Showing posts with label SALMA KIKWETE. Show all posts
Showing posts with label SALMA KIKWETE. Show all posts

16 Sept 2010




Zambian First Lady Dragged to Court

Zambian First Lady has been dragged to court for “unconstitutionally” using public resources to campaign for President Rupiah Banda's re-election bid in the 2011 General Election.

According to a statement of claim filed in the Lusaka High Court, the plaintiffs - Evelyn Kangwa and Marjorie Nakaponda - contended that Ms Thandiwe Banda has been using public funds, helicopters and vehicles to tour the country when in fact she was not entitled to the same in the constitution.

They stated that in August 2010 alone, the president's wife visited seven districts in Northern and Luapula provinces using two Zambia Air Force (ZAF) helicopters.

In the said districts, the duo said that Ms Banda visited traditional rulers and women clubs, and gave out money without disclosing the source of the same.

Ms Nakaponda and Ms Kangwa added that during Ms Banda’s visit to Chiengi District, she urged the residents to vote for Mr Banda in the 2011 presidential elections.
Source of money

They added that during the First Lady's visit to Mpulungu and Isoka districts, she was involved in the distribution of the ruling Movement for Multiparty Democracy (MMD) hammer mills and bicycles that were all transported in government vehicles.

The matter will come up before Lusaka High Court judge Phillip Musonda on September 24, 2010.

Zambia’s main opposition leader Michael Sata wrote to President Banda demanding to know the source of the money his wife was “generously giving out” to various women’s clubs countrywide, including Mpulungu constituency, which is due to hold parliamentary by-elections next month.
In addition, a local lobby group, the Anti Voter Apathy Project (AVAP), said Ms Banda had been distributing campaign materials bearing the portrait of President Banda.

Zambia’s ruling party spokesperson Dora Siliya defended Ms Banda, arguing that the First Lady was doing what every other previous First Lady had done in the country.

According Zambian Constitution, a First Lady has no immunity from prosecution. Further, the national budget does not provide funds for her as an individual.

News article sent by Mwl Nkuzi Mhango

15 Sept 2010

Dharau inayoonyeshwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kuendelea kutoa ahadi zaidi ilhali nyingi ya alizotoa mwaka 2005 hazijatimizwa,sasa imehamia kwa mkewe.Katika ukurasa wake wa Twitter (@salmakikwete),mke huyo wa Rais ameandika "“Tuwasikilize,tupembue chuya zikae upande wake,chenga upande wake na mchele ukae upande wake,tuseme lililo lililo la kweli,kama serikali haitatoza kodi,itaendeshaje shughuli zake?” Kauli hiyo pia inapatikana kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Kwanza,pamoja na kumheshimu kama First Lady lakini ilipaswa huyu mama akae kimya.Anatumia raslimali za taifa kumkapeni mumewe wakati anafahamu fika yeye (Salma) si mgombea.Huu ujasiri wa kinafiki wa kutetea kodi sijui unatoka wapi kwa vile tatizo letu kama taifa sio tu kwenye uzembe katika ukusanyaji kodi bali pia matumizi mabaya ya hata hiyo kodi ndogo inayokusanywa baada marafiki wa watawala kupewa misamaha ya kido kifisadi.

Hivi huyu mama anafahamu kuwa mumewe alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alitamka waziwazi kuwa anawafahamu watu wanaofanya ufisadi bandarini hapo?Na miongoni mwa ufisadi mkubwa sehemu hiyo ni dili za kukwepa kodi.

Sasa kama kweli ana uchungu na mapato ya serikali kwanini asimkumbushe mumewe kuhusu majina ya mafisadi wa Bandari ambao hadi dakika hii hajawataja au kuwasilisha majina yao kwa wahusika?

