8 Aug 2012


JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII
 
 





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI – (PRESS RELEASE) ILIYOTOLEWA NA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, MHE. BALOZI KHAMIS .S. KAGASHEKI LIWALE
TAREHE 8/8/2012


NDUGU WAANDISHI WA VYOMBO VYA  HABARI:

1.0    SALAMU ZA JUMLA:
NACHUKUA NAFASI HII KUWAKARIBISHA NA KUWAPONGEZA KWA JINSI MNAVYOSHIRIKIANA NA WIZARA HII KUPIGA VITA UHALIFU / UJANGILI WA RASILIMALI ZA TAIFA. AIDHA NATAMBUA JINSI MLIVYOTENGA MUDA WENU  NA KUFIKA HAPA ILI TUPEANE TAARIFA ZA KIUTENDAJI HUSUSANI OPERESHENI INAYOENDELEA KATIKA WILAYA YA LIWALE MKOA WA  LINDI.

NDUGU WANAHABARI:
2.0           UTEKELEZAJI WA  OPERESHENI:
KUMEKUWA NA ONGEZEKO LA VITENDO / WIMBI LA UHALIFU / UJANGILI WA NYARA ZA SERIKALI AMBAO UNAATHIRI RASILIMALI ZA TAIFA HUSUSANI WANYAPORI TEMBO, VIBOKO, SIMBA, MAMBA, TWIGA, NYATI NA WANYAMA WENGINE PAMOJA NA UVUNAJI HARAMU WA MAZAO YA MISITU. KUTOKANA NA HALI HIYO, WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII ILIOMBA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI KUPITIA WIZARA YA MAMBO NDANI YA NCHI KUANDAA OPERESHENI MAALUM WILAYANI LIWALE KUDHIBITI HALI HIYO. JESHI LA POLISI LILIKIAGIZA KITENGO CHA KUPAMBANA NA UHALIFU MKUBWA NCHINI (NATIONAL AND TRANSNATIONAL SERIOUS CRIME INVESTIGATION UNIT – NATIONAL TASK FORCE) AMBACHO KINAVISHIRIKISHA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYA (POLISI, JWTZ, TISS, MAGEREZA, UHAMIAJI NA OFISI YA DPP) KUTEKELEZA MAJUKUMU YA OPERESHENI MAALUM KAMA ILIVYOELEKEZWA. OPERESHENI HII ILIANZA TAREHE 22/07/2012  NA NI ENDELEVU. KATIKA OPERESHENI HIYO MAOFISA WAKUU WAANDAMIZI, MAOFISA WA KATI, WAKAGUZI NA ASKARI WA KAWAIDA KUTOKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA TAJWA HAPO JUU WANASHIRIKI UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HIYO.  

MATOKEO YA AWALI YA UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HII NI KAMA IFUATAVYO;
v WATUHUMIWA 101 NA KESI 101 ZIMEFUNGULIWA KITUO CHA POLISI LIWALE KATI YA HIZO:

i.                     KESI  15 ZIMEFIKISHWA MAHAKAMANI NA MIONGONI MWAKE KESI MOJA (1) IMETOLEWA HUKUMU NA ZILIZOBAKI ZIKO KWENYE HATUA MBALIMBALI MAHAKAMANI,

ii.                  KESI 20 ZIMESIKILIZWA NA KUPATA HUKUMU YA “BINDING OVER”, MIONGONI MWAKE KESI 7 ZIMEPATA MAAMUZI NA 13 ZINASUBIRI MAAMUZI YA MAHAKAMA. MASHARTI YA “BINDING OVER” YALIYOTOLEWA YAMETOLEWA DHIDI YA WATUHUMIWA;
a.                 KUTOTOKA NJE YA WILAYA YA LIWALE BILA KIBALI CHA HAKIMU MKAZI WA WILAYA

b.                KURIPOTI KWA OC CID KITUO CHA POLISI LIWALE  KILA MWISHO WA MWEZI

c.                 KUITWA KUHOJIWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA WAKATI WOWOTE KADRI ITAKAVYOONA INAFAA
d.                KUTOFANYA KOSA LOLOTE NDANI YA MIAKA MIWILI YA MATAZAMIO

e.                 KWA WALIOKUWA WAMILIKI WA SILAHA, SILAHA ZAO ZIMEHODHIWA POLISI LIWALE KWA MUDA WA MIAKA MIWILI NA MMILIKI ATAWAJIBIKA KUANZA TARATIBU ZA MAOMBI YA KUMILIKI SILAHA HIYO / HIZO UPYA PINDI UTEKELEZAJI WA HUKUMU HIYO ITAKAPOMALIZIKA

f.                  KUWEKA DHAMANA YA MALI ISIYOHAMISHIKA YENYE THAMANI YA TSH. 5,000, 000.00 NA MALI HIZO ZIWE NDANI YA WILAYA YA LIWALE


II.        KESI 66 ZINAENDELEA KUFANYIWA UCHUNGUZI ILI WAHUSIKA WAFIKISHWE MAHAKAMANI
v AIDHA KATIKA OPERESHENI HII VIJIJI 27 VYA WILAYA YA LIWALE VINGI VIKIWA VIMEPAKANA NA HIFADHI YA SELOUS VIMEHUSIKA. MATOKEO YAKE NI KUPATIKANA KWA SILAHA 80, RISASI 674 NA MAGANDA YA RISASI 289 KAMA IFUATAVYO;
v BUNDUKI 79 ZILIZOKAMATWA NI;
i.                    SAR - 1,
ii.                RIFLE - 16
iii.             SHOT GUN  - 63

v JUMLA YA RISASI 645 ZIMEKAMATWA NI;
i.                    SAR - 20,
ii.                RIFLE - 8
iii.             SHOT GUN – 647

v MAGANDA YA RISASI 289 YALIYOKAMATWA NI  ;
i.                   RIFLE - 99
ii.                 SHOT GUN – 190

v NYARA ZA SERIKALI;
SN
AINA YA NYARA ZILIZOKAMATWA
KIASI
THAMANI TSH
1
MENO YA KIBOKO,
80
18,892,500.00
3
MENO YA TEMBO
14
164,075,000.00
5
BANGILI MOJA YA USINGA WA MKIA WA TEMBO
1
23, 625, 000.00, 
6
NGOZI  ZA SIMBA,
2
15,435,000.00
7
NGOZI YA CHUI,
1
5,505,500.00
9
MIKIA MIWILI YA NGEDERE
2
378,000.00
10
KICHWA CHA NYATI CHENYE PEMBE 2,
1
2,992,500.00
11
NYAMA YA  NYATI ,
KG
2,988,700.00
12
KICHWA CHA POFU CHENYE PEMBE 2,
1
2,677,500.00
JUMLA KUU
212,944,700.00

v VIELELEZO VINGINEVYO
o       GARI NDOGO AINA YA  TOYOTA CORONA NO. T. 836 ADV 

o       PIKIPIKI MBILI ZA SANLG T. 901 BXQ NA T. 772 BSD

o       MSUMENO WA MBAO NA MBAO 149



3.0    LENGO LA OPERESHENI;
OPERESHENI HII MAALUM INALENGA KUZUIA, KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA UHALIFU / UJANGILI KATIKA MAENEO MBALIMBALI NCHINI WILAYA YA LIWALE IKIWA KAMA ‘ROLE MODEL’.

