22 Apr 2009


Na Waandishi Wetu

VURUGU kubwa zimeibuka katika Makao Makuu ya taasisi ya Development of Entrepreneurship for Community Initiative (Deci), wanachama wake walipokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi hizo kuorodhoresha majina yao kwa ajili ya kung’oa mbegu walizopanda.

Kati msongamano wa wanachama waliokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi za taasisi hiyo jana; baadhi ya watu walianguka chini, kumi kati yao walipoteza fahamu na saba walinusurika kufa baada ya kutumbukia kwenye kisima cha maji kilichopo katika eneo hilo.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa watu hao walianza kusukumana kwenye lango la kuingilia ndani ya ofisi hizo, muda mfupi baada ya kufunguliwa na kukaidi amri ya kufuata foleni iliyotolewa na muhudumu wa Deci.

Walisema baada ya wanachama hao kukaidi amri hiyo, walijazana kwenye mlango wa kuingilia ndani ya ofisi hizo na ndipo walinzi wa kampuni binafsi wanaolinda ofisi hizo walitumia nguvu kuwarudisha nyuma wanachama hao bila mafanikio.

“Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya walifunga mlango wa kuingilia na shughuli za taasisi hiyo kusimamishwa kwa muda,” alisema mmoja wa mashuhuda.

Alisema ofisi zilisitishwa kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:05 zilipofunguliwa baada ya kuwasili kwa askari polisi kutoka Kituo cha Magomeni.

Polisi hao wakiwa na silaha waliwasili kwenye ofisi hizo na kuingia ndani kupitia katika mlango uliokuwa umezingirwa na umati wa watu, ili waweze kuwalazimisha kufuata foleni.

Hata hivyo, zoezi hilo lilizidi kuwa gumu bada ya watu hao kuendelea kusukumana mlangoni hapo licha ya polisi kuingia ndani ya ofisi hizo na wahudumu wa Deci kutangaza kuwa wanachama waliopanda mbegu zao Machi mosi hadi 10, mwaka huu kuwa ndio wanatakiwa kuingia kupata huduma.

Kutokana na vurugu kuongezeka, ofisi hizo zilifungwa tena saa 7:45 mchana na kuwataka wanachama waondoke hadi kesho saa 2:00 asubuhi.

Hata hivyo muhudumu aliyekuwa anatoa taarifa kwa wanachama hao aliwataka kutofuata ratiba iliyoandaliwa na taasisi hiyo awali ya kuwahudumia waliopanda mbegu zao Februari. Badala yake aliwataka waliopanda mbegu zao kuanzia Machi mosi hadi 5, mwaka huu ndio watatakiwa kwenda kujiorodhesha leo.

Mmoja wa wanachama waliotumbikia kwenye kisima, Getruda Moto aliliambia Mwananchi kuwa akiwa na wenzake, alishituka baada ya mbao alizokuwa amesimamia juu yake zikizama.

“Mimi nilikuwa nimesimama pembeni, lakini kuna watu walikuja na kukanyaga mbao iliyogusa kwenye mgomba, ndipo ikatengua mbao zilizoegeshwa kwenye kisima hiki na mimi pamoja na wenzangu kutumbukia,” alisema Moto.

Hata hivyo alisema mara baada ya kuokolewa alifarijiwa na wanachama wenzake, wakimtaka asiilaumu Deci, bali serikali ambayo ndiyo chanzo cha yote hayo.

“Usiilaumu Deci hii haikudhamiria kufanya haya bali ni serikali iliyoifunga na kusababisha yote haya” alisema mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana.


Mchungaji wa Kanisa la Sharoom Gospel la Yombo Buza, Kamiliusi Macha ambaye ni mmoja wa wanachama wa Deci aliilalamikia serikali kwa kutoweka ulinzi wa kutosha katika eneo hilo linalokusanya umati mkubwa wa watu.

“Hapa walitakiwa kuwepo askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU), ndiyo wangeweza kuwalazimisha wanachi kupanga foleni na hali hii ya wanachama ya kujazana mlangoni isingekuwapo,” alisema Macha.

Akizungumzia kampuni hiyo alisema kwa sasa inakatisha tamaa kwani taarifa zake ni za kutatanisha. Ofisi hizo pia ziligubikwa na kila aina ya vituko baada ya vibaka kuibuka na kuwaibia watu simu za mkononi pamoja na risiti zao za Deci.