Kama unadhani namsingizi Kikwete hebu soma habari ifuatayoiliyochapishwa na gazeti la Nipashe la Machi 3 mwaka huu

Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA- Kikwete
2009-03-03 10:59:53
Na Joseph Mwendapole
Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na wadau wa bandari Tanzania alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo alilotoa mwezi uliopita kupunguza msongamano wa makontena.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoikosesha mapato.
Akitoa mfano namna wizi huo unavyofanywa, Rais Kikwete alisema wanaweza kuendesha zoezi hilo kwa simu ambapo mtu aliyeko Dubai anapewa maelezo namna atakavyojaza fomu ili mzigo wake usipite kwenye scanner, hali inayoweza kupitisha mizigo haramu kama dawa za kulevya.
Alisema wafanyakazi na wafanyabiashara hao wanatumia udanganyifu kuwa kontena hizo zimebeba mitumba, kumbe ndani ya mitumba hiyo wakati mwingine inatumika kufunika magari.
``Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia kuwa na wafanyakazi wanaokula njama za kuipotezea mapato.
Kikwete alisema bandarini kuna uzembe mkubwa ambao hauvumiliki na aliuagiza uongozi kuondoa matatizo yaliyopo badala ya kukaa na kunung`unika.
Alisema msongamano wa makontena umekuwa ukiisababishia serikali kukosa mapato mengi na alisisitiza kuwa bandari ni sehemu muhimu ambayo serikali haiwezi kuiacha iwe ya hovyo.
Akiwa katika kitengo cha kuchunguza bidhaa katika kontena, Tiscan, Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na TPA yanatofautiana na yale aliyopewa na viongozi wa Tiscan.
``Hapa mbona mimi sielewi naomba mnieleweshe, hawa Tiscan wanasema wana uwezo wa kuchunguza hata makontena 200 kwa siku ila wanasema tatizo ni nyinyi hamleti kontena za kutosha... Jamani fanyeni kazi na muachane na visingizio na malalamiko,`` alisema Kikwete.
Aliagiza mamlaka hiyo impe taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa upunguzaji wa makontena ndani ya wiki mbili zijazo na aliahidi kutembelea tena bandari hiyo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Forodha, Otieno Igogo, alimweleza Rais Kikwete kuwa wadau wa Bandari ya Dar es Salaam walikubaliana kulipa dola 30 ikiwa ni gharama za kuhamishia kontena moja katika bandari kavu.
Igogo alimweleza Rais kuwa ingawa wadau wote wamekuwa wakichangia, Kampuni ya Kimataifa ya Kupakua Kontena Bandarini (TICTS), imegoma kutoa fedha hizo.
Alisema dola 30 ambazo TICTS walipaswa kulipa kwa kila kontena linalohamishiwa bandari kavu kama wanavyolipa wadau wengine, zimekuwa zikitolewa na TPA.
Baada ya kauli hiyo ya Igogo, Rais alisema anashangaa kuona jeuri hiyo ya TICTS na kusema kuwa TPA ina mamlaka, lakini haitaki kuyatumia.
Kikwete alisema TPA imefanya vizuri kulipa gharama ambazo TICTS imekataa kuzilipa, lakini aliagiza mamlaka hiyo ihakikishe TICTS inazirudisha mara moja.
``Nyinyi mnashangaza sana, mna mamlaka, lakini hamyatumii... Sasa hizi gharama lazima walipe na wakiwashinda mwelezeni waziri na waziri akishindwa niambieni mimi,`` alisema.
Wakati huo huo, Kikwete alikataa maelezo marefu ambayo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, alitaka kuyasoma mbele yake na badala yake akamtaka amweleze sababu za msongamano kutoma lizika.
Baada ya kuelezwa hivyo, Mgawe alimweleza Rais Kikwete kuwa kikosi kazi kilichoundwa kufuatia agizo lake kinaendelea kujitahidi kuondoa msongamano uliopo.
Alisema Mamlaka inatarajia kuwa utekelezaji wa mikakati iliyowekwa itafanikisha kupunguza hali ya msongamano mwezi Machi mwaka huu.
Mgawe alisema katika kipindi cha mwaka 2007/08, TPA ilihudumia tani milioni 6.239, ambalo ni ongezeko la tani 227,222 au asilimia 3.8 ikilinganishwa na tani milioni 6.003 zilizohudumiwa mwaka 2006/07.
Alisema katika kipindi hicho mamlaka ilipata ziada ya Sh. bilioni 37.879 kutokana na mapato ya Sh. bilioni 168.789 na matumizi ya Sh. bilioni 133.909.
SOURCE: NIPASHE

Wito wangu kwa Salma Kikwete ni simple: kama alikuwa anataka kugombea uongozi angegombea lakini sio kuendelea kutumia raslimali za taifa kumkampenia mumewe.Anapaswa kutambua kuwa raslimali hizo zinagharamiwa na walipa kodi ambapo wengi wao si wana-CCM (takwimu za karibuni zinaonyesha wanachama wa CCM ni takriban milioni 5 tu kati ya Watanzania takriban milioni 45).

