1 Aug 2011


Show ya "Growing Up African" inayo onesha familia kutoka Tanzania na maisha yao Marekani imeanza kutoa video online. Kutoka mwezi wa tatu hadi saa hivi show ilikua inayonekana East Africa TV. Kwenye mwezi huu wa August kila Episode ya Season ya Kwanza itakua kwenye website yao. Kwenye hizi episodes utakutana na ndugu wote kwenye familia kutoka kwa Bea, Eliza, Jesca, Johnson hadi Andrew ambapo huwa maisha yao ni tufauti kwa kila mtu. Episode zitakuwa na familia nzima ambao utaona hile "family dynamic" ya ndungu. Hii show kwanza, niyasisi Watanzania na tunabidi tuwasikie mnavyosema kabla ya kuwa kwenye International Spotlight na kuja na Season ya pili September. Watu hizo episode wanaweza kwenda kwenye youtube.com, au kwenye website www.growingupafrican.com kuona hayo mambo. Website saa hivi hiko tayari na yenyewe ina mambo mengi kama mawazo ya familia kwenye issues kama musiki, fashion, urembo, na vinginevyo vingi kwenye blog zao.

Asanteni Sana, na ninaomba ushauri na mawazo kutoka kwenu kama watanzania wenzetu.

"Growing Up African" since it's inception through our supportive blogs in October 2010 has grown to become a household name in the East African Community. Currently the show is available only on East Africa TV that broadcasts to Uganda, Burundi, Kenya, Rwanda and lastly Tanzania. It is our deep honor to present the first Season of the show to those viewers outside the viewing area of these five countries. We have received numerous requests through mail and phone calls to let people from abroad into this well formed hype machine. In it's first Season, we did experience several setbacks but like any successful business development comes with time. The show is now available on our website at WWW.GROWINGUPAFRICAN.com and Youtube Channel at 

As we prepare to launch the Second Season in September on East Africa Television, we would like to give an opportunity to everyone to catch up on the show.










Qatar-based broadcaster has struck a deal with US network Time Warner Cable, taking it to around 2m homes in the region

The English-language arm of Arabic news channel Al Jazeera has launched on a US cable network in New York.

At midnight last night, Al Jazeera English (AJE) began broadcasting on US network Time Warner Cable, taking it to around 2 million homes in the region.

Six months on from the eruption of widespread protest across the Middle East, the agreement follows the most high-profile period in the history of the Qatar-based news channel.

In the immediate aftermath of the uprisings, some US media commentators – including Jeff Jarvis – called for US cable networks to add Al Jazeera, claiming that it was "downright un-American not to". AJE was at that point only available online to viewers in the US.

AJE's Arabic sister channel has been viewed with suspicion by the US, and was criticised by George Bush during his presidency after airing video messages from Osama Bin Laden. Its newsrooms were also bombed by the US in both Afghanistan and Iraq, although US authorities claimed the strikes were mistakes.

AJE, on the other hand, won praise from the US administration for its coverage of the uprisings in the Arab world, with secretary of state Hilary Clinton saying that the channel was airing "real news".

"Viewership of Al Jazeera is going up in the United States because it's real news. You may not agree with it, but you feel like you're getting real news around the clock instead of a million commercials and arguments between talking heads and the kind of stuff that we do on our news, which is not particularly informative to us, let alone foreigners."

Al Anstey, managing director of AJE, told the New York Times that early meetings with US networks had been about trying to correct "myths and misconceptions" about the AJE, but that now they don't come up.

Anstey added that the channel, which receives some funding from the Qatari finance ministry, will not be seeking the per-subscriber fee common to most US cable channels. "Revenue is not our priority," he said. "It’s being seen."

SOURCE:Journalism.co.uk


Familia yenye furaha: Kushoto ni Baba mtoto Jordan (15),akifuatiwa na  mama mtoto Tia (14) na kichanga  Gracie,na nyuma ni babu kijana  Shem (29) na kulia ni bibi kijana  Kelly (30)

Kwa namna ilivyozoeleka,unaposikia "babu" au "bibi" unadhani pasi wasi kuwa mtajwa ni aliyekula chumvi nyingi,na huenda umri wake upo kwenye miaka ya 50 na kuendelea.Na sia ajbu ana mvi lukuki.