Mwanachama mmoja aliporwa risiti zote za Deci zenye thamani ya Sh 200,000 akiwa nje ya makao makuu ya ofisi hizo. Mwanachama huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema aliporwa karatasi hizo alizokuwa amezishika mkononi na kuachiwa karatasi ya ratiba.

Alisema mara baada ya kuporwa stakabadhi hizo alikwenda kituo cha polisi cha Urafiki kutoa taarifa, lakini alipofika huko aliambiwa arudi katika ofisi za Deci ambako angepewa barua ya utambulisho.

Hata hivyo juhudi za kupata barua hiyo zilishindikana baada ya watendaji wa Deci kukataa kufungua mlango wa ofisi hizo kwa madai kuwa muda wa kufanya kazi ulikuwa umemalizika.

“Nifungulieni mimi nimeibiwa naomba mnisaidie, nimeshaenda polisi nimeambiwa nije huku mniandikie barua,” alilalamika bila mafanikio baada ya sauti kutoka ndani ya ofisi hizo ikidai muda wa kazi umeisha.

Mwenyekiti wa kamati ya dharura ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge alifika katika ofisi hizo na kuwatangazia wanachama juu ya mkutano wao utakofanyika Jumamosi wiki hii kuanzia saa 7:00 katika viwanja vya Jangwani na kuwataka wanachama wote kufika bila kukosa.

Kabla ya kufika katika ofisi hizo mkutano aliokuwa ameuitisha na waandishi wa habari Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, ulivunjwa na maofisa wa maelezo kwa kushirikiana na maafisa usalama, baada ya mchungaji huyo kutoa kauli iliyodaiwa kumdhihaki Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Mkutano huo ulivunjwa baada ya mchungaji huyo kusema kuwa kauli ya Waziri Mkuu kuwa Deci ina Sh1.8 bilioni katika akaunti yake badala ya 54bilioni zilizotajwa na viongozi wa taasisi hiyo, ni ya kuropoka na kupotosha umma.

Kauli hiyo iliwaudhi maofisa wa maelezo hivyo kumtaka aache kuongea habari za viongozi wa taasisi hiyo, hata wa serikali badala yake kusoma maandishi aliyoyaandika katika karatasi yake.

“Wewe siyo kiongozi wa Deci hivyo unatakiwa kuzungumzia masuala yako binafsi kwa kuwa ni mwanachama wa taasisi hiyo, si kumdhihaki na kumtukana Waziri Mkuu,” alisikika kiongozi mmoja wa maelezo na kuamsha kelele kutoka kwa waandishi waliokuwepo katika mkutano huo.

Hata hivyo mchungaji huyo aliitaka serikali kupitia Wizara ya Fedha kuwajengea wananchi mazingira ya kupata fedha zao.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alimtaka mchungaji huyo kufuata utaratibu uliowekwa na jeshi hilo kabla ya kufanya mkutano wake Jumamosi ijayo kwa kuwa kufanya hivyo bila kibali ni kukiuka Sheria namba 322 ya Jeshi la Polisi iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Katika tawi la Deci lililopo maeneo ya Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam umati mkubwa wa wanachama ulikusanyika huku ukiulalamikia utaratibu wa kujiandikisha majina na kuacha risiti mpaka siku ya kurudishiwa fedha zao.

Mwananchi lilishuhudia washiriki hao wakizozana na baadhi ya viongozi wa tawi hilo na kuwalazimu kubadili uamuzi huo kwa kubandika tangazo ambalo lilikuwa linaonyesha utaratibu wa malipo kwa waliopanda mbegu kuanzia Oktoba mwaka jana mpaka Aprili, mwaka huu.

“Hatutaki kabisa kuacha risiti hapa kwani ikifika siku ya malipo mtaturuka. Tunasema hatutaki, nyie tuambieni siku ya kuja kuchukua fedha zetu, tutakuja na risiti zetu,” walisema washiriki hao.

Wakati hayo yakiendelea Deci katika taasisi nyingine ya Malingumu Investment iliyopo maeneo ya Ukonga karibia na lilipo tawi la Deci wanachama wake walionekana wakiendelea kupanda kama kawaida.

