22 Dec 2008

Photo courtesy of MJENGWA

KURA YANGU INAWAANGUKIA WABABAISHAJI WA TRL.CHEKI "MBELEKO" NYINGINE HII KUTOKA KWA SUMATRA:

HATIMAYE Kampuni ya MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imeiruhusu Kampuni ya Reli (TRL) kuanza kutumia mabehewa yake 23 ya mitumba yaliyokodishwa kutoka Kampuni ya Reli ya India. Awali Sumatra waliizuia TRL kutumia mahehewa hayo kwa madai kwamba hayakuwa na obora unaotakiwa.

Hata hivyo, meneja uhusiano wa TRL, Midrahji Meiz alisema jana kuwa Sumatra sasa imewaruhusu kuendelea kutumia mabehewa hayo baada ya vigezo vilivyokuwa vinahitajika kukamilika.

“Tumesharuhusiwa na Sumatra kuanza kutumia mahehewa hayo na hivi sasa utaratibu unafanyika ili yanze kusafirisha abiria... baada ya utaratibu huo kukamilika tutatoa taarifa rasmi,” alisema Meiz na kuongeza: “Suala la usafiri wa treni ni suala la msingi kabisa na ndiyo maana tunajitahidi kuboresha usafiri huo kila wakati ili abiria wasafiri katika mazingira mazuri.”

Mkurugenzi na mdhibiti wa reli wa Sumatra, Alfred Nalitolela alikiri kuwepo kwa suala hilo na kusema kuwa wameamua kuiruhusu TRL indelee kutumia mabehewa hayo kwa kuwa wamekamilisha marekebisho yaliyokuwa yanahitajika.

“Tulibaini kwamba mabehewa hayo hayana ubora unaostahili kwa matumizi ya reli yetu, na moja ya vitu hivyo ni kiungio kati ya behewa moja na jingine, usambazi wa umeme ndani ya mabehewa, belling, spring, breki ya mkononi na magurudumu,” alisema Nalitolela na kuongeza:

“Tulipokwenda India kukagua mabehewa hayo, tuliwaeleza wafanye vitu hivyo lakini wakaleta mabehewa kabla ya kukamilika kwake ndipo ikabidi tuwakataze kuyatumia mpaka wamalize kuyafanyia marekebisho hayo.”

Alifafanua kwamba baada ya hapo walichukuwa moja ya kiungio cha mabehewa na kuyapeleka katika maabara ya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuyafanyia utafiti kama ni vifaa vipya na kuomba maelezo ya kina.

“Unafahamu katika suala hili lile jumba la behewa ndilo linalotakiwa kuwa mtumba, lakini vifaa vyote vinavyofanya mabehewa hayo yafanye kazi vinatakiwa kuwa vipya, ikiwemo usambaji wa nyaya za umeme ndani ya behewa. Na hicho ndicho tunachokikagua na kukiangalia na kuhakikisha kwamba viko salama kila wakati,” alifafanua Nalitolela.
CHANZO:Mwananchi
JE MWENZANGU KURA YAKO INAANGUKIA WAPI?


KAMPUNI iliyopewa jukumu la kusimamia na kutunza mali za lililokuwa Shirika la Reli Tanzania (RAHCO), imeanza kukatakata injini 27 na mabehewa 19 ili yauzwe kama chuma chakavu.

Mabehewa hayo na injini zake yanadaiwa yalikuwa na hali nzuri, lakini mwekezaji akayakataa wakati anachukua shirika kwa maelezo kuwa hayamfai.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya mwekezaji Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kudai kuwa, mabehewa hayo yalikuwa yamechakaa zaidi na hayawezi kutumiwa tena, huku Rahco ikidai kuwa yalikuwa yanafaa kuendelea kutumika.

Tayari zabuni ya kupata makampuni ya kununua vyuma hivyo chakavu imeshafanyika na washindi kupatikana.

Makampuni ambayo yameshinda zabuni yameshaanza kukata mabehewa hayo na injini katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Tabora na Kigoma.

