11 May 2009


AH,HAPA SIJUI NISEMEJE.HEBU SOMA KWANZA HABARI KAMILI HAPA CHINI KISHA TUJADILI.

Kompyuta za IGP, Mkemia Mkuu zaibwa
• Ni katika mazingira ya kutatanisha

na Deogratius Temba

WAKATI kesi ya watuhumiwa 11, walioiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ikiendelea imebainika Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, naye ameibiwa kompyuta ndogo (Laptop).

Wiki mbili baada ya tukio la wizi wa kompyuta za IGP Mwema, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, nayo iliibiwa kompyuta ya mezani ambayo inasadikika ilikuwa na kumbukumbu nyingi ambazo hazijabainishwa zinahusiana na mambo gani.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili, kwa wiki kadhaa sasa umebaini kuwa kumekuwapo kwa wasiwasi mkubwa wa kuibwa kwa nyaraka na vifaa mbalimbali katika ofisi za viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG).

Chanzo kimoja kimelidokeza Tanzania Daima Jumapili, uchunguzi wa wizi wa kompyuta hizo mpaka sasa unaendelea ili kuwabaini wahalifu waliotenda tukio hilo na kujua walikuwa na lengo gani.

Chanzo hicho kimebainisha kuwa kikosi maalum kimeundwa kufuatilia wizi huo ambao umeonekana kuanza kushamiri katika ofisi nyeti za serikali hasa katika kipindi hiki ambacho kumekuwa na tuhuma nyingi za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yanayofanywa na viongozi.

Taarifa za ndani zinadai kuwa kompyuta ya IGP iliibwa mezani kwake majira ya mchana siku ya Ijumaa wakati mkuu huyo akiwa amekwenda msikitini kuswali. Katika meza hiyo kulikuwapo na simu za mkononi na kiasi cha fedha kinachodaiwa kuwa sh milioni saba, lakini ni kompyuta pekee ndiyo iliyoibwa.

Habari zaidi zinabainisha kuwa IGP aliporudi alishangaa kutoikuta kompyuta hiyo ilhali simu na fedha vilikuwapo kama alivyoviacha, baada ya kubaini wizi huo zilichukuliwa alama maalumu za vidole zikaonekana ni za mlinzi wake wa karibu (Board guard), ambaye inadaiwa huwa na kawaida ya kuingia mara kwa mara katika ofisi pasi na kutiliwa shaka.

Chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa uchunguzi ulipofanyika ndani ya jeshi la polisi ilibainika kuwa kuna afisa wa jeshi hilo, mwenye cheo cha mkaguzi, ndiye aliyeichukua kompyuta hiyo, ambaye hadi sasa anahojiwa ili kulisaidia jeshi hilo liweze kupata chanzo cha uhalifu huo.

Aidha, taarifa zinasema kuwa aliyeichukua kompyuta hiyo, inadaiwa, amelipwa sh mil. 10 kama ujira wake kwa kazi hiyo. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alipoulizwa juu ya hatua ambazo jeshi hilo linazichukua dhidi ya wizi huo ambao unaonekana wazi kulenga kuiba nyaraka muhimu za serikali, alisema huo ni wizi kama mwingine kwani wezi hao hawakulenga kuiba kompyuta hizo kwa lengo maalumu.

“ Siyo kwamba wizi haufanyiki, unafanyika sana; mara hii umetokea katika ofisi nyeti inayomhusisha mkuu wa jeshi la polisi, wizi huo umefanyika tu kama unavyoweza kufanyika nyumbani kwako, haukulenga ofisi hizi tu,” alisema DCI Manumba.

Pamoja na kusema hivyo, alilithibitishia Tanzania Daima Jumapili kuwa hatua za uchunguzi zinaendelea ili kuwabaini wahalifu hao ambao wamefikia hatua mbaya.

“Tanzania hatuna wizi wa kulenga ofisi maalumu za serikali, ndiyo maana unapotokea unawashangaza watu wengi lakini tumejipanga vilivyo katika uchunguzi kuhakikisha tunawakamata wale wote waliohusika,” alisema Manumba na kuongeza:

“Nakwambia ukweli, wewe umekuja kuniuliza kwa sababu wizi umetokea katika ofisi hii, lakini matukio kama haya yanatokea pia katika nyumba za watu binafsi, hata siwezi kukuhesabia idadi ya kesi hizo, tusiwashtue watu waamini kuwa ulilengwa kwa kazi hiyo.”

