7 Oct 2011


Raia Mwema Ughaibuni
Kama hali ni hii, ustaarabu wa kisiasa tuusahau 2015!
Evarist Chahali
Uskochi
5 Oct 2011
Toleo na 206
HATIMAYE uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga umefanyika. Kama zilivyo chaguzi mbalimbali nchini tumeshuhudia kila aina ya vituko.
Kama kuna lolote la kujifunza, basi ,ni ukweli kwamba safari yetu ya kidemokrasia bado ni ndefu. Waingereza wana msemo kuwa katika jambo lililofanyika muda mrefu uzoefu una umuhimu wake (tafsiri isiyo rasmi ya in long run experience counts).
Lakini inapokuja kwenye masuala ya siasa zetu, uzoefu wa muda mrefu wa chama tawala CCM unageuka kuwa mithili ya kikwazo cha demokrasia.
Kwa vyovyote vile; matokeo ya uchaguzi huo mdogo wa jimbo la Igunga, yamezidi kudhihirisha kuwa CCM ipo tayari kufanya lolote lile ili mradi ibaki madarakani.
Haihitaji kuwa mchambuzi mzuri wa siasa kupata picha kwamba kama chama hicho tawala kimeweza kutumia kila mbinu katika kampeni zake kwenye uchaguzi huo wa jimbo tu, basi, ni dhahiri kuwa kama ilivyo kwenye chaguzi kuu zilizotangulia, mwaka 2015 tutashuhudia tena mambo yasiyoendana kabisa na ustaarabu wa kisiasa.
Pengine kabla ya kuendelea zaidi na makala hii niweke wazi msimamo wangu kisiasa. Mara kadhaa nimekuwa nikihusishwa na CHADEMA; huku wengine wakinituhumu kuwa kujiweka kwangu karibu na chama hicho ni kwa matarajio ya kupata madaraka iwapo kitafanikiwa kukamata dola.
Ni kweli kuwa maandiko yangu mengi yameonyesha kuiunga mkono CHADEMA; lakini hiyo haimaanishi kuwa mimi ni mfuasi au mwanachama wake. Msimamo wangu kisiasa ni kutofungamana na chama chochote cha siasa.
Kwa vile dhamira yangu ni kuwa mchambuzi ‘halisi’ wa siasa, kufungamana na chama fulani kunaweza kuathiri utekelezaji wa majukumu yangu.
Itikadi yangu kisiasa ni uzalendo. Japo kwa mujibu wa Katiba yetu yenye mapungufu ni vigumu kwa mwananchi kushiriki katika siasa kwa ukamilifu pasipo kuwa mwanachama wa chama cha siasa, binafsi ninaamini njia bora ya kuutumikia umma ni kutanguliza maslahi ya taifa bila kujali uanachama wa chama cha siasa.
Katika siasa tunafundishwa kuwa nchi ni lazima iendelee kuwepo; ilhali vyama vya siasa vinazaliwa na vinaweza kabisa kufa kwa sababu moja au nyingine. Lakini linapokuja suala la uhai wa nchi, kila mwananchi anapaswa kufanya kila jitihada kuhakikisha kuwa sio tu inaendelea kuwepo bali pia inakuwepo katika hali inayostahili.
Sasa, kwa muda mrefu CHADEMA imejitambulisha kwa umma kama mtetezi wa kweli wa wanyonge na maslahi ya nchi yetu. Chama hicho kumekuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi na mafisadi.
Kwa namna fulani, harakati za chama hicho zimeweza hata kuifanya CCM ijiangalie kama kweli ipo madarakani kuwatumikia Watanzania na si mafisadi pekee.
Kwa mantiki hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa kila anayeipenda Tanzania yetu kwa dhati kuungana na harakati za CHADEMA katika safari yake ya kuhamasisha na hatimaye kufikia ‘uhuru wa pili.’
Naam, vita ya uhuru ‘wa kwanza’ ilikuwa ya kumwondoa mkoloni, mgeni aliyetunyanyasa kwa vile -pamoja na sababu nyingine - hakuwa na uchungu na nchi hii.
Vita hii ya sasa ni dhidi ya Watanzania wenzetu ambao kwa tamaa na ulafi wao wameweka mbele maslahi yao pasipo kujali wanalipeleka wapi taifa letu.
Kama nilivyoandika katika makala yangu katika toleo la wiki iliyopita mazingira ya chaguzi zetu, na kama ilivyoshuhudiwa huko Igunga, hayatoi fursa kwa vyama vya upinzani kuchuana na CCM kwa haki.
Uhuni uleule wa kila siku ambapo timu moja ya soka yenye wachezaji 11 inalazimika kuchuana na timu pinzani yenye wachezaji 15 (kwa maana ya wachezaji 11 wa kawaida wakisaidiwa na refa, washika vibendera wawili na kamisaa).
Watendaji wa serikali wanaopaswa kusimamia chaguzi pasipo upendeleo wanalazimika (aidha kwa uoga wao au kwa kufuata maelekezo ya serikali) kuipendelea CCM waziwazi.
Na chanzo kikubwa cha tatizo hili ni kufeli vibaya kwa harakati za kuondoa itikadi za kisiasa kwenye utumishi wa umma serikalini.
