Showing posts with label MKAPA. Show all posts
Showing posts with label MKAPA. Show all posts

30 Jul 2009


Tume huru inayochunguza uhusika wa Uingereza katika vita ya Iraki imetangaza kuwa itamhoji Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.


Atakayenuna na anune,lakini ni dhahiri kuwa Rais wetu mstaafu ( wa awamu ya tatu),Benjamin William Mkapa,amekuwa akiandamwa na tuhuma za ufisadi wakati akiwa jengo takatifu la Ikulu.Hoja kubwa ya wanaomtetea Mkapa ni maneno kama "Mwacheni Mzee wetu apumzike".

Ni wazo zuri kutosumbua wazee wetu,lakini ingeleta maana kama wazee wote,na si Mkapa pekee,wangekumbukwa katika "maombi" hayo kuwa waachwe wapumzike.Mbona "busara" hizo hazijatumika kuwakumbuka wazee (halisi) wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?Wamesumbuliwa,wamezungushwa,wametishiwa FFU,na kufanyiwa kila aina ya vituko...tofauti na Mkapa-ambaye hajaomba atetewe au ajitetee-wastaafu hao wanadai stahili yao halali.Hawakutumia ofisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kununua japo vifusi vya kokoto au kuanzisha chama cha kuweka na kukopa,tofauti na Mkapa ambaye pamoja na mambo mengine anayetuhumiwa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kishkaji na pia kuhusishwa na kuanzisha benki.

Hivi njia bora zaidi ya kumwacha Mkapa apumzike ni kwa wanasiasa kumsafisha katika tuhuma za ufisadi zinazomkabili au kwa mahakama-chombo chenye mamlaka ya kikatiba kutoa haki-kufanya kazi hiyo?Wanasiasa wetu ni wavivu wa kufikiri.Wao ni binadamu,kwa maana hiyo leo wapo kesho hawapo-aidha kiuhai au kimadaraka.Utetezi wao leo unaweza kabisa kuondoka pindi nao watakapoondoka.Uzuri wa taasisi-kama mahakama-ni kwamba inastahili kuwepo kwa muda mrefu au hata milele ikibidi.Na hata ikibadilishwa,misingi yake itaendelea kuwepo.Kwa mantiki hiyo,namna pekee ya "kumwacha Mkapa apumzike" ni kumburuza mahakamani kisha haki itendekee huko.Kupuuza ushauri huu kunaweza kupelekea mzee huyo kuburuzwa kwa nguvu kwenda kujibu tuhuma zake wakati watetezi wake wa sasa hawako madarakani au nao wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kujibu.Hebu chukua mfano mwepesi kama huu.Unadhani Charles Taylor huko aliko anakumbuka flani aliyekuwa anamtetea?Hapo ni kila mtu anabeba mzigo wake.

Sawa,Tanzania sio Uingereza.Na ni kweli kwamba sio kila wafanyalo Waingereza lazima sie pia tulifanye.Lakini mfano wa Blair kufikishwa kwenye tume hiyo ya vita ya Irak inapswa kuwa changamoto nzuri kwa mamlaka zetu kuangalia umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu badala ya kuendekeza ushakaji na kubebana.By the way,si kila mtuhumiwa anayefikishwa kwenye vyombo vya sheria lazima aonekane ana hatia.

Mzee wetu Mkapa hatoweza kupumzika hadi sheria itakapochukua mkondo wake kumsafisha au kumtia hatiani.Kuzembea kufanya hivyo ni kuiachia "mahakama ya umma" (court of public opinion) kumhukumu pasipo kumpatia nafasi ya kujitetea.Na kwa vile mahakama hiyo ya umma haina utaratibu wa kukata rufaa pindi hukumu ikishatolewa,tuhuma dhidi ya Mkapa zitaendelea kuwepo hadi hapo......God knows!Kama wanaomtetea wanampenda kwa dhati (au hata kinafiki) basi ni vema wakamwepusha na hatari ya kuburuzwa mahakamani akiwa na mkongojo wake,say miaka 20 au zaidi kutoka sasa.

