11 Dec 2012


Baada ya kufanikiwa kutengeneza Android App ya blogu hii, sasa ni zamu ya Blackberry App. Jinsi ya kuizpata apps hizi ni rahisi. Kwa wasomaji mnaotumia smartphones za Android, cha kufanya ni kwenda kwenye Google Play (zamani Android Marketplace) kisha search (tafuta) 'CHAHALI BLOG'

Njia nyingine nyepesi ni ku-download app hiyo ya Android ya blog hii kwa kubonyeza hapo kwenye ukurasa mkuu wa blogu hii ambapo kuna mahala pameandikwa DOWNLOAD CHAHALI BLOG ANDROID APP kisha bonyeza hapo chini palipoandikwa'GET IT ON Google Play'

Kwa upande wa CHAHALI BLOG BLACKBERRY APP, unawezakuipata app hiyo kwenye Blackberry App World kisha search CHAHALI BLOG

Njia nyingine ni kamahiyo ya App ya Android, yaani nenda kwenye ukurasa mkuu wa blogu hii kisha nenda hapo palipoandikwa DOWNLOAD CHAHALI BLOG BLACKBERRY APP kisha bonyeza chini yake palipoandikwa 'Get it at Blackberry App World.'

KARIBUNI SANA


10 Dec 2012


SHOW  ITAKUWA ON AIR KESHO TAREHE DECEMBER 10th, 2012 FOR THE 1ST TIME EVER AT 10:30PM ON SKY 182, AND EVERY MONDAY AT 10:30PM ON SKY 182

9 Dec 2012

Nilizaliwa tarehe kama ya leo, miaka makumi kadhaa yaliyopita. Siku yangu ya kuzaliwa 'inagongana' na siku ya kuzaliwa kwa taifa letu la Tanzania (au Tanganyika?) tulipopata uhuru tarehe 9 Disemba mwaka 1961.

Tofauti na wengineo ambao haudhimisha siku za kuzaliwa kwa pati, mie hutilia mkazo zaidi katika sala (kumshukuru Mungu kwa kunijalia miaka yote hiyo,na kumwomba anibariki nipate miaka zaidi) na kufanya tafakuri ya wapi nimetoka,nilipo na ninakoelekea.

Kwa 'somo' wangu Tanzania, yeye birthday yake ni tofauti kabisa na yangu japo tuna-share tarehe moja (ila miaka tofauti). Mwenzangu huadhimishiwa siku yake kwa gwaride na hotuba mbalimbali.Lakini pia kwa vile birthday ya Tanzania inamgusa kila Mtanzania, sikuhii inakuwa na umuhimu wa kipekee kufanya tathmini ya taifa limetoka wapi, lipo wapi na linaelekea  wapi.

Kwabahati mbaya (au pengine kwa makusudi ya wenzetu wachache) kila inapojiri birthday ya Tanzania tunajikuta na maswali mengi zaidi kuliko majibu.Wengi wanajiuliza kwanini tuendelee kuwa masikini wa kutupa ilhali tuna kila aina ya utajiri.Kwamtizamo wangu, wa kulaumiwa zaidi si viongozi tuliowapa dhamana ya kutuongoza bali 'uzembe' wetu wakuchagua viongozi pasi kuzingatia kama wataweza kututumikia kwa dhati na uadilifu.

Enewei, hii sio siku ya kuandika makala ndefu. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia kumaliza na kuanza mwaka mwingine huku nikitarajia baraka zaidi kutoka Kwake. Nwashukuru pia wazazi wangu, Baba  Mzee Philemon Chahali na marehemu mama Adelina Mapango kwa kunizaa. Pasi mapenzi ya Mungu na wazazi wangu hao leo nisingekuwepo kuadhimisha siku hii ya kuzaliwa.Nawashukuru piawanafamilia wenzangu,ndugu,jamaa na marafiki kwa kuniwezesha kufika hapa nikiwa hai.

Nawashukuru pia ninyi mnaotembelea blogu hii kwani mmekuwa sehemu ya familia yangu ya kijamii tangu mwaka 2006. Baadhi yenu tunafahamiana,baadhi yenu hatufahamiani lakini kwa umoja wenu mmenifanya kuwa mwenzenu na kupita eneo hilimara kwa mara.