Katika mazingira ya kawaida, huwezi kumzuia Mkuu wa Wilaya asiipendelee CCM; ilhali anajua bayana kuwa iwapo chama hicho tawala kitashindwa kwenye uchaguzi unaofanyika kwenye jimbo lililopo kwenye wilaya ya DC huyo, basi naye atakuwa matatani.
Ni vigumu kwa Mkuu wa Mkoa ambaye amezawadiwa u-RC kutokana na ushiriki wake ndani ya CCM kumudu kusimamia uchaguzi kwa uhuru na haki na hatimaye kuruhusu CCM ishindwe kihalali.
Hali ni hivyo hivyo kwa Tume ya Uchaguzi na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambapo utendaji kazi wa taasisi hizo ni kama kwa njia ya ‘remote control’ kwa matakwa ya chama tawala, kiasi kwamba malalamiko yoyote ya vyama vya upinzani huchukuliwa kama ‘kelele za mpangaji ambazo hazimnyimi usingizi mwenye nyumba’.
Ni kweli kwamba mawaziri wote tulionao ni wana CCM, lakini jukumu la waziri na wizara, kama ilivyo serikali, ni kuwatumikia Watanzania wote pasipo kujali itikadi zao.
Sasa waziri anapokwenda kwenye kampeni za uchaguzi na kuwatisha wapiga kura kwamba wakidiriki kuchagua mbunge wa chama cha upinzani watanyimwa maendeleo, ni uhuni wa hali ya juu wa kisiasa.
Katika kampeni huko Igunga tulisikia ‘hadithi’ kwamba CHADEMA wameingiza magaidi kutoka nje ya nchi kwa minajili ya kufanya vurugu kwenye uchaguzi huo. Hizi si tuhuma ndogo na zinaweza kuwa na madhara makubwa kwa taifa letu.
Wanasema, moja ya athari za ugomvi kati ya wanafamilia ni uwezekano wa watu walio nje ya familia hiyo na ambao wana chuki na familia husika kutumia migongano huo wa kifamilia kuihujumu; huku wakijua fika itakapofika hatua ya ‘kusaka mchawi’ macho yataelekezwa kwa miongoni mwa wanafamilia wanaokorogana.
Kwa kutumia mfano huo wa kinadharia, iwapo kuna magaidi wanaotaka kuidhuru Tanzania wanaweza kutumia propaganda hizo mufilisi za CCM kuja kutudhuru; huku wakielewa fika uwepo wa imani fyongo kuwa ‘magaidi tishio kabisa kwa Tanzania wanalelewa na CHADEMA.’
Tunafanya yote hayo kwa faida ya nani? Sote tunawajua wabunge wetu na utendaji wa bunge lenyewe. Hivi kweli tunakubali kufarakanishwa kwa ajili ya watu ambao wengi wao wakishaingia bungeni wanakuwa bize zaidi na kutafakari namna ya kutumia mamilioni wanayolipiwa kama posho na mishahara?
Hivi kweli wapiga kura wanakuwa radhi kusikia porojo za Rais Mstaafu Benjamin Mkapa ambaye alikuwepo madarakani kwa miaka 10 na kumbukumbu kubwa aliyotuachia ni tuhuma dhidi yake kuwa aliigeuza Ikulu kuwa sehemu ya kufanyia biashara?
Kwa vyovyote vile; matokeo ya uchaguzi huo mdogo wa Igunga yanamaanisha kuwa waathirika wakubwa ni wana Igunga wenyewe. Rushwa mbalimbali zilizoambatana na burudani kutoka ‘mjini’ hazitadumu muda mrefu, na busara au ukosefu wa busara kwa kumchagua mbunge asiyeweza kulitumikia jimbo kwa manufaa, zitaanza kuonekana muda si mrefu.
Kwa CHADEMA, uchaguzi huu mdogo unapaswa kuendelea kuwa darasa zuri kwao kujiimarisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Kilicho wazi kwa kila aliyefuatilia mwenendo wa uchaguzi huo ni ukweli kwamba chama hicho kilikuwa kinapambana na CCM, CUF na serikali kwa ujumla.
Idadi ya kura ambazo CHADEMA imepata ni ‘mithili ya ushindi’; kwani upinzani dhidi yao ulikuwa mkubwa kuliko umri wa chama chenyewe.
Kwa ndugu zangu wa CUF, ninachoweza kuwatahadharisha ni kwamba pasipo umakini wa kujua kwa nini chama hicho kilianzishwa, kuna hatari ya sio tu kupoteza nafasi yake kama wapinzani nambari mbili nyuma ya CHADEMA, bali pia kinaweza kujichimbia kaburi.
Siasa za Zanzibar zinakiweka chama hicho katika nafasi ngumu ya kupambana kwa dhati dhidi ya CCM, na badala yake kinaelekeza mapambano yake dhidi ya wapinzani wenzao wa CHADEMA.
Lakini CUF wanafahamu fika kuwa CHADEMA si chama tawala, na kuiandama kunaweza kuzua hisia kuwa CUF ipo ipo tu na ‘inatumia uhasama usiokuwepo na CHADEMA kwa minajili ya umaarufu tu na kuinufaisha CCM.
Nimalizie kwa kuwakumbusha tena Watanzania wenzangu kuwa kamwe tusikubali kufarakanishwa kwa ajili ya maslahi ya chama au mtu binafsi. Maendeleo na ustawi wa Tanzania yetu ni jukumu letu kama wananchi na sio kuliacha mikononi mwa wanasiasa wasioishiwa na ahadi ambazo hata wasipozitekeleza bado wana uhakika wa kuingiza mamilioni kwenye akaunti zao.
Inawezekana, timiza wajibu wako


