22 Jan 2013
21 Jan 2013
20 Jan 2013
20.1.13
Evarist Chahali
IKULU, UFISADI
No comments

*Wadaiwa kukingia kifua waliotafuna
fedha za wastaafu
*Msaidizi wa JK Mtawa abeba siri
nzito, Katibu anena
*Mabilioni ya Hazina, bilioni 1.7 za
NORAD zaliwa
Kashfa nzito inawazunguka watendaji
wakuu wa Ofisi ya Rais Ikulu, wanaodaiwa kushirikiana na maofisa kadaa wa
Hazina ama kutafuta fedha za wastaafu au kuwakingia kifua wabadhilifu.
Maofisa hao wanalalamikiwa kuwazuia
waliokuwa wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kukutana na Rais,
Jakaya Kikwete wamueleze malalamiko ya mapunjo ya mafao yao.
Msaidizi wa Rais Kikwete, Kassim
Mtawa, ndiye anayelalamikiwa zaidi kwamba anawakingia kifua maofisa kadhaa wa
Serikali waliotafuna mamilioni ya fedha za wastaafu wapatao 933.
Wastaafu hao wanahitaji kukutana na
Rais wamweleze malalamiko yao baada ya kuchoshwa na danadana nyingi walizopigwa
katika ofisi mbalimbali za Serikali kwa zaidi ya miaka 16 sasa bila mafanikio.
Uchunguzi uliofanywa na JAMHURI umebaini
kuwa viongozi wa kamati ya wastaafu hao wanakwenda Ikulu karibu kila siku
wakihitaji kuonana na Rais wamweleze malalamiko yao lakini juhudi hizo
zimeendelea kugonga ukuta.
Mtawa aruka kimanga
Mtawa alipotakiwa na Jamhuri
kuzungumzia malalamiko hayo kwamba ndiye kikwazo kikubwa, amekanusha tuhuma
hizo na kuwatupia mzigo huo Katibu wa Rais, Prosper Mbena na Msajili wa Hazina,
Elipina Mlaki.
Huku akizungumza kwa jazba kiasi,
Mtawa amebeza malalamiko ya wastaafu hao akisema ni watu wanaopoteza muda kwa
vyombo vya habari na kwamba madai yao hayana ukweli wowote.
“Hizo habari siyo za kweli, hao
[wastaafu] wanawapotezea muda, liko kwa Katibu wa Rais, Mbena, mimi ni Msaidizi
wa Rais, anayeruhusu watu kuonana na Rais ni Katibu wa Rais,” amesema Mtawa na
kuendelea:
“Walikuja [viongozi wa wastaafu] mimi
nikawaunganisha na Katibu wa Rais. Lakini hao [wastaafu] ni waongo, suala lao
hasa liko kwa mama Mlaki [Elipina] ambaye ndiye analijua A hadi Z.”
Mbena awashutumu wastaafu
Kwa upande wake, Mbena alipotakiwa na
Jamhuri kuzungumzia suala hilo, naye ameishia kuwashutumu wastaafu hao akidai
madai yao ni ya uongo.
“Hizo habari si za kweli, hao wazee
ni waongo, madai yao si ya kweli,” amesema Mbena.
Nyaraka zaonyesha kinyume
Jamhuri inazo nyaraka zenye kuonyesha
kuwa wastaafu hao 933 wanaidai Serikali zaidi ya Sh bilioni saba ambazo ni
mapunjo ya mafao yao mbalimbali baada ya kustaafishwa kazi UDSM mwaka 1995 na
1996.
Baadhi ya wastaafu waliozungumza na
JAMHURI kwa siku na nyakati tofauti kwa sharti la kutotajwa majina, wamesema
uongozi wa chuo hicho umekuwa ukipotosha kwamba idadi halisi ya wastaafu hao ni
638.
“Awali idadi ya wafanyakazi wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam waliopaswa kupunguzwa miaka hiyo ni 265 kulingana na
fungu la fedha zilizokuwa zimetengwa, lakini wakaiongeza hadi 638 kwa sababu
wanazozijua wao,” amesema mmoja wa wazee hao.
Nyaraka zinaonyesha kuwa Shirika la
Maendeleo la Norway (NORAD) Oktoba, mwaka 2002 liliipatia Serikali kupitia
Hazina msaada wa Sh bilioni 1.727 kuchangia malipo ya mafao ya wastaafu hao.
Wastaafu hao wamesema nyaraka
nyingine zinaonyesha kuwa Juni 2012, Ofisi ya Msajili wa Hazina ilipokea Sh
milioni 460 kwa ajili ya malipo ya wastaafu hao lakini zikaelekezwa katika
matumizi mengine ambayo hayajabainishwa.
Pia inaelezwa kwamba mwaka 2008 hundi
za sehemu ya malipo ya wastaafu hao zilitayarishwa lakini zikazuiwa na
‘wanjanja’ wachache na hadi sasa haijajulikana zilikoelekezwa.
Inaelezwa pia kwamba viongozi wa