Shukrani pia kwa watu mbalimbali niliofahamiana nao aidha kupitia uandihi wa makala au kwa kukutana kwenye mitandao ya kijamii, hususan Twitter na Facebook.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI 

7 Dec 2012


MOJA ya kumbukumbu muhimu katika uchaguzi mkuu uliopita wa Marekani, ni ile ya Mitt Romney, aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Republicans, kuwa mgombea tajiri kabisa katika historia ya chaguzi za nchi hiyo. Hata hivyo, pamoja na utajiri wake, Romney aliishia kubwagwa na mgombea wa Democrats, Rais Barack Obama.
Licha ya utajiri wake binafsi, Romney pia alipata sapoti ya kutosha kutoka kwa matajiri mbalimbali ndani ya chama chake, huku wengi kati yao wakiweka bayana kuwa wangekuwa tayari kutumia kiasi chochote kile cha fedha kuhakikisha wanamng’oa madarakani Rais Obama. Kama ilivyokuwa kwa Romney, matajiri hao na fedha zao, hawakuweza kumwangusha Obama.
Kama kuna fundisho kubwa zaidi la muhimu kutoka katika uchaguzi huo wa Marekani kwa siasa zetu huko nyumbani, hasa kipindi hiki ambacho baadhi ya wanasiasa wanahangaika kumwaga fedha kujijengea mazingira ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao 2015, basi ni ukweli kwamba fedha si kila kitu katika kusaka ushindi wa kisiasa.
Wengi wa wachambuzi wa siasa za Marekani, wanaafikiana kwamba moja ya sababu kuu mbili zilizopelekea Romney kushindwa uchaguzi huo, ni kwanza; mwonekano wake kama tajiri aliye tofauti na Wamarekani wengi wanaokabiliwa na hali ngumu ya uchumi kutokana na kuyumba kwa uchumi wa dunia, na pili; chama cha Republicans kutokuwa na mvuto kwa makundi mbalimbali katika jamii ya Wamarekani.
Walipokuwa wakipita huko na kule kujinadi, Obama na Romney walionekana kama wanasiasa wanaotoka sayari mbili tofauti. Wakati ilikuwa rahisi kwa Obama kuonekana ni ‘mwenzetu’ kutokana na historia ya maisha yake, mtu aliyetoka familia ya kawaida na ambaye ni ushuhuda mwafaka wa ndoto ya Amerika (The American Dream), Romney alionekana kama mtu asiyejua maana ya ugumu wa maisha kwani alizaliwa na kukulia kwenye familia tajiri.
Kana kwamba historia kumhukumu kama mgombea tajiri asiyejua shida zinazowakabili wengi wa wapiga kura haikutosha kuwa kikwazo kwa Romney, chama chake chaRepublicans kimeendelea kuonekana kama kinawatenga wapigakura wengi wa Marekani. Kwa taifa linalojigamba kwamba linaheshimu uhuru wa mtu kujiamulia mambo yake mwenyewe, alimradi havunji sheria za nchi, upinzani wa chama hicho dhidi ya utoaji mimba, haki za mashoga, bima ya afya bure (Obamacare) na masuala mengine muhimu wa walalahoi wa Marekani, umezidi kukifanya chama hicho kijiweke mbali na mpigakura wa kawaida katika nchi hiyo.
Kadhalika, kuibuka kwa kundi la wahafidhina wenye msimamo mkali linalofahamika kama‘Tea Party,’ kimezidi kuwafanya Republicans waonekane kama chama cha kibaguzi, na hasa kwa upinzani wao mkali dhidi ya marekebisho ya mfumo wa Uhamiaji ambao kwa sasa unaathiri takriban wakazi milioni 12 ndani ya nchi hiyo ambao kimsingi hawana haki ya makazi hadi sasa.
Wakati Obama amekuwa na mtizamo wa kujenga dunia ya maelewano, kwa mfano kwa kujaribu kujenga mahusiano bora kati ya Marekani na nchi za Kiislam, Republicanswalitafsiri jitihada hizo kama udhaifu wa Rais huyo.
