Showing posts with label EPA SCANDAL. Show all posts
Showing posts with label EPA SCANDAL. Show all posts

4 Nov 2011






Vigogo watafuna marejesho ya EPA
Thursday, 03 November 2011 21:27
Leon Bahati na Furaha Maugo
KAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imebaini ufisadi mwingine wa mabilioni ya fedha kwenye marejesho ya zile zilizochotwa awali kifisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).Fedha hizo zaidi ya Sh50 bilioni zilizorejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa zitatumika kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo nchini, zinadaiwa kuchotwa kwenye Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa amri iliyotoka kwa vigogo serikalini.

Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.

"Mbaya zaidi, baadhi ya wafanyabiashara waliopewa mikopo hiyo wanaonekana kukwama kurejesha, huku wakitoa ahadi ambazo hawazitekelezi," Noni alisema.

Wabunge wengi wa POAC walionyesha kushangazwa na jinsi serikali ilivyoingilia kati TIB na kuchagua watu ambao wanapaswa kupatiwa mikopo.Huku miongoni mwa wabunge hao wakisema wana taarifa za vigogo walioingia mlango wa nyuma na kuchukua tena fedha hizo katika mazingira ya kifisadi, waliendelea kumbana Noni kwa maswali.

Ingawa baadhi ya wabunge walimtaka mkurugenzi huyo wa TIB awataje kwa majini vigogo hao, Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Filikunjombe, alisita na kumtaka Noni asitaje majina hayo.

Miongoni mwa wabunge waliotaka majina ya vigogo hao yawekwe hadharani ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya aliyesema, “Nina habari kuwa baadhi ya vigogo walihusika katika kupata mikopo hiyo… Naomba uyataje majina yao.”

Filikunjombe, alisema hakuna haja ya kutaja majina ya vigogo hao ambao alisema miongoni yamo kwenye taarifa waliyopatiwa kuhusu utendaji mzima wa TIB.

Lakini Noni ambaye alikuwa anasaidiwa pia na wasaidizi wake kujibu baadhi ya maswali mazito yaliyoulizwa na wabunge, alisema hakuna tatizo kutaja baadhi ya kampuni zilizohusika kwenye mikopo hiyo ambayo sasa inawatoa jasho TIB.

Noni alitaja mbele ya kamati hiyo kuwa moja ya kampuni zilizochukua fedha hizo na sasa zinaonyesha wasiwasi katika kuzirejesha ni Simon Group Ltd.Nyingine ni kampuni tano za kuuza maua nje ya nchi zenye makao yake makuu mjini Arusha, zikiwepo Tengeru Flowers na Mount Meru Flowers.

Kuhusu Kampuni ya Simon Group, ambayo ilielezwa kuwa ilikopeshwa Sh5 bilioni Noni alisema; “Tumekutana nao mara kadhaa na kutoa ahadi lakini hawakuzitekeleza.”

Aliongoza kuwa kampuni za kuuza maua nje ya nchi zilieleza tatizo lililowafanya kushindwa kurejesha mikopo hiyo kulingana na makubaliano kwamba, ni hasara waliyoipata kutokana na mdororo wa kiuchumi duniani.

Alifahamisha kuwa kutokana na hali hiyo, Serikali iliwaonea huruma na kuwaongezea kipindi cha miaka miwili kulipa deni hilo, muda ambao pia umeonekana kutotosha.

Ila akaahidi kwamba TIB itaanza mchakato wa kuwabana wadeni hao kwa kunadi mali ambazo ziliwekwa rehani wakati wa kuchukua mikopo hiyo.

“Uandaaji na usafirishaji wa maua walisema unahitaji gharama kubwa… Walilazimika kupitia Nairobi (Kenya)… Serikali iliona huruma ikawaongezea kipindi cha kulipa deni hilo,” alisema Noni huku wabunge wengi wakionyesha shauku ya kuendelea kumbana kwa maswali.

Miongoni mwa maswali yaliyoulizwa ni kwa nini TIB ilikubali kutoa mkopo kwa biashara ambazo hazitabiriki? Noni aliweka wazi kwamba, benki hiyo haikuhusika katika mchakato wa kuchambua na kuridhia mikopo kutolewa kwa kampuni hizo.

Filikunjombe ambaye ni Mbunge wa Ludewa, alishangazwa na jinsi Serikali ilivyoingilia uhuru wa TIB na kuweka wazi kwamba si mara ya kwanza Serikali kuingilia mashirika ya umma kiutendaji na kwamba, historia inaonyesha kila ilipofanya hivyo iliziingiza taasisi hizo kwenye mzozo.

“Serikali iliwahi kuingilia kati na kushawishi Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) kuingia mikataba (ya kuzalisha umeme wa dharura) na Richmond na Dowans na kusababisha mzozo,” alitoa mfano Filikonjombe.

Hivyo, akaonya TIB kuhusu kupokea maagizo holela Serikalini kwa sababu mzigo wa matatizo yatakayotokea, itajiweka kando na kuiachia taasisi hiyo ya umma lawama na vibano kutoka kwa wananchi.

Mapendekezo ya Kamati
Ili kuikoa benki hiyo, Filikunjombe alitoa mapendekezo sita ambayo miongoni mwake ni kuitaka TIB ijitegemee na kufanya kazi zake kama shirika la umme lenye uwezo wa kufanya maamuzi yake ya kiutendaji bila kuingiliwa na wanasiasa serikalini.

“Mhakikishe hamuingiliwi na Wizara ya Fedha au Serikali katika suala la utoaji wa mikopo,” alishauri Filikonjombe.
Mapendekezo mengine ni muundo wa manunuzi katika taasisi yao uendane na sheria ya manunuzi, kuwa ni mikakati ya kushindana kibiashara na benki nyingine na kuhakikisha kuwa mtaji unakua.

Katika hatua nyingine, POAC ilishangazwa kuona kuwa kati ya zaidi ya Sh50 bilioni zilizokusanywa kwenye marejesho ya fedha zilizochotwa EPA, ni Sh20 bilioni pekee zilizoifikia TIB.
Wabunge hao walielezea kushangazwa na kitendo cha Menejimenti ya TIB kupokea fedha hizo tu na kushindwa kuishinikiza Serikali itoe fedha zaidi.

Noni alisema kuwa TIB haikuwa na mamlaka ya kuishinikiza Serikali ili iipatie fedha zote za marejesho ya EPA.
“Sisi tulichopewa ndiyo hicho. Hatukuwa na sababu ya kudai fedha zaidi,” alisema huku akizidi kuzua mtafaruku wa maswali kwa wabunge hao.

Wabunge wengi walionyesha kuamini kuwa fedha zote zilipelekwa TIB baada ya Serikali kuahidi kuwa fedha za marejesho hayo zitapelekwa kwenye shughuli za kilimo.

TIB ndiyo benki iliyoanzishwa na Serikali kwa malengo ya kuinua kilimo nchini ambacho kinategemewa na asilimia 80 ya Watanzania.Wananchi wengi wanaojishughulisha na kilimo nchini ndio wanaogubikwa na wimbi la umasikini kuliko sekta nyingine.

