi za Manjano Glasgow zikitengeneza mandhari ya Philadelphia,Marekani.Yote ni maandalizi kwa ajili ya filamu ya World War Z inayorekodiwa hapa Glasgow lakini kwa minajili ya kutengeneza mandhari ya Philadelphia,Marekani.

Mjini kati (City Centre) Glasgow kukibadilishwa kuendana na mandhari ya Philadelphia

Alama za usalama barabarani za Mjini Kati Glasgow zikibadilishwa ili zishabihiane na za Philadelphia

Brad Pitt na patna wake Angelina Jolie ndani ya Glasgow

Treni ya kukodi ya kampuni ya usafiri ya Virgin iliyowaleta Pitt na patna wake Angelina Jolie na watoto wao.Hapa ni Stesheni Kuu ya Glasgow (Glasgow Central Station)

Brad Pitt


15 Aug 2011


Nadhani suaskia stori kadhaa kuhusu mama wakwe.Wajuzi wa ndoa wanadaia ukitaka ndoa ivunjike basi mruhusu mkeo amlete mama yake muishi pamoja.Sijui kwanini,lakini mama wakwe ni watu wanaotazamwa kama vyanzo vya matatizo kwenye ndoa.

Sasa leo katika pita pita zangu mtandaoni nimekutana na tangazo huko Gumtree ambapo kuna jamaa ameweka tangazo kuwa "anamtoa mama mkwe wake bure." Kwa Kiingereza chenye lahaja ya Kiskotishi tangazo husika linasomeka hivi:


Free Mother In Law
Glasgow

MOANY, GREETIN' FACED!!!!!! USES YOUR WASHING MACHINE ALL THE TIME FOR NOTHING....... DESPERATE TAE GET RID OF HER!!!!! APPLY A.S.A.P.


Sasa,kama yeye mwenye mkwe yamemshinda,anatarajia nani atakayekubali kupokea mtambo huo wa kuzalisha gubu?

13 Aug 2011




Bonyeza picha hapo juu kupelekwa moja kwa moja kwenye blogu ya MtotoSix.tk

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.