Manumba alizidi kusisitiza kuwa wizi upo dunia nzima na wanaweza kuiba mahali popote kama wataona kuna kitu, lakini hakuna wizi uliopangwa kulenga katika ofisi hizo za IGP, DPP , au kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Taarifa zimeeleza kuwa kompyuta iliyoibwa katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilikuwa kubwa ya mezani (PC), ambayo ilichukuliwa kupitia dirishani katika mazingira ya kutatanisha wakati milango ikiwa imefungwa.

Chanzo chetu kutoka ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, kimeeleza kuwa kompyuta hiyo ilikuwa ikitumika ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu, ambapo bado haijajulikana na nyaraka gani muhimu zilikuwa zimehifadhiwa humo.

“Ni kweli kompyuta iliibwa hapa, milango imefungwa tumefika tukaelezwa kuwa kompyuta ya msaidizi wa bosi wetu haionekani wakati milango ilikuwa imefungwa,” alisema mmoja wa watumishi wa ofisi hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Aidha kuhusu tukio hilo lililotokea katika ofisi hizo zilizoko karibu na Taasisi ya Saratani, Ocean Road, imeelezwa kuwa bado uchunguzi unaendelea ili kubaini mtu aliyehusika kuiba kompyuta hiyo kama ni mmoja wa wafanyakazi au la.

Kutokea kwa wizi huo kunawafanya baadhi ya watu kuwa na wasiwasi kuwa kuna njama zimepangwa na baadhi ya watu kupoteza vielelezo au ushahidi wa tuhuma au kesi mbalimbali zinazowakabili.

Wasiwasi huo umechangiwa zaidi na matukio ya hivi karibuni ya kupandishwa mahakamani kwa baadhi ya vigogo wa serikali, wafanyabiashara na watu binafsi kwa wizi au matumizi mabaya ya madaraka.

Mpaka sasa watu 11 wameshapandishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam kujibu tuhuma za kuiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugeni wa Mashtaka Nchini (DPP).

JANA NILIWEKA HABARI YA KIBAKA ALIYEFANIKIWA KUIBA UA IKULU.JUZIJUZI,USTAADH MMOJA ALIDIRIKI KUMZABA KIBAO RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI.SIKU KADHAA ZILIZOPITA,TULISIKIA KUWA DPP AMEIBIWA LAPTOP YAKE.LEO TENA TUNASIKIA IGP NAE KALAMBWA KOMPYUTA.MATUKIO YOTE HAYA YANAASHIRIA KWAMBA TUNARUKARUKA KWENYE UTANDO WA BUIBUI ILHALI CHINI YA UTANDO HUO KUNA BWAWA LA TINDIKALI.

SWALI LA MSINGI KUJIULIZA KUHUSIANA NA WIZI HUO WA LAPTOP YA IGP NI KWANINI HABARI HIYO IMEVUJA KIRAHISI HIVYO?NI HABARI YA FEDHEHA AMBAYO KWA MAZOWEA TULIYONAYO YA "WAKUBWA HUWA HAWAKOSEI" INGEDHIBITIWA KWA NGUVU ZOTE.NIITE CONSPIRANCY THEORIST,LAKINI I STRONGLY SMELL SOMETHING FISHY.IT'S EITHER KUNA MTU (HUYO ANAYEDAIWA KULIPA MILIONI 10 BAADA YA KUFANIKIWA "WIZI" HUO) ANAYETAFUTWA ILI AWE IMPLICATED AU KUNA EVIDENCE INAPOTEZWA KWA EXCUSE YA "ILIKUWA NDANI YA LAPTOP ILIYOIBIWA."KATIKA ZAMA HIZI ZA UFISADI,LOLOTE KATI YA HIZO CONSPIRANCY THEORIES ZANGU INAWEZA KUWA SAHIHI.


Na Frederick Katulanda, Busanda

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja jana alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzongwa na kundi la wananchi waliomuhoji juu ya ahadi zake za umeme alipowasili katika mji wa Katoro wilayani Geita.

Tukio hilo mithili ya mdahalo lilitokea kati ya majira ya ya saa 9:30 hadi saa 10:15 muda mfupi tu baada ya Ngeleja kuwasili Busanda akitokea Mwanza.