Tunatambua kuwa Salma anataka kuendelea kuwa First Lady lakini asifanye hivyo kwa kuwabebesha gharama Watanzania wote hata wasio wana-CCM.Anaweza kuitumia WAMA kumfanyia kampeni mumewe lakini Watanzania hawataki kuona ufisadi wa mchana mweupe unaofanywa kwa misingi ya kifamilia.

Naamini mwanamama huyu anafuatilia habari za kimataifa,na hivyo amesikia yaliyomkumba Vera Chiluba,mke wa aliyekuwa Rais wa zamani wa Zambia,Frederick Chiluba,aliyehukumiwa kwenda jela kwa ufisadi.

Ni vema Salma akasoma alama za nyakati ili pindi mumewe atakapokabidhi madaraka kwa Dokta Wilbroad Slaa hapo Novemba familia ya Kikwete isianze "kutafutana".

Na hiyo "tweet" yake ya kuchambua pumba na mchele nadhani ni vema akiielekeza kwa mumewe ambaye so far anaonekana kunogewa na "ugonjwa" wa kutoa ahadi.Mara uwanja wa ndege Kigoma,mara kuboresha kilimo cha kakao,mara atawapatia akinamama chanjo ya cervical cancer,mara vijiji 11 vya Mkinga vitapatiwa maji,mara hili mara lile alimradi ni "vurugu mechi ya ahadi".Kwani Rais wa Tanzania 2005-hadi sasa alikuwa nani kama sio Jakaya Mrisho Kikwete?Kwanini hayo anayoahidi sasa hakuyatekeleza katika awamu yake ya sasa?Na kwani tuamini kuwa atayatekeleza katika awamu yake ya mwisho-kipindi atakachokuwa bize kujitengenezea mazingira ya "kumpumzika kwa amani" kama Mkapa?

Blogu hii inawakumbusha tena wapiga kura kwamba Kikwete hayuko serious ndio maana ameamua kurejea nyingi ya ahadi zake za 2005 bila aibu wala kuwaomba msamaha Watanzania kwa kutozitekeleza.Kumrejesha tena Ikulu itakuwa ni kosa kubwa kupita kiasi kwani katika awamu yake ya mwisho atairejesha nchi yetu kwenye zama za mawe.

TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA
TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA
TANZANIA BILA KIKWETE,SIO TU INAWEZEKANA,BALI NI MUHIMU LAZIMA KWA USTAWI WA TAIFA LETU.
CHAGUA DOKTA SLAA KWA UKOMBOZI NA "UHURU WA PILI",CHAGUA CHADEMA KWA TANZANIA YENYE NEEMA.


4 Jan 2010


Je mama Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe?

na Nkwazi Mhango

Siku hizi mke wa rais, Salma Kikwete, anaonekana kwenye kurasa za mbele za magazeti karibu kila siku akiwa mikoani akihamasisha hili na lile. Wengi wanahoji. Kwanini sasa na si tangu mwanzo mume wake alipoingia ikulu? Na kwanini asiseme wazi kuwa anampigia kampeni mumewe? Maana, inajulikana alivyo mwana CCM damu damu tena mjumbe wa vikao vyake?

Watetezi wake wanaweza kusema anafanya kazi ya shirika lake lisilo la kiserikali la WAMA. Haiwezekani mumewe akawa mkuu wa serikali naye akawa na shirika lisilo la kiserikali kusiwe na mgongano wa kimaslahi kisheria. Uzoefu tulioupata toka kwa Anna Mkapa ungetosha kumsaidia rais Jakaya Kikwete kuondokana na aina hii ya ufisadi sugu na unyemelezi kwa kutumia mgongo wa ikulu kama angekuwa ni mtu wa kujifunza na kudhamiria kutenda haki kwa taifa.