Mwananchi Jumapili wiki hii ilishuhudia baadhi ya mafundi wa kampuni iliyoshinda zabuni wakikata mabehewa yaliyopo katika Stesheni ya Dar es Salaam.

Meneja Uhusiano wa RAHCO, Musita John aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa, wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa kuzifanyia kazi injini hizo na mabehewa.

Alisema kuwa endapo injini hizo na mabehewa zingefanyiwa ukarabati mdogo zingeendelea kuisaidia kampuni hiyo kupunguza matatizo ya usafiri lakini mwekezaji hakuzikubali.

John alisema wakati mwekezaji anachukua shirika hilo alikuta jumla ya injini 116 na 92 kati yake zilikuwa zinafanya kazi, lakini yeye aliamua kuchukuwa 79 tu na zingine akazikataa kwa madai kwamba hazimfai.

Alisema mbali na injini hizo, pia alikuta jumla ya mabehewa ya abiria 164, yaliyokuwa yanafanya kazi ni 125, lakini yeye aliamua kuchukuwa mabehewa 106 tu na 19 yaliyobaki aliyakataa.

John alifafanua kwamba baada ya mwekezaji huyo kumaliza tathimini ya mali za TRC alizokuta kabla hajaanza kazi waliamua kuziweka katika madaraja mbalimbali, ambapo daraja (A) lilikuwa ni mabehewa na injini yaliyokuwa yanafanya kazi.

Alisema Daraja (B) lilikuwa ni la mabehewa na injini zilizokuwa zinahitaji matengenezo madogo, ingawa yalikuwa bado yanaendelea na kazi ya kusafirisha abiria na mizigo wakati daraja (C) ni yale ambayo alikuta yameondolewa kazini, baada ya kuharibika na kupelekwa kwenye karakana ili yafanyiwe ukarabati, lakini pia aliyakataa kwa madai kwamba hayamfai.

Aliongeza kuwa kulikuwa na daraja (D) ambalo lilihusisha injini na mabehewa yaliyoharibika, yasiyofaa kutumika na daraja E ni yale ambayo yalishakaguliwa na kubainika kwamba, yalishafikia katika kiwango cha vyuma chakavu.

Hata hivyo, habari kutoka ndani ya TRL, zinaeleza kwamba mbali na injini na mabehewa hayo, mali zingine ambazo mwekezaji huyo alizikataa ni vifaa vya ofisini ambavyo hivi sasa pia viko katika orodha ya vitu vinavyouzwa na RAHCO kama vyuma chakavu.

Wakati RAHCO ikiendelea kukatakata injini hizo na mabehewa TRL hivi sasa inadaiwa kuwa katika hali mbaya kutokana na baadhi ya injini zake aina ya ‘73 class’ zilizokodishwa kutoka India kuwa na uwezo mdogo wa kuvuta mzigo, kiasi kwamba wanalazimika kuziunganisha mbili ndipo ziweze kuvuta mzigo ambao ungevutwa na injini moja aina ‘88 class’ za Tanzania alizozikataa.

Meneja Uhusiano wa TRL, Midlajy Maez alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake kuhusiana na suala hilo alisema wanaotakiwa kulizunguzia ni RAHCO.

CHANZO:Mwananchi

HIVI KWANINI TUNAENDELEA KUWANG'ANG'ANIA HAWA WABABAISHAJI WA KIDOSI?JIBU JEPESI NI KWAMBA WALIOWAKARIBISHA NI WABABISHAJI WENZAO,SO SIO RAHISI KWAO KUONA UBABAISHAJI ULIOPO.TUNA WAZIRI,NAIBU WAZIRI,KATIBU MKUU,NAIBU KATIKA MKUU,MKURUGENZI,NK,NK,NK WOTE KATIKA WIZARA HUSIKA.HAWA WANALIPWA MSHAHARA NA MARUPURUPU MENGINE KUTOKA KWA WALIPA KODI WA TANZANIA LAKINI SIJUI WANASHINDWA NINI KUCHUKUA HATUA STAHILI DHIDI YA USANII HUU ULIOPEWA JINA LA UWEKEZAJI.MWEKEZAJI GANI AMBAYE ILI ALIPE MSHAHARA KWA WAAJIRIWA WAKE NI LAZIMA APEWE TAFU NA SERIKALI?