Mwananchi lilifika eneo hilo saa tisa alasiri ilikuta wanachama wa taasisi hiyo wakigombania kuingia ndani, huku wakiwa wanazuiwa na walinzi wa kampuni binafsi waliokuwa wakilinda eneo hilo.

CHANZO: Mwananchi
Baadhi ya washiriki hao walikuwa na nia ya kung’oa mbegu zao kwa kuhofia taasisi hiyo kufungiwa kama ilivyofungiwa Deci.



KWA MFANO KATINA GAZETI LA SANI KUNA HABARI KWAMBA MWANANCHI MMOJA ALIYEPANDA MBEGU ZENYE THAMANI YA SHS MILIONI 20 "AMEPARALAIZI" (AMEPOOZA)UPANDE MMOJA WA MWILI WAKE BAADA YA HABARI KUWA HUENDA MBEGU YAKE HIYO IKAWA "IMEOZA ARDHINI".....KIBAYA ZAIDI NI KWAMBA MBEGU HIZO (SHS MILIONI 20) ZILIKUWA NI FEDHA ZA URITHI WA FAMILIA,NA "MPANDA MBEGU" HUYU ALITUMIA TU NAFASI YAKE KAMA MWEKA HAZINA WA FUNGU HILO AKIAMINI MBEGU ZINGEZAA FAIDA NA KISHA ANGEREJESHA KIWANGO HICHO......




Captured Somali pirates,like Abduwali Abdukhadir Muse (pictured above,smiling as he arrives on the U.S soil) are most likely to seek for asylum in the U.S. upon completion of their jail terms.Compared to the current situation in Somalia,life in a U.S. prison could most probably be perceived as a once-in-lifetime-luxury many Somalis could only imagine.Couldn't this encourage even more pirate attacks in the future?



May be that's why the captured pirate is all smiles....

1 When presidents get invited to the annual Gridiron Dinner for a night of political skits among the Washington press corps, they always go. Not this one, who became the first sitting President politely to decline.

2 We have had lots of canine companions on the rugs of the Oval Office, but Obama's is the first first whose name, Bo, is also his master's initials. Better still, Portuguese water dogs come with fine Democrat credentials – Senator Ted Kennedy has litters of them

3 Americans have become accustomed to knowing that the so-called "enemy combatants" were being held at a safe distance – at Guantanamo Bay. But BO comes into office and instantly declares he will close it within a year.

4 Never mind the Bush policy of hostility to Iran, BO has been making tentative overtures, asking Tehran to cooperate on Afghanistan and edging towards face-to-face talks on its nuclear programme without preconditions.

5 In his first formal press conference, BO took a question from a correspondent of The Huffington Post, the political blog site. In this White House, old journalism must compete with new journalism.

6 As soon as the first cherry buds were bursting in Washington, Michelle Obama, accompanied by local school children, was breaking sod for the First Family's organic vegetable patch.

7 America is no longer shrugging its shoulders at the drug cartel violence shaking Mexico. BO and Secretary of State Hillary Clinton acknowledged that the US is fueling the problem, supplying guns and consuming the drugs.

8 The Beast. The new first limousine – a Cadillac with more armour than your average tank and bullet-proof windows – has already prowled the streets of London, Strasbourg, Prague and Istanbul. And Pennsylvania Avenue on Inauguration Day.

9 Rush Limbaugh is the conservative blowhard on the radio who millions of Americans long ago learned to love or hate. But now his visibility, ratings and influence have soared. Some even tag him the unofficial head of the Republican opposition.

10 When Nato fed live footage of Barack and Michelle arriving for a dinner hosted by Angela Merkel into a packed press room, scores of normally cynical reporters rose to their feet to clap...CONTINUE

SOURCE: The Independent


21 Apr 2009

Shule ya Sekondari ya kutwa ya Marambo yenye wanafunzi 253 ya kidato cha Kwanza hadi cha Nne , iliyopo Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi ina mwalimu mmoja. Mkuu wa shule hiyo, Saidi Mbutuka ndiye pekee aliye shuleni hapo anayelazimika kushika nyadhifa zote.

Mbutuka aliliambia gazeti hili kuwa hali hiyo inatishia mustakabali wa elimu kwa wanafunzi shuleni hapo kwa kukosa elimu inayostahili. ''Mimi ndiye mkuu wa shule, ndiye mwalimu wa zamu, mwalimu wa taaluma, kila siku za kazi natakiwa kuingia katika madarasa yote manne, kwa siku ninakuwa na vipindi zaidi ya 10'', alisema.

