13 Feb 2012

12 Feb 2012


Whitney Houston, who found fame as one of pop’s biggest voices, has died. She was 48.
Houston died Saturday afternoon, a representative for the singer told the Associated Press. Houston’s death comes on the eve of the Grammys and on the night of Clive Davis’ annual pre-Grammy gala, at which she performed last year and was expected to attend this year.
No cause of death has been announced and law enforcement sources said the singer was found in a hotel room at the Beverly Hilton, where emergency medical personnel were called sometime Saturday.
The Hilton is the scene for Davis’ annual gala. On Thursday, Houston dropped by the rehearsals to offer vocal tips for Brandy and Monica, who were slated to be one of the evening’s headliners.
Press, including The Times, were in attendance for a junket with the reunited R&B divas and Davis. Though Houston greeted people her with a warm smile, she appeared disheveled in mismatched clothes and hair that was dripping wet with either sweat or water.
The visibly bloated singer displayed erratic behavior throughout the afternoon -- flailing her hands frenetically as she spoke to Brandy and Monica, skipping around the ballroom in a child-like fashion and wandering aimlessly about the lobby. It was mentioned by a Grammy staffer that security personnel received calls of the singer doing handstands by the pool.
After leaving rehearsals, Houston returned to the ballroom -- with her teenage daughter Bobbi Kristina in tow -- as camera crews set up for interviews. The singer smelled of alcohol and cigarettes. A Grammy staffer said that during the interviews with Brandy, Monica and Clive, Houston was dancing just off camera to make the singers and Davis laugh. Grammy personnel expressed concern that she'd be caught on camera, and that reporters would write about her behavior.
Finally her daughter pulled Houston out of the room, and the singer skipped off. In our post of the event, we called Houston's behavior "loose and lively."
“She really loves and supports us both. For me, I went through a lot of very tumultuous moments and she would show up, not just with a phone call but physically when I needed,” Monica said when we asked about Houston coaching them. “That's something that I've carried with me, especially with all that she's been going through over the years herself. She's never turned her back on the people she cared about.”
Later that evening Houston appeared at Hollywood nightclub Tru, for fellow R&B singer Kelly Price’s pre-Grammy party. "Kelly Price & Friends Unplugged: For the Love of R&B" served as both a celebration and a jam session to preserve that genre, which was scaled back from eight categories to four this year.
Houston was billed as one of the evening’s special invited guests but after her appearance earlier it was shocking to see the singer arrive. More put together in her appearance, Houston briefly sang a duet with Price. In what has become her final performance, clips of the two singing a gospel hymn made the rounds because of the singer’s unsteady vocals.
SOURCE: Los Angeles Times

And below is my most favourite Whitney's song GREATEST LOVE OF ALL



11 Feb 2012

Rais Kikwete na Lundo la Mawaziri Wanaounda Kabineti yake ya wababaishaji

Bunge letu linalosheheni walafu mia tatu na ushee ambao licha ya kutugharimu mamilioni kila mmoja wanataka fedha zaidi
Na hii ndiyo hali halisi ya umasikini wetu duniani





Source: Daily Mail


Uongo una tabia moja kuu: usipokanushwa huweza kujenga hadhi ya kuonekana ukweli.Ni kwa sababu hiyo,mara nyingi siruhusu kitu kisicho na ukweli kiachwe kuishi na hatimaye kionekane ni cha kweli.

Nilipoingia kwenye ukurasa wangu wa Twitter hapo jana nilikumbana na tweets za waungwana wawili, Bwana @semkae na Ndugu @chiume, ambapo pasipo kuingia kiundani kunukuu kila walicho-tweet,waliniona kiojakwa mambo mawili: kwanza, "kuingizwa mkenge" kunukuu tweets za Rais Jakaya Kikwete kwenye makala yangu katika toleo lililopita la jarida la Raia Mwema,na pili,kuandika "nilifanya maongezi yasiyo rasmi na Rais Kikwete."