KAMA KAWAIDA,JAMAA WATAHARIBU RELI WEE MPAKA IWE TOO MUCH THEN WATAINGIA MITINI,AU MZEMBE FLANI ATAKURUPUKA USINGIZINI NA KUDAI IUNDWE TUME YA UCHUNGUZI (ISOMEKE TUME YA KULA FEDHA ZA VIKAO) LAKINI WAKATI HUO HUDUMA YA RELI YA KATI ITAKUWA IMEKUFA KABISA.CALL IT MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA AS WE ARE APPROACHING 2009!


A Saudi court has rejected a plea to divorce an eight-year-old girl married off by her father to a man who is 58, saying the case should wait until the girl reaches puberty.

The divorce plea was filed in August by the girl's divorced mother with a court at Unayzah, 135 miles north of Riyadh just after the marriage contract was signed by the father and the groom.

Lawyer Abdullar Jtili said:"The judge has dismissed the plea, filed by the mother, because she does not have the right to file such a case, and ordered that the plea should be filed by the girl herself when she reaches puberty."

"She doesn't know yet that she has been married," Jtili said then of the girl who was about to begin her fourth year at primary school.

Relatives who did not wish to be named said that the marriage had not yet been consummated, and that the girl continued to live with her mother.

They said that the father had set a verbal condition by which the marriage is not consummated for another 10 years, when the girl turns 18.

The father had agreed to marry off his daughter for an advance dowry of £5,000, as he was apparently facing financial problems, they said.

The father was in court and he remained adamant in favour of the marriage, they added.

Mr Jtili said he was going to appeal the verdict at the court of cassation, the supreme court in the ultra-conservative kingdom which applies Islamic Sharia law in its courts.

Arranged marriages involving pre-adolescents are occasionally reported in the Arabian Peninsula, including in Saudi Arabia where the strict conservative Wahabi version of Sunni Islam holds sway and polygamy is common.

In Yemen in April, another girl aged eight was granted a divorce after her unemployed father forced her to marry a man of 28.

SOURCE: Daily Mail

21 Dec 2008

There are now more slaves on the planet than at any time in human history. True abolition will elude us until we admit the massive scope of the problem, attack it in all its forms, and empower slaves to help free themselves...CONTINUES HERE

19 Dec 2008


The man accused of masterminding the 1994 Rwanda genocide, Theoneste Bagosora, was jailed for life by an international court yesterday as prosecutors described his conviction as the most significant since Nuremberg.

Bagosora, 67, a former colonel who was the chief of staff in Rwanda's defence ministry, was convicted of genocide, crimes against humanity and war crimes at the end of a five-year trial after judges found that he used the military and an extremist Hutu militia to kickstart the massacre of about 800,000 Tutsis in 100 days.

The international criminal tribunal for Rwanda, sitting in Tanzania, also found Bagosora guilty of responsibility for overseeing individual massacres as well as the murder of Rwanda's prime minister, Agathe Uwilingiyimana, and the killing of 10 Belgian peacekeepers, which prompted the UN to withdraw most of its forces and abandon the Tutsi population to be slaughtered. Lieutenant General Romeo Dallaire, the UN commander in Rwanda, who called Bagosora the "kingpin" behind the genocide, described meeting him as like "shaking hands with the devil".

But the court did not convict Bagosora on the broader charge of conspiracy to commit genocide before the killing, saying that while he created, armed and trained the militia that carried out the massacres and headed an "enemy commission" that vilified Tutsis, that did not demonstrate that he had planned the extermination from the beginning.

"The chamber certainly accepts that there are indications which may be construed as evidence of a plan to commit genocide, in particular when viewed in light of the subsequent targeted and speedy killings immediately after the shooting down [of President Juvénal Habyarimana's plane which unleashed the genocide]," the judgment said. But the tribunal said these preparations were in the context of a war with Tutsi rebels and could not be said beyond doubt to be solely preparations to exterminate civilians.

