Showing posts with label MUSLIM-CHRISTIAN RELATIONS. Show all posts
Showing posts with label MUSLIM-CHRISTIAN RELATIONS. Show all posts

18 Apr 2013



Kwanini ninasema Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi a.k.a Mzee Ruksa AMELIKOROGA? Hebu soma msimamo wake wa awali kuhusu suala la kuchinja

Mwinyi: Kila mtu ruksa kuchinja • ASEMA IMANI NI NAFSI, HATA KULA CHURA SAWA
 na Asha Bani
RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amerejea kauli yake kuhusu mgogoro wa udini akisema kila mtu ana haki ya kuchinja kutokana na imani yake ilimradi tu asivunje sheria za nchi. 
Mwinyi alisema anashangaa kuona watu wakigombania kitu kidogo kama kuchinja ilihali Tanzania ina utamaduni wa amani siku zote na kwamba kila mtu ana imani yake ya dini anayoiamini. 
Kiongozi huyo mstaafu alitoa msimamo huo jana jijini Dar es Salaam katika kongamano juu ya utamaduni wa Kiislamu Afrika Mashariki ambapo Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji.
“Imani ni nafsi ya mtu na haitakiwi kumlazimisha kula nyama iliyochinjwa na mwenzie. Na kama unaona aliyochinja mwenzio ni kibudu basi usile chinja yako, kula hata ukitaka kula chura, mjusi, konokono, kula utakacho ruksa ilimradi tu usiingie katika jinai,” alisema. 
Mwinyi alikumbusha kuwa hata wakati wa utawala wake majaribu kama hayo yaliwahi kumtokea, lakini alijitahidi kuweka sawa kwa kumwambia kila mtu ale kile anachofikiri ni chakula bila kumlazimisha mwenzake. 
Alisema Watanzania wamezaliwa ardhi moja na kwamba kinachotakiwa ni kuwa na misingi ya kuvumiliana, na kwamba sifa ya Uislamu ni pamoja na kuwa na uvumilivu.
Aliongeza kuwa Uislamu si kufanya vurugu kama inayotafsiriwa na makundi ya wanaotaka kuvunja amani ya nchi kwa kutumia jina la dini ya Kiislamu.

Sasa linganisha msimamo huo wa awali na hicho alichoongea Mzee Ruksa kwenye video hapo juu.

Yawezekana Rais huyo mstaafu ameamua 'kulamba matapishi yake' (kusema 'amefafanua' ni kupotosha ukweli kwani alichoongea kwenye video ni tofauti kabisa na alichoongea awali) baada ya kupata shinikizo kutoka kwa Waislam wenzie. Au albda nafsi tu imemsuta.

Nitajadili kwa kifupi suala hili kama Mtanzania na pia kama Mkristo. Kama tunakubaliana kuwa Tanzania haina dini, lakini Watanzania wana dini,basi kila dini inapaswa kuheshimu uhuru na haki za wenzao. Kama sheria za kidini zinawataka Waislam kuchinja, na zile za Wakristo haziwalazimishi kuchinja, basi kila mmoja afuate kile kinachoelekezwa na dini yake.

Mzee Ruksa anaposema Biblia ipo kimya kuhusu suala la kuchinja haimaanishi kuwa ukimya huo unatoa ruhusa kwa Wakristo kulazimishwa kufuata matakwa ya Waislam au wapagani.Msimamo wake wa awali ulikuwa sahihi kabisa: kila mtu afuate imani yake, na hata mtu akitaka kula chura aachiwe uhuru wa kufanya hivyo.

Kimsingi, Mwinyi amechochea moto kwenye mjadala huo japo katika video hiyo anaonekana kama angependa Watanzania waishi kwa amani na umoja. Lakini haiwezekani kuishi kwa amani na umoja iwapo dini moja inafanywa kuwa yenye haki zaidi ya dini nyingine. Haki ya Waislam kuchinja shurti iendane na utambuzi wa haki ya Wakristo kutolazimika kuchinja. Hatuwezi kuzungumzia haki za Waislam lakini wakati huohuo tukapuuza haki za Wakristo.