Maswali yalianza baada ya Waziri Ngeleja kusalimiana na wananchi hao na akajibiwa kwa kuonyeshwa alama za vidole viwili.

Hali hiyo ilimfanya waziri huyo kuwauliza wananchi hao sababu za kuichukia CCM wakati imekuwa ikijitahidi kuwaletea maendeleo na ndipo walipoanza kumuuliza maswali huku akiyajibu wakati fulani kugeuka mabishano.

"Hatuwezi kuwashangilia nyinyi... mmetuahidi umeme siku nyingi na hatuuoni, leo mnakuja kutuambia nini. Alikuja hapa sijui (Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam) Malima akasema umeme utakuja, lakini wapi hatujaona lolote mpaka leo," alisema mwananchi mmoja.

Ngeleja alipotaka kujibu, mwananchi mwingine alidakia kusema: "Hata kwenye machimbo mmekuwa mkitunyang'anya maeneo yetu na kuwapa wawekezaji. Sisi mnatuona hatufai kama vile ni wakimbizi ndani ya nchi yetu."

Ngeleja alilazimika kuwatuliza na kuwaomba wapunguze maswali ili ajibu swali moja baada ya jingine, lakini kila mtu akataka kumuuliza swali na kukawa na msuguano kati yake na wananchi.

Alianza kujibu kwa kusema kuwa serikali ipo mbioni na kwamba kinachofanyika sasa ni kufuata taratibu kwa sababu mchakato wa suala hilo hauwezi kumalizika siku moja, hivyo akawaomba wawe watulivu wakati mchakato ukiendelea.

Ngeleja alidai kuwa suala lao kuhusu umeme liko katika hatua ya kuridhisha na kwamba wanapaswa kutambua utaratibu wa kushughulikia miradi ya serikali umekuwa ukifanyika kwa hatua.

Majibu hayo yalipingwa na wananchi ambao walimwambia wamekuwa wakidanganywa kama watoto kwa sababu ya kutaka kura na wakishapata, hutoweka.

"Sikiliza basi nikujibu, wewe naona umetanguliza ushabiki tuu. Naomba unisikilize. Ni kweli tulipowaahidi umeme tulidhani mchakato ungekamilika mapema, lakini kuna mambo yametukwamisha, tunaomba mtuvumulie," alisema huku wananchi hao wakiendeleza maswali.

Wakati wakiendelea na mjadala huo, lilipita gari la mgombea CCM wa kiti cha ubunge cha Busanda, Lolensia Bukwimba na mara moja wananchi hao wakageuka na kuanza kuzomea msafara.

Wakati wakiendelea kuzomea ndipo Ngeleja alipopata mwanya na dereva wake akawasha gari na kuondoka.

Waziri Ngeleja alitaja mlolongo wa maeneo ambayo alisema mengi yatapata umeme kabla ya kumalizika kwa mwaka huu, lakini mkakati wao wa umeme ulitibuliwa baada ya Bunge kukataa kuinunua mitambo ya umeme wa dharura ya Dowans Tanzania Limited.

CCM imekuwa na wakati mgumu tangu kuanza kwa kampeni za ubunge wa jimbo hilo lililoachwa wazi na Faustin Kabuzi Rwilomba ambaye alifariki akiwa nchini India alikoenda kutibiwa
.

CHANZO: Mwananchi

IWAPO KUNA LOLOTE LA KUJIFUNZA KATIKA KAMPENI HIZI ZA UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA BUSANDA BASI NI NAMNA CCM ILIVYO KICHWA NGUMU KUELEWA SOMO.THING IS,WAMESHAHADAA WAPIGA KURA KIASI CHA KUTOSHA KWA AHADI HEWA,HIVYO KUREJEA TENA AHADI HIZOHIZO AMBAZO HAWAJAZITEKELEZA NI MITHILI YA,ASHAKUM SI MATUSI,KUMTONGOZA MTALAKA WAKO.

