24 Jul 2013



Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.

Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.

Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.

Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.


Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.

Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.

Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!

Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.

SIJUI MTOTO WA MKULIMA ANAJISIKIAJE MUDA HUU....ONE THING FOR SURE, PINDA AMETHIBITISHA KWA MARA NYINGINE KUWA YEYE NI MTU MZIMA OVYO ASIYEFAA HATA KUONGOZA DARASA KAMA KIRANJA, ACHILIA MBALI HUO UWAZIRI MKUU.NI WABABSIAHJI KAMA PINDA WANAOIFANYA SIASA KUWA MCHEZO MCHAFU ZAIDI YA UCHAFU WA SIASA.

CAN'T WAIT TO SEE HIM GONE COME 2015, OR EVEN EARLIER...GOOD RIDDANCE.

23 Jul 2013

DSC 0061 f2b62
DSC 0062 6a196
DSC 0063 8ff99
DSC 0064 bce6b
DSC 0065 1a0ec

DSC 0066 edae5
DSC 0067 d75ad
DSC 0068 d64bf
DSC 0069 271a2
DSC 0070 77fb7
DSC 0071 5c9e4
DSC 0072 ec195
DSC 0073 a387f
DSC 0074 d8640
DSC 0075 78394

Picha kwa hisani ya MJENGWA BLOG



MF/NA: 836'04 Johnson Nguza
(Papii Kocha) Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es SalaamMh. Rais Jamuhuri ya Muungano Tanzania


YAH: MAOMBI YA KUPEWA MSAADA (MSAMAHA) WA KUFUTIWA ADHABU YA KIFUNGO NILIYOPEWA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU.
Husika na somo hilo hapo juu. Mimi ni mfungwa katika gereza kuu Ukonga. Kwa heshma na taadhima na kwa kutambua utu na huruma yako ya kiMUNGU ulionayo dhidi ya binadamu wenzako pamoja na mamlaka uliokabidhiwa na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Naanguka na kushika miguu yako mitukufu muheshimiwa rais....Nakuomba msaada (msamaha) kwako muheshimiwa rais, kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu. Mh.Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo, na ukweli kutoka moyoni sikufanya kosa hilo.
Si mimi, baba yangu Nguza wala ndugu yangu yeyote aliyefanya kitendo kile. Lakini wenye mamlaka wakatuona tuna hatia na kuamua kuteketeza kizazi chetu gerezani.

Natamani kiama ifike ili mwenyezi Mungu aweke wazi ukweli wote uliojificha nyuma ya pazia. Mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mh. Rais Naomba huruma yako muheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninaehitaji huruma yako wewe mzazi. Lakini pia sisi ni binadamu wenye nafsi na miili kama wengine. Waliotumia mamlaka yao kutuweka gerezani nao ni binadamu pia, wenye miili na nafsi.


Ipo siku nafsi zetu zitapaswa kutoa hesabu ya tuliyoyafanya hapa duniani. wakati huo miili yetu tunayoitumia kunyanyasa wanyonge itakuwa imeoza mavumbini.


Natumaini kauli yako ya mwisho ndio itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu. Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu. Mungu akubariki. Wako mtiifu


Mfungwa NO:836'04 JOHNSON NGUZA (PAPII KOCHA)

Nimemwomba Mheshimiwa LAZARO NYALANDU, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,kupitia mtandao wa Twitter, afikishe ujumbe huu kwa Rais Jakaya Kikwete. So far, amenijibu kuwa 'ame-copy that...' na nina matumaini atasaidia katika suala hili

22 Jul 2013

DSC 0046 d0783
DSC 0047 97a9a
DSC 0048 4d765
DSC 0049 b702c
DSC 0050 dc090

DSC 0051 7d9f9
DSC 0052 7ce1e
DSC 0054 dd80e
DSC 0055 76237
DSC 0056 c720c
DSC 0057 2ddf0
DSC 0058 3e6ca
DSC 0059 98116
DSC 0060 6c7d7
DSC 0061 584c0
DSC 0062 ad713

21 Jul 2013

DSC 0040 f2962
DSC 0041 6e376
DSC 0042 8b574
DSC 0043 4f04a
DSC 0044 11fb4

DSC 0045 7834c
DSC 0046 88013
DSC 0047 47f09
DSC 0048 98ae9
DSC 0049 7520c
DSC 0050 da1b5
DSC 0051 ab89c
DSC 0052 903f8
DSC 0053 bda17

Picha kwa hisani ya MJENGWA BLOG

20 Jul 2013







Na katika video hii, Lipumba anakiri kuwa alimsaidia JK katika kampenzi za uchaguzi mkuu uliopita...kwa kigezo cha dini

19 Jul 2013


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.