27 Dec 2008


POSTMORTEM NI MUHIMU HASA KWENYE VIFO VYENYE UTATA.LAKINI POSTMORTEM KWENYE MASUALA YA SIASA NI MBINU INAYOTUMIKA AIDHA KUKWEPA LAWAMA NA KUZIELEKEZA MAHALA KWINGINE AU KUPOOZA MAUMIVU YALIYOSABABISHWA NA MAPUNGUFU KWENYE UWAJIBIKAJI.KATIKA HABARI IFUATAYO,MBUNGE WA HANDENI,DKT ABDALLAH KIGODA, AMETOA POSTMORTEM REPORT YA MPANGO WA "MABILIONI YA JK",KWAMBA HAYAKUWANUFAISHA WATU WA VIJIJINI.PENGINE KABLA YA KUANGALIA VIJIJINI,SWALI KUBWA LILIPASWA KUWA "MABILIONI HAYO YAMEWANUFAISHA WATU WANGAPI REGARDLESS YA LOCATIONS ZAO-MIJINI AU VIJIJINI".LAKINI LA MSINGI ZAIDI,JE POSTMORTEM REPORT KAMA HIYO YA KIGODA INA UMUHIMU GANI KWA WANANCHI AMBAO HAWAKUNUFAIKA NA MPANGO HUO ULIOLENGA KUBORESHA MAISHA YA WATANZANIA?SOMA KWANZA HABARI YENYEWE KISHA TUENDELEE NA MJADALA:
Na Steven William, Handeni
MBUNGE wa Handeni Dkt Abdallah Kigoda, amesema kuwa dhamira ya Rais Jakaya Kikwete kutenga fedha kwa ajili ya kukopeshwa wajasiriamali wadogo alikuwa na dhamira nzuri, lakini fedha hizo zilivamiwa na 'wajanja' wachache waliozikopa na wananchi hasa wa vijiji hazikuwafikia.

Akizungumza katika mikutano ya hadhara kwenye vijiji vya kata ya Ndolwa wilayani hapa juzi kufuatia wananchi kumbana mbunge huyo kuhusu mikopo hiyo maarufu 'mabilioni ya Kikwete', mbunge huyo alisema kuwa fedha hizo zilitengwa na kupitia benki ambako wananchi wengi hasa wa vijijini hawana uelewa mpana wa kutumia benki zilizopo kukopa.

"Ndugu zangu wananchi dhamira ya Rais ilikuwa nzuri kwani alitenga fedha hizo kwa ajili ya kuwasaidia wenye mitajhi midogo wapandishe mauzo ya bidhaa zao lakini fedha zile zilipitia benki na nyie uwezo wa kuzitumia benki hamjui, hivyo wajanja wakajitokeza wakazichota," alisema Dkt Kigoda.

Aliwapa mfano wa mkoa wa Kagera fedha hizo zilizpopelekwa mkoani humo, ni watu watano tu waliopata fedha hizo kutoka katika benki hizo akiwemo meneja wa benki hiyo hali iliyoleta tafsiri mbaya kwamba waliozichukua ni watu wa mjini waliokuwa na fursa nzuri na uzoefu wa kukopa benki.

Hata hivyo, aliwatoa wasiwasi wananchi hao kwamba serikali itatoa tena fedha lakini walishauri kwamba pindi zikitolewa zishirikishe viongozi wa wilaya husika wachama na serikali ambao wamekuwa wakifahamu vikundi mbalimbali vya wajasiriamali katika maeneo husika hivyo fedha hizo zitafika kwa walengwa.

Kufuatia kuingizwa tena fedha hizo kwenye mabenki hayo, mbunge huyo aliwataka wananchi wa wilaya ya handeni kuhakikisha wanajiunga na vikundi vya ujasiriamali ambavyo vitatambulika na serikali ili waweze kuomba na kupata mikopo.