Hata hivyo, Serikali imeamua kuanzisha kampeni ya Kilimo Kwanza, yenye lengo la kufanya sekta hiyo kuwa yenye manufaa na inayoweza kuleta utajiri tofauti na mwonekano wa sasa wa kuwa ni ya kundi la wasio na taaluma.
Taarifa nyingine zilizopatikana jana baada ya kamati hiyo kumaliza kikao chake ni kwamba sehemu ya marejesho ya fedha za EPA, mbali na zile Sh20 bilioni zilizopelekwa TIB, zilitolewa kwa moja kwa moja kwa kampuni za pembejeo za kilimo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walielezea kutokuwa na imani kama fedha hizo zilitumika kikamilifu kwa ajili ya pembejeo hizo za kilimo.

Mmoja wa wabunge kutoka CCM ambaye hakutaka jina lake kutajwa gazetini alisema kuna uwezekano fedha hizo zimeliwa na wajanja.

“Hata ukiangalia suala la marejesho halikuwekwa wazi, maana Rais (Kikwete) mwenyewe alisema zimekusanywa Sh53 bilioni, mara wengine wakasema 60 bilioni na wengine 70 bilioni.Alisema kama ufisadi uliweza kupenya hadi fedha zilizotolewa kwenye taasisi makini ya benki (TIB) basi hakuna shaka hata zilizotolewa kimyakimya ziliingia kwenye mikono hiyo ya mafisadi.

Hata hivyo, gazeti la serikali liliwahi kumnukuu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mohamed Muya, akisema katika mgawanyo wa fedha za EPA, wizara hiyo ilipewa Sh40 bilioni ambapo Sh30 bilioni zilitumika kwa ruzuku ya pembejeo ya mbolea hali ambayo imesaidia katika uzalishaji. 



“Kutokana na ruzuku hizi, hata idadi ya wakulima wanaopata vocha za ruzuku hiyo imeongezeka kutoka wakulima 500,000 hadi wakulima milioni 1.5 mwaka huu na kupitia Kamati ya Maafa na ya Usalama wa Chakula, hali ya chakula mwaka huu ni nzuri kuliko mwaka jana,” alisema Muya. 



Alisema katika fedha hizo za EPA, Sh10 bilioni zilizobaki zilitumika katika maeneo matatu ya kilimo ambayo ni Mfuko wa Pembejeo ambao ulipewa Sh3 bilioni, Wakala wa Mbegu wa Taifa Sh1 bilioni na kutatua matatizo ya visumbufu kama vile nzige, kweleakwelea na viwavijeshi Sh6 bilioni.

CHANZO: Mwananchi

30 Jul 2009


Tume huru inayochunguza uhusika wa Uingereza katika vita ya Iraki imetangaza kuwa itamhoji Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.


Atakayenuna na anune,lakini ni dhahiri kuwa Rais wetu mstaafu ( wa awamu ya tatu),Benjamin William Mkapa,amekuwa akiandamwa na tuhuma za ufisadi wakati akiwa jengo takatifu la Ikulu.Hoja kubwa ya wanaomtetea Mkapa ni maneno kama "Mwacheni Mzee wetu apumzike".

Ni wazo zuri kutosumbua wazee wetu,lakini ingeleta maana kama wazee wote,na si Mkapa pekee,wangekumbukwa katika "maombi" hayo kuwa waachwe wapumzike.Mbona "busara" hizo hazijatumika kuwakumbuka wazee (halisi) wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?Wamesumbuliwa,wamezungushwa,wametishiwa FFU,na kufanyiwa kila aina ya vituko...tofauti na Mkapa-ambaye hajaomba atetewe au ajitetee-wastaafu hao wanadai stahili yao halali.Hawakutumia ofisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kununua japo vifusi vya kokoto au kuanzisha chama cha kuweka na kukopa,tofauti na Mkapa ambaye pamoja na mambo mengine anayetuhumiwa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kishkaji na pia kuhusishwa na kuanzisha benki.

Hivi njia bora zaidi ya kumwacha Mkapa apumzike ni kwa wanasiasa kumsafisha katika tuhuma za ufisadi zinazomkabili au kwa mahakama-chombo chenye mamlaka ya kikatiba kutoa haki-kufanya kazi hiyo?Wanasiasa wetu ni wavivu wa kufikiri.Wao ni binadamu,kwa maana hiyo leo wapo kesho hawapo-aidha kiuhai au kimadaraka.Utetezi wao leo unaweza kabisa kuondoka pindi nao watakapoondoka.Uzuri wa taasisi-kama mahakama-ni kwamba inastahili kuwepo kwa muda mrefu au hata milele ikibidi.Na hata ikibadilishwa,misingi yake itaendelea kuwepo.Kwa mantiki hiyo,namna pekee ya "kumwacha Mkapa apumzike" ni kumburuza mahakamani kisha haki itendekee huko.Kupuuza ushauri huu kunaweza kupelekea mzee huyo kuburuzwa kwa nguvu kwenda kujibu tuhuma zake wakati watetezi wake wa sasa hawako madarakani au nao wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kujibu.Hebu chukua mfano mwepesi kama huu.Unadhani Charles Taylor huko aliko anakumbuka flani aliyekuwa anamtetea?Hapo ni kila mtu anabeba mzigo wake.

Sawa,Tanzania sio Uingereza.Na ni kweli kwamba sio kila wafanyalo Waingereza lazima sie pia tulifanye.Lakini mfano wa Blair kufikishwa kwenye tume hiyo ya vita ya Irak inapswa kuwa changamoto nzuri kwa mamlaka zetu kuangalia umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu badala ya kuendekeza ushakaji na kubebana.By the way,si kila mtuhumiwa anayefikishwa kwenye vyombo vya sheria lazima aonekane ana hatia.

Mzee wetu Mkapa hatoweza kupumzika hadi sheria itakapochukua mkondo wake kumsafisha au kumtia hatiani.Kuzembea kufanya hivyo ni kuiachia "mahakama ya umma" (court of public opinion) kumhukumu pasipo kumpatia nafasi ya kujitetea.Na kwa vile mahakama hiyo ya umma haina utaratibu wa kukata rufaa pindi hukumu ikishatolewa,tuhuma dhidi ya Mkapa zitaendelea kuwepo hadi hapo......God knows!Kama wanaomtetea wanampenda kwa dhati (au hata kinafiki) basi ni vema wakamwepusha na hatari ya kuburuzwa mahakamani akiwa na mkongojo wake,say miaka 20 au zaidi kutoka sasa.

Binafsi siamini kuwa wanaomtetea Mkapa wanafanya hivyo kwa vile wanamheshimu sana au wanaamini kuwa tuhuma hizo ni uzushi.Badala yake,wanachelea kwamba wakiruhusu sheria ichukue mkondo wake,kesho wao nao watajikuta wakikabiliwa na hali hiyohiyo kama ya Mkapa.Waadilifu hawaogopi sheria bali wanaiheshimu na kuilinda,lakini wenye mapungufu kwenye maadili yao huiogopa sheria kama kirusi cha mafua ya nguruwe (japo huitumia kuwakandamiza wabaya wao).

