5 Mar 2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
mg23-w480-h580
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

3 Mar 2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.


1 Mar 2014


28 Feb 2014

HUYU naye vipi? Mhasibu mzima anapenda basi la wafanyakazi! Hana japo pikipiki na bado anaishi nyumba ya kupanga. Ama kweli kwenye miti hakuna wajenzi...”.  Hii ilikuwa kauli ya mfanyakazi mwenzangu wakati nilipokuwa mwajiriwa wa taasisi moja ya umma huko nyumbani.
Mhasibu aliyekuwa akiongelewa ni kijana mmoja ambaye baada ya kuhitimu masomo Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) na kurejea kazini alipandishwa cheo katika idara ya uhasibu katika taasisi hiyo. Yayumkinika kuhitimisha kuwa miezi kadhaa ya mwanzo baada ya kuwa mhasibu, kijana huyo aliandamwa sana na wengi wa wafanyakazi wenzake, ‘kosa’ lake pekee likiwa ‘kuishia maisha ya kawaida kulingana na kipato chake.’
Tofauti na kijana huyo, katika taasisi hiyo kulikuwa na jamaa mmoja ambaye japo hakuwa mhasibu kitaaluma, ndiye aliyekuwa na jukumu la usimamizi wa fungu la fedha kwa ajili ya matumizi ya mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo, hususan safari za nje ya nchi. Sehemu kubwa ya fedha alizokuwa akisimamia ndugu huyo zilikuwa za kigeni.
Huyu bwana alikuwa na uwezo mkubwa mno kifedha japo mshahara wake ulikuwa wa ‘kawaida’ tu. Alikuwa na misururu ya magari ya thamani huku ikidaiwa kuwa alikuwa na idadi kubwa ya nyumba jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi huyu alikuwa akinyenyekewa hata na baadhi ya mabosi wake.
Baada ya muda, inaelekea huyo mhasibu kijana alizidiwa na kebehi dhidi yake, na akaanza ‘kuishi kihasibu,’ na taarifa zilizopatikana zilionyesha kuwa alianza kununua nyumba, magari na hata matumizi yake yalibadilika yakawa makubwa. Na sifa zikaanza kumiminika kwake, na kama ilivyokuwa kwa yule ‘mhasibu’ wa mkurugenzi mkuu, naye akaanza kunyenyekewa.
Ninakumbuka kuhusu ‘kituko’ hiki kwa vile kilitokea mbele ya macho yangu katika taasisi niliyokuwa nimeajiriwa. Lakini kimsingi hali hiyo ilikuwa kama ya kawaida kwenye taasisi nyingi tu, za umma na za binafsi.
Huo ndio ‘ukweli mchungu’ kuhusu Tanzania yetu. Mhasibu atakayeishi kulingana na kipato chake (na mishahara ya wahasibu wengi ni ya kawaida kwa vile uhasibu si ‘fani adimu’- rare profession- kama urubani yenye mshahara mkubwa.
Huko mitaani hali ni mbaya zaidi ambapo wahalifu wanatukuzwa; wauza madawa ya kulevya wamepachikwa ‘uzungu’ na kuitwa ‘wazungu wa unga.’ Wananyenyekewa kama miungu-watu. Kwa hakika Tanzania yetu inaweza kuwa sehemu muafaka ya kuthibitisha ule msemo wa Kiingereza kuwa crime pays (uhalifu unalipa).
Utakutana na mtu ambaye hana shughuli ya kueleweka lakini ana fedha nyingi mno; hajaachiwa urithi mkubwa, hajawahi kushinda bahati nasibu, na kubwa zaidi hana kazi wala biashara ya kueleweka. Uwezekano pekee wa ‘utajiri’ wa mtu huyu ni kujihusisha na uhalifu kwa sababu fedha hazianguki kutoka hewani kiasi cha kuwa na mtu mwenye fedha nyingi lakini hana chanzo cha mapato.
Nikirejea kwenye uzoefu wangu huko nyumbani, kuna wakati niliwahi kufanya kazi na watumishi wa chombo kimoja cha dola (yaani kazi iliyofanywa kwa ushirikiano kati ya chombo hicho na taasisi niliyokuwa nikiitumikia wakati huo). Hali huko ilikuwa mbaya zaidi ambapo mtendaji aliyechukia rushwa alionekana kama adui wa watendaji wenzie.
Kisingizio kikubwa kilikuwa maslahi madogo na mazingira magumu ya kazi. Nilichojifunza kwao ni kwamba ilikuwa vigumu sana kuwa mzalendo katika chombo hicho cha dola kwa sababu rushwa ni sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya watumishi wake.
Mara nyingi tumekuwa tukiilaumu serikali na taasisi zake, wanasiasa na watawala wetu kuhusu kuporomoka kwa uadilifu sambamba na kushamiri kwa uhalifu. Lakini pengine mara nyingi zaidi ni nadra kwetu kama wananchi kujiuliza kuhusu nafasi zetu kupambana na au kuchochea kuporomoka huko kwa maadili na kushamiri kwa uhalifu. Ni vigumu kuuchukia uhalifu, kwa mfano, ilhali ndoto zako ni kuishi maisha ya kifahari kama anavyoishi mhalifu fulani.
Ninaambiwa kwamba baadhi ya wahalifu huko nyumbani wamekuwa na nguvu kubwa zaidi ya watawala wetu kiasi kwamba vyombo vya dola vinaogopa kuwagusa wahalifu hao. Na bahati nzuri kwao, baadhi yao wamefanikiwa kujenga ushirikiano na watu wa karibu wa familia za watawala wetu ambao wanatumiwa na wahalifu hao kama kinga dhidi ya hatua za kisheria.