kamati ya wastaafu hao wamefanikiwa kushinda mara kadhaa vishawishi vya kupokea
rushwa kutoka kwa maofisa husika serikalini waache kufuatilia madai hayo.
Mwaka 1997 wastaafu hao walifungua
kesi ya madai Na 299 chini ya Jaji Kalegea, lakini ikafutiliwa mbali kutokana
na kukosa vielelezo wakati huo. Wazee hao sasa wanasema vielelezo wanavyo ila
hawana fedha za kuwalipa mawakili kukata rufaa.
Profesa Mukandala ajitetea
Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa Rwekaza
Mukandala, yeye alipoulizwa amesema ofisi yake imefunga kushughulikia malalamiko
ya wastaafu hao baada ya mahakama kufutilia mbali kesi yao ya madai dhidi ya
Serikali kupitia Hazina.
Hata hivyo, Profesa Mukandala amesema
bado wastaafu hao wana haki ya kukata rufaa iwapo wanadhani hawakutendewa haki
katika hukumu iliyotolewa na mahakama.
“Haya mambo yote yameamriwa na
mahakama baada ya kuona madai haya hayana msingi… sisi tulikuwa tayari
kuwasikiliza na tungewasikiliza, lakini sisi kama taasisi ya Serikali lazima
tuheshimu mahakama kwani ndicho chombo cha sheria kinachotambulika na mamlaka
husika.
“Sisi kama chuo (UDSM) tunajua hili
suala limeisha, lakini kama wao wana hoja nyingine basi litaangaliwa na vyombo
husika lakini sisi tunajua mahakama ilishaliangalia suala hili na kulifunga,”
amesema Profesa Mukandala.
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa mamlaka
husika, hususan Ikulu, Wizara ya Fedha na UDSM zinasuasua kulipatia ufumbuzi
suala la madai ya wastaafu hao, wengi wao sasa wakiwa ni wazee wa umri kati ya
miaka 60 na 80.
Luhanjo adaiwa kulikoroga
Katibu Mkuu Kiongozi aliyestaafu,
Philemon Luhanjo, ni miongoni mwa viongozi wa Serikali walioshiriki kwa nyakati
tofauti kushughulikia suala hilo bila mafanikio huku wengine wakijaribu
kuuaminisha umma kuwa wastaafu hao hawastahili kulipwa wanachokidai.
JAMHURI limepata nyaraka kadhaa
zinazoonesha jinsi makatibu wakuu tofauti wa ofisi hizo walivyotoa maelekezo
mbalimbali kwa nyakati tofauti, ambayo hayakuweza kulipatia ufumbuzi suala la
wastaafu hao.
Nyaraka hizo ni pamoja na barua yenye
Kumb. Na. CEA110/404/IV/01 iliyotoka Ikulu kwenda Hazina ikiwa imesainiwa na
Msaidizi wa Rais, Kassim Mtawa, Januari 23, 2008.
Wazee wagonga mwamba wizarani
Uongozi wa Kamati ya Wastaafu wa UDSM
umefanya juhudi za kuwaona viongozi wa wizara za Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora, mawakili wa kujitegemea, chama tawala (Chama Cha Mapinduzi – CCM)
waingilie kati suala hilo kuwawezesha kulipwa mapunjo ya mafao yao bila
mafanikio.
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
imeagiza malalamiko ya wastaafu hayo yaendelee kushughulikiwa ikiwa ni pamoja
na wao (wastaafu) kupeleka mchanganuo wa mapunjo yao lakini hadi sasa hakuna
kilichotekelezwa hata baada ya kupeleka mchanganuo husika.
Msajili wa Hazina, Elipina Mlaki, hakupokea
simu mara kadhaa wala kujibu ujumbe mfupi wa maneno (sms) kutoka JAMHURI juu ya
sakata hilo.
Balozi Ombeni anena
Katibu Mkuu Kiongozi wa Ofisi ya Rais
- Ikulu, Balozi Ombeni Sefue, alipoulizwa na JAMHURI kuhusu sakata hilo alisema
yuko likizo, lakini Wizara ya Fedha ndiyo inastahili kulitolea ufafanuzi.
“Niko likizo. Waliostaafu miaka hiyo
inabidi wazungumze na Wizara ya Fedha,” amesema Balozi Sefue.
Waziri Mgimwa ‘auchuna’
Kama ilivyotokea kwa Mlaki, Waziri wa Fedha,
William Mgimwa, aweze kuzungumzia suala hilo ziligonga ukuta baada ya JAMHURI
kufika ofisini kwake mara mbilia bila kufanikiwa kumwona na hata simu yake
imekuwa ikiita bila kupokewa.
CHANZO: Jamhuri Media
19 Jan 2013

