23 Feb 2012


By Joyce Joliga
The Citizen Correspondent
Songea. Police in Songea allegedly shot dead four civilians yesterday, during a fracas associated with a public demonstration against a reported string of murders over the past four months, that the law enforcement organ is accused of neither curbing nor resolving.In a quick rejoinder, however, Ruvuma Regional Police Commander Michael Kamuhanda put the figure of those who had died at two.  

Several other people were injured when police officers used tear gas and live ammunition to quell angry demonstrators, some of whom had stormed the town’s main police station.The Ruvuma regional hospital chief medical officer, Dr Benedicto Ngaiza, confirmed that the hospital  had received four bodies and about 20 injured persons. 

He said two of the bodies had bullet wounds, and  two of the injured persons had bullet injuries  as well, and were rushed to the theatre for operations. All the bodies were delivered by the police,  he explained, adding that, one of them was that of a motorcyclist who had  accidentally hit a tree while speeding  away from the fracas.
Since November last year, nine people have been murdered in the town – a roughly monthly average of two –  some of whose bodies had been mutilated.

The trend has triggered much panic and anger amongst wananchi, who are in the dark over whether the crime is the work of a serial killer or a gang. Worrisome, too, is that, so  long as  the motives of the murders are not known, anyone was a potential next victim.

Chaos  and confusion reigned in Songea for a couple of hours yesterday, as most of the normal  official, business and social activities came to a standstill, as  much attention was  focused on the drama featuring chanting and stone-throwing demonstrators and law enforces who strived to restrain them.

Government offices,  the regional hospital, shops,  and the main bus stand, were among the  sensitive facilities that were temporarily closed and reopened only after relative calm had been restored.

The closures were  prompted by fears by  many people over  being caught in the cross-fire,  or falling victim to looters and petty thieves, since amongst the presumed demonstrators were  people who wielded crude weapons like iron bars.

Many people scattered in various directions towards safer places away from  the procession route, including crew  and passengers awaiting long distance  bus trips. Guards at the regional hospital closed the gates  of the facility as a precaution, as they couldn’t  establish whether  all the people in the huge crowd  that pleaded to be  allowed in were seeking protective shelter, or whether some  were thugs.

 The procession towards the police station  that started early in the morning, attracted hundreds of people marching on foot as well as motorcyclists in slow motion. The crowd swelled as word spread to various parts of the town and more people joined in.

Reports say that  the police fired live ammunition in the air and lobed teargas canisters into the crowds in a bid to restrain them, but, some amongst them continued pushing relentlessly into the police  station compound.

It was at that juncture that the police fired directly  into the crowd, killing two of the protestors, according to RPC Kamuhanda,  who explained that they had refusing to heed orders aimed at preventing a breach of peace. Mr Kamuhanda said investigations had been launched, but  hinted that initial indications pointed to  superstitious beliefs and politicking as causes of the chaos.

The Ruvuma Regional Commissioner, Mr Said Mwambungu,  expressed  dismay over the incident, and appealed to wananchi to remain calm while the Police was continuing with efforts to track down the  perpetrators  of the murders that had fuelled their anger.

He appealed  to Songea residents to avoid walking alone at night, especially if they didn’t have important engagements  that warranted taking risks.

In the evening, Mr Mwambungu chaired a crisis meeting of the regional peace and security committee, to chart  strategies  for containing the mysterious killings.

SOURCE: The Citizen


Chuck D,mwanzilishi na kiongozi wa lilikouwa kundi maarufu la rap huko Marekani,Public Enemy,aliwahi kusema muziki wa rap ndio CNN ya mtaa.Tangu awali,muziki wa rap umekuwa ukizungumzia masuala mbalimbali yanayoikabbili jamii-kutoka ukimwi,mihadarati,ubaguzi wa rangi hadi sera za ndani na za nje.Na sasa tunashuhudia baadhi ya wasanii wetu wakipata mwamko kama huo wa Public Enemy.Ushuhuda ni huu hapa chini.Sahau kidogo kuhusu video na sikiliza ujumbe kwa makini



CHANZO: Dj Choka's Blog

21 Feb 2012


Kwa maelezo zaidi BONYEZA HAPA


It's your birthday and I can't be there
But I'll send you a special birthday wish and a little prayer
Have a happy birthday
I hope that all of your birthday wishes come true
May you have a great time today and find happiness in everything you do.










