24 Nov 2010



Hurrah! No more potions, gruelling exercise, or all turnip diets.

In what could fairly be called a watershed moment, scientists have confirmed that drinking water before a meal helps shed the pounds.

Yup, it's that simple. And you don't even have to buy the book.

In clinical trials, US researchers found that drinking a pint of water before a meal leads to weight loss.
Dr Brenda Davy, an associate professor in human nutrition, who led the study said: "We found in earlier studies that middle aged and older people who drank two cups of water right before eating a meal ate between 75 and 90 fewer calories during that meal.

"In this recent study, we found that over the course of 12 weeks, dieters who drank water before meals, three times per day, lost about 5 pounds more than dieters who did not increase their water intake."

"People should drink more water and less sugary, high-calorie drinks. It's a simple way to facilitate weight management," Dr Davy added.

While drinking water to lose weight is very much common sense, Dr Davy said that there has been little scientific information on this topic.

Previous studies have suggested that drinking water before meals reduces calorie intake, but according to Dr Davy this is the first randomised controlled clinica trial to show that increasing the amount of water that you drink water is an effective way to lose weight.

The study tracked the weight of 48 adults aged 55 to 75, who were separated into two groups. The first group drank two cups of water before meals and the second group did not. All of the subjects ate a low-calorie diet during the study.

Over the course of 12 weeks, the water drinkers lost around 15.5 pounds, while the non-water drinkers lost around 11 pounds.

Dr Davy said water may be so effective simply because it fills up the stomach and has no calories, so that people feel full quicker and eat less during meals.

She also added that replacing diet colas and other artificially sweetened drinks with water also helps to cut calories, and aids weight loss.


20 Nov 2010


Well,it might not be a big deal for you but it still is for me.Last night I came across this wonderful post when I visited Candy1world .All I can say is THANK YOU.That's so kind of you.Being in your top ten is such a huge accolade for me and my blog.It's like winning an Oscar

Asante sana



Kwa muda mrefu sasa,Rais Jakaya Kikwete amekuwa akitahadharisha kuhusu kuwapo kwa mgawanyiko wa kidini huko nyumbani.Aliongea hayo wakati wa kampeni zake na amerejea tena katika hotuba yake ya uzinduzi wa Bunge.

Tuweke kando mjadala wa namna Kikwete na CCM walivyoshinda uchaguzi mkuu uliopita hivi majuzi.Tuijadili hoja yake ya udini.Hivi kama amepata ushindi halali,anaposema kuna mgawanyiko wa udini anamaanisha kura zote alipigiwa na Waislamubwenzake au?Maana kama kweli kuna mgawanyiko wa udini basi ni dhahiri kuwa matokeo ya uchaguzi huo yasingempa ushindi wa zaidi ya asilimia 60 ( tuki-neglect uchakachuaji).

Let's call a spade a spade.Hivi leo Kikwete anathubutu kulalamika kuhusu tatizo lisilokuwepo la udini ilhali yeye na wanamtandao wenzake walimwaga sumu kubwa ya udini mwaka 2005 to an extent "akawaingiza mkenge" Waislam wenzie kwa kuwaahidi Mahakama ya kadhi na kuahidi kushughulikia uanachama wa OIC?

Na hata tukiweka hilo kando,hivi ile kauli ya "CHAGUO LA MUNGU" haikutokana na jitihada za Kikwete na wanamtandao wenzie kuwaghilibu viongozi wa dini hadi wakamtangaza kuwa amechaguliwa na Mungu kuwakomboa Watanzania?Actually,huo haukuwa udini per se bali kufuru kwa Mwenyezi Mungu.Na kwa sie tunaofahamu kuwa Mungu si Athumani,na hapendi kuchezewa,ipo siku atawaadhibu wale wote waliotumia jina lake kwa minajili ya kusaka kura.

Mie nilikuwa Tanzania mwaka from Oktoba 2005 hadi April 2006 kwenye fieldwork yangu.Mungu huyohuyo tuliyeambiwa Kikwete ndio Chaguo lake mwaka 2005 anihukumu iwapo sentensi ifuatayo ni ya uzushi.Miongoni mwa maustaadhi niliowaintavyuu kwenye fieldwork yangu walibainisha waziwazi kuwa waliahidiwa na Kikwete na timu yake kuwa laiti angepata urais angeshughulikia vilio mbalimbali vya Waislam.Kwangu,huo sio udini as such kwa vile kuna matatizo ya msingi yanayowakabili Waislam na ambayo awamu mbalimbali za serikali tangu uhuru zimekwepa kuyashughulikia.Eneo moja la msingi ni elimu.Mwalimu Nyerere alikiri katika hotuba yake ya tarehe 9/12/1962 kwamba " wengi wa waliofanikiwa kupata elimu walifanya hivyo kupitia shule za misheni,na hivyo wengi ni Wakristo.Hapa tena,kwahiyo,tuna mgawanyiko ambao uwepo wake unaweza kuwa tishio kwa umoja wetu".Akaendelea kusema, " marafiki zangu,kila mmoja wetu afanye jitihada za kujenga Tanganyika ambayo hakutakuwa na tofauti na migawanyiko".Japo wakati Nyerere anastaafu mwaka 1985 alidai kuwa amefanikiwa kutimiza azma hiyo,ushahidi wa kitaaluma unapingana na kauli hiyo.

Kwahiyo,binafsi kama Mtanzania ninayependa kuona nchi yetu ikiwa na jamii yenye usawa,naamini kuwa viongozi wetu wana jukumu la kulishughulikia suala hili na kulipatia ufumbuzi.Kumekuwa na unafiki mkubwa katika kushughulikia malalamiko ya msingi ya Waislamu.Lakini kwa vile lengo la makala hii sio kuzungumzia suala hilo,nachoweza kuandika kwa kifupi ni kuwa kwa namna moja ua nyingine awamu zote nne za urais zimezembea kuyapatia ufumbuzi malalamiko ya Waislam huku Awamu ya Nne ikiingia madarakani kwa kujitambulisha waziwazi na kwa siri kuwa sio tu inayatambua matatizo na malalamiko ya Waislam lakini pia imedhamiria kuyatatua.Na katika kuonyesha iko serious,ahadi ya Mahakama ya Kadhi ikaingizwa kwenye manifesto ya uchaguzi ya CCM mwaka 2005.

Waislam wanajua,na sie tusio Waislam pia tunajua,kwamba ahadi hiyo ilikuwa ni danganya toto tu.Miaka mitano baadaye,suala la Mahakama ya Kadhi na kujiunga limeendelea kuwa ngonjera kama ilivyo kwa "maisha bora kwa kila Mtanzania".