CHANZO:Mwananchi

HIVI DKT KIGODA ALIKUWA WAPI WAKATI FEDHA HIZO ZIKIELEKEZWA KUSIKOSTAHILI?NA WAKATI ANATOA TAKWIMU ZA KAGERA,KWANINI HATAJI IDADI YA WALIONUFAIKA AU KUATHIRIKA KATIKA JIMBO LAKE LA HANDENI?PIA ANAPASWA KUWAOMBA RADHI ALIOKUWA AKIWAHUTUBIA KWA KUSEMA "..na nyie uwezo wa kuzitumia benki hamjui".HIVI NI KWELI WANAKIJIJI WOTE ALIOKUWA AKIWAHUTUBIA,NA WENGINEO AMBAO HAWAKUPATA MABILIONI HAYO HAWANA UWEZO WA KUZITUMIA BENKI?JE YEYE KAMA KIONGOZI NA MWAKILISHI WAO AMEFANYA NINI KUWASAIDIA WAPIGA KURA WAKE KUWA NA UWEZO WA KUJUA NAMNA YA KUZITUMIA BENKI?BY THE WAY,NENO "KUZITUMIA" NI CONTRADICTORY KWANI LINAWEZA PIA KUMAANISHA KUZITUMIA BENKI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA UFISADI WA EPA.ANYWAY,NADHANI ALIKUWA ANAMAANISHA WANAKIJIJI HAWAJUI KUZITUMIA HUDUMA ZA BENKI.IF SO,HAWAJUI KWA VILE HAKUNA BENKI,BENKI ZIPO LAKINI HAZITOI ELIMU YA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA ZAKE,WANAKIJIJI HAWATAKI KUELEKEZWA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA HIZO,AU...?

TATIZO KUBWA LINALOKWAMISHA MIPANGO MIZURI NI MIPANGO MIBOVU.WAINGEREZA WANA MSEMO POOR PLANNING PRODUCES POOR PERFORMANCE.UBOVU WA MPANGO WA MAMILIONI YA JK ULIKUWA KWENYE USIMAMIZI.NI DHAHIRI KWAMBA UKIPELEKA MAMILIONI,LET ALONE MABILIONI,PASIPO KUHAKIKISHA KUWA WAJANJA (ISOMEKE MAFISADI) HAWATABUNI MBINU ZA KUTAFUNA FEDHA HIZO,ITAKUWA NI MITHILI YA KUTWANGA MAJI KWENYE KINU.

MPANGO WA KUWAPATIA FEDHA WANANCHI WASIO NA UWEZO ILI ZIWASAIDIE KUJIKWAMUA KIUCHUMI ULIKUWA MZURI LAKINI ULIHITAJI UCHAMBUZI MAKINI KATIKA USIMAMIZI NA UTEKELEZAJI WAKE.KULIKUWA NA HAJA YA KUANGALIA POWER RELATIONS HUKO ZINAKOPELEKWA FEDHA HIZO,HUSUSAN MAHUSIANO KATI YA WASIMAMIZI NA WALENGWA.UDHAIFU KATIKA HILO NDIO UMEPELEKEA KESI KAMA HIYO YA KAGERA AMBAPO MENEJA WA BENKI NAE AKAJIINGIZA MIONGONI MWA WALENGWA JAPO SIDHANI KAMA ILIPASWA KUWA HIVYO.KILICHOPASWA KUFANYIKA KABLA YA KUPELEKA FEDHA HIZO NI KUTAMBUA WANAOZIHITAJI,KUFAHAMU MIPANGO YAO YA NAMNA WATAKAVYOTUMIA FEDHA HIZO AMBAZO KIMSINGI NI MIKOPO,KUTENGENEZA MAZINGIRA AMBAPO MAFISADI HAWATAZITAFUNA NA MWISHO,KUZIWASILISHA KATIKA WAKATI MWAFAKA.

PENGINE KABLA YA KUFIKIRIA KUTOA AWAMU NYINGINE YA MABILIONI NI MUHIMU KUFANYA TATHMINI YA MAFANIKIO NA FAILURES KATIKA AWAMU ZILIZOTANGULIA.SAMBAMBA NA HILO NI KUCHUKUA HATUA KALI KWA WOTE WALIOFUJA FEDHA HIZO.PIA NI MUHIMU KUFAHAMU FEDHA HIZO ZITAREJESHWA VIPI ILI BAADAYE WASIJE WAJANJA WAKAPORA ARDHI NA MALI NYINGINE ZA WALALAHOI KWA VISINGIZIO VYA KUDAI MAREJESHO YA FEDHA HIZO.

