Showing posts with label RAIA MWEMA UGHAIBUNI. Show all posts
Showing posts with label RAIA MWEMA UGHAIBUNI. Show all posts

30 Oct 2011




BLOGU HII INAPENDA KUTOA SALAMU ZA HERI YA SIKU YA KUZALIWA KWA JARIDA MWANANA LA RAIA MWEMA AMBALO LILIZALIWA SIKU KAMA YA LEO MIAKA MINNE ILIYOPITA.

BINAFSI,JARIDA HILI NI KAMA SEHEMU YA MAISHA YANGU.TANGU WAHUSIKA WANIPATIE NAFASI YA KUANDIKA KATIKA JARIDA HILO KWWENYE SAFU YA TAIA MWEMA UGHAIBUNI NIMEKUWA NIKISHIRIKIANA NAO HATA NJE YA FANI YA UANDISHI.NILIPOUGULIWA NA MAREHEMU MAMA MWAKA 2008 NA HATIMAYE ALIPOFARIKI,WAHUSIKA WA JARIDA HILI WALIKUWA NAMI BEGA KWA BEGA.

NAKUMBUKA VIZURI SIKU NILIPOZURU OFISI ZAO KWA MARA YA KWANZA NA JINSI NILIVYOPOKELEWA KANA KWAMBA SOTE TULIKUWA TUKITANA HAPO OFINI KILA SIKU YA WIKI.

LAKINI KUBWA ZAIDI NI MCHANGO WA JARIDA HILI KWA JAMII.LICHA YA HABARI ZAKE MAKINI JARIDA LA RAIA MWEMA LIMEJIJENGEA SIFA KUBWA KWA KUWA NA MAKALA ZINAZOANDIKWA KWA UMAKINI WA HALI YA JUU NA LIMEFANIKIWA KWA ASILIMIA 100 KUTOELEMEA UPANDE WOWOTE ZAIDI YA KUSEMA UKWELI NA KUWA SAUTI YA WASIO NA SAUTI.

NAJISIKIA FAHARI KUBWA KUWA MIONGONI MWA WANA-TIMU WA JARADA HILI,NA NI FURAHA KUBWA KUONA RAIA MWEMA LIKITIMIZA MIAKA MINNE HUKO LIKIZIDI KUPAA KWA KUAMINIKA KATIKA JAMII NA KUENDELEA KUUTUMIKIA UMMA KWA UADILIFU.

KWA MARA NYINGINE TENA,NA KWA NIABA YA WASOMAJI WA BLOGU HII,NAOMBA KUSEMA TENA HAPPY BIRTHDAY RAIA MWEMA

22 Oct 2010


Kama ilivyo ada,toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema limesheheni habari moto moto na makala zilizokwenda shule.

Makala yangu katika toleo hili inazungumzia kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Jumapili wiki ijayo.Nimejaribu kujenga hoja kwanini miaka mingine mitano kwa Jakaya Kikwete ni hatari kwa ustawi wa taifa letu.

Nisikupunje uhondo bali bingirika na makala hiyo kwa KUOBONYEZA HAPA.

15 Oct 2010


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida maridhawa la Raia Mwema inazungungumzia madai ya mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,kuwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete imesambaza maafisa usalama nchi nzima ili kuhujumu uchaguzi (kumsaidia Kikwete ashinde).Kwa kutumia taaluma na utaalam wa kutosha kuhusu masuala ya intelijensia,makala inajaribu kumpa mwangaza msomaji iwapo Idara yetu ya Usalama wa Taifa inaweza kutumiwa visivyo katika mazingira tuliyonayo sasa.

BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule katika jarida hili mahiri la Raia Mwema

8 Oct 2010

Katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema nazungumzia kuhusu tuzo ya milenia,msaada tuliopewa na Waingereza baada ya kuridhishwa kwao na "nidhamu na matumizi yetu" na sifa alizomwaga Obama kuhusu "utawala bora".Cheki makala hiyo hapa bila kusahau makala na habari nyingine motomoto ndani ya jarida hilo maridhawa.

12 Aug 2010

Baada ya kimya cha miaka miwili na mwezi mmoja hatimaye nimerejea katika ulingo wa uandishi wa makala zangu za Raia Mwema Ughaibuni katika jarida maridhawa la Raia Mwema.Haikuwa rahisi kwangu kukaa kimya huku nchi yetu ikiteketezwa na mafisadi lakini ililazimu kuwa hivyo ili kujipanga upya.

Katika makala ya wiki hii nimeelezea kwa kifupi kilichonisibu hadi nikafikia uamuzi wa kusitisha uandishi wa makala hizo.Basi nisikupunguzie uhondo bali bonyeza kiunganishi kifuatacho usome habari na makala nyingine motomoto katika jarida makini la Raia Mwema pamoja na makala ya wiki hii yenye kichwa MASLAHI YA UMMA NI ZAIDI YA VYOTE.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.