Naamini pia kuwa ipo siku Mkapa na watuhumiwa wengine wa ufisadi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.Inaweza kuwa sio kesho au mwaka kesho lakini siku hiyo itafika.Na hapa nazungumzia mahakama za kidunia na sio ile ya kwenye wimbo niupendao wa "na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe mbele ya Mungu,siku hiyo itafika...."

Kuendeleza ushkaji katika mambo yanayopaswa kushughulikiwa kisheria kunaweza pia kusambaza kirusi cha "ah mbona yule fisadi anatetewa na kusafishwa,what's wrong with me kufisadi pia?Si nami nitatetewa kama fisadi X..."Hapo tunafanya reproduction ya ufisadi katika jamii.Yayumkinika kuhisi kuwa kwa namna watuhumiwa wa ufisadi wa EPA,Richmond na maskandali mengine wanavyoendelea kuogopwa,tayari mafisadi hao wameshaambukiza virusi vya ufisadi kwa Watanzania wengine chungu mbovu.Thing is,kama wenye maamuzi wameamua kuhalalisha visivyo halali,then visivyo halali vinageuka kuwa halali.

Na kama kuna mzembe ataona wazo langu la kuchukua hatua dhidi ya Mkapa ni ukosefu wa nidhamu,then they can simply shove it up kunakostahili.

19 Nov 2008


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kusisitiza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinahusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Hayo yalibainishwa juzi na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe, alipohutubia wananchi wa Manispaa ya Iringa, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mwembe Togwa.

Alisema CCM inahusika na wizi wa fedha hizo, kwani chama hicho ndicho kilichotoa maelekezo kwa makampuni yanayotuhumiwa kuiba fedha hizo.

Alisema CCM ilitumia makampuni hewa yaliyoanzishwa kughushi na kujipatia fedha hizo kwa ajili ya kugharamia kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, uliomwingiza Rais Jakaya Kikwete madarakani kwa ushindi wa asimilia 80.

Akitoa mfano Zitto alisema, kutokana na rekodi za kibenki za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), CHADEMA ilibaini CCM iliitumia kampuni hewa ya Deep Green Finance, kuchota sh bilioni 10.4, katika kipindi cha miezi minne kati ya Agosti mosi na Desemba 10 mwaka 2005, na kisha kampuni hiyo kutoweka katika faili la Msajili wa makampuni nchini (BRELA).

Alisema katika kipindi hicho CCM pia iliitumia Kampuni ya Tangold Ltd ambayo haikuwa imesajiliwa kisheria, kujichotea kiasi kingine cha sh bilioni 9 kwa madhumuni hayo hayo ya kugharamia kampeni zake.

Aidha, alisema baadhi ya viongozi wa CCM wana uhusiano wa moja kwa moja na Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, ambayo ni moja ya kampuni kadhaa zinazodaiwa kuhusika na wizi huo, na kujipatia fedha kwa ajili ya kampeni, lakini vigogo wa CCM waliohusika na wizi huo hawajafikishwa mahakamani.

Alisema, CCM ilimtumia pia mfanyabiashara mmoja maarufu mwenye asili ya Kiasia (jina tunalo) kujipatia kiasi kingine cha fedha, na licha ya mfanyabiashara huyo kurejesha fedha alizochukua bado alifikishwa mahakamani kwa sababu ya kukataa kurejesha kiasi kingine cha fedha.

Alisema mfanyabiashara huyo aliikatalia serikali ya CCM, kurejesha sehemu ya fedha alizochukua kwa sababu kiasi hicho cha fedha ndicho alichokitumia kuwanunulia viongozi wa CCM magari aina ya Mahandra.

“Kama CCM inabisha kwamba haikufadhiliwa wala kununuliwa magari na mtuhumiwa huyo wa EPA, itoe vielelezo vyote vinavyothibitisha kwamba walinunua wenyewe magari hayo. Itoe risiti zote za usajili wa ....na iseme ilitumia fedha kiasi gani wakati wa kampeni. Iseme ilizipata wapi fedha hizo,” alisema Zitto huku akishangiliwa.

Alisema Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, hajui chochote kuhusiana na jinsi chama chake kilivyopata fedha za kampeni ndiyo maana amekuwa akitetea.

Alisema Chiligati hajui kwa sababu kampeni za CCM wakati wa uchaguzi mkuu 2005, hazikuratibiwa na viongozi wa makao makuu ya chama hicho, bali ziliratibiwa na kundi maarufu la wanamtandao lililokuwa mstari wa mbele kumuunga mkono Rais Kikwete, tangu katika hatua za awali za uteuzi wa mgombea wa chama hicho.

Alisema kwa mara ya kwanza, sakata la wizi wa fedha za EPA, liliibuliwa bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Willbrod Slaa, lakini wabunge na viongozi wa CCM walisema Slaa alitumia nyaraka za kughushi na hoja yake ilikuwa ya uongo.

Aliendelea kufafanua kwamba, sakata hilo lilipozidi serikali ililazimika kutumia kampuni kufanya ukaguzi ambayo ilithibitisha kwamba ilikuwa ni kweli.

Alisema suluhisho la msingi la kushughulikia kwa haki watuhumiwa wote wa EPA na kuhakikisha kwamba wizi huo hautokei tena, ni kwa serikali kuanzisha Mahakama Maalumu ‘Tribunal’ itakayohusisha wanasheria na majaji wastaafu wanaoheshimika na kuaminika nchini pamoja na wataalamu wazoefu wa masuala ya fedha, kwa ajili ya kushughulikia tuhuma zote za EPA.

Alisema bilioni 133 zilizoibwa ni fedha za umma na wala wananchi wasikubali kudanganywa kwamba fedha hizo si za serikali.

Katika mkutano huo, aliyekuwa kada maarufu wa Chama cha Wananchi CUF katika manispaa hiyo, Mlaki Mdemu, alitangaza kujiunga na CHADEMA na kukabidhiwa kadi ya uanachama na Zitto.

Wananchi waliohudhuria mkutano huo, waliichangia CHADEMA, takriban sh 300,000 na kukitaka chama hicho kiende kwenye Jimbo la Mbeya Vijijini, ambalo liko wazi kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wake, Richard Nyaulawa, kilichotokea hivi karibuni.

Hata hivyo, Zitto aliwaambia wananchi hao kwamba CHADEMA inakusudia kusimamisha mgombea katika jimbo hilo, lakini kwa sasa haiwezi kufanya lolote, kwa kuwa bado inaomboleza msiba huo.


IWAPO MADAI HAYA YA CHADEMA YANA UKWELI (AND CIRCUMSTANTIAL EVEDIENCE SEEMS TO BACK THEM) BASI HUENDA HATA KESI ZINAZOENDELEA MAHAKAMANI NI CHANGA LA MACHO TU.CCM NEEDS TO COME CLEAN ON THIS.