Hivi ikitokea Wakristo wanataka kuchinja nguruwe itabidi watafute Musilam wa kuwacvhinia ilhali nguruwe ni haramu kwa Waislamu?

Sorry Mzee Ruksa, hii flip-flop imeturejesha kwenye tatizo lile lile la udini: kuangalia upande mmoja wa imani na kupuuza upande mwingine. 



 

28 Nov 2010


Waislam wakiwa kwenye swala.Picha hii haihusiani moja kwa moja na habari ifuatayo
Waislam wenye msimamo mkali wanashukiwa kuyachoma moto majengo mawili ya kanisa huko Zanzibar,tukio lililotokea Jumapili iliyopita huku waumini wa makanisa hayo wakipokea vitisho vya kuuawa.

Majengo hayo ya Kanisa la Assemblies of God (TAG) na Evangelical Assemblies of God Zanzibar (EAGZ) katika kijiji cha Masingini kilichopo kilomita 5 kutoka mjini-kati Zanzibar yalichomwa moto takriban saa 2 usiku,kwa mujibu wa Askofu Fabien Obeid wa EAGZ.Polisi wa Mwera walipata taarifa ya tukio hilo kesho yake asubuhi.

Matukio hayo ni mwendelezo wa vitendo vya kuwatisha Wakristo katika eneo hilo lenye Waislam wengi,na kuibua hofu kwamba Waislam wenye msimamo mkali wanaweza kudiriki kufanya lolote lile kuzuwia ustawi wa Ukristo.

“Muislam mmoja alisikika akisema, ‘Tumesafisha eneo letu kwa kuharibu makanisa mawili,na sasa tuna mpango wa kuwaua waumini wa makanisa haya mawili-hatutaruhusu kanisa kujengwa tena,’” alisema muumini mmoja wa kanisa ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.

Jengo hilo la matofali la TAG lilikuwa katika hatua za mwisho za ujenzi,na kwa mara ya kwanza Jumapili hiyo waumini walifanya ibada katika jingo hilo jipya.Jengo la EAGZ ambalo waumini takrban 30 walihudhuria ibada lilikuwa la udongo.

Pasta Michael Maganga wa EAGZ na Pasta Dickson Kaganga wa TAG walieleza hofu yao kuhusu hatma ya kanisa hapo Masingini.Mapasta wa Zanzibar walitarajiwa kukutana jana (Jumamosi) kujadili namna ya kukabiliana na uharibifu huo,alieleza Mwenyekiti wa Usharika wa Mapasta Zanzibar,Askofu Lonard Masasa wa Kanisa la EAGT.

Kwa muda mrefu Waislam wenye msimamo mkali visiwani Zanzibar,wanaoungwa mkono na baadhi ya viongozi wa serikali katika maeneo husika,wamekwaza uwezekano wa Wakristo kupata ardhi kwa minajili ya ujenzi wa majengo ya ibada.Kuna nyakati ambapo wamebomoa majengo yaliyopo na badala yake kuanzisha ujenzi wa misikiti.

Huku wakikanganywa na kutopata ushirikiano wa serikali katika kuwashughulikia wahusika wa matukio hayo,viongozi wa makanisa wameeleza kuwa uwezekano wa waliochoma moto majengo hayo kukamatwa ni mdogo.Mara nyingi,serikali huegemea upande wa wanaofanya matukio hayo,kuchelewesdha uchunguzi kwa hofu ya kuwaudhi Waislam walio wengi ambao wanapinga kuenea kwa Ukristo.

Mwaka jana,maafisa wa serikali katika eneo la Mwanyanya-Mtoni waliungana na Waislam wa eneo hilo kujenga msikiti katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kanisa la EAGZ,alieleza Pasta Paulo Kamole Masegi.

Pata Masegi alinunua ardhi mwezi Aprili mwaka 2007 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa katika eneo hilo la Mwanyanya-Mtoni,na kufikia mwezi Novemba mwaka huohuo tayari kulikuwa na jengo lililotumika kama sehemu ya ibada kwa muda.Muda si mrefu Waislam wa eneo hilo walipinga hatua hiyo.

