10 Nov 2008


MVUTANO mkali uliibuka jana katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa NEC- CCM kuhusu mwenendo wa baadhi ya wabunge wa chama katika mambo mbalimbali yaliyolihusu taifa na chama hicho. Tanzania Daima Jumapili imedokezwa.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho vililieleza gazeti hili kuwa mvutano huo uliibuka baada ya baadhi ya wajumbe wa kikao hicho ambao si wabunge kuwashangaa wenzao ambao wamekuwa wakiibua hoja zenye mwelekeo wa kuishambulia serikali na wale wanaoendeleza hoja zenye mwelekeo wa kuchochea udini.

Habari hizo zilieleza kuwa wajumbe wa kikao ambao si wabunge walionyesha dhahiri kuchukizwa na hatua ya baadhi ya wajumbe ambao ni wabunge ya kuanza kuwachimba viongozi wa kitaifa wa chama hicho kwamba inahatarisha umoja wa chama hicho.

Sambamba na taarifa za kuwepo mjadala mkali kuhusu hoja hizo, taarifa nyingine zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa wakakti Bunge likisubiri hatua zitakazochukuliwa na serikali dhidi ya gazeti lake la Habari Leo, baada ya kufichua njama za kundi dogo la wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kusuka zengwe la kumpinga hadharani Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, kuhusu hatua alizozichukua dhidi ya wezi wa EPA, chama hicho kimeanzisha uchunguzi wa kuwabaini wabunge waliodaiwa kuhusika katika mpango huo.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya chama hicho, vimedokeza zaidi kuwa hatua hiyo ina nia ya kutaka kuthibitisha kilichoandikwa na gazeti hilo la serikali kama ni kweli au ni uongo na uchochezi, kama ilivyodaiwa juzi bungeni na Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka.

Sendeka, mmoja wa wabunge machachari ndani ya CCM, juzi akitumia kanuni ya Bunge namba 68, alieleza masikitiko yake kuhusu habari iliyoandikwa katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la Habari Leo kuwa ilikuwa ya uchochezi na kuitaka serikali ichukue hatua kama ilizochukua kwa gazeti la MwanaHalisi, ambalo limefungiwa miezi mitatu, kwa madai ya kuchapisha habari ya uchochezi kuhusu kuwepo mpango wa kumng’oa madarakani Rais Kikwete, ifikapo mwaka 2010.

Habari iliyochapishwa na Habari Leo ilieleza kuwa kuna kundi la wabunge ambalo kwa makusudi lilikusudia kuwasilisha hoja hiyo bungeni, lakini mkakati huo ulizimwa na habari iliyochapishwa na gazeti hilo kabla ya kundi hilo kuwasilisha linachokiamini kuwa Rais Kikwete hajachukua hatua stahiki katika kulishughulikia suala la wezi wa EPA.

“CCM imeshitushwa na hoja hiyo kuletwa bungeni, kuomba serikali ichukue hatua dhidi ya gazeti la Habari Leo wakati taarifa hiyo inaelezwa na walioitoa kuwa ni kweli tupu. Sasa chama kimeamua kufanya uchuguzi ili kije na majina ya wabunge waliokuwa na mpango huo na mahala walipoendeshea vikao hivyo ili kuuthibitishia ulimwengu kwamba habari hiyo ni sahihi na kwamba kuna wabunge waliopanga kumdhalilisha rais,” kilisema chanzo chetu hicho cha habari.

Juzi Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali ya Daily News na Habari Leo, Isaac Mruma, alikaririwa akieleza kuwa habari iliyoandikwa na gazeti analolisimamia ni sahihi na ya kweli.

“Kwanza napenda kusema kuwa tuna uhakika na tulichokiandika kuwa ni kweli, kwani chanzo chetu cha habari ni cha kuaminika,” alisema Mruma.

Alipoulizwa ni kwanini walichapisha habari hiyo upande mmoja bila kupata maelezo ya upande wa pili, yaani bungeni au kwa wabunge waliotuhumiwa, Mruma alisema taarifa hiyo waliipata usiku, hivyo walishindwa kuwatafuta wahusika, licha ya kwamba waliwajua kupitia chanzo chao cha habari.