Sasa kama katika hali inayokera na kukatisha tamaa tunaelekea kuruhusu na kuhalalisha upatikanaji kipato kwa njia zisizo halali, na kisha kuwaabudu wahalifu kana kwamba ni miungu-watu na kuwaenzi kwa ‘nyadhifa kama ‘mzungu wa unga’ au ‘pedejee,’ kwanini tunatahayari kusikia taarifa kwamba wajumbe wengi wa Bunge la Katiba wanalalamika kuwa posho ya shilingi 300,000 kwa siku haitoshi?
Hivi katika mazingira ya kawaida tu, tutarajie lipi kwa mjumbe wa Bunge la Katiba aliyeteuliwa na Rais  ‘anapogusana mabega’ (rubbing shoulders) na wajumbe walioingia katika Bunge hilo kama wabunge ‘wa kawaida’ wanaolipwa zaidi ya shilingi milioni 10 kwa mwezi?
Kwamba kama serikali ina uwezo na jeuri ya kulipa mamilioni hayo kwa wabunge zaidi ya 300 kila mwezi kwa miaka mitano, kwanini basi nao wasidai japo ‘kipande kiduchu cha keki hiyo ya taifa’?
Naomba ieleweke bayana kwamba si kuwa ninaafiki madai ya wajumbe hao wa Bunge la Katiba wanaodai waongezewe posho, bali ninachojaribu kubainisha hapa ni ukweli kwamba kelele za wajumbe hao zinaakisi hali halisi huko mtaani. Kama ni sahihi kwa wahalifu kuenziwa huko mtaani, kwanini basi ‘waheshimiwa hawa wa muda mfupi’ wasitumie fursa hiyo kujinufaisha?
Nchi yetu imekuwa kama msitu (jungle) ambapo kanuni pekee inayotawala ni ubabe: kula au uliwe. Na katika mazingira ya namna hiyo ni vigumu kweli kwa uzalendo au wazalendo kusalimika. Ndiyo maana niliposikia jina la mwanadada mzalendo, Maria Sarungi, kuwa miongoni mwa wajumbe walioteuliwa kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba nilitamani kungekuwa na angalau makumi kadhaa ya watu kama yeye.
Simsifii bali mwanadada huyu amekuwa mstari wa mbele katika kampeni ya mtandaoni inayoitwa 'Badili Tanzania' (Change Tanzania), ambayo kimsingi inahimiza mabadiliko ya kifikra, kitabia na vitendo kwa jamii badala ya kutilia maanani kuwategemea wanasiasa au taasisi za kisiasa kuleta mabadiliko chanya kwa nchi yetu.
Ikumbukwe kuwa kati ya mafanikio makubwa ya kampeni ya Change Tanzania ni kupinga ongezeko la kodi kwa kadi za simu (SIM card tax) ambapo hatimaye ilifutwa baada ya kilio cha umma kupitia kampeni hiyo kusikika kwa watawala.
Alipotajwa kuwa mmoja wa wajumbe wa Bunge la Katiba sikumpongeza, na hadi leo sijatoa pongezi zangu kwake. Sababu kubwa ya kuhifadhi pongezi zangu ni kwamba yeye ni mithili ya mwanasoka bora ambaye kwa hakika ni lazima achaguliwe katika timu ya taifa. Na tunapoongelea soka, kuna mfano mzuri hapa: mwanasoka Mtaliano Mweusi, Mario Balotelli, aliwahi kunukuliwa akisema kwamba anapofunga bao huwa hashangilii kwa sababu hiyo ni kazi yake. Na akasema ‘umeona wapi msambazaji barua wa posta anashangilia anapofikisha barua kwa mhusika? Huwezi kumshangilia kutimiza jukumu lake.”
Bunge la Katiba lilipaswa kuundwa na wazalendo wanaofikiria hatma ya taifa letu na si ‘nani atalipwa ada ya mwanangu wakati ninashughulikia mchakato wa Katiba mpya’ au wanaodhani posho ya ujumbe wa Bunge la Katiba ni fursa ya kuwabadilishia maisha yao (iwe kuwaongezea fedha au kuongeza idadi ya nyumba ndogo).
Tumeruhusu ‘uhuni’ katika shughuli hiyo muhimu kwa hatma ya taifa letu, na ndiyo maana tunashuhudia mtu kama Emmanuel Makaidi akigeuza mchakato wa kupata Katiba mpya kuwa fursa ya kiuchumi kwa familia yake kwa kumteua mke wake kuwa mjumbe mwenza katika Bunge hilo.
Bunge la Katiba lilihitaji akina Maria Sarungi wengi, yaani watu ambao historia ‘inawapendelea’ (kwa maana kwamba kuna mifano hai ya uchungu wao kwa Watanzania wenzao)’.  Bunge hilo halikustahili kuwa fursa kwa wababaishaji wanaodai eti waongezewe posho kwa vile wameambatana na wanasheria wa kuwashauri wakati wa mjadala wa Katiba mpya.
Kwa vile uteuzi wa wajumbe wa Bunge hilo haukufanywa kwa mtutu wa bunduki kuwa ‘lazima uwe mjumbe hata kama posho haitoshi’ ni vema kwa wanaodhani posho haitoshi wakajiuzulu na kurejea makwao.
Nimalizie makala hii kwa kuwaasa Watanzania wenzangu kujiandaa kisaikolojia kupokea Katiba mpya ‘fyongo au ‘bomu’ kwa sababu wengi wa wanaotuwakilisha katika mchakato wa kupata Katiba hiyo wapo huko Dodoma kwa maslahi yao binafsi. Yayumkinika kuhisi kwamba mjadala wa Katiba huo utakuwa mrefu, si kwa minajili ya kupata muafaka wenye maslahi kwa taifa bali ukweli kwamba urefu wa mjadala utamaanisha urefu wa posho pia.
Ningetamani sana kuhitimisha makala hii na ‘pendekezo la maana’ lakini nafsi inanisuta: ukipanda upupu shambani kamwe usitarajie kuvuna maharagwe.' Kinachojiri katika Bunge la Katiba Dodoma kinaakisi kinachojiri katika maisha yetu ya kila siku mtaani, na tusipoamua kwa dhati kubadili mtizamo wetu dhidi ya ‘wazungu wa unga’ na ‘mapedejee’ basi tusitarajie miujiza kwa watu wanaoteuliwa katika ‘nafasi za ulaji’ kama ujumbe wa Bunge la Katiba.