Nianze na hilo la pili.Tofauti na ilivyokuwa nyakati za Zama za Mawe ambapo njia pekee ya mawasiliano ilikuwa kukutana uso kwa uso,maendeleo ya teknolojia sasa yanawezesha mawasiliano kwa njia mbalimbali kama vile barua-pepe,SMS,mitandao ya jamii,nk.Kwa watu wenye mawazo ya kale,ukisema NIMEONGEA NA FLANI basi kwao lazima iwe aidha maongezi hayo ni ya barua kupitia posta,uso kwa uso au (kidogo) SMS au e-mail.Kwa mtizamo wa watu hao,ukijadiliana na mtu huko Facebook au Twitter basi huna haki ya kusema MMEONGEA.Kwao maongezi ni lazima ufumbue mdomo na maneno yatoke mdomoni kama si maandishi kwenye barua,nk.

Chanzo cha nukuu husika ni swali nililomuuliza Rais kuhusiana na mkanganyiko uliojitokeza kuhusiana na suala la posho za wabunge.Nilijibiwa na mheshimiwa,na kwa vile makala yangu katika toleo lililopita la Raia Mwema ilikuwa inazungumzia suala hilo basi sikuona ubaya wa kunukuu majibu hayo ya Rais Kikwete (pasipo kupunguza au kuongeza neno).Na kwa kuondoa utata,nikaandika "nilifanya MAZUNGUMZO YASIYO RASMI na Rais kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter kwa kumuuliza...."

Sikuandika hivyo kwa minajili ya kutaka sifa kuwa "eeh nimeongea na Rais..." bali kama muumini wa kuthibitisha hoja kwa mifano hai ilikuwa muhimu kuambatanisha nukuu hizo.

Lakini pengine kuwafumbua macho waungwana hawa kuelewa kuwa katika zama tunazoishi hata tweet ya kiongozi inaweza kuchukuliwa kama tamko lake rasmi,angalia taarifa ifuatayo ya Shirika la Utangazaji la Kenya ambalo (kama nilivyofanya mie) walinukuu tweet ya Rais Kikwete

Kama KBC walinukuu tweet ya Kikwete na haikuwa tatizo kwa @semkae na @chiume kwanini basi matumizi yangu ya nukuu ya aina hiyohiyo iwe tatizo?

Twende kwenye hoja ya kwanza kwamba handle ya @jmkikwete sio ya Rais Jakaya Kikwete.Awali ilidaiwa kuwa inatumiwa na timu yake ya mitandao ya kijamii lakini kadri mjadala ulivyoendelea ikadaiwa kuwa hiyo handle ya @jmkikwete ni feki,huku wengine wakiita ni mzimu.

Hoja baada ya hoja.Hivi kweli pamoja na madudu mbalimbali yanayoendelea huko nyumbani,inawezekana kweli mtu mmoja akakurupuka na kujiita Jakaya Kikwete,Rais wa Nne wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,na asichukuliwe hatua?


Lakini hata tukikutana na hoja kama "ah kama wameshindwa kuwakamata majambazi wa Kagoda wataweza kumkamata huyu anayejifanya Rais Kikwete huko Twitter?" bado kuna hoja nyingine kadhaa zinazoweka nguvu kwenye ukweli kuwa @jmkikwete ni Rais mwenyewe.

Hebu bonyeza LINK HII na utapelekwa kwenye ukurasa wa Social Good Summit iliyofanyika jijini New York Marekani kuanzia tarehe 19 hadi 22 Septemba mwaka jana.Kwenye ukurasa huo,ukishuka hadi profile ya mtoa mada (speaker) wa 31 utakutana na picha na wasifu mfupi wa Rais Kikwete.Chini ya maelezo hayo kuna link ya akaunti yake ya Twitter.Guess what?Ni hiyohiyo @jmkikwete ambayo @semkae na @chiume wanadai ni feki.