Hali si hivyo kwa Shem Davies,kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye wiki hii amekuwa "Babu Kijana Zaidi nchini Uingereza."Davies,ambaye hana kazi (unemployed),amefanikiwa kupata mjukuu baada ya bintiye wa kike aitwaye Tia (umri miaka 14!!) kujifungua mtoto aitwaye Gracie.
Baba na mwana:  Shem na mwanaye Tia na kijukuu Gracie

Kuzaliwa kwa Tia (miaka 14 iliyopita) ni matokeo ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Shem na mwandani wake wa zamani aitwaye Kelly John mwenye umri wa miaka 30 sasa.

Kuchanganya madawa zaidi,kijana aliyezaa na Tia (mama mtoto mwenye miaka 14) naye ni serengeri boy wa miaka 15 tu!Kwa jina anaitwa Jordan Williams (pichani chini akiwa na mzazi mwenzie na kichanga chao)

Kwahiyo mjukuu amepatikana kwa mama mwenye miaka 14 na baba mwenye miaka 15,na ana babu wa miaka 29 na bibi wa miaka 30!

Lakini ukiangalia kwenye picha zinazoambatana na habari hii itakuwia vigumu kutambua umri wa wahusika wa Isidingo hii.Tatizo ni kwamba ni vigumu sana kukadiria umri wa hawa "wazungu."

Uingereza ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mabinti wanaojifungua kabla ya kutimiza miaka 18.

CHANZO: Daily Mail


Rushwa Inavyoua Elimu ya Watoto Wetu

CHANZO: Haki Elimu


MAPENDEKEZO YA MASHIRIKA YA KIRAIA JUU YA MUSWADA WA SHERIA YA MAPITIO YA KATIBA, 2011.

The Biggest Spending Tanzanian Embassies 

- Budget 2011/12

A Rapid Analysis of the biggest spending Tanzanian Embassies - Budget 2011/12
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation Budget 2011/12
  • UN Missions alone to spend 5,051,259,000/-
  • Missions in Europe and Moscow to spend 12,481,913,000/-
  • Embassies in four EA capitals allocated 3,746,956,000/- 
  • The Africa allocation is 10,945,095,000/-
  • Administration costs nearly half of ministerial vote
  • Salaries for London mission the highest (Pensionable posts & non-pensionable) at 868,142,918/- and Kigali the lowest at 80,201,559/-

Programme 20 - Diplomatic MissionsTshs
Permanent Mission to the UN - New York2,882,502,000
Permanent Mission to the UN - Geneva2,168,757,000
Embassy of Tanzania - Paris2,133,493,000
Embassy of Tanzania - London2,009,942,000
Embassy of Tanzania - Moscow1,907,166,000
Embassy of Tanzania - Rome1,891,547,000
Embassy of Tanzania - Berlin1,776,946,000
Embassy of Tanzania - Washington DC1,714,958,000
Embassy of Tanzania - Abu Dhabi1,710,597,000
Embassy of Tanzania - Tokyo1,662,626,000
Embassy of Tanzania - Nairobi1,625,277,000
Embassy of Tanzania - Brasilia1,532,748,000
Embassy of Tanzania - Brussels1,465,353,000
Embassy of Tanzania - Ottawa1,367,032,000
Embassy of Tanzania - Beijing1,352,422,000
Embassy of Tanzania - Stockholm1,297,466,000
Embassy of Tanzania - Pretoria1,269,178,000
Embassy of Tanzania - New Delhi1,215,144,000
Embassy of Tanzania - Kuala Lumpur1,160,872,000
Embassy of Tanzania - Riyadh1,156,879,000
Embassy of Tanzania - Addis Ababa892,277,000
Embassy of Tanzania - Maputo873,151,000
Embassy of Tanzania - Kampala822,513,000
Embassy of Tanzania - Kinshasa797,422,000
Embassy of Tanzania - Abuja778,726,000
Embassy of Tanzania - Muscat765,066,000
Embassy of Tanzania - Harare722,034,000
Embassy of Tanzania - Lusaka692,592,000
Embassy of Tanzania - Bujumbura659,258,000
Embassy of Tanzania - Kigali639,908,000
Embassy of Tanzania - Cairo595,191,000
Embassy of Tanzania - Lilongwe577,568,000
TOTAL Programme42,116,611,000
Administration Programme 1038,486,246,000
Total of Vote 34 80,602,857,000
Less Retention Scheme funds14,872,492,146
Net total of vote65,730,364,854
 