Kadhalika, sera ya nje ya kibabe ya kutanguliza vitisho na vita badala ya kuipa fursa diplomasia, imeendelea kuwafanya wengi wa wapigakura wa Marekani kuwaonaRepublicans kama chama cha kuwabebesha mzigo wa gharama za kuendesha vita moja baada ya nyingine, bila kusahau gharama za uhai kutokana na vifo vya askari wa nchi hiyo.
Kwa huko nyumbani, siasa zetu za uchaguzi zimezidi kutawaliwa na matumizi makubwa ya fedha, hususan katika michakato ya kupata nafasi ya kugombea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na hatimaye katika kupambana na vyama vya upinzani kwenye uchaguzi mkuu.
Ninaamini kila msomaji anafahamu kuhusu matumizi makubwa ya fedha kwenye chaguzi za Jumuiya za CCM, ambapo kimsingi fedha hizo zimelenga zaidi kujenga mazingira mazuri ya ushindi kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
Tofauti na Marekani ambapo matumizi makubwa ya fedha yanalenga zaidi katika kumnadi mgombea kwa njia ya matangazo, huko nyumbani kwa kiasi kikubwa fedha zinatumika kununua kura. Kwa lugha ya moja kwa moja, fedha zinajenga uwezo wa mgombea kutoa rushwa kununua kura.
Matokeo yake sote tunayaona. Tumeendelea kuwa na wanasiasa ambao baada ya kununua ushindi kwenye chaguzi, wanakuwa ‘bize’ zaidi kujirejeshea fedha hizo kwa njia za kifisadi. Ninakumbuka wakati nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1996, takwimu zilikuwa zinaonyesha ili mgombea aweze kushinda uchaguzi katika jimbo lililopo jijini Dar es Salaam, alikuwa anahitaji takriban Shilingi milioni 100.
Sijawahi kupata takwimu za chaguzi za mwaka 2005 na 2010, lakini yayumkinika kuhisi kuwa kiwango cha mwaka 2006 kimeongezeka mara kadhaa. Sasa, kama huko Marekani ambapo hali ya maisha ni bora mara kadhaa kulinganisha na huko nyumbani, wapigakura wengi wameweza kukataa kuhadaiwa na mamilioni ya dola zilizotumika kumnadi Romney, kwanini Watanzania tuendelee kuwa watumwa wa pishi za mchele, doti za khanga, kilo za sukari na kadhalika zinazotumika kununua kura kisha kutupatia viongozi wasiojali maslahi yetu, na hivyo kuendeleza umasikini na ufisadi unaogubika taifa letu?
Ifike mahala tuweze kutofautisha mahitaji ya muda mfupi na yale ya muda mrefu. Kweli kilo moja ya sukari itamwezesha mpigakura kunywa chai kwa siku kadhaa, lakini rushwa hiyo itamgharimu mpigakura huyo kwa miaka mitano mfululizo.
Ingawa utajiri si dhambi, hususan ule uliopatikana kihalali, na ambao ni nadra katika nchi nyingi za Afrika, ni muhimu kwa wapigakura kuhoji huyo mgombea anayepita huko na kule kumwaga fedha, anazitoa wapi? Ni ukweli usiopingika kuwa wengi wa wanasiasa wanaotoa rushwa ili wapate uongozi, wanapata fedha hizo kupitia njia ambazo kimsingi ndizo zinafanya maisha ya wananchi kuwa magumu.
Kwa lugha nyingine, wanasiasa wa aina hiyo ni sawa na majambazi wanaotuibia, kisha wanatumia fedha zilizotokana na ujambazi wao kununua haki zetu za kupata wagombea sahihi, kisha wakishaingia madarakani wanaendeleza ujambazi wao huo!
Waingereza wanasema ‘once a thief always a thief’ (mtu akishakuwa mwizi ataendelea kuwa mwizi). Mwanasiasa anayehonga fedha kwa kutumia fedha zilizopatikana kwa ufisadi, lazima ataendeleza ufisadi wake pindi akiingia madarakani.
Nihitimishe makala haya kwa kuwasihi Watanzania wenzangu kubadilika. Tuweke kando haiba za wagombea. Tuweke kando tamaa ya vitu vya msimu kama vile sukari, mchele, khanga na kadhalika. Tuweke mkazo katika kuwachagua viongozi wenye kujua matatizo yetu na wenye nia ya dhati kuyatatua matatizo hayo. Inawezekana, timiza wajibu wako!