Once the killings began, the tribunal found that Bagosora was the highest authority in the defence ministry and oversaw control of the military as it murdered opponents and kickstarted the genocide. The court said the killings "formed part of an organised military operation pursuant to orders from superior military authorities". Bagosora said nothing as the verdict was delivered.

Two other army officers on trial with Bagosora, Aloys Ntabakuze and Anatole Nsengiyumva, were also given life sentences for genocide. Prosecutors called them "enemies of the human race". A fourth defendant, Gratien Kabiligi, the former chief of military operations, was acquitted of all charges and released.

Barbara Mulvaney, the lead prosecutor, described the verdicts as historic. "I think it's one of the most important verdicts ever because the body of work, in documents in black and white, in transcripts, in video tapes, lays out the planning and organisation of a genocide," she said. "And it's important to the Rwandan people because it finally puts to rest the claims by some people ... who still deny there was a genocide or deny that it was planned. No one can claim that any more."

But the relevance of the tribunal has been diminished in Rwanda by lengthy trials held outside the country. None of the Hutu leaders on trial have apologised for their role in the genocide, raising fears among some Tutsis that it could happen again.

SOURCE: The Guardian

Watch this tear jecking video about the genocide.WARNING: Contains disturbing images.



18 Dec 2008








Picha kwa hisani ya thread ya Jamii Forums.

Click HERE to read full story.

A polite word of caution: The video is  44.09 mins long.
SOURCE: WSHH

17 Dec 2008

SOMA HABARI HII KISHA ANGALIA UCHAMBUZI WANGU
MLOLONGO wa matukio ya kufikishwa mahakamani kwa waliokuwa viongozi waandamizi katika Serikali ya Awamu ya Tatu pamoja na watuhumiwa wa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), unaonekana kuwatisha viongozi wa Kanisa Katoliki na sasa wameanza kupanga mikakati ya kuliepusha taifa na hali ya machafuko.

Askofu Mkuu Msaidizi wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini, juzi aliiambia Tanzania Daima Jumatano katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake kuwa, matukio yanayotokea sasa hapa nchini yanatisha kwa sababu yanaweza kuhatarisha amani iliyopo.

Alisema matukio ya kukamatwa kwa baadhi ya Watanzania wakiwa na mabilioni ya fedha zinazoweza kununua vijiji au mkoa, kufikishwa mahakamani kwa viongozi wastaafu wa serikali wakihusishwa na ufisadi na matumuzi mabaya ya madaraka wakiwa watumishi katika ofisi za umma, viongozi wa juu serikali kujiuzulu na matukio mengi ya mauaji ya kikatili, ni mambo yasiyokuwa ya kawaida na ya hatari.

Alisema kwa kutambua hali inayolikabili taifa, Kanisa Katoliki limeamua kuweka mikakati ya kulinusuru taifa na machafuko, itakayoongozwa na sala maalumu ya kuomba amani iendelee kutawala nchini.

“Kutokana na mambo haya mazito kutoka hapa nchini, tuna jukumu la kuhakikisha tunaiombea nchi yetu ili amani iliyopo iimarike kwa vile mlolongo wa matukio haya yasiyo ya kawaida yanaweza kuhatarisha amani iliyopo.

Sisi Kanisa Katoliki tumepiga kelele tumechoka, wenye jukumu la kuongea sana ni viongozi wa vyama vya siasa na mashirika ya kijamii. Sasa tumeamua kuanza na silaha kubwa zaidi ambayo ni sala, tumewaambia waumini wetu waanze utaratibu maalumu uliotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC) wa kusali sala maalumu ya kuliombea taifa amani, ambao utafuatwa na waumini wote Wakatoliki,” alisema Askofu Kilaini.

Alisema pamoja na kusali, kanisa lina jukumu la kuishauri serikali juu ya mwenendo wa mambo nchini, pamoja na kukemea maovu, uvunjaji wa maadili, tabia za ushirikina zinazokithiri, mauaji ya kikatili ya mtu mmoja mmoja na ya koo na mambo mengine ya kifisadi yanayofanywa na baadhi ya viongozi ambao ni waumini wa makanisa au misikiti.

