13 Sept 2011


KATIBU Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo ama hakujua au alifanya makusudi kumsafisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo katika kashfa ya kuzichangisha fedha taasisi za wizara hiyo, kwa sababu Serikali ilishatoa waraka kuzuia utaratibu huo.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhani Khijjah alitoa waraka maalumu kwa makatibu wakuu wa wizara zote unaowazuia kuchangisha au kupokea fedha kutoka taasisi zilizo chini yake kwa sababu yeyote ile.

Waraka huo namba 3 wa Machi 7, mwaka huu, wenye kumbukumbu namba TYC/A/400/620/18, unaonyesha kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya kuonekana kwamba baadhi ya mashirika na taasisi za umma zinatoa ruzuku au mikopo kwa wizara, bila kuzingatia taratibu na sheria.

Kwa mujibu wa waraka huo, makatibu wakuu wa wizara, wakuu wa mashirika na taasisi za umma watakaoshindwa kuzingatia agizo hilo, watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa kanuni na taratibu zilizowekwa.

“Kwa kuzingatia misingi hiyo, Wizara haipaswi kupewa fedha za ziada kupitia mashirika na taasisi zilizo chini yake,” unaeleza waraka huo ambao Mwananchi imeuona.

Waraka huo unazidi kueleza: “Endapo kutatokea mahitaji yatakayolazimu Wizara kuzichangisha fedha taasisi zilizo chini yake, mashirika au taasisi za umma, lazima ipate kibali cha Waziri wa Fedha baada ya kushauriwa na Mlipaji Mkuu wa Serikali (PMG) na Msajili wa Hazina kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2008.”

inaaminika kuwa Luhanjo na Jairo wanaujua waraka huo kwa sababu nakala zake zilitumwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah hakutaka kuzungumzia waraka huo kwa madai kwamba amekuwa nje ya ofisi kwa muda mrefu. Alishauri mwandishi awasiliane na Msemaji wa Wizara ya Fedha na Uchumi au Kamishna wa Bajeti.

“Sikiliza ndugu yangu, mimi kwa sasa ni mgonjwa, nimekuwa nje ya ofisi kwa muda mrefu, hebu mtafute PR (Ofisa Uhusiano) au Kamishna wa Bajeti ndiyo wanaohusika na mambo hayo ni muda mrefu sasa sina kumbukumbu nzuri,” alisema Khijjah.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovic Utouh alipotakiwa kueleza kama katika uchunguzi wake dhidi ya Jairo walifahamu uwepo wa waraka huo, alisema asingeweza kusema chochote sasa kwa kuwa suala hilo sasa lipo mikononi mwa Kamati Teule ya Bunge.

“Mimi nakushauri upige simu huko ilipotoka barua hiyo, huenda tulipata au hatukupata hiyo haisaidii kwa sasa kwani kumeshaundwa Kamati Teule ya Bunge kufuatilia jambo hilo,” alisema Utouh na kuongeza: “Sitaki kuonekana naingilia kazi ya Kamati.”

Luhanjo hakutaka kuzungumzia suala hilo akisema: "Sipo tayari kujibu swali lako katika mazingira haya, elewa kijana!" Jairo hakupatikana kuzungumzia suala hilo kutokana na simu yake ya mkononi kuita bila ya kupokewa.

Taarifa za kuwapo kwa waraka huo zimepatikana wakati Bunge limeunda Kamati Teule kuchunguza utaratibu uliotumiwa na taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo kwa ajili ya kufanikisha mchakato wa kupitisha wa bajeti.
Julai 18 mwaka huu, Jairo alituhumiwa bungeni kwamba amezichangisha fedha taasisi zilizoko chini ya wizara yake kwa ajili ya kupitisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka 2011/2012.

Tuhuma hizo zilitolewa na Mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shellukindo alipokuwa akichangia Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini iliyowasilishwa na Waziri William Ngeleja.

Tuhuma nyingine zilizokuwa zimetolewa na Shellukindo ni za kulipa masurufu ya safari za watumishi walio chini ya wizara hiyo na taasisi zake, ambao tayari walikwishalipwa na wizara na taasisi zenyewe.Tuhuma hizo zilimfanya Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo kumpa Jairo likizo ya malipo ili kupisha uchunguzi ambao ulifanywa na Ofisi ya CAG ambao katika taarifa yake, haukuthibitisha madai hayo hivyo Jairo kurejeshwa kazini Agosti 23, mwaka huu.