20 Feb 2014

KABLA ya kuanza kuandika makala hii nilikutana na habari moja mtandaoni iliyonifanya nijiulize  iwapo Rais Jakaya Kikwete anapata muda wa kuangalia kalenda kufahamu muda uliobaki kabla hajamaliza muhula wake wa pili na wa mwisho wa Urais.
Habari hiyo ilihusu hotuba ya Rais Kikwete aliyoitoa mjini Dodoma kwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ambapo aliwataka wanachama wa chama hicho kuacha unyonge na kusema uvumilivu una kikomo chake.
Tunashindana na wenzetu wagomvi, maana wao ugomvi ndiyo sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa...Tulizungumza nalo hilo kwenye Kamati Kuu, tulikubaliana kuacha unyonge. Ndiyo, kwenye Kamati Kuu tumekubaliana, tumesema jamani watu wote waende wakaseme tumekubaliana kuacha unyonge,” alinukuliwa Kikwete ambaye licha ya kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama.
Kwa kifupi, Rais Kikwete ametoa ruhusa kwa wana-CCM kukabiliana na alichokiita tabia ya ugomvi ya vyama vya upinzani. Kwamba wana-CCM wachukue sheria mkononi pindi wakihisi wanafanyiwa ugomvi na wapinzani. Kwa lugha nyingine, jukumu la ulinzi na usalama katika shughuli zinazokihusu chama hicho zimeporwa kutoka vyombo vya dola na kukabidhiwa kwa wanachama wa chama hicho tawala.
Kwa tafsiri pana, iwapo wana-CCM ‘wataacha unyonge’ na kufanya mashambulizi ya kujihami dhidi ya wapinzani (yaani hata kama wapinzani hawajafanya ‘ugomvi’ wowote) bado watakuwa na ‘haki’ kutokana na ruhusa hiyo waliyopewa na Rais Kikwete.
Kadhalika, vyombo vya dola vitakuwa na wakati mgumu kuchukua hatua dhidi ya wana-CCM watakaowashambulia wapinzani kwa sababu amri ya kufanya mashambulizi hayo ina baraka za Rais ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu.
Hivi kweli Rais Kikwete hatambui kuwa amebakiwa na takriban miezi 20 tu kabla ya kuwa ‘raia wa kawaida tu’ ambaye anaweza kuwa miongoni mwa wahanga wa ruhusa hiyo ya vurugu aliyowapa wana-CCM wenzake?
Na hata kama angekuwa amebakiwa na miaka mingine mitano katika Urais, haihitaji busara kutambua kuwa ni rahisi kuruhusu uvunjifu wa sheria kuliko kuzuwia. Ni rahisi kwa Rais Kikwete ‘kuwapa rungu’ wana-CCM kupambana na wapinzani lakini ni vigumu mno kuwazuwia kutotumia ruhusa hiyo.
Binafsi ninadhani kinachomsumbua Rais Kikwete ni ‘kofia mbili za uongozi katika Taifa,’ yaani Urais na Uenyekiti wa Taifa wa CCM. Na suala hili la ‘unyonge wa wana-CCM’ si pekee linaloonyesha jinsi ‘kofia mbili’ zinavyomtesa Rais Kikwete.
Angalia suala la Katiba Mpya: anapozungumza nje ya hadhara za ki-CCM, Rais anaonekana kuwa na dhamira ya dhati kuona Katiba mpya inapatikana kulingana na matakwa ya Watanzania wote.
Lakini ukisikiliza hotuba zake mbele ya wana-CCM wenzake, inakuwa mwendelezo uleule wa kuweka mbele itikadi za kisiasa hata pale inapohitaji kutanguliza maslahi ya Taifa.
Kimsingi ‘kofia mbili’ hazipaswi kuwa tatizo iwapo kasumba ya kuweka mbele siasa katika kila jambo itaepukwa. Rais anaweza kabisa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria pasipo hofu ya kuathiri nafasi yake kama Mwenyekiti wa Taifa wa chama anachoongoza.
Na kwa kumrahisishia kazi, CCM inafahamika kwa ‘mshikamano’ wake, na ni dhahiri kuwa Rais ana nafasi kubwa ya kuungwa mkono na chama chake katika uongozi wake, na wakati huohuo Rais imara anatengeneza mazingira ya uenyekiti imara ndani ya CCM hivyo kuondoa uwezekano wa upinzani ndani ya chama.
Sitaki kabisa kudhani kuwa baada ya ruhusa hiyo kwa wana-CCM wenzake kuacha unyonge, Rais Kikwete atahamia kwa Watanzania na kuwaruhusu kuacha unyonge dhidi ya mafisadi, wafanyabiashara ya madawa ya kulevya na  majangili.
Lakini hata asipotoa ruhusa ya aina hiyo, uamuzi wake wa kuwakabidhi wana-CCM majukumu ya vyombo vya dola unaweza kuvuka mipaka ya kisiasa (yaani CCM dhidi ya wapinzani) na kuchukua sura ya kitaifa, kwani wahanga wa ufisadi, madawa ya kulevya, ujangili, nk ni Watanzania wote pamoja na hao wana-CCM.
Ruhusa hiyo ya Rais Kikwete kwa wana-CCM kuacha unyonge na kukabiliana na wapinzani si tu ni fyongo lakini pia imekuja wakati mbaya. Macho  na masikio ya Watanzania wote yameelekezwa Dodoma kufuatilia Bunge la Katiba ambalo limeanza kukiwa na matarajio Katiba mpya itaimarisha umoja na upendo miongoni mwa Watanzania.
Na kwa upande mwingine, kauli hiyo ya Rais Kikwete inaturejesha kwenye suala nililozungumzia katika makala yangu ya wiki iliyopita nikieleza kuwa tatizo kubwa la Katiba tuliyonayo na zilizotangulia huko nyuma ni utekelezaji wake.
Ni wazi kuwa Rais Kikwete anafahamu kwamba wenye jukumu la kukabiliana na ‘wagomvi’ wa CCM si wana-CCM bali vyombo vya dola. Huo ndio utawala wa sheria kwa mujibu wa Katiba. Inapotokea matamshi yetu yakaonyesha kuwa kuna ruhusa kwa wananchi kupora wajibu wa vyombo vya dola katika kulinda amani na usalama, tutarajie nini kutoka kwa mwananchi wa kawaida?
Kutarajia kwamba Rais Kikwete atabadili kauli yake ya ‘ruhusa kwa wana-CCM kuacha unyonge dhidi ya tabia ya ugomvi wa wapinzani wa chama hicho’ ni sawa na kutarajia ujangili utakwisha kwa vile Rais amedai serikali inawafahamu vigogo 40 wanaoendesha biashara hiyo haramu. Labda kinachoweza kutokea ni ‘kucheza na maneno’ na kuwalaumu waandishi wa habari kuwa “walinukuu vibaya.”
Nimalizie makala hii kwa kumkumbusha Rais Kikwete kuwa bado ana nafasi nzuri ya kujitengenezea mazingira mazuri ya ‘kustaafu kwa amani’ pindi atapomaliza muhula wake wa Urais mwakani.
Kuruhusu wana-CCM wachukue sheria mkononi dhidi ya ugomvi kutoka kwa vyama vya upinzani ni kuruhusu uvunjifu wa sheria.

- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/amri-hii-yaweza-kumfuata-kikwete-uraiani#sthash.9f8lBlwU.dpuf

14 Feb 2014

HATIMAYE mchakato wa kupata Katiba mpya unaelekea kufikia hatua nzuri baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya uteuzi wa wajumbe 201 wa Bunge la Katiba.
Hata hivyo, wakati uteuzi huo ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu hasa kwa minajili ya kujua wateuliwa, hatua inayofuata ya Bunge lenyewe la Katiba ni ngumu zaidi.
Kabla ya kuingia kiundani, ningependa kuweka bayana msimamo wangu kuhusu Katiba mpya: japo ninatambua umuhimu wa kuwa na Katiba mpya, bado sijaona jinsi itakavyoweza kuwa na msaada kwa mwananchi wa kawaida. Kwa mkulima wa mpunga kule kwetu Ifakara, muundo wa Muungano si suala la kumnyima usingizi kulinganisha na upatikanaji wa soko la uhakika la mchele, sambamba na udhibiti dhidi ya uhuni wa vyama vya ushirika ambavyo ni mahiri kwa kukopa mazao lakini wagumu kulipa.
Lakini suala jingine ambalo linanifanya nisiguswe sana na uwezekano wa kupata Katiba mpya ni ukweli kwamba tatizo kubwa linaloikabili Tanzania yetu si kuwapo kwa sheria, bali ni utekelezaji wake. Sambamba na hilo ni kasumba inayozidi kujengeka kwamba sheria huonekana msumeno pale tu inapohusu walalahoi lakini si kwa vigogo na maswahiba zao.
Sasa, ni hili ni swali la kuamsha tafakuri tu, kama sheria zilizowekwa wazi kwenye Katiba iliyopo na zilizopita hazikuheshimiwa, kipi cha kuleta matumaini kuwa sheria zilizomo katika Katiba mpya zitazingatiwa?
Tukiweka kando mtizamo wangu huo binafsi kuhusu nafasi ya Katiba mpya katika maisha ya mwananchi wa kawaida, tuangalie hekaheka zinazotawala safari ya kuelekea kwenye upatikanaji wa Katiba hiyo mpya.
Kati ya masuala yanayotarajiwa kutawala mjadala ndani ya Bunge la Katiba ni muundo wa Muungano. Lakini kwa wanaojua kusoma alama za nyakati, tayari wana jibu kuhusu hatma ya suala hilo.
Akihutubia mkoani Mbeya katika maadhimisho ya miaka 37 ya CCM mapema mwezi huu, Rais Jakaya Kikwete aliweka wazi alichokiita msimamo wa chama tawala kuhusu muundo wa Muungano, kuwa ni serikali mbili. Japo Kikwete aliyasema hayo kama Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, ukweli unabaki kuwa pia alitoa kauli hiyo akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sasa huhitaji kuwa mjuzi sana wa siasa za nchi yetu kuelewa kuwa ni nadra kwa ‘mtizamo wa Rais’ kupingwa, na pale inapoonekana kuwa huenda Rais akaumbuka endapo msimamo wake hautofanikiwa, basi mbinu mbalimbali zitatumika kuepusha ‘fedheha’ hiyo.
Lakini suala la serikali mbili si msimamo wa Kikwete pekee bali wa CCM nzima kama alivyobainisha huko Mbeya. Na kwa kila anayeielewa CCM vizuri ataafikiana nami kuwa chama hicho kina historia ndefu ya kulazimisha matakwa yake yawe hivyo, hata kama si kwa maslahi ya Watanzania.
Tatizo kubwa la CCM ni kujipa hakimiliki ya Tanzania: licha ya jumla ya wanachama wake kuwa asilimia ndogo tu ya Watanzania wote, chama hicho kimeendelea kutenda mambo kana kwamba kila Mtanzania ni mwana-CCM.
Kana kwamba hiyo haitoshi, CCM itaingia kwenye Bunge la Katiba ikijivunia wingi wa wajumbe wake: wabunge wake Bara na Visiwani na miongoni mwa hao wajumbe walioteuliwa na Rais. Na kwa vile chama hicho tawala ni sugu wa kuweka mbele maslahi ya kiitikadi kuliko maslahi ya taifa, ni wazi kuwa uwezekano wa Bunge hilo kuridhia  muundo wa Muungano wa serikali tatu ni mdogo mno.
Kwa sisi wengine, muundo wa Muungano ukibaki wa serikali mbili kama ilivyo sasa, serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Warioba au hata ukiwa wa serikali moja haitusumbui sana, alimradi nchi inaendeshwa kwa kuzingatia sheria, yenye viongozi wanaojali maslahi ya nchi badala ya maslahi yao binafsi na marafiki zao, mapambano ya dhati dhidi ya umasikini unaoigubika nchi yetu na si porojo za majukwaani, na masuala mengine muhimu kama hayo.
Kuna suala jingine ambalo kwa hakika limenishtua sana, nalo ni taarifa zilizochapishwa katika gazeti moja la kila siku kwamba posho za wajumbe wa Bunge la Katiba ni shilingi 700,000 kwa siku. Ninatambua kwamba demokrasia ina gharama zake, lakini kwa kiwango hicho ni zaidi ya gharama mahsusi ya demokrasia.
Kama ni kweli zitalipwa hizo kwa kila mjumbe, hizo ni fedha nyingi mno ambazo mlipa kodi wa Tanzania atalazimika kuzitoa. Na huyu ni mlipakodi masikini wa Kitanzania ambaye japo yawezekana ana haja ya Katiba mpya lakini umasikini unaomghubika hauruhusu kabisa matumizi ya anasa kiasi hicho.
Japo taarifa hizo za kiwango hicho kikubwa cha posho kwa wajumbe wa Bunge la Katiba hazijatolewa ufafanuzi na mamlaka husika, uzoefu unaonyesha kuwa mara nyingi posho nono kwa wajumbe ni nyenzo mwafaka ya kulainisha msimamo wowote imara wa wajumbe husika. Kwa lugha nyingine, posho nono ni mithili ya rushwa kwa minajili ya mamlaka husika kupata inachohitaji.
Licha ya tetesi zilizozagaa kwamba baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba wana ajenda binafsi (kubwa zaidi ikiwa ni kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya uchaguzi mkuu hapo mwakani), ninahitimisha makala hii kwa kuwasihi wajumbe wote kuzingatia ukweli huu: maamuzi yao yatakuwa na faida au hasara kwa vizazi vingi vijavyo. Iwapo maslahi ya taifa yatawekwa mbele ya maslahi binafsi au ya kiitikadi, basi wajumbe hao watawatendea haki Watanzania kwa kuwapatia kile walichopendekeza kwa Tume ya Warioba.
Mungu Ibariki Tanzania 