Kwahiyo,Kikwete aliingia madarakani kwa kutumia udini lakini sio kwa vile yeye ni Muislam bali alitambua kilio cha Waislam kisha akakitumia kama turufu yake (kwa ahadi kuwa angeshughulikia matatizo yake) kisha baada ya kupata madaraka akajifanya hahusiki na suala hilo (refer kauli ya Kikwete kuwa aliyeanzisha hoja ya Kadhi ni Agustino Mrema-anaedansi nae hapo chini.What a cheap excuse!).Kwa lugha nyepesi,kilichojitokeza ni utapeli kwa kutumia matatizo ya kidini.
Picha kwa hisani MICHUZI

Kikwete analalamika kuhusu udini wakati kwa miaka mitano iliyopita Tanzania imekuwa na Rais na Makamu wa Rais Waislam.Na kwa vile Makamu wa sasa nae ni Muislam,inamaanisha kuwa kwa miaka 10 Tanzania itakuwa imekuwa chini ya Rais na Makamu wa Rais Waislam.Hakuna anayelalamika kwa vile wengi wetu tuna upeo mkubwa zaidi ya wa Kikwete anayetaka kulazimisha kuwa tuna mgawanyiko wa kidini.Ishu ya Rais na Makamu wake kutoka dini moja ni muhimu kwa vile Rais asipokuwepo nchini urais unakaimiwa na Makamu wake.Na likitokea lolote la kutokea,Makamu huyo atakuwa Rais kwa muda.

Sasa huyu Mkwere anapotuambia kuna mgawanyiko wa udini anaashiria kitu gani?Wakristo hawajalalamika muundo wa uongozi wa juu wa CCM ambapo idadi ya Waislam ni kubwa kuliko ya Wakristo (rejea wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM).Kikwete hakuwahi kuekemea jitihada zilizokuwa zikifanywa na magazeti ya Kiislam kujenga picha kuwa Dkt Wilbroad Slaa ni mgombea alietumwa na Kanisa Katoliki.Kikwete hakukemea pale Daily News na Habari Leo,magazeti yanayoendeshwa kwa fedha za walipa kodi,yalifuata mkumbo wa magazeti hayo ya Kiislam kumtambulisha Dkt Slaa kama mgombea aliyetumwa na Kanisa.Hakukemea kwa vile nafsini mwake alikuwa na imani potofu kama hiyo ya wababaishaji hao kuwa Dkt Slaa ana ajenda ya Ukristo.
Tatizo ni kwamba Katiba yetu haitoi fursa ya kumkalia kooni Kikwete.Tatizo jingine ni kukosekana kwa ujasiri huko nyumbani wa kumkalia kooni Kikwete kisheria kwa tuhuma za kuhatarisha usalama wa taifa.Laiti Idara ya Usalama wa Taifa ingekuwa serious basi ni wazi wangemshauri Kikwete aache kuhatarisha usalama wa taifa kwa kauli zake zisizoambatana na uthibitisho kuwa kuna mgawanyiko wa kidini.Au inawezekana wanausalama wetu ndio wanamhadaa Kikwete kuwa kuna mgawanyiko wa udini?


Au inawezekana kuna tatizo kubwa zaidi kuhusu Kikwete,kwamba anaona vitu ambayo sie wengine hatuvioni?Je ni maono ya Sheikh Yahya?Au je kelele hizo za mgawanyiko wa kidini ni maandalizi ya kuihujumu Chadema,au pengine kumuibulia kesi Dkt Slaa kwa kigezo cha kucbochea vurugu za kidini?

Jamani,hata mwezi haujapita na tayari tunashuhudia mazingaombwe tusiyohitaji.Mara TAKUKURU wanamsafisha Chenge.Mara Kikwete anaendeleza ngonjera za mgawanyiko wa udini,mara Kikwete anamchagua Zakia Meghji kuwa mbunge licha ya mwanamama huyo kuhusishwa na suala la EPA ( na taarifa kuwa ana uhusiano wa kifamilia na Kikwete).

Tuspokuwa makini,2010-2015 itashuhudia miujiza ambayo haijawahi kutokea mahala popote duniani katika ulingo wa uongozi na siasa.Sad news is,sie kama wahanga tunaweza tusipate wasaa wa "kushangaa" na kujiuliza "what the hell is going on?"

19 Nov 2010


Pichani kwa hisani HAKI NGOWI

Suala ambalo limetawala maongezi ya Watanzania wengi kwenye social media kwa leo ni kitendo cha wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati anazindua Bunge jipya mjini Dodoma.Kwanza niweke wazi msimamo wangu kuwa naunga mkono uamuzi huo wa Chadema.Sifanyi hivyo kwa minajiki ya kukipenda chama hicho bali ni katika kuzingatia ukweli kuwa Chadema wametumia HAKI yao ya Kikatiba na kidemokrasia kuonyesha upinzani wak kwa vitendo.Nimeandika HAKI kwa herufi kubwa kwa vile neno hilo ni muhimu katika "kuwahukumu" Chadema.

Baadhi ya wenzetu wamekishutumu vikali kitendo hicho huku wengine wakikiita "utovu wa nidhamu wa hali ya juu".Lakini wakati wenzetu hao wanatumia HAKI zao za Kikatiba na kidemokrasia kuwalaumu Chadema,hawataki kutafakari japo kidogo kuhusu HAKI kama hizo kwa chama hicho,yaani HAKI yao ku-protest kwa amani dhidi ya mwenendo mzima wa uchaguzi uliopelekea Jakaya Kikwete kuwa Rais tena.

Inawezekana tukio hilo linaonekana sio la kawaida kwa vile ni mara ya kwanza kutokea nchini.Lakini kwa wanaojishughulisha kufahamu kinachoendelea sehemu nyingine duniani watafahaku kuwa hali hiyo imeshatokea kwenye mabunge mbalimbali,kwa mfano nchini Afrika Kusini,Gambia,Sudan, India,Pakistan na Iraki,to mention only a few.

Kwa namna moja au nyingine,vipengere dhalimu vya Katiba yetu vimewaacha Chadema na alternatives chache zaidi ya hatua kama hiyo ya leo kwa vile Katiba yetu inanyima uhuru wa kupinga matokeo ya ushindi wa Rais mahakamani hata kama ushindi huo umepatikana kwa njia zisizo halali.Leo mapungufu hayo makubwa kwenye Katiba yetu yanaweza kuonekana kama jambo dogo.Lakini yayumkinika kuamini kuwa inaweza tokea tukapata Rais dikteta ambaye ameshindwa kwa mabavu lakini tukajikuta hatuna njia ya kupinga "ushindi" wake kwa vile Katiba inamlinda.