Picha hizi na video hapo chini zinaonyesha jaribio la mauaji ya mwanasiasa wa Bulgaria Ahmed Dogan, wa chama cha Movement for Rights and Freedoms, alipokuwa akihutubia jukwaani. Kwa habari kamili BONYEZA HAPA






CHANZO: Daily Mail
19.1.13
Evarist Chahali
AFCON 2013, Soka Afrika
No comments
GROUP A

South Africa
Previous best: Winners 1996.
Manager: Gordon Igesund. South Africa's first major tournament with Igesund at the helm. A former prolific striker, he is the only man to coach four different teams to the Premier Soccer League championship. Key man:Siphiwe Tshabalala. The Kaiser Chiefs man, above right, will be a real handful for defenders, and was highly sought-after following the 2010 World Cup, where he shone in the opening game.
Prospects: The hosts are up there with the stronger teams in the tournament this year, and will hope that home advantage will allow them to spring a shock
====================================================================

Angola
Previous Best: Quarter-finalists 2008, 2010.
Manager: Gustavo Ferrin. Took over from Lito Vidigal as coach in June, having taking his native Uruguay to the world championships at U17 and U20 level respectively.
Key Man: Manucho, above left. Many Angolan hopes rest on the Valladolid forward's shoulders at the tournament, after his goals helped them to qualification.
Prospects: It is Angola's fifth consecutive appearance in the tournament, but they'll do well to get out of what is a tough group
=====================================================================

Morocco
Previous Best: Winners, 1976; Runners-up, 2004.
Manager: Rachid Taoussi. Appointed in September on the back of a poor start to qualifying, he caught the eye after leading Moroccan club Maghred Fes to the African Confederation Cup title back in 2011.
Key Man: Younes Belhanda. The playmaker was voted the Best Young Player in Ligue 1 last season after helping Montpellier's to the French title. Chose to play for Morocco over France in late 2010.
Prospects: Morocco should be expected to better last year's performance at the very least, after crashing out at the group stage in Equatorial Guinea and Gabon
===================================================================

Previous Best: Debutants
Manager: Lucio Antunes. The 46-year-old came up through the ranks as a coach of the national youth teams before being appointed in 2010, and is now receiving plenty of praise for guiding the Islands to this year's tournament.
Key Man: Heldon. The 24-year-old bagged a handful of vital goals in qualification, and has a Europa League goal to his name, after scoring against Club Brugge for Maritimo last month.
Prospects: They took some great scalps in qualification, but an opening game against the hosts could mean their tournament is over before it has really begun
=====================================================================
GROUP B

Ghana
Previous Best: Winners: 1963, 1965, 1978, 1982; Runners-up: 1968, 1970, 1992, 2010.
Manager: Kwesi Appiah. Has been an assistant to many national team coaches, and was caretaker manager shortly after the 2010 World Cup. Appiah is a former international defender with Asante Kotoko. Key Man: Asamoah Gyan, above right. The former Sunderland man missed a penalty with the final kick of the game, which ultimately cost Ghana a World Cup semi-final berth three years ago, and will be looking to return to form for his nation.
Prospects: Ghana will be fancied by many going into the tournament, but may fall short without the influence of Andre and Jordan Ayew
=====================================================================

