4 Sept 2012


Brooklyn Hip hop Festival




Wes Jackson, President and executive director of Brooklyn Hip hop festival in the middle Witnesz the Fitnes mkewe Ebonie Jackson ambaye yupo kwenye kitengo cha mahesabu ya shughuli kadhaa za mumewe ikiwemo Hip Hop Festival and Brooklyn Bodega





Brooklyn Bodega a complicated animal, creators of  BHF, Top notch blogazine (blog meets magazine) cultural programmers, Hip Hop Advocacy Group.

The bodega was founded in 2006 by Wes Jackson as the online home of the BHF , under the guidance of Bodega’s initial creative director and administrator James Blagden and Alma Geddy-Romeo.

The bodega grew into one of the most respected online destinations in the Hip Hop community Editorially, the Bodega  strives to add a more academic voice to the world of Hip Hop Journalism, It Derives deep into issue facing the Hip Hop community from music business to politics to technology and they offer a professional and intellectual voice.

Wes Jackson has over 15years experience as an entrepreneur and innovator in music business. His carrier began with producing concerts for Nas, The Roots, The Dave Mathews, band and de La Soul etc. He went on and started his own promotions company by the name seven Heads Promotions, seven Heads was instrumental in launching the career of MOs Def. ,Talib Kweli and others under Wes’ Leadership. Seven Heads expanded into a Record label and a management company, The record company that spun into the room Service Group (RSG) one of the leading digital marketing, RSG has worked with Def. Jam, Capitol, Warner Bros, Interscope, vivendi, and converse the list is endless.

 In addition to his successful business ventures Wes also serves as lecture at city University of New York (CUNY) Wes’s entrepreneurship spirit endure as he continues to grow the BHF into a world class event also as the Brooklyn Bodega Brand with the pop-up store Bbeats at DeKalb market in Downtown Brooklyn,

Wes aliweza eleza kiurefu zaidi juu ya biashara mjini New York kama mmiliki halisi wa hiyo Festival iitwayo Brooklyn Bodega na record label na mengineyo ambayo yote yanahusika na harakati za kihip hop zenye mafanikio makubwa up to date na kufafanua kibiashara zaidi mambo mbali mbali ikiwemo ujasiriamali na sababu za festival hiyo kutohusisha sana au kabisa wasanii kutoka nje wa Hip Hop,alisema wes kuwa wasanii wa hip hop Nchini New York wapo wengi mno mfano wa mafuriko na wote ni wa kali na kusbabisha eneo hilo kuwa hapatoshi hata kwa wakazi wenyewe so mtu yeyote akitoka nje ya nchi akitaka kuingia kwenye soko hilo ni lazima awe extra special, multitalented, unique na awe ni mchapa kazi mara tatu ya wasanii wa New York na ndivyo ilivyo kwa wanawake wanao fanya Hip Hop pia the half to beat men ambao they are flooded with extra energy has to be used In order to stay on the top of the game.
                                                                                                 
                                                                                                  
       Pia nilipata kujua maana ya neno Bodega kama ambapo iliwahi sikika kwenye moja ya nyimbo za Big punisher alipo sema my father’s Bodega kwenye intro na kufafanua ya kwamba neno Bodega ni la kispanish likimaanisha panapo tengenezwa wine, ama corner store mjini new york ambapo huuzwa wine,vilevi mbali mbali na vitu vyote vihusuvyo starehe ikiwemo urahisi wa kupata condoms hata nyakati za usiku huwa pako wazi masaa 24 siku saba za wiki 24/7 kwenye hiyo corner store  wanapatania ya kuwa ni an organized mess place,nikmrahisishia kwa kusema an organized place in a disorganized manner? akasema thats whats up kwa kuwa ukienda kwenye a corner store kulikuwa kuna taka taka karibia za aina zote anazohitaji mtu kwa nyakati za usiku na mchana na hutumika kama maskani na kupanga kuhusu mitikasi pamoja na kupeana mistari ma dj,rappers watu wa aina zote kwenye harakati walikuwa wakitia maguuhapo hata mkiwa hampatani mtaani mkifika hapo kila mtu huwa peacefull ni kiduka kona ambacho watu wa jinsia zote na kutoka pande zote kupata huduma,kwa upande wangu nilipata picha ya gengeni ambapo mara nyingi vijana hukaa hapo ndani ya bong na kuganga njaa ama wakihesabu magari ama kwa kuwalaghai mabinti hahahahaa!


