Showing posts with label POLICE BRUTALITY IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label POLICE BRUTALITY IN TANZANIA. Show all posts

30 Jan 2015

l


Angalia dakika ya 3,14  hadi dakika ya 3,19, baadhi ya waandamanaji wanasema "TUUENI..."
Angalia pia kuanzia dakika ya 3.21 ambapo polisi wanaanza kurusha risasi (sina hakika kama ni risasi za moto au bandia) lakini kitu cha kukiangalia kwa makini ni ukweli kwamba ukiacha watu wachache wanaoonekana kutishwa na milio hiyo ya risasi, idadi kubwa tu ya watu inaonekana kutotishika. Hali hiyo inaendelea hata baada ya 'king'oling'oli' cha polisi kinapooanza kulia na hatimaye polisi kutembeza kipigo cha kinyama.

Licha ya kuumia mno kuona Polisi wakitumia nguvu kubwa katika tukio ambalo lingeweza kabisa kumalizwa kwa amani pasipo haja ya kurusha risasi japo moja au kuwapiga na hatimaye kuwakamata waandamanaji akiwemo Mwenyekiti wa CUF Prof Lipumba, kilichonipa hofu ni jinsi taratibu wananchi wanavyoanza kuota 'usugu' dhidi ya unyanyasaji wa polisi. 

Inapofika mahala wananchi wanaashiria bayana kuwa wapo radhi kuuawa, na kuwaambia polisi waziwazi kuwa TUUENI, basi kwa haki tumeshafika mahala pabaya. Na kama nilivyobainisha hapo juu, na kama inavyoonekana kwenye video hiyo, imefika mahala wananchi wameanza kuzowea sauti za risasi sambamba na mabomu ya machozi.

Hii ina maana gani? Wakati tayari wananchi wameshaonyesha kuzowea unyanyasaji na unyama wa polisi wetu na kuwa tayari kwa lolote lile, yayumkinika kubashiri kuwa kuna siku sio tu wananchi wataweka kando uoga na kuendeleza 'usugu' huo nilioueleza hapo juu bali pia wanaweza kujibi mashambulizi.

Uchambuzi mwepesi ni kwamba wakati polisi hawana njia nyingine zaidi ya hizi wanazotumia kila siku: kutumia nguvu kuvunja maandamano ya amani, wananchi wanapata nguvu mpya kwa kuondoa uoga na kuwaacha polisi wafanye watakalo. Upo uwezekano wa wananchi hao kutoishia hapo tu bali badala ya kuwaachia polisi wawaonee, WANAWEZA KUJIBU MASHAMBULIZI. Na kwa mwenendo ulivyo, hatuko mbali na hali hiyo.

Ni vigumu kubashiri ni lini polisi wetu watathamini haki za binadamu na uhai wa wananchi wasio na hatia. Ni vigumu zaidi kutarajia mabadiliko kutoka kwa mwana-CCM yoyote yule atakayemrithi Kikwete baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.Na ndio maana hujaskia yeyote kati ya waliotangaza nia ya kuwania Urais kupitia CCM akilaani unyama huo wa polisi. Walaani kwanini ilhali wao wana kinga ya kudumu dhidi ya polisi? Japo Rais kutoka chama cha upinzani anaweza kutugeuka, lakini katika mazingira ya kawaida ya kibinadamu angalau yeye naye atakuwa ameshaonja unyama wa polisi wetu na ni rahisi kwake kuchukua hatua kuliko hao wasioguswa na polisi.

Kwako msomaji, nakusihi uiangalie video hii kwa makini zaidi ya hayo niliyotanabaisha hapo juu. Jiulize, kama wanaweza kumfanyia LIPUMBA hivyo, watashindwa kukufanyia wewe, familia yako, nduguzo au jamaa zako? Sikiliza malalamiko ya huyo mwanamama katika dakika ya  6.24 na uyafanyie kazi.

TANZANIA ISIYO NA UNYAMA WA POLISI INAWEZEKANA

2 Aug 2013


HATIMAYE PINDA KUWA WA KWANZA KUBURUZWA MAHAKAMANI ...
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemfungulia mashtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutokana na kauli yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni kwamba wanaokaidi maagizo ya dola wapigwe.

Hatua hiyo ya LHRC imepingwa vikali na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Dk Elieza Feleshi akisema hakuna uhalali wa mashtaka yoyote dhidi ya kiongozi huyo sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo Bisimba alifungua mashtaka hayo katika Mahakama Kuu jana akisema kuwa wanamshtaki Waziri Mkuu kwa maelezo kuwa amekiuka kifungu cha Katiba Ibara 13 (1). Pinda ametajwa kuwa ni mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 24.

Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia alisema jana kwamba, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ya kikatiba iliyofunguliwa na LHRC na Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.

Alisema katika kesi hiyo, kuna jopo la mawakili wasiopungua 20 na kwamba wamepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli hiyo ya Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.

Mjumbe wa Bodi ya LHRC, Wakili Dk Ringo Tenga alisema katika kesi hiyo wameangalia zaidi sheria na hasa haki za msingi za binadamu na kwamba kauli hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inahatarisha haki hizo.

Kauli yenyewe

Wakati wa Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu bungeni, Juni 19, mwaka huu, Waziri Mkuu akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”

Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.

“Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.” Kesi hiyo itakayosikilizwa na majaji watatu, haina uhusiano na kesi nyingine ambazo wajibu maombi hupewa siku 90 kujibu hoja zilizowasilishwa. Kesi hiyo imefunguliwa kwa mujibu wa Katiba Sura ya Tatu.

Akizungumza juzi kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma baada ya kufungwa kwa Warsha ya Wapelelezi na Waendesha Mashtaka wa Serikali ngazi ya mikoa, Dk Feleshi alisema hakuna uhalali wa mashtaka hayo kwa sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

“Hii haikuwa kuchochea apige watu, alichosema ni kupiga wale wasiotaka kutekeleza amri halali na zaidi alisema piga lakini si kupiga na kuua,” alisema.

Mkutano huo uliendeshwa chini ya ulinzi mkali huku kukiwa na udhibiti wa kuvuja siri kwa kiwango cha juu. Pamoja na mambo mengine, ulikuwa ukijadili mbinu za kisasa katika kuendesha kesi pamoja na kujiuliza sababu za Serikali kushindwa katika kesi nyingi.

“Kwa sababu lile neno kupiga ni lazima lipewe maana pana huwezi kumpiga tu mtu hivihivi ambaye hakuvunja sheria lakini nilivyoelewa, ilikuwa ni hivyo, ni sawa na mtu ambaye anamshambulia askari,” alisema Dk Feleshi.

Alisema kuna sheria ya kutumia nguvu pale ambako kuna mkusanyiko usiokuwa wa halali pindi raia wanapokaidi kutawanyika kwa hiari hivyo hakuna shaka kauli ya Waziri Mkuu ililenga hivyo.

Hata hivyo, alisema hajapata taarifa za LHRC kumshtaki Waziri Mkuu kimaandishi na kwamba akizipata atatoa ufafanuzi baada ya kuona lengo la mashtaka.

Msimamo

Akizungumza baada ya kufungua mashtaka hayo, Dk Bisimba alisema Waziri Mkuu anaweza kushtakiwa kwa kuwa alizungumza kwa nafasi yake ya Waziri Mkuu na si mbunge na kusisitiza kwamba hakuna aliye juu ya sheria na kudai kwamba kauli hiyo ni kinyume cha Katiba.