17 Nov 2008


*Wajipanga kuanika siri zote hadharani
*Vocha za malipo kwa CCM kuanikwa
*Kapt. Chiligati awakana, naye awatisha
*Asisitiza hakuna kikao kilichowatuma

Na Mwandishi Wetu 

BAADHI ya watuhumiwa wa ufisadi kwenye Akaunti ya EPA iliyokuwa Benki Kuu (BoT) sasa wameamua kuitisha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, uchunguzi wa Majira umebaini. 

Kitisho hicho kimekuja kufuatia baadhi yao kukamwatwa na kufunguliwa kesi mbalimbali za jinai huku ikionekana kuwa wao walikuwa mawakala tu katika kupitisha fedha hizo na vigogo husika wakiwa nje. 

Chanzo chetu kilicho karibu na baadhi ya watuhumiwa hao kilieleza kuwa kukamatwa, kufunguliwa mashitaka kumewadhalilisha sana baadhi yao huku wakiumia zaidi kwa kusota rumande, kwenye gereza la Keko na wale wanawake wakiweka Gereza la Wanawake Segerea. 

"Jamaa ameumia sana rohoni, hata kuhangaikia dhamana alisita mwanzo baada ya kuona kwa nini ahangaike kutoa mali zake, wakati alikuwa wakala tu," kilisema chanzo chetu kilicho karibu ni mmoja wa watuhumiwa waliokwisha funguliwa kesi na akasota sana kwenye gereza la Keko. 

Ingawa Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikikana mara kadhaa kuhusika kunufaika na fedha hizo katika chaguzi mbalimbali, duru za uchunguzi, zinawakariri baadhi ya watuhumiwa hao wakilalamika 'kutolewa kafara.' 

Ndugu mwingine wa mtuhumiwa ambaye ameshafanikiwa kwa kiasi kikubwa kulikwepa sakata la EPA, ingawa taarifa za kiuchunguzi bado zinaamini huenda akaburutwa naye kortini, aligusia kuwa kwa sababu yeye alitumiwa tu, ameandaa faili la utetezi ambalo pamoja na nyaraka nyingine, limeheheni kile alichokitaja kuwa vocha za malipo kwenda kwa baadhi ya vigogo wa CCM. 

"Hapa ndipo Serikali itakapoumbuka. Kila kitu kipo. Hajakamatwa bado, ameshahojiwa na kubanwa katika shughuli zake, anasubiri tu afikishwe kortini atoe vielelezo vyake, yeye si fisadi, aliombwa asaidie shughuli halali akafanya hivyo, kwa namna anavyojiheshimu, asingeweza kusaidia akakubali wizi," kilisema chanzo chetu kilicholiona faili hilo la utetezi. 

Wakati watuhumiwa hao wa EPA wakijipa 'kujiondoa katika ukafara,' Mwandishi Wetu Eckland Mwaffisi anaripoti kuwa uongozi wa juu wa CCM, umeendelea kusisitiza kuwa hawahusiki na ufisadi wa EPA. 

Akitoa tamko kwa niaba ya Chama chake Dar es Salaam jana, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Bw. John Chilligati, alisema CCM haikuhusika na wizi huo kama ilivyodhibitishwa na ripoti ya kamati ya wanasheria. 

Alisema pamoja na madai yanayotolewa na viongozi wa vyama vya upinzani, pasipo kuthibitisha madai hayo, CCM haikuchukua fedha hizo wala haikumtuma mwanachama wake au mkereketwa yoyote kwenda kuchukua fedha hizo katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT). 

Bw. Chilligati alisema pamoja na orodha ya watuhumiwa wa EPA kuhusisha majina ya wanachama wa CCM ama Wakereketwa, Chama hakijahusika kumtuma bali ni kitendo cha mtu binafsi. 

Hadi sasa miongoni mwa waliokamatwa kwa tuhuma za wizi wa fedha za EPA wanaohusishwa na ukaribu na vigogo wa CCM au kuwa makada ni Bw. Rajabu Maranda na mfanyabiashara, Bw. Jeetu Patel. 

"Kwenye ukweli, uongo hujitenga, madai yote ya kuihusisha CCM na ufisadi wa EPA ni uongo wenye nia ya kukivunjia heshima chama chetu machoni mwa jamii pamoja na hila za kuchafua jina la chama zinazofanywa na wapinzani ambazo kamwe, hazitafanikiwa," alisema Bw. Chilligati. 

Kutokana na hali hiyo, Bw. Chilligati aliongeza kuwa, baadhi ya wanachama wanaokiuka maadili hayo, isichukuliwe kwamba wanatumwa na vikao vya chama bali ni vitendo vyao binafsi na watachukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya dola kama ilivyo kwa wahalifu wengine. 

Alisema CCM, inapongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua alizozichukua katika kushughulikia sakata hilo. 

Hadi wiki inayoanza leo, ambapo zipo tetesi za watuhumiwa zaidi kuanza kufikishwa kortini huku Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), Bw. Eliezer Feleshi akikiri kuwa bado kuna mafaili yanapitiwa, idadi ya watuhumiwa waliokwishafikishwa kortini ni 20. 

Baadhi ya makampuni ambayo yameshafikishwa mahakamani ni pamoja na Money Planners, Kiloloma & Brothers, Njake Hotel, Rashhas, Mibare Farm, Changanyikeni, Bencon International, Kernel, Malta Mining, Navy Cut Tobacco na BC Grassel & Company. 

Makampuni yanayosubiriwa kwa hamu na wananchi katika Mahakama ya Kisutu ni pamoja na kampuni ya Kagoda ambayo inadaiwa kuchota fedha nyingi kulikoni kampuni nyingine.

CHANZO: Majira

16 Nov 2008

Photo courtesy of MICHUZI

From the outside, the highly protected Maximum Prison, located in the southern part of Dar es Salaam, could easily be mistaken for a Toyota showroom on weekend days. 

But the compound is not a showroom. It is the current home of 13 EPA suspects who have so far spent about ten days in the tiny prison's cells, since they were arrested last week. 

Behind these highly fenced and protected walls are men who were busy men who negotiated lucrative business deals over their sophisticated mobile phones, in fabulously furnished offices or in the restaurants of the city`s expensive hotels. 

Their arrests and prosecution last week changed their lifestyles suddenly and dramatically. 

One close family member of the prominent tycoon Jeetu Patel hinted to our reporter in the prison compound: ``Boss doesn`t believe what is happening,he feels he has been betrayed by his allies in the government.`` 

The person, who spoke on condition of anonymity last Sunday, explained further: ``He was extremely shocked on the day he entered prison, but he says he has surrendered his fate to the almighty God.`` 

For some, it has been a dream shattered by their sudden arrest, but for others it has been a time for short vacation after spending months on the streets of Dar es Salaam, trying to make ends meet. 

Their life hasn't changed much, though their freedom to move and mix with their buddies and families have been terminated, as they spend their nights and days at the Prison, pending the fate of their bail applications. 

According to a week-long survey conducted by The Guardian on Sunday, despite being locked behind bars, some suspects are still managing their businesses from the prison. 