 
                          So a lot of things happening at a bodega store you name it as the aim of the Brooklyn Bodega ambapo ndiye mama wa Hip Hop festival tamasha ambalo hufanyika kila mwaka mjini New York tangu lianze limekwisha fanya matamasha nane mpaka sasa na mwaka huu limekwisha fanyika ,ambapo watumbuizaji wa kuu walikuwa Buster Rhymes na Tribe called Quest na host Mkuu wa tamasha hilo miaka nenda miaka rudi akiwa ni Uncle Ralph.
                                                                                                                     Heshima Zizidi Kuendelea










31 Aug 2012


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemshukia Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kikisema kiongozi huyo si mwadilifu, si mwaminifu na mnafiki, akiwa ni mwakilishi na kielelezo cha mfumo uliooza katika serikali ya CCM uliolifikisha taifa hapa lilipo.
Kimesema kuwa tabia za Sitta hasa katika kuua mijadala ya kifisadi ndani ya bunge, kwa ajili ya kulinda maslahi yake binafsi ya kusaka vyeo, inamfanya asiwe tofauti na watuhumiwa wengine wa ufisadi ndani ya chama chake na serikalini, kikishutumu kuwa mlinda ufisadi na mafisadi ama ni naye ni fisadi kama wenzake au ni fisadi mkubwa kuliko mafisadi wenyewe.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Iringa jana Ijumaa, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibroad Slaa alisema kuwa Sitta hana uwezo wowote wa kukisema chama hicho wala viongozi wake, akimtaka amalize kwanza matatizo waliyonayo yeye na wenzake ndani ya CCM, likiwemo la kujivua gamba, ambalo linaonekana kuwashinda.

Katika mkutano huo chama hicho kilisema pia kuwa hatua ya polisi kuzuia mikutano ya Operesheni Sangara-M4C kwa siku tano, kupisha shughuli ya sensa, kumekisaidia chama hicho kugundua mbinu na mikakati mizuri ya kuwafikia wananchi kwa mikutano ya ndani, ikiwa ni maandalizi ya mikutano ya hadhara, hivyo kupata mafanikio zaidi mkoani Iringa kuliko ilivyokuwa mkoani Morogoro.

Sitta ni kielelezo

Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA ambaye aliwaambia waandishi wa habari kuwa amelazimika kumzungumzia mtu lakini kwa nia ya kuonesha alivyo kielelezo cha ubovu wa mfumo na uongozi wa serikali na CCM, alidai kuwa kwa sababu ya tabia ya unafiki aliyonayo Sitta, kiongozi huyo ni sawa na viongozi wengi wa serikali ya CCM akiwafafanisha na mbwa mwitu waliovaa ngozi ya kondoo.

“Nchi hii imefika hapa ilipo kwa sababu ya viongozi aina ya Sitta ambao hawasiti kusema uongo hadharani, wanafiki, hawana uadilifu, waongo, walio tayari kusaliti maslahi ya umma kulinda maslahi ya tumbo, Sitta yeye ana uzoefu gani, huu wa kulinda mafisadi bungeni kwa kupindisha hoja za ufisadi ili apate ubunge na uspika.

“Hivi Sitta atuambie anaposema CHADEMA haina watu wenye uwezo lini tuliwahi kusema tukiingia serikalini tutakuja na watu wetu wote au ndiyo yale mawazo ya kijinga kwamba CHADEMA wakishika nchi watapata wapi ikulu…atuambie kuna chuo kikuu chochote kinafundisha uwaziri au kuna chuo kikuu kinafundisha ukatibu mkuu wa wizara, asitupangie sisi namna ya kupata viongozi wetu.

“Hivi hajui kuwa Mwalimu alipopata nchi aliandaa watendaji. Hoja za kipuuzi, mtu akitoa hoja za kipuuzi, naye atakuwa mpuuzi tu wa kupuuzwa, tumefika hapa, nchi imegubikwa na uozo wa ufisadi kwa sababu ya mawaziri wa aina ya Sitta ambaye haogopi kuropoka hadharani, tena akiwatukana wapiga kura, ambao pia wengi wao ni vijana.

Hoja ya kuchezesha disko

“Anaposema Mbowe ni mchezesha disko anataka kupeleka ujumbe gani, anataka kusema nini…kwamba ni kosa, kwa hiyo anamaanisha wacheza disko ni criminals (watenda jinai), kwa hiyo wacheza disko ambao pia ni wapiga kura na wengi ni vijana ni criminals, je hajui kuwa kuna mawaziri wenzake wanaokesha pale Billicanas Club,” alisema Dkt. Slaa.