6 Oct 2011



1. Apple I (1976): Home computing

The Apple-1 had only 8k of memory and was sold by the Apple boss from his parents garage in California in 1976. The machine sold for $666 then - an early model sold recently for £133,000 at Christies in London
The Apple-1 had only 8k of memory and was sold by the Apple boss from his parents garage in California in 1976. The machine sold for $666 then - an early model sold recently for £133,000 at Christies in London

2. Apple II (1977): Mass-market PC

Apple co-founder Steve Jobs introduces the new Apple II in Cupertino
Apple co-founder Steve Jobs introduces the new Apple II in Cupertino

3. Apple 1984: The 'graphical' PC 

The 1984 Apple MacIntosh launched with a Superbowl commercial directed by Ridley Scott. The hit 'graphical' computer continued to sell well into the Eighties
The 1984 Apple MacIntosh launched with a Superbowl commercial directed by Ridley Scott. The hit 'graphical' computer continued to sell well into the Eighties


4. Pixar (1986): Digital Effects

After leaving Apple, Jobs founded Pixar - and helped launch the era of digital effects in films. Jobs had left by the time hits such as Toy Story came out, but was behind the early successes of the company
After leaving Apple, Jobs founded Pixar - and helped launch the era of digital effects in films. Jobs had left by the time hits such as Toy Story came out, but was behind the early successes of the company


5. NEXT (1989): Dawn of the web

After being pushed aside in 1985 by Apple's board of directors, Jobs founded NeXT, a computer platform development company - its computers offered the first web browsers
After being pushed aside in 1985 by Apple's board of directors, Jobs founded NeXT, a computer platform development company - its computers offered the first web browsers


During the low point of the NEXT years, Fortune magazine described Jobs as either a 'visionary' or 'a snake oil salesman'
During the low point of the NEXT years, Fortune magazine described Jobs as either a 'visionary' or 'a snake oil salesman'

6. Apple iMac (1998): 'Lifestyle PCs' 

The colourful iMac - the design team 'got inspiration' by going to a sweet factory - heralded Jobs's return to Apple
The colourful iMac - the design team 'got inspiration' by going to a sweet factory - heralded Jobs's return to Apple


7. iPod (2001): Digital music

The first-generation iPod offered a mere 5Gb of memory - smaller than even the cheapest iPhone model today
The first-generation iPod offered a mere 5Gb of memory - smaller than even the cheapest iPhone model today


8. iTunes Store (2003): The download era

The launch of iTunes store was a new era for media - turning Apple into the biggest music company on Earth
The launch of iTunes store was a new era for media - turning Apple into the biggest music company on Earth

9. iPhone (2007): Smartphones

Companies such as Sony Ericsson had touchscreen phones on the market before the 2007 launch of iPhone - but iPhone conquered the market
Companies such as Sony Ericsson had touchscreen phones on the market before the 2007 launch of iPhone - but iPhone conquered the market


10. iPad (2010): The post-PC era

Apple's iPad ushered in a new era of slim touchscreen devices - now being copied by every computer manufacturer on Earth
Apple's iPad ushered in a new era of slim touchscreen devices - now being copied by every computer manufacturer on Earth
 
Apple computers - a timeline
Apple computers - a timeline

Some that didn't work quite so well...


Every genius has his 'off' days - and some of Steve Jobs's most recognisable products weren't QUITE as successful as the others... 


The 'puck' mouse
G4 cube
The puck mouse for Apple's iMac computer looked pretty, but was almost unusable - and the G4 Cube was prone to overheating and unpopular with fans, despite walking off with design awards


Few people know this, but iPhone was not the first 'iTunes phone' - this monstrosity was. A partnership with Motorola, the ROKR worked with iTunes, but was far too fiddly
Few people know this, but iPhone was not the first 'iTunes phone' - this monstrosity was. A partnership with Motorola, the ROKR worked with iTunes, but was far too fiddly