``Each passing day the businessman signs several cheques amounting to millions of shillings. 

It is business as usual, the only difference being that it is being conducted in a prison cell instead of an office,`` one senior prison official who declined to have his identity disclosed, revealed. 

In what shows the smugness of money on Sunday, the Prison`s parking yards is full of posh cars as relatives and friends gathers here to see the EPA suspects. 

Inside prison however, some of them are enjoying a relatively good lifestyle compared to their fellow inmates, one of the aspects of which is the allowance for accessing food from outside, while ordinary inmates scramble for the little, unpalatable official variety. 

And to make life easier, some of the suspects reportedly spend much time in sickbays reserved for ailing inmates. 

It is being speculated, also, that confining the suspects to the sickbays is a deliberate security measure intended to protect them from attacks by ordinary remandees who may be infuriated by the EPA scum. 

``The way they are being treated is quite different from other prisoners,`` the official said. 
One of two brothers charged in the case remarked openly to prison warders: `It is a relief for me to stay away for sometime from the taxing business engagements. Two weeks here will do me some good.`` 

Sunday is a hectic day for prison warders, as they have to cope with hundreds of well-wishers of the EPA suspects. 

``I have never experienced such a situation since I became a warder ten years ago,`` one of them remarked. According to the Prisons regulations, visitors are allowed to see their relatives on Sundays. 

Security 

Alarmed by the prominence of the EPA suspects- considering that most of them are powerful financially who can even buy their way out-on Tuesday this week, strategic measures to improve security were taken by the government. 

Assistant Commissioner of Prisons Mtiga Omari, fearing a recurrence of the early 1980s when some treason trial suspects escaped from the prison, said effective from this mid-week all visitors of the EPA suspects must secure special permission from the Prisons Department Headquarters. 

``These suspects hold financial power which can easily corrupt some of our `weak` people. 

To play it safe, anyone seeking an audience with the suspects must get a permit from us,`` said Mtiga who incidentally overheard a group of people at Kisutu Court area joking that ``the police have taken theirs, it is now the turn of the judiciary to take theirs.`` 

The relatives or friends must give in writing their identities, the EPA suspects they want to visit and the reasons behind such visits to satisfy the Commissioner for Legal Affairs and Administration. 

This will also help in keeping track of them, he explained. 

``We are careful. Some of these persons are top executives in local and international businesses, others in high positions in the Bank of Tanzania, while some are decision-makers in companies involved in the scandal,`` Mtiga said. 

``Their offices may need them for some reasons or other.`` 

ACP Mtiga said the issue of segregating EPA suspects from other remanded prisoners at Keko or Segerea is the discretion of the Principal Commissioner of Prisons, although he dismissed any favouritism.



14 Nov 2008


TWO prominent business tycoons linked to Kagoda Agriculture Limited, who are considered as the main architects of the external payment arrears (EPA) scandal, will not face criminal charges despite stealing more than 40bn/- from the key Bank of Tanzania account, it has been revealed. 

Sources close to the EPA investigation say the well-known businessmen ’’will be protected from prosecution at all costs.’’ 

’’A deal has already been sealed. The Kagoda tycoons will never see the inside of a jail. They are untouchable,’’ a well-placed source told THISDAY. 

He added: ’’A lot of influential people have been compromised to make sure that the Kagoda case never goes to trial, despite the fact that it was responsible for the single biggest looting of the EPA account.’’ 

Insiders say an elaborate strategy had been put into action to ensure the two prominent businessmen, who are well known by the government, are not included in the high-profile EPA criminal cases at the Kisutu Resident Magistrate’s Court. 

It is understood that the concerned businessmen have vowed to ’silence’ whistle-blowers such as journalists, politicians and law enforcement officials who continue to raise the Kagoda issue. 

’’Those who question why the Kagoda tycoons have been left off the hook will be taken care of’’ said another source familiar with the EPA scandal. 

Informed sources say another prominent businessman, Jeetu Patel, might have been used as a scapegoat to divert attention from the Kagoda issue.

’’The fact that Jeetu Patel was prosecuted despite returning tens of billions of shillings to the government was deliberately meant to serve as a smokescreen as part of the elaborate scheme to ensure Kagoda crooks don't appear in court,’’ said our source. 

’’They thought that by sending Jeetu Patel to jail, people will forget about Kagoda since all the attention of the media and hence members of the public will have shifted to this particular business tycoon (Jeetu Patel).’’ 

Observers say if the Kagoda tycoons are not taken to court like the rest of other suspects, this would render the entire EPA criminal proceedings as ’’one big sham.’’ 

So far, 20 high-profile suspects have already been arraigned in court to face various criminal charges, including conspiracy, fraud and theft, in connection with the embezzlement of more than 90bn/- from the EPA account during 2005/06. 

The EPA probe team led by Attorney General Johnson Mwanyika is investigating nine other companies that were paid more than 42bn/- from the same BoT account without relevant supporting documents. 

Investigations by THISDAY have already revealed that the two business tycoons behind the Kagoda company were shifting the theft of BoT funds to a dead man as part of the plot to avoid criminal charges. 

One of the businessmen is believed to have personally told EPA investigators that his deceased father was the actual beneficiary of over $30.8m (approx. 40bn/-) fraudulently paid to Kagoda from the key BoT account. 

In doing so, the tycoon accepted financial liability and returned all the stolen funds to the government before the October 31, in an attempt to avoid criminal charges.

SOURCE: This Day

IT'S TOO EARLY TO MAKE ANY CONCLUSION BUT THOSE IN THE KNOW ALREADY DOUBT WHETHER THE ON-GOING TRIALS WOULD LEAD TO THE LAW NOT ONLY BEING DONE BUT ALSO SEEN TO HAVE BEEN DONE.DOUBTING THOMASES?WELL,THEY MIGHT HAVE A POINT SINCE IT NOW BECOMES MORE OBVIOUS THAT THE KAGODA TYCOONS (ONES WHO SWINDLED NEARLY A HALF OF THE MONIES) ARE BEING SHIELDED FROM PROSECUTION.FOR SOME OF US,THEY REMAIN GUILTY UNTIL PROVEN,BEYOND ANY REASONABLE DOUBT,INNOCENT.

12 Nov 2008

MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, amesema kuwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote wa ufisadi kwa pamoja kunaweza kusababisha nchi kuyumba.

Hoseah alisema hayo katika siku ambayo hakukuwa na mtuhumiwa yeyote katika sakata la wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) aliyefikishwa mahakamani baada ya wafanyabiashara 20 kupandishwa mfululizo kizimbani kuanzia Jumatano iliyopita hadi juzi.

Akitoa mada kwenye semina iliyohusisha vyuo vikuu tisa nchini iliyofanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl jijini, mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema: "Tukiwapeleka wote mara moja mahakamani, nchi inaweza 'ikaparalyse' (ikapooza) ni lazima kuwe na 'stability' (kutoyumba), tufanye kwa kuwa ni sahihi," alisema Hoseah.