Binafsi siamini kuwa wanaomtetea Mkapa wanafanya hivyo kwa vile wanamheshimu sana au wanaamini kuwa tuhuma hizo ni uzushi.Badala yake,wanachelea kwamba wakiruhusu sheria ichukue mkondo wake,kesho wao nao watajikuta wakikabiliwa na hali hiyohiyo kama ya Mkapa.Waadilifu hawaogopi sheria bali wanaiheshimu na kuilinda,lakini wenye mapungufu kwenye maadili yao huiogopa sheria kama kirusi cha mafua ya nguruwe (japo huitumia kuwakandamiza wabaya wao).

Naamini pia kuwa ipo siku Mkapa na watuhumiwa wengine wa ufisadi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.Inaweza kuwa sio kesho au mwaka kesho lakini siku hiyo itafika.Na hapa nazungumzia mahakama za kidunia na sio ile ya kwenye wimbo niupendao wa "na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe mbele ya Mungu,siku hiyo itafika...."

Kuendeleza ushkaji katika mambo yanayopaswa kushughulikiwa kisheria kunaweza pia kusambaza kirusi cha "ah mbona yule fisadi anatetewa na kusafishwa,what's wrong with me kufisadi pia?Si nami nitatetewa kama fisadi X..."Hapo tunafanya reproduction ya ufisadi katika jamii.Yayumkinika kuhisi kuwa kwa namna watuhumiwa wa ufisadi wa EPA,Richmond na maskandali mengine wanavyoendelea kuogopwa,tayari mafisadi hao wameshaambukiza virusi vya ufisadi kwa Watanzania wengine chungu mbovu.Thing is,kama wenye maamuzi wameamua kuhalalisha visivyo halali,then visivyo halali vinageuka kuwa halali.

Na kama kuna mzembe ataona wazo langu la kuchukua hatua dhidi ya Mkapa ni ukosefu wa nidhamu,then they can simply shove it up kunakostahili.

29 Jul 2009

(Picha kwa hisani ya MJENGWA)

Wenzetu wa huku Magharibi wanasifika kwa kuwajali watoto. Licha ya serikali zao kutunga sheria zenye kulenga kuzuia na kukomesha uonevu, unyanyasaji, ukatili na unyama mwingine dhidi ya watoto, kuna mlolongo wa taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zinazojihusisha na suala hilo. Hiyo sio kusema watoto wote wako salama.Ni vigumu katika ubinadamu wetu kufanya kitu kiwe absolutely perfect.

Pamoja na sifa hiyo ni shutuma kwamba upendeleo huo wa hali ya juu kwa watoto unachangia “kuwaharibu” watoto hao. Yayumkinika kusema kwamba miongoni mwa time bombs katika jamii za Magharibi ni watoto wanaodekezwa kupita kiasi. Kama ilivyo kwenye nyanja nyingine, uhuru usipokuwa na mipaka unaweza kupelekea matokeo yasiyopendeza.Hatahivyo, katika hili, uzuri (kuwajali watoto) unazidi ubaya (kuwadekeza).

Ni katika minajili hiyo kunajitokeza hofu kwa baadhi ya watu kutoa misaada kwa watoto kwa kuhofia misaada hiyo inaweza kutafsiriwa tofauti. Hivi karibuni niliona kwenye runinga mtunzi mmoja wa vitabu akilalamikia utaratibu wa kufanyiwa background checks (uchunguzi wa kiusalama,kwa tafsiri isiyo rasmi) kila anapokwenda kwenye shule za watoto kuwasomea vitabu anavyotunga.Mtunzi huyo analalamika kwamba kitendo hicho kinamfanya ajisikie kama mhalifu licha ya ukweli amekuwa akijihusisha na usomaji vitabu kwa watoto kwa miaka kadhaa sasa. Mamlaka husika zinajitetea kwamba utaratibu huo unalenga kuwalinda watoto.