Aliongeza kusema kuwa hoja hiyo ya kumshambulia Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwa sababu ya kumiliki ukumbi wa mziki, kuwa nayo ni hoja mbele ya watu makini, Dkt. Slaa alisema waziri huyo amedhihirisha alivyo mbumbumbu wa sheria na hajui lolote, tofauti na ambavyo siku zote ametaka kuonekana mbele ya jamii.

“Ni dhahiri hana uzoefu wowote na hajui, ndiyo maana ameishia kwenda kuwatukana wapiga kura yeye akifikiri anaimaliza CHADEMA, maana wacheza disko ndiyo wapiga kura hao hao, lakini yeye kama msomi kweli, tena anasema ni mwanasheria, alipaswa aelewe kuwa duniani kuna nyumba za disko za staha, zimesajiliwa na zinafanya kazi kwa mujibu wa sheria na zimepewa leseni na serikali.

“Huyu Sitta kila siku anajiita yeye mwanasheria kumbe mbumbumbu kupindukia tu hana tofauti na wana CCM wenzake ambao jamii inawashangaa kwa matendo na kauli zao, ku-run club ni sawa na ku-run biashara nyingine yoyote, almuradi iendeshwe kisheria na kihalali, sasa kama anaona ni kosa aiambie serikali yake ifute leseni ya biashara hizo.

“Tulitegemea mtu ambaye anataka kuonekana ni mstaarabu, anahoji uzoefu wa wenzake nay eye anasema ana uzoefu angekuja na mawazo ya kupeleka nchi mbele kumbe yuko sawasawa tu na wenzake ndani ya CCM,” alisema Dkt. Slaa.

Ameingia kichwakichwa, kwenye tope

“Leo nalazimika kumzungumzia mtu, Watanzania wanajua mara chache sana CHADEMA huwa tunalazimika kuzungumzia watu badala ya masuala…lakini nitazungumza kwa namna ambayo huyo mtu atakuwa anawakilisha mfumo huu wa serikali ya CCM na chama chao jinsi ulivyooza na kutufikisha Watanzania hapa tulipo.

“Samuel Sitta ameingia kichwa kichwa kwenye matope ambayo hawezi kutoka wala kujinasua, muda mrefu tumemhifadhi lakini leo tutampiga ngumi za uso lakini kwa namna ambayo atakuwa anawakilisha mfumo huu uliooza…

“Ghafla tu ameamua kuibuka na kuzingumzia CHADEMA, badala ya kujenga chama chake, bila kujua amedhihirisha kuwa CHADEMA sasa ni tishio kwao, maana huwezi kuzungumzia kitu ambacho hakikuathiri, amedhihirisha namna ambavyo yeye wenzake sasa wanatapatapa kweli kwa sababu ya CHADEMA.”

Makombora zaidi; mlinda ufisadi na mafisadi

Dkt. Slaa alisema kuwa wakati chama hicho kilipoanza kuasisi hoja ya ufisadi nchini kikiwa mstari wa mbele kupiga vita kila aina ya ufisadi, Sitta wakati huo akiwa Spika wa Bunge, ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuweka vikwanzo na vizingiti akilinda maslahi yake nay ale ya chama chake, badala ya maslahi ya wananchi.


“Yeye ndiye aliyepindisha hoja ya Zitto katika kashfa ya Buzwagi ambapo waziri alikuwa amesaini mkataba uliokuwa kinyume kabisa na maslahi ya nchi, tena akasaini nje ya nchi hotelini. Zitto aliposimama bungeni, Sitta badala ya kuangalia hoja hiyo kwa maslahi ya nchi, yeye na wenzake akaipindua kuwa Zitto amesema uongo bungeni.

“Huyu bwana hastahili hata kuwa waziri, anajidai yeye mpiganaji na mpambanaji, wapi? Katika hoja ile nani alikuwa mpiganaji Zitto au Sitta, akapindisha makusudi hoja ya ufisadi mkubwa wa Buzwagi kulinda maslahi anayoyajua mwenyewe. Wakamfukuza Zitto bungeni kwa miezi minne, baadae kelele zilivyozidi huku nje, wakaamua kumrejesha bungeni kimya kimya baada ya mwezi mmoja tu hivi.

“Lakini pia ni Sitta huyu huyu alizima hoja ya ufisadi wa BoT, mambo yote yale ya EPA, Kagoda, Deep Green sijui nini kila kitu kilichokuwa kikihusu BoT. Mtakumbuka aliwatangazia Watanzania kuwa nyaraka za Dokta Slaa ni fake za kuokoteza kwenye internet na nitampeleka polisi, mpaka leo hakunipeleka. Lakini Sitta alikuwa anajua tangu mwanzo, kadri nilivyokuwa nikikusanya documents alikuwa anajua na nampatia copy, mpaka ikafikia ile document kubwa ya mwisho.