SOURCE: Daily Mail

5 Oct 2011



Na Nova Kambota Mwanaharakati,

Mara kwa mara huwa nasema tatizo kubwa la Tanzania yetu ni kupenda kupindisha ukweli, hii imetufanya kuwa watu tusiopenda kufikiri kiasi kwamba tunalambishwa kila linalokuja “tumekuwa madodoki kila uchafu tunasomba”. Naandika hivi kwa nia ya kujenga si kubomoa, naandika hivi kwa mustakabali wa Demokrasia yetu ambayo nathubutu kusema imetikiswa kupita maelezo huko Igunga na tusipokuwa makini Taifa litadondoka siku za usoni.
Kwako Dr Kafumu ambaye umetangazwa kuwa mbunge wa Igunga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), naomba unaposhangilia ushindi wako nikiamini wewe ni msomi na mzoefu katika Nyanja za uongozi wa Taifa hili napenda usome maandishi yaliyo ukutani kisha malizia kwa kuunganisha dots za ushindi wako halafu niambie ikiwa ni kweli unaamini kuwa umeshinda kihalali? Au la niambie kile ambacho kinaitwa “changamoto za uchaguzi Igunga” ni nini kama siyo “mizengwe?”
Kama mchambuzi nisiyeegemea upande wowote nisingependa kutia mwaa mtiririko huu wa hoja zangu kwa hiyo sitaegemea upande wowote bali nitajadili kwa misingi ya hoja ili ikibidi kujibiwa pia nijibiwe kwa misingi ya hoja vivyo hivyo, nataka kuibua hoja zenye mashiko ili zitufikirishe na kutupa majibu ya kisayansi badala ya kumezwa na mawimbi ya watu wenye mkatiko wa mirija ya fikra ambao wamebaki na ushabiki badala ya hoja kiasi kwamba wanatoa majibu ya zamani kwa maswali mapya. Yafuatayo ni mambo manne ambayo yanatia doa ushindi wa Dr Kafumu;
Kwanza Tume Ya Uchaguzi;
Tume ya uchaguzi ya nchi hii haina sifa nzuri na haiwezi kuwa na sifa nzuri mpaka iwe huru, hata I gunga hali ni hivyohivyo tumesikia malalamiko dhidi ya tume hiyo lakini hasa kwa aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa uchaguzi huo ambaye pia ni mteule wa rais na bila shaka kwa kuunganisha mantiki haina shaka kuwa naye ni mwanachama wa CCM au basi anaipenda kimoyomoyo. Uchaguzi wa Igunga ukipimwa kwa mizania hii ya aina ya tume ya uchaguzi tuliyonayo ni vigumu sana kwa mtu mwenye kufikiri kwa mantiki kuridhia matokeo ya uchaguzi huo.
Pili Siasa Uchwara;
Hapa inahitaji moyo mgumu kuyasema lakini kwa vile tangu awali nilishasema kuwa lengo si kufukua makaburi bali kuweka shada la maua juu ya makaburi basi acha niseme hiki ambacho nakiita ni siasa uchwara. Kwanza kabisa jinsi serikali ya CCM ilivyoruhusu kubofywa kwa kile kinachoitwa “kitufe cha udini”, ikumbukwe kuwa hata wakati wa uchaguzi serikali bado ina jukumu la kuilinda katiba na kuhakikisha amani haivurugwi aidha kupitia mirija ya udini wala ukabila, nayasema haya kutokana na baadhi ya viongozi wa dini kuirushia makombora CHADEMA tena wakaenda mbali kwa kutoa wito kwa baadhi ya waumini wa dini Fulani kutompigia kura mgombea wa chamna hiko, lakini cha ajabu hata hiyo hoja ya DC kuvuliwa hijabu imekwama kama gazeti nguli la Mwanahalisi lilivyofunua kuwa Mama Fatuma Kimario uislamu wake una mashaka kutokana na yeye kuwa ni mke halali wa Bw Kimario ambaye ni mkristu wa madhehebu ya Kikatoliki ambapo hata mwanazuoni mashuhuri wa kiislamu nchini Sheikh  Issa Ponda amenukuliwa akisema kuhusu mwanamke au mwanaume wa kiislamu kubadili dini Sheikh Ponda amesema “Hilo ni kosa kubwa sana”.  Lakini cha kusikitisha kuwa wakati haya yote yanatokea CCM walikaa kimya kana kwamba “hawakuliona kosa”, je tukisema kuwa hii ilichangia Wana Igunga kupiga “kura za chuki” dhidi ya CHADEMA tutakuwa tumekosea? Haya ni maswali magumu kuhusu ushindi wa Dr Kafumu.
Jambo la pili ambalo linaangukia kwenye siasa uchwara ni pamoja na vitimbi vya rushwa na vitisho vya “kipuuzi” mfano gazeti la Dira linamtaja mwenyekiti wa mtaa wa Nkokoto huko Igunga Bw Abed Motomoto (CCM) kuwa amekutwa akigawa rushwa “live”kwa wanawake wa mtaa wake kwa lengo la kuwashawishi kumpigia kura mgombea wa CCM (Dr Kafumu), lakini kama hili halitoshi kuna hili la Mh Ismail Aden Rage kupanda na bastola ikining’inia kiunoni halafu tunaambiwa kapewa adhabu ya kulipa laki moja, sasa ladda nitumie fursa hii kumuuliza ndugu yangu Aden Rage kuwa alikuwa anamtisha nani na bastola yake? Au nani kamwambia kuwa ni utamaduni wa kitanzania kuonyeshana vyombo vya moto? Haya ni machache kati ya mengi yanayokinzana na maana ya demokrasia pia kupoteza mantiki nzima ya “uchaguzi huru na wa haki”
Tatu kuchelewesha matokeo;
Hili ni  tatizo linalotia huzuni sana kiasi kwamba nashawishika kuamini kuwa “bado tuna safari ndefu”, nayasema haya kwasababu kwanza idadi ya watu waliojiandikisha ni tofauti sana kwasababu waliopiga kura ni wachache wanaokadiriwa kuwa elfu sitini (60,000) lakini cha ajabu hata kiasi hiki kichache cha kura kimechukua masaa kibao zaidi ya kumi kuhesabu, hiki kama si kiroja ni nini? Au tuamini kuwa kuna lililojificha nyyuma ya pazia hapa?
Nne Matumizi Ya Nguvu;
Nalazimika kuyaandika haya kutokana na tabia inayozidi kukua siku hizi ya polisi kutumia nguvu dhidi ya wananchi , matukio ni mengi lakini hebu tutupie macho kwenye hili sakata la Igunga ambapo nasema kulikuwa na matumizi ya nguvu yasiyo na msingi, mabomu ya machozi ya nini? Watu walitawanywa kwasababu gani? Kwa mamlaka ya nani? Na faida ya nani? Je hii ndiyo demokrasia tunayoitaka? Huu ndiyo tunaouita ushindi halali? Uhalali uko wapi hapa?
Baada ya kuona upungufu huu , sasa tuone nini ambacho Dr Kafumu anaweza kufanya ili kuienzi Demokrasia na kuwapa haki yao Wana Igunga;
1. Awe wa kwanza kulaani matumizi ya nguvu dhidi ya Wana Igunga
2. Awe wa kwanza kuhakikisha Ismail Aden Rage anachukuliwa hatua kali za kimaadili
3.Awe wa kwanza kulaani harakati zozote za wanasiasa kuingiza udini kwenye siasa
4.Awe wa kwanza kuomba radhi kwa niaba ya chama chake kwa kukaa kimya au kushabikia siasa uchwara.
5 Awe wa kwanza ndani ya CCM na Tanzania kukataa ushindi huo na kuitaka Tume kuitisha tena uchaguzi wa jimbo dogo la Igunga , hili lifanywe pasipo kuangalia gharama za zoezi hilo, bali lifanywe ili kuuonyesha Ulimwengu kuwa Dr Kafumu na CCM wameamua kusiamamia misingi ya Demokrasia pasipo kujali gharama za hatua hiyo.
Haya ni mambo ya msingi kwa Dr Kafumu kuyasoma na kuyafanyia kazi, hii itamjengea heshima sio tu ndani ya CCM bali kwa watanzania wote na Ulimwengu mzima. Tafakari! A luta Continua!
  
Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Wesneday, 5october,2011
Tanzania, East Africa.


Hi, 
There are three benefits with Wanachuo programme East Africa, 
Cost benefits,professional benefits and community benefits 
1.Cost benefits 
In this cost benefit:- 
i.A student can know the exactly price of the product or service ie no need for window shoping,every thing is online. 
ii.Student can be updated with special deals and offers from different product and service providers through his mobile phone 
iii.Students can save minimum of 20% through buying from our discount providers. 
iv. Student can earn points by referring other students in the programme or through buying from our discount providers locations. 

We are in the second phase of developing the professional and community benefits, 
Join the programme its free 
www.wanachuo.com 
Best regards 
Abdalah Kileo

4 Oct 2011


Karibu  Kona ya Mangoma"It's all about East African Flava"
Habari zenu wadau wote... Tunapenda kuchukua nafasi hii ya kipekee kabisa kuwakaribisha katika Libeneke jipya kabisa la KONA YA MANGOMA  Ambapo mtapata kutazama video mpya na nyenginezo nyingi kutoka pande zote Afrika Mashariki yani Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi..Pia tunaomba wasanii wote ambao mnatoa Video mtutumie link kupitia barua pepe hii ([email protected]) ili tuweze wape sapoti ya juu, Kwa pamoja tunaendeleza Muziki wa Afrika. Tunatanguliza Shukrani  zetu za dhati kwenu. Ukiona link hii mpe na mwenzako.


Jina la Blog: Kona ya Mangoma  



Naamini wasomaji wapendwa wa blogu hii mlisoma POST HII niliyomjibu ndugu yangu Omar Ilyas aliyehitimisha kuwa Chadema inahitaji kushindwa ili ishinde

Naam,kwa hakika hicho ndicho kilichojiri jimboni Igunga ambapo licha ya CCM kuwekeza kila aina ya raslimali (halali na za kifisadi) imeibuka na ushindi mdogo tu wa tofauti ya kura takriban 2000.Ni wazi kuwa laiti CUF ingethamini umuhimu wa ushindi kwa vyama vya upinzani-na kumsapoti mgombea wa Chadema- muda huu CCM ingekuwa inahesabu hasara.

Ni rahisi kwa Chadema na wafuasi wake kuvunjika moyo kutokana na kutoibuka washindi katika uchaguzi huo.Lakini kimsingi Chadema imefanya vizuri kuliko ilivyotarajiwa.Unajua,kuna wakati ushiriki tu-na matokeo ya ushiriki huo-ni sawa na ushindi,hususan pale matokeo ya ushiriki huo yanapotoa picha ya kujenga matumaini.