Hata hivyo, alisema si wajibu wa kanisa kuwakataa waumini wake wanaohusishwa na matukio ya ufisadi nchini kwa sababu kuwafukuza kundini si kuwasaidia, bali ni wajibu wa kanisa kuwaelimisha na kuwajenga watu katika maadili mema.

“Sisi si polisi au mahakama, kwa hiyo hatuna jukumu la kumtaja mtu binafsi hadharani au kanisani, kama muumini anashiriki katika mamabo ya kifisadi, tunalo jukumu la kumrekebisha au kumkemea, lakini si kumtaja hadharani.

“Lakini ifahamike kuwa yanapotokea matukio makubwa nchini kama haya ya ufisadi na serikali ikachukua hatua au kutochukua hatua, ni lazima kanisa lizungumze.

Hata hivyo hatua iliyokwishachukuliwa na serikali ya kuwafikisha watuhumiwa wa EPA na wengine waliotumia madaraka vibaya mahakamani wakati wakiwa madarakani ni nzuri, ila ieleweke kuwa kanisa halisemi kuwa watuhumiwa wamekwisha, haliwezi kusema hivyo.

“Kanisa linathamini na kutambua hatua za awali zilizokwisha kuchukuliwa na serikali za kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, hatujui wapo wangapi, tunavuta subira kusikiliza kazi ya vyombo vya uchunguzi inayoendelea ili kuwafikisha wote mahakamani,” alisema Kilaini.

Akizungumzia mauaji ya albino, alisema kanisa linasikitishwa na hali inayoendelea nchini ya mauaji ya albino, vitendo ambavyo ni vya kikatili na ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyoweza kuvunja umoja wa kitaifa.

Alisema mauaji ya albino yanakera, yanaitia aibu nchi na kuikosesha heshima machoni pa jumuiya ya kimataifa. Kwamba dunia inawashangaa Watanzania wanaishi karne ipi.

Alisisitiza kuwa matukio ya mauaji ya albino yameichafua nchi kiasi cha wageni kuiona Tanzania kama mahali pasipofaa kuishi.

“Wageni nao wanaanza kuogopa kuja kwani albino wakiisha nchini watafuata kundi jingine la watu, na kwa mtiririko huo, baadaye Watanzania wote wataanza kuuana. Serikali inatakiwa ilitangaze suala hili kuwa janga la kitaifa.

“Kama taifa tunapaswa kuchukua hatua madhubuti kupambana na kukomesha mauaji haya kwa vile tunakoelekea ni kubaya, wakimaliza albino, watawataka wenye kipara, baadaye watu weusi au wa kabila fulani, tukifika hapo ni vita ya wenyewe kwa wenyewe.

“Kanisa linaitaka serikali kutumia mbinu zozote, kutoa elimu kwa raia wake ikiwezekana kuanzia kwenye shule za msingi na sekondari juu ya madhara ya mauaji hayo. Kanisa linaiomba serikali iunde idara maalumu ya usalama wa taifa, makachero watumwe vijijini kuangalia kazi inayofanywa na waganga wa kienyeji, wachunguze kazi zao, wanavyopiga ramli na kupata ufumbuzi wa chimbuko na misingi ya mauaji hayo,” alisema Askofu Kilaini.

Akizungumza sababu ya kanisa kuchukua hatua ya kuanzisha mkakati wa kuomba ili kunusuru taifa na hali yoyote ya uvunjifu wa amani, alisema, imetokana na hofu ambayo kanisa limeipata baada ya kuwapo kwa ongezeka kubwa la matukio ya ajabu ambayo kwa kipindi cha miaka mingi hata kabla ya uhuru hayakuwahi kutokea.


KAMA MKATOLIKI,NAKUBALIANA NA KAULI YA KIONGOZI WANGU WA DINI MHASHAMU KILAINI.LAKINI KAMA MCHAMBUZI (MCHANGA) WA STADI ZA SIASA,NAOMBA KUTOAFIKIANA NAE KATIKA MAENEO YAFUATAYO.