Alisema kuwa kila anayevunja Katiba lazima ashughulikiwe kisheria na kwamba mahali pake ni mahakamani tu. Alisema kwa mujibu wa hati hiyo ya madai, kauli na amri kama hizo zinapotolewa na kiongozi mwenye hadhi kama ya mdaiwa wa kwanza (Waziri Mkuu) huchukuliwa kama sheria inayopaswa kutekelezwa na wakala wa utekelezaji wa sheria kama vile polisi. Wadai hao wanadai kuwa kwa ufahamu wao polisi wanaweza kuchukulia kauli hiyo kama amri halali kutoka kwa mkubwa wao na hivyo kuwapiga na kuwatesa watu wasio na hatia, kinyume cha Katiba.

Pia wanadai wanatambua kuwa Ibara ya 100 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa kinga kwa wabunge na uhuru wa maoni bungeni. Hata hivyo, wanatambua kuwa Ibara ya 100 (2) ya Katiba hiyo inawawajibisha wabunge wote chini ya masharti ya Katiba na kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda inakiuka Ibara ya 12(12).

Hivyo wanaiomba Mahakama hiyo itamke kuwa kauli na amri hiyo aliyoitoa Pinda inavunja Katiba.

Mkurugenzi wa taasisi inayofuatilia Mwenendo wa Bunge (Watch), Marcos Albania alidai kwamba wamegundua kuwa kauli hiyo ya Pinda ni moja kati ya matamko makubwa yanayovunja Katiba.

Alisema mbali na shtaka hilo, kuna la pili dhidi ya Waziri Mkuu Pinda, ambalo hawajalifikisha mahakamani ambalo pia linatokana na kauli hiyo aliyoitoa bungeni kwamba: “Sasa wamechoka.”



12 Sept 2012

Iliwahi kuripotiwa kuwa Mkurugenzi wa Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu, aliipinga Tume iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt Emmanuel Nchimbi kuchunguza mauaji ya mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, marehemu Daudi Mwangosi.Moja ya sababu alizotoa Lissu ni Tume hiyo kuwa chini ya uenyekiti wa Jaji Mstaafu Stephen Ihema,ambaye alimtuhumu kuwa na rekodi ya utendaji kazi yenye walakini.

Katika pitapita yangu mtandaoni, nimekutana na habari inayomhusu Jaji Mstaafu Ihema, ambapo alikuwa mjumbe wa Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu vya Uwindaji wa Kitalii, na sasa kamati hiyo imevunjwa kutokana na kulalamikiwa mno kwa vitendo vya rushwa miongoni mwa wajumbe.

Binafsi nimeguswa sana na habari hii hasa kwa vile inahusu tuhuma za rushwa kwa kamati iliyokuwa inamjumuisha Jaji Mstaafu Ihema.Sasa tukiamini kuwa Jaji Ihema ameshindwa jukumu la ujumbe tu kwenye tume hiyo ya ushauri,kwanini tumwamini kwenye uenyekiti wa kamati ya uchunguzi wa kifo cha marehemu Mwangosi?

Wakati ninawapongeza wanahabari waliojitokeza jana kuifahamisha bayana Serikali ya Rais Jakaya Kikwete  kuwa wanalaani vikali mauaji ya mwanahabari mwenzao yaliyofanywa na jeshi la polisi,ningependa kushauri kuwepo upinzani zaidi dhidi ya Tume hii ambayo kuna kila dalili kwamba itaishia kuwa kiini-macho tu.Awali,hofu yangu kuhusu Tume hiyo ilielemea zaidi Watanzania wameshashuhudia utitiri wa tume ambazo mara nyingi ripoti zake zimeishia kufungiwa maandazi na vitafunwa vingine badala ya kuwekwa hadharani//hatua kuchukuliwa.Wengi wetu tunakumbuka kuhusu tume ya milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto.Hadi leo hakuna kilichoelezwa kuhusu ripoti ya tume hiyo...and life goes on.

Je wewe ni mdau wa habari? Unapenda kuona uchunguzi wa kifo cha marehemu Mwangosi unafanywa independently na watu wasio na harufu ya utendaji kazi wenye walakini?Basi ungana na wanahabari kupiga kelele dhidi ya tume hiyo ya kisanii

11 Sept 2012














Minister for Information, Youth, Culture and Sports, Dr Emmanul Nchimbi, embarrassingly leaving the vicinity after the demonstrating journalists rejected his request to address them

CLICK HERE for more details on how the journalist was killed by the police 





4 Sept 2012



Septemba 2, 2012: Pichani JUU: CCM inafanya mkutano wahadhara huko Bububu, Zanzibar licha ya Serikali "kusitisha shughuli zote za kisiasa ili kupisha sensa ya watu na makazi."

Septemba 2, 2012 Pichani CHINI,mwandishi wa habari wa kituo cha TV cha Channel Ten,Daudi Mwangosi akipata kipigo kutokakwa FFU kwa "kosa" la kufanya coverage ya KIKAO CHA NDANI cha Chadema huko Nyololo,Iringa,ambacho Polisi sio tu walikizuwia kwa SABABU ZILEZILE ZILIZORUHUSU MKUTANO WA HADHARA JIMBONI BUBUBU bali walipiga,kujeruhi wananchi wasio na hatia na HATIMAYE KUMUUA mwandishi Daudi Mwangosi ."



Mheshimiwa Rais, damu za wananchi wasio na hatia wanaouawa na polisi kwa "kosa la kutumia haki zao za kikatiba za freedom of association" hazitapotea bure. Polisi waliua Arusha,lakini hiyo haikuzuwia wanachama na wapenzi wa Chadema kukusanyika Morogoro ambapo polisi waliua tena.Hata hivyo,kifo hicho hakikuwatisha wana-Chadema kukusanyika tawini kwao huko Nyololo ambapo baada ya unyanyasaji wa hali ya juu,polisiwaliua tena.

Hivi Mheshimiwa Rais hujifunzi kitu kutoka kwenye JEURI hii? Labda umesahau kuwa hata tawala dhalimu kabisa za kikomunisti huko Ulaya Mashariki zilijidanganya kuwa ukatili na unyama wavyombo vya dola utazidumisha (tawala hizo) milele,lakini wakati ulipofika zilisambaratika.Na huko Afrika ya Kusini,makaburu walitawala kwa mtutu wa bunduki lakini hawakuweza kuzuwia kuanguka kwa mfumo wa kibaguzi.

Mwanafalsafa Karl Marx aliwahi kuusia kuwa "mnyonge hana cha kupoteza zaidi ya minyororo." Wakati mafisadi wanaishi kwa hofu ya kunyang'anywa walichotupora, wanyonge wasio na uhakika na mloujao wanaishi kwa matumaini tu.Lakini kuishi huko kwa matumaini kunaweza kuwa silaha yenye nguvu kuliko vipigo,risasi na unyama wa FFU.

Watu wameichoka CCM na ni wazi kuwa vitisho na mauaji ya raia yasiyo na hatia hayawezi kushusha chuki hiyo.Sana sana inawaongezea tu sababu ya kukichukia chama hicho. 2015 si mbali.CCM inaweza kung'olewa madarakani.Ni vema,Mheshimiwa Rais,ukaanza kutafakari hatmayako pindi hao wanyonge wanaonyanyaswa sasa wakishika madaraka.

Watanzania wana kila sababu ya kuichukia CCM lakini inaonekana kana kwamba chama hicho kinasaka sababu nzito zaidi.Sijui ni kuishiwa na uwezo wa kuongoza au ndio kimezeeka na kinasaka namna ya kujipeleka kaburini,lakini kilicho wazi ni kuwa kila tone la damu linalomwagika kutokana na unyama wa polisi wetu ni sawa na lita nyingi za petroli kuchochea moto wa mabadiliko.


23 Feb 2012


By Joyce Joliga
The Citizen Correspondent
Songea. Police in Songea allegedly shot dead four civilians yesterday, during a fracas associated with a public demonstration against a reported string of murders over the past four months, that the law enforcement organ is accused of neither curbing nor resolving.In a quick rejoinder, however, Ruvuma Regional Police Commander Michael Kamuhanda put the figure of those who had died at two.  