CHANZO: Jamii Forums

KWA MWENDENO HUU NDIO MAANA TUNASHUHUDIA "MAFURIKO YA WAWEKEZAJI" WANAOISHIA KUPORA AJIRA ZA WAMACHINA (KWA MFANO WACHINA).UKILINGANISHA FOMU HIYO HAPO JUU NA FOMU ZA KUOMBEA VIZA ZA KUINGIA NCHI KAMA UINGEREZA AU MAREKANI UTABAINI JINSI GANI HATUPO SERIOUS KATIKA MAMBO NYETI.

20 Feb 2012


WAPENDWA WATAZAMAJI WA TMTV.
 
TUNAPENDA KUWATANGAZIA KUWA KUTOKANA NA MATATIZO YA KIUFUNDI.
KUMEKUWA NA TATIZO LA KUINGIA KTK TV KATIKA SIKU CHACHE ZILIZOPITA.TATIZO HILO LINAENDELEA KUFANYIWA KAZI.
KWA SASA UNAWEZAENDELEA KUBURUDIKA NA TMTV KWA LINK HII  http://tmtv.eightzerodigital.com/player.php
TUNAWAAHIDI MAMBO MAZURI YANAKUJA,VIDEO KIBAO MPYA ZITAONGEZEKA KWA RAHA ZAIDI KAMA KAWAIDA 24/7 NON-STOP.


Familia ya JK yamkana aliyetoweka na mamilioni UVCCM 
Monday, 20 February 2012 07:38

Rais Jakaya Kikwete
Peter Saramba, Arusha
FAMILIA ya Rais Jakaya Kikwete imekana kuwa na nasaba na aliyekuwa Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilayani Simanjiro, Alhaj Omar Yufus Kariaki, anayetuhumiwa kutokomea na zaidi Sh26 milioni, mali ya jumuiya hiyo.

Dada wa Rais Kikwete aliyehudhuria harambee ya kuchangisha fedha hizo kwa mwaliko wa Alhaj Kariaki, Tausi Kikwete aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kitendo cha kijana huyo kujinasibu kuwa na undugu na familia yao, kililenga katika kujinufaisha isivyo halali.

“Ukweli ni kwamba kijana huyo siyo ndugu yetu hata kwa mbali. Kwanza yeye anatoka Kondoa, wapi na wapi na sisi Wakwere wa Bagamoyo, mkoani Pwani, Hatumfahamu kabisa kwenye ukoo wetu zaidi ya kufahamiana naye tulipokutana Hija,” alisema Tausi.

Alisema yeye na ndugu yake Mwanaisha Kikwete, walikutana na mtuhumiwa walipokwenda kuhiji Mecca, Saudi Arabia na baadaye kupeana mawasiliano yaliyowawezesha kuendelea kuwa karibu hata baada ya kurejea nchini.

Alisema baada ya kurejea, yeye na Mwanaisha waliendelea kuwasiliana na Alhaj Kariaki aliyeonyesha kuwa kijana mwenye upendo na busara zilizowavutia wao kutembelea nyumbani kwao, Kondoa kwa mwaliko wake.
“Ukaribu wetu ulifikia hatua ya sisi kutembelea nyumbani kwao Kondoa baada ya yeye kutualika. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kijana huyo si ndugu yetu wala hana nasaba yoyote na kina Kikwete.” alisisitiza Tausi.

Alisema ilipofika wakati wa  harambee ya kutunisha Mfuko wa Mradi wa Maendeleo ya Vijana wa Wilaya ya Simanjiro, kijana huyo akiwa Katibu wa UVCCM wilayani humo, aliwaalika yeye na Mwanaisha kwenda kutoa semina kwa vijana kuhusu mbinu za ujasiriamali na miradi midogo.

Kwa mujibu wa Tausi, semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano ya Hoteli ya Manyara Inn, iliyoko Mererani siku mbili kabla ya harambee iliyoongozwa na aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani katika Serikali ya Muungano.
Hata hivyo kauli hiyo ya Tausi inapinga na kauli yake ya awali kupitia simu mwaka jana, ambapo licha ya kukiri kumfahamu Alhaj Kariaki, pia alisema wana unasaba naye.