KWANZA,KANISA KATOLIKI LINAPASWA KUKUBALI KWAMBA HALIJAFANYA VYA KUTOSHA KUPAMBANA NA MAOVU NDANI YA JAMII.NA KATIKA HILO,SIO KANISA PEKEE LINALOWEZA KUTUPIWA LAWAMA BALI TAKRIBAN MADHEHEBU YOTE HUKO NYUMBANI.TUNAWEZA KWENDA MBALI ZAIDI KWA KUANGALIA BAADHI YA MAMBO YANAYOWEZA KUWA SABABU KUU YA "UOGA" WA BAADHI YA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA MAUMI MENGINE KATIKA JAMII.WENGI WETU TUNAFAHAMU "UCHAFU" WA BAADHI YA VIONGOZI HAO,NA JAPO KANISA LIMEKUWA LIKISISITIZA KUFUATA MAFUNDISHO YA VIONGOZI NA SIO MATENDO YAO,UKWELI UNABAKI KWAMBA NI VIGUMU KUTENGANISHA MANENO NA VITENDO VYA MSEMAJI.HIVI INALETA MAANA KWELI.KWA MFANO,MTUMISHI WA MUNGU ANAYEBANJUA AMRI YA SITA (MZINZI) KISHA AKAHUBIRI KUHUSU DHAMBI YA UZINZI?NI DHAHIRI MJUMBE WA YESU ANAPASWA KUISHI KAMA YESU MWENYEWE.YAYUMKINIKA KUSEMA KWAMBA LAITI MITUME WETU WASINGEKUWA WASAFI KATIKA MATENDO YAO,LEO HII TUSINGEKUWA WAUMINI WA DINI ZETU.

TUKIREJEA KWENYE HABARI HIYO HAPO JUU,SIJAMWELEWA VIZURI MHASHAMU KILAINI ANAPOSEMA "matukio yanayotokea sasa hapa nchini yanatisha kwa sababu yanaweza kuhatarisha amani iliyopo".JE ANAMAANISHA KWAMBA AMANI ITAHATARISHWA KUTOKANA NA TUKIO KAMA KUWAFIKISHA WATUHUMIWA WA UFISADI MAHAKAMANI?KWANINI SUALA HILO LISIWE KIGEZO CHA KUREJESHA IMANI YA WANANCHI ILIYOPOTEA KUTOKANA NA HISIA KWAMBA MAFISADI WANALINDWA?AMANI HAIWEZI KUHATARISHWA KWA KUWACHUKULIA HATUA MAFISADI,REGARDLESS YA NAFASI ZAO KATIKA JAMII.KWA NAMNA FLANI KAULI HIYO YA MHASAHAMU KILAINI INASHABIHIANA NA ILE ILIYOWAHI KUTOLEWA NA MKURUGENZI WA TAKUKURU,BW EDWARD HOSEA,KWAMBA WATUHUMIWA WOTE WA EPA WAKISHTAKI NCHI ITAYUMBA.

SITAKI KUINGIA KWA UNDANI KUHUSU DHANA KUWEPO KWA AMANI HUKO NYUMBANI,KWA SABABU DHANA HIYO NI TETE.JE AMANI NI KUTOKUWEPO KWA VITA PEKEE?JE KUNA AMANI KWA VILE WENYE VIPARA,VITAMBO,MAWOWOWO,ETC HAWAWINDWI KAMA MAALBINO?JE KUNA AMANI WAKATI IDADI YA WASIO NA UHAKIKA WA MLO WA KESHO NI KUBWA ZAIDI YA WALE WENYE UHAKIKA HUO?SIKU CHACHE ZIJAZO NITAINGIA KWA UNDANI KUANZISHA MJADALA KUHUSU DHANA YA AMANI NCHINI TANZANIA.LAKINI TUNALOWEZA KUHOJIM KWA SASA NI IWAPO MATUKIO YANAYOZUNGUMZWA NA MHASHAMU KILAINI YANAWEZA KUHATARISHA AMANI (KAMA TUNAKUBALIANA KUWA AMANI HIYO IPO,IN THE FIRST PLACE).