Akitoa mada katika semina hiyo iliyowahusisha wajumbe wa kamati za maadili kutoka vyuo hivyo, Hoseah alieleza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa kubwa yanapaswa kufanyika kukiwa na utashi wenye nguvu wa kisiasa, mikakati sahihi ya kiuchumi pamoja na kuzuia rushwa.

Alisema kuwa watuhumiwa wa rushwa kubwa wana nguvu kutokana na fedha nyingi wanazomiliki, kiasi cha kuweza kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa kutumia vibaya fedha zao.

Dk Hoseah ni kigogo wa tatu kuzungumzia uwezo wa mafisadi na hatari ya kuwashughulikia bila ya umakini baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulieleza bunge kuwa, kushughulikia watu wenye uwezo wa kifedha ni kazi ngumu, kama ilivyoelezwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Ali Hassan Mwinyi kuwa mafisadi ni hatari.

Watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA wanadaiwa kuchota fedha hizo katika kipindi cha mwaka 2005/06 wakisingizia kupewa au kulipa madeni na makampuni ya nje yaliyokuwa yakiidai serikali. Watuhumiwa hao wanadaiwa kuchota Sh133 bilioni.

Pamoja na kilio cha wananchi kuwa wote waliochota fedha hizo wapandishwe kizimbani, Rais Jakaya Kikwete alitoa maagizo kuwa wale ambao wangeshindwa kurejesha fedha walizochota kabla ya Oktoba 31, ndio waliotakiwa kufikishwa mahakamani.

Na watuhumiwa hao 20 waliofikishwa mahakamani hadi sasa wamekuwa wakipandishwa kizimbani kwa nyakati tofauti na wengi wameshtakiwa kwa makosa tofauti, wakipandishwa mmoja mmoja na wakati mwingine kuunganishwa na wenzao na kwa mahakimu tofauti.

Akitoa mada yake jana, Dk Hosea alisema Takukuru peke yake haiwezi kumaliza tatizo la rushwa nchini bila kuwepo ushirikiano kutoka kwa taasisi za elimu, mashirika mbalimbali na wananchi.

Aliongeza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa, kubwa na ndogo yanapaswa kuwashirikisha wananchi wote, huku akielezea Watanzania kuwa ni waoga kutokana na kukosa ufahamu wa masuala mbalimbali yanayowahusu.

Hoseah alisema kuwa katika mapambano ya rushwa ni vema kuzuia rushwa na kwamba uadilifu ndiyo njia bora ya kulitokomeza tatizo hilo.

Alisema moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi nyingi dhaifu, zisizo na uwezo zinazofanya kazi zake bila ya uwazi, hali aliyoielezea kuwa inakaribisha rushwa.

"Moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi dhaifu, zisizo na uwazi... lazima tufanye kazi kuzipa nguvu kwa kurejesha maadili," alisema Hoseah.

Aliongeza kuwa, ndani ya serikali pia uadilifu upo chini na kueleza kuwa kuwa kutokana na hali hiyo ni vema wananchi wakaacha kulalamika badala yake kutafuta ufumbuzi wa tatizo kwa kushiriki kurejesha maadili na kupambana na rushwa.

Alisema kuwa Watanzania wengi wamekuwa wakilalamikia tatizo la rushwa huku wakishinikiza Takukuru ichukue hatua bila wao kushiriki katika mapambano hayo ambayo alisema kuwa ni ya kila mmoja.

Mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema kuwa katika kutilia maanani umuhimu wa kuongeza jitihada za kuzuia na kupambana na rushwa nchini, wameanzisha mkakati maalumu wenye lengo la kurejesha uadilifu nchini.

"Tunataka kurejesha maadili, lengo ni kuzuia rushwa, jukumu letu ni kuwawezesha watu wafahamu na kushiriki katika mapambano hayo," alisema.

Kwenye Mahakama ya Kisutu, hali jana ilikuwa shwari baada ya siku nne za purukushani za kupandisha kizimbani watuhumiwa hao 20, ambao kati yao ni wawili tu waliopata dhamana kutokana na mahakama kuweka masharti magumu, anaripoti James Magai na Paulina Richard.

Hadi majira ya alasiri jana, hakuna mtuhumiwa hata mmoja mpya kwenye kesi hiyo ambaye alikuwa amefikishwa mahakamani hapo.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Inspekta Charles Kenyela, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi mchana huo hakuwa na taarifa za kuwepo kwa watuhumiwa wengine ambao wangepandishwa kizimbani.

Mpaka sasa ni wamiliki wa kampuni 10 tu kati ya 22 zinazodaiwa kuchota fedha hizo ambao walikuwa wameshafikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, akiwemo mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya Kiasia, Jayatkumar Chantubhai Patel, ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Jeetu Patel.

Tofauti na siku nyingine jana hali ilionekana kuwa tulivu mahakamani hapo huku kukiwa na pilikapilika chache za baadhi ya ndugu wa watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA ambao walikuwa wakishughulikia dhamana za watuhumiwa hao.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Elieza Feleshi, hakutaka kuwaambia waandishi kama kuna watuhumiwa zaidi ambao wangefikishwa mahakamani jana na badala yake alisema aulizwe msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Hata hivyo, msemaji huyo, Omega Ngole alijibu kwa ufupi kuwa hawawezi kusema ni lini watuhumiwa wanapelekwa mahakamani na badala yake taratibu zinapokamilika na DPP kujiridhisha, wahusika hufikishwa mahakamani.

“Hivyo ninachoweza kukuambia ni kwamba, tumwache DPP afanye kazi, kama kuna watu wa kuwapeleka mahakamani akishajiridhisha atawapeleka,” alisema Ngoe.

Wamiliki wa makampuni waliofikishwa mahakamani mpaka sasa ni Johnson na Mwesiga wanaomiliki kampuni ya Kernel, Ketan Chohan, Jeetu Patel na Amit Nandy (Bina Resort na Itoh), Bahati Mahenge, Manase Mwakale, Davis Kamungu, Godfrey Mosha na Edah Nkoma Mwakale (Changanyike Residential Compelex Ltd)

Wengine ni Rajabu Farijala, Japhet Lema na Rajabu Malanda (Mibale Farm), Rajabu Farijala na Rajabu Malanda (Money Planner), Japhet Lema (Njake Enterprises) na Ajay Somani na Jay Somani (Liquidity Services).

Wengine ni Jeetu Patel na ndugu zake wanaomiliki kampuni za Bencon International Ltd, Maltan Mining Ltd na Navy Cut Tobacco (T) Ltd.

CHANZO: Mwananchi

HAYO NDIO MATUNDA YA PhD YA HOSEA KATIKA KUPAMBANA NA RUSHWA AU NDIO APPLICATION YA THEORY FLANI YA KULINDA UHALIFU INAYODAI KWAMBA UKIFUTA KABISA UHALIFU KWENYE JAMII BASI VYOMBO VYA KUPAMBANA NA UHALIFU VITAKUWA HAVINA KAZI YA KUFANYA?MBONA VITA YA SOKOINE DHIDI YA WAHUJUMU UCHUMI HAIKUYUMBISHA NCHI?