Ni rahisi pia kwa watu kuikebehi Chadema-kama anavyofanya Bwana Nape Nnauye na viongozi wengine kadhaa wa CCM.Ikumbukwe kuwa CCM ililazimika kulamba matapishi yake hadi kufikia hatua ya kushinda uchaguzi huo.Sote tunafahamu kuwa Nnape na wenzie walitupa imani kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kabla ya uchaguzi,mtuhumiwa wa ufisadi Rostam Aziz,alikuwa gamba.Na hiyo ndio sababu ya msingi ya kufanyika uchaguzi huo baada ya gamba hilo kuamua kuondoka lenyewe.

Lakini wafuatiliaji wa kampeni za uchaguzi huo watakuwa bado na kumbukumbu za Rostam kupandishwa majukwaani kuiombea kura CCM.Well,hilo sio kosa kwani Rostam bado ni mwanachama wa CCM.Lakini ni kituko kisicho na maelezo kumshirikisha kwenye kampeni hizo mtu anayefahamika kama gamba ndani ya chama hicho.Inadaiwa kuwa Rostam alibembelezwa ashiriki kwenye kampeni hizo kutokana na nguvu zake kubwa za kisiasa jimboni Igunga.

Ni wazi kwa mwenendo huu tusitarajie kusikia magamba mengine ie Edward Lowaasa na Andrew Chenge wakijiuzulu nyadhifa zao kwani wanafahamu fika kuwa bado wanahitajika kwenye chama hicho kama ilivyokuwa kwa Rostam.

Sipati tatizo katika kuhitimisha kuwa Chadema ni kama wameshinda kwa vile katika ucgauzi huo walikuwa kama timu ya soka inayopambana na timu pinzani yenye wachezaji 15 (11 wa kawaida,refarii,kamisaa na washika vibendera wawili).CCM ilipewa kila aina ya sapoti kutoka serikalini,tukiweka kando vitisho vilivyotolewa na mawaziri kwa wapiga kura wa Igunga kuhusu "athari za kuwachagua wapinzani."

Lakini hapa tunazungumzia tuliyosoma magazetini na tuliyasikia redioni au kuyaona kwenye runinga.Kuna nguvu za giza ambazo hazikuweza-na kamwe haitowezekana-kuripotiwa.Hawa ni ndugu zangu wa Idara ya Usalama wa Taifa.Ukweli usiofahamika ni kwamba jamaa hawa ni kikwazo kikubwa sana kwa maendeleo ya demokrasia Tanzania kwani wanafanya kila wawezalo-kwa kutumia usiri wao-kuhakikisha CCM inaibuka na ushindi katika chaguzi mbalimbali.

Sasa kama Chadema imeweza kupata kura zote hizo licha ya vikwazo lukuki ilivyokabiliana navyo jimboni Igunga ni dhahri kuwa laiti chama hicho kikishikamana na kudumisha umoja na mshikamano basi 2015 tunaweza kurejea historia iliyojitokeza nchini Zambia hivi karibuni.

Ni muhimu kutoangalia kushindwa kwa Chadema katika uchaguzi huo pasipo kuhusisha jithada (halali na haramu za serikali,taasisi zake na watumishi wake).Kama Chadema imediriki kupata kura takriban 2000 tu pungufu ya mgombea wa CCM basi kitakwimu na kiuhalisi ni kama wameshinda vile.

Of course najua kuna watakaosema najipa matumaini.Well,mimi si mwanachama wa Chadema na sitegemei kuwa mwanachama wa chama hicho au chama kingine chochote kile huko nyumbani.Kwanza sina sifa ya kuwa mwananchama na pili malengo yangu ya kiajira yananizuwia kujihusisha na chama chochote kile cha siasa.

Basi nimalizie kwa kuipongeza Chadema kwa kumudu kutoa upinzani wa dhati licha ya vikwazo vyote ilivyokabiliana navyo.Uchaguzi huu-na kushindwa kwake-iwe changamoto muhimu ya kuwaandaa kukamata nchi hapo mwaka 2015.Mkiamua kiwa kitu kimoja basi ni dhahiri kuwa yaliyotokea Zabia hivi karibuni yatarudia tena mwaka 2015.