7 Feb 2014


TANGU Januari 7 mwaka huu, Rwanda imekuwa katika maadhimisho ya miaka 20 ya mauaji ya kimbari yaliyotokea kati ya mwaka 1994 hadi 1995, na kugharimu maisha ya takriban watu milioni moja.
Maadhimisho hayo yaliyopewa jina la Kwibuka 20 (‘kwibuka’ ni neno la Kinyarwanda lenye maana ya ‘kumbuka’) yanaambatana na kukimbiza ‘mwenge wa kumbukumbu’ ndani na nje ya nchi hiyo, sambamba na mijadala ya kimataifa katika miji mbalimbali duniani.
Kwa bahati mbaya-au pengine makusudi- wakati Wanyarwanda wakijaribu kuionyesha dunia kuwa wanasonga mbele katika umoja na mshikamano, hivi karibuni kumejitokeza propaganda za waziwazi katika baadhi ya vyombo vya habari vya nchi hiyo, ambazo mlengwa mkuu amekuwa Rais Jakaya Kikwete, na pengine, Tanzania kwa ujumla.
Na kama kuna chombo cha habari kinachoweza ‘kushikwa uchawi’ basi ni gazeti linalomilikiwa na serikali ya Rwanda la News of Rwanda. Gazeti hili limekuwa mstari wa mbele kupandikiza chuki dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania kwa ujumla.
Kinachokera zaidi ni ukweli kwamba gazeti hilo linamilikiwa na serikali, na kinachoandikwa kinaweza kuwa msimamo wa serikali ya Rwanda.
Katika mlolongo wa propaganda zake chafu, hivi karibuni gazeti hilo lilichapisha habari zilizodai kwamba Rais Kikwete hivi karibuni alikuwa na mazungumzo na viongozi wa vikundi viwili vya waasi wanaoipinga serikali ya nchi hiyo, vya Rwanda National Congress (RNC) na The Democratic Forces for Liberation of Rwanda (FDLR).
Kichekesho ni kwamba wakati gazeti hilo likidai hivyo, Rais Kikwete alikuwa nchini Switzerland kuhudhuria mkutano wa kila mwaka wa uchumi dunia (World Economic Forum). Ni wazi kuwa isingewezekana kwa Kikwete kuwaalika ‘wageni hao’ ilhali yeye mwenyewe yupo nje ya nchi.
Na hata kama habari hizo zingekuwa na ukweli, kwanini basi mlengwa awe Rais Kikwete na si Serikali ya Tanzania? Jibu la wazi ni kwamba News of Rwanda linawakilisha tu chuki inayozidi kukua dhidi ya Rais Kikwete hasa baada ya kutoa ushauri kwa serikali ya Rwanda kukaa chini na waasi kujadili amani.
Sawa, pengine Wanyarwanda hawakupendezwa na ushauri huo, lakini kelele walizopiga baada ya wito huo wa Kikwete zilipaswa kuisha wakati huo na si kuliendeleza suala hilo kana kwamba Kikwete amerejea au kuendelea kutoa ushauri huo.
Ilitarajiwa kwamba wakati Rwanda inaadhimisha miaka 20 ya mauaji ya kimbari kungekuwa na tafakuri kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kujenga au kubomoa amani. Ikumbukwe kuwa miongoni mwa nyenzo zilizotumika kuchochea mauaji hayo ya kimbari ni vyombo vya habari, kwa mfano, gazeti hatari la Kangura.
Lakini ukiangalia kwa makini, kinachofanywa na News of Rwanda kwa Kikwete na pengine Tanzania kwa ujumla hakina tofauti na propaganda hatari za gazeti la Kangura. Kila mara gazeti hilo linapokuja na ‘exclusive story’ kuhusu Kikwete, msomaji hahitaji kuwa na uelewa wa tasnia ya uandishi wa habari kubaini kuwa kilichoandikwa ni porojo tu hasa kutokana na matumizi ya ‘nyenzo za kidaku’ kama vile “kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika” lakini visivyo na majina.
Kwa kiasi kikubwa Watanzania wameendelea kupuuza jitihada za makusudi zinazoendelea nchini Rwanda kuharibu uhusiano kati ya nchi hizi jirani. Pengine kupuuza huko kunatokana na silka ya Watanzania kuwa easy going lakini pia wengi wetu bado tuna kumbukumbu ya Vita ya Kagera na athari zake ambazo zimeendelea kudumu hadi sasa (kwa mfano jinsi vita hiyo ilivyoathiri uchumi wetu).
Lakini pia, Tanzania yetu inakabiliwa na changamoto mbalimbali- umasikini, rushwa, nk- na hata kama jitihada za kukabiliana na changamoto hizo hazijazaa matunda makubwa, kitu cha mwisho ambacho nchi yetu inahitaji ni kuingia kwenye mgogoro usio na tija na jirani zetu wa Rwanda.
Yayumkinika kuhisi kuwa kwa wapenda chokochoko huko Rwanda, kwa mfano News of Rwanda, ukimya na upole wetu unatafsiriwa kama aibu ya “hila zetu dhidi ya nchi hiyo kuwekwa hadharani” au hata uoga. Ukimya wa Tanzania haujasaidia hata kidogo kuwapa akili wachochezi hao kutambua kuwa amani ni muhimu kuliko chokochoko.
Hata hivyo ni muhimu kwa News of Rwanda na wote wanaoendekeza mkakati dhalimu wa kuvuruga mahusiano kati yetu na Rwanda wakatambua mchango wa Tanzania katika kuisaidia nchi hiyo wakati wa mauaji ya kimbari.
Licha ya umasikini wetu, tulijibana na kuhifadhi lundo la wakimbizi kutoka nchi hiyo. Na japo hivi karibuni Serikali ililazimika kuendesha operesheni dhidi ya wahamiaji haramu ambayo kwa kiasi fulani iliwaathiri baadhi ya Wanyarwanda, ukweli unabaki kuwa Rwanda ina deni kubwa kwa nchi yetu kutokana na wema tuliowafanyia licha ya matatizo yetu lukuki.
Naam, mikwaruzano ya hapa na pale katika nyanja za siasa na wakati mwingine kidini inaweza kutoa picha kwamba umoja wa Watanzania upo shakani. Hata hivyo, ni vema kwa yeyote anayedhani kuwa tutaendelea kukaa kimya ilhali Rais wetu anadhalilishwa bila makosa akatafakari upya. Tofauti zetu haziondoi ukweli kuwa sisi ni Watanzania tunaojivunia nchi iliyotoa mchango mkubwa kuleta amani kwa majirani zetu.
Nihitimishe makala hii kwa kukumbushia kuwa japo ni mapema kuzungumzia vita, ni vema kwa kila anayeichokonoa nchi yetu akarejea ufanisi na uhodari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Majuzi tu, mashujaa wetu hao wameonyesha uimara na utaalamu mkubwa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambako jeshi letu lilikuwa sehemu ya jeshi la kimataifa la kurejesha amani nchini humo.
Vilevile, ningependa kutoa rai kwa Rais Paul Kagame na serikali ya Rwanda kwa ujumla kukemea vikali propaganda chafu zinazoongozwa na News of Rwanda kumdhalilisha Rais wetu Kikwete sambamba na kuchochea uhasama kati ya nchi hizi mbili.
Ili ‘Kwibuka 20’ izidi kuwa na maana kusudiwa basi ni muhimu pia kuhamasisha amani hata nje ya mipaka ya Rwanda, ikiwa ni pamoja na kukemea jitihada zozote za kuathiri mahusiano kati ya nchi hiyo na Tanzania yetu.
When we are unified, working together, no challenge is insurmountable” (Tukiwa na umoja, tukishirikiana, hakuna changamoto ya kutushinda) ~Paul Kagame

- See more at: http://raiamwema.co.tz/chokochoko-hizi-na-zilaaniwe#sthash.URpf2wgf.dpuf