4.0           MAFANIKIO;
I.                  KWA KUWA OPERESHENI HII IMEPANGWA NA KUENDESHWA KITAALAM NA KISAYANSI (INTELLIGENCE LED OPERATIONS), MAFANIKIO YAFUATAYO YAMEJIDHIHIRISHA;

a.                 IMEUNGWA MKONO NA KUSIFIWA NA RAIA NA WANANCHI KWA UJUMLA KWA MAELEZO KUWA HAKUNA MTUHUMIWA ALIYEKAMATWA KWA KUONEWA.

b.                 KUMEKUWEPO NA MAPOKEO CHANYA (POSITIVE IMPACT) KUTOKANA NA WANANCHI KUTAMBUA KUWA MWENENDO WA OPERESHENI HII UNAIPA HESHIMA KUBWA SERIKALI

c.                 HAKUKUWA NA RAIA MWEMA ALIYEBUGHUDHIWA AU KULALAMIKIA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA OPERESHENI HII

ii.                MTANDAO WA UHALIFU WA UJANGILI UNAVUNJWA NA WAHUSIKA WOTE SASA WANAFAHAMIKA NA UCHUNGUZI MAKINI NA WA KINA UNAENDELEA DHIDI YAO NA WATAFIKISHWA MBELE YA MAHAKAMA NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE

iii.             BAADHI YA WAZEE WENYE UMRI MKUBWA NA AMBAO AFYA ZAO ZILIONEKANA KUTOMUDU MASHARTI YA KUENDELEA KUMILIKI SILAHA WALIZISALIMISHA WENYEWE NA KUOMBA ZIHIFADHIWE KATIKA KITUO CHA POLISI LIWALE MPAKA MAAMUZI YATAKAPOTOLEWA NA MAHAKAMA DHIDI YA SILAHA HIZO.

iv.             WALE AMBAO MAHAKAMA ITAONA WAMEPOTEZA SIFA ZA KUMILIKI SILAHA ZITAHODHIWA KITUO CHA POLISI KUSUBIRI UTEKELEZAJI WA MAAMUZI YA MAHAKAMA


5.0           CHANGAMOTO:
i.                   BAADHI YA WAMILIKI WA SILAHA SIO WAAMINIFU    KWA KUWA WANATUMIA SILAHA ZAO KUFANYA UJANGILI AU KUZIAZIMISHA KWA MAJANGILI. 

ii.                BAADHI YA WAMILIKI WA SILAHA WAMEPOTEZA SIFA ZA UMILIKI KUTOKANA NA MATATIZO YA KIAFYA; MFANO KUKABILIWA NA UPOFU, UGONJWA WA KIHARUSI N.K JAMBO AMBALO LINACHANGIA WAO KUSHINDWA KUZINGATIA NA KUTEKELEZA TARATIBU ZA UMILIKI WA SILAHA

6.0           MUONO WA MBELE (WAY FORWARD);
i.                   WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII ITAENDELEA KUTOA ELIMU KWA JAMII ZINAZOISHI KANDOKANDO YA MAPORI YA AKIBA /  HIFADHI KUHUSU UMUHIMU WAO WA KUTOJIHUSISHA NA UJANGILI NA WAWE VYANZO VYA TAARIFA ZA KIINTELIJENSIA KUFUATIA MKAKATI MADHUBUTI WA KUDHIBITI MTANDAO WA UJANGILI NCHINI.

ii.                UTAKUWEPO MWENDELEZO WA KUBORESHA NA KUIMARISHA DORIA, MISAKO NA HATUA NYINGINE ZA KIOPERESHENI KWENYE MAPORI YA AKIBA NA HIFADHI ZA TAIFA MARA KWA MARA KUFUATIA MUONGOZO WA TAARIFA ZA KIINTELIJENSIA KADRI ITAKAVYOONEKANA INAFAA KATIKA KUFANYA OPERESHENI ZA PAMOJA (JOINT OPERATIONS INVESTIGATIONS & INTELIGENCE –JOII)  KWA KUTUMIA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUPITIA “TASK FORCE” YA KITAIFA .

7.0    MWISHO
NAWAPONGEZA MAOFISA WAANDAMIZI, MAOFISA WA KATI, WAKAGUZI NA ASKARI WA VYEO MBALIMBALI WANAOSHIRIKI UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HII INAYOENDELEA. KWA UJUMLA NAMALIZIA KWA KUWASHUKURU TENA NYINYI WANAHABARI MLIOFIKA HAPA KWA USHIRIKIANO MNAOUTOA KATIKA KUPAMBANA NA UHALIFU HUU.


ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA
//////////////////////////////////////////MWISHO///////////////////////////////////////

IMETOLEWA TAREHE  08/08/2012  NA

MHE. BALOZI KHAMIS .S. KAGASHEKI (MB)
WAZIRI


NAKALA KWA:
VYOMBO VYA HABARI

6 Aug 2012

Champion again: Jamaica's Usain Bolt crosses the finish line to win gold in the men's 100-metre final in the Olympic Stadium in London
BOLT AKIVUKA MSTARI NA KUSHINDA


Outright winner: Usain Bolt streaks clear of the field to claim gold from lane seven in one of the most eagerly awaited Olympic events ever
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO NA KUSHINDA 



Showman: Usain Bolt celebrates his victory by striking his customary lightning bolt pose in the Olympic Stadium in London
USAIN BOLT AKIONYESHA POZI YAKE MAARUFU YA 'RADI' (LIGHTNING BOLT) BAADA YA KUSHINDA


Points ahead: Usain Bolt proved his doubters wrong and retained the Olympic 100m title he first won in Beijing in 2008
USAIN BOLT AKIWEKA POZI YAKE BAADA YA KUSHINDA