Tatizo la Katiba nyingi katika "Nchi za Dunia ya Tatu" na hususan barani Afrika ni ile tabia hatari ya katiba hizo kutumika kwa mahitaji na maslahi ya watawala walio madarakani.Na kwa vile wengi wa watawala hao ni walafi na waroho wa madaraka,na kwa vile madaraka makubwa waliyonayo yanawapa uhuru wa kufanya lolote wapendalo,katiba hizo huwekwa viraka hapa na pale sio kwa minajili ya ustawi wa taifa husika bali kikundi kidogo cha watawala.

Laiti Katiba ingekuwa inaruhusu ushindi wa Rais kupingwa mahakamani basi ni dhahiri Chadema wangeshafungua kesi.Kuna wanaosema "sasa wakitoka nje ya Bunge ndio inasaidia nini?"Majibu ni mengi ila hapa nitatoa machache tu.Kwanza,ikumbukwe kuwa Chadema ndio chama kikuu cha upinzani bungeni.Pamoja na uchache wa idadi ya wabunge wao ukilinganisha na wale wa CCM,hadhi ya chama kikuu cha upinzani ni kubwa na muhimu ndani na nje ya nchi.Pamoja na mazingira na sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani,kwa nchi masikini kama Tanzania kuna kila sababu ya sote kuonekana tumeshikamana hata kama mshikamano huo ni wa kinafiki na unawanufaisha zaidi mafisadi.Ndio maana basi nchi wafadhili zilikuwa zikiwakalia kooni watawala wetu kuhusu upatikanaji wa suluhisho la kudumu huko Zanzibar,ambapo hatimaye CCM kwa shingo upande (na licha ya ngebe za akina Makamba) leo hii tunashuhudia serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar.

Of course,hali ya kutoelewana huko Zanzibar ilikuwa serious sana hasa kutokana na vurugu za uchaguzi zilizopelekea mauaji ya watu kadhaa,ukweli unabaki kuwa msimamo thabiti wa chama kikuu cha upinzani visiwani humo,yaani CUF,kutotambua matokeo ya chaguzi mbalimbali,sambamba na kelele walizopiga kwa jumuiya ya kimataifa ndivyo vilivyopeleka leo hii kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.

Kwahiyo wanaohoji umuhimu wa wabunge wa Chadema kususia hotuba ya Kikwete wanapaswa kuelewa kuea msimamo imara sambamba na matendo yanayothibitisha msimamo huo yanasaidia kuleta mabadiliko yanayokusudiwa.Leo pale Dodoma kulikuwa na wawakilishi wa nchi na jumuiya mbalinbali za kimataifa.Vyovyote itavyokuwa,wameguswa na tukio hilo ambalo kwa hakika limetia dola utawala wa Kikwete.Baadhi ya nchi hizo ni wafadhili ambao bila wao basi mambo yanakuwa si mambo.

Lakini jingine la muhimu ni kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake (including vyombo vya dola na Tume ya Uchaguzi) kuwa zama za "ndiyo mzee" zimefika kikomo.Hata kama Katiba inaendelea kuhalalisha sheria dhalimu (kama hiyo inayonyima fursa ya kupinga ushindi wa rais mahakamani) mwanya mdogo wa uhuru wa kidemokrasia kupingana pasipo kupigana unawezesha Chadema kuzalisha harakati mpya za mapambano dhidi ya udhalimu lakini pasipo vurugu au umwagaji damu.Kwa tunaotaka kuona Tanzania yenye kuheshimu na kuzingatia haki na stahili za Watanzania,kitendo cha leo cha Chadema kinafungua ukurasa mpya wa matumaini.Kadhalika,kitendo hicho ni hatua kubwa na muhimu ya kukua kwa demokrasia yetu kutoka vyama vinavyokubali yaishe hata pale penye uthibitisho kuwa vimejumiwa kwenye chaguzi,kwenda kwenye zama ambapo uchakachuaji wa chaguzi unaharamishwa hadharani tena kwenye live tv.Message delivered!

Ni wazi kuwa tukio la leo limemgusa Kikwete na serikali yake kama ambavyo limewagusa Watanzania wengi na jumuiya ya kimataifa.Yayumkinika kuwa inawezekana nguvu kubwa iliyotumika kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliopita sasa itaelekezwa katika kuihujumu Chadema ili idhoofike na hatimaye kuachana na msimamo wake wa kukataa kumtambua Kikwete.Zitafanyika jitihada za kuwqgombanisha viongozi wa chama hicho kama ilivyokuww kww NCCR-Mageuzi ya Mrema.Kuna uwezekano pia wa Dokta Wilbroad Slaa kuzushiwa zengwe zaidi ya lile ya maisha yake binafsi.Lakini hayo yanaweza kupita pasipo madhara makubwa kwani hata Baba wa Taifa na wenzake walipokuwa wanahangaikia ukombozi wa Tanzania kutoka himaya ya mkoloni walikumbana na vizingiti hivyo.Haya ni mapambano kati ya wenye uchungu na nchi yao dhidi ya wale wanaotaka kuigeuza nchi yetu kuwa "shamba la bibi" na makao makuu ya ufisadi.

Sie Wakristo tunaamini kuwa mwenye haki ataanguka saba mara sabini ( hapa simaanishi kuanguka kama kule kwa Kikwete pale Jangwani) lakini mwishowe atasimama.Kukubali uchakachuaji wa kura kutapelekea matokeo ya ain moja tu: uchakachuaji zaidi.Historia inatufundisha bayana kuwa kukubali kitu kibaya hakusaidii hata chembe kitu hicho kibaya kugeuka kizuri au athari zake kupungua.Wanaoshauri Dkt Slaa na Chadema "wakubali matokeo" hawana tofauti na wanaoweza kusema tuache mapambano dhidi ya malaria au ukimwi kwa vile magonjwa hayo yamekuwepo miaka nenda miaka rudi.

Laiti Nyerere na mashujaa wengine wa mapambano dhidi ya mkoloni wangepatwa na mawazo hayo ya "kukubali yaishe" leo hii tungeendelea kuwa chini ya mkoloni ( I know kuna watakaosema bora mkoloni kuliko fisadi.Mie nasema ukoloni na ufisadi ni mbaya kama ilivyo kwa kansa na ukimwi.Hakuna cha nafuu,wote ni maadui wanaostahili kuangamizwa).Na laiti Nyerere "angekubali yaishe pale Nduli Idi Amini alipotuvamia,basi huends leo tungekuwa sehemu ya Uganda chini ya dikteta Idi Amini au mrithi wake.