6 Dec 2012


4 Dec 2012

30 Nov 2012


NILIPOSIKIA Abdulrahman Kinana ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) hisia zangu zilikwenda kwa Karl Rove, Mmarekani anayeweza kuelezwa kama gwiji la mikakati ya siasa (political strategist) katika duru za siasa za Marekani.
Kwa uelewa wangu wa siasa za Marekani na za huko nyumbani, Rove na Kinana wanafanana kwa karibu katika utendaji kazi wao. Wote wawili ni watu waliopata mafanikio makubwa katika majukumu yao ya kuhakikisha ushindi wa mgombea waliyekuwa wakimuunga mkono; George W. Bush kwa upande wa Rove, na Rais Jakaya Kikwete kwa upande wa Kinana.
Hata hivyo, wakati Kinana amefanikiwa katika chaguzi mbili ‘kumpatia’ ushindi Kikwete, Rove alijaribu na kushindwa kupata ushindi wa mgombea zaidi ya Bush, harakati zake kwa kutumia taasisi za American Crossroads na Crossroads GPS (Grassroots Political Strategy) na mikakati wa ‘kumwaga’ dola bilioni moja kumuunga mkono aliyekuwa mgombea wa Republicans, Mitt Romney, kumwangusha Rais Barack Obama, hazikuzaa matunda.
Kimsingi, baadhi ya wachambuzi wa Uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka huu wanayumkinisha kuwa ukiachilia mbali kushindwa kwa Romney, wahanga wakubwa wa uchaguzi huo ni Rove na baadhi ya wachambuzi wa siasa (political pundits).
Wakati Rove, ambaye pia ni miongoni mwa pundits hao, ‘aliangukia pua’ licha ya matumizi makubwa ya fedha kupitia taasisi alizokuwa akiongoza, wachambuzi wengine wa kisiasa wanatafsiriwa kuwa ‘walipigwa bao’ na magwiji wa takwimu wakiongozwa na Mmarekani nguli wa ubashiri kwa kutumia takwimu, Nate Silver.
Katika ubashiri wake, Silver alisema Obama angepata kura za uchaguzi (electoral college votes) 313 (akapata 332) na Romney 225 (akapata 206). Kwenye uchaguzi wa Seneti, Silver alibashiri Democrats wangepata viti 52.5 (wakapata 53) na Republicans viti 47.5 (wakapata 45). Kitakwimu, ubashiri huo unaweza kuitwa sahihi. Hiyo ni kinyume kabisa na Rove aliyebashiri Romney angeshinda kwa angalau kura za uchaguzi 279 dhidi ya Obama.
Nirejee kwa Kinana. Baada ya kuteuliwa kwa mwanamikakati (strategist) huyo wa CCM kunikumbusha kuhusu Rove, nikakumbana na swali jingine kichwani: baada ya mafanikio makubwa kwa awamu mbili za Kikwete (2005 na 2010), je, uamuzi wa Kinana kuingia kwenye ‘active politics’ utadumisha rekodi yake au ndio political suicide (kujiua mwenyewe kisiasa) yake?
Kimsingi, japo nimemfananisha Kinana na Rove kana kwamba siasa za uchaguzi huko nyumbani ni za uwazi kama za Marekani, lakini pengine tukiingia kwa undani na kuangalia vigezo vingine vilivyosaidia ushindi wa Kikwete - kwa mfano nafasi ya ‘Wanamtandao’ na ‘usaidizi’ wa Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Polisi kwa CCM - inawezekana kazi ya Kinana ilikuwa nyepesi tu kwa vile mazingira yalikuwa mwafaka kwa mgombea wa CCM kushinda.
Lakini wakati ninajaribu kumtendea haki Kinana kwa kutoihukumu rekodi yake kwa vitu ambavyo havipo wazi kirekodi (yaani kama vigezo nilivyovitaja hapo juu), Jumapili iliyopita zikapatikana habari na picha zikimwonyesha anagawa leseni 21 za uchimbaji madini kwa wananchi huko Mugusu, Geita.