Penye nia pana njia

3 Oct 2011


Wenzetu Zambia wameweza, sie ‘tumerogwa’ na nani?
Evarist Chahali
Uskochi
28 Sep 2011
Toleo na 205
WIKI iliyopita tumeshuhudia wenzetu wa Zambia wakiamua kukipa kisogo chama tawala baada mgombea wa kilichokuwa chama cha upinzani cha Patriotic Front, Michael Sata kuibuka mshindi katika uchaguzi mkuu wa nchini humo.
Sata, anayefahamika pia kwa jina la utani la King Cobra, alimbwaga aliyekuwa Rais na mgombea wa chama tawala cha Movement for Multiparty Democracy (MMD), Rupiah Banda.
Katika mazingira ya kawaida ya siasa za Afrika, yayumkinika kuhitimisha kuwa ni vigumu sana kwa chama cha upinzani kushinda uchaguzi mkuu. Kikwazo kikubwa ni jinsi vyama tawala barani Afrika hutumia kila mbinu kuhakikisha kuwa utawala wao unadumu milele.
Kimsingi, hakuna tatizo kwa chama kimoja kuwa madarakani muda mrefu.Tatizo ni pale uwepo madarakani wa chama hicho unavyozidi kuididimiza nchi husika katika nyanja mbalimbali za maisha.
Kanuni isiyo rasmi ya kisiasa katika bara hili inatanabaisha kuwa ‘chama tawala hakiwezi kushindwa uchaguzi,’ na ikitokea kikashindwa basi labda ni kutokana na sababu kuu tatu.
Kwanza, kuteua mgombea asiyekubalika na wengi ndani ya chama hicho na hivyo kupelekea kura za chuki dhidi yake ambazo zitamnufaisha mpinzani wake mkuu.
Pili, katika sababu inavyoweza kushabihina na hiyo ya kwanza, ni pale chama tawala kinapogubikwa na migogoro isiyoisha na hatimaye baadhi ya waandamizi ndani ya chama hicho kukimfanyia hujuma mgombea wao kwa minajili ya kukomoana.
Sababu ya tatu ni ulevi wa madaraka. Pengine mfano mwepesi ni wa nyoka chatu ambaye akishakula kiumbe mkubwa anakuwa kama mfu. Anajisahau na laiti ukimwona kichakani baada ya mlo huo unaweza kudhani amezimia kama si kufa kabisa.
Sasa, baadhi ya vyama tawala baada ya kuwa madarakani muda mrefu vinafikia hatua ya kujisahau kwanini vipo madarakani.Vinaendesha mambo kwa mtindo wa ‘bora liende.’
Lakini sababu zote hizo hapo juu zinaweza zijitosheleze kukiondoa chama tawala madarakani kwa sababu mara nyingi uwepo madarakani wa chama hicho unazinufaisha taasisi nyingine  zisizo za kisiasa, kwa mfano vyombo vya dola.
Kuna imani kwamba taasisi za usalama kama vile jeshi la polisi, idara za usalama wa taifa na hata jeshi huenziwa vya kutosha na vyama tawala kiasi cha kujenga kile kinachofahamika katika elimu-viumbe (baiolojia) kama symbiotic relationship. Huu ni aina ya uhusiano wa kutegemeana, uhai wa mmoja ni uhai wa mwingine.
Taasisi hizo za dola hujenga au kujengewa imani potofu kwamba pasipo chama tawala kuwepo madarakani basi nazo zinaweza kupoteza uhai wake.Unaweza kujiuliza kwa nini taasisi yenye watu kadhaa ikajazwa imani potofu kirahisi namna hiyo?
Jibu ni kwamba mara nyingi taasisi hizo, kama ilivyo mazoea ya siasa katika nchi mbalimbali za Afrika, huongozwa kibinafsi. Mkuu wa taasisi husika hugeuka kuwa kama mmiliki wake.
Na marais huwa makini katika kufanya teuzi ambapo kigezo kikubwa huwa utiifu wa mteuliwa kwa Rais (sio utiifu kwa mujibu wa sheria na kanuni bali kwa sababu za kibinafsi).
Kwa hiyo, viongozi wa taasisi hizo hugeuka kuwa kama kirefusho (extension) cha matakwa binafsi ya Rais katika taasisi husika. Lengo ni kuhakikisha rais na chama chake wanaendelea kuwepo madarakani; huku taasisi hizo zikipindisha utekelezaji wa majukumu yake kwa manufaa ya chama tawala.
Watendaji katika taasisi hizo huaminishwa kuwa wanachofanya ni kwa mujibu wa sheria zinazoongoza utendaji kazi wao; japo kiuhalisia wanaotekeleza matakwa binafsi ya rais na swahiba yake aliyekabidhiwa jukumu la kuongoza taasisi husika.
Katika mazingira ya kawaida ya siasa zetu, vyama vya upinzani vinapopambana na chama tawala vinakutana na mazingira kama haya ya kinadharia ambapo kesi dhidi ya mtuhumiwa mahakamani inaendeshwa na mshtak ambaye pia ndio hakimu na mwendesha mashtaka. Ni wazi katika kesi ya aina hiyo ni lazima mtuhumiwa ashindwe na mshtaki ashinde.
Au mfano mwingine rahisi (wa kinadharia pia) ni pale timu ya soka inapopambana na timu nyingine yenye wachezaji 15; yaani wachezaji 11 wa kawaida wakisaidiwa na refa, washika vibendera wawili na kamisaa. Haihitaji kuwa na ufahamu wa soka kuelewa timu gani kati ya hizo mbili itaibuka mshindi.