Several other people were injured when police officers used tear gas and live ammunition to quell angry demonstrators, some of whom had stormed the town’s main police station.The Ruvuma regional hospital chief medical officer, Dr Benedicto Ngaiza, confirmed that the hospital  had received four bodies and about 20 injured persons. 

He said two of the bodies had bullet wounds, and  two of the injured persons had bullet injuries  as well, and were rushed to the theatre for operations. All the bodies were delivered by the police,  he explained, adding that, one of them was that of a motorcyclist who had  accidentally hit a tree while speeding  away from the fracas.
Since November last year, nine people have been murdered in the town – a roughly monthly average of two –  some of whose bodies had been mutilated.

The trend has triggered much panic and anger amongst wananchi, who are in the dark over whether the crime is the work of a serial killer or a gang. Worrisome, too, is that, so  long as  the motives of the murders are not known, anyone was a potential next victim.

Chaos  and confusion reigned in Songea for a couple of hours yesterday, as most of the normal  official, business and social activities came to a standstill, as  much attention was  focused on the drama featuring chanting and stone-throwing demonstrators and law enforces who strived to restrain them.

Government offices,  the regional hospital, shops,  and the main bus stand, were among the  sensitive facilities that were temporarily closed and reopened only after relative calm had been restored.

The closures were  prompted by fears by  many people over  being caught in the cross-fire,  or falling victim to looters and petty thieves, since amongst the presumed demonstrators were  people who wielded crude weapons like iron bars.

Many people scattered in various directions towards safer places away from  the procession route, including crew  and passengers awaiting long distance  bus trips. Guards at the regional hospital closed the gates  of the facility as a precaution, as they couldn’t  establish whether  all the people in the huge crowd  that pleaded to be  allowed in were seeking protective shelter, or whether some  were thugs.

 The procession towards the police station  that started early in the morning, attracted hundreds of people marching on foot as well as motorcyclists in slow motion. The crowd swelled as word spread to various parts of the town and more people joined in.

Reports say that  the police fired live ammunition in the air and lobed teargas canisters into the crowds in a bid to restrain them, but, some amongst them continued pushing relentlessly into the police  station compound.

It was at that juncture that the police fired directly  into the crowd, killing two of the protestors, according to RPC Kamuhanda,  who explained that they had refusing to heed orders aimed at preventing a breach of peace. Mr Kamuhanda said investigations had been launched, but  hinted that initial indications pointed to  superstitious beliefs and politicking as causes of the chaos.

The Ruvuma Regional Commissioner, Mr Said Mwambungu,  expressed  dismay over the incident, and appealed to wananchi to remain calm while the Police was continuing with efforts to track down the  perpetrators  of the murders that had fuelled their anger.

He appealed  to Songea residents to avoid walking alone at night, especially if they didn’t have important engagements  that warranted taking risks.

In the evening, Mr Mwambungu chaired a crisis meeting of the regional peace and security committee, to chart  strategies  for containing the mysterious killings.

SOURCE: The Citizen

12 Nov 2011

Vitanda vilivyokuwa vikitumiwa na wangonjwa katika Zahanati ya Ipinda, iliyopo Mwanjelwa jijini Mbeya vikiwa wazi baada ya wagonjwa kukimbia mara baada ya bomu la machozi lililopingwa na Jeshi la polisi kutua ndani ya Wadi

02. Mgonjwa aliyekuwa akitibiwa Zahanati hapo akiwa amezirai baada ya bomu la machozi lililopingwa na Jeshi la polisi kutua ndani ya Wadi.

03.  Mganga Mkuu wa zahanati ya Ipinda jijini Mbeya Dk. Lute Kibopile ambaye pia ni mmiliki wa zahanati hiyo akionesha Bomu la machozi lililopigwa na Jeshi la polisi na kuingia ndani ya Wadi.

04.  Mganga Mkuu wa zahanati ya Ipinda jijini Mbeya Dk. Lute Kibopile ambaye pia ni mmiliki wa zahanati hiyo akielezea jinsi bomu la machozi lilivyopingwa.

05. Muuguzi akionesha eneo ambalo bomu la machozi lilipotua katika Zahanati ya Ipinda, eneo la Mwanjelwa jijini Mbeya.

06. Mtaalamu wa masuala ya maabara katika Hospitali ya UHAI BAPTIST Dk Ngangele Lisukile akiwa ameshika kigae kilichodondoka mara baada ya bomu la machozi lililopingwa hospitalini hapo majira ya saa 5:30 asubuhi.
 CHANZO:  www.mbeyayetu.blogspot.com
:

26 May 2011

Rais Kikwete na Waziri Mkuu Pinda na wakuu wa vyombo vya dola.Wa kwanza kushoto ni CDF (Mkuu wa Majeshi) Davis Mwamunyange,akifuatiwa na IGP (Mkuu wa Jeshi la Polisi) Mwema na DGIS (Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa) Othman Rashid


Sio siri kwamba Jeshi la Polisi Tanzania lina sifa chafu na yayumkinika kuamini kuwa ni taasisi inayochukiwa sana na walalahoi.Sifa kuu mbili za jeshi hili linaloongozwa na IGP Saidi Mwema ni RUSHWA ILIYOKUBUHU na UBABE WA KUPINDUKIA.

Sifa hizo zinahusiana kwa karibu.Rushwa ya polisi inachangiwa zaidi na kipato duni kisichoendana na wajibu wao (ambao kwa asilimia kubwa hawautekelezi).Kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili,ambao tegemeo kubwa la kuutatua ni kwa kulazimisha rushwa (wakinyimwa hawakawii kumbambikia mtu kesi),askari wa jeshi la polisi wanakuwa na hasira muda wote.Lakini badala ya kuelekeza hasira hizo kwa mwajiri wao-yaani serikali-wao wanaelekeza hasira hizo kwa wananchi wanyonge wasio na watetezi (sambamba na wanasiasa wa vyama vya upinzani hususan Chadema).

Kingine kinacholifanya jeshi la polisi lifanane na Nazi Police wa Hitler ni uhaba wa elimu.Polisi limekuwa kimbilio la vilaza (watu wenye uwezo duni kimasomo) na kwa upande mwingine jeshi hilo limegeuzwa mahala pa vigogo kupeleka watoto wao watukutu.Kimsingi,jeshi hili halina nidhamu isipokuwa kwa vigogo na mafisadi wanaowatunza.

Inafahamika kuwa Rais Jakaya Kikwete na IGP Said Mwema wana mahusiano ya kibinafsi zaid ya hayo ya kiserikali.Na hili ndio tatizo la kuendesha nchi kiushkaji.Kinachompa jeuri kubwa IGP Mwema ni ukweli kwamba moja ya sababu zilizopelekea kupewa wadhifa huo ni ukaribu wake na Kikwete.Kwa maana hiyo anajua wazi kuwa Kikwete hawezi kumtosa hasa kwa vile uteuzi huo ni wa misingi ya nilinde nikulinde.

Lakini Kikwete akae akitambua kuwa moja ya sababu zilizopeleka dikteta Hosni Mubarak kung'olewa madarakani huko Misri ni unyama wa jeshi lake la polisi.Jeshi hilo ndilo lililopelekea vifo vingi wakati wa maandamano ya kudai mageuzi nchini humo.Kama wenzao wa Tanzania,polisi wa Mubarak walikuwa wanafahamu lugha moja tu:UBABE.

Kikwete atambue kuwa kuwaachia wahuni waliovaa yunifomu za polisi wanyanyase wananchi wapendavyo,waue wanachi kila wanapojiskia na waendelee kuwabambikia kesi walalahoi,siku ya siku wananchi hao wataamua liwalo na liwe.Ubabe sio ufumbuzi wa kila kitu.Kulikuwa na tawala ngapi za kibabe zilizoishia kuwa historia?

