20 Apr 2012

Mtalii akijaribu  souvenir huko Brazil


Nchi yetu inaelekea kubaya japo asilimia kubwa ya Watanzania bado wanalichukulia suala hili kama mzaha.Ukimya,upole na kutochukua hatua madhubuti dhidi ya majambazi wanaofilisi nchi yetu ni kama tumewapa ruhusa ya kufanya wapendavyo.

Moja ya makosa makubwa yaliyofanywa na Watanzania wenzangu ni pale walipoamua kuiweka nchi yetu rehani kwa kumkabidhi urais Jakaya Kikwete.Miaka yake mitano ilitawaliwa na matukio yaliyoashiria bayana kuwa TUMELIWA.Lakini makosa yakarejewa tena mwaka juzi na kwa kumpa dhamana ya 'kumalizia alipoishia.'

Kwanini ninamlaumu Kikwete?Yeye ndiye aliyewateua majambazi hawa wanaotafuna raslimali zetu kana kwamba kuna ligi ya ufisadi.Majuzi,Rais alikabidhiwa Ripoti ya Ukaguzi wa Mahesabu ya Serikali,ambapo ndani ya ripoti hiyo kuna maelezo yanayoweza kukupa ugonjwa wa moyo.Ni wizi wa hali ya juu.Lakini badala ya kuchukua hatua,Kikwete huyooo safarini.Amekwenda Brazil kwa ziara ya siku tano.Mzururaji huyu ni nadra kupitisha mwezi bila kwenda ng'ambo.

sINTOFAHAMU YAKE KATIKA UTEUZI WA MAJAMBAZI NA SINTOFAHAMU YAKE KATIKA KUCHUKUA HATUA KALI DHIDI YA WABABAISHAJI ALIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUTUNGOZA NDIO CHANZO KIKUBWA CHA YOTE TUNAYOSHUHUDIA HIVI LEO.

Hebu soma habari ifuatayo ya kuchukiza.
Ufisadi wa mabilioni kila kona



Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo
NI KWENYE MAGARI YA SERIKALI,TANESCO,MALIASILI,MABILIONI YA JK,AFYA NA MISHAHARA HEWA
Daniel Mjema Dodoma na Fidelis Butahe
WABUNGE jana waliijia juu Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha za umma na ufisadi ulijitokeza kwenye taasisi zake mbalimbali katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.

Hasira za wabunge hao zilitokana na ripoti tatu za Kamati za Bunge; Mashirika ya Umma (POAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kuonyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi yaliyotumika katika nyanja mbalimbali ikiwemo mishahara hewa na mikataba mibovu.

Mbunge wa Longido (CCM), Michael Laizer alisema ni aibu kila mwaka kuwa na ripoti za wizi wa mali za umma lakini Serikali inakaa kimya.

Alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mmoja wa maofisa wake aliidhinisha Sh11 milioni kwa ajili ya matengenezo ya gari. “Labda Serikali imechoka sasa inafanya makusudi fedha za wananchi zinaliwa lakini yenyewe inakaa kimya. Serikali itujibu hizi fedha zinazopitishwa kila mwaka zinakwenda wapi?” alihoji Laizer

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya alisema Serikali inapaswa kuona aibu kwa kutekeleza pendekezo moja tu kati ya 12 yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Alihoji suala la mishahara hewa kuendelea kujitokeza huku Serikali ikikaa kimya na kila mwaka CAG anatoa ripoti yake… “Kuna vitabu vya halmashauri za wilaya ambavyo CAG hakuvikagua kwa kuwa havikuonekana vilipo, sasa hapo tunakwenda wapi? Kuna Sh8 bilioni hazikufika katika halmashauri husika zimekwenda wapi? Wabunge tunatakiwa kuhoji na kupewa majibu sahihi.”

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alisema sasa Tanzania imekuwa kama Saccos kwa kuwa fedha za umma zinatafunwa bila utaratibu huku vielelezo vikitoweka kusikojulikana.

“Wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, mawaziri walijaa bungeni ila sasa tunajadili hatima ya Watanzania hawaonekani. Wabunge tuwe kitu kimoja tuibane Serikali itueleze hizi fedha zimekwenda wapi?” alisema Nassari.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alisema chama tawala kisipokuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kitahukumiwa na vijana.