Kwa huko nyumbani, ushindi wa Sata si habari njema kwa chama tawala CCM, chama ambacho hakina maelezo ya msingi ya kwa nini nchi yetu yenye utajiri lukuki inaendelea kuelemewa na lindi la umasikini unaochangiwa zaidi na ufisadi (huku wahusika wakuu wa ufisadi wakiwa ni baadhi ya viongozi wa chama hicho au wanapatiwa hifadhi salama dhidi ya hatua za kisheria).
Yayumkinika kuhisi kuwa CCM wanaombea hali nchini Zambia ichukue mkondo kama ule wa Kenya pale muungano wa wapinzani ulipofanikiwa kuking’oa madarakani chama kikongwe cha KANU. Kwa bahati mbaya (au makusudi) mabadiliko ya kisiasa nchini Kenya yalianza kwa dalili mbaya za vurugu zilizopelekea vifo kadhaa vya wananchi wasio na hatia.
CCM hawakushindwa kutumia mfano wa Kenya kuhalalisha hoja yake mfu kuwa ‘wapinzani wapo kwa ajili ya vurugu tu.’
Sijui sasa watasemaje kuhusu wapinzani kuchukua serikali nchini Zambia tukitarajia yaliyojiri Kenya hayatojitokeza kwa jirani zetu hao tunaounganishwa nao na Reli ya TAZARA (ambayo nayo iko hoi bin taaban kama ulivyo uchumi wetu).
CCM pia wana hoja yao nyingine maarufu kila unapokuja uchaguzi, iwe ni uchaguzi mdogo au uchaguzi mkuu ambapo huwalaghai wapigakura kwamba wasifanye kosa kuwapa madaraka wapinzani ambao hawana uzoefu wa kuongoza.
Hoja hiyo ni fyongo kwa sababu hakuna mwananchi anayehitaji chama chenye uzoefu wa ufisadi. Ni bora kufanya majaribio na chama mbadala cha upinzani - ambacho yawezekana kabisa kikawa makini kwenye utawala wake kwa kuhofia kung’olewa kama mtangulizi wake - kuliko kuking’ang’ania chama kilichoishiwa na uwezo wa kuongoza.
Ukiona chama kikongwe kinaruhusu viongozi wake kupanda majukwaani na silaha waziwazi (kama huko Igunga), basi, ujue tukiendelea kukiweka madarakani tutafika pabaya.
Siichukii CCM; bali nachukizwa sana na jinsi kinavyowafanya Watanzania kama wapangaji katika nchi yao. Kila kukicha ni hadithi za kukera na zisizoleta matumaini, ukiweka kando tuzo lukuki anazotunukiwa Rais wetu mpendwa Jakaya Kikwete huko nje ‘kwa kazi nzuri anayofanya kuongoza taifa letu.’
Ni fahari kuona Rais akipewa tuzo lakini ni matusi makubwa kutoka kwa watoa tuzo hizo pale wanapofumbia macho sababu zinazotufanya tuendelee kuwa masikini wa kutupa. Rais Kikwete anaweza kumaliza uongozi wake akiwa na historia ya kutunikiwa tuzo nyingi zaidi pengine zaidi ya Baba wa Taifa, lakini Watanzania hawatamkumbuka kwa tuzo hizo au picha aliyopiga na rapa 50 Cent; bali aliwafanyia nini katika miaka yake 10 ya utawala.
Mazoea yana athari moja kubwa ya kumfanya mwadamu akubali mabaya kwa vile tu yamekuwepo siku zote. Mazoea kwamba siku zote tumekuwa tukitawaliwa na CCM ni miongoni mwa sababu za takriban kila baya linaloweza kukufanya umlaumu Muumba kwa kukufanya uzaliwe nchini Tanzania.
Kwa hakika, wanaomlaumu Mungu kwa matatizo yetu wanatafuta ugomvi nae tu; kwani ametupa macho ya kuona uhuni tunaofanyiwa,ametupa ubongo wa kutuelewesha kuwa chini ya utawala wa CCM tutaendelea kuwa na maisha bora kwa mafisadi; huku walalahoi wakizidi kudidimia katika lindi la umasikini.
Na  ametupa masikio kusikia jinsi tuliowakabidhi dhamana ya kutuongoza wakitufisadi na kutukejeli kwa anasa zao za safari zisizoisha huko ng’ambo, visenti kwenye akaunti zao Ughaibuni, na utitiri wa mahekalu, magari ya kifahari na mapande makubwa ya ardhi waliyohodhi.
Kama Zambia wameweza, basi, nasi tunaweza pia. Na pengine hakuna namna nzuri ya wapiga kura kutoa pongezi kwa wenzao wa Zambia zaidi ya kuanza na fundisho la kwanza kwa CCM huko Igunga.
Kwa vile uhuni wa mbunge wa CCM Ismail Aden Rage kupanda na bastola kwenye mikutano wa kampeni hautopelekea hatua zozote za kisheria (hadi muda huu ninapoandika makala hii kilichofanyika ni kauli tu ya Waziri wa Mambo ya Ndani kutaka Rage ahojiwe badala ya kukamatwa),adhabu kubwa inaweza kutolewa na wapiga kura wa Igunga kwa kuigaragaza CCM, na kuitumia salamu kuwa kama imewezekana Zambia, Igunga napo inawezekana, na kwa hakika hata 2015 inawezekana kwa mapana zaidi.
Ndio, inawezekana iwapo kila mzalendo mwenye uchungu na Tanzania yetu atakapoamua kuwa IMETOSHA!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.