3 Nov 2008


Kizitto Noya, Kilwa Masoko
WAKATI baadhi ya watu wakiamini kuwa serikali ilitumia busara kuhakikisha fedha zilizochotwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), zinarejeshwa kabla ya wezi kufikishwa mahakamani, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad haamini kama fedha hizo zimerejeshwa.

Na badala yake waziri huyo kiongozi wa zamani wa Zanzibar anasema madai ya kurejeshwa kwa Sh69 bilioni kati ya Sh133 ni mwendelezo wa usanii wa chama na serikali yake.

Maalim Seif alisema hayo mwishoni wa wiki alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Lindi kwenye Uwanja wa Kilwa Masoko, baada ya kupokea maandamano ya CUF ya kupinga ufisadi na kushinikiza wezi hao wa fedha za EPA wafikishwe mahakamani.

Alisema hawezi kuamini kwamba mafisadi hao wamerudisha fedha mpaka aone kwamba wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili za kuiba Sh133bilioni.

"Mimi naamini kwamba, hakuna hata mtuhumiwa mmoja wa ufisadi wa EPA aliyerudisha fedha na kauli ya Rais (Jakaya) Kikwete ni mwendelezo wa usanii wa serikali ya CCM kuwalaghai Watanzania ili waamini kuwa kazi imefanyika," alisema.

Alisema yeye kama Watanzania wengine wenye akili timamu, hataamini kwamba kuna fedha iliyorudishwa na mafisadi wa EPA na kwamba atafanya hivyo ikiwa ataona mafisadi hao wanafunguliwa kesi mahakamani.

Kauli ya Maalim Seif ilifuatia maswali ya waandamanaji hao kumtaka aeleze msimamo wa CUF kuhusu ufisadi wa EPA na mazungumzo ya mwafaka baina ya chama chake na CCM.

Alisema CUF hairidhishwi na namna serikali inavyoshughulikia suala la EPA na ndio maana viongozi wake wakuu wanazunguka nchi nzima kufanya maandamano ya amani kupinga ufisadi huo na kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani.

Rais Kikwete alitaka wezi hao warejeshe fedha kabla ya Oktoba 31 na kwamba wale ambao watashindwa kuzirejesha, wafikishwe mahakamani ifikapo Novemba mosi.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Oktoba 31, Rais Kikwete alisema jumla ya Sh69 bilioni zimesharejeshwa na kwamba, ametoa ruhusa kwa watuhumiwa kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, hadi jana Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), alikuwa bado hajawasimamisha watuhumiwa hao mahakamani.

Kuhusu mwafaka, Maalim Seif alisema CCM ilianza kutumia nguvu ya ulaghai katika suala hilo kwa kujifanya inataka kumaliza mgogoro wa mpasuko wa Zanzibar wakati ikijua kuwa haina nia hiyo.

Alisema: "CUF tumegundua ulaghai huo na sasa tumewaambia kwamba haturudi tena kwenye mikutano ya mwafaka. Tunataka kama wana nia njema na mwafaka, wasaini makubaliano yaliyofikiwa," alisema.

Alisema CUF pia imefunga mjadala na vikao vya mwafaka baina yake na CCM baada ya kuona kuwa wenzao wa CCM wanawarubuni na kuwahadaa.

Kuhusu nguvu ya utajiri wa kifisadi, Maalim Seif alisema CCM inatumia fedha nyingi kuwarubuni wananchi kwa zawadi ili waendelee kuiamini na kuwachagua, fedha ambazo baadaye wanazirudisha kwa wizi wa mali za umma na ufisadi.

"Pia CCM wanatumia ya nguvu dola kuwatisha wananchi na kuwapiga wananchi ili wasiwe huru kuwachagua vingozi wanaowapenda," alisema.

CHANZO: Mwananchi

PENGINE HOFU YA AINA HII INATOKANA NA UKWELI KWAMBA HAO WANAODAIWA KUREJESHA MABILIONI HAYO WAMEENDELEA KUWA ANONYMOUS.IWAPO MAJORITY YA WATOA SADAKA MAKANISANI NA ZAKA MISIKITINI (SUALA AMBALO NI LA HIARI NA SI LA KISHERIA HUJIWEKA WAZI) HOW COME THEN WADAIWA (SUALA LA KISHERIA) WAHIFADHIWE?NI SIMPLE LOGIC:KAMA MDAIWA NI ANONYMOUS,ITAPOELEZWA KUWA AMELIPA DENI NA KUENDELEA KUBAKIA ANYNYMOUS BASI LAZIMA KUTAKUWA NA STRONG SUSPICION KAMA DENI HILO LIMELIPWA KWELI.

31 Oct 2008


*Yataka sheria ziachwe zifuate mkondo wake
*Yasubiri uamuzi kuhusu sakata la ufisadi
*Yaguswa na usanii wa kampuni ya Richmond
*Yaahidi Rais Obama au McCain kuja nchini

Na Hassan Abbas


BALOZI wa Marekani nchini, Bw. Mark Green amekuwa mwanadiplomasia wa kwanza nchini kumshauri Rais Jakaya Kikwete kuhusu nini anachopaswa kukifanya saa chache kabla hajaamua hatima ya waliokwapua mabilioni kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). 

Balozi Green aliyesisitiza kuwa mafisadi si watu wa kuachwa hata kama ni vigogo na kutaka sheria zichukue mkondo wake, ameifafanulia Majira jinsi alivyoguswa baada ya kuona kampuni ya kimarekani ya Richmond ilivyohusika katika utata kwenye sekta ya umeme nchini. 

Balozi Green alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili ofisini kwake Dar es Salaam kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Marekani, mtikisiko wa uchumi, hali ya kisiasa nchini na mtazamo wake kuhusu wagombea, maseneta Barack Obama na John McCain. 

EPA na Richmond 

Balozi Green alisema hawezi kujinasibu kuwa Marekani ni Taifa la mfano katika kupambana na rushwa, lakini alisisitiza kuwa katika miaka 232 ya Uhuru wa Taifa hilo, ujenzi wa jamii yenye kuwajibika kwa kufuata utawala wa sheria usiomwogopa mtu ndio msingi. 

"Rais Kikwete anafanya kazi kubwa ya kujenga Taifa. Lakini vita dhidi ya ufisadi inahitaji kutowaacha watu wakatamba. Sheria ichukue mkondo wake hata kama mtu ni mashuhuri kiasi gani. 

"Sisi Marekani tumekuwa na azma ya wazi kuwa kiongozi wa umma akiiba fedha za watu, anachunguzwa na kuchukuliwa hatua. Wamarekani ni wakarimu sana kutoa fedha zao kusaidia watu, lakini ni wakali sana wanapoona inafanyiwa ufisadi. Rais Kikwete akitumia sheria atafanikiwa," alisema Balozi Green na kusisitiza kuwa katika sakata la EPA, waliopoka fedha hizo wanapaswa kuwajibishwa. 

Akifafanua kuhusu hilo, Balozi Green alisema Rais Kikwete alitaja mikakati mizuri alipozungumza bungeni kuhusu namna atakavyowashughulikia mafisadi wa EPA. 