Kila mtoa mada ameweka link ya social media profile zake.Sasa kwanini Rais Kikwete atumie profile ya mtu hewa?Halafu habari husika imewekwa kwenye tovuti ya Mashable ambayo kwa anayefuatilia teknolojia na social media atakuwa anaelewa fika hadhi yake mtandaoni.Au nao waliingizwa "choo cha kike" (kunukuu kebehi ya @chiume)?


Ukienda kwenye ukurasa husika  na hatimaye kwenda kwenye wasifu wa Kikwete,ukibonyeza 'kindege cha Twitter' utapelekwa @jmkikwete.Hiyo ina maana gani?Tuwaachie @semkae na @chiume watueleze

Lakini hata kama hiyo si hoja ya msingi,ukienda kwenye ukurasa wa profile @jmkikwete ambayo hadi sasa ina followers 11336 (yani watu wote hawa nao wameingizwa "choo cha kike"?) utakuta watu na taasisi zenye heshima waki/zikimufata @jmkikwete.Kuanzia CCM hadi Chadema,Mbowe hadi  Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Salva Rweyemamu na Ubalozi wa Uingereza huko nyumbani.Lakini kubwa zaidi ni familia ya Kikwete mwenyewe,yaani mkewe Mama Salma na wanae Ridhiwani na Miraji.Yaani hata familia ya Kikwette nayo inamfuata @jmkikwete 'feki'!!!!?????

Na MAKALA HII kutoka Rwanda inatanabaisha kuwa Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi wachache wa Afrika-pamoja na marais Paul Kagame na Jacob Zuma-ambao wapo Twitter.Je @semkae na @chiume wanaweza kutwambia kama @jmkikwete sio Rais Kikwete then anatumia handle gani?

Talking of Zuma,waungwana hao walidai kuwa kinachowafanya waamini kuwa @jmkikwete si Rais Kikwete ni kwa vile akaunti hiyo haijawa verified.Wanasema hayo ilhali wao wenyewe akaunti zao haziko verified lakini tunaamini tunao-interact nao ni wao halisi.Na kama suala ni verification,mbona hata Rais Zuma naye akaunti yake ya Twitter (@therealjz) sio verified?Au naye ni mzimu?Hoja mfu hazina uhai mrefu kabla ya kurejea tena kaburini.
La mwisho,na ambalo nisngependa kuingia kwa undani ni vyanzo vyangu binafsi.Kila mmoja wetu ana past yake.Kwa sababu za kimaadili,huwa sipendi kuzungumzia past yangu.Ninachoweza kuandika hapa ni kwamba kupitia past hiyo nimeweza kuthibitisha mambo mbalimbali kabla siyaandika kwenye makala zangu.Na licha ya past hiyo,hakuna kitu ninachoepuka kwa nguvu zote kama kupotosha wasomaji wa jarida lenye heshima kubwa huko nyumbani la Raia Mwema.Mara nyingi ninalazimika kuwapigia simu angalau watu wawili hadi watatu kabla sijaandika makala ili kuhakikisha kuwa ninachoandika ni sahihi.Na watu hao ninaowauliza ni vyanzo vya uhakika kabisa.Lakini kwa mtu mbishi anaweza kudai huo pia ni uzushi...au kwa kunukuu nkauli ya Bwana @semkae, ni MISREPRESENTATION tu.

Nakuachia msomaji ufikie hitimisho mwenyewe.



Taarifa Kwa Umma Na Madaktari Wote Nchini Juu Ya Maamuzi Yaliyofikiwa Leo February 9

9 Feb 2012

Nani anasema ukweli kuhusu posho za wabunge?

WIKI iliyopita inaweza kuingia katika vitabu vya historia ya nchi yetu kufuatia mlolongo wa matukio yanayozidi kuashiria kuwa hali si shwari katika uongozi wa nchi yetu.