1 Feb 2014

MOJA ya matukio makubwa duniani yaliyojiri wiki iliyopita ni kongamano la uchumi lililofanyika huko Davos, Uswizi. Kongamano hilo la kila mwaka huwakutanisha wadau mbalimbali wa uchumi wa dunia. Rais Jakaya Kikwete amekuwa akihudhuria takriban kila mwaka.
Kati ya yaliyojitokeza katika kongamano hilo ni 'ndoto' ya binadamu tajiri kabisa duniani, Bill Gates, ambaye alidai kuwa anatarajia itakapofika mwaka 2030, miaka 16 kutoka sasa, dunia haitakuwa na nchi masikini hata moja.
Kwanza ni muhimu kutambua mchango wa bilionea huyo katika miradi na misaada mbalimbali kwa nchi masikini kama yetu. Akishirikiana na mkewe, Melinda, kupitia taasisi yao ya Bill and Melinda Gates Foundation, wamefanya mengi mazuri kiasi kwamba makala hii haitoshi kuyaorodhesha yote. Kwa kifupi, tajiri huyu amekuwa akiutumia utajiri wake kuwasaidia wasiojiweza huku akiamini kwa dhati kuwa kuna siku umasikini utakuwa historia.
Kinachompa Bill Gates matumaini kuwa takriban muongo mmoja na nusu kutoka sasa dunia haitakuwa na nchi masikini ni kile kile ambacho Watanzania wengi hushindwa kukielewa, takwimu za uchumi. Tajiri huyo anadai kuwa takwimu zilizopo zinaonyesha maendeleo ya kuridhisha kwa nchi masikini.
Kwa huko nyumbani, mara kadhaa wananchi hushindwa kuamini kama viongozi wao ni 'wazima' au wapo ndotoni wanapoelezea kukua kwa uchumi ilhali hali ya maisha ikizidi kuwa ngumu. Tatizo la viongozi wetu, na pengine kwa Bill Gates pia, ni kuzifanya takwimu kuwa sawa na watu. Ndio, takwimu hizo hutokana na vigezo fulani vinavyohusisha watu lakini hiyo haina maana kwamba takwimu ni watu. Namba ni namba na watu ni watu.
Japokuwa nami ni 'mchovu' (dhaifu) linapokuja suala lolote linalohusiana na namba, ikiwa ni pamoja na takwimu, miongoni mwa machache ninayoyaelewa ni kwamba takwimu nyingi huwa kiwakilishi tu cha hali halisi.
Nitoe mfano halisi, ni rahisi kuhitimisha kuwa Tanzania imepiga hatua kimaendeleo kwa kuhesabu idadi ya magari yanayosababisha foleni jijini Dar es Salaam. Na huko nyuma, Rais Kikwete aliwahi kunukuliwa akijigamba kuwa foleni kubwa za magari barabarani jijini Dar es Salaam ni uthibitisho wa maisha bora kwa Mtanzania. Tatizo ni kwamba asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi maeneo ya vijijini, ambapo kwa baadhi ya maeneo, magari sio tu ni anasa wanayomudu wachache bali pia ni ndoto kuyamiliki.
Kwa hiyo, pengine Jiji la Dar es Salaam licha ya kupiga hatua katika idadi ya magari na majengo ya kuvutia, sio kiwakilishi kizuri cha hali halisi ya Watanzania walio wengi wanaoishi vijijini. Na japo kuna jitihada za kuleta matumaini zinazofanywa na viongozi wetu kuhamasisha maendeleo maeneo ya vijijini, ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya maisha ya mijini na vijijini.
Kila linapofanyika kongamano hilo la Davos, wachambuzi mbalimbali wa uchumi wa dunia wamekuwa wakihoji ufanisi wake katika kuzinusuru nchi masikini, hususan za Afrika. Kimsingi, moja ya ajenda kubwa za kongamano hilo ni misaada kwa nchi masikini. Yayumkinika kuhitimisha kuwa misaada inaonekana kama mwarobaini wa tatizo la umasikini kwa nchi masikini.
Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wanakwenda mbali zaidi na kuhoji kuhusu hao 'wenye roho nzuri' wanaohamasisha misaada kwa nchi masikini. Kimsingi, kongamano la Davos linatafsiriwa na baadhi ya wachambuzi kama sehemu muhimu kwa matajiri kukutana na fursa mpya za kupanua biashara zao kwa mgongo wa misaada. Kwamba ninakupa msaada wa magari ili nipate soko la viwanda vyangu vya vipuri za magari.
Lakini hata tukiangalia wasifu wa 'manabii wa kupambana na umasikini kwa njia ya misaada,' baadhi yao ni wakwepa kodi katika nchi zao, kwa kuficha fedha zao kwenye 'mbingu za kodi' (tax havens) au katika offshore accounts.