Alisema kutokana na hali hiyo, waliamua kuyaondoa majina ya wabunge wote waliokuwa wakitajwa kuhusika katika mpango huo wa kumpinga Rais Kikwete, kuhusu namna alivyoeleza jinsi suala la EPA litakavyoshughulikiwa, wakati akilihutubia taifa hivi karibuni.

Mruma aliwataka wabunge kutambua kwamba gazeti la Habari Leo ni chombo cha serikali na lina dhamana ya kuchukua tahadhari kwa kuandika jambo lolote linaloonekana kwa namna moja ama nyingine kujaribu kuiyumbisha serikali au rais aliye madarakani.

Habari zaidi kutoka mjini hapa ambapo kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kinaendelea, zilieleza kuwa huenda suala la habari hiyo likaibua mjadala mzito katika kikao cha NEC kinachoendelea leo mjini hapa.

Akiwasilisha maelezo yake juzi bungeni, Sendeka alisema habari hiyo iliyokuwa na kichwa kisemacho ‘Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA, ilikuwa na lengo la kuleta mtafaruku na uchochezi kati ya wabunge wa CCM na serikali.

Hoja ya Sendeka iliungwa mkono na Spika Samuel Sitta, ambaye alieleza kushangazwa kwake na habari hiyo kutoa maelekezo kwa serikali kufuatilia suala hilo na kupelekewa taarifa.

Kwa upande wake serikali, ilisema tayari ilishaanza kulishughulikia suala hilo kwa kuwahoji wahusika.

CHANZO: Tanzania Daima

9 Nov 2008


UTATA umegubika mchakato wa zabuni nyeti ya matengenezo ya mfumo wa usalama ndani ya Benki Kuu Tanzania (BoT), ambayo imetolewa kwa Kampuni ya Siemens ya Afrika Kusini.

Kuibuka kwa utata huo kumekuja wakati Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu akiwa katika mipango ya kuisafisha benki hiyo na tuhuma mbalimbali, ikiwemo ya ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Nyaraka ambazo gazeti hili inazo, zinaonyesha utata huo umeibuka kutokana na malalamiko kutoka kwa Kampuni ya ESS ya Afrika Kusini, ambayo haijaridhishwa na taratibu za mchakato zilivyofanyika.

Kwa mujibu wa nyaraka hizo, ESS inaonekana kulalamikia hatua ambayo imeita kuwa ni kuwepo mawasiliano kabla, kati ya watendaji wa Siemens na baadhi ya watu ndani ya Bodi ya Zabuni ya BoT.

Mawasiliano hayo yalinaswa katika barua pepe kati ya mwakilishi wa Simens nchini Julai 29,2008, akifahamisha viongozi wake kufanya mawasiliano na mtu mmoja muhimu ndani ya BoT.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka, " Nimeweza kuzungumza na mtu mmoja wa kuaminika ndani ya BoT, na amesema zipo zabuni mbili tofauti, ila sisi tutapatiwa moja tu ya utengenezaji mfumo wa usalama."

Barua hiyo, iliandikwa Julai wakati mshindi wa zabuni alipatikana Oktoba 28, ambapo ESS kama mmoja wa washiriki, alifahamishwa.

Utata mwingine katika zabuni hiyo unatokana na kile kinachoelezwa kwamba, Siemens ilishiriki katika uwekaji mfumo huo katika ujenzi wa jengo la ghorofa 18 maarufu kama Twin Towers na lile la Gulioni Zanzibar, ambayo yanachunguzwa.

"Sasa ikitokea ukaguzi wa Twin Towers umeonyesha kulitumika mabilioni bila kuangalia Value for money (thamani ya pesa kwa kitu), itakuaje?" kilihoji chanzo kimoja.

Siemens katika mkataba huo wa miaka miwili iliomba zabuni kwa sh 3.4 bilioni, hata hivyo, makampuni mengine kwa mujibu wa nyaraka za BoT yako juu zaidi.

Hata hivyo, akizungumzia utata huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Gavana Ndulu, alisema hadi sasa ana imani kwamba, mchakato wa zabuni hiyo ulifuata taratibu husika.

Kwa mujibu wa Profesa Ndulu iwapo atabaini kuna tatizo lolote ikiwemo ukiukwaji wa mkataba huo hatasita kuisitisha.

Profesa Ndulu alisema dai la kwamba Siemens ilijenga Twin Towers ni kweli, lakini akabainisha kuwa hata kampuni nyingine ambayo ni pamoja na ESS na Group 5, pia zilishiriki katika ujenzi huo na pia ziliomba zabuni hiyo.