Aliongeza, ''kwa hali hiyo hata kama ningekuwa mwalimu mzuri, kuna kila sababu ya kutilia mashaka na ubora wa elimu, mimi ni mwalimu wa masomo ya Sanaa, lakini nalazimika kufundisha Sayansi,'' alisema Mbutuka.

Alifafanua kuwa tatizo hilo limejitokeza mwaka huu baada ya walimu wanne waliokuwa shuleni hapo kwenda kusoma. 'Tunao wanafunzi wa kidato cha Nne ambao wanahitaji wafanye mtihani wa kuhitimu elimu yao, hivi tujiulize nini watavuna wanafunzi hawa kwa kufundishwa na mwalimu mmoja ambaye pia ndiyo nguzo kwa wanafunzi wa vidato vingine,'' alihoji.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo, akiondoka kwenda mjini hulazimika kuwatawanya wanafunzi au kuwaacha chini ya uangalizi wa wanafunzi wenzao ambao ni viongozi.
Mbutuka alibainisha kuwa pamoja na tatizo hilo shule hiyo inakabiliwa na tatizo sugu la mdondoko wa wanafunzi unaotokana na wanafunzi hao kukimbilia katika machimbo ya madini ya Miruwi, Nachianji na Mituguru yaliyopo jirani na shule hiyo.

Alisema mwaka 2006, wanafunzi 53 waliripoti shuleni hapo hata hivyo waliobakia ni 31, wakati mwaka 2007 wanafunzi walioripoti walikuwa 111 waliopo 73. Mwaka 2008 wanafunzi 80 waliripoti na waliopo ni 50. Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Nachingwea, Bakari Mussa, alikiri kuwapo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa halmashauri inashindwa kuwahamishia walimu shuleni hapo kutoka shule zingine ili kupunguza ukubwa wa tatizo kutokana na kukosa fedha za uhamisho.

''Kuna waraka wa serikali unaomtaka mwajiri kutomhamisha mtumishi yeyote bila kumlipa stahiki zake, kwa sababu halmashauri haina pesa tunashindwa namna ya kuiisaidia shule hiyo, lakini uwapo wa tatizo hilo sote tunautambua'' alisema Mussa.

CHANZO:Habarileo


HALAFU 2010 CCM WATAKUJA KUTUIMBIA MAFANIKIO KATIKA SEKTA YA ELIMU,NA KUDAI WAPEWE TENA MUDA WA KUIPELEKA NCHI YETU WANAKUJUA WAO.MIAKA ZAIDI YA 40 BAADA YA UHURU BADO TUNAKUWA NA SHULE YENYE MWALIMU MMOJA?WATETEZI WATASEMA SIE MASIKINI.MASIKINI GANI ANAYEWALIPA WABUNGE ZAIDI YA 300 SHS MILIONI 7 KWA MWEZI?MASIKINI GANI ALIEIBIWA BILIONI 40 NA KAGODA LAKINI ANAMWONEA AIBU HATA KUMTAJA HADHARANI?






Baraza la Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) limepitisha uamuzi wa kuishirikisha Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhakiki vyeti vya wote wanaoomba kuwania nafasi za kisiasa ili sifa zao kielimu zitambulike.

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya, aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, TCU imewasiliana na NEC kwa barua, ili utaratibu huo uanze kutumika katika uchaguzi mkuu ujao mwakani.

Nkunya alitoa taarifa hiyo wakati akizungumzia maonyesho ya vyuo vikuu yaliyoandaliwa na TCU yatakayoanza kesho hadi Aprili 24, mwaka huu. “Baraza letu limepitisha uamuzi ili watu wanaotaka kugombea nafasi za kisiasa, vyeti vyao vihakikiwe, ili akipita sifa ijulikane rasmi kama ni daktari basi awe daktari na si daktari feki,” alisema Profesa Nkunya.

Hatua hiyo ya tume inatokana na kilichoelezwa na Nkunya kuwa ni kukithiri kwa vyuo na vyeti bandia nchini, jambo ambalo alisema wamejipanga kulivalia njuga kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha Tanzania haiangamii kitaalamu na kitaaluma.