Kwa kweli sikuamini kwamba Kinana niliyefikia hatua ya kumlinganisha na Rove angeweza ‘kuingia mkenge’ wa kuigeuza CCM kuwa Wizara ya Nishati na Madini. Hivi kweli Kinana hatambui kuwa kusimamia na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM hakumaanishi kupora majukumu ya Wizara? Kama hatambui hilo basi hapaswi kuwa japo mwenyekiti wa serikali ya mtaa, achilia mbali huo ukatibu mkuu wa CCM.
Kwa upande mmoja kitendo hicho cha Kinana kinarejesha ‘machungu’ ya ufisadi wa Kampuni ya Meremeta ambapo Watanzania walidanganywa kuwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania lilijihusisha na biashara ya madini. Ninasema hivi, hili la Kinana kugawa hati za vitalu vya kuchimba madini lina kila dalili ya kuturejesha kwenye skandali kama hiyo ya Meremeta.
Hivi leseni alizotoa Kinana ziliombwa na nani huko wizarani? Yeye Kinana, CCM au hao wananchi waliokabidhiwa leseni? Kama Kinana ana uchungu na wachimbaji wadogo wa madini basi angeanza na hizo kampuni kubwa za madini ambazo kila mmoja wetu anatambua zinavyonufaika kutokana na udhaifu wa serikali yetu katika sera ya madini.
Hivi Kinana atanilaumu nikizua ‘conspiracy theory’ kuwa hao wananchi waliopewa leseni za kuchimba madini ni mwendelezo tu wa ufisadi ambapo walalahoi hutumiwa kwa maslahi ya mafisadi (yaani jina kwenye leseni ni la mlalahoi lakini mnufaika ni kigogo fulani)?
Leo CCM ‘mpya’ ya Kinana inapora jukumu la Wizara ya Nishati na Madini na kugawa leseni za uchimbaji madini, kwa nini kesho isipore jukumu la Ofisi ya Rais na kuiagiza Idara ya Usalama wa Taifa kuangamiza vyama vya upinzani vinavyoonekana tishio kwa CCM?
Naam, Waingereza wana msemo ‘once a cheater always a cheater’ (yaani, ukishawahi kuwa msaliti kwenye uhusiano wa kimapenzi utabaki kuwa msaliti wa mapenzi milele). Kama Kinana na CCM yake wameshaonja ‘utamu wa kuhonga leseni za uchimbaji madini’ (na yayumkinika kuamini kuwa hakuna mwenye uwezo wa kubadilisha kashfa hiyo ya kikatiba) kwa nini ‘asichonge mzinga’ na kupora majukumu ya wizara na idara/taasisi nyingine za serikali?
Laiti ningekuwa ninafahamiana na Kinana ningemshauri hivi: “Kinachoifanya CCM ionekane adui wa maendeleo ya Mtanzania wa kawaida ni uamuzi wa chama hicho kutelekeza msingi wake kama chama cha ‘jembe na nyundo’ (yaani wakulima na wafanyakazi) na kugeuka chama cha ‘bunduki na kisu’ (yaani hifadhi ya mafisadi na waporaji wa rasilimali zetu).”
CCM haiwezi kupendwa na Watanzania kwa kuingilia majukumu ya wizara. Kwamba wizara hizo zipo chini ya serikali ya CCM haimaanishi chama hicho kiingilie utendaji kazi wake.
Nimalizie makala hii kwa utabiri, sio ‘fyongo’ kama wa Rove niliyemlinganisha na Kinana, bali wa Nate Silver: kwa mwenendo huu wa Kinana kupora majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini na kutoa leseni za uchimbaji madini kwa wananchi, ninabashiri kuwa anaweza kuishia kukumbukwa zaidi si kwa kuwa mmoja wa wanamikakati wa kisiasa mahiri kabisa katika historia ya Tanzania bali kwa ‘madudu’ (kama ya Karl Rove mwaka huu) ya kuwapa sababu za ziada wapiga kura wa Tanzania ‘kuizika’ CCM ikiwa bado hai hapo mwaka 2015.