Profesa Ndulu alisema kabla ya kushirikisha kampuni hizo tatu ambazo zote zilishiriki katika uwekaji wa mfumo wa usalama kwa ngazi tofauti, ilibidi bodi itafute mwongozo kutoka Mamlaka ya Zabuni (PPRA), ambayo ilithibitisha hakuna tatizo.

Mwananchi Jumapili ilifanikiwa kuona nakala ya baraka za PPRA kwa BoT, ikieleza kuwa hakuna matatizo kwa makampuni hayo kushiriki ili mradi vigezo vizingatiwe.

"Najibu moja baada ya jingine, unanijua sifichi kitu na sipendi kupindisha mambo, kuhusu Siemens kushiriki katika Twin Towers, ni kweli, lakini hata ESS na Group 5 walishiriki kwa ngazi tofauti, Group 5 ndiyo wanaojenga jengo hilo, lakini pia wameshiriki," alisema Profesa Ndulu na kuongeza;

"Kama ni kigezo hicho, tusingeruhusu hata ESS na Group 5, kampuni hizi mbili na Siemens zote zimeshiriki katika Twin Towers, ndiyo maana kabla ya zabuni tukaenda PPRA kupata ufafanuzi, wakaruhusu," alisema.

Akifafanua kuwepo mawasiliano kati ya watu ndani ya bodi na Siemens, alisema hadi sasa hajaona tatizo kwani ni kweli zabuni zilikuwa mbili, lakini BoT ikaamua yenyewe kuchukua kazi moja ya kushughulikia uendeshaji wa mambo mbalimbali na kuacha hilo la ukaratabati mfumo wa usalama.

"Ni kweli, zabuni zilikuwa mbili, tulipoona wenyewe tunayo idara ya kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo usafi na ununuzi wa vifaa, tukaamua tuipunguzie gharama kwa benki kwa kuipa zabuni kampuni moja, lakini pia si kwamba tunamwachia peke yake, wapo vijana wetu mahiri wanashirikiana nao," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema hajaona tatizo katika hatua hiyo kwani zabuni ilitangazwa Juni na mawasiliano yamefanyika Julai, huo ni utaratibu wa kawaida kwa sababu kuna vitu ambavyo kampuni zote zinapaswa kuelezwa baada ya zabuni kufunguliwa.

"Sasa kusema kwamba zabuni ambayo itatolewa kwa ajili ya kugombaniwa ni ya usalama si uendeshaji, si tatizo ndicho tulichoeleza kwa kampuni zote," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema ingawa haingii wala kuruhusiwa kuingilia mambo ya zabuni, lakini amekuwa akiuliza na kupatiwa taarifa za mara kwa mara kwa lengo la kuangalia utaratibu wa kutekelezwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

"Mimi sitaki watu wapindishe mambo hata kidogo, nitasimamia sheria na kanuni, ndiyo maana huwa wakati mwingine nataka ufafanuzi wa mambo mbalimbali," alisisitiza Gavana Ndulu.

BoT katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000 imekuwa na matatizo mbalimbali, ambayo hata hivyo, chini ya uongozi wa Profesa Ndulu amekuwa akijaribu kuisafisha na tuhuma hizo.

Baadhi ya mambo aliyoahidi kuyashughulikia ni kuchunguza mchakato wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo jijini Dar es Salaam na lililoko Zanzibar, kupitia ajira za watumishi wa BoT ambaye ametekeleza kwa kiasi kikubwa.

CHANZO: Mwananchi

8 Nov 2008


US President-elect Barack Obama would never have become the British Prime Minister because of "institutional racism" in the Labour Party, the head of Britain's equality watchdog has claimed. Skip related content

Trevor Phillips (pictured above), chairman of the Equality and Human Rights Commission, told The Times: "If Barack Obama had lived here I would be very surprised if even somebody as brilliant as him would have been able to break through the institutional stranglehold that there is on power within the Labour Party."

He said the Conservative Party had made more progress when it came to its selection procedures than Labour.

He said: "The parties and unions and think-tanks are all very happy to sign up to the general idea of advancing the cause of minorities but in practice they would like somebody else to do the business. It's institutional racism."

He added that he opposed all-black shortlists but said "positive action" was needed by all parties.

