27 May 2010


Baraka Baraka ndio mhariri (Editor) wa £ovely Gamble. Huyu Bwana ni Photograher, Director na Producer. Amesha fanya kazi kwenye uzalishaji wa vipindi vingi ambavyo vimeshaonyeshwa katikaTelavisheni tofauti Uingereza na Ulaya kama vile OBE TV, MATV na TVT (ZE COMEDY London Special). Baraka pia ni mkali wa na advertising shot films kama vile ‘KARMA’ na ‘The ONE’ vilevile amesha Direct documentary programmes za kisiasa kama ‘A PATH TO WAR’ na za kijamii kama IN A ‘FOREIGN LAND’

Kwenye upande wa Photography amebobea kwenye fani ya fashion and advertsing. Kijana huyu ana freelance na kampuni tofauti za media na advertising agencies ikiwa ni pamoja na prestigious PUBLIC LTD. Baraka ameshawahi kufanya maonyesho (Exihbition) ya kazi zake za Photohgraphy mara tatu sasa. Hivi sasa anajitayarisha kushoot shot film iitwayo ‘JIKO LA SAIDI’ . Pia anakuwa moja ya wamiliki wa URBAN PULSE CREATIVE ya hapa UK.

Mahojiano haya (hapo juu) yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK. Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gambl kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU
WYCLIFF
233 KINGSROAD,
READING, RG1 4LS


TANGAZO MAALUM
KWA WAKAZI WA WA UGHAIBUNI
KUTOKA URBAN PULSE NA BUZZIE  PRODUCTION
Mashabiki na Wapenzi wa filamu wa Kitanzania tunapenda kuwataarifu kuwa tumepokea malalamiko yenu kuhusu ubora DVD za filamu ya £ovely Gamble.  Kwamba zina  giza na sauti  si bora  na picha zinacheza. Hili tumelichunguza na kugundua ya kuwa  linasababishwa na DVD HARAMIA (PIRATE COPIES) zinazouzwa kinyume ya sheria.

Tunaelewa tatizo hili ni sugu dunia nzima na  linawanyima thamani ya utamu wa filamu.  Vilevile lina changia kudumisha kiwanda cha uzallishaji wa filamu. Kuepukana na adha hii ,Wazalishaji wa £ovely Gamble wanawaomba na kuwashauri kununua  filamu hii kutoka kwa DVD za halali zitakazopatikana kuanzia Jumamosi ya tarehe  29-10-2010 kwenye  uzinduzi maaluma wa kuchangia yatima wanao ishi na vijirusi wa UKIMWI  nyumbani TANZANIA  na kwa wakala maalumu  watakao tangazwa rasmi   siku hiyo

DVD MAALUM “DIRECTOR'S CUT”  WITH BONUS MATERIAL
*FILMMAKERS
*HATAKAMA
*SEXY MAMA

                    WYCLIFFE VENUE                                                                                                           
233 KINGS ROAD                                                                                              
        READING RG1 4LS.                                                                                                       
 6.30pm-11.30pm
TCKT IN ADVCE £10 FOR VIP’s SEATS AND £5 FOR STANDARD SEATS. (*VIP TCK HOLDERS GETS FREE AFTER PARTY PASS*)
WOTE MNAKARIBISHWA


26 May 2010


Rennison Okenwa ndio kichwa kilicho Direct movie £ovely Gamble. Rennison-au maarufu kama 'Renny'- ni ndugu yetu kutoka Kenya. Huyu jamaa ndio aliyekuja na wazo la kue-xperiment namna ya kutumia picha na muziki kuelezea hadithi. Renny ni msomi wa uzalishaji wa vipindi vya television aliyehitimu katika chuo kikuu cha Thames Valley. Renny ameshatengeneza documentary programmes mbili kuhusu vifaa vya hospitali na kuhusu matatizo ya magonjwa ya akili. Kwa sasa ana shoot documentary kuhusu wazazi watoto 'Young Mums'

Mahojiano haya yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK.

Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gamble kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU Usiku.
WYCLIFFE VENUE,
233 KINGS ROAD,
READING, RG1 4LS

WATANZANIA WOTE WA UK MNAKARIBISHWA
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

Tanzania imeshuhudia vituko vingi mwezi huu wa Mei,kutoka Rais Kikwete kutetea takrima  hadi mtumishi wa Bwana Askofu Kilaini kudai kuwa Kikwete bado ni chaguo la Mungu,kutoka sakata la Masauni kufoji umri (oh Mungu, inawezekanaje?) hadi kifungo cha Liyumba (wengine wanadai alistahili kunyongwa kabisa).Na kutoka kauli ya Waziri Kombani kuwa daraja la mto Kilombero litajengwa katika awamu ya pili ya Kikwete (as if JK ameshashinda uchaguzi) hadi ajali ya gari la msafara wa JK.Makala hii inajaribu kuibua maswali kuhusu hili la mwisho,yaani ajali hiyo.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari,uchunguzi mkali unaendelea ku-establish chanzo cha ajali hiyo.Lakini wakati uchunguzi huo ukiendelea tayari kuna wingu limeigubika ajali hiyo huku kukiwa na maswali kama ilitokana na hujuma,au uzembe au ni bahati mbaya tu.

BAHATI MBAYA: Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi,ajali hiyo ni bahati mbaya.Gazeti la Tanzania Daima limemnukuu Msika akisema, “Tunaamini ni ajali ya bahati mbaya ambayo ilisababishwa na matatizo ya kiufundi, lakini jambo la kushukuru kiongozi wetu hakupata madhara kwa matukio yote mawili.” Yah,inawezekana ni bahati mbaya.Lakini kichekeksho ni pale Msika kutoa kauli hiyo kabla ya uchunguzi.Majibu rahisi katika maswali magumu?Well,hiyo ndio Bongo yetu.Kauli hiyo ya Msika inaweza kupewa nguvu na kauli nyingine iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Salva Rweyemamu,aliyenukuliwa na gazeti hilohilo la Tanzania Daima (toleo la Jumapili) akisema "hitilifu za magari alizokabiliana nazo Rais Kikwete zilikuwa ni za kawaida".Again,tunashuhudia watu walokabidhiwa dhamana muhimu wakikurupuka kutoa majibu mepesi hata kwenye masuala nyeti.Yani kuchomoka tairi ya gari la kiongozi wa nchi ni kitu cha kawaida!Au ni kwa vile ajali kubwa zimezoeleka sana kiasi kwamba hiyo ya msafara wa JK inaonekana 'cha mtoto'?

HUJUMA: Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,kamanda Msika haamini kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hujuma.Anasema, "Nasisitiza hatuamini kama kulikuwa na hujuma na ndiyo maana hatutafanya uchunguzi kuhusu matukio yote mawili, lakini kwa suala kama kulikuwa na uzembe wa ukaguzi wa gari, mtafute Salva (Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu), ndiye anaweza kulizungumzia.” Kwa mara nyingine tena tunashuhudia Msika akitoa majibu ya hisia zake (na pengine Jeshi analoongoza) badala ya kusubiri matokeo ya uchunguzi wa kitaalam.Hivi kulikuwa na ugumu gani kwa Msemaji huyo wa jeshi la polisi kutoa jibu lenye mantiki kwamba 'tusubiri matokeo ya uchunguzi badala ya kufanya guesswork'?
Tanzania Daima linakwenda mbali zaidi na kuihusisha ajali hiyo na matukio ya mbalimbali ambapo Rais amekuwa akipewa taarifa potofu (rejea Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na taarifa za vikao kati ya TUCTA na Serikali).Kwa mtizamo mpana,gazeti hilo linajaribu kueleza kuwa yayumkinika kuhisi kuwa ajali hiyo ni muendelezo wa 'hujuma' zinazofanywa dhidi ya Rais Kikwete.