PENGINE JINGINE NI NAMNA CHAMA HIVYO KISIVYO SERIOUS NA USTAWI WA WANANCHI.WHY?BADALA YA KUREJEA AHADI HIZO AMBAZO HAZIJATEKELEZWA,CHAMA HICHO KWANZA KILIPASWA KUWAOMBA RADHI WAPIGA KURA KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA AHADI HIZO HADI SASA,NA ANGALAU BAADA YA HAPO KINGEWEZA KUJARIBU KETE YA KUREJEA AHADI HIZO.NASEMA THAT IS INDICATIVE OF LACK OF SERIOUSNESS KWA VILE CCM INAAMINI KUWA KAMA ILIKUWA IKITOA LOTS OF EMPTY PROMISES FOR AGES NA WAGOMBEA WAKE WAMEENDELEA KUCHAGULIWA,BADO KUNA IMANI KUWA SUCH A RISKY STRATEGY COULD WORK AGAIN AND AGAIN.

CCM HAIDHANI KUWA IMAGE YAKE IKO SEVERELY TARNISHED NA USWAHIBA WAKE NA UFISADI/MAFISADI.INAENDELEA KUAMINI KUWA SHUTUMA DHIDI YAKE KWAMBA NI KICHAKA NA HIFADHI YA MAFISADI NA ZA WATOVU WA NIDHAMU WACHACHE KAMA SIE LAKINI SIO KWAMBA KELELE ZETU NI UWAKILISHI TU WA VILIO VYA MAMILIONI YA WATANZANIA WALIOCHOKA KUFANYWA WAJINGA.

HIVI KIONGOZI MWENYE BUSARA ANAWEZA KUDIRIKI KU-BRING UP ISHU ZA DOWANS KWENYE BY-ELECTION KAMA YA BUSANDA?CAN'T BLAME NGELEJA KWA KUWA KWA YEYE NA VIGOGO WENZIE WA CCM,EQUATION YA DOWANS=RICHMOND HAIJAMWINGIA KICHWANI.

10 May 2009

PICHANI,NI MBUNGE WA IGUNGA,ROSTAM AZIZ,AKIKABIDHI KINACHODAIWA KUWA DOSSIER LENYE TUHUMA DHIDI YA MFANYABIASHARA RAGINALDMENGI.ANAYEKABIDHIWA NI AFISA UCHUNGUZI WA TAKUKURU GWAKISA.Picha hii ni kwa mujibu wa gazeti la The African.

HUU NI NI UPUUZI.YAANI HAINGII AKILINI HATA KIDOGO.JAMANI,HIVI LINI MMEWAHI KUONA TAKUKURU WAKIKABIDHIWA USHAHIDI/TUHUMA MBELE YA VYOMBO VYA HABARI AS SEEN IN THE PICTURE ABOVE?

HUYU ROSTAM AMEKUWA MITHILI YA MUNGU MTU: ALIPOTAJWA TU NA MENGI,MAWAZIRI WAZIMA NA BUSARA ZAO (SOPHIA SIMBA NA KAPTENI MKUCHIKA) WAKALIPUKA KUMTETEA (JAPO SASA WAMEKAA KIMYA ROSTAM ALIPORUDIA KILEKILE ALICHOFANYA MENGI).KISHA TAKUKURU NAO KATIKA HALI INAYOONYESHA NAMNA GANI TAASISI HIYO NI WABABAISHAJI WA DARAJA LA JUU WAKAANDAA MITHILI YA PRESS CONFERENCE YA KUMPOKEA ROSTAM NA KINACHODAIWA KUWA NI USHAHIDI WAKE DHIDI YA MENGI (JAPO KUNA MADAI KUWA WAJANJA WAMEMWINGIZA MJINI KWA KUMUUZIA "CHENI BANDIA"-ISOMEKE DATA FEKI).

HAWA TAKUKURU NI WAZEMBE ZAIDI YA WAZEMBE.HIVI UBABAIKAJI KAMA HUO WALIOFANYA KWA ROSTAM WANGEUELEKEZA KWA KAGODA SI TUNGEPIGA HATUA FLANI?AU WANGEKUWA "FASTA" NAMNA HIYO KATIKA,SIO KUITETEA BALI KUICHUNGUZA IPASAVYO KAMPUNI YA RICHMOND,KWA HAKIKA TUSINGEKUWA HAPA TULIPO SASA.

MBONA WENZETU MNAJIDHALILISHA KIASI HICHO?NI HIZO FEDHA ZA ROSTAM AU NJAA ZENU?THIS IS MORE THAN TOO MUCH.IT'S ABSURD,CRAZY AND UTTERLY NONSENSE.