Tukio la kwanza lilikuwa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu kukanusha habari kwamba Rais Jakaya Kikwete ameshasaini kuridhia ongezeko la posho za wabunge kutoka shilingi 70,000 kwa siku hadi shilingi 200,000.

Kukanusha huko kulifuatia taarifa kwamba Spika Anne Makinda aliwaambia wandishi wa habari kwamba Rais alikuwa ameridhia posho hizo, na kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwaaambia wabunge kwamba Rais alikubali posho zilipwe.  

Binafsi, nilibahatika kufanya maongezi yasiyo rasmi na Rais Kikwete kwenye mtandao wa  jamii wa Twitter. Kama ilivyoeleza taarifa ya Kurugenzi ya Ikulu, Rais Kikwete alieleza kwamba (namnukuu), “Upo mkanganyiko na upotoshaji mkubwa kuhusu jambo hili. Wengi hawaelewi bado. Litatolewa ufafanuzi kwa kina.

Jibu hilo lilitokana na ombi langu kwa Rais ambapo niliandika (ninajinukuu), “Mheshimiwa Rais, ninakusihi umwajibishe ‘mtoto wa mkulima (Waziri Mkuu Pinda) kwa kukuchonganisha na umma eti umebariki posho...

Kadhalika, Rais alifafanua kwamba (namnukuu) “Nilitoa maelekezo kuhusu suala la posho za wabunge. Maelekezo hayo hayakuwa kuridhia jambo hilo.” Baada ya tweet hiyo Rais aliongeza, “Nilikubali haja ya kuangalia upya posho kwa wabunge na niliwataka wabunge kutumia busara na hekima katika kutafakari hili...Wabunge watumie kikao cha Februari cha Bunge kulizungumzia suala hili. Ni muhimu.

Kabla ya kuendelea na mjadala kuhusu suala hili sina budi kumpongeza Rais, si tu kwa majibu yake ya kistaarabu bali pia kuchukua muda wake kusoma na kujibu tweets mbalimbali zinazoelekezwa kwake.
Kwa tabia ya kimungu-mtu iliyozoeleka miongoni mwa viongozi wetu wengi wa Kiafrika, ni nadra sana kwa Rais kufanya mawasiliano na wananchi wa kawaida hasa katika mitandao ya jamii.

Yawezekana kabisa kuwa maelezo yake hayajakidhi shauku ya Watanzania wengi kufahamu nani anasema ukweli lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba kwa kutumia muda wake adimu kulizungumzia suala hilo ‘katika maongezi yasiyo rasmi’ ni jambo linalostahili pongezi.

Lakini pamoja na majibu hayo mazuri ya Rais, wananchi wengi bado wanatatizwa na mkanganyiko wa kauli za viongozi kuhusu posho za wabunge.

Kuna maswali kadhaa ambayo hayana majibu hadi sasa (licha ya ufafanuzi wa Rais).Hivi inawezekana kweli Waziri Mkuu kuzusha kuwa Rais aliridhia ongezeko hilo la posho? Ukisoma maelezo ya Rais ‘kati ya mistari’ (between the lines) unaweza kuhisi kuwa labda Pinda hakuyaelewa vizuri maelekezo ya ‘bosi’ wake. Lakini kama ukweli ndio huo, kwanini basi Makinda aje na maelezo mapya? Na kwanini Pinda amekuwa kimya hadi leo?

Binafsi ninaona kuwa suala hili linaweza kumalizwa na Rais Kikwete kwa kuwakumbusha wabunge kuwa japo maombi ya nyongeza ya posho zao yanaweza kuwa ya msingi, ukweli ni kwamba hayaendani na hali halisi ya uchumi wetu.