His views were supported by Adam Afriyie, Conservative MP for Windsor, who said he did not believe he would see a black PM in his lifetime.

But Sadiq Khan, Labour MP for Tooting, disagreed and predicted a black or Asian Labour PM would be elected in his lifetime.

A Labour Party statement in response to Mr Phillips said it continually reviewed its procedures to ensure its elected positions reflected British society.

A spokesman for the party said it has a "proud record of promoting ethnic minority candidates".

SOURCE: Yahoo! News


SERIKALI kwa mara nyingine imeingilia kati na kuamua kulipa mishahara ya wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), baada ya mwekezaji wake kushindwa kulipa mishahara ya mwezi uliopita.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alitangaza uamuzi huo bungeni jana, alipokuwa akijibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mamuya (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kuhakikisha mwekezaji huyo anaiendesha kampuni hiyo kwa ufanisi na kama alikuwa akijua kuwa hadi jana wafanyakazi wa kampuni hiyo walikuwa hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita.

“Serikali imelichukua tena tatizo hilo na tunalifanyia kazi. Ninaahidi kuanzia sasa wafanyakazi hawa hawatakosa tena mishahara, tutajaribu kuona kama hiyo nyongeza tutaweza kuilipa,” alisema Pinda.

Agosti, mwaka huu, tatizo la wafanyakazi kukosa mishahara lilipotokea kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuokoa jahazi na hadi jana na juzi alikuwa akihaha kuhakikisha wafanyakazi hao wanalipwa mishahara yao ya Oktoba.

“Hadi juzi nilikuwa nahangaikia suala hili, ahadi ya serikali ilimalizika Agosti na tulitarajia uongozi wa TRL ungeendelea kulipa viwango vipya vya mishahara kuanzia Oktoba kama tulivyokubaliana, lakini kwa bahati mbaya wameshindwa na tunalazimika tena kulipia mishahara ya wafanyakazi hao hadi Novemba,” alisema Pinda.

Hii ni mara ya tatu kwa serikali kulazimika kuiokoa kampuni hiyo, baada ya uongozi wake kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Miezi mitano tangu mwekezaji alipolichukua shirika hilo wakati huo likiitwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), serikali iliingia mfukoni na kutoa fedha za walipa kodi zaidi ya sh bilioni tatu kuikopesha TRL kwa ajili ya kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Septemba, mwaka huu, TRL ilikwama tena kulipia viwango vipya vya mishahara na serikali iliamua kulipa mishahara ya mwezi huo kwa ahadi kwamba kuanzia Oktoba mwekezaji angeweza kuendelea kulipa wafanyakazi wake bila matatizo.

Kampuni hiyo imeshindwa tena kulipa mishahara ya mwezi uliopita. Serikali kwa mara ya tatu sasa inajikuta ikilazimika kuingia tena mfukoni kuokoa jahazi.

Juzi wafanyakazi wa TRL walitangaza kuanza mgomo baridi, huku wakisubiri hatua zinazochukuliwa na mwekezaji kuikoa kampuni hiyo. Mbali na sula la TRL, Waziri Pinda pia alizungumzia suala la kuvuja kwa mitihani aliposema serikali inaliangalia kwa umakini Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwani ndipo penye tatizo.

Serikali inajitahidi kuangalia namna bora ya kulisimamia kwani ni aibu kwa taifa kukaa na kuulizana maswali juu ya uvujaji wa mitihani. Amewataka wazazi na wanafunzi wanaotafuta mitihani kuacha kuendekeza tabia hiyo ya aibu.

“Natoa rai kwa wazazi kuwa tusikubali na tuwe wa kwanza kutoa taarifa tunapoona watoto wana mitihani ya kununua,” alisema Pinda.

Jibu hilo la Waziri Pinda lilitokana na swali la Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya (CUF), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kukabiliana na tatizo la kuvuja kwa mitihani na uchapishaji wa vyeti feki vinavyosambazwa mashuleni na kusababisha kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.

Akizungumzia hali ya kiuendeshaji ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Pinda alikiri kwamba kwa sasa kampuni hiyo iko taabani, hali iliyosababisha serikali ilazimike kufanya mazungumzo na shirika moja nchini China, lengo likiwa ni kuinusuru ATCL katika hali hiyo mbaya.