Idd Simba aitabiria kifo CCM

• AKERWA NA MALUMBANO NDANI YA BUNGE

na Waandishi wetu

MWANASIASA mkongwe nchini, Idd Simba, amekitabiria kifo Chama cha Mapinduzi (CCM) endapo hakitachukua hatua za haraka kudhibiti makundi yaliyo ndani yake ambayo mengi yanatokana na baadhi wanachama kuanza mapema mbio za kukimbilia Ikulu wakitaka urais.

Idd Simba, mwenyekiti wa baraza la wazee wa mkoa wa Dar es Salaam alisema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kufungua semina ya maimamu na wanazuoni wa Kiislamu, iliyofanyika katika hoteli ya Starlight, Dar es Salaam.

Alisema makundi yaliyojengeka ndani ya CCM yamesababisha chama hicho kupoteza kuaminika na wananchi hali ambayo inahatarisha amani nchini.

Alisema kutokana na hali hiyo moja ya mkakati wa kwanza wa baraza la wazee wa mkoa wa Dar es Salaam ni kuhakikisha linadhibiti hali hiyo ili kuweka mazingira mazuri ndani ya CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Pamoja na mambo mengine, aliwaonya wanachama wanaojiundia makundi ya mtandao kwa kuelekeza nguvu zao za kuelekea Ikulu badala ya kukisaidia chama kuwa imara mbele ya wananchi.

“Kupoteza mwelekeo kwa chama chetu kunatokana na makundi ya watu ambao wana nia ya kukimbilia Ikulu na hali hii sisi wazee wa mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na wenzetu nchi nzima tumejipanga kuthibiti hali hii.

“Kila anayesema hivi sasa anamtolea mfano Mwalimu Nyerere, sasa hayupo nani anayeendeleza na kukienzi chama kama ilivyokuwa wakati wake? Ili kuondokana na tabaka hili sisi wazee tunajipanga kukishauri chama kama kunatokea matatizo kama ilivyo sasa wazee tuweze kushauri kwa maslahi ya chama na wanachama kwa ujumla pamoja na kujenga misingi imara ya uzalendo na siasa zilizotukuka ndani na nje ya CCM,” alisema Simba ambaye amepata kuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu.

Alisema ili kujenga misingi imara lazima siasa ndani ya CCM, zijengwe na watu hasa kwa kuongozwa na itikadi kama aliivyokuwa ikisimamiwa na Mwalimu Nyerere na wasaidizi wake.

“Sisi wazee na wanachama wote wa CCM tusiposimama imara kuna hatari ya chama kupoteza mwekelekeo; sasa juhudi zinazofanywa za kurudisha misingi ya chama na mwenyekiti wa taifa, Rais Jakaya Kikwete, na sekretarieti tunahitaji kusimamia na kukomesha makundi yanayokitafuna chama ndani,” alisema Simba.

Hali ya kisiasa nchini

Akizungumzia mwenendo wa kisiasa alisema hivi sasa amani imekuwa ikivurugwa na vyama vya siasa kutokana na kila chama kutanguliza utashi na maslahi ya chma husika kuliko wananchi na taifa kwa ujumla.

Alisema malumbano yanayotokea mara kwa mara bungeni, siku moja yanaweza kuwaingiza wananchi barabarani kwa kuhisi wawakilishi waliowachagua hawana tija kwao.

“Haya yanayoendelea hivi sasa bungeni ni ya kusikitisha sana kwani hivi sasa muhimili muhimu wa Bunge unayumba na hata kukosa mwelekeo kutokana na baadhi ya wabunge kuona pale ni jukwaa la kisiasa.