Mwezi Agosti mwaka jana,Waislam hao walianza ujenzi wa msikiti futi tatu tu kutoka kitalu cha kanisa.Mwezi Novemba mwaka huohuo,Pasta Masegi alianza ujenzi wa kanisa la kudumu.Waislam wenye hasira walivamnia eneo hilo na kubomoa msingi wa jengo hilo,alieleza Pasta huyo.

Viongozi wa kanisa waliripoti tukio hilo kwa polisi,ambao hawakuchukua hatua yoyote- na walikataa kutoa ripoti ya tukio,hivyo kukwamisha suala hilo kufikishwa mahakamani,alisema Pasta Masegi.

Wakati huohuo,ujenzi wa msikiti ulikamilika mwezi Desemba (mwaka jana).Hatma ya mpango wa ujenzi wa kanisa ilielekea kufikia ukomo mapema mwaka huu baada ya Mkuu wa Wilaya Ali Mohammed Ali kumfahamisha Pasta Masegi kuwa hana haki ya kufanya ibada katika jengo husika.

Kihistoria, wafanyabiashara wa Kiislam kutoka Ghuba ya Uajemi walifika visiwani Zanzibar mapema karne ya 10 baada ya kusukumwa na pepo za monsoon katika Ghuba ya Aden.Muungano wa visiwa hivyo na Tanganyika mwaka 1964 (na kuunda Tanzania) uliwaacha Waislam visiwani humo wakiwa na hofu kuhusu Ukristo,wakiuona kama njia inayoweza kutumiwa na Tanzania Bara kuwatawala,na tangu wakati huo kumekuwa na hali ya mashaka.


1 Dec 2008


Over 300 people have died in Muslim-Christian clashes in the worst sectarian violence in Nigeria since 2004.
Angry mobs burned homes, churches and mosques on Saturday in the central state of Plateau, according to The Associated Press.

Initially a clash between supporters of the region’s two main political parties, the violence was soon divided along ethnic and religious lines.

Tension began when electoral workers did not post the results in ballot centers, causing many locals to assume the election was going to be another fraudulent political event. After riots broke out, a curfew was declared and the governor of Plateau state ordered troops to shoot on sight to enforce the curfew in neighborhoods affected by the violence.

About 7,000 people in conflict areas have left their homes and are seeking refuge in government buildings and religious centers, the Red Cross reported.

Sectarian violence is not new in Plateau, with more than 1,000 people killed in Jos – the state’s capital – in September 2001 due to Christian-Muslim hostility.

This weekend’s sectarian violence was the worst clash in the West African nation since 2004, when as many as 700 died in Plateau and over 100 churches were destroyed. The 2004 violence was said to have been sparked by land disputes between members of the predominantly Christian Tarok tribe and Muslim Hausa-Fulani farmer.

Nigeria is split nearly evenly between a predominantly Muslim north and a Christian south. According to Compass Direct, religious conflicts between Muslims and Christians have claimed more than 10,000 lives since 1999.

SOURCE: EURWEB

WAKATI HAYO YAKIENDELEA HUKO NIGERIA,INAELEKEA BADO KUNA WENZETU HUKO NYUMBANI TANZANIA WANGEPENDA TUONJE HAYO YANAYOWAKUTA WENZETU WA NIGERIA.HEBU SOMA KWANZA STORI HII HAPA CHINI

Waislamu, Wakristo waishika pabaya CCM
NI KATIKA SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI, OIC

Na Geofrey Nyang’oro

WAUMINI na dini mbili kuu nchini za Kiislamu na Kikristo wameiweka pabaya serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kufanya maamuzi kutokana na mvutano mkali unaoendelea, huku pande hizo zikiwa zimeshikilia misimamo mikali kuhusu hoja ya Mahakama ya Kadhi na nchi kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC).

Mjadala kuhusu masuala hayo mawili ulikuwa umepoa, lakini uliibuka hivi karibuni baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk Bernard Membe, kuzungumzia suala la OIC wakati akizungumza na waandishi kuhusu ziara ya rais nje ya nchi.