“Serikali ndiyo chanzo cha fedha kutafunwa… inakuwaje Naibu Waziri wa Maji anasimama na kuahidi mambo mengi wakati anajua wazi kuwa fedha za kutekeleza miradi hazipo?” alihoji.

Alisema mwaka 2015, utakuwa mgumu kwa CCM kwa kuwa wakati huo vijana watakuwa asilimia 85 na wanaweza kukinyima kura kutokana na Serikali yake kushindwa kusimamia masuala ya msingi ya maendeleo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliwataka wabunge kuacha kulalamika kwa kuwa wao ndiyo wenye rungu la kuishikisha adabu Serikali: “Tukilalamika wananchi waliotuchagua nao watatushangaa kwa kuwa wametutuma kuwawakilisha na si kulalamika.”

Alisema umefikia wakati wa wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni na kuwashughulikia mawaziri wa wizara husika ambazo zinaonekana kuwa tatizo.

Mbunge wa Mwibara (CCM), Alphaxard Lugola alimlipua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema alihusika katika uuzaji wa mali ya Serikali katika Kiwanja namba 10 Barabara ya Nyerere na kwamba anaingilia utendaji wa mashirika ya Serikali.

Alisema kuwa kiwanja hicho awali, ilikuwa kiuzwe kwa Shirika la Tanzania Motors chini ya Kampuni ya Mashirika Hodhi ya Umma (CHC) kwa Sh1.3 bilioni lakini baadaye Mkurugenzi Mkuu wa CHC alipewa barua kusitisha uuzwaji wa jengo hilo na kumtaka kuitisha mazungumzo upya na Morad Sadik, ambaye alikuwa akitaka kununua eneo hilo awali.

“Inakuwaje wizara inaingia utendaji wa taasisi au kampuni zilizopo chini yake?” alihoji.

Awali, baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu, Wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge; Zitto Kabwe (POAC), John Cheyo (PAC) na Augustine Mrema (LAAC), waliwasilisha ripoti za kamati zao zinazoonyesha kukithiri kwa vitendo vya ufisadi serikalini na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kamati ya PAC
Cheyo alisema kamati yake imebaini kuwapo kwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na kutaja Maonyesho ya Sabasaba, Nanenane na Utumishi kama sehemu ambako fedha hizo zilitumika.

Alisema mwaka 2009/2010 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitumia fedha za matumizi ya jumla ya Sh1.10 bilioni kwa ajili ya Maonyesho ya Nanenane ambazo hazikuwamo kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema hata matumizi ya Sh21.63 bilioni zilizotumika kuendesha Mfuko wa Kukwamua Wananchi kiuchumi maarufu kama ‘mabilioni ya JK’ hazikuwapo katika bajeti iliyopitishwa na Bunge. Alipendekeza kuwa ili kuondoa hali hiyo, mfuko huo unatakiwa kuwa na mtu au taasisi ya kuusimamia badala ya kuachwa bila usimamizi.

Alisema kuwepo kwa udanganyifu na ukwepaji kodi kumeisababishia Serikali hasara ya Sh15.4 bilioni na Dola 2.6 milioni za Marekani.

Alisema Wizara ya Maliasili na Utalii na ilipoteza Sh874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrabaha kwa mazao ya misitu.
  
Kuhusu magari ya Serikali, Cheyo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo ya lazima katika uendeshaji na ukarabati wa magari hayo. Hadi Juni 30, 2010 Serikali ilikuwa inamiliki magari yenye thamani ya Sh5 trilioni.

Alisema mwendelezo wa ununuzi wa magari unaofanywa na Serikali unaongeza gharama za uendeshaji na kusisitiza kwamba matumizi hayo si ya lazima kwa Serikali yenye uchumi mdogo uliozidiwa na madeni.

Kuhusu ukaguzi wa magari uliofanywa na wakala chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), PAC imependekeza kuwajibishwa kwa ofisa masuuli wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuisababishia Serikali hasara ya Dola 18,343,540 za Marekani ambazo ni karibu Sh30 bilioni na kusisitiza: “Sh30 bilioni zilitumika kufanyia ukaguzi wa magari ambao haukuwepo.”