Kikwete na serikali yake ya CCM hawawezi kukemea uhuni na ukatili wa polisi kwa vile jeshi hilo,kama zilivyo taasisi nyingine za dola,limeendelea kuwa tawi lislo rasmi la chama tawala.Laiti Kikwete angekuwa anathamini haki za binadamu asingeruhusu jeshi hilo litangulize nguvu hata pale panapohitaji diplomasia.Kwanini awakemee ilhali wanawakomoa Chadema na walalahoi wengine?Unadhani Kikwete asingechukua hatua laiti polisi wangelalamikiwa na mafisadi?

Enewei,soma habari zifuatazo zinazohusu jeshi hilo la polisi

Polisi wapambana na raia Dar
Wednesday, 25 May 2011 21:56

Felix Mwagara na Ellen Manyangu
VURUGU kubwa zilizuka usiku wa kuamkia jana katika eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, baada ya maofisa wa Manispaa ya Temeke kuendesha operesheni ya kubomoa vibanda vya wafanyabiashara wadogo kwenye hifadhi ya barabara.

Ilibidi polisi kuingilia kati kuwatawanya wafanyabiashara hao waliokuwa na hasira, wakipinga uharibifu wa mali zao wakidai kuwa mkakati huo umetekelezwa bila wahusika kupewa taarifa.Zaidi ya mabanda 50 ya wafanyabiashara hao yalibololewa katika agizo hilo kwenye eneo lililopo karibu na Feri, ambalo mji wa Kigamboni unakua kwa kasi.

Baadhi ya walioshuhudia vurugu ambazo ziliandamana na vitendo vya uporaji wa mali na fedha, walisema wafanyabiashara wapatao 50, walikamatwa. Hadi jana mchana, kulikuwa na idadi kubwa ya polisi kwenye eneo hilo wakiwazuia wafanyabiashara hao wasifanye fujo huku maofisa wa manispaa wakibeba bidhaa mbalimbali zilizozagaa hapo.

Wafanyabiashara hao walisema kwamba walilazimika kupambana na askari hao ili kunusuru mali zao katika mpango huo uliotekelezwa bila notisi.

"Ilitulazimu kupambana ili kuokoa japo mali kidogo kwani ubomoaji huo umefanyika usiku wa manane pasipo taarifa yoyote. Hatujapewa notisi yoyote ya kuhama katika eneo hili," alisema Rajabu Mohamed.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara katika eneo hilo, Omary Mkwesu alisema tukio hilo ni la kusikitisha kwa sababu wamepoteza mali nyingi.

Alihoji kuwa kama ubomoaji huo ulikua wa haki kwa nini wasingewapa notisi ili walau watoe mali zao katika mabanda hayo?

Alidai kwamba hatua hiyo ni njama za diwani wa eneo hilo: "Zoezi hili limesimamiwa na diwani wetu ambaye amekuwa akitutishia kwa muda mrefu kuwa ipo siku atatubomolea na kwa kuthibitisha hilo, tumemuona akisimamia zoezi hili la ibomoaji hovyo saa nane usiku."

Hata hivyo, Diwani wa eneo hilo, Dotto Msama alikanusha kuhusika na tukio hilo akisema Manispaa ya Temeke ilishatoa notisi zaidi ya sita kuwataka wafanyabiashara hao waondoke katika eneo hilo.

"Jambo hili limenisikitisha hata mimi na sasa hivi naelekea manispaa kuongea na uongozi wake juu ya tukio hili. Ni kweli sikuwa na taarifa za zoezi hili kufanywa leo, tena usiku wa manane, ila notisi zilishatolewa na nakala yake iko kwa mtendaji na mwanasheria wa manispaa.

Polisi kwa upande wake, wamekanusha kuwanyanyasa wananchi hao na kusema walikuwepo kwa ajili ya kulinda usalama hasa baada ya wananchi hao kufunga barabara.

CHANZO: Mwananchi

Na habari ifuatayo ni kuhusu moja ya SIFA KUU MBILI za Jeshi la Polisi,yani RUSHWA (nyingine ni UKATILI)
Polisi, mahakama zazidi kutajwa kwa rushwa 
Wednesday, 25 May 2011 21:54

Minael Msuya

IDARA za POLISI na Mahakama zimetajwa tena kuwa ni taasisi sugu zinazoongoza kwa kudai rushwa nchini.Kituo cha Sheria na Haki za binadamu (LHCR) katika taarifa yake imezitaja idara hizo kwamba ndizo kinara kwa kudai rushwa.
Hivi karibuni, Taasisi ya Kupambana na kuzuia Rushwa Takukuru) nayo ilizitaja idara hizo kwamba ndizo zilizo mstari wa mbele kudai rushwa nchini.

Ripoti ya mwaka 2010 ya LHCR iliyofanywa katika mikoa 26 nchini na kuhoji watu zaidi ya 5,000, ilibainisha kuwa polisi inaongoza kwa asilimia 65.1 huku Mahakama ikifuatia ikiwa na asilimia 56.4. Akisoma ripoti hiyo, Mwanasheria wa LHCR, Pasience Mlowe alisema polisi na mahakama zinaongoza kwa rushwa na matumizi mabaya ya ofisi na kwamba zinashika nafasi ya 10 kwa Afrika Mashariki.

“Utafiti wa LHCR ulibaini kuwa polisi na mahakama ni taasisi sugu zinazoongoza kwa rushwa na zinashika nafasi ya 10 kwa Afrika Mashariki,” alisema Mlowe.

Alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) nayo inafuatia kwa asilimia 37.8 na kwamba inaendelea kushuka kiwango kila siku ikilinganishwa na 2009 ambapo ilikuwa katika nafasi ya tano. “Hali hii inayonyesha ni jinsi gani baadhi ya watu walivyozitelekeza sheria na haki za binadamu, wananchi wengi wanataabika usiku na mchana, lakini hawapati haki zao stahiki, tunaomba marekebisho ya vifungu vya sheria yafanyiwe kazi ili haki ya binadamu iweze kupatikana,”alisema.

Mlowe alisema, matatizo hayo ya taasisi hizo nyeti za serikali yanachangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha uchumi wa nchi na kwamba serikali inatakiwa kusimamia sheria muhimu. Kwa upande wake ,Mtafiti na Mwanasheria wa LHCR, Onesmo Olengurumwa alieleza kuwa, utafiti huo ulibaini kuwa mauaji ya raia wengi yanasababishwa na vyombo vya dola kutokana na wao kujichukulia sheria mikononi.

“Vifo vya watu 52 vilivyotokea mwaka 2010 vilisababishwa na walinzi wa kampuni mbalimbali na polisi kwa kujichukulia sheria mikononi badala ya kutumia sheria inayowaongoza,”alisema Olengurumwa na kuongeza: ”Mfano mzuri ni wananchi wanaoishi kando ya Mgodi wa North Mara kule Tarime wanauawa bila sababu na ukichunguza utakuta sheria za mgodi, walinzi wa kampuni ndio wanaopaswa kulinda eneo lote sasa serikali inaingiliaje huko,”alisema.

Alisema mauaji ya watu yaliyotokana na mgodi huo, serikali haiwezi kujitetea kwa lolote na kwamba utetezi wake ni wakisiasa. Alisema serikali ikisimamia tume ya sheria na haki za binadamu nchi itaweza kuondokana na changamoto za ukiukwaji wa haki hizo zinazoikabili.

CHANZO: Mwananchi

25 May 2011

Askari wa Kikosi cha Kuzuwia Ghasia (FFU) wakiwa tayari kuvunja haki za binadamu nchini Tanzania.Picha hii haihusiani na habari ifuatayo.