Baada ya maaskofu kuitahadharisha serikali ya CCM kuwa hawatafanya nayo kazi iwapo itashikilia msimamo huo wa kujiunga na OIC, jana Waislamu nao waliipa serikali mwezi mmoja iwe imeshatoa tamko rasmi kuhusiana na hoja hizo, vinginevyo wataing'oa CCM madarakani kwa kuwa imeshindwa kutekeleza suala hilo, wakidai suala la Mahakama ya Kadhi limo kwenye ilani ya chama hicho tawala.

Kauli hiyo ilitolewa na Waislamu kwenye kongamano la "Hatima ya Elimu ya Uislamu na Urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi," lililofanyika kwenye Ukumbi wa PTA jana jijini Dar es Salaam jana.

Pia kwenye kongamano hilo, Waislamu walimtaka Waziri Membe kuomba radhi au kujiuzulu kutokana na kauli yake ambayo walidai kuwa, inakashifu fedha kutoka OIC kwa madai kuwa ni ya shetani.

Walitoa msimamo huo wakati waumini wa makanisa mbalimbali yaliyo chini ya CCT, KLPT wakiwa wameshatoa tamko lao la nguvu kupinga hatua ya serikali kudhamiria kujiunga na OIC, wakieleza athari ambazo serikali itapata iwapo haitakuwa makini.

"Tuna uhakika kuwa yaliyomo ndani ya OIC ni hatari kabisa, kwani endapo yakikubalika katiba, nchi itakuwa imevunjika na Watanzania watakuwa wameingia katika migogoro itakayoua maridhiano, mshikamano, utengemano na umoja wa kitaifa, " walisema maaskofu hao katika tamko lao.

Rais Jakaya Kikwete pia alitaka waumini wa Kiislamu kuwa na subira na kuiachia serikali itafakari kwa utulivu ili ifanye uamuzi ya hekima utakaojenga na kulihakikishia taifa umoja, amani, utulivu na upendo miongoni mwa raia.

"Tujiepushe na vitendo au kauli ambazo zitawatia watu hofu na kujenga chuki miongoni mwa raia wa nchi yetu wanaopendana na kujenga chuki na kutoaminiana baina ya raia na serikali yao inayowapenda na kuwathamini," alisema Rais Kikwete mwezi uliopita.

Lakini Waislamu jana wakawa na kauli kali wakati wakijadili masuala hayo kwenye kongamano hilo, ambalo pia lilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa Kikristo na kufikia hatua ya kutoa tamko hilo na wameazimia kufanya maandamano makubwa jijini Dar es Salaam ambayo yatakwenda sambamba na mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika kesho kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Akizungumza kwenye kongamano la jana, Katibu Mkuu wa Baraza la Habari la Kiislamu Tanzania (Bahakita), Sheikh Sadiki Godigodi alisema suluhisho la uwepo wa haki na usawa kwa wote hapa nchini ni urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi pamoja na upatikanaji wa haki ya kielimu kwa Waislamu.

Alisema ukimya wa serikali ya CCM kuhusu Mahakama ya Kadhi unaonyesha kuwa serikali hiyo, ambayo walidai inaongozwa na Jumuiya ya Kikristo (CCT), kutokana na kuonyesha kuipinga dhana hiyo, haina nia ya kutekeleza ilani yake licha ya kwamba suala hilo halina madhara kwa Watanzania wote na ni muhimu kwa dini ya Kiislamu na Uislamu kwa ujumla.

Godigodi alisema kwa sasa Uislamu hapa nchini hautakuwa tayari kudhulumiwa haki zake na hautakuwa tayari kuona mtu yeyote anajitokeza kukwamisha jitihada za kudai haki zao ambazo ni urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi na nchi kujiunga na OIC na kudai kuwa mtu yeyote atakayejitokeza kupinga jitahada hizo, atakuwa anatangaza uadui kati yake na Uislamu.

Sheikh Mustafa Lema kutoka Arusha alisema anashangazwa na serikali ya CCM licha ya kuliweka suala la Mahakama ya Kadhi kwenye ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005, imeamua kukaa kimya katika utekelezaji wake.