A woman accused of tormenting her neighbours with her noisy love-making has appeared in court. Skip related content

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in ten days.

Magistrates in Sunderland slapped her with a four-year order on April 17, banning her from "making excessive noise" anywhere in England.

But Houghton le Spring Magistrates' Court heard that police arrested her on April 18, April 22 and April 26 after neighbours complained she was flouting the ban with the help of husband Steve.

Prosecutor Claire Ward said there were complaints of early morning shouting, moaning, groaning and the sound of a bed banging against the wall. Cartwright was arrested on Sunday and charged with three counts of breaching her Asbo.

Cartwright, of Hall Road, Concord, Washington, Tyne and Wear, whose husband sat in the public gallery, elected trial by jury and her case will be transferred to Newcastle Crown Court.

A bail application from defence solicitor Peter Lothian was refused.

Cartwright was remanded in custody and ordered to appear via video link before Sunderland Magistrates' Court on May 5.

On April 17, she was convicted for five breaches of an abatement notice and fined a total of £515.
Magistrates also imposed the Asbo, banning her from making excessive noise, knocking, shouting, screaming or vocalisation that can be heard in neighbouring properties or outside the house, and playing loud music.


SOURCE: ITN

9 May 2009




Kibaka aduwaza walinzi Ikulu

2009-05-08 13:51:35
Na Jacqueline Mosha

Mfanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es Salaam, Ally Nasoro (41) amefikishwa mahakamani kujibu shitaka la kuingia Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete na kuiba ua moja lenye thamani ya Sh. 5,000, mali ya Ikulu hiyo.

Mshitakiwa huyo alifikishwa mbele ya Hakimu Mwajuma Diwani wa Mahakama ya Mwanzo Kariakoo jijini Dar es Salaam jana, na kusomewa shitaka hilo.

Akisoma hati ya mashitaka, karani wa mahakama hiyo, Caphren Maduhu, alidai mbele ya hakimu Diwani kuwa mshtakiwa alifanya kitendo hicho Mei 2 mwaka huu.

Mahojiano mahakamani hapo yalikuwa kama ifuatavyo:

Karani: Kesi hii ni ya wizi na imefunguliwa na mlalamikaji ambaye ni askari mwenye namba E 4716 Koplo Mnyaga.

Mshitakiwa katika shitaka hili ni Ally Nasoro, anaishi eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na anakabiliwa na kosa wizi alilofanya Mei 2, mwaka huu, saa 4:24 usiku huko Ikulu ya Rais.

Hakimu: Mshitakiwa umesikia mashitaka ya kosa lako, unajibu nini?

Mshitakiwa: Mimi nilikuwa napima uwezo wa akili wa walinzi waliowekwa Ikulu ili kumlinda Rais wa nchi, maana isije ikawa wako wako tu kumbe hawana hata uwezo wa kumlinda.

Hakimu: Ile ni sehemu ya heshima na inalindwa iweje wewe upate wazo la kutaka kuingia ndani, ulikuwa na nia gani?

Mshitakiwa: Nilichokigundua siku hiyo ni kwamba kumbe naweza kuingia Ikulu kiulaini bila hata ya kuguswa na mtu. Kwanza nilipofika pale getini nilitaka kufahamu kama naweza kufanikiwa kuingia, hivyo, nilisimama kwa saa nne nje ya geti bila hata kuulizwa chochote na walinzi. Baadaye nilifanikiwa kupata mwanya wa kuingia ndani na kweli niliingia kiulaini bila hata 'shobo'.

Hakimu: Ilikuwaje mpaka ukaiba hilo ua?

Mshitakiwa: Nilipolichukua lile ua na kulibeba ndipo walinzi waliniona na baada ya kuniona walinzi hao walibaki wakitetemeka huku mimi nikiwa nimeshikilia ua na ndipo waliponikamata na kunichukulia hatua. Kama naweza kuchukua ua si ningeweza hata kuingia ndani kwa Rais kiulaini? Yaani walinzi wamelala pale. Hawako makini kama nilivyodhani.

Hakimu: Unajibu nini kuhusu shitaka la wizi huo?

Mshitakiwa: Si kweli, sijaiba ua.