Tanzania yetu inaelekea wapi?Tangu lini kupiga picha jeneza imekuwa kosa linalopelekea polisi kukamata waandishi wa habari waliopiga picha majeneza?

Kwa kweli Jeshi la Polisi linafanya kila jitihada kuhakikisha amani na utulivu vinaondoka nchini.Jeshi hilo limekuwa likiendeshwa kibabe pasipo kujali haki za binadamu.Inachukiza kuona polisi wanakurupuka kumkamata mtu yeyote yule wanapojisikia lakini wanakuwa wagumu kuchukua hatua dhidi ya wabaka uchumi wanaotenda uhalifumkubwa kwa taifa kuliko raia wema hao wasio na hatia.

Kadhalika,jeshi hilo limekuwa halina heshima yoyote kwa wanasiasa na wanachama wa vyama vya upinzani ambapo polisi wanawakamata ovyo ovyo.Wito wa tovuti hii ni kwa wanaokamatwa kufungua kesi za madai wanapoachiwa bila kufunguliwa mashtaka.Tkuwaacha wahuni hawa waliokabidhiwa jukumu la usalama kwa raia lakini badala yake wanapelekea adha kwa raia wasio na hatia tutaishia kujilaumu huko mbeleni.Violence begets violence,wananchi watafika mahala wakaamua liwalo  na liwe na hao polisi waonevu hawatakuwa salama.

Ubabe sio ufumbuzi wa matatizo kwani kama tumeshuhudia tawala kadhaa za kibabe zikiondoka madarakani pale wananchi wanapoamua kuwa imetosha,enough is enough.Soma habari ifuatayo na utaelewa ninacholalamikia hapa

Polisi wadaiwa kupora maiti Tarime 
Tuesday, 24 May 2011 22:44

WADAIWA KUVAMIA MOCHWARI USIKU,
WABUNGE CHADEMA WATUPWA RUMANDE
Waandishi Wetu
POLISI Kanda Maalumu ya Tarime, wanadaiwa kuvamia chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime, Mara kuchukua maiti za watu wanne waliouawa katika tukio la uvamizi wa Mgodi wa Nyamongo na kuziweka chini ya ulinzi.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa tukio hilo lilikwenda sambamba na kukamatwa kwa watu 12 wakiwemo wabunge wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Waliokamatwa katika tukio hilo ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Matiko. Wengine ni kada wa Chadema, Waitara Mwita na wakazi wengine sita wa Tarime ambao majina yao hayakupatikana mara moja.

Chanzo kimoja cha habari kilisema jana kwamba watu hao walikamatwa majira ya saa 3:23 juzi usiku baada ya polisi kupiga mabomu ya machozi eneo la chumba cha kuhifadhia maiti kuwatawanya watu waliojitokeza kuzuia polisi kuchukua miili ya marehemu usiku huo.

Taarifa zilisema kuwa mbali na watu hao kukamatwa juzi, jana majira ya saa 4:30 asubuhi waandishi wa habari watatu; Anthony Mayunga (Mwananchi), Beldina Nyakeke (The Citizen) na Anna Mroso (Nipashe), walikamatwa.

Waandishi hao walikamatwa jana na mbunge huyo wa viti maalumu wa Chadema katika Kijiji cha Nyakunguru na kuhojiwa kwa muda katika Kituo cha Polisi Nyamwaga kabla ya kupelekwa kwa Kamanda wa Operesheni Maalumu, Paul Chagonja. Waliachiwa kwa kujidhamini wenyewe saa 9:30 jioni.

Hata hivyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema alipotafutwa kuzungumzia suala hilo simu yake ya mkononi ilipokewa na msaidizi wake ambaye alisema anayeweza kulitolea ufafanuzi ni msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso.

Senso alipotafutwa naye alisema hawezi kulizungumzia akimtupia mpira Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime, Constantine Massawe.

Hata hivyo, Massawe alikanusha madai hayo ya kupora maiti akisema kwamba walipata taarifa kutoka kwa ndugu wa marehemu kwamba kuna baadhi ya watu waliokuwa wakiwazuia kuchukua miili ya ndugu zao.

"Jana baada ya kufanyika uchunguzi kama walivyotaka, miili yote ilikuwa chini ya familia. Sasa uamuzi wa kuzika ulikuwa juu yao, lakini majira ya saa mbili usiku tulipata taarifa kuwa kuna watu wako mochwari wamezuia ndugu wanaotaka kuzika wasichukue miili ya jamaa zao," alisema Kamanda Massawe na kuongeza:

"Tulipofika tulikuta wapo watu wanane, wanne walikuwa ni wakazi wa Singida na wengine wanne wakiwa ni wakazi wa Tarime. Tuliwakamata na kusimamia ulinzi wa ndugu waliotaka kuchukua miili ya jamaa zao wakachukua."

Alisema baada ya miili hiyo kuchukuliwa, polisi ililitoa msaada wa kuwasafirishia ndugu hao hadi majumbani kwao na walikuwa wanaishusha kadri walivyokuwa wameambiwa na ndugu hao.

‘Sasa asubuhi hii (jana), tumeelezwa kuwa kuna kundi la watu wengine lilikuwa likipita nyumba hadi nyumba kuwahamasisha wafiwa kutokubali kuzika maiti za ndugu zao baada ya kufuatilia tuliwakamata na hawa waandishi wakiwa wanapiga picha jeneza," alisema Kamanda Massawe.

Awali, Katibu wa Chadema Tarime Mjini, Paschal Warioba alidai kuwa polisi walipora maiti hizo na kwamba viongozi wa chama chake walikamatwa juzi usiku majira ya saa nne.

"Lissu yuko 'lockup' (rumande) hapa Nyamongo, walikuwa wakifuatilia maiti za watu waliouawa katika vurugu mgodini ili leo (jana) ziende kuzikwa, lakini kabla ya kufanikisha zoezi hilo jana (juzi), polisi walizipora maiti hizo kwa kuwadanganya baadhi ya ndugu kwa kuwapa fedha ili waende kuzizika," alisema.

Warioba alidai kuwa baadhi ya maiti tayari wamezikwa, lakini wengine wameonekana katika maeneo karibu na walipokuwa wakiishi.

Juzi alasiri, maiti hao walifanyiwa uchunguzi wa mwisho tayari kwa ajili ya maandalizi ya mazishi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika jana chini ya uratibu wa Chadema kabla ya vurugu kubwa kuibuka katika chumba cha maiti baada ya polisi kufika na kukuta umati wa watu uliokuwa tayari umekusanyika kuanzia saa 1:30 jioni ili kuchukua miili hiyo kwa ajili ya mazishi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika leo.

Hata hivyo, Chadema kinadai kwamba baadhi ya ndugu wa wafiwa waliona maofisa wa polisi wakinunua majeneza manne na kuyapakia katika gari lao kabla ya kufika hospitali hapo kuchukua miili hiyo.

Kutokana na taarifa hiyo, Lissu, Waitara na makada wengine wa Chadema wakiwa na wananchi wengine waliamua kufika katika eneo la mochwari na muda mfupi baadaye, idadi ya watu iliongezeka kwa lengo la kuzuia Polisi kubeba miili hiyo.

"Wakati tukio hilo hapo mochwari polisi walifika majira ya saa mbili usiku na kukuta timu kubwa ya watu ambao walikuwa wamejitolea kulinda maiti hao wasichukuliwe," alisema mkazi wa Tarime aliyejitambilisha kwa jina la Mwita Nyankaira na kuongeza:

"Walianza (polisi) kupiga mabomu ya machozi kuwatawanya watu na ndipo walipowakamata kina Lissu na wengine. Sisi tulifanikiwa kukimbia."