Alisema pia wamegundua kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kukodi majengo ya wizara na kusisitiza kuwa moja inaweza kulipa kodi ya Sh485 milioni.

Alisema kuna watumishi hewa takriban 3,000 na kwamba Serikali haifahamu lolote kuhusu hali hiyo… “Kuna Sh1.8 bilioni ambazo hutumiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa watumishi hewa. Pia imebainika kuwa Serikali haijui thamani ya majengo yake yaliyopo ndani na nje ya nchi.”

POAC

Zitto kwa upande wake, alielezea maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi ya fedha ambayo yanahusisha ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake.

Alitola mfano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo kwa mwaka mmoja wa fedha linafanya ununuzi wenye thamani ya kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2009/2010, Tanesco  ililitumia Sh1.8 bilioni ukilinganisha na Sh65 milioni zilizokuwa zimepangwa katika bajeti ya ukarabati wa gati mojawapo katika Kituo cha Bwawa la Mtera. 

“Ongezeko hilo la gharama za ununuzi kwa ajili ya ukarabati, ni kiasi kikubwa na Kamati haikuridhika na majibu ya menejimenti hivyo kuagiza uchunguzi wa ndani ili kubaini uhalisia wa ununuzi huo,”alisema na kuongeza:

“Tumependekeza Tanesco ianze kutumia vyanzo vyake vya umeme na iache kununua umeme hasa wa kampuni ya IPTL kwani inatumia Sh62.4 kununua umeme katika kampuni hii kwa mwaka.”
  
Alisema Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (MUCE) kilishindwa kuthibitisha kwa wakaguzi wa hesabu uwepo wa vifaa vya maabara vilivyonunuliwa ambavyo vina thamani ya Sh267 millioni.

Katika ripoti hiyo, Zitto alisema imebainika pia mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), na Kampuni ya Startimes unatakiwa kupitiwa upya ili uinufaishe TBC.

Pia aliugusia matumizi mabaya ya fedha katika Bodi ya Pamba ambako alisema kuwa kiasi cha Sh2 bilioni zilizotolewa na Serikali hazijulikani zilipo na wala hazikuwafikia wakulima wa zao hilo.

LAAC

Kwa upande wake, Mrema aliitaka Serikali ivunje mtandao wa wezi wa mali za umma na kuhoji inakuwaje inawakumbatia mafisadi?
Alihoji majalada ya watuhumiwa wa ufisadi kukaa zaidi ya miaka 10 katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) na ile ya Makosa ya Jinai (DCI) wakati kesi za uchaguzi zimewekewa kikomo.

Alisema ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2010, inaonyesha kuwa Sh583.2 milioni zililipwa kama mishahara hewa kiasi ambacho alisema kingetosha kujenga madarasa 194.

Mrema alisema katika ripoti hiyo, imebainika kwamba Sh8 bilioni zilitumika katika ununuzi usiokuwa na nyaraka na ama wenye nyaraka pungufu hali inayoashiria kuwapo kwa wizi.

Aliwataja watumishi wa Halmashauri ya Kishapu akisema ni vinara wa ubadhirifu wa Sh6 bilioni na kudai kuwa walishirikiana na baadhi ya watumishi wa Benki ya NMB Tawi la Manonga, Shinyanga kuiba fedha hizo za umma.

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Mweka Hazina, Muhdin Mohamed, Mtunza Fedha wa Halmashauri hiyo, Walugu Mussa, Boniface Nkumiming na Mhandisi wa Halmashauri, Leonard Mashamba.

Alisema fedha hizo zilitafunwa kwa kutumia nyaraka feki, uhamisho wa fedha bila idhini na kuzitumia kinyume cha malengo, uhamisho wa fedha ambao haukufika kwenye akaunti husika na malipo kwa walipaji wasiofahamika.

Mrema aliilaumu Serikali kwa kuwahamisha kutoka halmashauri moja kwenda nyingine na Serikali Kuu, watumishi wanaotuhumiwa kwa ufisadi badala ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Kamati hiyo imependekeza Bunge likubali kuitaka Serikali kutoa maelezo ya kuridhisha ni kwa nini ubadhirifu huo umeachwa ukishamiri kwa miaka mitatu mfululizo bila wahusika waliotajwa na CAG kuchukuliwa hatua.