MHASHAMU KILAINI ANASEMA "Kanisa Katoliki limeamua kuweka mikakati ya kulinusuru taifa na machafuko, itakayoongozwa na sala maalumu ya kuomba amani iendelee kutawala nchini".NATAKA KUAMINI KWAMBA MKAKATI HUU WA KANISA UMEKUWEPO KWA MUDA MREFU ILA SASA UNAIMARISHWA.KINYUME CHA HIVYO ITAMAANISHA KWAMBA KANISA LIKO OUT OF TOUCH NA HALIJALI MADHILA YANAYOWAKUMBA WENGI WA WAUMINI WAKE.SI KWELI KWAMBA MATATIZO YANAYOIKABILI TANZANIA YAMEANZA MAJUZI KIASI CHA KANISA KUSHTUKA NA KUJA NA MKAKATI HUO,BALI MATATIZO HAYO YAMEKUWEPO KWA MUDA MREFU SASA.HATA MAUAJI DHIDI YA ALBINO HAYAJAANZA MWAKA HUU KIASI CHA KANISA KUSHTUKA WAKATI HUU TUNAPOELEKEA MWISHONI MWA MWAKA.

LAKINI TWENDE MBELE ZAIDI NA KUJADILI IWAPO MKAKATI HUO WA SALA UNAWEZA KUWA NA MAFANIKIO.TUNAFAHAMU KWAMBA BAADHI YA WATUHUMIWA WA UFISADI NI WAKRISTO WANAOHUDHURIA KANISANI KILA JUMAPILI.TUAMINI PIA KWAMBA MAHUBIRI MENGI HUKO KANISANI YANASISITIZA UPENDO NA KUPINGA VITENDO VYA KIFISADI.SASA KWA VILE VITENDO HIVYO SIO TU VIMEENDELEA BALI VIMESHIKA HATAMU TO ANA EXTENT YA KULIFANYA KANISA KUJA NA MKAKATI MPYA,NI DHAHIRI KWAMBA SALA PEKEE HAZIWEZI KULETA MABADILIKO YA MAANA.HAWA MAFISADI TUNAOJUMUIKA NAO MAKANISANI WANAPASWA KUWEKWA "KITIMOTO" HATA KAMA KUFANYA HIVYO NI KINYUME NA TARATIBU ZA KANISA.VIONGOZI WETU WA DINI WANAPASWA KUWAITA WAUMINI WAO WANAOTUHUMIWA NA UFISADI NA KUWAAMBIA (KATIKA LUGHA YA KIROHO) KWAMBA MATENDO YAO YANAMKERA MUNGU (NA MUNGU TUNAYEMZUNGUMZIA HAPA NI YULE TULIYEAMBIWA WAKATI WA KAMPENI KWAMBA "ANA CHAGUO LAKE KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2005").

NADHANI WENGI WETU BADO TUNA KUMBUKUMBU NAMNA ASKOFU LAIZER WA KKKT ALIVYOTUMIA MIMBARI YAKE KUMSAFISHA LOWASSA (REJEA MAKALA HII KATIKA JARIDA LA RAIA MWEMA).VIONGOZI WENGI WA DINI WAMEKUWA MASHABIKI WA WANASIASA,PENGINE KWA MASLAHI YAO BINAFSI BADALA YA YALE YA WAUMINI WAO AMBAO NDIO WANAOONJA JOTO YA JIWE KILA KUKICHA KUTOKANA NA MADUDU YA BAADHI YA WANASIASA HAO.NAKUMBUKA LECTURE MMOJA PALE MLIMANI (UDSM) WAKATI NASAKA SHAHADA YANGU YA KWANZA AMBAPO MHADHIRI MMOJA,DR MAX MMUYA,ALIELEZA KWAMBA FORCES KUU ZA KUWEZA KUBADILI TABIA,MAAMUZI NA MATENDO YA WANASIASA NA TAASISI ZA DINI NA WAHISANI.VIONGOZI WA DINI WAKTITISHI KUMTENGA KIONGOZI FISADI LAZIMA ATABADILIKA KWANI ANAJUA KESHO KUNA KIFO.WAHISANI WAKITISHIA KUNYIMA MSAADA BASI HATA WATUHUMIWA WA ANBEM WATAFIKISHWA MAHAKAMANI.KWA KIFUPI,MADHEHEBU YA DINI NCHINI YAMETUANGAUSHA WAUMINI WAKE KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI.