Mali
Previous Best: Runners-up: 1972; Third: 2012.
Manager: Patrice Carteron. Named as Mali head coach in July, some will remember him for scoring in the Tyne-Wear derby, while others will point to his management at Cannes and Dijon in France.
Key Man: Momo Sissoko. Back in the squad after turning down several call-ups in the aftermath of a poor tournament in 2010, he could play a major part in his country's fortunes.
Prospects: Mali surprised a few people by finishing third in 2012, and will be confident of reaching the knockout stages again this time
=====================================================================

Niger
Previous Best: Group Stage.
Manager: Gernot Rohr. Took over the Niger job in September, having led co-hosts Gabon to the quarter-finals of the last Nations Cup, where they eventually lost on penalties.
Key Man: Moussa Maazou. The powerful striker, above left, is Niger's best hope of goals, and has appeared for several European clubs, the last of which was Zulte Waregem in Belgium.
Prospects: Niger lost each of their three group games in their only appearance at the Nations Cup last year, and are likely to suffer the same fate again this year
===================================================================

DR Congo
Previous Best: Winners in 1968 and 1974; third in 1998.
Manager: Claude Le Roy. A veteran of the Nations Cup, after spells with several nations since 1986, when he coached Cameroon. Le Roy has never failed to get past the group stages as a coach.
Key Man: Tresor Mputu. Certainly one to watch, after captaining his club to two successive African Champions League titles, before being banned for attacking a match official at a regional tournament. Prospects: Congo will be confident heading into the tournament, backed by Le Roy's Nations Cup experience, and they could ensure that there will be a real battle to reach the second round
====================================================================
GROUP C
GROUP C

Zambia
Previous Best: Winners, 2012; Runners-up, 1974 and 1994.
Manager: Herve Renard. The Frenchman is in his second spell as Zambia coach, and led the team to the Nations Cup title last year. Renard was subsequently named Africa's coach of the year.
Key Man: Chris Katongo. Lifted the trophy in 2012 after playing a big part in Zambia's success. Katongo has scored in each of the last four finals, and will need to perform again this year. [Fun fact - He was promoted to sergeant in the Zambian army after scoring a hat-trick in a Nations Cup qualifier against South Africa in 2007.]
Prospects: Zambia provided the shock of the Nations Cup last year by winning the tournament, but will face a tough task in trying to defend their crown
===================================================================

Nigeria
Previous Best: Winners 1980,1994; Runners-up 1984, 1988, 1990, 2000.
Manager: Stephen Keshi. He was captain of the side that last won the Nations Cup for Nigeria, and can now become just the second man to win the tournament as both a player and coach.
Key Man: Victor Moses. The tricky Chelsea winger won his first Nigeria cap in February 2012 in a qualifier against Rwanda, and has since scored twice for the national side.
Prospects: Nigeria failed to qualify for last year's Nations Cup, and will be looking to atone for previous errors this year. They could stand an outside chance

Burkina Faso
Previous Best: Semi-finalists, 1998.
Manager: Paul Put. After being banned from his native Belgium in 2007 for match-fixing, the 56-year-old managed Gambia before taking over as coach of Burkina Faso in March.
Key Man: Charles Kabore. The versatile Marseille midfielder, above left, will be vital for his nation at the tournament. After winning the French title in 2010, he has often been monitored by several European clubs. Prospects: Burkina Faso have only reached the second stage of the tournament once, when they hosted the event in 1998. They will struggle to do so again this year
======================================================================
Previous Best: Winners, 1962; Runners-up, 1957.
Manager: Sewnet Bishaw. The 60-year-old has managed a host of top clubs in his homeland, and has experienced two spells as national team coach.
Key Man: Saladin Seid. The 24-year-old, above right, was the top scorer in the Ethiopian league in back-to-back seasons between 2008 and 2009, before moving for a country record transfer fee of 240,000 dollars to Egypt in 2011.
Prospects: Ethiopia are making their first appearance at the finals for the first time in over 30 years, and despite improvements, they are likely to crash out early on this year
============================================================
GROUP D

Ivory Coast
Previous Best: Winners 1992; Runners-up 2006, 2012.
Manager: Sabri Lamouchi. Appointed as coach last May, Lamouchi is yet to be beaten in his first six games in charge.
Key Man: Didier Drogba. Twice a runner-up at the tournament, the former Chelsea man missed a penalty in last year's final. The elusive Nations Cup remains Drogba's final goal in football.
Prospects: The Ivorians go into the tournament as clear favourites once again, and possess the squad to match expectation. Only a major slip-up would see them fail to reach the later stages
================================================================