Taking a bow: Jamaica's Usain Bolt kneels and rests his head against the track in the Olympic Stadium after recording the second-fastest time ever
USAIN BOLT AKIINAMISHA KICHWA ARHDINI BAADA YA KUSHINDA


Star attractions: Jamaican sprinters Usain Bolt (right) and Yohan Blake (left) are mobbed by fans after winning gold and silver in the race
USAIN BOLT NA YOHAN BLAKE WAKISHANGILIA NA MASHABIKI


Golden boy: The Olympic champion in typical pose with the Olympic mascot
USAIN BOLT AKIWA NA MDOLI (MASCOT) WA OLIMPIKI


They're off: Usain Bolt (third left) did not start well in lane seven but he was comfortably leading the field as the athletes entered the final 20 metres
USAIN BOLT HAKUANZA VIZURI SANA KWENYE MSTARI (LANE) WA SABA LAKINI AKAMUDU KUSHINDA KWA KISHINDO


Effort: The world's fastest men - Usain Bolt (second left), Justin Gatlin (left), Yohan Blake (second right) and Tyson Gay (right) - strive to reach the line first
BINADAMU WENYE KASI KULIKO WOTE DUNIANI


Storming in front: Bolt (second left) crosses the finish line first, ahead of fellow Jamaican Yohan Blake (second right) and bronze medallist Justin Gatlin (centre)
NI USAIN BOLT TENA


Global appeal: Some 80,000 spectators in the Olympic Stadium watched the 100-metre race, as well as an estimated worldwide television audience of up to two billion
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO KWA KISHINDO


Picture perfect: Cameras flash as spectators capture the moment that Usain Bolt left his competitors in his wake
BINADAMU MWENYE KASI ZAIDI USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA YA OLIMPIKI HUKU PATNA WAKE  WA MAZOEZI ,MJAMAIKA YOHAN BLAKE (WA TATU KULIA) AKISHIKA NAFASI YA PILI NA MMAREKANI JUSTIN GATLIN (WA TATU KUSHOTO) AKISHIKA NAFASI YA TATU


Number one: Usain Bolt raises a finger after clinching victory, with the time reading 9.64 seconds on the electronic board behind. The time was later officially rounded down to 9.63 seconds
USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA 


Rapid results: Bolt ran the second-fastest time ever - an Olympic record of 9.63 seconds. Yohan Blake won silver with a time of 9.75 and Justin Gatlin took bronze in 9.79. Seven men clocked a time below 10 seconds
MATOKEO


World order: American bronze medallist Justin Gatlin (left) can only look on with envy as Jamaica's Usain Bolt (right) rewrites Olympic history once again
MWANARIADHA WA MAREKANI JUSTIN GATLIN ALIYESHIKA NAFASI YA TATU AKIMWANGALIA USAIN BOLT



On fire: Usain Bolt runs past the Olympic flame after winning the sprint final for Jamaica in scintillating fashion
USAIN BOLT AKIPITA PEMBENI YA 'MWENGE WA OLIMPIKI'  BAADA YA KUSHINDA MBIO ZA MITA 1OO WANAUME


Out of contention: Usain Bolt's Jamaican team-mate Asafa Powell, who pulled up injured during the race, looks forlorn after finishing eighth
MWANARIADHA WA JAMAIKA ASAFA POWEEL AKIWA AMESHIKA TAMA BAADA YA KUMALIZA WA MWISHO KUFUATIA MATATIZO YA MISULI


Bolt's our boy: Fans in Brixton watch Usain storm to victory in the 100m
MASHABIKI KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON JIJINI LONDON WAKISHANGILIA USHINDI WA USAIN BOLT


Fans who watched the race at the O2 Arena salute their hero with his 'Lightning Bolt' pose
MASHABIKI WAKISHANGILIA KWENYE UWANJA WA O2 HUKU WAKIONYESHA POZI YA USAIN BOLT


By Royal appointment: The Duke and Duchess of Cambridge and Prince Harry, sitting in front of the Culture Secretary Jeremy Hunt, were among the 80,000 spectators inside the Olympic Stadium
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE NA PRINCE HARRY WAKIWA NA 'WAZIRI' WA UTAMADUNI JEREMY HUNT (NYUMA YA DUKE)



Behind Bolt: Prince Harry wore Jamaican colours as he accompanied his brother and sister-in-law at the athletics
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE (PRINCE WILLIAM NA MKEWE KATE MIDDLETON-WA KWANZA NA WA PILI KUSHOTO) WAKIFUATILIA KASI YA USAIN BOLT HUKU PRINCE HARRY AKIWA AMEJITUNDIKA BENDERA YA JAMAIKA


Psyched: Jamaica's Yohan Blake, pictured gesturing prior to competing in his semi-final, was one of the favourites for the Olympic title as he came into the race in excellent form
YOHAN BLAKE, PATNA WA MAZOEZI WA USAIN BOLT ALIKUWA AKITARAJIA KUTOA UPINZANI MKALI LAKINI AKAISHIA KUWA WA PILI


Fighting fit: Usain Bolt, who had been troubled by a hamstring injury, claimed he was only 95 per cent fit but he looked in fine condition before the eagerly awaited final
USAIN BOLT AKIFANYWA MBWEMBWE KABLA YA MCHUANO


Fervour: Spectators from the Jamaican community in Brixton, south London, watch their heroes in action on television on the 50th anniversary of the Caribbean island's independence from Britain
JUMUIYA YA WAJAMAIKA KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON,JIJINI LONDON WAKIFUATILIA USHIRIKI WA WANARIADHA WAO 


CHANZO: Daily Mail

5 Aug 2012


Makada wa CCM wakiwa na kadi za  uwanachama kwa wanachama wapya  katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM

  
Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV

Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  Makada wa CCM Tawi la DMV shoto Mbunifu wa Ma Winny Casey Khanga Wrap Designer, pamoja na Peter Ligate (Picha ya kulia) wakiwa katika mpango mzima wa futari ya pamoja ilioandaliwa na wanatawi la CCM DMV

Watanzania  waliojumuika  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  
Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi  wageni walikwa  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Baadhi ya wanachama wa  CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda 


Wanachama wa  CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza

Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na  ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani


Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na  Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa  na kuwa mwanachama rasmi wa CCM



Chanzo: SWAHILIVILLA

4 Aug 2012


The Arab Spring has changed the landscape in North Africa, not only politically but also culturally and musically. Spreading throughout the region alongside demands for political freedom, rap music has become a popular way for people to express their desire for change.

The Arab Spring: Dawn of a musical revolution 
Across North Africa and the Middle East people have risen up and demanded a voice. And while the calls may have been political in nature, protestors have used various cultural means to express their desire for change, including music and, specifically, rap.