“Ni kweli mimi na Mwanaisha ni dada wa mheshimiwa Rais (Kikwete) pia ni ndugu wa karibu wa kijana huyo (Alhaj Kariaki). Lakini binafsi sina mawasiliano naye tangu awe diwani huko kwako Kondoa. Kwa kifupi sijawasiliana naye tangu tuachane Mererani,” alisema Tausi mwaka jana alipoulizwa kuhusu mtuhumiwa huyo.

Katika harambee hiyo iliyohudhuriwa na viongozi na watu kadhaa maarufu kutoka Mikoa ya Manyara na Arusha, Nahodha alichangia Sh2 milioni fedha taslimu  wakati aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Henry Shekifu akichangia 500,000.
Kwa sasa Shekifu ni Mbunge wa Lushoto.

Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Simanjiro, Kiria Laizer, alisema baada ya yeye kukabidhiwa mfuko wenye fedha mara baada ya harambee ambayo mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka naye alichangia Sh1.5 milioni, alikabidhi mfuko huo kwa katibu wake Alhaj Kariaki ambaye hadi juzi alipojitokeza baada ya gazeti hili kuripoti suala hilo.

Mwenyekiti huyo aliwataja wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya UVCCM wilaya walioshuhudia makabidhiano kati yake na katibu wake  kuwa ni Bonny Shongo na Paul Sipitet.

Laizer aliyetoa pongezi na shukrani kwa mwandishi na gazeti la Mwananchi kwa kufanikisha mtuhumiwa kujitokeza, alisema awali walikuwa wakihofia kufuatilia suala hilo kwa karibu kwa hofu kwamba mtuhumiwa ana undugu na familia ya Rais.

Alhaj Kariaki ambaye sasa ni Diwani wa Kata ya Kwa Delo wilayani Kondoa, aliibuka wiki iliyopita baada ya habari zake kuripotiwa katika gazeti hili.

Alikiri kutokabidhi fedha zilizopatikana kwenye harambee hiyo iliyofanyika Mei 9 mwaka juzi akidai sehemu ya fedha hizo amezitunza kwenye akaunti yake, akisubiri kumalizika kwa kile alichodai kuwa mgogoro baina ya viongozi wa CCM mkoani Arusha ili azikabidhi