Kwa bahati mbaya (au kwa makusudi) Watanzania hawatapata fursa ya kujua ukweli kuhusu tukio hilo.Kwanini nahitimisha hivyo?Well,labda mwenzangu umeshasahau kuhusu ripoti ya chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala.Najua kwa wengine,nikitaja Mbagala wanakumbuka zaidi kuhusu mwana-Bongofleva Diamond kuliko ukweli kwamba kuna wenzetu walipoteza maisha yao,tukaambiwa tume imeundwa kuchunguza milipuko hiyo,tukaonyeshwa picha ripoti ikikabidhiwa kwa waziri husika,na hadithi ikaishia hapo.Na kama hufahamu,tume iliyoundwa kuchunguza milipuko hiyo ilitumia fedha za walipa kodi.Sasa sijui wana-tume waliamua kufanya uchunguzi wao baa kisha 'kutokana na kilevi' wkaafikiana kuwa hakuna haja ya kuweka hadharani ripoti hiyo.

UZEMBE: Ni rahisi zaidi kuhisi kuwa ajali hiyo sio bahati mbaya au hujuma bali ni uzembe kwa kuangalia mlolongo wa matukio ya uzembe yanayojiri mara kwa mara.Kwa bahati mbaya,au makusudi,baadhi ya matukio hayo yanamhusisha Rais Kikwete moja kwa moja.Hebu angalia ishu ya Masauni,kwa mfano.Katika kudhibiti songombingo kati ya (Benno) Malisa na Bashe huko UVCCM,JK alionelea ni vema Mwenyekiti wa Umoja huo atoke Zanzibar.Na huyo ndiye Masauni.Kwa hiyo tunapozungumzia 'fojari' ya umri wa Masauni tunapaswa pia kukumbuka nani aliyemuibua.

Lakini tofauti na uzembe uliozoeleka katika shughuli mbalimbali za serikali,huu wa ajali ya gari la Rais hauwezi kuhusishwa na rushwa.Unajua,mara nyingi neno 'uzembe' linatumika kupunguza makali ya neno 'rushwa'.Yaani,utaskia mtu flani 'alifanya uzembe kusaini mkataba flani' lakini ukweli ni kwamba mtu huyo hakuwa mzembe bali alikuwa makini katika kuhakikisha teni pasenti inakwenda kwenye akaunti yake.

Kwanini ajali hii inaweza kuwa matokeo ya uzembe?Kwa wenye ufahamu wa usalama wa kiongozi kama rais,gari analotumia linapewa uangalizi wa hali ya juu kama ilivyo kwa afya,ustawi na usalama wake kwa ujumla.Kuna mlolongo wa watu (wanaolipwa vizuri tu) wanaowajibika kuhakikisha kuwa kila atakachotumia rais kipo katika hali nzuri (na ya juu kabisa).Sitaki kuingia kwa undani sana katika hili kwa sababu zangu binafsi,lakini nachoweza kusema hapa ni kuwa kuna wazembe flani ambao hawakutilia maanani hitilafu zilizojitokeza katika chombo cha usafiri wa rais.

Tatizo linaloweza kuwa limepelekea uzembe huo ni MAZOWEA.Nadhani kuna wanaokumbuka masahibu yalomkumba JK wakati wa kampeni yake huko Mwanza mwaka 2005.Naamini pia kuna wanaokumbuka balaa lilomkumba Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi pale aliponusurika kupigwa akiwa msikitini jijini Dar.Nahisi pia kuna wengi wanaokumbuka habari za msafara wa Kikwete kurushiwa mawe huko Mbeya.Matukio yote hayo yanaweza kuhusishwa na ajali hii ya gari la Rais,na yote yananyooshea kidole uzembe mahala flani.

Nihitimishe makala hii kwa kuusia kwamba matukio kama hilo la ajali ya gari la Rais yataendelea kutokea kama tutaendelea kukabidhiana majukumu kwa minajili ya urafiki (au kishkaji,kama wasemavyo mtaani.Tunapoweka kando professionalism na kuruhusu umimi tutambue kuwa tunajichimbia kaburi letu sie wenyewe.Ujuzi na uzoefu hauwezi kuwa replaced na udini,urafiki au kujuana.

Mwenye macho na asome,mwenye masikio na asikie.

You have been warned!