Kamati ya Bunge ya kuchunguza sakata ya Jairo, ni ya pili kuundwa wakati wa uongozi wa Rais Jakaya Kikwete, zote zikiwa kwa wizara hiyohiyo ya Nishati na Madini.

Februari 7, 2008 aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na waliowahi kuwa mawaziri wa Nishati na Madini, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi walilazimika kujiuzulu baada ya kutajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mkataba tata wa Kampuni ya Kufua Umeme wa Dharura ya Richmond. Kamati hiyo iliongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Dk Harrison Mwakyembe. Dk Mwakyembe sasa ni Naibu waziri wa Ujenzi.

Agosti 25, mwaka huu Spika wa Bunge, Anne Makinda alitangaza majina ya wabunge watano, wanaounda Kamati Teule kumchunguza Jairo. Walioteuliwa ni Injinia Ramo Makani Matala, Gosbert Blandes, Mchungaji Yohane Israel Natse, Khalifa Suleiman Khalifa na Martha Umbulla.

CHANZO: Mwananchi

Sidhani kama kulikuwa na umuhimu wa kuunda tume kuchunguza kosa lililo wazi.Jairo alivunja sheria makusudi kwa vile kwa hakika wakati anapitisha mchango huo alikuwa anafahamu bayana kuwa hilo ni kosa.Luhanjo aliamua kumsafisha Jairo huku akijua wazi kuwa rafiki yake huyo alitenda kosa la makusudi.Kimsingi,wote-Jairo na bosi wake Luhanjo- wanapaswa kuwajibishwa mara moja.

Haihitaji kupoteza muda na fedha kwa njia ya Kamati Teule ya Bunge kuchunguza jambo lililo wazi kabisa,unless lengo liwe kuwasafisha Jairo na Luhanjo.Cha kufanya ni kumkumbusha Rais Jakaya Kikwete,aliyewateua marafiki zake Luhanjo na Jairo,kuwawajibisha mara moja.

Historia inatukumbusha jinsi serikali ya Kikwete ilivyoamua kupuuza mapendekezo ya Kamati nyingine ya Bunge (ya Mwakyembe) kuwawajibisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johnston Mwanyika na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Edward Hoseah waliohusishwa na ufisadi wa Richmond.Sasa kwanini tutarajie matokeo tofauti iwapo Kamati ya kuchunguza sakata la Jairo/Luhanjo itawakuta na hatia,na kisha kumshauri Kikwete awawajibishe?

Nimelizie kwa kubainisha kuwa tatizo la msingi ni Kikwete.Tuna Rais ambaye utadhani hajui kwanini yeye ni Rais.Kimsingi,ubabaishaji na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watendaji (kama huo wa Jairo na Luhanjo) ni matokeo ya watendaji hao kufahamu udhaifu wa bosi wao aliyewateua kwa kuzingatia zaidi ushkaji kuliko uwezo wao.

12 Sept 2011






JUMUIYA ya Taasisi za Kisilamu, imesema utatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kwamba hatua hiyo inakuja baada ya kushindikana kwa njia ya kidiplomasia, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Hayo yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Shehe Issa Ponda, alipokuwa akisoma tamko la msimamo wa Taasisi za Kisilamu kufuatia kauli ya Rais Kikwete katika Baraza la Idd el Fitri, lililofanyika Septembe mosi mwaka huu mjini Dodoma, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Shehe Ponda alizitaja taasisi zilizokutana na kuazimia kutoa tamko hilo kuwa ni pamoja na Baraza Kuu, Jopo la Mashehe, Baraza la Vijana wa Kiislamu na Basuta.

Alisema, baada ya kukutana wameamua kutoa tamko la kupinga hotuba ya Rais Kikwete na kwamba hatua hiyo imetokana na kutokubaliana na baadhi ya vipengele vilivyomo katika hotuba yake kuhusu kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

“Moja ya vipengele vilikuwamo katika hotuba yake (Rais Kikwete) ni kwamba Serikali haitaanzisha Mahakama ya Kadhi na kwamba badala yake Waislamu wenyewe ndiyo waanzishe mahakama hiyo. Hii moja inonyesha kutokukubaliana juu ya kuanzishwa kwa mahakama hiyo,” alisema Shehe Ponda.

Alisema hakuna mahakama yoyote inayoweza kuanzishwa ikiwa nje ya dola na kwamba vinginevyo mahakama hiyo haitakuwa na nguvu katika kutekeleza majukumu yake.