Zamani kidogo niliwahi kukutana na simulizi moja kwamba jamaa flani (mwanaume) alimwona mtoto wa kike anakaribia kuzama kwenye bwawa la kuogelea.Kwa huruma, akajitosa majini kumwokoa mtoto huyo ambaye kwa bahati mbaya chupi yake ilimvuka katika hekaheka hiyo ya kukaribia kuzama.Alipomwokoa na kumpeleka mtoto huyo kwa mama yake akapigwa swali la kutatanisha: “Chupi ya mtoto iko wapi?”Kabla hajatafakari jibu akatandikwa kigongo kingine, “Hivi lini mibaba kama wewe mtaacha kunyemelea watoto wetu kwenye sehemu za kuogelea huku mkisubiri wakumbwe na matatizo kisha muwatomasetomase kwa kisingizio cha kuwaokoa? Hebu nipe chupi ya mwanangu kabla sijakuripoti kwa polisi”.Sijui ungekuwa wewe ungefanyaje!

Tafiti zisizo rasmi zinadokeza kwamba wanaume wengi wamekuwa waoga kusaidia watoto, hususan wa kike, kwa kuhofia kwamba ukarimu na msaada wao usije kuwaingiza matatizoni kwa tuhuma za child molestation.

Nadhani kufikia hapa unajiuliza naelekea wapi! Well, nataka kuzungumzia namna mamlaka zetu zinavyowadekeza mafisadi, lakini nataka kwanza nikupe mifano ya kuiweka akili yako vema kabla hatujaivaa hoja ya ufisadi.Twende kwenye mfano mwingine. Katika miaka ya hivi karibuni baadhi ya watu wanaoporwa na vibaka wameishia kupata vipigo kutoka kwa raia baada ya washirika wa kibaka aliyepora kupiga ukelele wa “mwiz,mwizi...” dhidi ya aliyeporwa.Na kama kanuni za mob justice zilivyozoeleka,hakuna muda wa kuhakiki iwapo aliyepigiwa ukelele ni kibaka halisi au victim.

Back to hoja kuhusu mafisadi. Inaelekea mamlaka husika huko nyumbani zimeamua kuwalinda mafisadi mithili jamii za Magharibi zinavyowalinda watoto dhidi ya suspected/potential/career child molesters.Na anayediriki kupiga kelele dhidi ya mafisadi anakumbana na yaleyale ya anayeporwa na kibaka na kisha kupigiwa ukelele wa “mwizi,mwizi...” na washirika wa kibaka mhusika, na kuishia kupewa kipigo cha haja katika mtindo wa mob justice.

Wachunga kondoo wa Bwana walipobaini kwamba kondoo wao wanakamuliwa hadi damu baada ya maziwa kumalizika miilini mwao wakaamua kuja na kinachoitwa roughly muongozo wa kanisa kuhusu elimu ya uraia hususan uchaguzi wa viongozi. Tuliyekuwa tukimwamini kuwa swahiba wa karibu wa Baba wa Taifa, Kingunge Ngombale Mwiru,akatuthibitishia his true colours kwa kuwakemea wachunga kondoo wa Bwana.Hata kama Kingunge aliasi Nyumba ya Bwana (tukiaminishwa kuwa ni matokeo ya kuamini Ujamaa kupitiliza hadi kuufanya kuwa dini yake) tunapaswa kumshangaa babu huyu ambaye hivi karibuni ameibuka kuwa mtetezi mahiri wa mafisadi. Gazeti la Taifa Letu limemnukuu mtumishi mmoja wa Mungu akim-describe Kingunge kama BABA WA TAIFA WA MAFISADI.

Walioliibia taifa kwa kununua mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa kana kwamba wanachonunua ni kifusi wameishia sio tu kusafishwa bali kufidiwa kwa wizi wao. This is more than crazy! Yaani tunawafidia majambazi!?Tunalipeleka wapi taifa letu? Wakati hatujui hizo milioni kadhaa walizotumia kununulia mgodi huo walizitoa wapi (lakini kwa vile hawakuwa wafanyabiashara basi yayumkinika kuhisi ni fedha za kifisadi),tuna uhakika wa asilimia zaidi ya 1000 kwamba hayo mabilioni watakayolipwa kama “fidia za kutufisadi” ni fedha zangu, zako na zetu walalahoi,walalawima,walala kichwa-chini miguu-juu, na wanyonge wengineo.