Giving up is not an alternative.Mapambano ya kudai haki (kwa amani) lazima yaendelee.Waingereza wana msemo kwamba kukubali kitu pungufu kwa minajili ya bora liende hatimaye hupelekea kupata kilicho pungufu zaidi ya kilichostahili kupatikana.Kadhalika,hatua zote za mabadiliko huanza kwa hatua chache na pengine ndogo lakini zenye impact na hatimaye kutengenrza mazingita mazuri kwa hatua kubwa zenye impact kubwa zaidi na pengine zenye kuweza kuandika historia mpya.Vilevile,actions speak louder than words.Na hiyo imethibitka leo kwani japo Chadema walishatangaza kuwa hawatomtambua Kikwete uzito wa tamko hilo haukuwagusa wengi kulinganisha na tukio la leo la kususia hotuba ya Kikwete.

And by the way,hotuba hiyo ilikuwa na tofauti gani na hotuba lukuki alizotoa wakati wa utawala wake 2005-2010?Hivyo vipaumbele sijui 13 (or were they 19) tulishavisikia kwenye kampeni za 2005 na zikarudufiwa kwenye kampeni za mwaka huu.Kama kuna yeyote aliyechukulia vimpaumbele hivyo seriously all I can say asubiri muda si mtefu atabaini "imekula kwake" as they say in the streets.




Video kwa hisani ya Mwanakijiji

18 Nov 2010



Face to face
Firstly, I should make clear that in a serious relationship, I would always conduct this nasty business in person. And maybe in a casual relationship too, if forced...

Pros: Instant right to reply for the dumpee.
Cons: You are vulnerable to the threat of tears and possible violence.

Ignoring
This very common tactic involves blanking your lover until they work out that it's over. At first, they will send lots of texts and mails. Eventually, they will give up.

Pros: You never have to officially dump them.
Cons: They will never know for sure why you stopped contacting them; they may even think you are dead.

Text/email
The fastest, simplest and by far most popular method of ending a casual fling is to fire off a carefully-worded message. Almost everyone has received - or dished out - some form of electronic dumping. But killjoys deem it impolite.
Pros: Fits in perfectly with a fast-paced modern lifestyle.
Cons: The victim could receive the message at an unfortunate moment, such as during an important business meeting or while they’re having a really good time at Alton Towers.

Letter
I suppose this was considered the text dumping of its day. But now it seems slightly more classy and respectful. At least you're paying for a stamp.

Pros: Old-fashioned and somehow romantic. Your jilted lover can keep it forever as a memento of how much of a berk you are.
Cons: You have to pay for a stamp.

Facebook
The ’relationship status’ option on Facebook is the best way of keeping up-to-date with your friends' love lives... so why not your own too? Just change your status and your newly-dumped ex will receive the news straight to their Wall.

Pros: For you, it's painless. Just the simple click of a button.
Cons: Your ex will be furious and may retaliate by announcing to Facebook that you have a small willy.

Note
This is similar to the letter but less comprehensive. It could be piece of paper through the letterbox or a Post-it note stuck to their box of Alpen. The key is the brevity.

Pros: Everyone likes receiving little notes, it’s fun.
Cons: You’d have to pick a strategic time to leave the note, otherwise you could get caught and end up in a face-to-face situation.

Via someone else
This only generally happens when you are under the age of 15. It happened to me once in my school lunch break while I was queuing up in Dixy Fried Chicken and it was brutal.

Pros: If they cry, you don't have to see it.
Cons: Not acceptable behaviour if you are an adult.

In public
At a Birmingham City football match last weekend, a fan proposed to his girlfriend on the pitch. So why not do the opposite and announce to the world your decision to end it? Maybe the announcer could do it when they read out the birthdays. Or you could request a shout-out on your lover’s favourite radio station.

Pros: This could be her 15 seconds of fame.
Cons: Live broadcasting is unpredictable and they may omit your dedication.

Don’t tell them
Tell your friends and family you've split up, chat people up in bars, go online dating, stop having sex - essentially, become single. Just don't tell your partner about it.

Pros: Awkward dumping conversation avoided.
Cons: There's a high chance they will eventually find out you have stopped going out with them and then bad things will happen.

Phone call
As for me, I opted against all these methods and called her. I semi-rehearsed what I was going to say; my main aim was to avoid clichés such as "it's not you, it's me" and not to panic and tell her I was gay. I bumbled through it awkwardly, using the phrase "I really like you but…" more than once (it was true though). And although she went a bit quiet, the conversation ended on fairly amicable terms. I didn't feel great, but I felt like slightly less of an arsehole than if I’d used the methods above.

Pros: Makes you feel like an adult.
Cons: Scary.


17 Nov 2010

• RIPOTI MPYA YA UNDP YAANIKA KILA KITU

na Tutindaga Mwakalonge

SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limetoa ripoti yake ya hali ya maendeleo duniani inayoichambua Tanzania kuwa moja ya nchi zilizo nyuma sana kimaendeleo kwa kuwa na watu wengi wanaokabiliwa na umaskini.

Ripoti hiyo inayopima maendeleo ya nchi husika kwa kutazama maendeleo ya watu wake ilizinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam jana na kuitaja Tanzania kuwa nchi ya 148 kati ya nchi 169.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, katika kila Watanzania mia moja, 36 wanaishi katika hali mbaya sana ya umaskini, sawa na asilimia 36 ya watu wote, milioni 41.3.

Pia ripoti hiyo ya kimataifa imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 97 wanaishi kwenye umaskini wa kipato wa chini ya dola 2 za Marekani kwa siku, sawa na chini ya takriban sh 2,000 za Kitanzania kwa siku.

Aidha, ripoti hiyo iliyobeba kauli ya ‘Utajiri halisi wa mataifa’, imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 89 wametajwa kuishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku.

“Kwa takwimu hizo, Watanzania wengi wako katika umaskini wa kutisha kwa sababu ya kuwa na uwezo duni wa kifedha wa kumudu maisha yao ya kila siku”, alifafanua mtaalamu mmoja aliyehudhuria uzinduzi huo.