Hakimu Diwani aliahirisha kesi hiyo mpaka itakapotajwa tena mahakamani hapo Mei 11 mwaka huu. Mshitakiwa alipelekwa mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ambayo ni kuwa na wadhamini wawili.

CHANZO: Nipashe

SOMEONE SOMEWHERE IS NOT UP TO THE TASK.AWALI,RAIS MSTAAFU MWINYI ALIZABWA KIBAO HADHARANI,A COUPLE OF WEEKS AFTER MSAFARA WA JK KURUSHIWA MAWE HUKO MBEYA.SUPPOSE HUYU KIBAKA HAD INTENDED TO,NOT TEASE THE GUARDS WITH A STOLEN FLOWER BUT, CAUSE HARM TO THE PRESIDENT.....

SECURITY SLACKNESS

8 May 2009


Venance George, Kilombero

BAADHI ya wadau katika Wilaya ya Kilombero, wameitahadharisha serikali kuhusu uanzishwaji wa taasisi zenye mtazamo kama wa Deci ili kuwanusuru wananchi wasipoteze mali zao.

Tahadhari hiyo inafuatia kuanzishwa kwa PUFDIA, katika mji mdogo wa Ifakara ambayo watu wanaifananisha na Deci. Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wadau hao, Ibrahim Madon na Kenedy Haule waliishauri serikali kudhibiti uanzishwaji wa taasisi kama hizo. Walisema kama serikali haitakuwa makini, baadhi ya watu wachache wanaojali maslahi yao, watakuwa wanaanzisha taasisi hizo na kuendelea kuwakamua wananchi maskini.

Walitolea mfano wa Deci ambayo ilipigwa marufuku na serikali hivi karibuni, baada ya kuanzisha kwa mchezo wa upatu ambao baadaye ungesababisha hasara kubwa kwa wateja wengi wao wakiwa ni wananchi maskini. Taasisi ya PUFDIA imeingia wilayani humo hivi karibuni na kujinadi kwamba ni taasisi mpya inayotoa huduma za miradi mitano endelevu kwa ajili ya maendeleo ya watu wa nchi nzima.

Miradi inayoshughulika na taasisi hiyo ni pamoja na udhamini wa masomo ya sekondari hadi chuo kikuu kwa kwa mtoto wa mtu yeyote. Katika mchakato wake taasisi hiyo inaeleza kuwa chini ya mradi wa elimu, itatoa fedha za kulipia gharama zote za masomo na bajeti inayotolewa kwa kila mtoto ni Sh 570,000 kwa wale wanaosoma shule za msingi wakati wale wanaosoma shule za sekondari watapewa Sh980,000 na Sh 2.64 milioni kwa vyuo vikuu.Gharama hizo ni kwa kila muhula.

Mradi mwingine ni wa kujengewa nyumba za thamani ya Sh 6 milioni kama msaada kwa mwananchi yeyote mwenye shida ya nyumba wakati wanaotaka kujengewa shule wanatakiwa kwenda katika ofisi hiyo kujaza fomu yenye uwezo wa kujengewa shule yenye thamani ya Sh 46.2 milioni

Taasisi hiyo pia imesema itasaidia wananchi kwa kuwapa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya Sh 2,470,000. Mwandishi wa habari hizi alikwenda katika ofisi za PUFDIA na kuwahoji maofisa wake ambao hata hivyo, hawakutaka kutaja majina yao. Maafisa hao walidai kuwa huduma wanazotoa ni halali na kwamba wanalipia kodi.

Kwa mujibu wa maelezo yao, taasisi hiyo inafadhiliwa na taasisi kubwa ya kidini iliyoko nje ya nchi. Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, alikiri kuwepo kwa taasisi hiyo na kwamba maafisa wake, walikwenda ofisini kwake kuomba kutoa huduma hiyo.

Alisema hata hivyo atalipitia upya jalada la taasisi hiyo na kuelezea mustakhabali wake.


CHANZO: Mwananchi


ASHANTI ft CROOKED I "Baby-Remix"

Featured by FAT JOE in What's Love

Foolish (TERRENCE HOWARD cameo)


Ja Rule ft. Ashanti & Rkelly - Wonderful
by Shameek


MTV NEWS reports that Ashanti and Murder Inc will soon be partying company.

It's weekend,let's have some fun.How about this?




That's according to ThisIs50.Com

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.