25 May 2010


Kijana ambaye yuko kwenye £ovely Gamble anaitwa Kisiri Elly anacheza part ya Frank. Huyu actor chipukizi wa Kitanzania ambaye ameingia katika fani ya usanii wa filamu. Kisiri amecheza filamu hii na staa za kitaaluma unaweza kufikiri ni mzoefu wa siku nyingi. Hivi tuzungumziavyo kesha tafutwa na Nollywood na ataanza production ya 'Man Alone' itakayotengenezewa Lagos na London shooting itaanza August mpaka September. Tumfagilie mbongo huyu ambaye anaanza career hii kwa kasi.

Mahojiano haya yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK.

Onyesho maalum la Filamu ya £ovely Gamble kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5 NA NUSU Usiku.
WYCLIFFE VENUE,
233 KINGS ROAD,
READING, RG1 4LS

WATANZANIA WOTE WA UK MNAKARIBISHWA
-------------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA

24 May 2010


Binti mdogo na mrembo ambaye yuko kwenye £ovely Gamble  anaitwa Ann-Lyyn Kapinga anacheza part ya Jasmeen. Huyu binti ni actress wa ukweli kwa sababu anasomea  fani hii na huwa ana perform kwenye theatres tofauti za South of England.

Mahojiano haya yamefanywa na Watayarishaji wa kipindi cha ALL ABOUT WOMEN ambacho presenter wake naye ni Dada wa  kibongo aitwaye Tina George, Kipindi hiko hurushwa kwenye  vituo vya television vya AILTV na Ben TV huku UK. 

Onyesho maalum la  Filamu ya £ovely Gambl kuchangia watoto yatima wanaoishi na virusi vya UKIMWI Litafanyika

                                                                   JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
                                              SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5.30 Usiku. 
                                                       WYCLIFFE VENUE,  
                                                        233 KINGS ROAD, 
                                                      READING, RG1 4LS

WATANZANIA WOTE WA UK MNAKARIBISHWA
------------------------------------------------------------------------
BARAKA BARAKA


Hatimaye kesi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Benki Kuu,Amatus Liyumba,inafikia ukingoni leo ambapo atasomewa hukumu.Japo zamani hizoo nilishawahi kuwa 'mnajimu/mtabiri wa kizushi' nilipoandikia magazeti ya Sanifu,Kasheshe na Komesha huku nikijiita 'Ustaadh Bonge' (na baadhi ya watu walikuwa wakiamini 'unajimu' huo),siwezi kwa hakika kubashiri lolote kuhusu hukumu hiyo.Kibaya zaidi,upeo wangu wa taaluma ya sheria ni dhaifu kama uchumi wa Somalia.

Lakini kabla ya kuzungumzia kwa undani kuhusu hukumu hiyo,pengine ni muhimu kuangalia kidogo mwenendo wa kesi hiyo inayogusa hisia za wengi (na wengine wakiwa na sababu zao binafsi).Hadi sasa sielewi mantiki iliyotumika katika kumweka Liyumba gerezani muda wote huu ilhali kisheria yeye anabaki kuwa mtuhumiwa hadi itakapoamuliwa vinginevyo na mahakama.Naomba ieleweke kuwa simtetei Liyumba japo ni 'mwana wa pakaya' kwangu.Ninachohoji hapa ni uhalali wa kumweka mtuhumiwa rumande kwa zaidi ya mwaka mzima pasipo kumpatia dhamana.Hii ni mithili ya kuwa na kiji-Guantanamo chetu ndani ya jamii inayodai kuzingatia utawala wa sheria.Hatari iliyopo ni kwamba kama akishinda kesi,Liyumba anaweza kudai fidia kubwa zaidi ya kiwango anachotuhumiwa kukifanyia ubadhirifu.Afungwe au aachiwe huru,kwa kuwekwa gerezani muda wote huo pasipo kupewa dhamana ni kama alishakuhukumiwa kabla ya hukumu ya leo.Badala ya kuwa 'innocent until proven guilty',hii imekuwa 'guilty until proven innocent'.