Alisema baada ya polisi kuwasambaratisha wananchi, walirudi hospitalini hapo na kuchukua maiti hao na kuanza kuwapeleka usiku huohuo kwenye familia za wafiwa.

Habari zimeeleza maiti ya Chawali Bhoke ilipelekwa katika Kijiji cha Bonchugu, wilayani Serengeti na Mwenyekiti wa kijiji hicho, Mwikwabe Makena alisema kulikuwa na vurugu kubwa jana asubuhi kijijini hapo baada ya polisi kuwalazimisha ndugu kupokea mwili huo kwa ajili ya kuuzika.

"Kumekuwa na vurugu kubwa iliyoambatana na polisi kurusha mabomu ya machozi," alisema mwenyekiti huyo.

Maiti nyingine ilipelekwa katika Kijiji cha Nyakunguru, Kata ya Kibasuka. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nyamanche kilichoko kwenye kijiji hicho, Isaack Marara alisema jana saa 12:00 asubuhi, alifuatwa na mkazi wa eneo hilo, Kisabo Ghati na kumweleza kuwa kuna jeneza limewekwa barabarani lakini hawajui kuna nini ndani yake.

"Watu walishtuka sana kwani hawajawahi kuona tukio hilo. Baba mdogo wa marehemu Emmanuel Magige, Ambrose Nyabwanya alidai kuwa saa 6:00 usiku wa juzi, magari mawili ya polisi yalisimama na kushusha jeneza mita 200 kutoka nyumbani kwao kisha magari hayo yakaondoa haraka.”

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Mwanasheria na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabere Marando alisema kitendo cha polisi kuchukua kinguvu miili ya watu hao wanne kwa lengo la kwenda kuizika ni kinyume na walivyokubaliana.

Marando alisema walikubaliana na polisi pamoja na ndugu wa marehemu Jumapili iliyopita kwamba shughuli za mazishi zifanyike leo katika Uwanja wa Sabasaba.

“Chadema siyo kama tumeshikilia kidedea msiba huu. Tunafanya hivi kwa kuwa waliouawa ni makada wa Chadema na hiyo ndiyo siasa."

Ripoti ya uchunguzi wa miili yawekwa hadharani

Uchunguzi wa miili ya maiti wanne waliopigwa risasi na askari polisi katika Mgodi wa African Barrick North Mara uliofanywa na daktari bingwa kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Makatta imebaini kuwa marehemu wote walipigwa risasi maeneo ambayo hayakulenga kujeruhi, bali kuua.

Uchunguzi huo uliochukua saa 4:27 ulianza saa 5.20 asubuhi hadi saa 9.47 alasiri. Upande wa familia za wafiwa ulisimamiwa na Dk Greyson Nyakarungu kutoka Hospitali ya Wilaya ya Tarime na askari wawili. Taarifa hiyo itakabidhiwa kwa hospitali

Dk Nyakarungu alisema Emmanuel Magige mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari namba za PM1/5/2011 (TGH), alipigwa risasi katika nyonga ya kushoto ambako kulikuwa na tundu la duara llilokuwa na upana wa sentimita 0.5 ilipoingilia na sentimita 2.5 ilipotokea.

“Mishipa ya damu iliharibiwa, kibofu cha mkojo, mishipa ya fahamu, mfupa wa nyonga ulisagika, damu ikavia ndani ya tumbo, lakini chini ya mgongo karibu na risasi ilipotokea kulikuwa na tundu linaloonyesha kuwa alichomwa na kitu chenye ncha kali kama singa ya bunduki,” alisema na kuongeza:

“Tumebishana sana kwa hilo wenzangu wakidai huenda aliangukia kitu kikamchoma, ikumbukwe kuwa alipigwa kwa nyuma akikimbia hivyo asingeweza kuanguka chali zaidi ya kifudifudi,” alisema.

Kuhusu Chacha Ngoka mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM 2/5/11 (TGH), uchunguzi ulibaini kuwa alipigwa risasi mgongoni karibu na kiuno na kutokea katikati ya mbavu chini ya titi, tundu la kuingilia likiwa ni sentimita za duara 0.3 na ukubwa wa tundu pa kutokea ikiwa ni sentimita tano.

Mishipa mikubwa ya damu iliharibiwa, ini likasagwasagwa, damu iligandia kwenye mfumo wa upumuaji hali ambayo inadhihirisha kuwa alipumua kwa nguvu, damu ilikwisha mwilini na kuwa alipigiwa risasi kwa mbali.

Alisema marehemu Bhoke mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM/3/5/11(TGH) alipigwa risasi ya kichwani karibu na sikio na kidonda chake pakuingilia ni sentimita za duara 0.2 ,pa kutokea sentimita tano za duara kwenye paji la uso hivyo kuharibu ubongo, fuvu na mifupa yote kubomolewa.

Kuhusu uchunguzi wa Mwikwabe Marwa Mwita mwenye jalada la uchunguzi wa kidaktari PM/4/11 (TGH) alisema alipigwa risasi karibu na nyonga na kuacha tundu la sentimita za duara 3,5 na risasi haikutoka nje na kuharibu mifupa yote ya nyonga, misuli ikawa imeharibiwa na kipande cha risasi kilikutwa katikati ya misuli (PSOAS), damu ikiwa imevia tumboni.

“Kilichoonekana hapo ni kuwa walipigwa risasi kwa mbali tena kwa nyuma maana wote zimeingilia kwa nyuma na maeneo waliyopigwa risasi ni yale ya kuua si kuwapunguza nguvu kama walikuwa wamegoma kusalimu amri,” alisema daktari huyo.

Kuzuiwa kwa maziko ya pamoja

Awali, Chadema kilipanga kuendesha ibada ya maziko katika Uwanja wa Sabasaba leo kuanzia saa 2:00 asubuhi kabla ya kupelekwa katika vijiji vyao kwa ajili ya mazishi ya kifamilia.

Lissu alisema juzi usiku kuwa licha ya kukubaliana na wanafamilia na Kamishina wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja, jeshi la polisi lilibatilisha kibali hicho baadaye.

"Tumekuwa katika maandalizi ya mazishi hayo tangu jana jioni. Hata hivyo, jioni hii tumeletewa barua ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Tarime kututaarifu kwamba haturuhusiwi tena kuwaaga marehemu wetu kama ilivyokubaliwa jana," alieleza Lissu.


Waandishi waeleza walivyokamatwa

Baadhi ya waandishi waliokamatwa katika sakata hilo walieleza kuwa walikuwa kazini kutekeleza majukumu yao.

Mmoja wa waandishi waliokamatwa, alisema baada ya kusikia taarifa juzi usiku juu ya polisi kupiga mabomu na kuchukua miili ya marehemu aliamua kuingia kazini kufuatilia tukio hilo.

“Tulipofika hapo kijijini tulikuta pia kuna mbunge wa viti maalum wa Chadema, sasa wakati tukiwa tunamhoji, polisi wakafika na kutukamata wakieleza kuwa tumekuwa tukichochea ndugu wasizike miili ya marehemu," alisema

Alisema kitendo cha polisi kuwahoji jana kuanzia saa 5:10 asubuhi hadi saa 6:20 mchana kimewafanya washindwe kuwajibika ipasavyo jambo ambalo linapaswa kulaaniwa na wadau wote wa habari.

“Tulihojiwa hapa kwa zaidi ya saa moja na ilipofika saa 6:20 mchana walituambia tusubiri maelekezo kutoka kwa kamanda wa polisi…" alisema.

Mei 16, mwaka huu polisi wilayani Tarime iliwaua kwa kuwapiga risasi watu wanne kati ya zaidi ya watu 1,000 waliovamia mgodi wa Nyamongo wilayani humo kwa lengo la kupora mchanga wa dhahabu.

