19 Dec 2007

Wiki hii nazungumzia unafiki wa baadhi ya wanasiasa wetu wakongwe waliokuwa karibu na Mwalimu Nyerere.Mwalimu aliwaamini,nasi pia tuliwaamini.Walikuwa wakiongea "lugha" ya Mwalimu:ujenzi wa jamii sawa isiyo na matabaka,inayothamini utu wa binadamu na yenye kumpa Mtanzania matumaini katika ardhi aliyozaliwa.

Lakini wakongwe hawa wa siasa waligeuka kama vinyonga mara tu baada ya Mwalimu kung'atuka,lakini their true colours zimejidhihirisha zaidi baada ya kifo cha Baba wa Taifa.Unaweza kujiuliza:walikuwa wapi akina Kingunge wakati linapitisha Azimio la Zanzibar (lililoua Azimio la Arusha)?Au kwa hivi karibuni,wako wapi maswahiba wa Mwalimu wakati tunashuhudia taifa letu likimung'unywa na mafisadi kwa "madili-kichaa" kama ya IPTL,Richmond,Buzwagi,nk?

Katika makala hiyo nimejaribu kutoa mfano hai wa maisha yangu udogoni kuonyesha namna nilivyokwepa kuwa mnafiki,lakini nisikumalizie uhondo.Bingirika na makala hiyo HAPA na ufaidike pia na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya Gazeti la RAIA MWEMA.




0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.