Tuje kwenye mwenendo wa kesi yenyewe.Kulikuwa na mikanganyiko kadhaa kwa upande wa mashtaka huku baadhi ya mashahidi wake wakimtetea mshtakiwa waziwazi.Pigo jingine kwa upande wa mashtaka ni kutokuwepo kwa mtu ambaye wangeweza kumfanya 'shahidi nyota' (star witness),aliyekuwa Gavana wa BOT,hayati Daudi Ballali (huyu nae alikuwa 'mwana wa pakaya' just like alivyo 'mrithi' wake,Prof Benno Ndulu).Kwa vile haingekuwa rahisi kwa Liyumba kufanya ubadhirifu huo pasipo Gavana kufahamu kinachoendelea kwa kipindi chote hicho,yayumkinika kusema kuwa marehemu Ballali angekuwa na umuhimu wa kipekee katika kesi hiyo.Na japo 'star witness' huyo hakuwepo,ushahidi ulotolewa na Naibu Gavana na watendaji wengine wa BOT unaweza kutafsiriwa kama 'habari njema' kwake badala ya kumkandamiza.

Halafu kuna tatizo jingine,nalo ni udhaifu wa wanasheria wa serikali/ waendesha mashtaka.Mjuzi mmoja wa masuala ya mahakamani aliwahi kuniambia kwamba wahitimu wa sheria waliofanya vizuri kwenye masomo yao hukimbiliwa na kampuni binafsi za sheria,na hivyo kuwaacha 'wale wa kawaida' wakitarajia ajira kutoka serikalini au vyombo vya sheria vya umma.Sote twaweza kubashiri nini kitajiri pindi wahitimu hawa wanapokutana mahakamani,huku wale wa 'daraja la kwanza' wakiwa upande wa washtakiwa au washtaki dhidi ya serikali.Inaelezwa pia kuwa kipato cha mawakili binafsi kipo juu zaidi ya cha wenzao wa serikalini/taasisi za umma.Ni dhahiri mwanasheria anayelipwa kwa saa au mwenye maslahi bora atakuwa katika nafasi nzuri dhidi ya mwenzie ambaye si ajabu wakati akiwa mahakamani atakuwa bize zaidi kupiga mahesabu ya namna ya kumudu maisha hadi siku ya mshahara wake kijungujiko kuliko kutimiza wajibu wake sawasawa.

Kwa wengi tunaofahamu ugumu kwa mtu wa tabaka la juu kama Liyumba kuhukumiwa kifungo,let alone kufunguliwa mashtaka (akina Chenge 'wanapeta' tu huku kesi ya Pro Mahalu ikisuasua na mafisadi wa Kagoda wakiendelea 'kula bata'),kuna hisia kuwa Liyumba 'anafanyiziwa' tu.Yani,si kwamba anachotuhumiwa kufanya hakikupaswa kumfikisha mahakamani bali ni imani inayozidi kushamiri katika Tanzania yetu kuwa mashtaka na vifungo ni kwa wanyonge na wasio na uwezo wa 'kununua au kutetea haki zao.'Wambeya' wanadai kuwa ishu ya Liyumba inaweza kuwa kama ya 'Babu Seya' ambapo inadaiwa kuwa kesi zao ni matokeo ya 'kuingilia maslahi ya watu'.By 'watu' haimaanishi mie na wewe bali vigogo ambao 'kugusa mali zao' ni zaidi ya kosa la jinai.Inadaiwa kuwa mtu anaweza kufisadi atakavyo na asichukuliwe hatua alimradi hagusi 'mali' za 'wenye nchi'.Na kama hujaelewa by 'mali' namaanisha nini,well,huijui vema Tanzania unayoishi au unayotoka.

Ok,tusubirie hukumu lakini kama umesoma vema between lines katika nilichoandika hapo juu basi utakuwa unafahamu bet yangu ikoje.

23 May 2010



MMOJA wa mawaziri wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete anatuhumiwa kushinikiza kuachiwa kwa dhamana ndugu wawili waliokamatwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na viungo vinavyosadikiwa kuwa vya binadamu.

Taarifa hizo za waziri huyo, ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa, kuhusishwa katika kashfa hiyo, ni mwendelezo wa mawaziri wa serikali ya awamu ya nne kuingia kwenye kashfa ambazo baadhi zimetinga mahakamani na nyingine kutolewa maamuzi.