“Shida iliyopo hapa ni Serikali kuonekana inawakumbatia wahusika kwa kisingizio cha uchunguzi unaendelea… nini kinachochunguzwa badala ya kupeleka watu mahakamani na kumuita CAG kama shahidi?”


CHANZO: Mwananchi


CAG na madudu ya taasisi zetu

Raia Mwema Ughaibuni
Uskochi
NIANZE kwa kutoa samahani kutokana na safu hii kutoonekana katika matoleo mawili yaliyopita. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo.
Makala ya wiki hii inalenga kuamsha tafakuri kuhusu taifa letu na hatma yake. Na pengine njia mwafaka ya kuanzisha tafakuri hiyo ni kwa ‘mchapo’ ufuatao (ambao nilishawahi kuutumia huko nyuma).
Miaka machache iliyopita nilipokuwa safarini kutoka jijini London kuja huku Uskochi nilipata nafasi ya kuzungumza na babu mmoja wa Kiskochi ambaye aliwahi kuishi huko nyumbani Tanzania pamoja na sehemu nyingine mbalimbali za Bara la Afrika.
Maongezi yetu yalilenga zaidi katika tofauti zilizopo kati ya nchi za Afrika na Ulaya, na hususan kati ya Tanzania na Uingereza. Na moja ya maswali aliyonidadisi babu huyo, na ambalo linaendelea kunigusa hadi leo, ni hili: kwa nini nchi yangu ni masikini licha ya utajiri mkubwa ilionao?
Katika ‘kujitetea’ nilikimbilia hoja ya kuwalaumu wakoloni, nikajitutumua na kudai kwamba laiti mkoloni asingekuja Afrika basi huenda bara hilo lingeweza kuwa na kiwango sawa (au zaidi) cha maendeleo kulinganisha na nchi kama Uingereza.
Lakini ‘utetezi’ wangu haukuwa na uhai mrefu kwani babu huyo alizidi kunitupia maswali yaliyopelekea nikose majibu ya maana. Kwa mfano, alikiri kwamba ni kweli ukoloni ulichangia kudumaza maendeleo ya Afrika lakini kwa nini hoja hiyo iendelee kutumiwa kama kisingizio takriban nusu karne tangu nyingi za nchi za bara hilo zipate uhuru?
Baada ya kuniona ‘ninatapatapa’ na sina majibu ya kueleweka, mzee huyo akaamua kunipa msaada kwa kubadili ‘maswali na majibu’ kuwa mjadala wa pande mbili. Alidai kwamba kwa mtizamo wake, tatizo kubwa linalozikabili nchi nyingi za Kiafrika lipo kwenye uongozi na wanaoongozwa (yaani wananchi).
Alieleza kwamba pengine atakuwa hawatendei haki viongozi wa Afrika kwa kuwalaumu  kwa kudumaa maendeleo ya nchi zao. Hoja yake ilikuwa kwamba wengi wa viongozi hao walifanikiwa kuingia madarakani kwa ridhaa za wananchi.
Kimsingi,  alikuwa anawalaumu wananchi wanaohadaika kuwachagua viongozi wabovu lakini badala ya kuwang’oa madarakani kila zinapojitokeza fursa za kufanya hivyo, wananchi hao wanaendelea kuhadaiwa. Babu huyo alidai kuwa takriban kila Mwafrika anayekutana naye analalamika kuhusu viongozi wa nchi yake, lakini ni nadra kusikia mtu mwenye angalau ufumbuzi wa tatizo la kulalamikia. Alieleza bayana kuwa matatizo ya nchi kama Tanzania hayawezi kuisha kwa lawama.
Akaeleza kuwa Uingereza ‘ya kisasa’ tuliyonayo leo ni matokeo ya jitihada zilizofanyika miaka mingi iliyopita. Mzee huyo akatanabaisha kuwa kwa mtizamo wake anaona nchi nyingi za Kiafrika zinaendeshwa kwa mihula ya utawala wa kiongozi (yaani kwa vipande vya muda) kiasi kwamba ni vigumu kubashiri hali itakuwaje kwa mfano miaka 50 ijayo.
Akanipa mfano wa jinsi mifumo ya reli za ardhini mijini (underground railways) na ule wa reli ya chini ya bahari unaounganisha Uingereza na Bara la Ulaya kupitia Ufaransa (Eurotunnel) ilivyotokana na mtizamo ya kuangalia miaka kadhaa mbele.