CHANZO: Mwananchi

16 Feb 2012


Wafuateni kina Zitto, Januari Makamba

MAKALA katika toleo lililopita la jarida hili ilizua mjadala mrefu kwenye mtandao wa kijamii wa twitter kutokana na kunukuu matamshi ya Rais Jakaya Kikwete na utata kama wasifu uliopo kwenye mtandao huo ni wa Rais mwenyewe.
Katika makala hiyo niliandika kuwa “nilifanya mazungumzo yasiyo rasmi na Rais kuhusu mkanganyiko uliojitokeza kufuatia kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda juu ya nyongeza ya posho za wabunge.”
Baadhi ya wananchi hawakupendezwa na matumizi ya maneno ‘nilifanya maongezi na Rais...’ wakidai huko ni kupotosha ukweli. Pengine hali hiyo ilisababishwa na kasumba iliyozoeleka kuwa ni nadra mno kwa kiongozi (achilia mbali Rais) kufanya maongezi (hata yasiyo rasmi) na ‘mtu wa kawaida’ kama mimi.
Kwa upande mwingine, imezoeleka kuwa ‘maongezi’ ni pale tu mtu anapozungumza nawe uso kwa uso, kukuandikia barua, kukupigia simu au kukutumia SMS.
Maendeleo ya teknolojia yanayowezesha mazungumzo kufanyika kupitia mitandao ya kijamii kama twitter, facebook, google+, nk, bado ni kitu kigeni kwa wengi. Na si tu ni jambo geni kwa vile watumiaji ni wachache bali pia mazoea ya wengi wetu yanapeleka kuyaona mawasiliano ya aina hiyo kutostahili kuitwa maongezi.
Kimsingi, maendeleo katika teknolojia yamebadili kwa kiwango kikubwa jinsi habari zinavyokusanywa au/na kupatikana. Wakati kabla ya kuja kwa radio, runinga, simu, nk njia pekee ya kupata habari ilikuwa kwa kukutana uso kwa uso na chanzo cha habari, hali sasa ni tofauti kabisa.
Wakati kauli mbalimbali za viongozi wetu zinaendelea kupatikana kupitia mikutano yao na wanahabari au/na press releases, waandishi wengi wamekuwa wakifuatilia ‘kurasa’ za viongozi (na watu wengine maarufu) kwenye mitandao ya kijamii kwa minajili ya kupata habari.
Kadhalika, kuna nyakati viongozi hufanya maongezi na watumiaji wengine wa mitandao hiyo. Kwa mfano, huko twitter unaweza kumuuliza kiongozi swali (ili kufanya hivyo unapaswa kuandika jina analotumia kwenye wasifu wake likianza na tarakimu @) na yeye akakujibu.
Na hivyo ndivyo ilivyotokea kwangu. Nilimuuliza swali Rais Kikwete naye akanijibu. Sikuona ubaya wa kutumia ‘maongezi’ hayo (yasiyo rasmi) kwenye makala husika hususan kwa kuchelea kuonekana nimepandikiza maneno yangu binafsi kwenye habari hiyo.
Jambo la pili lililozua mjadala ni uhalali wa akaunti ya Rais Kikwete huko twitter. Kwa upande mmoja, baadhi ya watu walidai kuwa yote yanayoandikwa kwenye ‘ukurasa’ wa Rais hufanywa na timu yake ya mitandao ya kijamii (social media team).
Hoja hiyo inaingia akilini kwa sababu sote tunafahamu jinsi Mkuu wa Nchi anavyokuwa na majukumu mengi yanayoweza kumkwaza kufuatilia kila kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii, magazetini, nk. Hata hivyo, yayumkinika kuamini kuwa wasaidizi wa Rais waliokabidhiwa jukumu hilo (kama wapo) wanafanya hivyo kwa ridhaa ya Rais mwenyewe.
Hiyo ni kama jinsi taarifa mbalimbali zinapotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Mwandishi wa Habari wa Rais. Japo anayeandika na/au kusambaza taarifa hizo si Rais mwenyewe, ridhaa yake na ukweli kwamba kinachoongelewa kinamhusu yeye kunapelekea taarifa za aina hiyo kupokewa na umma kama kauli (au msimamo) ya Rais.
Mkanganyiko kuhusu akaunti ya Rais huko twitter unachangiwa pia na kukosekana na alama inayoashiria kuwa akaunti husika imehakikiwa na wamiliki wa mtandao huo wa kijamii (yaani kuwa verified).
Wakati Rais Kikwete anatajwa kuwa miongoni mwa viongozi wachache barani Afrika wanaoitumia mitandao ya jamii mara kwa mara, si yeye pekee ambaye akaunti yake ya twitter haijahakikiwa (kwa mfano, ya Rais Jacob Zuma na Yoweri Museveni pia zipo katika hali hiyo).
Lakini japo pengine ingependeza akaunti rasmi ya Rais inaonyesha alama ya verified na hivyo kuondoa ‘sintofahamu’ kuhusu mmiliki wake, ukweli kwamba licha ya Ikulu kutoikana, na miongoni mwa followers wake ni watu na taasisi zenye hadhi kwenye jamii (kwa mfano CCM, CHADEMA, na familia ya Kikwete mwenyewe) basi kwa sasa tunaweza kuamini kuwa akaunti hiyo ni yake.