Media has been at the very heart of the demands for change, with the young using tools such as the internet to spread their message. Music has been another weapon. So often a voice for the disenfranchised, rap music has political defiance and revolutionary ideals at its very core. So it is hardly surprising that the genre has taken off in North Africa in the past 18 months, providing people with the means to express themselves.

The changing voice of rap music
Coming out of the U.S. in the 70s, rap became a global phenomenon in the 80s and has had a presence in North Africa since the 90s. But it is only with the demise of dictatorships in Tunisia, Egypt and Libya that the genre was able to free itself from censorship.

Previously, few had dared to speak out against their governments, fearful of retribution. But the Arab Spring has given young musicians the confidence to speak out. Some of the biggest artists in this musical groundswell are Tunisia's El General, DJ Costa and Psyco-M; Egypt's Ahmed Mekky, Ramy Donjewan and Arabian Knightz; and Libya's Emad Abbar and Hamza Sisi. The popularity of these and other artists continues to grow by the day.

The revolution will be televised… online
The internet has made it easier than ever to share music and in the face of state censorship artists relied on the Web to spread their message enabling their songs to spread from city to city and cross national boundaries.

Traditional media channels such as newspapers and television may have been muted by state control, but crumbling regimes were powerless to contain Twitter and Facebook. These social tools gave young people across North Africa a way to connect with others who felt the same and unite behind the revolutionary ideals expressed in the lyrics of their songs. 