“Lakini kwa unafiki wake ameahirisha bunge Ijumaa, Jumamosi akachukua ile document na kwenda nazo TBC akisema ni fake na atanipeleka polisi, lakini leo yako wapi…sasa mtu wa namna hii hafai hata kuwa naibu waziri, mtu yeyote anayelinda mafisadi na ufisadi ni fisadi kuliko mafisadi wenyewe, nawaambia haya kwa sababu tumefika hapa kwa sababu ya kuwa na viongozi, wakiwemo mawaziri wanafiki na waongo kama hawa.

“Lakini ili mjue Sitta ni mtu wa aina gani na kwamba hastahili kuaminika na Watanzania, haikuishia hapo, ufisadi wa Richmond mnajua alivyomaliza mjadala ule kihuni bungeni. Hadi leo hoja ile haina majibu, wakati tunahoji bungeni akafunga hoja ile kidikteta, sasa tunauliza huo ndiyo uzoefu alionao yeye au walionao wenzake, uzoefu wa kulinda mafisadi na ufisadi wa CCM na serikali yao, lakini sisi tunajua kwa nini alipindisha hoja ya Richmond, wakati huo alikuwa anabembeleza ili ateuliwe kuwania ubunge na baadae uspika, mnaona huyu ni mtu wa kuaminika kweli?”

“Hivi kwa matendo ya aina hii Sitta anaweza kutoka nje na kusema yeye ni jasiri na mzalendo, katika majasiri na wazalendo wa kweli Sitta hana sifa hizo, ndiyo maana wameshindwa hata kuyavua magamba kama walivyosema, sasa aende kwanza kwenye chama chake na serikalini, asaidie kuyaondoa magamba kabla hajaanza kutafuta aibu ya kuanikwa zaidi,” alisema Dkt. Slaa.

Siri zaidi; Sitta haaminiki

Dkt. Slaa aliongeza kusema kwa kutoboa siri zaidi namna ambavyo, yeye na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbowe, walikuwa wakiendesha mazungumzo na Sitta wakati mwingine kwenye Ofisi ya Spika juu ya Sitta kuhamia CHADEMA na kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, akisema kuwa ulikuwa ni wakati ambapo waziri huyo pamoja na wenzake walipokuwa wameunda Chama Cha Jamii (CCJ) wakiwa bado wako CCM.

Alisema kuwa hata wakati huo bado Sitta alikuwa akionekana kutojiamini na maamuzi yake, ambapo wakati wa majadiliano ya kugombea urais, Sitta alisema kuwa kuna kundi la wabunge takriban 55 watiifu kwake ambao walikuwa tayari kuhama naye kumfuata CHADEMA. 

“Leo natoa siri ambayo sijawahi kuitoa, Sitta ni mhanini. Tumekutana naye mara 100 na zaidi, tumeandikiana vimemo bungeni vya kukutana, wakati mwingine tumekutana hata Speaker’s lounge, tumekutana na Sitta na Mwenyekiti Mbowe, ambaye leo anamwita ni mchezesha disko mara nyingi tu. Lakini hata wakati huo pia hakuonekana kuwa jasiri, maana alikuwa ana wasiwasi nani wanamfuatilia au nani wanamuona, si mtu jasiri hivyo. 

“Zikiwa zimebaki kama siku tano kabla ya kumaliza bunge la mwezi wa saba, kila nikimwandikia kimemo, hataki hata kunitazama, Sitta akayeyuka bila hata kutuaga, baadae CHADEMA tukaamua kutumia utaratibu mwingine na tukaweza kusonga mbele mpaka kufika pale tulipofika. Lakini baada ya uchaguzi akaja mwenyewe kunifuata akinishukuru sana na kunipongeza kuwa nilikuja na hoja tofauti kwenye uchaguzi akisema hata yeye asingeweza kufika tulipofika.

“Lakini hapo sasa tulishamshtukia na kugundua kuwa anataka kugombea uspika kupitia CHADEMA, nataka kuonesha namna huyu mtu alivyo mnafiki, mpotoshaji, nampatia challenge kama kweli yeye ni muumini mzuri akanushe haya, maana ametulazimisha kusema, kwa hoja zake za kupotosha watu na akumbuke, maana huwa anakwenda makanisani na anachanga mapesa, akumbuke maandiko yanasema, yeyote atakayepotosha wadogo hawa, anastahili kutoswa baharini, Makamu Mwenyekiti hapa ametumia Quran kufafanua vizuri,” alisema Dkt. Slaa.