Uingereza ni moja ya mataifa yanayoongoza duniani kwa kutoa misaada, na Waziri Mkuu Donald Cameron, amekuwa akishutumiwa vikali hususan na wenzake katika chama tawala cha wahafidhina (Conservative Party), kwamba asilimia kubwa ya misaada hiyo inaishia katika akaunti za watawala wabadhirifu katika nchi masikini.
Na kwa hakika kama kuna jambo moja ninashindwa kabisa kuwaelewa hawa 'wazungu' ni jinsi wanavyomwaga fedha zao kama misaada kwa nchi masikini lakini hawasumbuliwi na jinsi sehemu kubwa tu ya misaada hiyo inavyotumika kinyume cha malengo na matarajio.
Hivi inaingia akilini kweli kuona msafara wa kiongozi wa nchi tajiri ukiwa na magari machache ya 'bei ya kawaida' huku ule wa kiongozi wa nchi masikini ukisheheni magari lukuki ya thamani kubwa kabisa? Yaani kwa haraka haraka unaweza kudhani 'tajiri ndiye masikini na masikini ndiye tajiri' kwa kuangalia tofauti ya 'lifestyles' zao.
Tukirejea kwenye dhana ya misaada kama mwarobaini wa tatizo la umasikini, ni wazi kuwa nchi tajiri zitaendelea kumwaga misaada na japo sehemu fulani ya misaada hiyo itatumika kama wanavyotaka watoa misaada, kiwango kikubwa kitaishia kwenye akaunti za mafisadi, kuongeza idadi ya magari na mahekalu yao ya thamani, pasi kusahau udhaifu wao mkubwa, yaani kuongeza idadi ya 'nyumba ndogo' zao.
Akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha New York, Marekani, Cameron alisema jambo la muhimu si kiwango (quantity) cha misaada bali kile alichokiita 'kamba ya dhahabu', akimaanisha kwamba maendeleo yatapatikana tu kwa kamba ya dhahabu inayounganisha serikali imara, kutokuwepo ufisadi, uwepo wa haki za binadamu, utawala wa sheria na taarifa za wazi.
Na alichotanabaisha Waziri Mkuu huyo wa Uingereza sio sayansi ya roketi (rocket science) kwani hata katika mazingira ya kawaida tu, ukimpatia msaada wa fedha mtu ambaye mara tu baada ya kupata fedha hizo anakwenda baa kunywa pombe, ni wazi msaada huo hautoleta matokeo yanayokusudiwa. Ni sawa na kujaza maji kwenye pipa lililotoboka.
Majuzi nimesoma gazeti moja lenye habari kuwa Rais Kikwete ameiomba Uingereza msaada wa mabehewa mitumba. Sawa, sisi ni masikini kwa hiyo inatulazimu wakati mwingine tuishi kwa kutegemea misaada. Lakini tuwe wa kweli, hivi kama tulishindwa kuyamudu mabehewa yetu wenyewe katika reli ya kati na Tazara, miujiza gani itayafanya mabehewa hayo 'ya bure' kutoka kwa Waingereza yasalimike?
Inaweza kuonekana kama mzaha lakini sitashangaa kusikia Mwingereza katuletea mabehewa lakini miezi kama si wiki chache baadaye, viti vya mabehewa hayo vimeng'olewa na kugeuzwa viti katika 'pub' ya kigogo fulani (kwa taarifa yako msomaji mpendwa, viti katika nyingi ya treni za hapa ni kama vya kwenye ndege, ukikaa unatamani safari isifike kikomo).
Nihitimishe makala hii kwa kusisitiza kwamba mimi si mpinzani wa misaada kwa nchi masikini kama Tanzania lakini ningependa kuona misaada hiyo ikizaa matunda yanayokusudiwa. Ni muhimu kwa nchi na taasisi wahisani wakaanzisha mkakati wa makusudi wa kusisitiza, na ikibidi kulazimisha, udhibiti dhidi ya majambazi wanaodhulumu wananchi wenzao kwa kuchota misaada ya wafadhili kwa manufaa yao binafsi. Ni suala la akili tu, vinginevyo uwe na fedha za kuchezea, unapotoa msaada unalazimika kufuatilia ili kuona unakidhi malengo yaliyokusudiwa.
Na kwa akina sisi ambao 'tumelemazwa kwa misaada,' ni muhimu kutambua kuwa japo Bill Gates 'anaota' kwamba mwaka 2030 dunia haitakuwa na nchi masikini, kuna uwezekano mkubwa katika miaka michache tu ijayo, nchi na mashirika wahisani wakapunguza misaada yao kwetu kutokana na mtikisiko wa uchumi wa dunia, ambao hauonyeshi dalili ya kuondoka hivi karibuni.
Tukiendelea na matumizi ya anasa, usimamizi mbovu na ufisadi katika rasilimali zetu, sambamba na kutojijengea uwezo wa kujitegemea wenyewe badala yake kutumaini misaada, tunaweza kuumbuka huko mbele.
Penye nia pana njia.