SOURCE: Yahoo! News


KUNA msemo mmoja ninaopenda sana kuutumia kusisitiza hoja katika maongezi, ambao unasema, “Ili uweze kulielewa giza inabidi utoke au uende katika mwanga, na kinyume chake (vice versa).”
Huwa ninautumia msemo huu kubainisha ‘faida’ tuliyonayo baadhi yetu (Watanzania) tulio nje ya nchi yetu. Kwamba, kuwa kwetu huku kwa namna fulani kunatusaidia kuwa kama kile kinachofahamika katika tafiti kuwa ni “participant as an observer,” yaani kwa tafsiri isiyo rasmi ‘mshiriki ambaye pia ni kama mwangalizi.’
Kwa kuwa huku ughaibuni sio tu tunapata fursa ya kulinganisha tofauti ya mambo kati ya hapa na huko nyumbani bali pia tunaweza kuiangalia jamii yetu inayotuhusu lakini tukabaki watazamaji.
Hata hivyo, kuna wakati baadhi yetu tulio nje hukumbanana wakati mgumu kuzungumzia mambo ya huko nyumbani, hususan, kutokana na madai kuwa yanayotokea huku hayatugusi moja kwa moja.
Baadhi ya ‘wapinzani wetu’ hudiriki kwenda mbali zaidi na kutulinganisha na Watanzania ‘tusio kamili’ kwa maana ya kwamba shida au raha za huku  hazitukabili katika namna zinavyowakabili wao.
Huu ni mtizamo potofu hasa ikizingatiwa kuwa wengi wetu, kama si sote, bado tuna ndugu, jamaa na marafiki huko nyumbani. Kimsingi, kuwa nje ya Tanzania hakumpunguzii mtu Utanzania wake, isipokuwa tu kwa wenzetu wachache ambao kuwa kwao huku kunamaanisha ‘talaka’ kati yao na asili yao.
Ni katika kuiangalia nchi yetu kwa mtizamo huo wa ‘mshiriki ambaye ni kama mwangalizi’ ndipo nimejikuta nikifikia hitimisho kwamba mwenendo wa mambo huko nyumbani una mushkeli.
Kati ya wiki iliyopita na muda huu ninapoandaa makala hii kumejitokeza matukio kadhaa yanayoweza kuashiria kuwa nchi yetu inakwenda ‘ndivyo sivyo.’
Nitatoa mifano machache. Habari ambayo imetawala katika vyombo vingi vya habari kwa sasa kuhusu mambo yalivyo huko nyumbani ni hili suala la baadhi ya wabunge kutuhumiwa kupokea rushwa.
Habari hiyo inapata uzito mkubwa zaidi pale inapotanabahisha kuwa licha ya baadhi ya wabunge kuandamwa na tuhuma hizo, baadhi ya Kamati za Bunge pia zinatuhumiwa kujihusisha na rushwa, hali iliyopelekea Spika wa Bunge kuamua kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Lakini tuhuma hizi za rushwa zimefichua kitu ambacho binafsi ninakiona kama tatizo la msingi katika jamii yetu. Katika siku chache zilizopita, nimekuwa nikitumia muda wangu mwingi katika mtandao wa kijamii wa twitter kuzungumzia tuhuma hizo dhidi ya wabunge, hususan, wale wanaodaiwa kupokea mlungula ili kulifisadi Shirika la Umeme (TANESCO).
Jumapili iliyopita mmoja wa tunaoweza kuwaita watu maarufu (celebrities) alionekana kuchukizwa na twiti zangu ambazo kimsingi zilikuwa zinaelekezwa kwa mbunge mmoja wa chama cha upinzani ambaye ametangaza dhahiri kuwa ana nia ya kuwa rais wetu huko mbele.
Katika mazingira ya kawaida tu, mwanasiasa anayetamka hadharani kuwa anataka kuwa rais ni lazima aangaliwe kwa makini ili wapiga kura wapate fursa nzuri ya kumuelewa.
Kwa sababu anazozijua yeye binafsi, celebrity huyo wa kike alinivurumishia maneno makali akidai kuwa tuhuma nilizotoa dhidi ya mwanasiasa huyo zina dalili za chuki binafsi, hasa kwa ile haijathibitishwa kuwa mwanasiasa huyo ni fisadi.
Lakini kabla sijatulia,      mwanamama mwingine msomi na mwenye wadhifa kwenye taasisi moja ya umma naye akanihoji ni mahali gani mwanasiasa huyo ametajwa kuwa ni mwizi. Labda hadi hapa msomaji unaweza kujiuliza kwanini ‘utetezi’ dhidi ya mwanasiasa huyo unaonekana kwa jinsia moja tu.
Huyu mtu wa pili kukerwa natwiti zangu kuhusu mwanasiasa huyo ndiye aliyenigusa zaidi, kwa sababu kimsingi, elimu na madaraka yake yanamweka katika kundi la kijamii linalofahamika kama tabaka la kati.
Nilishawahi kuandika katika makala moja huko nyuma kuhusu jinsi tabaka hili la kati linavyoshindwa kuwa kiunganishi cha kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi.
Nilieleza katika makala hiyo kwamba tabaka la kati lingeweza kuwa nguvu muhimu ya kupigania maslahi ya tabaka la chini kutambuliwa, na hatimaye kufanyiwa kazi na tabaka la juu (ambalo hujumuisha tabaka tawala).
Nikinukuu maneno ya binti huyo wa pili, alinieleza kuwa “wanamchukia mwanasiasa huyo wajinyonge, kwani njia yake kuelekea Ikulu ipo wazi.” Niliguswa sana na maneno haya kwa sababu wakati mwanasiasa huyo anaonekana kupata utetezi katika tuhuma zinazomkabili kuhusu kuifisadi TANESCO, sio tu kuna watuhumiwa wengine wasiotetewa bali pia hata huko nyuma baadhi ya wanasiasa waliotuhumiwa kuwa mafisadi hawakuwahi kutetewa kiasi hicho.
Japo ninatambua na kuheshimu haki ya kila Mtanzania kumtetea mwanasiasa anayempenda, ukweli ni kwamba licha ya utetezi huo kuwa wa ‘upendeleo’ (kile kinachoitwa na Waingereza kuwa ni haki ya upendeleo-selective justice), kwa maana ya kuwa watuhumiwa wengine kwenye kashfa hiyo hawapati utetezi kama ilivyo kwa mwanasiasa huyo, tunapotetea tuhuma za ufisadi kwa vile tu ‘tuna mahaba’ na tunaowateta, tunaweza kuwafahamasisha mafisadi wengine waendelee kuitafuna nchi yetu wakijua watatetewa.
Moja ya mambo yanayokwaza sana maendeleo yetu ni kile ninachokiita ‘siasa za mahaba.’ Kwamba mgombea uongozi hapimwi kutokana na sifa na/au uwezo wa kutumikia umma bali kinachoangaliwa ni urafiki, haiba na vitu kama hivyo visivyoweza kuwa vigezo vya uongozi bora
Bado ni mapema kutoa hitimisho kuhusu wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa, hususan hiyo ya kuihujumu TANESCO, ukweli kwamba tuhuma hizo zimewekwa hadharani unaeleza bayana kuwa ufisadi umeingia katika hatua mpya na ya hatari zaidi ambapo baadhi ya watu tuliowakabidhi dhamana ya kutunga sheria (ikiwa ni pamoja na zile za dhidi ya ufisadi) nao ni sehemu ya tatizo la ufisadi.
Nimebainisha hapo mwanzoni kuwa matukio ya hivi karibuni yanaashiria kwamba hali ya mambo si shwari. Jingine lililonigusa ni suala la mgomo wa walimu ambapo japo kumekuwa na taarifa za kukanganya, kuna dalili kuwa mgomo huo unaendelea.
Lakini tukio lililotokea katika shule ya msingi ya Maili Moja, Kibaha, linaweza kutufumbua macho zaidi kuhusu mwenendo wa nchi yetu. Inaelezwa kuwa katika tukio hilo, wanafunzi wenye hasira waliamua kuvurumisha mawe shule yao. Sina hakika kama walifanya hivyo kama ishara ya kupinga mgomo wa walimu wao au kuwaunga mkono, lakini kilicho wazi ni kuwa pindi inapofika mahala wanafunzi wa shule ya msingi wanachukua ‘sheria mkononi’ basi ni wazi kuwa Taifa letu limefika mahali pabaya.
Wanafunzi hawa ndio kizazi cha kesho, ndio mawaziri na wabunge wetu, ndio viongozi wa kesho. Sasa inapofika mahala nao wanaingia katika utamaduni mpya wa ‘vurugu kama ufumbuzi wa matatizo’ sijui huko mbele itakuwaje.
Majuzi tu tulishuhudia mgomo wa madaktari ambao bado unaelekea kuwa haujaisha kwa utimilifu (taarifa kwenye mtandao mmoja wa jamii inaeleza kuwa baadhi ya madaktari wameonyesha dhamira ya kutaka kurejea tena kwenye mgomo). Kabla hatujasahau kuhusu mgomo huo tunasikia jinsi baadhi ya wabunge wanavyoshiriki kuihujumu TANESCO.
Wakati huohuo tunashuhudia baadhi ya walimu wakiamua kutimiza azma yao ya siku nyingi ya kugoma. Lakini pengine kubwa na la kutisha zaidi ni taarifa kuwa mmoja wa viongozi maarufu wa dini amekumbwa na kashfa ya shule yake kuiba uniti za umeme wa TANESCO. Haya yote (na mengine ambayo nafasi hairuhusu kuyataja) yanaashiria kuwa hali si shwari huko nyumbani.
Je, viongozi wetu wanafanya nini kukabiliana na hali hii? Usidhani hiki ni kichekesho lakini siku moja kabla sijaandaa makala hii kulikuwa na taarifa kuwa Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai alionekana anaongea na simu wakati kikao cha Bunge kinaendelea.
Labda ilikuwa ni simu muhimu kutoka kwa Spika au pengine Rais, lakini taswira ilivyotokana na tukio hilo inaweza kutanabaisha ni jinsi mtizamo wangu kuwa hali ya mambo si shwari huko nyumbani ilivyotofautina baadhi ya viongozi wetu, ambapo hata kwenye majukumu muhimu ya kuogoza Bunge wanamudu kuongea na selula zao.
Funga kazi ni uamuzi wa Serikali kulifungia jarida la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa jarida hilo limekuwa likiandika habari za uchochezi.
Katika toleo lililopita jarida hilo kulikuwa na habari kuhusu suala la Dk. Steven Ulimboka na mtumishi wa taasisi nyeti ya serikali alihusishwa nayo. Je, serikali haidhani kuwa uamuzi wake kulifungia jarida hilo unaweza kutafsiriwa kama unalenga kulizuia kuibua ‘makubwa zaidi’ kuhusu sakata hiyo?
Hivi isingewezekana kulifikisha jarida hilo mahakamani ili haki si tu itendeke bali ionekane imetendeka? Na je, uamuzi wa kulifungia unasaidiaje kuzifanya habari zilizoandikwa nalo zionekane ni uchochezi tu.
Nimalizie kwa kutoa rai ya haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu hatma ya Taifa letu. Tunakoelekea si kizuri. Na hili la mjadala si kuhusu tabaka tawala (walio katika bunge, serikali, nk) bali pia kuna haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu nafasi ya tabaka la kati katika kuhamasisha, kutetea na hata kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi linaloelekea kuachwa bila mtetezi wala msomaji.
Tanzania ni yetu sote. Tuweke kando siasa za mahaba, tuepuke kutanguliza maslahi binafsi badala ya maslahi ya Taifa, tutatue tofauti zetu (migomo, nk) kwa njia za kidiplomasia, na kubwa zaidi tuungane kwa pamoja kuhangaikia kuipeleka nchi yetu katika mwelekeo sahihi.
Inawezekana, timiza wajibu wako.