Ngo yake ni ya mashaka-kwanini ianzishwe baada ya mumewe kuwa rais? Kuanzisha NGO baada ya mume kuwa rais ni ishara tosha ya ufisadi na usasi wa ngawira. Mbona hatuoni wake wa viongozi wa vyama vingine wakiwa na NGOs? Hata wakiwa nazo nani atazichangia iwapo wanaochangia NGOs za wake wa marais wanatafuta kuwa karibu na ikulu ili waihujumu nchi kwa kupata upendeleo kama ilivyokuwa kwa EOTF ambayo ilitumiwa na watu wengi kuliibia taifa? Mke wa Kaisari hapaswi kutenda tendo lenye kuweza kutia shaka au doa utawala wa mumewe.

Tuliishi na kumuona baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Mkewe-mama Maria-hakuwahi kujihusisha na upuuzi mdogo mdogo wa kutafuta pesa kwa mgongo wa mumewe.

Niliwahi kuwaandikia barua EOTF na WAMA kuwaonya juu ya hatari ya kuitumia ikulu. Hawakuwahi kunijibu zaidi ya kufumba macho na kuendelea kutengeneza pesa kwa mgogo wa ikulu. Ila nafurahi. WAMA wamefanya jambo moja (la maana la kuondoa aibu)-kuondoa maneno yasemayo WAMA Foundation the office of the First Lady of the United Republic of Tanzania kwenye wavuti wao. Niliandika baruapepe ifuatayo kwa WAMA tarehe 3 Septemba 09:

Kama mzalendo, nimejaribu kukusanya baadhi ya maoni kuhusiana jinsi ufisadi unavyoingia ikulu kiasi cha kututatiza. Kwa sasa Anna Mkapa mke wa rais wa zamani na mumwe wako msambweni. Ukiangalia kinachofanywa na WAMA hakina tofauti na Fursa sawa kwa Wote (Wake za wakubwa).
Kuondoa aibu, nimejitolea kuwasiliana nanyi ili angalau mjue tunavyojihisi kwenye wimbi hili la ufisadi wa kutumia madaraka ya waume zenu. Mama Salma NGO yako ni ulaji mtupu kusema ukweli. Acha kuna kesho. Ni uamuzi wako kuamua. Kuna kesho wakati madaraka yatakuwa mikononi mwa wengine. Hasa nikizingatia kilichompata Regina Chiluba ambacho kinapaswa kumpata hata Anna Mkapa, nimeona bora niseme hata kama nitapuuziwa. Ila najua ujumbe utafika. Someni alama za nyakati na mjue kuwa madaraka yana mwisho na yanalevya. Kuna siku mtakumbuka mchango huu.
Kila la heri,

Bahati mbaya sana , hata wavuti wa Kurungenzi ya habari Ikulu unaonekana kutangaza biashara ya WAMA badala ya wizara za serikali! Ajabu hakuna anayestuka wala kupiga kelele!

Kama umma ukishupaa NGO hii inaweza kufutwa hata na mahakama kutokana na mgongano wa maslahi ukiachia mbali kuwa kichaka cha ufisadi kutokana na uwezekano wa kuchangiwa pesa chafu kutokana na kutokuwapo sheria makini ya kuchuja na kutangaza wafadhili wa WAMA.

Hata hivyo nimefarijika kuwa sauti yangu imesikika na fedheha imeondoka. Maana neno Jamhuri ya Muungano, kisheria, halipaswi kutumiwa na mtu au taasisi yoyote isipokuwa mihimili mitatu ya dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala. Cheo cha Ofisi ya First lady hakimo katika katiba yetu.

Kwanini mapenzi kwa wanawake na watoto yaanze baada ya kuupata urais kama siyo gea ya kuitumia vibaya ikulu? Ina maana rais na washauri wake hawalioni hili au wameridhia kwa sababu NGO ya mke wa rais inaweza kutumika kama kivuli cha kuanza kampeni hata kabla ya tume kutanganza hivyo? Inabidi tustuke. Ajabu hata wapinzani hawajaliona hili!