Hata hivyo, pamoja na takwimu hizo, Wizara ya Fedha na Uchumi, kupitia kwa Katibu wake, Ramadhani Khijjah, iliendelea kusifia mwenendo wa ukuaji wa uchumi nchini huku ikidai kuwa sekta za elimu na afya zimekuwa zikichochea ukuaji wa uchumi.



You can't access the internet. And it doesn't have a camera or games you can play.In fact, this new mobile phone doesn't even let you send text messages.The designers of 'John's Phone' have created a device that has only one function: it lets you make calls.Hailed as the world's simplest phone, it is designed to be a tongue-in-cheek 'basic backlash' by targeting users who do not want the flashy features of next-generation models.

Dubbed the 'anti iPhone', the £67 device with a brightly coloured facade and big buttons resembles a toy.
The phone's Dutch makers, advertising agency John Doe, are hoping it will be a hit with technophobes and children buying their first phone.The manual is only one page long and, unlike its battery-hungry smartphone counterparts, the makers of 'John's Phone' claim that a single charge will provide users with three weeks' battery life.Even the phone's 'built-in' address book is old-fashioned - concealed behind a flap at the rear of the phone, it's a physical pen-and-paper notepad used to store your contacts.
For those in a rush, the device does have the ability to record ten speed dial numbers.The phone's designers wanted the phone to have 'no frills and no unnecessary features such as a camera, text messaging and an endless number of ringtones'.

Designer Diedriekje Bok said: 'At a time when there is an abundance of choices and oppressive channels, we wanted to develop a simple gadget.

'It is also a useful phone while travelling, exercising or weekend sailing.

'You always reach for your close family and friends, so John's Phone is for when the rest of the world does not matter.'

It remains to be seen whether all mobile phone users will be rushing to swap their hi-tech phones for this new, pared-down model just yet.

Customer Ben Reed, 24, from Preston, said 'I think it looks quite cool. The design is stylish and I like the simplicity of it.

'But I don't know if I could use it instead of my current phone. I rely on it to coordinate my social life, keep an eye on my work e-mails and to follow news updates online.

'I can see how this phone might be good for old people or very young kids, though


TANGAZO MAALUM



Utawala na wafanyakazi wa URBAN PULSE wakishirikiana na Tanzania Community Europe wanapenda kuwatangazia washabiki wote wa Diamond UK na watu wote wanao support kampeni ya vita na Malaria ya kuwa kuna mabadiliko ya lazima yaliyotokea kuhusu show ya Diamond ya tarehe 27 November Birmingham. Kwamba kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotegemea kujitokeza siku hiyo imebidi ukumbi ubadilishwe ili uweze kukidhi idadi yao,Kwa hiyo jambo hili limepelekea ulazimu wa kubadilisha kumbi kwenda

27 November 2010
116 GAR GOSFORD STREET
PALMS BAR
COVENTRY
CV1 5 EA


Mabadiliko haya ni ya lazima na tunaomba radhi kwa ufumbufu wowote utakojitokeza

WOTE MNAKARIBISHWA

Utawala
URBAN PULSE


16 Nov 2010


Springburn, Glasgow
Tillydrone,Aberdeen
Gallowgate, Glasgow



BONUS TRACKS FROM UK'S FINEST (BELOW)

Griminal -Supa Dupa


Marvell- We Know


I really like music,hip-hop to be specific.One of my teenage dreams was to become a music producer (inspired by Dr Dre and old pal Profesa Ludigo), had I not indulged myself into academics.A day late and a dollar short,I suppose!

Talking of Dr Dre (above), HERE is some good news about the eagerly-awaited Detox album.Click HERE to listen to a leaked track "KUSH" featuring Snoop Dogg and Akon.


Enjoy Dre's old tune "Been there Done that"





Jadden and his Dad Will in The Pursuit of Happyness



Jada as Stoney in Set It Off




Willow's hit song Whip My Hair


Husband and Dad Will Smith the actor


...and Will Smith the rapper




Last year it was Rage Against The Machine - this year a rap song selling milk is set to challenge The X Factor winner for the coveted Christmas No 1 slot.

The music from the Yeo Valley advert - which features four rustic rappers 'bigging up' the West Country dairy's products - has become hugely popular since it was first shown during the show's commercial breaks.

The Sunday after it was first aired it went on to be featured as a 'top trend' on You Tube's home page - and since then has been watched online 1.5million times.

Unlikely rappers: The rustic foursome from the Yeo Valley adverts could soon be enjoying chart success
The advert sees the unlikely rap stars dressed in flat caps and wellies, and features the lyrics 'rollin' with my Massey on a summer's day' - in reference to the quartet's tractor.

It was made by Los Angeles based director Julien Lutz, who has made music videos for a host of stars including R Kelly, Usher, Kanye West and Nelly Furtado.

Among the 'rappers' in the advert is 21-year-old Alexandra Evans, who was the winner of the fourth series of Britain's Next Top Model.

Model rapper: Former Britain's Next Top Model winner Alexandra Evans features in the commercial
'I'm really surprised so many people like it,' she said of the song. 'Getting the Christmas No 1 is a long shot but who knows?'

Yeo Valley, which is based in Somerset, has committed to showing the commercial exclusive during breaks in The X Factor, at a cost of £5million.

The track was released for download via iTunes due to public demand, after Facebook groups calling for its release were set up and fans took to Twitter to air their views.

The Massey massive: The rappers pay tribute to their tractor in the tongue-in-cheek track
Among those who have shown their support for the track are Radio 1 DJ Zane Lowe, who is known as a champion of new music.

'Must be intimidating for The X Factor finalists to have to compete with the infinitely better Yeo valley crew each week,' he recently said on his Twitter page.

A spokeperson for the dairy added, 'It's not your usual chart topper but the positive response from the public suggests people want to hear it in the top 40.'

Dairy good: The track could pose an unusual threat to The X Factor winner for the Christmas No 1 spot
However the song is not the only one which is being championed to reach the top spot in the Christmas chart, with a number of campaigns popping up on Facebook.

Several pages have emerged to push the Sixties hit Surfin' Bird by The Trashmen, which was made famous by the film Full Metal Jacket, while there are growing campaigns to see Rick Astley's Eighties hit Never Gonna Give You Up and Meat Loaf's Bat Out Of Hell at number one for Christmas.

Also gathering momentum is the four and a half minute silent track by John Cage, which some Facebook fans have dubbed 'Cage Against The Machine' in reference to last year's Christmas campaign on the social networking site.

That one saw Rage Against The Machine's Killing In The Name deprive 2009 X Factor champion Joe McElderry of the festive chart-topper with his winner's single The Climb.