MWISHO,VIONGOZI KAMA DKT KIGODA WANAWEZA KUWA NA UMUHIMU ZAIDI KATIKA KULETA UFANISI WA MPANGO HUO WA MABILIONI YA JK SIO KWA KUTULETEA POSTMORTEM PINDI MAMBO YAKIENDA MRAMA BALI KWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KUHAKIKISHA MAFANIKIO YANAPATIKANA.HILO HALIHITAJI SEMINA ELEKEZI KWANI LIKO NDANI YA UWEZO WETU.KINACHOHITAJIKA NI DHAMIRA NA UWAJIBIKAJI.YES WE CAN!

26 Dec 2008

MASTANTA KIBWENA (Picture for illustrative purpose only)
CLICK HERE TO READ FULL STORY.

CHAGUZI NDANI YA CCM HAZIISHIWI VIOJA.RUSHWA IMETAPAKAA MNO NDANI YA CHAMA HICHO KANA KWAMBA NI SEHEMU YA KATIBA YAKE.SIO MATUSI KUAMINI KWAMBA PENGINE INGEKUWA RAHISI ZAIDI KWA CCM KUAHIDI KUENDELEZA LIBENEKE LA RUSHWA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 KULIKO AHADI ZA MAISHA BORA,MAHAKAMA YA KADHI,NK MAMBO AMBAYO HADI SASA YAMEENDELEA KUWA AHADI ZISIZOTEKELEZEKA.NI WAZI,RUSHWA HUZAA VIONGOZI WABOVU,MAFISADI NA WABABAISHAJI.HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI ZA KUISHA KWA GONJWA HILO HATARI NDANI YA CHAMA TAWALA.TAASISI ZA UMMA ZA KUKABILIANA NA RUSHWA ZINAISHIA KUALIKWA TU KWENYE CHAGUZI "KUZUIA RUSHWA" NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO WAMEISHIA KUPIGA KELELE TU (SINA HAKIKA KAMA NI ZA DHATI) KUHUSU RUSHWA KWENYE CHAGUZI,LAKINI SOTE TUNAJUA KWAMBA KELELE ZA CHURA HAZIMZUII NG'OMBE KUNYWA MAJI.ENEWEI,HEBU CHEKI MKASA HUU HAPA CHINI KISHA SOMA HITIMISHO LANGU BAADA YA HABARI HII:
Zikiwa zimesalia siku 14 kufika siku ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mambo si shwari katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wake. 

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 7, mwakani ambapo nafasi ya uenyekiti itagombewa na Janet Kahama, Sophia Simba na Joyce Masunga. 

Hali hiyo, ambayo inazidi kuipaka matope CCM, imedhihirika baada ya mgombea wa nafasi ya Janeth Kahama kuwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akimtuhumu mpinzani wake, Sophia Simba kwamba amewahonga wajumbe wote wa Mkutano Mkuu rushwa ya Sh. 100,000 ili wampe kura. 

Mbali na tuhuma za rushwa, Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), anatuhumiwa pia na Kahama kuwa yeye na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu. 

Kahama, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), amewasilisha malalamiko hayo kupitia barua yake yenye kumbukumbu Na. JBK/01/08 ya Desemba 20, mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam. 

Nakala ya barua hiyo, ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT Taifa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi jioni kama amepokea nakala ya barua hiyo, alithibitisha kuipokea. 
Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha kwa lengo la kuwatakia heri ya Mwaka Mpya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa. 

Kadi hizo, ambazo zinadaiwa kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, zina picha, jina na saini ya Waziri Simba, kalenda ya Mwaka Mpya wa 2009 na nembo ya CCM. 

Barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho: `Yah: Malalamiko dhidi ya Mhe. Sophia Simba kugawa vipeperushi mikoani`, Kahama anamueleza Mwenyekiti Kikwete kama ifuatavyo: 

``Kwa heshima ya pekee, nakuomba uhusike na mada ya barua hii kama inavyosomeka hapo juu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyofahamu, Jumuiya yetu ya UWT hivi sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani.`` 

``Mimi nikiwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, natambua kuwa wagombea wote tulizuiwa na vikao vya UWT Taifa kutoa vipeperushi vya aina yoyote kwa minajili ya kujinadi kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UWT.`` 

``Lakini, ajabu ni kwamba, mgombea mwenzangu, Bi Sophia Simba amechapisha kalenda na kadi za `Heri ya Mwaka Mpya` zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzisambaza kwa wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa nchi nzima, ndani zikiwa na kitita cha Sh. 100,000 (kwa kila kadi).`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nalazimika kukuandikia waraka huu ili kukupa angalizo juu ya suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa Mheshimiwa Sophia Simba ni Waziri katika ofisi yako mwenye dhamana ya Utawala Bora.`` 