Tanzania inaweza kuwa nchi pekee ambapo rais na mkewe wote ni marais. Kikwete ni rais wa jamhuri huku mkewe akiwa rais wa WAMA. Ukitaka kujua hili jikumbushe mapokezi anayopewa na coverage anayopata Salma kwenye vyombo vya habari. Ajabu ukitafuta uhalali wake kikatiba haupo!

Hata kama anajulikana kwa ubabe na upayukaji wake, bado mke wa rais wa Kenya Lucy Kibaki hana mamlaka kama aliyo nayo Salma ambaye anaweza kuingia mkoa wowote kwa kisingizio cha NGO yake na kufanya shughuli za kisiasa kama kulakiwa na viongozi wa mikoa na kukagua miradi ya maendeleo ukiachia mbali kutoa kauli mbiu zinazoonyesha wazi kumpigia debe mumewe.

Salma anchomzidi Lucy ni ile hali ya kufanya kitu waitacho waingereza one woman show. Kwani kila lilipo jina WAMA yupo yeye. Hii maana yake ni kwamba yeye ni dikteta na mpenda madaraka anayetaka kufanya kila kitu peke yake. Kwanini hatuoni makamu wake au hata wasaidizi wengine wakifanya shughuli za WAMA kama kweli ni ya umma kama anavyodai? Kuthitibitisha hili, tembelea tovuti ya WAMA uone ukweli huu. Hii haiwezi ikawa taasisi ya wanawake na watoto wa Tanzania .

Kuonyesha kuna namna ya kampeni na kutumia mamlaka ya mume wake, hivi karibuni, Mama Kikwete amewahi kutoa namba yake ya simu ya mkononi ambayo ni 0754-294450 kwa wanawake mkoani Singida ili waweze kumpigia au kumtumia ujumbe mfupi wa maneno pindi waume zao watakapowanyanyasa kutokana na kitendo cha wao kwenda kupima kwaajili ya kujua afya zao. Japo kwa juu hili linaweza kuonekana ni jambo bora, kwa mtu anayejua mipaka ya mamlaka yake na utaratibu wa utawala kisheria, angeshauri wahusika waelekeze madai yao kunakohusika-polisi, vituo vya kutetea haki za binadamu hata wizarani.
Licha ya kuwa ubabe, hii ni kampeni ya wazi kuonyesha wahusika wanawajali wananchi jambo ambalo si kweli. Kwanini hasira zake zisielekezwe kwenye kumshauri mumewe kupambana na ufisadi kama ana uchungu na nchi hii? Yaani hajui kuwa ujinga na umaskini ndivyo vyanzo vya haya yote? Sijui hata kwenye kupokea misaada anauliza usafi wa mtoaji.

Kwa nijuavyo upenzi wa sifa wa watawala wetu na watu wao, kama utafanyika uchunguzi huru juu ya matumizi ya MAWA, ushingae pesa inayotumiwa kwenye ziara ikawa kubwa kuliko hiyo inayowafikia walengwa. Bahati mbaya sijwahi kusoma popote taarifa ya mahesabu ya mwaka ya si WAMA wala EOTF.

Wengi wanaweza kuona kama tunamuandama mke wa rais au kutotambua umuhimu wa kupigania haki za akina mama. Kwanini mke wa rais wakati tuna wizara yenye watendaji wanaolipwa pesa ya kodi yetu? Kwanini misaada hiyo anayopokea isipelekwe wizarani au kwenye mashirika huru kama kweli ana uchungu na walengwa na si kujipatia umaarufu, pesa na kubwa zaidi kutumia ikulu kwa manufaa binafsi yawe yake au mumewe na marafiki zake?

Je Salma Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe hata kabla ya kipenga kupulizwa? Je akina mama wa Tanzania wataingia mkenge wake huku waume na kaka zao wakizidi kuteswa na sera za Kikwete za kuvumilia mafisadi? Je atawalainisha wasahau kuwa Kikwete hajatimiza ahadi hata moja? Je watahoji uhalali wa NGO yake na kumwambia ukweli kuwa ni ya mashaka na ulaji?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.