“Maana kwa hakika anataka kupotosha watu ili waone kuwa kuchezesha disko ni suala lisilokuwa sahihi, huo ni upotoshaji, kama anataka kuonesha si sahihi mbona serikali yake hiyo hiyo inaendelea kukusanya kodi. Sasa ilipofikia kwenye suala la kugombea uspika, siku ile jina lake limekatwa kwa sababu walitaka mgombea mwanamke, alinipigia simu usiku wa saa tisa, bahati mbaya nilikuwa nimeweka simu silence, hakunipata.

“Saa 12 nikapokea simu ya mke wake, Margreth Sitta, anasema baba anakutafuta tangu usiku, anataka kuzungumza nawe, nikasema sawa, akaniambia Dokta Slaa wamenifanyia kitu kibaya sana, mimi nimeamua sasa nitagombea uspika kwa tiketi ya CHADEMA, najua umeshateua tayari mtu wa kugombea tayari, lakini naomba nikuhakikishie nafanya press conference saa 4 asubuhi leo, natangaza rasmi kugombea uspika kupitia CHADEMA. Nikamjibu CHADEMA maamuzi hayafanywi na mtu mmoja, nikamwambia asubiri niwasiliane na Mwenyekiti wangu wa chama.

“Baadae tukakubaliana tukutane nyumbani kwake, lakini akawa anasema tusubiri kwanza anamalizia kupanga mikakati na wabunge 55 wa CCM, lakini akisisitiza kuwa uamuzi wake uko pale pale, nikamuuliza vipi kuhusu press conference mbona muda unakaribia, akasema hakuna shida yeye atatuma tu watu wake wataitisha haraka, akasema lakini wanataka kumpatia unaibu waziri, hivyo bado anasumbuana nao, kengele ikalia kichwani sasa huyu mtu akipewa uwaziri itakuwaje.

“Baadae ananiambia, Dokta Slaa nimepigiwa simu na bwana mkubwa naenda kuonana naye, tangu wakati huo Sitta akapotea mpaka saa 8 ndiyo anapatikana, akaanza kuniambia ni lazima aende kwanza Urambo kuwaaga wazee, maana hawezi kuhama bila baraka zao, nikamuuliza vipi kuhusu press conference akasema tutaifanya Jumatatu ijayo Dar es Salaam, akaniambia; tena saa 9 uje uone statement ambayo nimeshaiandika ili na wewe uongeze inputs, Sitta huyu akaniambia kuwa Anne Makinda hatakaa zaidi ya miezi sita kwenye kiti cha uspika.”

Dkt. Slaa alisisitiza akisema kuwa nchi imefika hapa ilipo ikiwa imegubikwa na uozo wa ufisadi kila kona, ukiongeza idadi ya maadui wa taifa, kutoka watatu hadi wanne (umaskini, ujinga, maradhi na ufisadi/CCM) kuanzia ngazi ya chini hadi juu, kwa sababu ya ukosefu wa uadilifu, uaminifu kama Waziri Sitta.

Atalipuliwa zaidi


Dkt. Slaa alisema kuwa ameamua kuzungumza hayo machache kwa sasa, lakini ataongeza ‘kumlipua’ zaidi Sitta endapo atajitokeza kujibu haya ya sasa.

“Yeye ana uzoefu gani Sitta, hana uadilifu, si mwaminifu, nchi hii imeoza kwa sababu ya viongozi ya aina ya Sitta, nataka ajibu kwanza hayo kisha nitamlipua zaidi. Ana uadilifu gani katika nchi hii, ametumia mabilioni ya hela ya walipa kodi wa Tanzania kujijengea Ofisi ya Spika Urambo, tunauliza kuna spika wa Urambo au alijua yeye atakuwa spika wa milele au basi Makinda awe anakwenda Urambo wakati wa mapumziko ya bunge.
“Tulichoamua bungeni ni kwamba kila mbunge ajengewe ofisi yenye thamani isiyozidi milioni 40, lakini yeye akaenda kujijengea ofisi ya milioni 350 tena kwa kasma tofauti na inavyotakiwa lakini kibaya zaidi tendering process ya vifaa vya ofisi haikufutwa na vililetwa na kampuni ambayo majuzi imehusishwa na Blandina Nyoni, hakuna mahali tendering imefanyika, amefanyia ufisadi mali ya taifa,” alisema Dkt. Slaa.


More still to come about the press conference...