Taariofa hizo pia zimeibuka siku chache baada ya mtu anayedaiwa kuwa mtoto wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Celina Kombani kuhusishwa na tukio la utekaji kijana mmoja anayejulikana kwa jina la Minja, tukio ambalo polisi imesema inaendelea kulichunguza wakati watuhumiwa wakiwa mahabusu.

Taarifa zilizolifikia Mwananchi kutoka wilayani Urambo mkoani Tabora zinasema waziri huyo alishinikiza kuachiwa kwa watuhumiwa hao kwa kumtumia mkuu wa wilaya hiyo, Anna Magoha.

Habari zinasema kuwa watuhumiwa hao waliokamatwa walikuwa wakiuza mifupa hiyo ya binadamu kwa kukata vipande vidogovidogo ambavyo waliviuza kila kimoja kwa Sh2,000.

Ilielezwa kuwa viongozi wa Kata ya Kaliua, akiwemo diwani, waliandaa watu kwa maelekezo ya waziri huyo ambaye alikodi magari mawili ambayo Jumatano wiki hii yaliwapeleka watu ambao walienda kufurika kwenye ofisi ya Magoha kulalamikia kukamatwa kwa watuhumiwa hao.

Akizungumza kwa simu na Mwananchi, Magoha alikiri kupokea malalamiko ya watu hao na kwamba kutokana na maelezo ya mashahidi walioshuhudia watuhumiwa hao wakikamatwa, waziri huyo aliwaita polisi, akiwemo mkuu wa upelelezi wa wilaya hiyo, na kuagiza watuhumiwa hao wadhaminiwe.

“Nafahamu kwamba suala hilo ni la kisheria zaidi, lakini, kwa kweli watu walikuwa wengi na malalamiko yao nilihisi yalikuwa ya msingi, nikawaita polisi akiwemo OC-CID, nikazungumza nao na kuwaagiza wataalamu wa sheria wapitie sheria kuona zinasemaje, nikaagiza wadhaminiwe wakati uchunguzi ukiendelea,” alieleza Magoha.

Kwa mujibu wa habari za kimahakama, waliokamatwa na viungo hivyo vinavyodhaniwa kuwa ni vya binadamu ni Risasi Jumanne, 27, na Mashaka Juma, 26, wakazi Kaliuwa kitongoji cha Mwangaza.

Kamanda wa polisi mkoani humo, David Mwakiruma, alithibitisha taarifa hizo  na kueleza kwamba watuhumiwa hao walitiwa mbaroni Jumapili iliyopita wakiwa na viungo hivyo.

Alisema polisi ilipata taarifa za kuwepo kwa watu wanaouza vipande vya mifupa ya viungo vya binadamu, ambavyo walikuwa  wakiuza kila kipande kidogo Sh2000 na baada ya kufuatilia polisi ilibaini kuwepo dalili za ukweli na baada ya kufanya upekuzi ndani ya nyumba ya watuhumiwa wakiongozwa na kamanda wa upelelezi wa wilaya hiyo, ASP Kaijanente, walibaini viungo hivyo.

Alisema upekuzi huo ulifanyika saa 12:50 jioni, Jumapili mbele ya mwenyekiti wa kitongoji hicho na jirani wa watuhumiwa na kwamba ndani ya chumba kimoja kati ya viwili vinavyotumiwa na watuhumiwa hao, darini kulikutwa viroba viwili kimoja kikiwa na madaftari.

Kifurushi kingine kinaelezwa na Mwakiruma kuwa kilikutwa na fuvu la kichwa kilichopasuliwa katikati, lakini kikiunganishwa kinaonyesha kuwa ni cha binadamu, taya la gego la chini lenye meno matatu na mfupa mmoja wa mguu kuanzia gotini kuteremka chini.

Vipande vyote vinasadikiwa ni viungo vya binadamu na polisi imesema vitapelekwa kwa mkemia mkuu wa sarikali ili vichunguzwe.

Taarifa kutoka Mirambo zilisema watuhumiwa walifikishwa mahakamani Juma nne wiki hii na kusomewa shitaka la kukutwa na viungo vya binadamu.