1 Aug 2012



MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI


MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Ndugu Waandishi,
Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote  zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi cha kuukanganya umma.
Nafahamu nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa, jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa taifa.
Mkakati huo wa kuniunganisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wanaotuhumiwa kwa kupokea Rushwa unatekelezwa kwa njia zifuatazo:
  1.   Kumekuwa na kauli za watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakizieneza na hususan kutoa taswira kwamba baadhi ya kauli zangu zinatokana na ushawishi wa rushwa;
  2.   Kuna taarifa ambazo zimeandikwa tena katika kurasa za mbele za baadhi ya vyombo vya habari  zikidai ’’Zitto kitanzini’’ ama ’’Zitto sawa na popo nundu’’  zikiashiria kwamba na mimi ni mla rushwa; na
  3.   Waandishi wa habari na jamii kwa ujumla wamefikia kuaminishwa habari hizi kiasi cha wengine kuuliza kwa nini Mhe. Zitto Kabwe hakutajwa katika orodha iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani.
Ndugu Waandishi,
Naomba kutoa ufafanuzi wa hicho kinachoelezwa kwamba nina ushiriki katika masuala ya rushwa hususan kwenye masuala yanayohusu sekta ya Nishati na Madini:-
  1. Mara baada ya bodi ya Wakurugenzi ya  Shirika la Usambazaji wa Umeme Tanzania (TANESCO) chini ya Uenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Robert Mboma kutangaza kwamba imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nd. William Mhando ili kupisha uchunguzi wa baadhi ya vitendo/mwenendo wake, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) ambayo mimi ni Mwenyekiti wake ilimuandikia Mhe. Spika kumuomba aridhie ili Kamati iweze kuwaita Bodi ya TANESCO, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali  (CAG) na pia Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kujiridhisha na tuhuma zote zinazotajwa zinafanyiwa uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa;
  2. Kamati ya POAC ninayoiongoza ilimuomba Mhe. Spika kuwaita wahusika tajwa kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi huyo siku chache kabla ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ’madudu’ makubwa zaidi kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana. Isitoshe, Kamati kutaka kujiridhisha na hatua za Bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge na pia Shirika la TANESCO ni moja kati ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na pia ufanisi wake kwa ujumla. Tumefanya hivyo pia katika mashirika mengine, hili la TANESCO sio tukio la kipekee;
  3. Kitendo hiki cha halali na kwa mujibu wa Kanuni kilichofanywa na Kamati yangu  kimetafsiriwa kwa makusudi na baadhi ya watu kwamba ni ishara ya kuwa sisi au zaidi kwamba mimi nina maslahi binafsi na TANESCO na hususan Mkurugenzi wake Injinia Mhando, ndio maana tumetaka maelezo ya Bodi. Ukweli kwamba Kamati ya POAC tumewaita pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa jambo hilo hilo umefichwa kwa makusudi!
  4. Baada ya  tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
  5. Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti.
Sasa naomba kutoa ufafanuzi rasmi kuhusu mlolongo wa matukio hayo tajwa ambayo yanatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuonesha kwamba eti nimehusika na vitendo vya rushwa.
  1. Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa TANESCO kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndio imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika. Ieleweke wazi kabisa kuwa, hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi binafsi au Kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi;
  1. Ni kwa sababu hiyo, na kwa kujiamini kabisa nimeunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na  Madaraka  ya  Bunge kwa kina;
  1. Nimekwenda mbali zaidi kukiomba chama changu CHADEMA kifanye pia uchunguzi na tathmini yake kwa kina kujiridhisha na tuhuma hizo;
  1. Natumia fursa hii pia kuomba vyombo vya Dola vichunguze tuhuma hizo kwa nafasi yake ili kuweza kupata ukweli;
  1. Ninaahidi kushiriki kikamilifu iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yeyote.
Napenda niwatoe hofu wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa Bungeni na Watanzania wote kwa ujumla kwamba:-
  1. Mimi Zitto Zuberi Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni. Daima nimesimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa, na nawaahidi sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo;
  1. Nafarijika na salam mbali mbali zinazotolewa kunifariji na kusisitiza kuwa nisilegeze kamba katika mapambano haya, nimepokea ujumbe mwingi kwa simu, sms, tweeter na hata facebook na niko pamoja nanyi Watanzania wenzangu kamwe sitarudi nyuma hadi kieleweke. Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi’ wa baadhi ya watanzania wenzetu;
  1. Napenda kuweka rekodi sawa kwa Watanzania kwamba nimekuwa Mbunge hiki ni kipindi cha pili, Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) huu ni takriban mwaka wa saba sasa, Kamati yangu inasimamia mashirika 259 ya Umma na si TANESCO peke yake. Mchango wa Kamati hii katika Bunge na kwa ustawi wa Mashirika ya Umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali za umma na kuokoa fedha za umma kutokana na umakini wake. Tumefanya hivyo CHC hivi karibuni, Kiwira na kwenye mashirika mengine mengi. Kote huko uadilifu na uzalendo wa Kamati hii haujawahi kuhojiwa. Inatuwia vigumu kuona kuwa tunahojiwa katika suala hili la TANESCO. Hapa pana kitendawili.
  1. Zipo hoja pandikizi za kutaka Kamati ya POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa Kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi. Kwa maoni yangu, Kamati ya POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi kama mimi na sio kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu. Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na maslahi ya taifa letu kwa kujiuzulu Uenyekiti iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu zaidi kuliko mimi.
  1. Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
  1. Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.
  1. Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule, au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Mwisho
Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.
Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.
Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga”.
Ahsanteni sana.

