30 Jul 2009


Tume huru inayochunguza uhusika wa Uingereza katika vita ya Iraki imetangaza kuwa itamhoji Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.


Atakayenuna na anune,lakini ni dhahiri kuwa Rais wetu mstaafu ( wa awamu ya tatu),Benjamin William Mkapa,amekuwa akiandamwa na tuhuma za ufisadi wakati akiwa jengo takatifu la Ikulu.Hoja kubwa ya wanaomtetea Mkapa ni maneno kama "Mwacheni Mzee wetu apumzike".

Ni wazo zuri kutosumbua wazee wetu,lakini ingeleta maana kama wazee wote,na si Mkapa pekee,wangekumbukwa katika "maombi" hayo kuwa waachwe wapumzike.Mbona "busara" hizo hazijatumika kuwakumbuka wazee (halisi) wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?Wamesumbuliwa,wamezungushwa,wametishiwa FFU,na kufanyiwa kila aina ya vituko...tofauti na Mkapa-ambaye hajaomba atetewe au ajitetee-wastaafu hao wanadai stahili yao halali.Hawakutumia ofisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kununua japo vifusi vya kokoto au kuanzisha chama cha kuweka na kukopa,tofauti na Mkapa ambaye pamoja na mambo mengine anayetuhumiwa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kishkaji na pia kuhusishwa na kuanzisha benki.

Hivi njia bora zaidi ya kumwacha Mkapa apumzike ni kwa wanasiasa kumsafisha katika tuhuma za ufisadi zinazomkabili au kwa mahakama-chombo chenye mamlaka ya kikatiba kutoa haki-kufanya kazi hiyo?Wanasiasa wetu ni wavivu wa kufikiri.Wao ni binadamu,kwa maana hiyo leo wapo kesho hawapo-aidha kiuhai au kimadaraka.Utetezi wao leo unaweza kabisa kuondoka pindi nao watakapoondoka.Uzuri wa taasisi-kama mahakama-ni kwamba inastahili kuwepo kwa muda mrefu au hata milele ikibidi.Na hata ikibadilishwa,misingi yake itaendelea kuwepo.Kwa mantiki hiyo,namna pekee ya "kumwacha Mkapa apumzike" ni kumburuza mahakamani kisha haki itendekee huko.Kupuuza ushauri huu kunaweza kupelekea mzee huyo kuburuzwa kwa nguvu kwenda kujibu tuhuma zake wakati watetezi wake wa sasa hawako madarakani au nao wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kujibu.Hebu chukua mfano mwepesi kama huu.Unadhani Charles Taylor huko aliko anakumbuka flani aliyekuwa anamtetea?Hapo ni kila mtu anabeba mzigo wake.

Sawa,Tanzania sio Uingereza.Na ni kweli kwamba sio kila wafanyalo Waingereza lazima sie pia tulifanye.Lakini mfano wa Blair kufikishwa kwenye tume hiyo ya vita ya Irak inapswa kuwa changamoto nzuri kwa mamlaka zetu kuangalia umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu badala ya kuendekeza ushakaji na kubebana.By the way,si kila mtuhumiwa anayefikishwa kwenye vyombo vya sheria lazima aonekane ana hatia.

Mzee wetu Mkapa hatoweza kupumzika hadi sheria itakapochukua mkondo wake kumsafisha au kumtia hatiani.Kuzembea kufanya hivyo ni kuiachia "mahakama ya umma" (court of public opinion) kumhukumu pasipo kumpatia nafasi ya kujitetea.Na kwa vile mahakama hiyo ya umma haina utaratibu wa kukata rufaa pindi hukumu ikishatolewa,tuhuma dhidi ya Mkapa zitaendelea kuwepo hadi hapo......God knows!Kama wanaomtetea wanampenda kwa dhati (au hata kinafiki) basi ni vema wakamwepusha na hatari ya kuburuzwa mahakamani akiwa na mkongojo wake,say miaka 20 au zaidi kutoka sasa.

Binafsi siamini kuwa wanaomtetea Mkapa wanafanya hivyo kwa vile wanamheshimu sana au wanaamini kuwa tuhuma hizo ni uzushi.Badala yake,wanachelea kwamba wakiruhusu sheria ichukue mkondo wake,kesho wao nao watajikuta wakikabiliwa na hali hiyohiyo kama ya Mkapa.Waadilifu hawaogopi sheria bali wanaiheshimu na kuilinda,lakini wenye mapungufu kwenye maadili yao huiogopa sheria kama kirusi cha mafua ya nguruwe (japo huitumia kuwakandamiza wabaya wao).

Naamini pia kuwa ipo siku Mkapa na watuhumiwa wengine wa ufisadi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.Inaweza kuwa sio kesho au mwaka kesho lakini siku hiyo itafika.Na hapa nazungumzia mahakama za kidunia na sio ile ya kwenye wimbo niupendao wa "na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe mbele ya Mungu,siku hiyo itafika...."

Kuendeleza ushkaji katika mambo yanayopaswa kushughulikiwa kisheria kunaweza pia kusambaza kirusi cha "ah mbona yule fisadi anatetewa na kusafishwa,what's wrong with me kufisadi pia?Si nami nitatetewa kama fisadi X..."Hapo tunafanya reproduction ya ufisadi katika jamii.Yayumkinika kuhisi kuwa kwa namna watuhumiwa wa ufisadi wa EPA,Richmond na maskandali mengine wanavyoendelea kuogopwa,tayari mafisadi hao wameshaambukiza virusi vya ufisadi kwa Watanzania wengine chungu mbovu.Thing is,kama wenye maamuzi wameamua kuhalalisha visivyo halali,then visivyo halali vinageuka kuwa halali.

Na kama kuna mzembe ataona wazo langu la kuchukua hatua dhidi ya Mkapa ni ukosefu wa nidhamu,then they can simply shove it up kunakostahili.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.