Showing posts with label KADHI COURT. Show all posts
Showing posts with label KADHI COURT. Show all posts

13 Mar 2009


BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limeibua upya hoja za kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na Jumuiya ya nchi za Kiislamu Duniani (OIC), kwa kuitaka serikali kutafakari kwa kina na hekima juu ya kuridhia kuanzishwa kwa vyombo hivyo.

Kuibuka tena kwa hoja hizo kumekuja miezi michache baada ya Rais Jakaya Kikwete kufunga mijadala hiyo iliyokuwa ikielekea kuwagawa wananchi kwa misingi ya kidini.

Hoja hizo zimeibuliwa juzi kwenye Baraza la Maulid na Naibu Katibu Mkuu wa Utawala wa Bakwata, Suleiman Lolila, ambaye aliitaka serikali iangalie upya na kwa hekima na kama inawezekana iharakishe masuala hayo mawili.

“Tunaipongeza serikali kwa hekima kubwa na jitihada inayoitumia katika kushughulikia masuala ya Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, Waislamu wanangoja kwa hamu na shauku kubwa ridhaa ya serikali, Inshallah, tunaiombea serikali ipate wepesi katika masuala haya maridhawa.

“Tunawaomba Waislamu wadhamirie kwa dhati katika suala hili la OIC na mahakama ya kadhi kwa kutokuruhusu mwanya wowote wa mifarakano miongoni mwetu, kwani mifarakano itakaribisha mgawanyiko na utengano miongoni mwa jamii,” alisema Lolila.

Naibu Katibu Mkuu huyo, akisoma risala ya Bakwata mbele ya Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alisema ili kuridhiwa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na OIC kuna hitaji utulivu wa hali ya juu miongoni mwa waumini wa dini zote mbili (Waislamu na Wakristo) ili kuipa serikali nafasi ya kufanya maamuzi ya busara kwa lengo la kuimarisha umoja wa kitaifa miongoni mwa jamii.

Suala la uanzishwaji wa mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, mwishoni mwa mwaka jana lilizua mjadala mpya nchini, baada ya kufika bungeni na kutishia kuwagawa wabunge kwa itikadi za kidini.

Oktoba mwaka jana katika hotuba yake, Rais Kikwete, hakutaka kuweka wazi ni lini Tanzania itaridhia kujiunga na OIC pamoja na uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, na badala yake aliwatuliza wananchi kwa kuwaambia wavute subira wakati serikali ikilifanyia kazi suala hilo kwa masilahi ya umma.

Rais Kikwete aliweka bayana kuwa ni mapema mno kuanza kutoa uamuzi wa masuala hayo, kwa kuwa bado utafiti haujakamilika pamoja na serikali kutotoa uamuzi wa mwisho, hivyo hakuna sababu kwa wananchi kulumbana.

26 Oct 2008


Moja ya matokeo (findings) katika utafiti wangu wa shahada ya uzamifu (ambao unahusu harakati za Waislamu nchini Tanzania) ni mtizamo wa asilimia kubwa ya Waislamu kwamba hawatendewi haki.Wapo wanaoona kuwa chanzo cha tatizo hilo ni sera za mkoloni (hawa si wengi),wengine wanaliona Kanisa Katoliki kama chanzo,huko wengine wakiilaumu serikali.Makundi hayo yako more complicated than nilivyoeleza.Kuna wanaohusisha ukoloni na ukristo,hivyo upinzani dhidi ya uislamu.Kuna wanaouona ukoloni kama mfumo wa kibaguzi (hapo ni siasa zaidi kuliko dini).Na kwa wanaolilaumu kanisa katoliki (au tuseme Wakristo),baadhi wanamwona Mwalimu Nyerere kama kibaraka wa Kanisa,wengine wanawatuhumu viongozi watengeneza sera hasa waliosomeshwa na kanisa (seminari) kuwa wanalitumikia kanisa indirectly.As to lawama kwa serikali,wengi wanaoiona kama inatumiwa na kanisa (hao ni wengi),na wanatuhumu baadhi ya viongozi wa serikali ambao ni waislamu kuwa wanatumika aidha kwa tamaa zao za kidunia au kwa vile hawana jinsi (mtumikie kafiri upate mtaji wako).Kwa kifupi,manung'uniko ya waislamu yalikuwepo wakati wa ukoloni (hasa kutokana na sera za kikoloni),yalikuwepo mara baada ya uhuru (japo hayakuonekana kutokana na siasa zilizozuia uhuru wa kujieleza) na yamejidhihirisha zaidi baada ya mageuzi ya miaka ya 80.Moja ya matatizo ya msingi ni ukimya wa policy makers katika at least ku-acknowledge existence ya manung'uniko hayo na dhamira thabiti ya kuyafanyia kazi.Kutambua kuwapo kwa tatizo ni hatua muhimu katika kulitafutia ufumbuzi.