Kinachosikitisha ni kwamba kuna waungwana wanalipwa mishahara minono kuzuia upuuzi wa namna hii lakini badala ya kutumia nguvu za kikatiba walizonazo kustopisha ujambazi wa aina hii, wanakuwa bize zaidi na wale wanaowasaidia (waungwana hao) kupiga kelele dhidi ya ufisadi na mafisadi. Kama hufahamu basi naomba nikujulishe kwamba shughuli ya hatari kabisa kwa Mtanzania ni kudiriki kukemea ufisadi.Utaandamwa,utatishwa,utafanywa ujione mhaini,na kufanyiwa kila anachopaswa kufanyiwa Osama bin Laden pindi akikamatwa!Na shughuli yenye uhakika wa kipato, heshima na ulinzi kuliko zote ni ufisadi. Correct me if I’m wrong!

Siku zote nimekuwa nafahamu kwamba kimbelembele changu (according to how those in the know describe it) dhidi ya mafisadi ni kujiingiza kwenye kundi la dead men walking. I know, you’re thinking I’m scared of my own shadow. Kwa vile hapa si mahala mwafaka kutoa ushuhuda wangu, then ni bora tuliache hilo kwa sasa. Hata hivyo, naamini kwa nguvu zote kwamba ukimya sio suluhisho la matatizo yetu. Silence is not an option at all.

Kinachonisikitisha zaidi ni namna baadhi ya wenzetu wenye nguvu, uwezo na sababu wanapokosa nia au ujasiri wa kuendeleza kelele hizi. Inasikitisha zaidi unapoona wasomi wenye uwezo mkubwa wa uchambuzi wanageuka vibaraka wa kusifia pasipo kugeuza upande wa pili wa shilingi kukemea mwenendo tete wa taifa letu.Hate me or love me, ninachofanya ni kinachopaswa kufanywa na kila Mtanzania mwenye uchungu wa dhati wa taifa letu, na anayefahamu kwamba it’s no use crying over spilled milk. Imani kwamba “hata tukipiga kelele hatuwezi kubadili kitu” ni hatari sana kwa vile japo Ukimwi umekuwepo kwa miongo kadhaa sasa bado jamii inaendelea kuhamasisha vita dhidi ya gonjwa hilo hatari.

Kinachopaswa kuwaamsha wanaochelewa kujiunga kwenye mapambano dhidi ya ufisadi ni ukweli ufuatao.Katika utafiti wangu wa kitaaluma unaoelekea ukiongoni,kuna ushahidi wa kutosha unaoonyesha kwamba vurugu za kidini (utafiti wangu unahusu dini) na nyinginezo katika jamii zinachangiwa sana na jamii kukatishwa tamaa na mwenendo wa watawala kushughulikia matatizo yanayozikabili jamii hizo.Na kwa vile watawala wa aina hiyo hufanya kila wawezalo kuzuia “sauti zisizopendeza masikioni mwao”,kimbilio pekee hubaki kwa nyumba za ibada na dini kwa ujumla.

Tatizo ni kwamba masuala ya dini yanaelemea zaidi kwenye hisia kuliko reasoning. Sote tunafahamu, kwa mfano, kuwa piga ua huwezi ku-reason na Mkatoliki kuhusu ishu “ngumu kuelezeka” kama Utatu Mtakatifu, namna Bikira Maria alivyomzaa Yesu pasipo “kukutana” na Josefu, na maswali mengine kama hayo.Na katika masuala ya dini, ambapo mara nyingi emotions tend to come in front of common sense, hakuna taratibu kama za jeshini kwamba amri ya jenerali lazima iheshimiwe na brigedia, au ya kanali iheshimiwe na meja, au ya kapteni kwa lance corporal. Kwenye dini, kauli ya askofu au shehe haina nguvu sana katika kutuliza hamasa za waumini pindi wanapoamua kupambana na mamlaka za kidunia kwa jina la Mungu.