Na majuzi Rais Kikwete ameeleza waziwazi kuwa serikali yake inakabiliwa na hali ngumu kifedha alipozungumza katika maadhimisho ya Siku ya Sheria, ambapo miongoni mwa wageni waalikwa alikuwa Spika Makinda. Je, inawezekana Rais alikuwa anafikisha ujumbe ‘kistaarabu’ kwa Spika?
Wito wa safu hii kwa Rais Kikwete ni mwepesi na mfupi: huko nyuma alishaweka bayana kuwa tabasamu lake lisitafsiriwe vibaya, na urais wake hauna mbia. Kutegemea hekima na busara za wabunge kujadili maslahi yao ni sawa kabisa na kuwasihi mafisadi waionee huruma nchi yetu. Wabunge wanaopiga kelele kutaka nyongeza ya posho wapo ‘out of touch’ na hali halisi ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.
Haiwezekani kuwasihi watumie hekima na busara wakati wameshaonyesha tangu mwanzo kuwa wana uhaba wa vitu hivyo linapokuja suala la posho.

Mwanzoni mwa makala hii nimeandika kuwa wiki iliyopita ilikumbwa na mlolongo wa matukio na hadi muda huu nimeongelea tukio moja tu. Kwa kifupi, matukio mengine yanayoweza kuonyesha kuwa ombwe la uongozi wa taifa letu linazidi kuwa kubwa ni pamoja na habari zilizopatikana kutoka bungeni Dodoma kuwa Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo ‘aligoma’ kujibu swali aliloulizwa na Spika. Kichekesho ni kwamba japo Spika Makinda amejijengea umaarufu kwa kuliendesha Bunge kwa ‘mkono wa chuma’ dhidi ya wabunge wa vyama vya upinzani katika tukio hilo hakuchukua hatua yoyote dhidi ya Waziri Mkulo.

Kana kwamba hiyo haikuwa ‘kali kubwa ya wiki,’ taarifa zinaeleza kuwa wabunge wa CCM waligoma kukutana na Rais Kikwete kuzungumzia muswada wa mabadiliko ya Katiba, ambapo inasemekana wabunge hao wamedhamiria kuikwamisha.

Je, wabunge hao wamegoma kwa sababu wamechukizwa na kauli ya Rais kuwa hajaridhia matakwa yao ya nyongeza ya posho? Taarifa zinaeleza kuwa sababu iliyopeleka hatua hiyo ni mtizamo wa wabunge hao kuwa marekebisho yaliyofanywa kwenye muswada huo yatapelekea CCM kuangushwa na CHADEMA. Pia inaelezwa kuwa wabunge hao hawajapendezwa na kitendo cha Rais kukubaliana na mapendekezo ya CHADEMA katika maboresho ya muswada huo.

Japo sisi tusio wana-CCM hatuna haki ya kuingilia mambo ya ndani ya chama hicho, lakini kwa vile ni chama tawala na chochote kinachokihusu kinamgusa takriban kila Mtanzania, ni muhimu kukemea utovu huo wa nidhamu ambao unaweza kutafsiriwa tu kuwa ni njama za wazi za kumkwaza Rais kuleta mwafaka wa kitaifa utakaosaidia kuiongoza nchi yetu katika njia sahihi.

Nimalizie makala hii kwa kumkumbusha Rais Kikwete kuwa licha ya kuwa Mwenyekiti wa taifa wa CCM yeye ni Rais wa Watanzania wote.

Kamwe asiruhusu maslahi ya waroho na walafi wachache yaathiri maslahi ya Watanzania wote pasipo kuangalia itikadi zao za kisiasa.

Kadhalika, ninawasihi wazalendo wote (bila kujali tofauti zetu) kumuunga mkono Rais Kikwete katika masuala yenye maslahi kwa Watanzania wote hata kama yeye mwenyewe amelea matatizo haya na sasa yanataka kutupeleka kubaya.

Lakini ili Rais aweze kupata sapoti hiyo ni muhimu na yeye aamue ‘liwalo na liwe,’ lakini Tanzania kama nchi ni muhimu kuliko mtu binafsi au kikundi cha walafi wachache.