Tukio hilo lililotokea katika Kijiji cha Matongo, lilizua msuguano baina ya polisi, Chadema na wananchi wa eneo hilo ambao juzi waligoma kuzika miili ya marehemu hao na kukataa rambirambi ya polisi.

Habari hii imeandaliwa na Antony Mayunga, Tarime,
Frederick Katulanda, Mwanza na Fidelis Butahe Dar


CHANZO: Mwananchi

20 May 2011



Mauaji Tarime yalikoroga taifa
• Mbunge Lema apambana na kamishna wa polisi

na Mwandishi wetu

MAUAJI ya watu watano waliouawa na polisi, Tarime mkoani Mara kwa madai walikuwa ni wahalifu waliotaka kuvamia mgodi wa North Mara Barrick sasa ni dhahiri yameikoroga serikali na taifa kwa ujumla.

Jana Jeshi la Polisi pamoja na kutuma timu ya maofisa waandamizi kutoka makao Makuu ya Jeshi hilo, lilishindwa kuwashawishi ndugu wa marehemu hao ambao walikataa kusitisha mgomo kususia miili hiyo hadi serikali itoe tamko la kukomeshwa mauaji hayo na wahusika kuchukuliwa hatua.

Timu ya maofisa waandamizi kutoka makao makuu ya jeshi hilo ikiongozwa na Mkuu wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja walilazimika kuondoka pasipo kufikia muafaka katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya wilaya baada ya mamia ya waombolezaji waliopiga kambi tangu Jumatatu kukataa mapendekezo yao.

Awali Kamishna Chagonja aliwahutubia wananchi hao akiwataka waridhie miili hiyo ifanyiwe uchunguzi na kuchukuliwa kwa ajili ya mazishi yatakayogharamiwa na serikali lakini juhudi zake ziligonga mwamba baada ya ndugu wa marehemu kukataa mapendekezo hayo, kwanza wakitaka taarifa ya serikali kulaani mauaji hayo.

“Sisi tumekuja hapa kushirikiana nanyi kwa lengo la kutafuta ufumbuzi sasa tunawaomba mridhie kufanyika uchunguzi halafu taratibu nyingine za mazishi zifuatwe ambapo pia tumejitolea kama jeshi la polisi kushiriki kwa kutoa msaada wa hali na mali ili tufanikishe zoezi hili, tunaomba mkubali kufanyika uchunguzi na tume huru itaundwa kuchunguza tukio hilo,” alisema Changonja.

Kauli yake hiyo ilipingwa vikali na waombolezaji hao ambao walishikilia kuwa kwa vyovyote vile ilivyotokea hakukuwa na sababu ya kuhalalisha vifo hivyo kwa sababu polisi ndio wahusika na walitumia nguvu nyingi kupita kiasi kukabiliana na raia wasiokuwa na silaha za moto.

Wakiongozwa na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema (CHADEMA) aliyepiga kambi katika eneo hilo, wana ndugu hao walidai ingawa hawakupinga kuendelea na zoezi la mazishi lakini wasiwasi wao ulitokana na uharaka wa jeshi hilo kutaka kupoteza ushahidi kwa kulazimisha kufanyika mazishi.

Lema apambana na kamishna wa polisi

Katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti, mbunge wa Arusha mjini, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, Lema alilazimika kumhoji Kamishna Changoja kwa maswali mazito akitaka kujua uharaka wa Jeshi la Polisi kufanya maziko tena ya watu waliowaita kuwa ni wahalifu.

“Kwa nini mnaharakisha maziko bila kuwepo kwa mtu anayewafanyia postmotem? Wewe unasema umetumwa na serikali umetoka makao makuu kuja kuiwakilisha serikali ni serikali ipi unayoiwakilisha?

“Asubuhi Waziri Kagasheki amesema waliouawa ni wahalifu… umekuja hapa huna mkuu wa mkoa, wilaya wala mbunge unamwakilisha nani kwenye serikali iliyokutuma? Ninatilia mashaka uharaka wa serikali kuwazika watu hawa. Ina maana serikali inazika majambazi? Umeanza lini utaratibu huu?” alihoji Lema.

Alisema polisi na serikali yao kuamua kutoa sh milioni tatu kwa kila marehemu kwa ajili ya maziko haijawahi kutokea.

Akizungumza na gazeti hili Lema alisema; “Wakati namuuliza chagonja anasema nisilete siasa kwenye jambo hilo hivi nani sio mwanasiasa? Huyo waziri aliyesema waliokufa ni wavamizi naye mwanasiasa.

“Kwa niaba ya chama changu tumefanikiwa kushwawishi ndugu wote wa marehemu na wameshawishika tukaondoka kwa pamoja pale chumba cha kuhifadhi maiti tukamuacha Chagonja na polisi wenzake, tumemwambia tunaahirisha maziko haya hadi postmotem itakayosema marehemu waliuawa kwa kupigwa risasi wapi kama ni mguuni au kichwani tujue,” alisema Lema.

Kauli nyingine ya Kagasheki

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamis Kagasheki, amemtuhumu mbunge mmojawapo wa chama fulani cha siasa (hakukitaja) kuhusika katika tukio la kushambuliwa kwa Mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwile (CCM), aliyedai kufika katika eneo la Nyamongo kwa ajili ya kuwafariji ndugu wa marehemu waliouawa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, katika uzinduzi wa sera ya ukimwi eneo la kazi kwa jeshi la polisi nchini, Waziri Kagasheki alisema mbunge wa chama hicho cha siasa alitoka jimboni kwake na kufika kwenye jimbo lingine kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kufanya fujo.

“Suala la Nyamongo sitaki kulizungumzia kwa kina, ila niseme kwamba kuna mbunge mmoja wa chama fulani cha siasa, alisafiri kutoka jimboni kwake na kwenda jimbo hilo kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kufanya fujo….

“Kitendo kama hicho na vingine vinavyowiana kamwe haviwezi kuvumiliwa ndani ya nchi…,” alisema Waziri Kagasheki.

Alipoulizwa ni hatua gani serikali itazichukuliwa dhidi ya mbunge huyo, Waziri alishindwa kuweka wazi.

“Nimeshasema sitaki kulizungumzia kwa kina suala hilo, na kuliweka wazi mbele ya umma….” alimaliza na kuondoka.

Ngeleja naye azungumza

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ameeleza kusikitishwa na vurugu zilizotokea katika mgodi wa dhahabu wa North Mara. Ngeleja alieleza hayo jana alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua tamko la wizara yake kuhusu vurugu hizo mgodini.

“Tumesikitishwa na taarifa hizo pamoja na vifo vilivyotokea tunatoa salamu za pole kwa wafiwa, kwa sasa vyombo vya usalama vinashughulikia hali hiyo,” alisema Waziri Ngeleja baada ya kuzindua bodi ya wakala wa ukaguzi wa madini.

Alisema pamoja na mambo mengine, serikali kupitia wizara yake imekuwa ikifanya juhudi kuhakikisha katika eneo hilo kunakuwa na mahusiano mazuri kati ya wawekezaji na wananchi wa eneo hilo.

Alieleza pamoja na changamoto mbalimbali zilizopo katika eneo hilo tayari serikali na wawekezaji wamebuni mradi wa uchimbaji mdogo wa madini ambao utaanza baadaye mwaka huu ili kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi.

Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 23 wameuawa kwa vipindi tofauti kwenye mgodi huo. Hata Barrick wenyewe wanasema nia yao si kuua raia hivyo hawakubaliani na kitendo kilichofanywa na polisi.

CHANZO: Tanzania Daima

14 Jan 2011



Pichani ni Jeshi La Polisi Tanzania likiwa KAZINI.Hii ilikuwa huko Arusha ambapo WALIUA,na sasa WAMEUA TENA huko Mbeya.