Kinachoniogopesha zaidi ni vuguvugu linaloendelea huko nyumbani ambapo ishu kama ahadi hewa za CCM kuanzisha mahakama ya kadhi,mwongozo wa Kanisa kuhusu uchuguzi wa viongozi waadilifu,mwendelezo wa madai kuwa Wakristo wanapendelewa na Waislam wanaonewa,nk zimetawala anga za habari. Kibaya zaidi, hayo yanatokea katika kipindi ambacho mafisadi wako tayari kufanya lolote alimradi wafanikiwe kuendelea kutufisadi. Yayumkinika kuamini kwamba hawawezi kusita kutumia fursa hii ya “kuwachanganya Watanzania” kwa misingi ya dini na hivyo ku-deflect attention yao (Watanzania) kuhusu ufisadi na mafisadi kwa vile watakuwa bize zaidi kunyoosheana vidole kwa misingi ya udini.

Tukiunyamazia ufisadi, utatumaliza!

It can be done if you play your part.

It’s now or never!

28 Jul 2009

Picha kwa Hisani ya MJENGWA.Uchambuzi zaidi kesho,panapo majaliwa.

21 Apr 2009


SAKATA la mgodi wa Kiwira kufikishwa bungeni, limeendelea kugubikwa na wingu zito, kutokana na ratiba za bunge kutoonyesha kama serikali itatoa ripoti.

Mgodi wa Kiwira, ambao unamuhusisha Rais wa Serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati, Daniel Yona umejaa utata kutokana na madai kuwa kampuni ya Tan Power Resources Limited iliununua kwa Sh70 milioni badala ya thamani yake halisi ya Sh4 bilioni.

Hadi sasa serikali haijatoa ufafanuzi wowote kuhusu utata huo licha ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuahidi katika mkutano wa 13 wa bunge kwamba,ingetoa taarifa bungeni.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alisema tu kwa kifupi "vuta subira".

Iwapo serikali haitatoa ripoti hiyo katika mkutano unaoendelea itakuwa ni mara ya tatu kupigwa tarehe suala hilo.

Katika mkutano wa 13, wakati mjadala wa mgodi wa Kiwira na Meremeta ukiwa umepamba moto, Pinda alisema serikali ilikuwa ikiandaa taarifa lakini akasema ni bora asulubiwe kuliko kutaja wamiliki wa Meremeta kwa maelezo kuwa inahusu usalama wa taifa.

Lakini, hadi mkutano huo unamalizika hakukuwa na ripoti yoyote ya serikali na hata ulivyokuja mkutano wa 14 hakukuwa na ripoti kama hiyo.

Tayari ratiba ya bunge imetoka na kuonyesha kwamba, hoja nzito inayotarajiwa kutikisa bunge hadi sasa ni ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo imepangwa kuwasilishwa bungeni Aprili

24 Dec 2008

SAFARI YA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI BADO NI NDEFU NA YENYE VIKWAZO LUKUKI.KATIBA NA SHERIA ZINAZOWATOFAUTISHA VIONGOZI NA WANANCHI WA KAWAIDA ZINATUMIKA KAMA KINGA DHIDI YA MATENDO AMBAYO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE YANAHUSU UVUNJAJI WA SHERIA.PIA KINGA HIZO ZINAWEZA KUWA KICHOCHEO KIZURI KWA VIONGOZI WAPYA KWANI KAMA WATANGULIZI HAWAKUCHUKULIWA HATUA WALIPOBORONGA (KWA VILE WANA KINGA) THEN KWANINI WALIOPO MADARAKANI WAOGOPE KUBORONGA?HIVI KAMA WENZETU HUKO MAREKANI WANADIRIKI KUMHOJI RAIS MTEULE,IWEJE VIGUMU KWETU KUMHOJI RAIS MSTAAFU?ANYWAY,SOMA STORI HII HAPO CHINI KISHA TUENDELEE NA MJADALA WETU
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, hachunguzwi kwa kosa au tuhuma yoyote ya jinai, imeelezwa. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema uvumi kuwa Rais huyo mstaafu anachunguzwa na vyombo vya dola ikiwamo taasisi hiyo, hauna ukweli wowote. 