``Hivyo hatua yake na nembo ya CCM, inakwenda kinyume na kanuni za uchaguzi za CCM, kipengele cha Miiko ya Kuzingatiwa wakati wa Shughuli za Uteuzi na Uchaguzi`, ibara ya 33 kifungu kidogo cha 14 kinachosema: `Ni mwiko kutumia makaratasi ya kampeni nje ya utaratibu wa chama au kutumia vishawishi vya aina yoyote ile kwa minajili ya kupata kura.`` 

``Je, hatua hii ya Mheshimiwa Simba kuchapisha nyaraka hizo zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzitawanya nchi nzima, si uvunjaji wa makusudi wa kanuni hizo za uchaguzi za CCM tena kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa UWT?`` 

``Je hatuoni kwamba hatua yake hiyo ambayo haijakemewa mpaka sasa ni kielelezo kingine cha ubabe na matumizi mabaya ya madaraka yake kama Waziri tena mwenye dhamana ya Utawala Bora? 

Nasisitiza hili kwa sababu Mheshimiwa Simba na wapambe wake wamekuwa wakipita mikoani na kupotosha wapigakura kuwa yeye ndiye chaguo la Ikulu.`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha kwako waraka huu wenye malalamiko haya ili uweze kujua nini kinaendelea na kuchukua hatua kwani kama kitaachwa, kinaweza kujenga matabaka ndani ya UWT na mpasuko usio wa lazima ndani ya chama chetu, hasa pale hisia za mgombea mmoja kuandaliwa mazingira ya ushindi dhidi ya wenzake zinapoanza kujengwa.`` 

``Naambatanisha moja ya vipeperushi hivyo vya Mheshimiwa Simba vilivyosambazwa mikoani kinyume na utaratibu nilioueleza hapo juu.`` 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi, licha ya kukiri kupokea nakala ya barua hiyo ya Kahama, alimtaka mwandishi kama ana swali lolote kuhusiana na suala hilo, akamuulize Rais Kikwete kwa vile ndiye aliyeandikiwa barua hiyo. 

``Mtafute Mwenyekiti wa CCM, yeye ndiye aliyeandikiwa barua, aliyeandikiwa ndiye anayejibu. Mimi nimepewa nakala, anayepewa nakala, anaarifiwa tu,`` alisema Makamba. 

Nipashe ilipowasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alisema kwa vile malalamiko ya Kahama yanahusiana na Chama, anayepaswa kujibu suala hilo ni Katibu Mkuu. 

Baada ya Makamba kuulizwa tena, alisema: ``Mimi sina cha kusema, sijaisoma (hiyo barua), sijajua maudhui. 

Nitakapoisoma na kujua maudhui, nitatoa maoni yangu.`` 

Kahama alipoulizwa na Nipashe jana kama barua hiyo ndiye aliyeiandika, hakukiri wala kukanusha, badala yake alisema kwa sasa hawezi kuzungumza lolote kwa vile kipindi hiki ni cha sikukuu ya Krismasi, ambayo yeye kama Mkristo anapaswa kuitukuza. 

``Sina comments (maoni) kabisa kabisa, mpaka nionane na Katibu Mkuu. Pia mimi ni Mkristo na kipindi hiki ni cha Krismasi,`` alisema. 

Naye Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, alipoulizwa juzi, alikataa kuzungumzia suala hilo, badala yake alimtaka mwandishi akamuulize Simba. 

``Kwani Sophia Simba mimi ni nani kwake?`` alihoji Kondo, ambaye alipojibiwa na mwandishi kuwa ``Simba anadaiwa kuwa ni mtu wake wa karibu``, alisema: ``Nenda kamuulize Simba.`` 

Tangu juzi hadi jana jioni Nipashe ilimtafuta Simba bila kumpata na baadaye kuelezwa na mmoja wa wanafamilia yake kuwa yuko safarini Malaysia. 