My bad, nimesahau kuweka anwani ya mtandaoni ya RADIO MBAO. Ni www.radiombao.com na itakuwa hewani kuanzia Februari Mosi 2014. Sie tunaamini katika #SharingIsCaring , na RADIOMBAO inakuhamasisha nawe ku-share nasi habari yoyote ile . Usihofie kwamba “ah mie sio mwandishi” tutahariri habari yako na itasomwa/kusikika katika nchi 138 duniani. Na wala usikwazwe na “ah mie sijawahi kuandika” kwani kama unaweza kuandika SMS basi kwa hakika unaweza pia kuandika habari. Pia kila jambo lina mwanzo, mtoto hazaliwi akitembea. Kwahiyo yawezekana RADIOMBAO ikaibua kipaji chako…lakini ili hilo liwezekane basi usihofie ku-share nasi habari. Ni Jumamosi Februari 1, 2014, mahali pa kukutana ni www.radiombao.com #SharingIsCaring  (at Glasgow)

RADIO MBAO: Ninaomba kuwafahamisha kuwa mie na mwenzangu @djkvelli mkongwe wa masuala ya entertainment kama dj nchini Marekani na mmiliki wa kituo maarufu cha radio mtandaoni, RADIOMBAO, tumeunganisha nguvu, na kwa pamoja tunawaletea uzinduzi RADIOMBAO katika sura mpya. Licha ya matangazo ya radio, RADIOMBAO sasa inakuletea habari mbalimbali katika namna tofauti (bringing you news not in your traditional way). Uzinduzi rasmi utakuwa LEO  Jumamosi ya Februari 1 mwaka huu 2014.

 Tunataka nawe uwe mshiriki kwa kututumia habari kwa email [email protected] nasi tutataja jina lako kama utapenda tufanye hivyo. Hii pia ni fursa adimu kwa wasanii kutangaza kazi zenu DUNIANI kwani RADIOMBAO inasikika katika NCHI 138 DUNIANI. Tutatangaza kazi yako ya sanaa BURE. Kwa kuunganisha uzoefu na ujuzi wa muda mrefu wa @djkvelli katika masuala ya entertainment nchini Marekani, na uzoefu wangu wa takriban miaka 10 katika fani ya habari, tunawaahidi kuwaletea kitu kipya,tofauti na kitakachokidhi mahitaji yako ya habari,mahojiano,burudani na soka, maisha najamii, teknolojia na mengineyo mengi. Ombi letu kwako ni kuwa sehemu ya familia ya RADIOMBAO: Mfahamishe ndugu, jamaa na rafiki yako kuhudu ujio mpya wa RADIOMBAO. Karibuni sana kutembelea tovuti yetu inayopatikana katika anwani hii

Wasiliana nasi kwa email [email protected]

29 Jan 2014

Wale wateja wetu wa Plus Size tumesikia kilio chenu na sasa Zurii Fashion & Beauty Boutique kuna Stock Mpya kwa ajili yenu Plus Size ladies (wale mlio jaliwa neema hahaha). Size 14-20 sasa zinaptikana ZuRii. Kuna Nguo nzuri sana na quality nzuri sana za kazini, kanisani na za mitoko.
Size ndogo 8-12 pia zipo.
 Tuko Sinza Legho, nyuma ya Rombo Green View Hotel, Dar Es Saalm. Whatsapp au tupigie +255659189769 kwa maelezo zaidi. Karibuni sana.
LOOK GOOD, FEEL GOOD with ZuRii.








Follow us on Instagram @zuriiboutique
Like our page on facebook Zurii Fashion Boutique

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.