“Huwezi ukawa na wabunge wenye kuonyesha ufundi wa kuzungumza na kila mara mwongozo wa Spika au taarifa wakati hivi sasa Watanzania wanahitaji kutatuliwa matatizo yao na watunga sheria hao,” alisema mwenyekiti huyo wa wazee wa mkoa wa Dar es Salaam.

Amani ya nchi

Kuhusu suala hilo, Simba ambaye alikuwa waziri katika utawala wa awamu ya tatu kisha baadaye kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi Taifa, alisema hivi sasa amani ya nchi iko shakani kutokana na kauli za viongozi wa vyama vya siasa wanazozitoa katika Bunge na mikutano yao ya kisiasa.

“Kila mbunge au kiongozi ametanguliza maslahi yake binafsi kwa kugombea vyeo vya uwakilishi na kulumbana kupitia Bunge kuliko watu waliomchagua huku akisahau lilolompeleka pale, kwa hatua hii kuna kila dalili za kuchafua amani yetu,” alisema Simba.

CCK yasikitishwa na Bunge

Katika hatua nyingine, Chama cha Kijamii (CCK), kimesema Bunge limepoteza heshima kutokana na wabunge kusimama kutetea maslahi ya vyama vyao na kusahau wananchi ambao walichagua serikali yao kukaa madarakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa CCK, Renatus Muabhi, alisema kuwa kupoteza heshima kwa Bunge kumetokana na wabunge kuwakilisha vyama na kuacha wananchi wakiwa hawana imani na serikali yao katika kupata maisha bora.

Alilaani wabunge kutohudhuria kwa wingi bungeni hali inayosababisha wabunge wanaopitisha bajeti kuwa wachache hivyo kuwafanya wananchi wengi kukosa kuwakilishwa ipasavyo.

Dowuta yatoa tamko

Wakati huo huo, Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA) kimesema Buge la sasa limekosa dira na kutokana na hali hiyo kuna haja ya kuwepo kwa chuo kinachofundisha uongozi kabla ya watu hao kuteuliwa katika nafasi za uongozi.

Akizungumza na Tanzania Daima, ofisini kwake mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa Dowuta, Abdallah Kibunda, alisema Bunge la sasa linatia aibu machoni mwa jamii hivyo kulifanya kukosa dira.

“Bunge la sasa ni la ghasia tu, wabunge wamejisahau kwani badala ya kujadili masuala ya maendeleo wanalumbana bila mpango wakati malumbano yalishaisha wakati wa kampeni
“Hao ni wawakilishi wa wananchi hivyo hawana budi kujirekebisha. Hata hivyo suala la uongozi linahitaji taaluma na kungekuwa na chuo ambacho moja ya sifa ni viongozi wakiwemo mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wengine kupitia huko kabla hawajateuliwa ingekuwa vizuri,” alisema Kibunda.

Alisema malumbano hayo hayawanufaishi wapigakura kwani asilimia kubwa ya wapigakura si wanachama wa CCM, CHADEMA, CUF wala TLP bali waliwapigia kura wabunge hao kutokana na kunadi sera zao kwao wakitegemea watapata maendeleo lakini kinyume chake wabunge hao wamekuwa wakilumbana siku hadi siku badala ya kupaza sauti zao bungeni kusaidia kuondoa kero za wananchi.

Alisema kwa hali hiyo wabunge hawana budi kurekebisha mara moja tabia hiyo kabla haijaleta athari zaidi.

Kwa mujibu wa katibu huyo, mkutano huo wa Bunge ni muhimu kwa sababu unajadili maendeleo ya taifa yakiwemo ya wafanyakazi katika kukuza uchumi wa taifa ili kukuza uchumi.

Alisema badala ya wabunge hao kujadili matatizo ya wafanyakazi kama vile mazingira mabovu ya kazi waliyonayo, kukatwa kodi na mengine badala yake kila mtu anafanya jambo analojisikia.