CHANZO: Afisa Habari wa Chadema TUMAINI MAKENE


SOURCE:Yemeni Times

26 Aug 2012



New Africa: the politician fighting corruption in Tanzania

Government minister January Makamba is full of innovative ideas for harnessing technology to help his country
January Makamba
Tanzanian minister January Makamba on the campaign trail. Photograph courtesy of January Makamba
January Makamba is Tanzania's deputy minister for communication, science and technology. In 2009, President Kikwete introduced him to Barack Obama, who was much taken by his dynamism, observing that he was the sort of politician likely to help transform the fortunes of the continent.
Makamba is an interesting combination of old and new Africa. He attended university in the US, but explains that, although he is the son of a teacher, politician and public servant, it was the time spent in Tanzania's rural areas as a child that most influenced his development. "The most rewarding experience was living with my grandmother. The daily routine was testing – I'd wake at 5am, walk 8km to school, come home at 3pm and go out to herd goats." This gave him, he feels, the "empathy needed for good decision-making".
It was empathy that turned him into a politician when, in his gap year, he was manager of Mtabila refugee camp, overseeing 120,000 Burundi refugees. "Witnessing that misery made me political." It made him "philosophical". But Makamba has emerged as a politician who does more than philosophise. He is an innovator with formidable drive. He is determined to unshackle his country from reliance on aid. He set upBumbuli Development Corporation to borrow $10m from Wall Street philanthropists, invested in bonds with dividends to be spent in his constituency. "We decided not to find an NGO to help us but start our own – and not make it a charity. We have had a flurry of NGOs with little impact. This corporation would be a driver for development and private enterprise. It would be a social business with huge potential." The corporation money is already funding community projects. He gives an example: "Fifty per cent of our fruit and vegetables used to be spoiled before going to market." Now, a "new aggregation centre" is putting this right.
His most exciting innovation, launching next month, is a new text message anti-corruption campaign, a global naming-and-shaming project. "Only 6.9% of corruption cases are currently reported. We want to solve the problem. Almost everyone in Tanzania has a mobile." He sets the scene: "At a hospital you are asked for a bribe. You have a USP code, you enter the location and details of the bribe and send it to a web platform: it will appear as a dot on a map so everyone can see that at a certain hospital a bribe was asked for."
Africans he admires
Fred Swaniker Ghanaian founder of African Leadership Network.
Malusi Gigaba A minister in South Africa, and a voice of reason and reassurance