Previous Best: Winners 2004; Runners-up 1965, 1996.
Manager: Sami Trabelsi. Following his success as coach of the 2011 African Nations Championship winning side, Trabelsi was rewarded with the national team role shortly after. He has featured for Tunisia at three Nations Cup finals.
Key Man: Issam Jemaa. Now playing in Kuwait, Tunisia's all-time top scorer (with 32 goals) will play for the national side at his fifth consecutive Nations Cup.
Prospects: Tunisia won the Nations Cup when they hosted the event in 2004, and will fancy themselves to fight it out with Algeria for second spot in Group D this year
================================================================

Algeria
Previous Best: Winners 1990; Runners-up 1980.
Manager: Vahid Halilhodzic. The 60-year-old took Ivory Coast to the 2010 Nations Cup, but was sacked after an unexpected early exit. He was replaced by Sven Goran Eriksson ahead of the World Cup in South Africa.
Key Man: Sofiane Feghouli. Voted Algeria's Footballer of the Year for 2012, following impressive displays at national and club level, the creative midfielder, above right, is one to watch.
Prospects: Undoubtedly a squad packed with promise, but Algeria's inconsistency means their tournament could go one of two ways
=====================================================================

Togo
Previous Best: Group Stage.
Manager: Didier Six. Managed to lead Togo to the Nations Cup amid strikes and wage disputes. The 58-year-old was in the France squad that won the 1984 European championship.
Key Man: Emmanuel Adebayor. The Spurs centre-forward looks like he will continue to be Togo's main goal threat this year after finally being persuaded to take part in national team affairs, but will need help from those around him for the whole side to be effective.
Prospects: The controversy surrounding Togo ahead of the tournament won't have helped their preparations, and they'll be tipped to fall at the first hurdle after being placed into a tough group
CHANZO: The Guardian