Akaeleza kuwa wengi wa Waingereza walioshiriki kubuni na kutekeleza miradi hiyo hawakuwa wakifikiria kizazi chao tu bali vizazi vingi vijavyo mbeleni.
Akaendeleza mjadala kwa kutupa lawama kwa viongozi wengi wa Afrika ambao aliwaita walafi na wasio na chembe ya uzalendo. Alibainisha kuwa ulafi wa viongozi hao huonekana bayana katika maisha yao ya anasa licha ya kuzungukwa na mamilioni ya wananchi ambao ni masikini kupindukia.
Kuhusu kukosa uzalendo alitoa mfano wa rafiki yake mmoja aliyejitolea kupelekea mradi mmoja wa maendeleo barani Afrika lakini serikali ya nchi husika ikamkwamisha kwa vile hakukubali kuwapa rushwa (haingii akilini kudai rushwa ili uruhusu usaidiwe).
Tukiweka kando maongezi yangu na babu huyo wa Kiskochi (ambaye tunaendelea kuwasiliana kujadili masuala mbalimbali ya Afrika, na hususan Tanzania), ni muhimu kwa kila mwenye uchungu na nchi yetu ajaribu kuangalia ni kwa namna gani anaweza kuchangia kubadili mwenendo wa mambo.
Majuzi, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, aliwasilisha ripoti kwa Rais Jakaya Kikwete, ambapo kama ilivyokuwa huko nyuma, imethibitika kuwa kuna ufisadi wa kutisha unaoendelea huko nyumbani.
Kilichonigusa zaidi ni changamoto aliyotoa Utoh kuhusu deni la Taifa ambalo limepanda kutoka shilingi trilioni 10.5 mwaka wa fedha 2009/10 hadi shilingi trilioni 14.4 kwa mwaka 2010/11, na misamaha ya kodi ambayo imeongezeka kwa takriban asilimia 49.
Ni vema tukafahamishana kuwa deni hilo la Taifa lina madhara kwetu na kwa vizazi vijavyo hasa ikizingatiwa kuwa badala ya kuwekeza nguvu kwenye kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, watawala wetu wanachuana kutuongezea mzigo huo.
Moja ya maeneo yanayoongeza mzigo huo  ni safari za viongozi wetu nje ya nchi. Tusiume maneno, moja ya mizigo mikubwa anayobebeshwa mlipakodi wa Tanzania inachangiwa na hizi safari zisizoisha za viongozi. Haiingii akilini hata kidogo kuona viongozi wa moja ya nchi masikini kabisa duniani wanakuwa ziarani nje ya nchi mara nyingi zaidi ya viongozi wa mataifa tajiri duniani kama Marekani, Uingereza, Ujerumani, Japan.
Hata kwa majirani zetu ambao wanatajwa kama ‘matajiri wanaochipukia Barani Afrika’ yaani nchi kama Rwanda na Msumbiji, viongozi wao hawasafiri mfululizo kama wa kwetu.
 Sawa, hata tukiafiki porojo kuwa inabidi wasafiri kwenda kutembeza bakuli huko nje. Lakini kama hilo ni la muhimu zaidi basi tufunge balozi zetu. Maana hata hizo balozi nazo zinatajwa katika takriban kila Ripoti ya CAG kama vinara wa matumizi yanayokiuka taratibu.
Awali niliposikia kuwa misamaha ya kodi imeongezea takriban mara dufu nikahisi labda ni katika utekelezaji wa sera ya Kilimo Kwanza (ambapo ni muhimu kutoa misamaha kwenye pembejeo zinazoingizwa nchini kuinua sekta ya kilimo) au katikaimports zinazolenga sekta muhimu za elimu, afya, nk. Kinachokera ni ukweli kwamba asilimia kubwa ya misamaha hiyo ilitolewa kwa mawaziri na wabunge.
Jamani, hawa watu wanaopata mishahara minono na posho lukuki wanapewa misamaha hiyo ili iweje? Au ndiyo yale yale ya ‘mwenye nacho ataongezewa na yule asiyenacho ataporwa hata kile kidogo alichonacho’?
Kama ambavyo yule babu wa Kiskochi alivyotahadharisha, tunaweza kukesha tukimlaumu huyu na yule lakini hali yetu inazidi kuwa mbaya huku wenzetu kama Rwanda wanamudu kutoka ‘kwenye majivu’ (mauaji ya kimbari) na kufikia hatua ya kuitwa economic tiger wa Afrika.
Tafakari. Chukua hatua.