Tamko la taasisi hiyo limekuja huku kukiwa na uvumi katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa kiongozi huyo anachunguzwa na Takukuru, kutokana na vitendo vingi vya ufisadi vinavyodaiwa kufanywa wakati wa uongozi wake. 

Tayari mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona waliowahi kushika nyadhifa nyeti katika Serikali ya Awamu ya Tatu ukiwamo uwaziri wa Fedha, wameshafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7. 

Lakini pia baadhi ya watuhumiwa katika kesi za kuchota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT), ambao wamefikishwa mahakamani, wanadaiwa kufanya wizi huo kati ya mwaka 2004 na 2005 kipindi ambacho Rais Mkapa alikuwa madarakani. 

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kipwani alisema jana kuwa, taasisi yake haina uwezo wa kumchunguza kiongozi huyo kutokana na Katiba ya nchi kutotoa nafasi hiyo katika Ibara ya 46 (3) ya Katiba ya Tanzania. Kapwani alieleza kuwa taasisi yake inaheshimu Katiba na ina wajibu wa kuilinda na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba. 

“Takukuru inawafahamisha wananchi kwamba uvumi huu hauna ukweli wowote, hatumchunguzi kiongozi huyu kwa kosa au tuhuma yoyote ya kijinai,” alisema. “Ni kwa msingi huu, Takukuru imeona ni vyema kuwafahamisha wananchi ukweli dhidi ya uvumi huu. 

Tukumbuke wakati wote kwamba taifa letu lina Katiba ya Nchi ambayo imeweka misingi mikuu ya kuendesha nchi yetu, haki na wajibu wa kila Mtanzania. Katiba kama sheria mama imeweka pia mipaka katika kushughulikia mambo mbalimbali ya nchi na kwa mantiki hii, haina budi kuheshimiwa wakati wote.” 

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa “Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.” 

Kapwani alisisitiza kuwa Takukuru itaendelea kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na sheria ya nchi na sio vinginevyo. Katika siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vinaripoti kuwa Mkapa anachunguzwa na Takukuru licha ya kuwa ana kinga ya kutoshitakiwa. 

Vyombo hivyo vimekuwa vikimwandama kwa madai kuwa ufisadi mkubwa umefanyika katika kipindi ambacho alikuwa madarakani. Watu wenye mtazamo huo wamekuwa wanataka kiongozi huyo aondolewe kinga na afikishwe mahakamani kujibu tuhuma mbalimbali za ufisadi. 

Wiki hii, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi katika kikao kijacho cha Bunge kuomba kifungu kinacholinda marais wastaafu kutoshitakiwa kirekebishwe. Mkapa anatajwa katika tuhuma kuhusu ununuzi wa ndege ya Rais, ununuzi wa rada, wizi wa mabilioni ya EPA, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba yenye utata kama ya NetGroup, Alex Stewart na ubinafsishaji wa mgodi wa Kiwira.
CHANZO: Habari Leo