TUREJEE KWENYE HABARI HUSIKA.MHASHAMU KILAINI ANASEMA "Sisi Kanisa Katoliki tumepiga kelele tumechokawenye jukumu la kuongea sana ni viongozi wa vyama vya siasa na mashirika ya kijamii. Sasa tumeamua kuanza na silaha kubwa zaidi ambayo ni sala...".HIVI KAMA KANISA LIMECHOKAM KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI LITAWEZA KWELI KWENYE MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI YANAYOLENGWA KUWASAIDIA WAUMINI WAKE WAUFIKIE UZIMA WA MILELE?THIS IS SHEER IRRESPONSIBILITY!KANISA HALIPASWI KUCHOKA,SIO TU KWENYE KUPIGA KELELE DHIDI YA UFISADI BALI PIA KWENYE KILA JAMBO LITAKALOWASAIDIA WAUMINI WAKE KUUONA UFALME WA MBINGU.KUDAI KUWA JUKUMU LA KUPIGA MAKELELE LIMEACHWA KUONGELEWA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA NA MASHIRIKA YA KIJAMII NI TUSI KWA WAUMINI WA KANISA HILO.KWANI HAKUNA WAKATOLIKI MIONGONI MWA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA NA VYAMA VYA KIJAMII?KAMA WAPO,WAPI WATAPATA MWONGOZO WA KIROHO WA KUWAPA UJASIRI WA KUKEMEA MAFISADI KAMA SIO KANISANI?TANGU LINI KANISA LIKACHOKA?HIVI YESU ANGECHOKA KATIKA MISSION YAKE YA KUMKOMBOA MWANADAMU TUNGEKUWA NA AKINA MHASHAMU KILAINI?SALA PEKEE PASIPO KUPIGA KELELE HAZIWEZI KULETA MABADILIKO KWANI HIYO HAINA TOFAUTI NA KWA MWANAFUNZI KUSALI SANA LAKINI BILA KUJISOMEA KISHA AKATEGEMEA KUFAULU MTIHANI.SALA ZIENDANE NA MAKELELE ZAIDI YA KUKEMEA UFISADI.

MHASHAMU KILAINI AMEJITAHIDI KUNYAMBULISHA MAJUKUMU YA KANISA KWA WAKATI HUU (ACTUALLY,KWA MUDA WOTE) NA HAPO NDIPO ANAPOZUA CONTRADICTION KUBWA ZAIDI KWANI MAJUKUMU HAYO HAYATATEKELEZEKA IWAPO KANISA LITAKUWA LIMECHOKA.BY THE WAY,UCHOVU UNAOZUNGUMZIWA HAPA NI ULE UNAOSHABIHIANA NA KUKATA TAMAA AU UVIVU,NA VYOTE HIVYO NI MIZIZI YA DHAMBI.TUTAMUANIJE MHASHAMU KILAINI KWAMBA BAADA YA KUCHOKA KUPIGA MAKELELE KANISA HALITACHOKA PIA KUISHAURI SERIKALI?

MWISHO,NAUNGANA NA MHASHAMU KILAINI JUU YA UMUHIMU WA KUTANGAZA MAUAJI YA ALBINO KUWA NI JANGA LA KITAIFA.NAAFIKIANA NAE PIA KWAMBA SERIKALI INAPASWA KUZI-MOBILIZE TAASISI ZA USALAMA ZIONGEZE NGUVU ZAO KUKABILIANA NA JANGA HILO.KAMA INAFANYWA HIVYO KATIKA KUKABILIANA NA UJAMBAZI AU KUDHIBITI WAKIMBIZI,KWANINI ISIANZISHWE OPERESHENI MAALUMU DHIDI YA MAUAJI YA ALBINO?


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.