14 Nov 2010

Image and video hosting by TinyPic
The man himself.The Haymaker.A professional KO (Knock Out) Artist.A handsome assassin

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
David Haye akitoa kichapo cha nguvu

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Machampioni wa zamani.Lennox Lewis (kushoto) na Frank Bruno.Wote ni Waingereza
Picha kwa hisani ya magazeti ya The Guardian na The Daily Mail

12 Nov 2010


Raymond Kaminyoge
TANGU Machi mwaka jana alipostaafishwa kazi na Rais Jakaya Kikwete, akiwa Mkuu wa Wilaya ya Mbalali, Mbeya, Hawa Ngulume amekuwa haonekani hadharani wala kusikika kwenye vyombo vya habari kama tulivyomzoea.

Tunakumbuka jinsi alivyoendesha operesheni ya kuwaondoa wafugaji katika Bonde la Ihefu wilayani humo na kusababisha habari zake kutawala kwenye vyombo vya habari na kusababisha malumbano makali kati ya wafugaji na wanamazingira.

Tunakumbuka pia alivyoendesha operesheni hiyo kwa yeye mwenyewe kutembea kwa miguu akisindikiza ng’ombe kuondoka kwenye bonde hilo hali iliyomfanya achukiwe na wafugaji hao lakini akapendwa na wanamazingira.

Tunashuhudia hivi sasa baada ya kuondoka kwa wafugaji kwenye bonde hilo, hali mazingira ni shwali kwani ukijani na uoto wa asili umeanza kurejea katika bonde hilo.

Hayo aliyafanya akiwa mkuu wa wilaya ya Mbalali kabla hajastaafishwa na kumpisha mwenzake Luteni Cosmas Kayombo.

Hayo yote yanakumbukwa na Ngulume, ambaye hivi sasa yuko katika hali mbaya kiafya nyumbani kwake Goba Kinzudi, jijini Dar es Salaam akisumbuliwa na maradhi ya vichomi na mapafu.

Hata hivyo, bado madaktari hawajathibitisha ni nini hasa kinachomsumbua kutokana na kukosekana kwa kipimo mbadala cha kupima kansa ya mapafu.

Mwananchi lilifika nyumbani kwake na aliamua kueleza yaliyokuwa moyoni mwake: “Nimeona bora nitumie chombo cha habari kufikisha ujumbe wa ugonjwa kabla sijafa.”

Anaongeza: “Kwa miezi mitatu sasa niko hoi kitandani, siwezi kutembea bila kusaidiwa, naiomba serikali inisaidie niweze kwenda India ambako kuna vipimo na tiba ya maradhi yanayonisumbua.”

Anasema ameamua kutumia gazeti hili ili kufikisha ujumbe kwa serikali na CCM kuhusu maradhi yanayomsumbua baada ya njia nyingine kushindikana.

“Nilipeleka taarifa kwenye chama changu kwamba naumwa nahitaji msaada, lakini sikujibiwa, pia nimefanya juhudi za kutaka kumwona Waziri Mkuu ili anisaidie lakini juhudi zangu hazikuzaa matunda, nimeamua nitumie chombo cha habari kabla sijafikwa na mauti,” anasema.

Ngulume ambaye ni kada maarufu wa CCM aliyetumikia nafasi ya ukuu wa wilaya kwa miaka 18, anasema maradhi yanayomsumbua yalianza baada ya kumalizika kwa mchakato wa kura za maoni za chama hicho.

Anasema aliomba ridhaa ya chama hicho kimsimamishe kuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Singida Mjini lakini hakufanikiwa.

“Katika mchakato ule, Mohammed Dewji alishinda na mimi nikawa mshindi wa pili, niliporudi Dar es Salaam nikaanza kujiandaa kwenda kumpigia debe Dewji, kama ulivyo utaratibu wa chama chetu, ndipo nikaanza kuumwa ghafla,” anasema na kuongeza:

“Nilipenda kushiriki kwenye kampeni ili kuwasaidia wagombea mbalimbali wa chama changu lakini anadhani Mungu hakupenda nifanye hivyo.”

Ngulume ambaye amewahi kuwa mkuu wa wilaya mbalimbali zikiwemo za Kinondoni, Bagamoyo na Kibaha anasema baada ya kuumwa amekuwa akipata tiba za aina tofauti lakini hazijamsaidia.

“Nasikia maumivu makali tumboni, utadhani kuna msumeno unakata viungo vyangu, usiku kucha sipati usingizi ni maumivu tu ndiyo yanayotawala mwili wangu,” anasema.

Anasema amekwishatibiwa kwenye Hospitali za Lugalo, Ocean Road na Imtu zote za Dar es Salaam lakini mbali ya kutopata nafuu, hali yake inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.

“Katika hospitali ya Ocean Road nilitakiwa kupima kama mapafu yana maji ili kuthibitisha kama ni kansa ya mapafu lakini kipimo kilichopo kinatakiwa kukaa katika kinywa nami sina pumzi, hivyo ikashindikana kupima,” anasema.

Anaongeza kuwa hadi sasa hawezi kuweka wazi kuhusu maradhi yanayomsumbua kwa vile vipimo mbadala ya vile vya kuwekwa katika kinywa vinapatikana nje ya nchi.

“Ndiyo maana naomba msaada wa kwenda kutibiwa nje kwani nikipimwa ndipo naweza kupata tiba ya uhakika,” anasema kwa taabu.

Anasema katika kuhangaika kutafuta tiba aliwahi kwenda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini cha kushangaza alikaa kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 11.00 jioni bila kuhudumiwa.

“Ndipo mtu mmoja anayenifahamu alipopita nilipoketi akanisalimia kwa kuniita mheshimiwa. Muuguzi mmoja jina ninalihifadhi akaja kutaka kunihudumia, nikamwambia ina maana siwezi kuhudumiwa hadi niwe mheshimiwa? Nikaondoka kwa hasira nikakataa kuhudumiwa,” anasema.

Siku moja baada ya kuzungumza na gazeti hilo, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi) aliyokuwa akifanya kazi chini yake ilitoa tamko la kusimamia matibabu yake nje ya nchi.

Ujumbe wa maofisa wa Tamisemi ulifika nyumbani kwa mkuu huyo wa zamani wa wilaya kumjulia hali. Hatua hiyo imekuwa faraja kwa Ngulume ambaye anasema ingawa bado ana maumivu makali, amefurahi kwani kuna maofisa kutoka Tamisemi waliomtembelea na kumpa matumaini kwamba huenda akaenda nje kutibiwa.