“Lakini pia Jumuiya ya Taasisi za Kislamu, inapingana na kifungu cha pili na cha tatu cha hotuba kwamba Mahakama ya Kadhi haitowekwa ndani ya katiba, jambo linalomaanisha kwamba haitakuwa na nguvu kama ilivyo kwa mabaraza ya Kiisilamu ambayo yamesajiliwa kwa utaratibu wa kawaida lakini hayana uwezo wa kisheria,”alisema Shekhe.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Jumuiya za Taasisi za Kiislamu, Ramadhani Sanze, alisema njia pekee ya kudai haki ya kutaka kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi hapa nchini ni kufanya maandamano ya usiku na mchana ili kilio cha Waislamu kiweze kusikilizwa.

“Wasilamu hawawezi kukubali kuona haki yao ya msingi ya kutaka kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi haipatiwi majibu sahihi, Kumekuwa na maneno mengi ya kuzungushwa kuhusu undwaji wa chombo hiki muhimu ambacho tunaamini kitasaidia kupunguza matatizo ya Waislamu,” alisema Shehe Sanze.

Alielezea kushangazwa kwake na kauli ya Rais Kikwete kwamba mahakama hiyo, itanzishwa na Wasilamu wenyewe.Alisisitiza kuwa waumini wa dini hiyo, wanaamini kuwa hakuna mahakama yoyote inayoweza kuwa na nguvu kama itakuwa nje ya dola.

“Kauli ya Rais Kikwete inaashiria kwamba hakuna uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, mahakama yoyote haiwezi kuwa nje ya chombo cha dola vinginevyo, haitakuwa na nguvu za kisheria,” alisema Sanze.

CHANZO: Mwananchi

11 Sept 2011

WHY THE COURT OF APPEAL’S BUILDING SHOULD NOT BE DEMOLISHED

10 Sept 2011

 
 "Jinamizi la  Bongo Dansi" LINASUMBUA ULAYA !
 USO KWA USO NA WASHABIKI BREMEN CITY !
 
 
Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa Band" aka FFU,
wanatarajiwa kutumbuiza katika onyesho kubwa la aina yake "AFRIKA MESSE"
mjini Bremen,nchini Ujerumani siku ya ijumaa 16-09-2011 majira ya alhasiri.
Bendi hiyo yenye tabia za kuwadatisha akili washabiki katika kila kona duniani na
mdundo wake "Bongo Dansi" made in Uswahilini.
 
Ngoma Africa band aka FFU imejikuta inapambanishwa tena uso kwa uso na washabiki
wengine katika mji wa Bremen,huko ujerumani Ughaibuni !ambapo maelfu ya washabiki
wamekaa mkao wa kula makombora ya muziki kutoka kwa bendi hiyo inayoongozwa na
kamanda Ras Makunja,bendi hiyo yenye utajiri wa wanamziki wenye vipaji wakiwemo
mwanadada Diva Bedi Beraca aka Princess Bedi Bella,pia yupo yule mcharaza solo
mahili Christian Bakotessa aka Chris-B,aka "Mshenzi wa Gitaa la solo" na wengineo,
Ngoma Africa band kwa sasa wanatamba na nyimbo zao "Supu ya Mawe" na
"Bongo Tambarare" zisikilize at www.ngoma-africa.com





9 Sept 2011


BONYEZA VIUNGO (LINKS) VIFUATAVYO KUMPIGIA KURA





BONYEZA KIUNGO (LINK) IFUATAYO KUMPIGIA KURA


BLOGU HII INAWATAKIA AY NA SHAA KILA LA HERI.USHINDI WENU UTAKUWA FAHARI KUBWA SI KWENU TU BALI KWA TANZANIA KWA UJUMLA.


Sijui imetokea kwa bahati mbaya tu au makusudi,lakini kuongoza shirika la ndege lisilo na ndege kunaweza kabisa kumtia mtu UCHIZI.Hatimaye Serikali imemteua Bwana Paul CHIZI kuwa Kaimu Mkurugenzi wa ATCL,moja ya mashirika ya ndege vichekesho kabisa duniani.

Tatizo kubwa linaloikabili ATCL ni sawa kabisa na yale yanayoyakabili mashirika mengi mengine yaliyoendelea kuwa chini ya milki ya serikali.Kama ambavyo Tanesco imegeuzwa mradi wa mafisadi,manyang'au wanaendelea kuyanyonya mashirika hayo mithili ya ng'ombe dhaifu ambaye baada ya kuishiwa maziwa sasa anatoa damu.