13 Apr 2012


Go!go It’s My Birthdayyyy!!!

SISTER Stands For



S stands for sincerity, that your world is filled with,


I stands for innocence, of your mind that makes you so rich. 


S stands for strong, that describes your heart best,


T stands for talented, that makes you stand out from the rest. 

E stands for encouraging, just the way you always do,

R stands for rare, and my dearest sister that's true.

Happy Birthday to you! 





12 Apr 2012

Kisiwani Zanzibar walikusanyika kundi la watu katika baraza la wawakilishi wakitaka kuitishwe kura ya maoni.
Wananchi wa Zanzibar wataka kuitishwe kura ya maoni
Wananchi wa Zanzibar wataka kuitishwe kura ya maoni
Huko Zanzibar Tanzania, kundi la watu walikusanyika leo (11.04.2012) katika viwanja vya baraza la wawakilishi wakidai kuitishwa kura ya maoni kuhusu suala la Muungano kati ya iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar 1964 na kuundwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliopo hii leo.
Mohamed Abdul-rahman alizungumza na Rashid Hadi anayedaiwa kuwa kiongozi wa kikundi hicho na kwanza anaelezea sababu za kukusanyika kwao.
(Sikiliza maogezi hayo hapa chini)


Mwandishi: Mohammed Abdul-Rahman
Mhariri: Daniel Gakuba

11 Apr 2012

8 Apr 2012



Mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mzee Edwin Mtei, amezungumzia uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Kuratibu Maoni ya Katiba iliyotangazwa majuzi na Rais Jakaya Kikwete.Katika bandiko lake kwenye mtandao wa jamii wa Jamii Forums,Mzee Mtei amepongeza hatua ya Rais Kikwete kuteua Tume hiyo na hatua nzima ya kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba tuliyonayo sasa.

Hata hivyo,mwanasisasa huyo mstaafu ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu katika Serikali ya Awamu ya Kwanza,ameonyesha wasiwasi wake kuhusu muundo wa Tume hiyo huku akitafsiri kuwa muundo wa Tume hiyo unadhihirisha kuwa demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania.

Katika bandiko hilo,Mzee Mtei amehoji mantiki ya kukosekana uwiano halisi kati ya wajumbe wa Tanzania Visiwani na wale wa Bara kwa kuzingatia kigezo cha idadi ya watu,na akagusia pia kukosekana kwa uwiano wa imani ya kidini miongoni mwa wajumbe (yaani Waislam na wasio Waislam).

Tayari kauli hiyo ya Mzee Mtei inaelekea kuzua mjadala hata ndani ya Chadema,ambapo Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia chama hicho, Mheshimiwa Zitto Kabwe, amenukuliwa kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema, "Yeyote anayeangalia #TumeyaKatiba kwa misingi ya #Dini za wajumbe amefilisika kimawazo, ni kirusi dhidi ya Utanzania wetu. Azomewe"


Bandiko halisi la Mzee Mtei ni hili hapa chini (BONYEZA PICHA KULIKUZA)





7 Apr 2012

BREAKING NEWSSSSSSSSSSS: MUIGIZAJI STEVEN KANUMBA AFARIKI DUNIA

Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya wasanii wenzake wa filamu Steven Kanumba amefariki dunia usiku huu.

Kwa mujibu na hisani ya SHAFFIH DAUDA's BLOG

30 Mar 2012

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.