Akijibu swali la Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro, aliyeitaka serikali ichukue jukumu la kununua vitabu vya kiada kwa shule za msingi na sekondari na kuvisambaza badala ya jukumu la sasa la kutumia wakandarasi, Waziri Pinda alisema utaratibu wa sasa ni kwamba serikali inatoa fedha kwa halmashauri, nazo zinatumia wakandarasi ambao wengine si waaminifu.

“Wakandarasi mara nyingine hununua vitabu vya mitaani vinavyokuwa katika kiwango cha chini, hivyo tumekubaliana na wizara tutafute utaratibu mzuri wa upatikanaji wa vitabu,” alisema.


CHANZO: Tanzania Daima

KUMWOKOA MWEKEZAJI KILA ANAPOKWAMA SIO UFUMBUZI,BALI UAHIRISHAJI WA UFUMBUZI,WA TATIZO.NI MUHIMU KUJIULIZA HUYU MWEKEZAJI ATAENDELEA KUOKOLEWA HADI LINI,AND WHAT'D HAPPEN IF HATOOKOLEWA!







These pics are so lovely that no wonder we keep on hearing bull***t LIKE THIS.

Na Daniel Mjema, Dodoma
SERIKALI imekiri kuwa gazeti lake la Habari Leo liliandika habari ya uchochezi na kuliahidi Bunge kuwa italichukulia hatua zinazostahili gazeti hilo.

Hatua hiyo ya serikali inafuatia agizo la Bunge kwamba ilichukulie hatua kali gazeti hilo kwa kuchapisha habari za uchochezi dhidi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), serikali na Rais Jakaya Kikwete.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo baada Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, kulalamika kuhusina na kitendo cha gazeti hilo la serikali kuchapisha habari hiyo.

Awali mbunge huyo aliomba mwongozo wa Spika jana kuhusiana na habari hiyo akisema kuwa ni nzito na ya uchochezi kuliko iliyoandikwa na gazeti la MwanaHALISI lililofungiwa miezi mitatu hivi karibuni na waziri huyo.

Habari hiyo iliyochapwa Jumatano wiki hii katika toleo namba 636 ilikuwa na kichwa cha habari likichosema ‘Kundi la wabunge wa CCM lasuka zengwe la EPA” na kuelezea njama za wabunge hao wa CCM kumpinga Rais kuhusu hatua zake dhiti ya watuhumiwa wa EPA.

Ole Sendeka alisema habari hiyo ni ya uchochezi mkubwa, hasa inapodai kuwa zipo njama za wabunge wa CCM za kumpinga Rais Jakaya Kikwete kuhusu uamuzi wake katika sakata la kashfa ya fedha za EPA.

Mbunge huyo alisema gazeti hilo limejenga hoja kuonyesha kwamba wabunge hao wa CCM wamekuwa wakitumiwa na watu waliopo nje ya Bunge kupinga maamuzi ya Rais baada ya kuagiza kuwa watuhumiwa wafikishwe kortini.

Ole Sendeka alisema habari hiyo ni nzito na ya uchochezi kuliko ile ya gazeti la MwanaHALISI, kwa sababu inawagombanisha wabunge hao na Serikali pamoja na Rais na kutaka mwongozo wa Spika ni hatua gani zitachukuliwa.

Baada ya maelezo hayo, Spika Samwel Sitta aliungana na Mbunge huyo na kusema kuwa hata yeye alishtuka sana aliposoma habari hizo na kuongeza kuwa huo ni mchezo mchafu ambao serikali inapaswa kuuchukulia hatua kali.

“Hata mimi nilishtuka sana niliposoma habari hiyo, kwa kweli ni mchezo mchafu sana, ingekuwa imeandikwa na gazeti hovyo hovyo hivi tusingeshangaa sana, lakini hili ni gazeti la Serikali,” alisema Sitta.

Sitta ambaye alionekana kukerwa na habari hiyo aliongeza kusema kuwa: “Linapokuwa limechapisha gazeti la Serikali, hili ni jambo zito sana, hivyo naagiza wahusika waliotajwa na gazeti hilo waandike malalamiko rasmi kwa waziri husika”.

Spika alisema pamoja na wahusika ambao ni wabunge wa CCM, kuwasilisha malalamiko hayo na kupeleka kwa waziri nakala za gazeti hilo, Bunge litafuatilia kujua hatua zilizochukuliwa dhidi ya chimbo hicho cha habari cha serikali.