Huyu CHIZI aliyekubali uteuzi huu atakuwa anaenda kujichukulia mshahara wa bure tu.Yaani Tanzania yetu imekuwa hadhithi nyiiingi lakini utendaji sifuri.Inakera kuona kuna burudani kadhaa zinazoendelea sehemu mbalimbali kusherehekea MIAKA HAMSINI TANGU TUPATE UHURU.Tuwe wakweli,TUNASHEREHEKEA NINI?Miaka 50 ya kuwa na shirika la ndege lisilo na ndege huku wenzetu Wakenya wakitikisha dunia na Kenyan Airways yao?Yani tumepigwa bao hata na nchi iliyo mahututi kiuchumi ya Zimbabwe?

Unajua nini?Laiti huyu Rais wetu mzururaji Jakaya Kikwete angekuwa analazimika kuzurura kwa kutumia ndege za ATCL basi lazima angalau kungekuwa japo na ndege moja ya kumwezesha kutekeleza jukumu lake la kuzunguka dunia.Sawa,tungeendelea kupigia kelele safari hizo lakini angalau pale anapochoka kusafiri ndege husika ingeweza kutumika kwa shughuli za kibiashara.

Lakini mtu huyu ambaye hana idea as to kwanini aligombea kuongoza nchi ni sehemu ya tatizo linaloua mashirika yetu ya umma.Hivi mtu mwenye uchungu na nchi anaweza kumteua swahiba wake mwenye rekodi chafu kufufua shirika kama ATCL?Tusiume maneno,miongoni mwa watu walioisindikiza kaburini ATCL ni pamoja na David Mattaka,ambaye wakati anang'atuka alijigamba kwa MAFANIKIO YA NEMBO MPYA YA ATCL.Hovyooo!

Kama ambavyo wizara mbalimbali za serikali zinavyoendeshwa kwa mtindo wa bora liende ndivyo ambavyo taasisi nyingine za umma zinavyojikuta katika hali hiyohiyo.Rais anateua wazembe kwa vigezo anavyojua mwenyewe.Lakini tutegemee nini kutoka kwa mtu aliyehongwa suti na Waarabu naye akawapa fadhila ya pande la ardhi kwenye mbuga ya wa wanyama?Hata Chifu Mangungo hakuwa mzembe wa kufikiri kiasi hicho.Suti tano kwa ardhi wapi na wapi?

Nimalizie kwa kusema kuwa I can't wait kuona mwaka 2015 unafika na Kikwete anafungasha virago vyake.Lakini ni muhimu kwake kutambua kuwa dunia inabadilika, Tanzania nayo inaweza kubadilika.Japo Kikwete na CCM wanaamini watatawala milele,inawezekana kabisa mwaka 2015 tukashuhudia hadithi tofauti.Sasa aendelee kuomba CCM ibaki madarakani maana itaendelea kumlinda kama yeye anavyomlinda fisadi mwenzie Benjamin Mkapa aliyegeuza Ikulu kuwa sehemu ya biashara huku akiwahadaa wananchi na kauli za "Uwazi na Ukweli." Labda alikuwa anamaanisha uwazi wa afya yake iliyokuwa inashamiri kila kukicha, ukweli kuwa hakuna nchi nyepesi kuongoza (hata kama ni fisadi) kama Tanzania.Lakini hayo yana mwisho,na ikibidi tutaingia kwenye siasa kuhakikisha mwisho huo hauji 2050 bali miaka michache tu ijayo.