Alisema orodha ya vyuo visivyotambulika vya nje ambavyo Watanzania wengi wakiwamo mawaziri na wabunge wamesoma, ni ya kweli na kwamba kama kuna mtu anahisi kuonewa ruhusa kwenda mahakamani...ENDELEA

CHANZO: Habarileo.

TAMKO ZURI LAKINI LINALOSTAHILI UMAKINI KATIKA KULIAMINI.HAWA TCU WAKATI WANAZUNGUMZIA UCHAGUZI WA 2010,WANATAKA KUTUMBIA HAWAKUWEPO 2005?AU WATAPATA NGUVU HIYO 2010?JE KAMA SASA WANASHINDWA KUWASHUGHULIKIA HAO "MADAKTARI WA FALSAFA" WALIOKWAA SHAHADA ZAO MTANDAONI TUTAAMINI VIPI KUWA WATAWEZA HIYO 2010?
TATIZO LA NCHI YETU SIO SHERIA,KWANI ZIMEKUWEPO TANGU TUNAKABIDHIWA UHURU NA MKOLONI.TATIZO NI UTEKELEZAJI WA SHERIA HIZO.KUNA MBUNGE ALIKUWA NA TUHUMA ZA KUFOJI ELIMU (SIO YA CHUO KIKUU) BALI YA SEKONDARI.CHA AJABU HADI LEO "ANAPETA".JE HII HAILETI USHAWISHI KWA VIHIYO WENGINE KUJARIBU BAHATI ZAO?

TATIZO LA PILI LA NCHI YETU SIO SHERIA BALI UTEKELEZAJI WAKE UNAOELEMEA ZAIDI AINA YA MKOSAJI.YALEYALE YA ANAEIBA KUKU KWA NJAA KUITWA MWIZI LAKINI ANAYEFUJA MABILIONI ANAOTWA M-BADHIRIFU (NA SANASANA BADALA YA KWENDA JELA ATAHAMISHWA KITUO CHA KAZI).KUNA SHERIA KWA AJILI YA VIGOGO (KAMA AKINA CHEYO WANAOUA KWENYE AJALI LAKINI WANAUNDIWA TUME BADALA YA SHERIA KUCHUKUA MKONDO WAKE) NA SHERIA NYINGINE NI KWA AJILI YA MAKABWELA.


SAKATA la mgodi wa Kiwira kufikishwa bungeni, limeendelea kugubikwa na wingu zito, kutokana na ratiba za bunge kutoonyesha kama serikali itatoa ripoti.

Mgodi wa Kiwira, ambao unamuhusisha Rais wa Serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati, Daniel Yona umejaa utata kutokana na madai kuwa kampuni ya Tan Power Resources Limited iliununua kwa Sh70 milioni badala ya thamani yake halisi ya Sh4 bilioni.

Hadi sasa serikali haijatoa ufafanuzi wowote kuhusu utata huo licha ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuahidi katika mkutano wa 13 wa bunge kwamba,ingetoa taarifa bungeni.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alisema tu kwa kifupi "vuta subira".

Iwapo serikali haitatoa ripoti hiyo katika mkutano unaoendelea itakuwa ni mara ya tatu kupigwa tarehe suala hilo.

Katika mkutano wa 13, wakati mjadala wa mgodi wa Kiwira na Meremeta ukiwa umepamba moto, Pinda alisema serikali ilikuwa ikiandaa taarifa lakini akasema ni bora asulubiwe kuliko kutaja wamiliki wa Meremeta kwa maelezo kuwa inahusu usalama wa taifa.

Lakini, hadi mkutano huo unamalizika hakukuwa na ripoti yoyote ya serikali na hata ulivyokuja mkutano wa 14 hakukuwa na ripoti kama hiyo.

Tayari ratiba ya bunge imetoka na kuonyesha kwamba, hoja nzito inayotarajiwa kutikisa bunge hadi sasa ni ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo imepangwa kuwasilishwa bungeni Aprili

20 Apr 2009



Mie adhabu zangu HUKO O'level zilikuwa kwenye namba (HISABATI) ambayo kwa miujiza mikubwa nillibuka na D (japo ilikuwa dhaifu mno,na chupchup iwe F) na FIZIKIA ambayo sikuwa na ujanja nayo na nikaambulia F.

18 Apr 2009


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.