18 Aug 2012


16 Aug 2012



Home
TUMEROGWA na aliyeturoga naye karogwa, kisha kafariki.”
Hapana, hatujarogwa ila nadhani bongo zetu zimefungwa, na funguo zimetumbukia chooni.”
Hizo ni baadhi ya kauli zinazoanza kuzoeleka masikioni mwa Watanzania wanapojadili mustakabali wa nchi.
Ukisikia kauli hizo unaweza kuishia kucheka kwa kuzitafsiri kuwa ni utani tu. Lakini ukichukua muda kuzitafakari, unaweza kujikuta unaungana kimtizamo na watu hao.
Hivi katika mazingira ya kawaida unawezaje kuelezea ‘busara’ za Kamati ya Olimpiki kujaza viongozi wengi zaidi wa wanamichezo kwenye msafara wa wawakilishi wetu kwenye mashindano ya Olimpiki ya majira ya joto yaliyomalizika juzi jijini London, hapa Uingereza?
Wakati wenzetu Wakenya wakirejea na medali kadhaa huku Waganda wakijivunia medali ya dhahabu, sisi tumeendelea kupigilia mstari ‘sifa’ yetu ya kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Lakini ukidhani uhuni huo katika ushiriki wetu kwenye Olimpiki unachefua, basi sikiliza hii ‘kali kubwa’ kutoka kwa Bunge letu tunaloliita ‘tukufu.’ Wiki iliyopita, Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai aliwaeleza Watanzania kuwa baadhi ya wawakilishi wao bungeni (wabunge) wamekuwa wakiingia kwenye vikao vya chombo hicho cha kutunga sheria wakiwa wamelewa pombe na sigara zisizo za kawaida.
Kabla hatujaenda mbali kujadili taarifa hii ya kuogofya ni vema tukakumbushana kuwa kwa mujibu wa marekebisho ya hivi karibuni, waheshimiwa wabunge wanalipwa shilingi milioni 11 kwa mwezi. Ni muhimu kutaja kiwango hicho ili tunapowajadili watu hawa tuwe na uelewa kuwa pamoja na umasikini wa nchi yetu tumejikamua na kuwapatia waheshimiwa hawa maslahi manono kabisa.
Kwa namna fulani ninampongeza Naibu Spika Ndugai kwa kutufungua macho kuhusu swali ambalo ninadhani wananchi wengi wamekuwa wakijiuliza, “kwanini baadhi ya waheshimiwa huonekana wamelala bungeni huku kikao kinaendelea?”
Mitandaoni kumejaa picha za ‘wachapa usingizi bungeni’ na kuna waheshimiwa wengi tu wanaopenda kuligeuza Bunge kuwa sehemu ya kulala.
Baadhi yetu tulipoona picha za aina hiyo tulijaribu kujipa matumaini kuwa labda waheshimiwa hao wanazidiwa na usingizi kwa vile ‘wanakesha wakitafakari jinsi ya kuwatumikia wapigakura wao, na pengine nchi kwa ujumla, kwa ufanisi mkubwa zaidi.’
Kadhalika, kauli ya Ndugai imetusaidia pia kutupa mwanga kuhusu michango ya baadhi ya wabunge ambayo mwananchi hawezi kulaumiwa akihisi mchangiaji anatafuta nafasi ya ushiriki wa Bongo Star Search kwa kipaji cha mipasho. Inakera lakini ndio ukweli wenyewe, baadhi ya waheshimiwa hutumia fursa ya kuchangia hoja kuonyesha umahiri wao wa kukebehi, kudhihaki na hata kutusi.
Lakini kilichonikera katika maelezo ya Ndugai ni ‘utetezi wa kitoto’ kuwa, (ninamnukuu) “Wabunge ni watu kama watu wengine, wana tabia kama walivyo wanadamu wengine, wapo ambao kwa namna ninavyohisi wanaingia bungeni hasa vikao vya kuanzia mchana wakiwa wamepiga bia.”
Kwanza, wabunge wetu si sawa na ‘watu wengine.’ Ni ‘watu wengine’ wangapi wanaitwa ‘waheshimiwa’? Na ni wangapi wanaolipwa posho kwa kutimiza wajibu wao (licha ya kulipwa mshahara kwa nyadhifa zao)? Na ni ‘watu wengine’ wangapi wanaolipwa mishahara minono japo kwa kiasi kikubwa ufanisi wao upo zaidi kwenye mipasho, kukashifiana na porojo nyingine zisizomsaidia Mtanzania?
Ndugai hayupo sahihi kudai kuwa wabunge wanaoingia bungeni wamelewa ‘wana tabia kama walivyo binadamu wengine.’ Mimi kama mwanafunzi siruhusiwi kuingia darasani nikiwa nimelewa. Hata kwenye sehemu za vinywaji ‘baamedi’ haruhusiwi kuingia kazini amelewa. Sasa hao ‘binadamu kama wengine’ anaotueleza Naibu Spika wametoka sayari gani?
Halafu cha kuchukiza zaidi ni ukweli kwamba Naibu Spika anafahamu kuwa kuna wabunge wanaingia kwenye vikao vya Bunge wakiwa wamelewa lakini hachukui hatua zozote bali anasubiri hadi apate nafasi ya kumwaga jambo hilo kwenye mahojiano na kituo cha runinga.
Huyu ni kiongozi dhaifu. Japo tunaweza kumpongeza kwa ‘kutuibia siri ya yanayojiri bungeni’ lakini dhamana aliyokabidhiwa si kunyooshea watu vidole (kwa maana ya kubainisha kuna wabunge walevi) bali kuchukua hatua stahili dhidi ya ‘wahalifu’ hao.