8 Feb 2012


Habari za kazi Wadau, poleni na majukumu ya ujenzi wa Taifa.
Kufuatia tatizo la kiufundi lililojitokeza hapo nyuma blogu yako ya Mamapipiro ilishindwa kuendelea na utendaji wake, nawaomba radhi wadau wangu wote ambao mlikosa kupata matukio muhimu ya michezo na burudani kwa zaidi ya wiki moja,hivyo kwa sasa mambo yamekaa sawa hivyo endeleleeni kuperuzi blogu yenu kwa habari kem kem za michezo na burudani kupitia www.mamapipiro.blogspot.com.
Natanguliza shukrani zangu za dhati!



Huku mgomo wa madaktari ukiendelea kushika kasi,kuna dalili kwamba walimu nao wanaelekea kuchukua hatua hiyo kutokana na taarifa za magazeti ambapo wamekumbushia kilio chao cha muda mrefu kuhusu maslahi yao.

Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,toleo la leo Jumatano,walimu wametoa wito kwa serikali kutekeleza matakwa yao ya maboresho ya maslahi huku wakitaja viwango wanavyostahili kulipwa.

Habari kamili ni hii hapa chini

Walimu wawasha moto mpya
• WATAKA MISHAHARA YA 900,000/-
na Datus Boniface

WIMBI la wafanyakazi wa umma kudai nyongeza ya mishahara, posho na marupurupu limechukua sura mpya baada ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kupendekeza viwango vipya vya mishahara wanavyopaswa kulipwa walimu. 
CWT kimesema mwaka wa fedha unaoanza Julai mwaka huu kinataka kuwe na ongezeko la asilimia 100 kwa walimu wote kulingana na viwango vya madaraja yao, ambapo wa Cheti (Daraja A), anatakiwa kulipwa sh laki tano, stashahada alipwe sh laki saba na nusu na yule wa shahada alipwe zaidi ya sh laki tisa. 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kwa niaba ya Rais wa CWT, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Ezekiah Oluoch, alisema ongezeko hilo linatokana na kupanda kwa gharama za maisha. 
“Tumefanya tathmini na kujiridhisha kuwa mapendekezo yetu yanawezekana, serikali inaweza kutulipa fedha hizo kwa sababu ina rasilimali za kutosha,” alisema. 
Oluoch alisema mapendekezo hayo yametokana na kikao cha Baraza la Taifa la chama hicho lenye wajumbe 163 wanaowakilisha walimu katika mikoa 21, kilichoketi Januari 31 hadi Februari mosi mjini Morogoro. 
Alibainisha kuwa baraza la taifa limeagiza kuwa majadiliano kuhusu nyongeza ya mishahara yaanze mara moja na yawe yamekamilika mwishoni mwa Machi mwaka huu. 
Alisema wanataka majadiliano hayo yafanywe mapema ili serikali iyaingize makubaliano kwenye bajeti yake ya mwaka huu. 
Oluoch alisema CWT inaamini kuwa majadiliano ni njia pekee ya kupata mwafaka wa ongezeko hilo la mishahara. 
Malipo ya posho
CWT inahitaji kulipwa kwa posho za kufundishia na za mazingira magumu kwa walimu hao, kwa kuwa muda wa kazi zao ni tofauti na watumishi wengine wa umma. 
Kinataka walimu wote wapewe posho ya asilimia 55 kwa walimu wa masomo ya Sayansi na asilimia 50 wa Sanaa, na posho hizo zianze kulipwa kuanzia Julai. 
CWT kimesema kuwa nyongeza ya posho hizo si ngeni kwani Rais Jakaya Kikwete aliwapa ahadi hiyo Siku ya Walimu Duniani Oktoba 5, mwaka 2010. 
Olouch alisema posho ya mazingira magumu, inatakiwa kulipwa kwa asilimia 70 kwa mwalimu anayefanya kazi maeneo ya vijijini, kama utekelezaji wa ahadi ya Rais Kikwete aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Walimu Duniani Oktoba 2010. 
Madeni yasiyohusiana na mishahara
CWT kimeitaka serikali kuwalipa walimu fedha zao za madeni yasiyohusiana na mishahara kabla ya Februari 15 na iwapo itashindwa kufanya hivyo, chama hicho kitachukua hatua dhidi ya waajiri waliokaidi makubaliano yaliyofikiwa. 
Oluoch aliongeza kuwa awali walikubaliana na serikali kuhusu utaratibu wa kulipa madeni hayo ambayo walihakiki kwa pamoja, wakishirikiana na viongozi wa serikali wa ngazi za wilaya, ambapo sh bilioni 22.5 zilitumwa kwenye halmashauri za wilaya na sh bilioni 3.5 zilitumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. 
Alibainisha kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha alitoa waraka ambao umetafsiriwa vibaya na baadhi ya watendaji wa serikali. 
Aliongeza kwamba, baadhi ya watendaji wametafsiri kinyume kuwa ni kuhakiki upya madai ya walimu badala ya kujiridhisha kama anayelipwa ndiye aliyehakikiwa. 
Alisema utata huo umechangia halmashauri 50 kutowalipa fedha walimu licha ya kuzipata fedha hizo. 
Kulipwa madeni ya mishahara
CWT kinataka kufanyike marekebisho yote ya mishahara na malipo ya mapunjo yafanyike ndani ya mwezi huu bila kukosa. 
Oluoch alisema CWT ilifanya kikao na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Simfue Ombeni, Januari 13 mwaka huu na serikali ilitoa taarifa ya kulipwa kwa walimu 18,000 kiasi cha sh bilioni 18. 
Aliongeza kuwa CWT kupitia Baraza lake limesikitishwa na kauli ya serikali ya kukosa fomu hizo huku serikali ikificha ukweli, kwani tatizo linafahamika na kwamba walimu wengi hawajarekebishiwa mishahara yao baada ya kupanda madaraja. 
Chama hicho kimetaka kufutwa kwa waraka wa serikali wa kupunguza zoezi la upandishwaji wa madaraja kwa asilimia 50 kutokana na maelezo kuwa serikali haina pesa. 