CHANZO:Nipashe

WAKATI MAMA KAHAMA AMETUMIA HAKI YAKE YA MSINGI KAMA MGOMBEA NA MWANANCHAMA WA UWT/CCM KUWASILISHA MALALAMIKO YAKE KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA (JK),NADHANI ANGEWEZA PIA KUWASILISHA TUHUMA HIZO POLISI AU TAKUKURU.HIVI KUTOA RUSHWA SI NI KOSA LA JINAI?JE MAMA KAHAMA YUKO MORE CONCERNED NA RUSHWA HIYO KUATHIRI NAFASI YAKE YA KUCHAGULIWA KULIKO UKWELI KWAMBA MTUHUMIWA (SOPHIA SIMBA) SIO WAZIRI TU BALI NI WAZIRI MWENYE DHAMANA YA UTAWALA BORA (ISOMEKE MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA)?


The Afghan chieftain looked older than his 60-odd years, and his bearded face bore the creases of a man burdened with duties as tribal patriarch and husband to four younger women. His visitor, a CIA officer, saw an opportunity, and reached into his bag for a small gift.Four blue pills. Viagra...CLICK HERE FOR FULL STORY


25 Dec 2008


Kiongozi wa mapinduzi hayo,Kapteni Moussa Dadis Kamara,aliyejitangaza kiongozi mpya wa Guinea baada ya kifo cha Rais Lansana Conte.Kwa habari zaidi,BONYEZA HAPA.


HIVI TUNA UHABA MKUBWA SANA WA WATENDAJI NA VIONGOZI WAZURI HADI TUENDELEE KUWANG'ANG'ANIA HATA WALE WALIOKWISHAFANYA MADUDU HUKO NYUMA?KUNA STORI KATIKA GAZETI LA MWANANCHI KUHUSU ALIYEKUWA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE,JOHN LUBUVA,AMBAYE ALISIMAMISHWA KAZI KUTOKANA NA SAKATA LA UBOMOAJI NYUMBA HUKO TABATA DAMPO.CHA AJABU ETI KWA SASA NI MKURUGENZI WA MANISPAA YA SHINYANGA VIJIJINI.HII SIO TU DHARAU KWA WAKAZI WA MANISPAA HIYO ILIYOLETEWA "MTENDAJI MPYA" BALI PIA NI MUENDELEZO WA HAKA KAMTINDO KA KUNG'ANG'ANIA VIONGOZI WALIOPUNGUKIWA NA SIFA.JE,KUMREJESHA KIONGOZI HUYO MADARAKANI HAKUWEZI KUWA KICHOCHEO KWA VIONGOZI WENGINE KUREJEA MADUDU KAMA YA MWENZAO ALIYEBORONGA,AKAPEWA MAPUMZIKO MAFUPI KISHA AKAREJESHWA MADARAKANI?TANGU LINI ADHABU KWA MAKOSA YA UONGOZI IKAWA KUHAMISHWA KUTOKA TEMEKE NA KUPELEKWA SHINYANGA?HIVI AKILIKOROGA TENA HUKO SHINYANGA ITAKUWAJE?THIS IS NOT ONLY UNFAIR BUT INAKERA NA KUCHUKIZA PIA.


Serikali imeridhia Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA- JKT), liongezewe nguvu kiutendaji na kuwa kampuni ya ulinzi itakayotoa ushindani kwa makampuni binafsi ya ulinzi yanayotoa huduma hiyo kwa kiwango kisichoridhisha. 

Kwa sasa SUMA, imejikita katika ujenzi wa nyumba za serikali, barabara na kutengeneza samani. 

Uamuzi wa JKT kuwa na kampuni ya ulinzi, una lengo la kuajiri vijana wanaohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi. 

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Kanali Ayoub Mwakang’ata, alitoa taarifa hiyo jana wakati akihutubia katika kilele cha mafunzo ya Operesheni Uadilifu yaliyokuwa yakifanyika katika Kambi ya 835 JKT Mgambo wilayani Handeni. 

Katika taarifa yake alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na Jeshi hilo wameridhia kampuni hiyo kuanza kazi rasmi mapema mwakani. 

Kampuni hiyo imepanga kuboresha huduma za ulinzi kwa kuajiri askari waliopitia Jeshi hilo pekee na kuwasambaza katika maeneo mbalimbali nchini kote wakichuana na makampuni mengine yaliyoko sasa, lakini bila ya kuathiri utendaji wao. 

``Suma JKT itakuwa kampuni ya ulinzi rasmi kuanzia mwakani na itachukua vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi na si askari wa akiba wa mgambo, mpango huu ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia vijana kama hawa kupata ajira za uhakika baada ya kuhitimu mafunzo haya… na ukweli ni kwamba hatua hii itakuwa ni changamoto kwa vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne kujiunga JKT,``alisema. 