31 Jul 2012



Mara nyingi kwa wenzetu huku nchi za Magharibi kila jambo linapotokea watu wa kada mbalimbali hujihangaisha kusaka maelezo yanayojitosheleza kuhusu chanzo cha tukio husika na jinsi linavyoweza kuzuiwa mbele ya safari.
Ukiangalia nchini Marekani, kwa mfano, mara baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11, 2001, taasisi mbalimbali zilikuna vichwa kusaka chanzo cha mashambulizi hayo na jinsi nchi hiyo itakavyoweza kuzuia uwezekano wa mashambulizi kama hayo kujirudia.
Ninaamini kwa wanaofuatilia siasa za kimataifa watakumbuka kazi iliyofanywa na Kamisheni ya Septemba 11 ambayo kwa kiasi kikubwa ilifukua kila eneo kuhakikisha inapata taarifa sahihi kuhusu mashambulizi hayo ya kigaidi na usalama wa nchi hiyo kwa ujumla.
Yayumkinika kuhitimisha kwamba jinsi Marekani ilivyoshughulikia ‘aftermath’ ya mashambulizi hayo imesaidia kwa kiasi kikubwa si tu kuuawa kwa mtuhumiwa nambari moja, Osama bin Laden, bali pia imesaidia kuepusha mashambulizi mengine.
Kwa hapa Uingereza, matukio ya vurugu za mwezi Agosti mwaka jana yaliyoanzia kitongoji cha Tottenham, jijini London, na kusambaa maeneo kadhaa yalisababisha taasisi na watu mbalimbali kuhangaika kusaka chanzo cha matukio hayo, zoezi ambalo hadi sasa linaendelea.
Na kutokana na umuhimu wa jiji la London-na Uingereza kwa ujumla-kwa dunia, vurugu hizo zilivuta hisia hadi nje ya mipaka ya nchi hii. Ripoti kuhusu vurugu hizo zilikamata vichwa vya habari kuanzia Zimbabwe hadi India, Amerika ya Kaskazini hadi Kusini, na kwingineko.
Lakini binafsi niliguswa zaidi na maelezo ya gazeti la mrengo wa kushoto la Ujerumani la Berliner Zeitung ambalo lilihitimisha ifuatavyo kuhusu vurugu hizo (ninanukuu)
The country has lost faith in every authority: the banks, politicians, the media, the police. The corruption has reached even the smallest unit - the family. There is a generation growing up without values of any kind.” (Tafsiri isiyo rasmi: nchi imepoteza imani kwa kila mamlaka: benki, wanasiasa, vyombo vya habari, polisi. Rushwa imetamalaki hadi kwenye eneo dogo la chini kabisa, yaani familia. Kuna kizazi kinachokua kisichokuzwa katika maadili ya aina yoyote ile)
Gazeti hilo likaendelea kueleza (ninanukuu tena) “In the economic crisis the financial establishment declared bankruptcy, and British politicians became mired in the expenses scandal of 2009. Then this year the media and politicians have been damaged by the Murdoch scandal...When the country's elites don't take the law seriously, why should we? No question is more dangerous for a society.” (Tafsiri isiyo rasmi: katika mtikisiko wa kiuchumi, taasisi za fedha ziliishia kutangaza kuwa zimefilisika, na wanasiasa wa Uingereza wakakumbwa na skandali ya posho mwaka 2009. Kisha, mwaka huu kashfa ya Murdoch imeathiri sana taswira ya vyombo vya habari na wanasiasa...Sasa kama wasomi wa nchi wanapuuza sheria, kwanini sie tuijali? Hakuna swali la hatari kwa jamii kama hili.”
Nukuu hizo mbili kuhusu vurugu za London zinaweza kabisa kutumika kuelezea mwenendo wa baadhi ya mambo huko nyumbani kwa sasa. Kimsingi, mwananchi wa kawaida anakumbana na matarajio makubwa kutoka kwa watawala wetu lakini licha ya Watanzania wengi kukidhi matarajio hayo ya tabaka tawala, wameendelea kushuhudia watawala na mamlaka za utawala zikishindwa kwa makusudi kuthamini matarajio na mahitaji ya wananchi.
Moja ya taasisi za utawala ambazo zimekuwa zikiwaangusha ambayo imekuwa ‘ikiwaangusha’ sana Watanzania ni Bunge, tunaloambiwa ni tukufu. Katika siku za hivi karibuni, Bunge letu limekuwa likifanya kila jitihada kujivunjia heshima na imani kubwa waliyonayo wananchi kwa taasisi hiyo.
Kimsingi, Bunge letu limegeuka zaidi ya kituko. Lakini baya zaidi, taasisi hiyo ya kutunga sheria imegeuka pia kuwa ‘utani mbaya’ (a bad joke), ambapo watu wanaotubebesha mzigo mkubwa kumudu maslahi yao ambayo kwa mwananchi wa kawaida ni ya kufikirika tu wameamua kuigeuza taasisi hiyo kuwa uwanja wa mipasho, vijembe, matusi na tabia nyingine unazoweza kuzikuta maeneo ya vijiweni tu.
Lakini tukirudi nyuma, Bunge ‘liliharibiwa’ tangu zamani, na tunachoshuhudia sasa ni mwendelezo tu wa uharibifu huo. Tukiangalia Bunge la mfumo wa chama kimoja tunabaini kuwa lilikuwa mkusanyiko wa watu waliopaswa kuwa na fikra za aina moja, kupitisha kila kinacholetwa na serikali ya chama kimoja kilichoshika hatamu, na mawazo yoyote yaliyokinzana na mtizamo wa watawala yalichukuliwa vibaya, lakini walau wakati huo zilikuwapo pia sauti zilizokuwa zikisema ukweli kwa jinsi ulivyokuwa.
Hatimaye tukapata Bunge la vyama vingi chini ya Spika Pius Msekwa. Kimsingi, Bunge hili liliendelea kuwa mithili ya lile la mfumo wa chama kimoja kwani wabunge wachache wa upinzani hawakupewa fursa yoyote ya maana kuipa changamoto serikali, na Bunge likaendelea kuwa kibaraka wa serikali kwa kutumia wingi wa wabunge wa chama tawala.
Lakini kama awamu zilizotangulia zilikuwa mbaya, basi zilizofuatia zilikuwa zaidi ya mbaya. Bunge lililokuwa chini ya Uspika wa Mheshimiwa Samuel Sitta lilizaa kile kinachofahamika sasa kama siasa za majitaka. Nisingependa kuingia kwa undani ni jinsi gani Sitta alifanikiwa kupata uspika lakini ninachoweza kusema pasi uoga ni kuwa Bunge hilo lililogubikwa na migongano lukuki ya kimaslahi, lilifanikiwa kupigia mstari hoja kuwa ni rahisi sana kuwaghilibu Watanzania.
Lakini ukidhani ‘Bunge la Sitta’ lilikuwa hivyo lilivyokuwa, na kama unakumbuka kituko kikubwa zaidi (tuhuma za ushirikina bungeni?) basi subiri tulichambue kidogo ‘Bunge la sasa la Spika Anne Makinda.’ Pengine hili litamkera Spika Makinda lakini moja ya maelezo mepesi ya utawala wake ni kuwa anaiendesha taasisi hiyo kidikteta ‘kupita maelezo.’
Kuna hoja moja ya kisiasa inayodai kuwa kuna nyakati udikteta ni muhimu. Kwamba kuna udikteta wa aina mbili: kwa ajili ya watu na dhidi ya watu. Udikteta mbaya ni huo wa aina ya pili (dhidi ya watu) kwani ni kwa ajili ya maslahi ya wachache. Lakini udikteta kwa ajili ya watu unaweza kuwa muhimu na lazima hususan pale maslahi ya wengi yanapoelekea kusipofaa.
Spika Makinda amekuwa ‘mungu-mtu’ wa Bunge letu, akitumia kila aina ya ubabe dhidi ya wabunge wa vyama vya upinzani, akiwatimua nje ya Bunge kadri apendavyo huku akiwaacha watu kama Mwigulu Nchemba kuigeuza taasisi hiyo kuwa mithili ya kituo cha mafunzo ya vijembe, mipasho, matusi na upuuzi mwingine.
Lakini tatizo si Makinda tu bali hata kiti cha Uspika. Yayumkinika kuhitimisha kuwa kiti hicho ni kama ‘kimerogwa’ kwani kila anayekikalia anajisikia mwenye nguvu zisizomithilika na kama ni lazima awathibitishie wabunge wa vyama vya upinzani kuwa wao ni sawa na kile Waingereza wanakiita ‘evil necessity’ (yaani jambo la kishetani ambalo inabidi liendelee kuwapo kwa vile tu ni muhimu, angalau kwa mujibu wa taratibu za kimaandishi na si kivitendo).
Kabla sijaandaa makala hii nimesoma habari katika gazeti moja inayomnukuu Waziri wa Makazi, Prof Anna Tibaijuka, akitoa wito kwa Watanzania kuwaombea viongozi wa ngazi zote wakiwamo wabunge ili wapate hekima na busara kutoka kwa Mungu.
Japo wazo la Waziri Tibaijuka lina maana laini sidhani kama Watanzania ambao tayari wanabebeshwa mzigo kumudu maslahi ya viongozi kama wabunge wapo tayari kujitwika ‘gunia jingine la misumari’ kufanyamaombi kwa ajili ya watu walioko bungeni kuendekeza mipasho na vijembe badala ya kuzungumzia kero za wananchi.’
Tuwaombee ili wapate busara za kusaka vina (verses) kali zaidi za mipasho yao ya kila siku? Tuwaombee ili waendelee kupigania kuboreshewa maslahi yao ambayo hayaendani kabisa na hali halisi ya uchumi wetu? Ninaamini kabisa kuwa hakuna Mtanzania mwenye ‘muda mchafu’ wa kuwaombea watu hawa. Wajiombee wenyewe ili wapatwe na akili ya kutambua kuwa ‘utoto’ wa vijembe, kashfa na matusi si tu unaisukuma taasisi hiyo kwenye lindi la ukosefu maadili bali pia unaweza kuzua mjadala kama kuna umuhimu wa kuwaita watu hawa waheshimiwa ilhali baadhi yao wana kauli chafu zaidi ya zile za vijiweni. Kwanini tuwe na waheshimiwa wasiojiheshimu?
Nimalizie makala hii kwa kukumbushia nukuu ya Berliner Zeitung kuwa kama ‘waheshimiwa’ hawajali sheria na taratibu kwanini basi wananchi waone umuhimu wa kuzijali? Kwa bahati mbaya, kufanya hivyo ni kukaribisha uvunjifu wa amani zaidi ya huo uliojiri hapa Uingereza mwaka jana.
Nihitimishe kwa kutoa wito kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa marekebisho tarajiwa ya Katiba yetu kuangalia uwezekano wa wapigakura kuwadhibiti wabunge ‘wasio na heshima’ kutokana na kauli au/na vitendo vyao, sambamba na kutengeneza mazingira ya kudhibiti udikteta wa Spika na/au kiti cha uspika.


