Showing posts with label POLISI TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label POLISI TANZANIA. Show all posts

30 May 2009


MHH,AJALI ZINAZOWAANDAMA WABUNGE "WA AINA MOJA" ZINAWEZA KUZUA MASWALI YA NAMNA FLANI JAPO YAWEZEKANA KABISA KUWA NI AJALI KAMA NYINGINEZO.HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO,KISHA TUJIULIZE MASWALI MAWILI MATATU:

Ally Sonda na Rehema Matowo, Mwanga

MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Aloyce Kimaro amenusurika kufa baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kuparamia mawe yaliyopangwa barabarani na kupata ajali usiku wa kuamkia jana. Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na Kimaro na polisi zinasema kuwa, ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mikongeni kata ya Lembeni wilayani Mwanga, Kilimanjaro kwenye barabara kuu ya Moshi-Tanga, akiwa safarini kutoka Dar es Salaam kwenda jimboni kwake.

Kwa mujibu wa habari hizo, wakati ajali hiyo inatokea, Kimaro alikuwa na rafiki yake Joseph Temu ambaye ndiye aliyekuwa anaendesha gari hilo aina ya Mercedes Benz akiwa na mkewe na watoto wake watatu. Katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa.

Kimaro alisema baada ya ajali hiyo mfanyabiashara wa Mwanga, Shafii Hasanal alitoa msaada wa kulivuta gari hilo hadi kwenye kituo cha mafuta Kisangara.

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko alisema kuwa ajali hiyo ilitokea saa 2:30 usiku, chanzo kikiwa ni mawe makubwa na matofali yaliyokuwa yamepangwa barabarani katika eneo lenye kona na mlima.

Kamanda Ng’hoboko alisema kuwa watu wanaosadikiwa kuwa ni wezi, walipanga mawe hayo barabarani kwa lengo la kusababisha ajali ili kuwaibia abiria.

“Gari ya mbunge huyo ilipofika katika eneo hilo likiwa katika mwendo wa kawaida na mbele yao kukiwa na lori ambalo liliweza kuyapita mawe hayo bila tatizo, wao walipojaribu kuyapita tairi la mbele upande wa kulia na ‘sampo’ ya gari hilo vilipasuka wakashindwa kuendelea na safari,” alisema Ng’hoboko.

Kamanda huyo alisema kuwa miaka ya nyuma eneo hilo lilikuwa na matukio mengi ya aina hiyo ambayo yameanza kujitokeza upya, kwa kuwa awali wananchi wa eneo hilo kwa kushirikiana na polisi walikuwa wameyamaliza. Alibainisha kuwa polisi wanafanya operesheni ili kuwadhibiti wezi hao na kuwasaka waliohusika na tukio hilo ili wafikishwe mbele ya sheria.


Kimaro ni miongoni mwa wabunge waliojitokeza hadharani kupambana na vitendo vya ufisadi. Mwaka jana aliibua hoja bungeni kutaka, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ashitakiwe kwa kutumia madaraka vibaya ya kufanya biashara akiwa ikulu.

Hii ni ajali ya pili inayohusisha wabunge kutokea ndani ya wiki mbili baada ya ajali iliyomhusisha mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe iliyotokea eneo la Ihemi, Ifunda mkoani Iringa. Dk Mwakyembe, alinusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kutoka Kyela kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka.

Ripoti ya polisi iliyotolewa wiki hii ilieleza kwamba ajali hiyo ilitokana na uzembe wa dereva, lakini mbunge huyo ameiponda na kuifananisha na ripoti ya mpiga ramli kwa vile haikuzingatia vigezo na utaalamu katika uchunguzi.


CHANZO: Mwananchi
NAAMINI WENGI WETU TUNAKUMBUKA AJALI ILIYOMHUSISHA MHESHIMIWA CHEYO a.k.a "Mzee wa Vijisenti" AMBAYO ILIPELEKEA VIFO VYA WATU WAWILI.TOFAUTI KATI YA AJALI YA CHENGE NA HIZI ZA MWAKYEMBE NA KIMARO NI REACTION YA POLISI.BAADA YA GARI LA CHENGE KUUA,SIKUWAHI KUSIKIA RPC AU RTC AKIKURUPUKA KUELEZA CHANZO CHA AJALI HUSIKA (JAPO KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA,NI RAHISI KUIHUSISHA AJALI YA SAA 10 ALFAJIRI NA STIMU ZA KILEVI).BADALA YAKE ILIUNDWA TUME AMBAYO HADI LEO HAIJATUELEZA MATOKEO YA UCHUNGUZI WAKE (IF AT ALL ILIFANYA UCHUNGUZI).WORSE STILL,INAELEZWA KUWA WAKATI AJALI HIYO INATOKEA GARI LA CHENGE LILIKUWA NA BIMA ILIYOISHA MUDA WAKE.


ALIPOPATA AJALI MWAKYEMBE,RPC AKAKURUPUKA NA KUDAI KWAMBA CHANZO CHA AJALI NI MWENDO MKALI NA SHIMO LILILOKUWA BARABARANAI.BAADAYE TUME YA KAMANDA KOMBE IKAZIDI KUCHANGANYA MADAWA KWA KUTOA FINDINGS AMBAZO SI TU ZIMEINGILIA KAZI YA MAHAKAMA KWA KUWAHUKUMU MWAKYEMBE (kuwa alikuwa amelala wakati wa ajali) NA DEREVA WAKE (kwa uzembe) LAKINI PIA HAZIKUHUSISHA MAELEZO YA MWAKYEMBE KWA VILE HAKUHOJIWA NA TUME HIYO!