Alisema Mahakama ya Kadhi ni suala la kiimani katika dini ya Uislamu na wala si la dini ya Kikristo wala serikali, hivyo jambo la msingi linalotakiwa kufanywa na serikali ni kurudishwa kwa chombo hicho.

“Ukimuuliza Mkristo anajua nini kuhusu dini atakupa habari kuhusu maaskofu, mashemasi na wachungaji na mambo yote yanayofanyika ndani ya imani yao, ukimuuliza Mwuislamu yeye atakueleza habari za masheikh, OIC na Mahakama ya Kadhi, hiyo ndiyo imani yao iweje leo Wakristo waje kuipinga Mahakama ya Kadhi ambayo siyo suala la imani yao?” alihoji Godigodi.

“Sisi tunataka Mahakama ya Kadhi ili tuweze kutetea haki zetu, hatuwezi kushughulikia mambo yahusuyo Uislamu ikiwa ni pamoja na mirathi, talaka na mali za Uislamu kama kiwanja cha Chang’ombe,” aliongeza.

Walisema kutokana na serikali ya CCM kuendelea kudhulumu haki za Uislamu na kuwachezea mara kwa mara kwa kushindwa kushughulikia masuala hayo, hawatakuwa tayari kukichagua chama hicho na badala yake watafanya kila linalowezekana kuhakikisha Waislamu wanakitosa chama hicho kwenye chaguzi zijazo.

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema suala la Mahakama ya Kadhi linapaswa kuanzishwa, lakini akasisitiza uwepo wa elimu ya kutosha katika suala hilo.

Alisema tatizo lililopo ni watu kutojua nini maana ya Mahakama ya Kadhi na kazi zake na kwamba kama watapatiwa elimu ya kutosha na kueleweshwa vema, itaanzishwa kwa amani na utulivu.

Alisema elimu pekee ndiyo itakayokwenda sambamba na mijadala ya uso kwa uso kati ya makundi yote mawili na hivyo kuwezesha uanzishwaji wa mahakama hiyo kuwa wa amani.

“Tatizo linalosababisha watu kupinga ni kutoelewa Mahakama ya Kadhi nini na kazi zake. Hapa inatakiwa elimu kwa wananchi wote kuhusu mahakama hiyo ili kuwaondoa hofu," alisema.

Hata hivyo Mbatia aliwataka Waislamu kuiachia serikali ifanye kazi zake katika kushughulikia hilo kutokana na ukweli kuwa iliahidi kulishughulikia.

Katika kongamano hilo, Waislamu hao walianzisha mchango wa hiari ili kupata Sh2 milioni kwa kwa ajili ya kuendesha zoezi la kufanya kampeni ya kuzunguka nchi nzima kutangaza azma yao ya kukusanya kadi na kuzirudisha kwa CCM kama serikali haitatekeleza suala hilo.

CHANZO: Mwananchi

TATIZO LETU NI KUKURUPUKA KWA WANASIASA AMBAO WAKATI WA CHAGUZI HUTOA AHADI KAMA ZILE ZA KWENYE WIMBO NDIO MZEE WA PROF JAY ILHALI WANAJUA KABISA HAWANA UWEZO WA KUZITEKELEZA.KULIKUWA NA HAJA GANI KWA CCM KUINGIZA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 AHADI YA KUPATIA UFUMBUZI SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI IWAPO HAIKUWA INAJUA NAMNA YA KUITEKELEZA?NA NANI ALIMTUMA MEMBE KUROPOKA HUKO DODOMA KUHUSU OIC WAKATI MAMBO BAADO KABISA?KAMA ILIVYO RAHISI KWA DEREVA ASIYE MAKINI KUSABABISHA AJALI NDIVYO WANASIASA WASIO MAKINI WANAVYOWEZA KUINGIZA NCHI KATIKA MATATIZO AMBAYO YANAWEZA KABISA KUEPUKIKA.NA KAMA ILIVYO KAWAIDA,WALIOWASHA MOTO HUO WAKO KIMYA KWA SASA KANA KWAMBA SIO WAO WALIOTUFIKISHA HAPA.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.