25 Jul 2012

KIKUNDI cha vijana wanaoendesha vitendo vya kihalifu unaoendana na mauaji kinachojiita ‘Kunguru Hafugiki’ kimeibuka na kuwa tishio kwa wakazi wa manispaa ya Moshi na vitongoji vyake.

Kikundi hicho hukodishwa na watu walioibiwa mali zao kwa kulipwa ujira mdogo na huwakamata washukiwa wanaodaiwa kuiba mali ya mtu husika na kuendesha vitendo vya utesaji kushinikiza watu hao kutaja walipoficha mali.

Katika tukio la juzi huko Pasua Manispaa ya Moshi, kikundi hicho kinadaiwa kukodiwa na mfanyabiashara mmoja jina limehifadhiwa, siku moja baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumba yake na kupora mali kadhaa.

Baada ya tukio hilo, mfanyabiashara huyo alimhisi jirani yake kuwa ndiye pengine alihusika na tukio hilo na ndipo alipomkamata yeye na nduguye na kuwapeleka kwenye kikundi hicho.

Baada ya kuwafikisha hapo aliwakabidhi kwa kikundi hicho ambacho kiliendesha mateso ya kila aina kikiwashinikiza wataje walikoficha mali za mfanyabiashara huyo bila mafanikio.

Katika tukio hilo, Sultan Mallya (28), alipigwa hadi akapoteza fahamu na kufariki katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph iliyoko eneo la Soweto katika manispaa ya Moshi.

                                

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz, alidhibitisha jana kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu wawili, Achibodi Maleko (52), pamoja na mfanyabiashara huyo wanashikiliwa na polisi kutokana na tukio hilo la mauaji.

Akifafanua juu ya tukio hilo, Boaz alisema Julai 22 usiku mfanyabiashara huyo alivunjiwa nyumba yake na alipata tetesi kwamba Michael Mallya na nduguye Sultan Mallya walihusika na kuvunja nyumba yake.

Alidai kuwa baada ya kupata tetesi hizo aliwakamata ndugu hao na kuwapeleka kwenye kikundi hicho na kuwapa mateso ya kila aina na hadi sasa Michael yuko mahututi katika hospitali ya rufaa ya KCMC baada ya kuumizwa vibaya.

Kufuatia tukio hilo, wananchi wenye hasira walizingira nyumba za watuhumiwa hao na kufanya uharibifu mkubwa wa mali kabla ya polisi hawajaingilia kati na kuwatia mbaroni watu wanane.
Wanaoshikiliwa kutokana na kufanya uharibifu wa mali kwenye nyumba za watuhumiwa hao ni Issa Haji, Issa Athuman, Juma Rajab, Issa Maulid, Bakari Kiduka, Bakari Evarist, Selestine Joseph na Hamis Mohamed.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.