UFAFANUZI HUO WA TAKUKURU HAUWEZI KUZIMA KELELE ZA WANAOTAKA KUMUONA TUHUMA DHIDI YA MKAPA ZINATHIBITISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA.PAMOJA NA KUILINDA NA KUIHESHIMU KATIBA,TAKUKURU INA WAJIBU WA KULINDA NA KUTETEA RASLIMALI ZA WATANZANI ZINAZOFUJWA NA MAFISADI.LAKINI TUKIACHANA NA EXCUSE HIYO YA TAKUKURU (WAMESHATOA LUKUKI) THIS IS A WAKE UP CALL KUHUSU HIZI KINGA DHIDI YA VIONGOZI WASTAAFU (NA PENGINE HATA KWA WALIO MADARAKANI).WAKATI WAZO LA KINGA NI ZURI LIKITUMIWA VIZURI,KWA MFANO DHIDI YA WANAOTAKA KUDHALILISHA VIONGOZI KWA SABABU BINAFSI AU KISASI,WAZO HILO NI HATARI KWA VIONGOZI WALIOZITUMIA VIBAYA OFISI ZAO WALIPOKUWA MADARAKANI.MAHALA PEKEE PANAPOWEZA KUMSAFISHA MKAPA NI MAHAKAMANI NA WALA SIO KWA KAULI ZA KULINDANA KAMA HIZO ZA TAKUKURU.

22 Aug 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum,

Naanza makala yangu kwa kuelezea majonzi makubwa niliyonayo kufuatia kifo cha mwanataaluma maarufu huko nyumbani,Profesa Seith Chachage.Majonzi yangu yanachangiwa na ukweli kwamba mimi ni miongoni mwa wanafunzi wake wa zamani hapo Mlimani.Mungu ndiye mtoaji na yeye ndiye mchukuaji kama Maandiko Matakatifu yanavyosema,lakini pengo aliloliacha msomi huyu aliyebobea ni vigumu kuzibika.Nimepitia tovuti mbalimbali na nimegundua kuwa marehemu alikuwa kipenzi cha wengi hasa wale wenye uchungu na Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla.Kwa tuliomjua Profesa Chachage tutakumbuka jinsi alivyokuwa akichanganya usomi wake na kauli za utani.Yaani ilikuwa vigumu kuchoka kusikia mhadhara wake.Kwa tunavyowajua wasomi wetu ni nadra kumkuta mmoja wao akipenda vitu kama bongofleva,lakini nimesoma kwenye tovuti moja kwamba marehemu alikuwa anapenda muziki wa kizazi kipya na inasemekana aliweza hata kuimba verses za wimbo maarufu wa TID uitwao Zeze.Mungu ailaze ahali pema roho ya marehemu Profesa Chachage,Amen.

Alhamisi ya tarehe 13/06 mwaka nilisoma kwenye tovuti ya gazeti la Uhuru habari iliyonukuu Rais mstaafu Benjamin Mkapa akisema kwamba “katika baadhi ya mashirkika kama ATC serikali iliingia mikataba bila kuwa na tathmini halisi ya faida ambayo ingepata kwenye mashirika hayo.”Hizi si habari njema hasa ikizingatiwa kwamba serikali haitegemei wataalamu wa njozi kujua kama mkataba flani una manufaa au la bali inapaswa kuwatumia wataalam wake kuhakikisha kuwa kinachofanyika sio bahati nasibu ila ni kitu cha maslahi kwa Taifa.Tunaweza kutomlaumu Chifu MangungO alisaini mikataba feki na akina Karl Peters nyakati za ukoloni kwa sababu enzi hizo hakukuwa na wataalamu wa kupitia mikataba na kujua kama ina manufaa au la.Lakini zama hizi hali ni tofauti.Pale serikali inapoona kwamba jambo flani liko nje ya uwezo wake ina uwezo wa kutafuta na kupata uhakiki flani kutoka nje ya nchi.Yaani hapo namaanisha kwamba yapo makampuni kadhaa ya kimataifa ambayo yanaweza kutoa huduma ya ushauri kwa serikali iwapo itaonekana kwamba wataalam wetu wa ndani wameshindwa kazi hiyo.Hivi inawezekanaje mtu akaingia mkataba bila kujua faida yhalisi ya mkataba huo?Utapangishaje nyumba yako kama huna hakika kuwa kwa kufanya hivyo wewe mwenyewe au familia yako mnaweza kuishia kulala gesti hausi?Na je inapobainika kwamba kuna tu flani,kwa sababu anazozijua yeye,alisaini mkataba usio na faida kwa Taifa,tunafanyaje?Suala hapa sio kunyooshena vidole bali ni kuhakikisha kuwa makosa ya aina hiyo hayajirudii.Na njia nyepesi ya kufanya hivyo ni kuwachukulia hatua wale waliofanya makosa hayo-iwe walifanya kwa makusudi,uzembe au kutojali maslahi ya nchi yetu.