Na si kama nimetumia neno ‘wahalifu’ kwa bahati mbaya. La hasha. Mtu anayelipwa shilingi milioni 11 kama mshahara wa kumwakilisha mwananchi, kisha akaamua kufanya uwakilishi huo akiwa amepata bia kadhaa, au amevuta sigara isiyo ya kawaida (bangi?) au amelamba vitu fulani (‘unga’-madawa ya kulevya?), hana tofauti na mhalifu.
Ni jambazi anayesababisha watu waishi kwa shida ili wamudu maslahi yake kwa matarajio kuwa maslahi hayo manono yataleta ufanisi katika kazi lakini yeye anaishia kutekeleza majukumu yake akiwa na ‘faida kichwani’ (kalewa)!
Katika moja ya makala zangu huko nyuma niliweka wazi msimamo wangu kuwa mishahara mikubwa kupita kiasi ya wabunge wetu ni ujambazi wa mchana kweupe (daylight robbery) kwa sababu haiendani na hali mbaya ya uchumi watu. Na sasa ujambazi huo unajidhihirisha bayana kwa uhuni wa baadhi ya waheshimiwa wanaopuuza kanuni za Bunge na wajibu wao, na kutinga bungeni wamelewa.
Lakini kuna swali moja la msingi ambalo kila Mtanzania anapaswa kujiuliza, “IMEKUWAJE TUMEFIKA MAHALA BAADHI YA WABUNGE WANATINGA BUNGENI WAKIWA WAMELEWA?”
Msomaji mmoja wa jarida hili, Omary Abdallah, Mtanzania anayeishi nchini Ujerumani alinitumia ujumbe kupitia mtandao wa facebook akishauri kuwa badala ya kuendelea kuwalaumu viongozi wabovu inabidi sisi Watanzania wenyewe tuangalie mapungufu yetu yanayotufanya kuchagua viongozi wasiofaa (kwa mfano hao walevi).
Kwa kifupi, msomaji huyo anahitimisha kuwa Taifa limegubikwa na utapeli na uvivu. Rejea kwenye kampeni za ubunge. Utaona mgombea ‘anatoka jasho mwilini na mapovu mdomoni’ kuwahadaa wapigakura jinsi anavyowajali. Na kwa uvivu wetu wa kufikiri, wala hatuhoji iwapo ‘uchungu’ wa mgombea huyo ni kwa ajili ya maslahi yetu au ya tumbo lake (na pengine ‘nyumba ndogo’ zake). Matokeo ndio hao tunaoambiwa wanatuwakilisha wakiwa wamekunywa, kuvuta au kulamba kilevi.
Lakini pia, katika skandali hii ya ulevi wa baadhi ya wabunge, ninaona kipato cha waheshimiwa hao kuwa miongoni mwa vichocheo vya kuwasahaulisha wajibu wao.
Katika mazingira ya kawaida tu, mtu anayepewa fedha nyiiingi zaidi ya mahitaji yake anaweza kuishia kufanya mambo ya ajabu kabisa. Kwa huku Ughaibuni tunashuhudia baadhi ya wanasoka, kwa mfano, ambao wanalipwa mamilioni ya fedha, na kuna aina ya mwafaka wa kimtizamo kuwa ‘madudu’ yanayofanywa na baadhi yao yanachangiwa na wingi wa fedha usiowiana na mahitaji yao ya kawaida.
Suala la nyongeza ya mishahara ya wabunge linaonekana kama limeridhiwa na umma. Wakati madaktari na walimu wakiambiwa serikali haina fedha za kuboresha stahili na mazingira ya kazi zao, hatujapewa sababu za msingi za kuongeza mishahara ya wabunge ambao tayari walikuwa na mishahara mikubwa kabisa.
Utendaji kazi wa wengi wao hauendani na hata ‘kidogo’ walichokuwa wanapewa kabla ya mishahara mipya. Ikumbukwe kuwa mamilioni hayo kwa wabunge wetu ni fedha za walipakodi ambao wengi wao ni masikini wa kupindukia. Kuna kila sababu ya si tu kulaani ‘unyonyaji’ huu bali pia kuupinga kwa nguvu zote.
Sasa, kwa vile tumeruhusu ubunge uwe njia ya mkato ya kukwaa utajiri basi tutarajie kuona chaguzi zetu huko mbele zikiandamana na kila aina ya vituko na vioja miongoni mwa wanaotaka kuwa sehemu ya ‘mradi huu wa utajiri wa chap chap’ (get-rich-quick scheme).
Katika hali ya kawaida tu, nani asiyetaka kulipwa japo shilingi elfu kadhaa tu kwa kazi ya kulala huku una bia mbili tatu kichwani? Ni kama kwenda baa kisha unalipwa kwa kulewa.
Naomba ieleweke kuwa si kila mbunge hatimizi wajibu wake. Kuna wazalendo wachache wanaotambua majukumu yao. Baadhi yao, wameishia ‘kuumbuliwa’ na Kiti cha Spika kwa ‘kukiuka kanuni za Bunge (isomeke: kutetea maslahi ya wapigakura katika namna isiyokubalika kwa watawala).
Mashujaa hawa wachache wana ujasiri wa ziada kwani wakati wao wanatolewa nje kwa kutimiza wajibu wao, wanashuhudia baadhi ya wanaoachwa waendelee na vikao wakiwa wamelala kutokana na kinywaji, sigara zisizo za kawaida au kulamba vitu flani.
Nimalizie kwa kurejea maswali niliyoyanukuu mwanzoni mwa makala hii. Tumerogwa na aliyeturoga nae karogwa kisha kafariki, au akili zetu zimefungwa kisha ufunguo umepotea? Naomba usinijibu bali jibu lako liwe kwenye sanduku la kura katika uchaguzi ujao.
Penye nia pana njia


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.