Alitoa rai kwa wabunge kufanya kazi kwa hekima, umakini na busara wawapo bungeni kwa maslai ya taifa.



يجوز للشهر الكريم من وحي القرآن الحاجب عليكم السلام والسعادة والازدهار

30 Jul 2011


Mitandao ya jamii ya Facebook na Twitter imetengeneza kizazi kinachoendekeza umimi kupita kiasi kiasi kwamba watu hawajali masuala mengine huku wakiwa na tamaa kama watoto wadogo kuona watu wanasema mazuri kuhusu wao,picha zao,wanayoandika kwenye mitandao hiyo,nk.

Kuendelea kuwepo kwenye mitandao hiyo kwa muda mrefu kunamwacha mtumiaji akiwa na mgogoro wa kujitambua (identity crisis),tamaa ya kutambulika katika namna ileile mtoto mdogo anamwambia mzazi wake, "Mama,nimefanya hivi."

Baroness Greenfield,profesa wa taaluma ya madawa (pharmacology) katika Chuo Kikuu cha Oxford,anaamini kuwa kukua kwa urafiki wa mtandaoni-sambamba na matumizi makubwa ya michezo ya kompyuta-vinaweza kupelekea kuuchanganya ubongo.

Hii inaweza kusababisha upungufu kwenye kukazani mambo ya muhimu,hitaji la kutamani kusifiwa na uwezo mdogo wa mawasiliano yasiyohitaji kutumia maneno (non-verbal communication) kwa mfano kumwangalia mtu usoni wakati wa maongezi.

Zaidi ya watu milini 750 duniani wanatumia mtandao wa Facebook kuonyeshana picha na video na mara kwa mara hubandika maelezo kuhusu mienendo na mawazo yao.

Mamilioni pia wamejiunga na mtandao wa Twitter ambao huwawezesha watumiaji kusambaza ujumbe mfupi na picha kuhusu wao wenyewe.

Baroness Greenfield,mkurugenzi wa zamani wa taasisi ya utafiti ya Royal Institution alisema, "kinachonipa wasiwasi ni ile hali ambapo unaweza kutarajia mtu atawaza au kusema nini ambayo ni hali ya kawaida huko Twitter."

"Kwanini mtu ahitaji kujua umekula nini wakati wa kifungua kinywa?Inanikumbusha jinsi mtoto mdogo anavyosema, 'mama angalia ninachofanya' "

"Ni kama mgogoro wa kujitambua.Kimsingi,hali hii inaufunga ubongo kwenye kuhusisha wakati/muda"

Mwanataaluma huyo alidai kuwa baadhi ya watumiaji wa Facebook wanajisikia wanapaswa kuwa "watu maarufu wadogo wadogo" (mini celebrities) ambao wanaangaliwa na kunyenyekewa na watu wengine kila siku.

"Wanafanya vitu vinavyoendana na Facebook kwani njia pekee wanayoweza kutumia kujitambulisha kwa umma ni kwa kuwafahamisha watu wengine kuhusu kinachoendelea kwenye maisha yao."

"Ni kana kwamba watu wanaishi katika dunia isiyo halisi bali dunia ambayo kinachomata ni nini watu wanafikiria kuhusu wewe au kama wanaweza kubonyeza kwenye picha au ulichoandika," alisema Profesa huyo.

"Fikiria kuhusu madhara kwa jamii ikiwa watu wanajali zaidi kuhusu nini watu wengine wanafikiria kuhusu wao kuliko nini wanachofokiria kuhusu wao wenyewe."

Mawazo ya mwanazuoni huyo yaliungwa mkono na Sue Palmer,mtaalam wa fasihi andishi na mtunzi wa vitabu,ambaye alisema kuwa wasichana hususan wanaamini wao ni bidhaa ambayo lazima iuzwe kwenye Facebook.

Alisema: 'Watu walizowea kuwa na picha ya kuchora (zinazowaonyesha wao) lakini sasa tunaweza kujichora wenyewe mtandaoni.Ni kama kuwa mshiriki kwenye shoo yako mwenyewe ya TV ambayo umeiunda na kuiweka hadharani kwa dunia kuiona.'

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.