“Baada ya gazeti lenu kuandika habari zangu, ujumbe wa Tamisemi umefika nyumbani kwangu kuniangalia na kuniahidi kwamba utafanya mipango kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili niweze kwenda nje kutibiwa,” alisema.

Alisema mbali na ujumbe huo, watu wengi ambao hawakuwa na taarifa zake, wameanza kumtembelea na wengine kumpigia simu wakimuombea kwa Mungu ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua.

“Nawashukuru waandishi wa mwananchi, kwani nyie ndiyo mlioujulisha umma kuhusu hali ya afya yangu, ninaomba kwa Mungu usiku kucha ili niweze kufanikiwa kutibiwa kwani maumivu ninayoyapata ni makali.

CHANZO: Mwananchi


UPDATE: Soma "utetezi" wa serikali HAPA

10 Nov 2010


Muungwana mmoja amenitumia comment ambayo kwa hakika imenigusa sana.Naomba niinukuu
Mbona umekatisha mijadala ya kuendeleza nchi ghafla mno. nilitegemea utakuwa na tasmini ya matokeo ya uchaguzi lakini umezimika ghafla. Vipi au jamani inakuwaje uchungu na nchi unakuwa kwa muda tu? Au wameshakutishia na wewe?
Naelewa kwanini mzalendo huyu anataka tufanye tathmini ya uchaguzi mkuu ambao wengi wetu tuliupa umuhimu wa kipekee kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo huko nyumbani.Baada ya kushuhudia taifa likienda mrama kwa kugubikwa na ufisadi ilionekana ni lazima Watanzania wenye uchungu wa dhati kwa nchi yao wachukue hatua zinazostahili.Na hatua mwafaka ilionekana kuwa ni kuing'oa CCM madarakani.

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,ameweka bayana msimamo wake kuwa uchaguzi huo ulichakachuliwa.Baadhi ya taasisi zilizotuhumiwa kufanya uchakachuaji huo zimejitokeza hadharani na kukanusha tuhuma hizo.Haihitaji hata cheti cha kozi ya siku 1 ya uchambuzi wa siasa kumaizi kuwa hakuna hata mmoja kati ya wanaotuhumiwa atakiri mchango wake katika kuirejesha CCM madarakani.Wakubali ili waadhibiwe?

Kadhalika,kuna dhana iliyojengeka kuwa katika uhalisia barani Afrika na katika baadhi ya nchi "za dunia ya tatu" sio rahisi kwa chama tawala kushindwa uchaguzi,na ikitokea kimeshindwa basi yayumkinika kuhitimisha kuwa hayo ni matokeo ya uzembe wa chama husika au migogoro ndani ya chama hicho.Hebu chukulia mfano mazingira ya uchaguzi wetu.Vyombo vya dola vilionyesha waziwazi kuipendelea CCM huku watendaji wa taasisi zinazopaswa kuwa huru wakijibidiisha kumlinda mgombea wa chama tawala.Ndio maana haikumtia hofu Mhariri wa Daily News,gazeti linaloendeshwa kwa kodi za walalahoi,kutamka bayana kuwa Dkt Slaa asingeweza kuwa rais hata baada ya miaka mitano.Kujiamini huko hakukutokana na uimara wa CCM bali ndoa ya kifisadi kati ya taasisi za umma na chama hicho tawala.

Tulisikia taarifa kadhaa kuhusu watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutowatendea haki wagombea wa vyama vya upinzani.Kadhalika,ilifika mahala Msajili wa Vyama vya Siasa akaamua kuweka wazi mahaba yake kwa CCM na kujipachika jukumubla kuitetea hata pale ilipokosea waziwazi.

Sasa unaweza kujiuliza,"kama tulishaona mwenendo wa aina hiyo ie wa kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi,kwanini tulijipa matumaini kuwa Dkt Slaa angeibuka mshindi?".Jibu rahisi kwa mtizamo wangu ni kwamba kulikuwa na matumaini kuwa sauti kubwa ya umma ingeweza kukwaza jitihada zozote za uchakachuaji.Au hata kama jitihada hizo zingefanyika basi zingezidiwa nguvu na sauti hiyo ya umma.

Naomba kukiri hadharani kuwa hofu yangu kubwa haikuwa kwenye mikakati ya kundi dogo lakini lenye nguvu kubwa la mafisadi bali MTAJI MKUU WA CCM yaani umasikini wa Watanzania walio wengi.CCM inategemea sana masikini na hata matokeo "halali" yanathibitisha hilo ambapo maeneo yaliyogubikwa na umasikini ndio yaliyoipa CCM kura nyingi.Huu ni uhusiano ambao kitaaluma unaweza kuelezwa kama wa mnyanyasaji na mnyanywasaji (abuser-abused relationship).Mnyanyasaji anawekeza nguvu nyingi kumwaminisha mnyanyaswaji kuwa pasipo uwepo wake (mnyanyasaji) basi mnyanyaswaji hatakuwa na maisha.Ndio hadithi za amani na utulivu,umoja wa kitaifa,mshikamano,na madude mengine kama hayo.

Kitaaluma,mnyanyaswaji anaweza kufikia mahala akawa anaskia raha kunyanyaswa (punch drunk).Ni kama hali ya kuzowea makonde kwa bondia.Hakuna maelezo mengine mwafaka ya kuelezea namna watu wanaoamka wakiwa hawajui siku iyaisha vipi,wanaotembea maili kadhaa kusaka maji safi japo wafadhili wanamwaga fedha za miradi ya maji,wanaoshinda juani kutwa nzima na kulala vibambazani wakiuza peremende lakini bado wanaandamwa na jeshi la mgambo huku polisi wakiwawinda wawabambikizie kesi,wanaokwenda mahospitalini na kuambulia matibabu hewa kwa vile hakuna madawa,watu wenye watoto ambao makalio yanaota sugu kwa kukaa sakafuni mashuleni,watu ambao haki zao hazipatikani bila kutoa "kitu kidogo" kisha watu haohao wakipigie kura chama kinachostawisha mateso yao.

Na kwa waliodhani akina sie tuliokuwa tukipiga kelele za nguvu kutaka CCM iondoke tulikuwa na chuki binafsi basi matukio mawili yaliyojiri hata masaa 72 hayajapita baada ya CCM kurejea madarakani yanapaswa kuwafumbua macho.Tukio la kwanza ni la mtuhumiwa wa ufisadi wa rada,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge kuchukua fomu ya kugombea Uspika kisha kufanya press conference iliyojaa ngebe,nyodo na dharau kwa wote wanaokerwa na ufisadi.Binafsi,naamini kuwa Chenge katumwa na kundi flani linalotaka kuifakamia keki ya taifa kwa kasi ya marathon hasa kwa vile wanaelewa kuwa Awamu hii ya Tano inaweza kuwa ni lala salama.Chenge ameonyesha bayana kuwa anataka kuwa Spika ili kusafisha majina ya "waliosingiziwa kuwa mafisadi".