"Rais alitaja mikakati mizuri. Tunasubiri kuona atakavyoitekeleza," alisema. Akizungumza bungeni Agosti 21 mwaka huu, Rais Kikwete aliwapa mafisadi hao hadi Oktoba 30 (jana) wawe wamerejesha fedha hizo, vinginevyo ifikapo Novemba mosi (kesho) wawe wameburutwa kortini. 

Sakata la Richmond, kampuni iliyoshinda zabuni ya kufua umeme wa mamilioni nchini ikijieleza kuwa ilitokea Marekani, ni moja ya matukio yaliyoitikisa Serikali ya Rais Kikwete mwanzoni tu mwa utawala wake. 

Akilizungumzia sakata hilo, Balozi Green alisema Serikali ya Tanzania katika kupambana na rushwa inapaswa kufuata sheria bila kujali mhusika au kampuni husika imetoka nchi gani. 

"Suala la Richmond najua ilikuja ikafanya kazi kupitia kampuni iliyosajiliwa nchini. Lakini bila kujali kampuni hiyo ilitoka wapi, Serikali inapaswa kuchukua sheria haraka inapoona kuna ufisadi," alisema huku akikiri kuwa ukweli kwamba kampuni hiyo ilijieleza kutoka Marekani, ulimsumbua wakati wa sakata hilo, ingawa ubalozi wake hauwajibiki moja kwa moja katika mikataba inayohusu kampuni binafsi. 

Uchaguzi wa Marekani 

Balozi Green alikiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu wa nchi hiyo umekuwa na hamasa kubwa hasa kutokana na ushiriki wa Seneta Obama, Mmarekani mwenmye asili ya Afrika wa kwanza kuteuliwa na chama kikuu kuwania urais. 

"Ni kweli kwamba ushiriki wa Seneta Obama umeibua hamasa miongoni mwa Wamarekani wengi, hilo ni suala lisilo na ubishi. Lakini pia hata uteuzi wa Seneta McCain naye umeibua ushawishi katika baadhi ya nchi. 

"Wakati huku Afrika Obama anaonekana kuwa na ushawishi, McCain naye ni kivutio hasa katika nchi za Mashariki ya Mbali ambako kutokana na historia yake ya kushiriki vita ya Vietnamu na kwa miaka mingi aliyokaa kwenye Kamati ya Mambo ya Nje kwenye Bunge la Seneti, alishiriki masuala mengi yanayohusu eneo hilo," alisema Balozi Green ambaye ni mfuasi wa Republican. 

Alisema, akiwatathmini wagombea hao wawili, anaona kuwa wote kwa sera zao, wana uwezo wa kuisaidia Marekani iwapo mmojawapo ataingia Ikulu. 

"Ukiangalia sera zao, hakuna shaka kwamba wote (McCain na Obama) wana mikakati ya dhati kuisaidia Marekani na historia zao zinaonesha wana uwezo mkubwa," aliongeza. 

Akizungumzia somo ambalo nchi za Afrika zinaweza kujifunza kutokana na kampeni zinazoendelea sasa nchini Marekani, Balozi Green alisema kubwa ni umuhimu wa watu kujadiliana masuala ya kitaifa kwa uwazi na mwishowe kila mwananchi akawa na fursa ya kupiga kura na kumchagua kiongozi anayemtaka. 

"Siwezi kusema kuwa Marekani ina demokrasia ya kuigwa, sote bado tunajifunza kutoka kwa kila mmoja. Lakini kama ilivyoonekana, mijadala ya wazi ni kitu muhimu ili kujadili masuala ya kitaifa na mwishowe kuheshimu uhuru wa kupiga kura. Naamini mkiimarisha hili, Afrika na Tanzania zitafanikiwa," aliongeza. 

Msukusuko wa uchumi na Afrika 

Balozi Green alikiri kuwa uchumi wa Marekani umetikisika, lakini akazitoa wasiwasi nchi za Afrika hususani Tanzania, kuwa kiwango cha misaada ya Marekani hakitaathirika kutokana na hali hiyo. 

"Kwa mfano, miradi ambayo tumekubali kuisaidia Tanzania ilishapitishwa na fungu lake lipo, kwa hiyo haitaathirika, sioni sababu ya Watanzania kuwa na wasiwasi," alisisitiza. 

Pia alisema hofu ya miradi mingi iliyoanzishwa chini ya utawala wa chama cha Republican nayo kubatilishwa, iwapo kitaingia madarakani chama cha Democrat haina msingi, kwani wakati wa upitishaji wa miradi hiyo Wamarekani hukubaliana kwa pamoja bila kujali itikadi ya vyama. 

"Kwa bahati nzuri nilikuwa kwenye Baraza la Wawakilishi, ni mmoja wa wawakilishi waliopigania kupitishwa kwa sheria iliyounda shirika la Millenium Challenge Account, linalotoa misaada mbalimbali kwa Afrika ikiwamo Tanzania. 

"Bahati nzuri wakati wa kujadili masuala haya, wabunge walikuwa wamoja bila kujali itikadi. Kwa hiyo hakuna atakayeweza kuzuia miradi hii, iliamuliwa kwa sauti ya Wamarekani wote," alisema.

Obama au McCain kuja Tanzania 

Akizungumzia ushirikiano mzuri baina ya Tanzania na Marekani, Balozi Green aliisifu kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa zamani wa Marekani, Bw. Bill Clinton, ambaye ujio wake nchini na kazi za taasisi zake, ziliwafanya Wamarekani wengi kuijua au kuwa na nia ya kuijua Tanzania. 

"Hata ujio wa Bush, watu wanaweza kunipongeza kwa kufanikisha kuja kwake, lakini historia nzuri iliyowekwa na Clinton ndiyo iliyowazindua Wamarekani wengi kisha akaja Bush na baadaye mkutano wa Sullivan, lakini pia wadhifa wa Rais Kikwete kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, vimeifanya Tanzania kujulikana zaidi. 

Akizungumzia uwezekano wa ofisi yake kuhakikisha Rais ajaye wa Marekani anafuata nyayo hizo kwa kufika nchini, Balozi Green alisema: 

"Nitafurahi kuona siku moja Rais ajaye wa Marekani awe Seneta McCain au Seneta Obama anaitembelea Tanzania, kuimarisha uhusiano mzuri uliopo. Niko tayari kushughulikia hilo ili afike hapa. 

"Bahati nzuri Seneta McCain nimeshawahi kukutana naye wakati nikiwa kwenye Baraza la Wawakilishi, Obama hatujaweza kukutana kwa sababu wakati huo nikiwa kwenye siasa, yeye alikuwa bado yuko chini, lakini naamini wote watakuwa tayari kuja kuiona nchi hii nzuri," aliahidi. 

Balozi Green kitaaluma ni mwanasheria aliyepata kujaribu kuwania ugavana wa jimbo la Wisconsin kupitia chama cha Republican mwaka juzi akapoteza.

Chanzo:Majira

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.