Yuko nje ya nchi kwa matibabu
*Waziri Mkuchika akataa kusema lolote
* Manumba aendelea kupumulia mashine
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Dk. Joseph Hosea, anaumwa na amepelekwa nje ya nchi kwa matitabu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya TAKUKURU, Dk. Hosea, alianza kuugua tangu mwanzoni mwa Desemba mwaka jana na ilipofika Desemba 15 hali ilibadilika.
Hata hivyo, chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya TAKUKURU kilisema hadi sasa haijafahamika ugonjwa unaomsumbua.
“Ni kweli Mkurugenzi anaumwa na kuna taarifa yuko ya nje ya nchi kwa matibabu kati ya Ujerumani au Uingereza.
“Kwa mara ya mwisho nilimuona Mkurugenzi akiwa hayupo sawa kiafya na hata alipokuwa anakuja kazini alikuwa katika muonekano ambao ni wazi anaumwa. Lakini katika wiki hizi sijamuona hapa ofisini,” kilisema chanzo hicho cha kuaminika kutoka ndani ya TAKUKURU.
MTANZANIA pia ilimtafuta Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) George Mkuchika kwa njia ya simu kupata taarifa za kina kuhusu tukio hili lakini alisema hana taarifa yoyote.
“Mhhhh katika hili la ugonjwa wa Dk. Hosea sina taarifa na kama ujuavyo nilikuwa katika msiba wa baba yake Naibu Waziri wa Mifugo, kule Kiteto. Tangu jana nilikuwa n rejea na nimefika Morogoro nimelala hapa na sasa nimeanza safari ya kuelekea Dar es Salaam.
“Kama kuna taarifa yoyote kuhusu hilo kwa sasa siwezi kusema lolote hadi nitakapofika ndugu yangu,” alisema Waziri Mkuchika.
Hata hivyo mmoja wa wafanyakazi wa taasisi hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema Dk. Hoseah yupo nje ya nchi kwa mapumziko ya likizo.
“Ni kweli ofisa uhusiano yupo likizo na pia mkubwa (Dk. Hoseah) naye yupo Marekani ameenda kwa ajili ya mapumziko ya likizo hakuna mtu anayeumwa,” alisema.
MTANZANIA ilimtafuta Msemaji wa TAKUKURU Dorine Kapwani ambaye muda wote simu yake ilikuwa ikiita bila kupokewa hata alipopigiwa kwa simu ya mezani.
Mbali na hatua hiyo hata alipotumiwa ujumbe mfupi kwa simu ya kiganjani ambao ulisomeka; “Dada habari, kuna taarifa Dk. Hosea anaumwa na amepelekwa nje ya nchi kwa matibabu je kuna ukweli gani” hakujibu chochote hadi tunakwenda mitamboni jana usiku.
DCI Manumba apumulia mashine
Naye Elizabeth Mjatta anaripoti kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba sasa anapumua kwa msaada wa mashine baada ya hali yake kuendelea kuwa mbaya tangu alipofikishwa katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.
DCI Manumba jana alitumia takribani siku nzima kuwa katika chumba cha uchunguzi kwa ajili ya vipimo zaidi, baada ya kutolewa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) kwa ajili ya uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi.
MTANZANIA ilishuhudia DCI akitolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi saa 11:25 akipelekwa katika chumba cha uchunguzi huku akiwa amezungukwa na madaktari na wauguzi huku baadhi yao wakiwa wameshikilia vifaa maalumu ambavyo vilikuwa vikimsaidia kupumua.
Hata hivyo, baadhi ya madaktari waliokuwa wamemzunguka hawakuweza kuthibitisha iwapo vifaa alivyokuwa amewekewa DCI Manumba vilikuwa ni sehemu ya mashine iliyokuwa ikimsaidia kupumua.
Hali hiyo iliwafanya ndugu na watoto wa kamanda huyo kuwa katika hali ya taharuki ambako baadhi yao walionyesha kushikwa na huzuni huku mmoja wa watoto wake ambaye jina lake halikupatikana akiwa katika hali ya majonzi makubwa.
Hadi MTANZANIA inaondoka katika Hospitali ya Aga khan saa 5:45 jioni mgonjwa huyo bado alikuwa hajatolewa katika chumba cha uchunguzi hali iliyowafanya ndugu kuendelea kusubiri katika eneo la mapokezi ya wagonjwa mahututi.
Alihojiwa na waandishi wa habari kuhusu hali ya mgonjwa, Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali hiyo, Dk. Jaffer Dharsee alisema kwa sasa hawezi kusema lolote hadi vipimo vya uchunguzi vitakapokamilika, huku akiwaahidi waandishi wa habari kuwa atatoa taarifa hiyo leo asubuhi.
“Siwezi kusema kitu kwa sasa kwani bado hali ya DCI inahitaji uchunguzi wa karibu wa madaktari na hadi sasa bado yupo katika chumba cha uchunguzi zaidi hivyo sina cha kusema nasubiri nikamilishe ripoti yote labda kesho ndiyo nitakuwa katika nafasi nzuri ya kusema kitu,” alisema Dk Dharsee.
Hata hivyo katika kipindi chote hicho, hali ya ulinzi ilikuwa imeimarika ambako polisi na askari kanzu walikuwa wamezunguka katika maeneo mbalimbali ya hospitali hiyo kuhakikisha kunakuwa na ulinzi wa kutosha.
Viongozi
Jana viongozi mbalimbali waliendelea kufika hospitalini hapo kumjulia hali Manumba. Miongoni mwao ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima ambaye aliwasili hospitali hapo mchana pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadick.
Viongozi wote hao walipokewa na daktari mkuu wa polisi aliyefahamika kwa jina moja la Dk Makata ambaye aliwapeleka moja kwa moja katika jengo la tatu kilipo chumba cha uchunguzi kwa ajili ya kumjulia hali DCI Manumba.
Dk. Nchimbi baada ya kutoka katika chumba cha mgonjwa hakutaka kuzungumza chochote licha ya kutakiwa kufanya hivyo na waandishi wa habari. “Mnataka niseme nini kwamba mgonjwa hali yake nzuri au mbaya? Mimi si daktari lakini kwa namna nilivyomuona nasema anaendelea vizuri,” alisema Dk. Nchimbi.
DCI Manumba aliugua ghafla na kulazwa katika Hospitali ya Muhimbili na Januari 14 alihamishiwa katika Hospitali ya Aga Khan kwa ajili ya uchunguzi zaidi ambapo alilazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).
Manumba ambaye aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo mwaka 2006 akichukua nafasi ya Adadi Rajabu, haijaelezwa wazi kuwa anasumbuliwa na ugonjwa gani, ingawa taarifa za awali zinasema amekuwa akisumbuliwa na tatizo la figo.
CHANZO: Mtanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)

