Wafuatiliaji wa sakata hilo walilieleza Mwananchi kwa sharti la kutotajwa majina yao kuwa dhamana hiyo ilitolewa; juzi jioni baada ya Magoha kuwaita viongozi wa polisi na hakimu wa wilaya hiyo ofisini kwake na kuwashinikiza watekeleze agizo hilo linalosadikiwa kutolewa na waziri huyo.

CHANZO: Mwananchi

22 May 2010



Katika siku za hivi karibuni,Rais Jakaya Kikwete amekuwa akitoa kauli ambazo kwa namna flani zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani.Sote tunakumbuka hotuba yake kali aliyotoa mbele ya walioitwa 'wazee wa jiji la Dar es Salaam' ambapo baadhi ya maneno yake yanaweza kabisa kuwatia jeuri wanadola wanapoagizwa kudhibiti wananchi.Kwa ujumla hotuba hiyo ilitawalia zaidi na kauli za ubabe na vitisho badala ya kuelimishana kistaarabu.Mbona ukali huo haukutumika kwenye hotuba yake ya Agosti 2008,ambapo pamoja na mambo mengine na kinyume na matarajio ya wengi,aliongea kwa upole na kukumbushia haki za binadamu kwa mafisadi.Nadhani msomaji unakumbuka kijembe alichotoa Spika Samuel Sitta kwa JK kwamba haki za wananchi ni za muhimu pia (tena zaidi ya za mafisadi).

Majuzi akarejea tena kauli ambazo kwa hakika zinapaswa kukemewa vikali.Kwanza, 'aliwapa jeuri' vijana wake wa UVCCM kwamba wasikubali kufanyiwa vurugu kipindi cha uchaguzi.Huku akitambua wazi kuwa yeye ni Amiri Jeshi Mkuu,na mwanajeshi mstaafu,bado alitoa uhuru kwa vijana hao 'kukabiliana na vurugu kama zile za katika baadhi ya chaguzi ndogo zilizopita'.Hivi Rais wetu anajifanya hajui kuwa wenye jukumu la kukabiliana na vurugu ni jeshi la polisi na sio UVCCM?Hivi kiongozi wetu huyu haelewi kwamba kuna uwezekano wa wahuni kujichanganya na vijana hao wa CCM kisha katika 'kukabiliana na vurugu za wapinzani' wakapelekea maafa,na halafu wakajitetea kuwa waliamriwa na Rais 'kudili na vurugu kwa namna hiyo'?

JK anapaswa kufahamu kuwa si yeye wala hao vijana wake wa UVCCM wako juu ya sheria au wana mamlaka ya kujichukulia sheria mkononi.Kwa kuruhusu hilo,Rais anaweza kuyapa changamoto makundi mengine katika jamii 'kufuata busara zake' na kuchukua sheria mkononi badala ya kuviachia vyombo vya dola vitimize wajibu huo.

Lakini ukidhani hiyo ndio kauli pekee ya kutisha kutoka kwa JK,basi hujaiskia hii.Akiwa ziarani huko Mtwara,Rais aliagiza msako wa nyumba hadi nyumba kusaka wanafunzi waliofaulu na kuchaaguliwa kujiunga elimu ya sekondari lakini hawajafanya hivyo kutokana na sababu moja au nyingine.Kwa mujibu wa gazeti moja,Rais alisema "ikibidi hata nguvu itumike" katika utekelezaji wa agizo hilo.Hivi JK anaweza kutueleza ni nguvu ya namna na kiasi gani itakuwa halali katika utekelezaji wa agizo hilo?Je Rais hadhani kuwa agizo lake linaweza kupelekea ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kwa wanafunzi hao na wazazi wao?Kwanini badala ya msako uliopewa baraka za kutumia nguvu kusifanyike vikao kati ya wazazi wa wanafunzi hao na serikali ngazi ya mtaa,kata,au wilaya?Hivi Rais haelewi kuwa hata kama amri yake haitopelekea balaa kwa wanafunzi hao na wazazi wao (si unajua mgambo wanavyonyanyasa watu),na wanafunzi hao kupelekwa mzobe mzobe mashuleni,bado wanaweza kabisa kugoma kusoma wakiwa mashuleni?Shule sio sawa na baa ambapo unaweza kumpeleka mtu kibabe na kumshikia mtutu anywe pombe na akainywa kwa kuchelea matokeo.Kwa shule,hakuna namna unaweza kumlazimisha mtu asome na kuelewa.hata kama utampeleka shuleni kwa kikosi cha mizinga.