27 Nov 2012









 
Picha zimetumwa na Ndg Frank wa URBAN PULSE


26 Nov 2012


The excitement that drove the discovery of "emerging markets" in the 1980s and the easy money that turbocharged growth during the booming 2000s are over. The most hyped countries -- Brazil, Russia, India, and China -- are all slowing sharply, taking the average growth rate in the developing world back to the old normal of about 5 percent. Today's global economy is all about moderate, uneven growth, with stars emerging in previously underappreciated nations. Forget about the BRICs -- these seven countries are the real breakout nations to watch:
1. Philippines: This country's huge wealth in natural resources is still largely untapped, and its long stagnant per capita income is still less than $3,000 -- but that means it has lots of room to grow. Since his election in 2010, President Benigno "Noynoy" Aquino has worked to finally deliver his political dynasty's promise to restore the luster of the Philippines of half a century ago, when it was billed as the next East Asian tiger. Aquino has overseen economic reforms that have made government spending more transparent and pushed for more tax revenue. And thanks tosuccess in the outsourcing industry, the Philippine economy has watched incomes grow and new wealth spread.
2. Turkey: The next two members of the club of trillion-dollar economies will be large Muslim democracies -- Indonesia and Turkey. Turkish Prime Minister Recep Tayyip Erdogan has brought to his country both economic orthodoxy, taming the hyperinflation that raged when he took office in 2003, and normalcy, opening up opportunities for pious Muslims who had been shut out of plum jobs by the previous secular regimes. This was tantamount to welcoming the majority into the commercial mainstream, and Turkey has prospered ever since, riding the success of its surging auto exports and the boom in the financial services sector.
3. Indonesia: Most economies that have thrived mainly by exporting raw materials -- think Brazil and Russia -- have slowed sharply amid the global financial downturn. Indonesia, however, is a commodity-fired economy that has achieved balance: between its export market and its healthy consumer economy, between the national capital and increasingly vibrant provincial generators of growth, and in the form of a leader, Susilo Bambang Yudhoyono, who understands the basics of economic reform. That makes the country the model example of those Southeast Asian tigers that were defanged in the 1997 financial crisis but are roaring once again today.
4. Thailand: Like the rest of its neighbors, Thailand suffered during the late-1990s East Asian financial crisis, when the devaluation of the Chinese currency suddenly made Southeast Asia uncompetitive. But as the renminbi has appreciated over the last few years, while Chinese wages have risen, the region, and Thai manufacturing in particular, is competitive again. Thailand's wild card is the seemingly never-ending political tension between capital and countryside. If Prime Minister Yingluck Shinawatra can contain it, Thailand is in a strong position to prosper as the central trade corridor of the Greater Mekong.
5. Poland: Poland, which entered the European Union in 2004, is a case study of a country in the "sweet spot" -- the period after a member state enters the EU but before it adopts the euro. It is stable, attracting investment, and benefiting from EU subsidies, and it has made required reforms to financial institutions and curbed its deficits to meet EU requirements. At the same time, it suffers none of the instability that comes with adopting the euro (see Portugal and Spain). It continues to grow much faster than the European average and is in no hurry to join the euro. In fact, Poland recently confirmed its status as a model European reformer with a tough pension overhaul that raised the retirement age to 67, at a time when many Europeans still retire in their late 50s.
6. Sri Lanka: The outbreak of war has derailed many high-growth economies, but few for as long as Sri Lanka, where the uprising of Tamil rebels that began in the 1980s did not end until just a few years ago. It was a miracle that the Sri Lankan economy was able to grow at even 4 to 5 percent during the war years, when nearly 30 percent of the landmass and 15 percent of the population had been cut off by the fighting. Now the country is reincorporating the provinces once controlled by the rebels, and, with its strategic location on shipping routes between India and China and a highly literate population, Sri Lanka is poised to grow much more rapidly.
7. Nigeria: In a country plagued for years by corrupt leaders, President Goodluck Jonathan has committed himself to reform, encouraging investment in Nigerian agriculture, oil and natural gas, and, most importantly, electrical power. For now, the whole country generates only as much electricity as some small towns in England, and this lack of a reliable power supply has made Nigeria one of the world's most expensive markets for operating a business. But the key in a place like Nigeria is that it doesn't take much to grow from a very low base, given its per capita income of just $1,500. The landmark change from bad to good leadership, now focused on improving basic infrastructure and boosting investment, may be enough to make Nigeria among the world's fastest-growing economies over the next five years -- and in the process make it the largest economy on the African continent.

24 Nov 2012

Spoof! The fake advert for an MI6 'Target Elimination Specialist' appeared on the DirectGov Jobs website on Friday afternoon
Hacked: The advert went on to state that successful candidates would be trained in the use of sniper rifles, mini-submarines and jet packs
Vigogo katika Idara ya Kazi na Pensheni ya hapa Uingereza walikumbwa na taharuki baada ya hackers kubandika tangazo feki la kazi kwenye tovuti ya Idara hiyo kwa nafasi ya 'mtaalam wa kuangamiza watu wasiotakiwa na serikali' Government Elimination Specialist.

Katika tangazo hilo (angalia picha hapo juu) hackers hao walidai kuwa "katika nyakati fulani, serikali ya Uingereza huwa na hitaji la kuwaondoa watu ambao uwepo wao unatishia amani."

Katika tangazo hilo ka 'kuzushi' pia kuliwekwa anwani ya barua pepe ya Shirika la Kijasusi la Uingereza ambalo makao yake makuu yapo jirani na Daraja la Vauxhaul jijini London (pichani chini)

New workplace: The 'Target Elimination Specialist' would presumably work out of here, the MI6 HQ near Vauxhall Bridge

Kwa habari kamili BONYEZA HAPA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.