Awali Ofisa Utumishi wa JKT Makao Makuu, Meja Elvis Massawe alipohojiwa kuhusiana na hatua iliyofikiwa hadi sasa na Kitengo hicho cha SUMA alikiri kwamba Ofisi hiyo imeshapokea maombi zaidi ya robo tatu ya vijana waliohitimu katika Jeshi hilo nchi nzima wakisubiri kuajiriwa rasmi. 

Kwa mujibu wa Ofisa huyo ni kwamba Kampuni hiyo mbadala ya ulinzi itachukua askari wa rika mbalimbali bila kujali umri wao na kwamba bado jeshi hilo linapokea maombi ya yawanaotaka kujiunga na kampuni hiyo...

CHANZO: Nipashe

SINA HAKIKA KAMA UMEFANYIKA UTAFITI WA KUTOSHA KUHUSIANA NA MAAMUZI HAYA MAZITO (IT'S PERSONAL KWANI NAMI NI MMOJA KATI YA WALIOPITIA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA MIAKA YA 90).NAAMINI TATIZO KUBWA LINALOKWAZWA KUIREJESHA JKT KUWA KAMA YA ENZI HIZO NI PAMOJA NA MIPANGO DHAIFU ISIYOANGALIA MBALI.SIJUI BABA WA TAIFA HUKO ALIKO AKISIKIA JKT INATAKA KUGEUZWA KAMPUNI YA ULINZI ATAJISIKIAJE LAKINI KWA HAKIKA NI JAMBO LINALOTIA SHAKA SANA HASA IKIAZINGATIWA KWAMBA JESHI SIO TAASISI YA BIASHARA.NI VIGUMU KUTUAMINISHA KWAMBA JKT ITAWEZA KUHIMILI USHINDANI WA KIBIASHARA KATIKA SEKTA YA ULINZI BINAFSI ILHALI UFANISI WA VITENGO VYA KIBIASHARA KATIKA JESHI HILO (KWA MFANO SUMA NA MRADI WA KOKOTO KUNDUCHI) WENYE MUSHKELI.

JKT INGEWEZA KUWA KITUO CHA KUZALISHA AJIRA KWENYE SEKTA YA KILIMO NA HATA UJASIRIAMALI IWAPO KUTAKUWA NA MAANDALIZI SAHIHI.MSISITIZO WA JKT NI KUWAANDAA VIJANA KULITUMIKIA TAIFA LAO KWA UZALENDO NA SIO KWENDA KULINDA MALI ZA WATU (INCLUDING MAFISADI).HATA KAMA WAZO LA BIASHARA YA ULINZI NI ZURI BADO KUNA WASIWASI KUHUSU MASLAHI YA VIJANA HAO,JAMBO AMBALO LISIPOANGALIWA KWA MAKINI LINAWEZA KUZAA MAJAMBAZI BADALA YA WALINZI BINAFSI.ULINZI NI TAALUMA NYETI NA ISIPOTENGENEZEWA SERA MAKINI INAWEZA KUZAA MAYHEM KATIKA JAMII.

24 Dec 2008


SAFARI YA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI BADO NI NDEFU NA YENYE VIKWAZO LUKUKI.KATIBA NA SHERIA ZINAZOWATOFAUTISHA VIONGOZI NA WANANCHI WA KAWAIDA ZINATUMIKA KAMA KINGA DHIDI YA MATENDO AMBAYO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE YANAHUSU UVUNJAJI WA SHERIA.PIA KINGA HIZO ZINAWEZA KUWA KICHOCHEO KIZURI KWA VIONGOZI WAPYA KWANI KAMA WATANGULIZI HAWAKUCHUKULIWA HATUA WALIPOBORONGA (KWA VILE WANA KINGA) THEN KWANINI WALIOPO MADARAKANI WAOGOPE KUBORONGA?HIVI KAMA WENZETU HUKO MAREKANI WANADIRIKI KUMHOJI RAIS MTEULE,IWEJE VIGUMU KWETU KUMHOJI RAIS MSTAAFU?ANYWAY,SOMA STORI HII HAPO CHINI KISHA TUENDELEE NA MJADALA WETU
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, hachunguzwi kwa kosa au tuhuma yoyote ya jinai, imeelezwa. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema uvumi kuwa Rais huyo mstaafu anachunguzwa na vyombo vya dola ikiwamo taasisi hiyo, hauna ukweli wowote. 