Si nia yangu kutoa summary ya matokeo hayo hapa (nataraji kuchapisha kitabu baada ya kumaliza ngwe iliyobaki) bali lengo langu ni kuonyesha wasiwasi katika masuala mawili,kuanzishwa kwa mahakama za kadhi na Tanzania kujiunga na OIC,kwamba pasipo umakini nchi yetu itaelekea kubaya (I hope hapa sintaitwa mchochezi).Tayari viongozi wa kidini upande wa Wakristo wameeleza bayana upinzani juu ya masuala hayo.Viongozi wa Waislam nao wameeleza bayana kuchukizwa kwao na upinzani wa wenzao viongozi hao wa Wakristo,huku wakitarajia kuwa kinachosubiriwa ni utekelezaji tu.

Naomba kuweka wazi kuwa uchambuzi huu mfupi unafanyika kitaaluma,na hauhusiani na imani yangu kama Mkristo.Ni wazi kwamba hoja za kadhi na OIC zimekuwa zikitumiwa vibaya na wanasiasa,na wao ndio waliotufikisha hapa.Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 katika Sura ya Nane,Kipengere 108 (b) inaeleza dhamira ya chama hicho kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi Tanzania Bara.Kwa kutotoa ufumbuzi huo hadi zaidi ya nusu ya muhula wake madarakani,yayumkinika kuhitimisha kuwa suala hilo liliingizwa kwenye Ilani aidha pasipo kufanyika utafiti wa kutosha au kwa madhumuni ya kupata kura za Waislamu.Kama ambavyo baadhi ya findings za utafiti wangu zinavyoonyesha,ukimya katika masuala yanahohitaji ufafanuzi au maamuzi unachangia sana kuelta mkorogani kwa wadau wa mambo hayo.Wanaodhani kwamba kwa suala hili litapotea kwa kukaa kimya,sio tu wanajidanganya bali pia wanaiweka nchi yetu mahala pabaya.

Kuhusu suala la OIC,again, kauli za wanasiasa ambazo hazilengi kutoa ufumbuzi wa matatizo bali kuyaahirisha kwa kuahidi "mchakato" (Man,I really hate this word) ndio zimetufikisha hapa tulipo.Kama hoja ilikuwa ni mchakato,then why not kufanya huo mchakato kabla ya kukurupuka kuongea as if maamuzi yameshafanyika?Kuna mfano unaotolewa mara kwa mara kuhusu uanachama wa Uganda kwenye OIC.Does it mean kila wanachofanya Waganda lazima nasi tufanye?Binafsi nisingependa kusema hapa kwamba naunga mkono au napinga Tanzania kujiunga na OIC (nina sababu zangu za msingi kitaaluma) lakini busara nyepesi tu ingeweza kutumika katika the so-called mchakato:kuwa honest kwa Watanzania pasipo kujali imani zao.Honesty nayozungumzia hapa ni pointi kama je Watanzania wanahitaji uanachama wa OIC?Nasema Watanzania na sio Waislamu au Wakristo kwa vile katiba inasema nchi yetu haina dini,ila wananchi wana dini.Tatizo la OIC ni la kikatiba zaidi kuliko kisiasa,na ilipaswa wanaolizungumzia walioanishe na vifungu husika vya katiba.Unfortunately,katiba yetu nayo ni sehemu ya matatizo yanayotukabili.

Kwa kuhitimisha,naomba akili na busara itumike katika kuyashughulikia masuala haya mawili.Let's put common sense infront of emotions.Kwa bahati mbaya,masuala ya imani yana tabia ya kuwafanya wahusika kuwa emotional.Ni muhimu pia kwa wanasiasa wetu kuweka mbele maslahi ya taifa na sio ya kufurahisha nafsi zao au kuwafurahisha watu wachache.It can be done,tukiweka mbele maslahi ya umoja,mshikamano,upendo na utaifa wetu. 

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.