KINGINE CHA KUSHANGAZA NI KWAMBA WHILE KWENYE AJALI YA CHENGE,DEREVA WA BAJAJI NA MMILIKI WAKE WALIAMRIWA KUJISALIMISHA POLISI MARA MOJA,HATUJASIKIA KAULI YOYOTE KUTOKA KWA POLISI KUHUSU DEREVA WA LORI LILIOHUSIKA KWENYE AJALI YA MWAKYEMBE!


NA SASA KATIKA AJALI YA KIMARO TUNAELEZWA KUWA MAWE HAYO YALIPANGWA NA WEZI.HOW DID THE POLICE KNOW KUWA WALIOFANYA HIVYO NI WEZI NA SIO WATU WALIOKUWA WANAWINDA UHAI WA MHESHIMIWA KIMARO?KWANINI(ANGALAU KWA KUTUZUGA) ISIUNDWE TUME KAMA ILE YA AJALI YA CHENGE AMBAPO HAKUKUWA HATA HAJA YA KUFANYA SPECULATION LET ALONE KUUNDA TUME?


CALL ME A CONSPIRACY THEORIST,LAKINI NADHANI AJALI HIZI ZINA TAFSIRI KUBWA ZAIDI YA TUNACHOSIKIA AU KUONA KWA MACHO YETU.LET'S WAIT AND SEE!



29 Mar 2009

(Picha kwa hisani ya KENNEDY)

Gazeti la Majira limepotea mtandaoni kwa muda mrefu sasa,na kwa akina sie tunaotegemea habari za nyumbani kupitia nakala za kielektroniki za magazeti husika mkombozi wetu mkuu amebaki Mr Kennedy.Na ni kwa kupitia tovuti yake ndipo nilikutana na version isiyopendeza ya habari kuhusu ajali iliyomhusisha Mzee wa Vijisenti,Andrew Chenge,na kupelekea vifo vya akinadada wawili.

Gazeti la Majira lilidai kuwa marehemu hao ni "machangudoa waliokuwa wanatokea Maisha Club".Sijui vyanzo (sources) vyao vya habari husika ni vipi lakini mwandishi yeyote mwenye busara angepaswa kujiridhisha kuhusu identity halisi ya marehemu hasa kwa vile tunazungumzia watu waliopoteza maisha.Hivi mwandishi huyo atajisikiaje iwapo baada ya uchunguzi itagundulika kuwa marehemu hao hawakuwa machangudoa?In fact,magazeti kadhaa yameripoti maelezo ya ndugu za marehemu yanayoeleza kwamba mmoja wao alikuwa mfanyabishara na mwingine mfanyakazi wa hoteli jijini Mwanza.

Pengine haikuwa nia ya mwandishi kuwa-describe marehemu hao kama changudoa (labda kutokana na haraka ya kuwahisha habari kwa mhariri) lakini taswira ya haraka iliyopatikana kutoka katika habari hiyo ni ujenzi wa matabaka:kigogo (mzee wa vijisenti) kagonga fukara (changudoa).By the way,hata hata kama hao mabinti wangekuwa machangudoa as suggested by the Majira reporter bado haiondoi haki yao ya kuwa hai muda huu!

Kingine ambacho hakihusiani na uandishi japo kinahusu tukio hilo la kusikitisha ni namna Jeshi la Polisi linavyoonekana "kubabaika" katika kushughulikia ajali hiyo.Kwa mujibu wa vyombo vya habari,Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Suleiman Kova,ameunda TUME MAALUM ya kuchunguza ajali hiyo eti kwa "kuzingatia uzito wa tukio hilo".Chenge ni Mtanzania kama mie na wewe,na kama amehusika na ajali basi sheria za uslama barabarani zifanye kazi yake.Sijui ni madereva wangapi walalahoi wanaopata "bahati" kama ya Chenge ya kuundiwa tume!

Kamanda Kova anadai kuwa tume hiyo imeundwa ili "kusiwepo mwanya wowote ,taratibu zote zitafuatwa bila kujali nani na wala nafasi aliyonayo....na kuleta uwazi na utawala bora" (kwa mujibu wa gazeti la Majira) na pia amenukuliwa na gazeti la Mwananchi akisema kuwa "hapa bwana hakuna mchezo wala hakuna kuangalia vyeo wala nani ni nani...".Hivi matamshi kama hayo (iwapo kesi itapelekwa mahakamini) hayawezi kutumiwa na wakili wa Chenge kudai "ameonewa kwa vile Kamanda Kova alishadai hawataangalia vyeo-which directly points to Chenge ambaye licha ya kuwa ex-minister,pia ni munge na kigogo wa CCM?"

Kama nilivyoandika jana,tuendelee kuwapa polisi benefit of doubt kwa matarajio kwamba wanafahamu bayana kuwa tukio hilo linaangaliwa na Watanzania wengi kama kipimo cha haki sawa kwa wote (huku wakiwa na kumbukumbu ya kesi ya marehemu Ditto).

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.