Lengo la makala hii si kuendeleza mjadala huo ambao kwa hakika si wa muhimu kulinganisha na masuala mbalimbali muhimu kwa Taifa. Hata hivyo, unaweza kutupa fursa nzuri kutathmini nafasi ya teknolojia ya mawasiliano katika mwingiliano (interactions) kati ya watawala na watawaliwa au viongozi na wananchi.
Kuna ugumu mkubwa katika kupata taarifa rasmi kutoka taasisi za umma. Wahanga wakubwa wa tatizo hilo si waandishi wa habari tu bali pia watafiti wanaosaka takwimu kwa ajili ya tafiti zao na wananchi kwa ujumla.
Uzuri wa namna ya kutumia teknolojia kama ya mitandao ya jamii upo kwenye urahisi wa namna ya kuitumia. Mitandao kama twitter na facebook inafikika kirahisi kwa kutumia hata simu (ili mradi iwe na huduma ya intaneti).
Pasipo kujali ni kiongozi mwenyewe au wasaidizi wake wanaosimamia ukurasa husika mtandaoni, uwepo wa ukurasa huo unaweza kutoa nafasi nzuri kwa wananchi kuwasiliana na kiongozi husika, sambamba na kuepusha mkanganyiko unaoweza kujitokeza pindi kauli ya kiongozi inapowasilishwa na mtu mwingine.
Mfano hai katika hilo ni mkanganyiko uliojitokeza siku chache kuhusiana taarifa zilizohusu ongezeko la posho za wabunge.
Ninatambua kuwa kwa mwananchi wa kawaida kule kijijini (ambako uhaba wa huduma muhimu za jamii unaumiza kichwa zaidi ya suala kama intaneti) anaweza asione umuhimu wa kuhamasisha viongozi wetu kuitumia mitandao ya kijamii, ukweli ni kwamba njia yoyote itakayowezesha kuwaweka viongozi hao karibu na wananchi inapaswa kutiliwa mkazo.
Wenzetu katika nchi zilizoendelea wana sheria zinazolazimisha upatikanaji wa habari zenye maslahi kwa umma, kwa mfano, sheria ya uhuru wa kupata habari (Freedom of Information Act).
Kwa huko nyumbani, tatizo si kuwapo (au kutokuwapo) kwa sheria ya aina hiyo, bali utashi kwa upande wa watawala kuona habari zenye maslahi ya umma zinapatikana kwa wananchi pasipo vikwazo.
Sasa katika mazingira ambapo habari kutoka taasisi za umma au viongozi zinapatikana kama fadhila (badala ya kuwa haki ya msingi), kuwa na viongozi kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kusaidia sana kupunguza ombwe hilo.
Kwa kuwa Rais Kikwete (bila kujali ni yeye mwenyewe au wasaidizi wake) anaonekana kuwa ‘muumini mzuri’ wa matumizi ya mitandao ya kijamii, anaweza kuhamasisha watendaji wake na taasisi kuiga mfano wake.
Lakini kwa vile ‘mtoto hazaliwi akatambaa’ (kwa maana itachukua muda kabla mwingiliano wa viongozi wa/taasisi za umma na wananchi kwa kutumia mitandao ya kijamii haujaenea kwa kiwango kikubwa) bado kuna nafasi ya kutumia vyombo kama blogu za Kitanzania (ambazo idadi yake inaongezeka kwa kasi) kutimiza jukumu hilo.
Kwa sasa, njia pekee ya blogu kuwasilisha habari kutoka kwa viongozi au taasisi mbalimbali ni kwa kunukuu habari kutoka vyombo ‘vya asili’ vya habari (yaani magazeti, radio na runinga).
Kibaya zaidi ni ukweli kuwa tovuti za taasisi chache za umma (zilizoona umuhimu wa kuwa na tovuti) aidha haziwekwi habari mpya mara kwa mara au zimebaki kuwa anwani tu (kwa maana hazipatikani mtandaoni).
Ukienda kwenye blogu ya Ikulu (inayoendeshwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu) utaona habari ‘mpya’ ni mwanzoni mwa mwezi uliopita. Wakati viungo (links) ni kwa Wizara pekee, kuna video moja tu kwenye ukurasa wa video. Blogu hii ingeweza kabisa kuwa na kipengele cha maandiko ya Rais na/au Ikulu kwenye mitandao mingine ya kijamii (kama twitter na facebook), hiyo ingesaidia kuondoa mkanganyiko kama nilioubainisha awali.
Nimalizie makala hii kwa kuwapa changamoto viongozi wetu kuiga mfano wa baadhi ya wanasiasa kama Zitto Kabwe, Januari Makamba, Dk. Faustine Ndugulile, Dk. Hamisi Kigwangalla, Mo Dewji na John Mnyika (na wengineo wachache) ambao kama Rais Kikwete mwenyewe, wamekuwa mahiri katika matumizi ya teknolojia ya mawasiliano kwa kutumia mitandao ya jamii.
Licha ya kuwa nyenzo muhimu katika shughuli zao za kisiasa, mitandao hiyo inawaweka karibu zaidi na wananchi na kurahisisha upatikanaji wa habari zinazowahusu au zenye maslahi kwa umma.


14 Feb 2012

13 Feb 2012


Katuni kwa hisani ya KING KINYA na Global Publishers

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.