Tamko la taasisi hiyo limekuja huku kukiwa na uvumi katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa kiongozi huyo anachunguzwa na Takukuru, kutokana na vitendo vingi vya ufisadi vinavyodaiwa kufanywa wakati wa uongozi wake. 

Tayari mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona waliowahi kushika nyadhifa nyeti katika Serikali ya Awamu ya Tatu ukiwamo uwaziri wa Fedha, wameshafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7. 

Lakini pia baadhi ya watuhumiwa katika kesi za kuchota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT), ambao wamefikishwa mahakamani, wanadaiwa kufanya wizi huo kati ya mwaka 2004 na 2005 kipindi ambacho Rais Mkapa alikuwa madarakani. 

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kipwani alisema jana kuwa, taasisi yake haina uwezo wa kumchunguza kiongozi huyo kutokana na Katiba ya nchi kutotoa nafasi hiyo katika Ibara ya 46 (3) ya Katiba ya Tanzania. Kapwani alieleza kuwa taasisi yake inaheshimu Katiba na ina wajibu wa kuilinda na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba. 

“Takukuru inawafahamisha wananchi kwamba uvumi huu hauna ukweli wowote, hatumchunguzi kiongozi huyu kwa kosa au tuhuma yoyote ya kijinai,” alisema. “Ni kwa msingi huu, Takukuru imeona ni vyema kuwafahamisha wananchi ukweli dhidi ya uvumi huu. 

Tukumbuke wakati wote kwamba taifa letu lina Katiba ya Nchi ambayo imeweka misingi mikuu ya kuendesha nchi yetu, haki na wajibu wa kila Mtanzania. Katiba kama sheria mama imeweka pia mipaka katika kushughulikia mambo mbalimbali ya nchi na kwa mantiki hii, haina budi kuheshimiwa wakati wote.” 

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa “Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.” 

Kapwani alisisitiza kuwa Takukuru itaendelea kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na sheria ya nchi na sio vinginevyo. Katika siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vinaripoti kuwa Mkapa anachunguzwa na Takukuru licha ya kuwa ana kinga ya kutoshitakiwa. 

Vyombo hivyo vimekuwa vikimwandama kwa madai kuwa ufisadi mkubwa umefanyika katika kipindi ambacho alikuwa madarakani. Watu wenye mtazamo huo wamekuwa wanataka kiongozi huyo aondolewe kinga na afikishwe mahakamani kujibu tuhuma mbalimbali za ufisadi. 

Wiki hii, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi katika kikao kijacho cha Bunge kuomba kifungu kinacholinda marais wastaafu kutoshitakiwa kirekebishwe. Mkapa anatajwa katika tuhuma kuhusu ununuzi wa ndege ya Rais, ununuzi wa rada, wizi wa mabilioni ya EPA, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba yenye utata kama ya NetGroup, Alex Stewart na ubinafsishaji wa mgodi wa Kiwira.
CHANZO: Habari Leo

UFAFANUZI HUO WA TAKUKURU HAUWEZI KUZIMA KELELE ZA WANAOTAKA KUMUONA TUHUMA DHIDI YA MKAPA ZINATHIBITISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA.PAMOJA NA KUILINDA NA KUIHESHIMU KATIBA,TAKUKURU INA WAJIBU WA KULINDA NA KUTETEA RASLIMALI ZA WATANZANI ZINAZOFUJWA NA MAFISADI.LAKINI TUKIACHANA NA EXCUSE HIYO YA TAKUKURU (WAMESHATOA LUKUKI) THIS IS A WAKE UP CALL KUHUSU HIZI KINGA DHIDI YA VIONGOZI WASTAAFU (NA PENGINE HATA KWA WALIO MADARAKANI).WAKATI WAZO LA KINGA NI ZURI LIKITUMIWA VIZURI,KWA MFANO DHIDI YA WANAOTAKA KUDHALILISHA VIONGOZI KWA SABABU BINAFSI AU KISASI,WAZO HILO NI HATARI KWA VIONGOZI WALIOZITUMIA VIBAYA OFISI ZAO WALIPOKUWA MADARAKANI.MAHALA PEKEE PANAPOWEZA KUMSAFISHA MKAPA NI MAHAKAMANI NA WALA SIO KWA KAULI ZA KULINDANA KAMA HIZO ZA TAKUKURU.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.