Nilishawahi kuandika huko nyuma kwamba kuna watu hawana uchungu na Taifa letu,na hawa ni pamoja na hao wanaosaini mikataba kama ile ya Chifu Mangungu utadhani wakati wanasaini mikataba hiyo walikuwa bwii(wamelewa) au wamesainishwa wakiwa usingizini.Marehemu Chachage na baadhi ya wasomi wengine wa nchi hii walijikuta wakitengeneza maadui kila walipojitahidi kukemea mambo yanayoendana kinyume na maslahi ya Taifa.Kuna watu hawapendi kuambiwa ukweli hata pale wanapoharibu na si ajabu makala hii ikapata upinzani wao.Lakini hiyo haitatuzuwia sie wenye uchungu na nchi yetu kusema yale yanayotupeleka pabaya.

Nimesikia kuna kampuni ya Kisauzi Afrika imepewa haki za utafutaji mafuta huko nyumbani.Pia kuna tetesi kwamba nchi yetu ina utajiri wa Uranium.Mungu akitujalia,siku moja na sisi tutakuwa na sauti kwenye siasa za kimataifa kwa vile mafuta ni silaha,ukiwa nayo lazima utaheshimika.Lakini bila mipango madhubuti utajiri hio unaweza kuwa kama laana kwa Taifa kama letu lililozowea amani.Huko Nigeria kumekuwa na matukio kadhaa ya vurugu ambazo kimsingi zinatokana na ukweli kwamba wenye ardhi (wananchi) wanaishia kuona tu mabomba ya mafuta na magari ya thamani kwa wale wanaowatumikia wenye makampuni ya mafuta ya kutoka nje,huku walalahoi wakizidi kuwa masikini.Mwanafalsafa Karl Marx aliwahi kusema kuwa masikini hana cha kupoteza anapoamua kupigania haki yake.Watu hawawezi kuendelea kuwa kimya wakati utajiri wao wa asili kwenye nchi yao unawanufaisha wachache kutoka nje na wapambe wao wanaosaini mikataba hewa.

Naomba ieleweke kwamba sizilaumu serikali za awamu zilizotangulia kuwa mikataba yote zilizoingia ilikuwa bomu.Kilio changu hapa ni kwenye hiyo mikataba ya iliyosainiwa ndotoni.Nafahamu kwamba wataalamu wazalendo wanatoa ushauri mzuri tu kabla ya mikataba kusainiwa lakini tatizo linakuja pale maslahi binafsi yanapowekwa mbele ya maslahi ya Taifa.Kwa kuwa mtu ana mamlaka ya kupuuza ushauri wa kitaalamu basi anatumia fursa hiyo kujifanya madudu kana kwamba madhara ya anachokifanya hayatamgusa kwa namna flani.

Naamini serikali ya Awamu ya Nne haitawalea wazembe wanaotaka kutulostisha.Narudia kusema kwamba sisi sio masikini wa namna tulivyo kwa sababu tuna raslimali za kutosha ambazo zinaweza kabisa kutuweka pazuri.Tunachopaswa kuelewa ni kwamba miaka 25 au 50 ijayo vizazi vya wakati huo vinaweza kutushangaa sana pale vitakapokuta kila kitu kimeuzwa na faida ya mauzo hayo haionekani.Inaweza kuwa vigumu sana kwa walimu wa somo la Historia wa wakati huo kuwaelewesha wanafunzi wao kuwa tofauti na mikataba feki ya kina Karl Peters na baadhi ya machifu wetu,mikataba iliyobomoa nchi yao ilifanywa na Watanzania haikuwa ya kilaghai bali ni sababu ya kitu kidogo (sijui wakati huo watakuwa wanatumia msamiati gani kumaanisha rushwa),

Alamsiki

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.