Mara baada ya maelezo hayo , Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika, ambaye ndiye aliyelifungia gazeti la MwanaHALSI alisimama na kukiri kuwa gazeti hilo la serikali kuandika habari hizo za uchochezi.

Hata hivyo, alisema kuwa wizara yake imekwishachukua hatua kwa kuwaandikia wahusika kuwataka wajieleze kuhusu ukweli wa habari hiyo na baada ya kupokea maelezo hayo serikali itachukua hatua zinazostahili.

Pamoja na maelezo hayo, Spika alimweleza waziri huyo kuwa ni vyema taarifa ya jinsi serikali ilivyolishughulikia suala hilo iwasilishwe katika ofisi ya Spika ili naye aishirikishe Kamati ya Bunge ya Maadili.

Mwezi mmoja uliopita serikali ililiufnugia kwa miezi mitatu gazeti la MwanaHALISI kwa maelezo kwamba limeandika habari ya uchochezi iliyokuwa na kichwa kisemacho: ‘Njama za kungoa Kitwete zafichuka’, ambayo ilieleza kwamba ndani ya CCM kuna watu wanataka kumzuia Rais Kikwete asigombee urais tena kipindi cha pili.

Waziri husika alisema serikali imechukua hatua kwa sababu gazeti hili imeandika habari yenye lengo la kumchonganisha Rais na mtoto wake aliyedaiwa kutumiwa na kundi la baadhi ya vigogo wa CCM wanaotaka kumwengua ili asigombee kipindi cha pili.

Hatua ya waziri huyo kulifungia gazeti hilo kilipingwa na wadau mbali mbali wa habari na kufuatiwa na maandamano ya amani ya wahiri wa vyombo vya habari nchini hadi katika ofizi za wizara hiyo wakiwa wameziba midomo na gundi ya karatasi au plasta.

CHANZO: Mwananchi


7 Nov 2008


Barack Obama's motorcade had an unexpected occurrence while ferrying the president-elect to a security briefing at Chicago FBI headquarters Thursday morning.

As the motorcade pulled onto Van Buren, towards the Loop, a couple in a tan sedan tried to drive around the heavily-armed line of vehicles, wrote pool reporter P.J. Hufstutter of the Los Angeles Times:

The SUV cut the car off immediately, and the security team aimed their weapons at the car. The driver and passenger in the sedan stopped, and looked stunned -- until the male driver appeared to understand what was happening (your pool reporter could see him mouth "Obama"). The motorcade continued on. The sedan remained stopped, near the side of the road. [...] Some of the drivers here in Chicago do not seem to understand that a) the Chicago police car at the end of the president-elect's motorcade is serious about having traffic pull over when the officers flash their lights and hit their sirens, and b) it's not a great idea to jump ahead of traffic by trying to cut around the black SUV filled with five heavily-armed secret service CAT members.



THROWN out by the Ugandan government on grounds of corruption, a South African firm has landed a multi-billion-shilling deal in Tanzania to produce Smartcard driving licences. 

The Tanzania Revenue Authority (TRA) has embraced Face Technologies of South Africa to undertake the project, despite the fact that quotations of the firm have raised eyebrows among local information technology experts. 

According to informed sources, the company is charging $21.53 (approximately 25,200/-) per Smartcard driving licence but local experts claim that the amount is more than double the real cost. 

Reports from Uganda said the firm, established six years ago, was ordered to pack its bags from Kampala because it had inflated the cost for a similar project in the country. 

Media reports quoting Uganda’s internal affairs ministry said that Face Technologies quoted $97m while the ministry’s own evaluation had put the cost at $56m. 

In addition, Uganda’s Inspector-General of Government reported that the tender submitted in 2006 by the South African company was tainted with corruption. 

The company has since resorted to court for remedy, but Kampala has reportedly ignored the case. 

Meanwhile, TRA Commissioner General Harry Kitillya, has affirmed to THISDAY that the Smartcard driving licences tender, awarded to Face Technologies in 2006, is on track and that the authority and the Tanzania Police Force would soon introduce the licences to local motorists. 

Kitillya said yesterday that preparations for the licences had reached a final stage but he declined to mention the date for the kick-off of the exercise. 

He dismissed allegations that the project had stalled because the government intended to integrate it with the national identity card project. 