Je inawezekana kauli hizi za JK zinazobeba (au kuruhusu) matumizi ya nguvu zinatokana na ukweli kuwa yeye ni mwanajeshi mstaafu?Nauliza hivyo kwa vile kuna imani kwamba mentality anayojengwa askari jeshi huweza kudumu kwa mjeshi huyo kwa takriban muda wake wote wa uhai wake hata anapostaafu.

Kuna watakaotafsiri makala hii kama alarmist,yaani yenyebkubeba wasiwasi usio na msingi.Yote kheri,lakini tukumbuke kuwa pindi amani yetu ikivurugika kwa sababu ya matumizi mabovu ya nguvu ya uongozi wa umma,hakutakuwa na nafasi ya kuzuia uvunjifu wa amani.Kadhalika,ni vema kidhibiti dalili za udikteta kabla hazijaota mizizi na kushamiri.

Kwa bahati mbaya,au makusudi,ni kama watu wako usingizini (na usingizi wenyewe ni ule wa kupuliziwa dawa ya kulala bila kushtuka hata ukiangukiwa na paa).Namna mambo yalivyo ni kama watu 'wamekubali matokeo kabla ya kipenga cha mwisho'.Jeuri za watawala wanaopuuza haki za binadamu za wanyonge huimarishwa zaidi na 'usingizi huo wa pono'.Kama mtu anakufinya na wewe unazubaa tu,hutoi japo yowe,basi ni dhahiri kuwa sio tu mtu huyo atakubana zaidi bali pia ataamini kuwa huumii.

Amkeni!

21 May 2010



ONYESHO MAALUM LA FILAMU £OVELY GAMBLE TAREHE 29TH OF MAY 2010.  KARIBUNI KUCHANGIA YATIMA WALIOATHIRIKA NA UKIMWI TANZANIA NA JUMUIA YETU  YA TANZANIA. WATOTO HAWA WANAANGALIWA NA TANZANIA MITINDO HOUSE INAYOENDESHA SHUGHULI ZAKE TANZANIA.
      JUMAMOSI TAREHE 29/05/2010.
          SAA 12 Jioni MPAKA SAA 5NA NUSU Usiku.
         WYCLIFFE VENUE, 
        233 KINGS ROAD,
         READING, RG1 4LS.

VILEVILE KUTAKUWA NA CHAKULA, VINYWAJI, BURUDANI YA MIZIKI NA  VICHEKESHO . NYOTE MNAKARIBISHWA NA KUFIKA KWENU NDIO KUFANIKISHA SHUGHULI HII. TUNAWAOMBA MJE KUSAIDIA WATOTO HAWA NA JUMUIYA YETUWETU.
DRESS CODE: LADIES: DRESS SEXY & GENTS: SMART
MUSIC: LIVE MUSIC, AFRO BEAT, BONGO FLAVOR, HIP HOP, MDUARA AND RNB
TIKETI ZIPO KUANZIA £10 KWA VITI VYA VIP’s NA £5 KWA VITI VYA KAWAIDA.TIKETI ZINAPATIKANA –
SWIFT FREIGHTS UK (TZUK) – LONDON 0208 801 9800
AFRICANS IN LONDON TV (TINA) – LONDON
MOUDY – LONDON 078884441222
KAYE MARIE – LEICESTER 0794665430
BARAKA - LEICESTER 07909260435
BONGO FLAVOUR – READING 0118 958 5878
VINCENT BAR – READING 0118 959 3130
TANZANIA ASSOCIATION – READING 07865673756
FRANK – READING 07865594576
                                   INFO:[email protected]                                                                                             www.wix.com/effeort111/urbanpulse-tmh               
   http://www.youtube.com/watch?v=zNltrl096hU

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.