Kama nilivyoandika kwenye makala yangu katika toleo la wiki iliyopita la jarida la Raia Mwema,moja ya madhara ya muda mrefu ya mgomo wa madaktari ni kutoa hamasa kwa watumishi wengine wa umma kudai haki zao kwa njia ya mgomo.

Kwa upande mmoja,iwapo serikali itasalimu amri na kutekeleza matakwa ya madaktari,kuna uwezekano mkubwa wa watumishi wa umma katika sekta nyingine nao kudai watendewe haki kama madaktari (iwapo madai ya matabibu hao yatatimizwa na serikali).

Kwa upande mwingine,hata kama madai ya madaktari yataendelea kupuuzwa,umoja na mshikamano wa wataalamu hao wa afya za binadamu unaweza kuwafanya watumishi wengine wa umma kujiuliza mara mbili kwanini nao wasifuate mkumbo.

Hakuna anayetaka kuona migomo ikitawala nchi yetu lakini kwa makusudi kabisa serikali imeonyesha wazi kuwa inathamini zaidi matakwa yasiyo ya lazima ya wabunge kuliko watumishi wengine wa umma ambao licha ya kuwa na mishahara midogo wanakabiliwa na matatizo chungu mbovu,kubwa likiwa uhaba wa vitendea kazi na makazi duni.Ikumbukwe kuwa wabunge wanaolipwa mamilioni kwa kupiga porojo bungeni wanapatiwa kila huduma na mazingira yao ya kazi ni mithili katika nchi zilizoendelea.

Sijui hatma ya harakati hizi za watumishi wa umma kudai haki zao itakuwaje lakini ni muhimu kuikumbusha serikali kwamba kuna tawala kadhaa zilizoanguka kutokana na ngumu ya migomo ya wafanyakazi.

7 Feb 2012


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.