’’We talked to [Dickson] Mwaimu regarding integration of the project into the national identity card project but he was of the opinion that we proceed,’’ Kitillya said. 

Mwaimu is chief executive officer of the Registration, Insolvency and Trusteeship Agency. 

The South African company is also said to be vying for the national identity cards project. 

A number of local and international companies submitted bids for the computerised drivers licence system tender which was based on a build, operate and transfer arrangement in 2006. 

Those companies included Contec Global Limited, Global Enterprises Technologies, Techno Brain Limited, Electronics Corporation of India Limited & AKS Smart Card System Limited, Shivacom Limited, Quality Group Limited, Simba Technology (T) Limited, Afsat Communication (T) Limited & G Fischer Consulting (Pyt) Limited, 3i Infotech Limited and Starten Limited & LR Group Limited. 

The South African company’s Managing Director, Serfies Sorfontein, and Tshepo Boikanyo, General Manager of its holding company Arivia, did not respond to several mails sent by THISDAY over the past fortnight. 

On its website, however, the company has posted its TRA car registration computerisation system and Smartcard driving licences as projects that have been completed successfully. 

’’Face Technologies has become arivia.kom’s human face of information technology in Africa. The subsidiary is active in 11 African countries and gained major new public sector contracts on the continent in the past two years,’’ said the announcement. 

Since its establishment in 2002, the company claims it has won several tenders which included a drivers’ licence system for Namibia, traffic information systems for Malawi and Zambia, motor vehicle registration system for Tanzania and a national social security fund system and police identification systems for Uganda. 

In its court plea to Uganda’s Commercial Court, Face Technologies is seeking a $23m payment as compensation and damages for the alleged breach of contract. 

According to the suit documents, the firm claims it spent a lot of funds before the project was suspended in February 2006 by the Uganda Bureau of Statistics (UBOS) on orders of the Inspector General of Government (IGG).The firm claims it had started rolling out the project after carrying out a feasibility study . 

The project was suspended following a complaint from one of the bidders, Contec Global, which accused UBOS of flouting the laws in awarding the deal to Face Technologies.

SOURCE: This Day

CLICK HERE to listen  to the audio,and HERE for analysis.


Na John Daniel, Dodoma 

SERIKALI imeeleza kukasirishwa na gumzo la uvujaji wa mitihani na tatizo la vyeti visivyo halali na kuahidi kumulika upya kwa ukali zaidi Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na kuhakikisha tatizo hilo linakwisha. 

Akijibu maswali ya papo kwa hapo bungeni jana, Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, alisema ni aibu kwa Taifa kuzungumza kuvuja kwa mitihani mara kwa mara na kwamba analazimika kulizungumzia suala hilo kwa kuwa ni tatizo lililopo, lakini ni wakati muafaka wa kulikomesha. 

Katika swali lake kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Viti Maalumu, Bibi Magdalena Sakaya (CUF), aliitaka Serikali kutoa tamko kutokana na tatizo hilo, ambalo lililikumba Taifa hivi karibuni na kusababisha wanafunzi wa kidato cha nne kuahiroisha kufanya mtihani wa Hisabati. 

Pia Mbunge huyo aliitaka Serikali kutoa tamko akiihituhumu NECTA kwamba ndiye mhusika mkuu wa kuchapisha na kuuza vyeti bandia mitaani, jambo linalochangia kushusha kiwango cha elimu nchini. 

"Kwanza ni aibu sana kwa Taifa mitihani inavuja ni aibu kwa wazazi kununua mtihani mtaani, rai yangu kwa wazazi na Watanzania wote, tukatae tatizo hili, tumekubaliana na Waziri wa Elimu chombo chetu hiki NECTA lazima kiangaliwe kwa ukali zaidi,” alisema Bw. Pinda. 

Alisema licha ya mtihani wa Hisabati ulioandaliwa kwa ajili ya kidato cha nne mwaka huu kuvuja, lakini mitihani mingine haikuvuja na badala yake baaadhi ya watu waliibuka na kuuza makaratasi mitaani na kuvutia hisia za watu kwamba ndiyo mitihani halisi. 

CHANZO:
Majira

KUKASIRISHWA PEKEE NA KUINGALIA NECTA KWA UKALI ZAIDI PASIPO KUWAWAJIBISHA WAHUSIKA ITASAIDIAJE KUTATUA TATIZO HILI?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.