Candidate grades are based on both performance and success in using the debate to improve their standing in the nomination contest.
Romney
Style: Proved every bit as tough as Perry in opening jousts. More natural and comfortable than usual, even/especially when delivering his pre-canned lines—many of which scored powerfully.
Substance: Strong on a variety of issues, but surprisingly, never shifted the focus to his detailed economic plan unveiled Tuesday.
His worst moment: Had trouble defending his Massachusetts health care law, still sounding addled and uncertain every time it comes up.
His best moment: Fluid, politically potent slap-down of Perry on his inflammatory Social Security rhetoric: “Our nominee has to be somebody who isn’t committed to abolishing Social Security.”
The main thing: Came prepared with clear stats and a good attitude. Showed he won’t back down in the face of the Perry surge. Smart enough to retreat after Perry’s Social Security flap, increasing the odds that it will be the story of the night. Once again, looked fit, at ease, and more like a president than anyone on stage--including his main competition.
Grade: A
___________________________
Perry
Style: Jabbed at Romney whenever possible, and was smooth and confident while doing so. Often looked straight to the camera, rather than at the moderators or in-room audience—an effective alpha male move. Smiled, mugged, and joked easily, flaunting his earthy Texan charm, although occasionally appeared a bit tentative.
Substance: Stood by his stark “Ponzi scheme” record on Social Security. Claimed the federal government is to blame for Texas’ dead-last standing on insurance coverage. Never sounded like a policy wonk, but evinced a reasonable command of policy basics—although he faltered on climate change at debate’s end. Offered a robust defense of the death penalty.
His worst moment: Defiantly stood by the passages about Social Security in his controversial 2010 book ”Fed Up” in a manner as ominous as it was unclear.
His best moment: Telling the world that Michael Dukakis had a better record on jobs than Romney.
The main thing: Largely followed his advisors’ strategy: severe on Romney without being mean-spirited, solution-oriented when discussing the nation’s problems, adept at dodging unwelcome questions, appealingly loose and accessibly human. But his Social Security answer is sure to get a lot of scrutiny from the press, Democrats and Republicans (Romney included). The press will kill him on climate change, too. Not bad for a first debate, but second best is second best.
Grade: B+
___________________________
Huntsman
Style: Displayed the reasonable, conservative persona of a Republican leader. Although mild in manner, sounded smart and constructive.
Substance: Talked in generalities for the most part, but was decent in broad strokes.
His worst moment: Fighting sickness, he seemed to lose energy (and his voice) after a strong start.
His best moment: Made a powerful, sweeping case for his experience on jobs and internationally in response to a question on China.
The main thing: Launched into the debate with aggression and purpose, but faded by the end. With the overheated Perry-Romney focus, did perhaps as well as he could–- but had difficulty breaking through and regaining ground.
Grade: B-
___________________________
Bachmann
Style: Bright and collected, if somewhat tense. Kept her focus on Obama, even when invited to critique RomneyCare.
Substance: Still just skimming the surface, although refrained from excessively touting her record in the House, in contrast to past debates.
Her worst moment: Shied away from attacking Perry despite proffered opportunities--she’ll have to take him on if she wants back in the hunt.
Her best moment: Didn’t really have any, which was her chief problem.
The main thing: Still smoother and more composed than her cartoonish pre-candidacy image, but is no longer benefiting from low expectations. There is an air of desperation around her efforts now that she has been muscled out of the first tier by Perry.
Grade: C-
___________________________
Santorum
Style: Mr. Consistent –- mild, earnest, eager for everyone to know that he was an activist Senator.
Substance: Didn’t own any issue in an eye-catching manner.
His worst moment: More than once, sounded a bit tinny, a little whiny.
His best moment: Defended America’s role around the world in a principled, passionate manner.
The main thing: Wants desperately to be a player in this thing, but has not found the alchemy required to mirror Joe Biden in 2008 and play above his poll standing as a debater.
Grade: D+
___________________________
Gingrich
Style: Cantankerous, accusatory, and unfocused.
Substance: Rarely showed his substantial policy chops.
His worst moment: Angrily suggested that moderator efforts to explore differences between the GOP candidates are a media plot against the Republican Party.
His best moment: Gave a strong, detailed answer on immigration reform, the likes of which hasn’t been seen much in these debates so far.
The main thing: Failed to appear presidential and distinguished. Despite hearty audience approval, didn’t execute any discernable strategy to win the nomination.
Grade: D
___________________________
Cain
Style: Adopted a more presidential mien than in past debates, but was crowded out and made no distinct impression.
Substance: Still unable to break through with a signature policy issue.
His worst moment: A rambling answer about Chile and retirement.
His best moment: Decent response on taxes, just as the debate was ending.
The main thing: Had less verve than usual. Failed to stand out or improve his standing.
Grade: D-
___________________________
Paul
Style: Adopted a more negative tone towards the other candidates, as he and his campaign have started to do in recent weeks.
Substance: Demonstrated a familiarity with Perry’s Texas record that allowed for some detailed critiques.
His worst moment: Hemmed and hawed when challenged by Perry on his record of fidelity to Reagan (at the Reagan library!).
His best moment: Nothing stood out.
The main thing: Was given many opportunities to talk, but made little substantive use of the time. His new strategy -- going after the frontrunner, rather than just following his own drummer -- noticeably tanked. He came across as angry, and he made his ire seem personal, a petty Texas feud.
Grade: D-


SOURCE: The Page

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.