Lakini kubwa zaidi ni hisia zangu kuwa Chenge ana baraka kamili za uongozi wa juu wa CCM ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti Jakaya Kikwete.Si bado tunakumbuka jinsi Kikwete alivyokwenda jimboni kwa Chenge kumpigia debe na kisha akatetea uamuzi wake wa kuwapigia debe watuhumiwa wa ufisadi kwa kudai kuwa kinachowakabili ni tuhuma tu.Kama tuhuma si tatizo mbona Bashe aliondolewa kwenye mchakato wa mchujo wa kupata wagombea ubunge kwa tiketi ya CCM kwa tuhuma kuwa sio raia wa Tanzania?Kwahiyo tuhuma kwa Chenge,Mramba,nk zinapaswa kubaki tuhuma tu lakini kwa wengine tuhuma ni sawa na hukumu!

Na kwa wanaidhani Chenge anafanya utani mbaya ( a bad joke) basi labda hawaielewi CCM vizuri.Chenge anaweza kabisa kupitishwa katika mfumo wa "kidemokrasia" wa CCM.Yea,kama ameendelea kuongoza kamati ya maadili ya chama hicho na kupitishwa kugombea ubunge (na kushinda) iweje basi kuukwaa uspika liwe suala gumu?Nguvu anayo,sababu anazo,sapoti anayo na VIJISENTI anavyo.Kipi cha kumzuwia kumrithi Samuel Sitta?

Tukio la pili linahisiana na hilo la kwanza ambapo Taasisi ya Kuzuwia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imekurupuka na kudai kuwa Chenge alishasafishwa katika tuhuma za ufisadi wa rada.Yaleyale ya kuisafisha Richmond japo angalau katika ishu ya Richmond serikali ya Kikwete ilikuwa na umri wa zaidi ya mwaka madarakani.Safari hii vimbwanga vimeanza hata kabla ya wiki kumalizika tangu iingie madarakani!Maumivu ya kichwa huanza polepole...

Na kwa kuthibitisha kuwa kura za kuirejesha CCM madarakani zilikuwa kura za kuubariki ufisadi,Ubalozi wa Uingereza umeishushua TAKUKURU kwa kutoa ufafanuzi kuhusu suala la ufisadi wa rada.Sijui nani ameipa TAKUKURU madaraka ya kusafisha watuhumiwa lakini hata sie tusio na uelewa mkubwa wa masuala ya sheria tunafahamu kuwa jukumu la kuhukumu ni la mahakama.Badala ya taasisi hiyo kumpeleka Chenge mahakamani ili kama kusafishwa asafishwe huku,yenyewe imekurupuka na utetezi wake wa kifisadi pasipo hoja za msingi.Hii yote ni katika kuandaa mazingira mazuri kwa Chenge kuwa Spika wa Bunge jipya.

Nitaendelea na tathmini yangu kadri siku zinavyosonga mbele.Najua kuna mengi tu ya kuyazungumzia hasa tukizingatia mazingaombwe yaliyotawala Awamu iliyopita hivyo ni suala la muda tu kabla hayajajiri mengine mengi ya kuwasuta wale wote waliotarajia miujiza kutoka kwa CCM.

6 Nov 2010


Urban Pulse Inawaletea video fupi kuhusu ziara ya Diamond hapa UK kwa ajili ya kuchangia vita dhidi ya Malaria. Tarehe 03.11.2010 Timu nzima Ya Urban Puse ikiwa na Diamond walipata fursa ya Kutembelea Ubalozi wa Tanzania kwa ajili ya kumtambulisha Diamond na kutoa shukrani.



Urban Tour itaanza Rasmi jumamosi tarehe 6.11.10 Milton keynes Club Opus ikifuatana na Croydon London tarehe 12.11.10


Asante sana,

Urban Pulse



Picha zote hapo juu ni za mtu mmoja.Alipanda ndege huko Hong Kong akiwa "kibabu" na kuteremka Kanada akiwa kijana.Actually,huyu ni kijana halisi lakini alijivika kinyago na kuonekana kikongwe,lengo lake likiwa kuingia nchini Kanada kuomba ukimbizi.


4 Nov 2010


Scores of iPhone users were late to work on Monday, after a bug in the software meant the device's alarm clock feature failed to adjust to Daylight Saving Time. Skip related content

Hundreds of angry comments were posted on the social networking website Twitter about the glitch on the Apple device, which occured even though the rest of the phone's features updated the time automatically.

"Well done Apple - you've made me decide I need to use a proper alarm clock rather than relying on my iPhone," one user tweeted.

"Stupid iPhone alarm clock went off an hour late. What a great start to the week," said another.

Australian iPhone users experienced similar problems three weeks ago, although alarms went off an hour early there rather than an hour late.

Apple said at the time that a software patch was being developed to resolve the issue. The technology giant has not yet issued an official response to the British version of the glitch.

The popular gadget has suffered a turbulent year. The latest iPhone 4 model has been blighted by problems with its antennae, proximity sensor and security system.

The latest fault can apparently be avoided by using one-off alarms instead of pre-set daily wake-up calls.


Baada ya kutua na kutulia ndani ya UK Diamond alifanikiwa kufanya promo pamoja na kuongea na fans wake





asante

Urban Pulse creative

3 Nov 2010

MGOMBEA urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema, atayakataa matokeo ya urais yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kumefanyika wizi mkubwa wa kura.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema, kama NEC inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.

"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa

Chanzo: Mwananchi
ENDELEA KUFUAtILIA BLOGUNI HAPA



Habari za kuthibitisha kutoka Urban Pulse zinathibitisha kuwa Msanii Diamond tayari katua Ndani ya UK tayari kwa ajili ya kukamua show ya Urban Tour kwa ajili ya kuchangia kupigana vita dhidi ya Malaria. Show yake ya kwanza itafanyika katika Mji wa Milton keynes Jumamosi hii tarehe 6.11.10 ndani Ya Club OPUSPRICE  

Price £10.00 BEFORE MIDNIGHT MORE AFTER
VIP £20.00

WOTE MWAKARIBISHWA,

URBAN PULSE CREATIVE MEDIA

Promo

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.