Brandy Nelson, Mbeya na Ramadhan Semtawa

POLISI nchini wameendelea kutumia risasi za moto dhidi ya raia na jana wanadaiwa kuwauwa watu wawili kwa kuwapiga risasi katika vurugu zilizotokea katika wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.

Habari kutoka Mbarali zinasema polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi na risasi za moto kuzima vurugu ambazo chanzo chake ni mabishano baina ya raia na polisi hao.

Vurugu hizo zilizotokea jana majira ya saa nane mchana zinadaiwa kusababishwa na baadhi ya wakazi wa kata ya Ubaruku kuzuia kuingia katika eneo lao lori lenye uzito wa zaidi ya tani kumi.

Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo walisema hatua ya wananchi kuzuia kwa lori hilo inatokana na kuwepo kwa amri ya serikali wilayani Mbarali itayokataza magari yenye uzito mkubwa wa zaidi ya tani kumi kuingia katika kata ya Ubaruku.

Mmoja wa mashuhuda hao alisema lori hilo lilipokuwa likijaribu kuingie katika eneo hilo wananchi walianza kulizuia huku wakimhoji dereva wake sababu za kuvunja amri iliyopo.

“……walipokuwa wakiendelea kuhojiana na dereva, polisi walifika hapo na hapo wananchi wakaanza kuwauliza polisi sababu za kuruhusu gari kuingie katika eneo lao wakati serikali imeishakataza..,” alisema shuhuda huyo na kuongeza:

“ ni kama polisi na wananchi walishindwa kuelewana lugha hapo tukaanza kusikia mabomu ya machozi na risasi…”.

Alisema hatua ya polisi iliwafanya wananchi kutawanyika na wengine kuanza kuyavamia magari yaliyokuwa kwenye kituo cha mafuta likiwemo gari lililosababisha mvutano huo.

Katika tafrani hiyo magari mawili yaliyokuwa kwenye kituo cha mafuta yalichomwa moto. Magari hayo yanasadikiwa kuwa ni mali ya ndugu wa mwekezaji katika shamba la mpunga la Mbarali.

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Kanali Cosmas Kayombo alipohojiwa alikiri kupata taarifa hizo lakini akadai kwamba yuko mbali na tukio hilo na amedai kuwa amewasiliana na mbunge jimbo la Mbarali Dickson Kulufi afike eneo la Tukio.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi alipohojiwa alisema kuwa analifuatilia tukio na mpaka tunakwenda mitamboni tayari gari nne mbili zikiwa zimebeba askari wa kutuliza ghasia (FFU), moja ikiwa imebeba polisi waliovalia kiraia huku wakiongozwa na king`ora kikipiga kelele zikiwa zinaelekea eneo la tukio.

CHANZO: Mwananchi

6 Jan 2011


10 wauwawa kwenye ghasia mjini Arusha

Dr Wilbroad Slaa naye pia amekamatwa
Watu wasiopungua kumi wameripotiwa kuuwawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mji wa Arusha Tanzania, kwenye makabiliano baina ya Polisi na wafuasi wa chama cha upinzani cha CHADEMA.

Ghasia zilianza baada ya Polisi kumkamata mwenyekiti wa kitaifa wa chama hicho Freeman Mbowe na mbunge wa Arusha mjini Godbless Jonathan Lema, wakiwa wanaelekea kuhutubia mkutano wa kisiasa.

Baadaye polisi pia walimkamata aliyekuwa mgombea wa chama hicho cha CHADEMA kwenye uchaguzi wa Urais uliofanyika mwezi Oktoba Dr Wilbroad Slaa.

Taarifa zinasema biashara kadhaa zilichomwa moto kwenye vurugu hizo.

Kwa mujibu wa waandishi wa habari mjini Arusha, Polisi walikuwa wamewakataza viongozi wa CHADEMA na wafuasi wao kufanya maandamanao kabla ya mkutano wa kisiasa wa Jumatano, lakini mamia ya wafuasi wa chama hicho wakawafuata viongozi hao walipokuwa wanaelekea eneo la mkutano.

Bwana Slaa amenukuliwa akisema maandamano hayo yalikuwa ya kupinga ufisadi katika serikali mpya ya Rais Jakaya Kikwete.

Polisi walifyatua risasi hewani mara kadhaa kutoa tahadhari kwa maelfu ya wafuasi waliokwenda kutaka viongozi wao waachiwe huru, na baadaye wakafyatua gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya.

Walioshuhudia wanasema Polisi waliendelea kufyatua risasi mchana kutwa, huku wafuasi wa CHADEMA wakiendelea kukabiliana na askari Polisi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Arusha.

Kwenye mkutano huo wa kisiasa, Dr Slaa aliwataka Polisi kumwachilia huru Bwana Mbowe na wengine, na pia akamtaka Rais Kikwete kujiuzulu.

Hadi kufikia Jumatano jioni hakuna taarifa iliyokuwa imetolewa na serikali kuhusu mzozo huo.

Kumekuwa na mvutano wa kisiasa nchini Tanzania tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa Urais ambao vyama vya upinzani vinadai ulikuwa na udanganyifu.

Kufuatia uchaguzi huo shinikizo zinaendelea za kutaka Tanzania iwe na katiba mpya tofauti na iliyopo sasa, ambayo hairuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais kupingwa mahakamani yanapotangazwa na tume ya uchaguzi.

CHANZO: BBC Swahili

25 Aug 2010



Well,not really.But a quick look at the above picture showing members of the notorious Tanzania Police Field Force Unit (FFU)  in their anti-riot gear could mislead you into thinking they were bracing themselves for a chemical or biological attack of some sort!

Photo courtesy of Mzee wa Sumo

4 Oct 2009


Polisi waua raia 33 bila ya hatia kati ya 2007-2009

Na Waandishi wetu

MAUAJI ya mkazi wa Segera yaliyotokea katikati ya wiki hii yamefanya idadi ya raia waliouawa na askari wa Jeshi la Polisi bila ya hatia kufikia 33 katika kipindi cha miaka miwili (2007 hadi 2009), kwa mujibu wa takwimu za Mwananchi Jumapili.

Mwananchi huyo, Idd Mtimbasi ambaye ni fundi redio wa Segera, aliuawa wakati wananchi walipofunga barabara itokaye Chalinze kwenda mikoa ya kaskazini wakipinga kuporwa ardhi. Polisi aliyekuwa kwenye gari la fedha la benki ya CRDB alifyatua risasi iliyomuua raia huyo katika harakati za kutawanya wananchi kutoka barabarani.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari nchini, matukio hayo ni pamoja na lile lililotokea mkoani Kilimanjaro ambako watu 14, miongoni mwao wakiwa ni raia wa Kenya, waliuawa na jeshi hilo kwa kwa kupigwa risasi kwa tuhuma za ujambazi.

Watu hao wote waliuawa katika tukio ambalo Jeshi la Polisi lilidai kuwa lilitokana na kurushiana risasi, lakini wananchi waliibuka baadaye na kukanusha taarifa hizo huku wakidai waliouawa hawakuwa majambazi.

Waliouawa katika tukio hilo ni Hannah Kingara, mkazi wa Kiambu, ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Annkan, aliyekutwa na kitambulisho cha kazi namba 6256476, huku wengine wakikutwa na hati za kusafiria za nchi hiyo.

Wengine ni Simon Maina Ndabuki, Moses Kuria Kamau, David Njuguna Mbugua, Peter Maina Waweru, William Muiruri Kamau na Phillipo Irungu Wanjiru, wakazi wa maeneo mbalimbali jijini Nairobi. Wengine ambao pia ni wakazi wa Nairobi ni Rudovick Giceru Kariuki, John Gikonyo Buku, Zacharia Mwangi Kamathiro na Jeremiah Macharia.

Mkoani Dodoma watu nane waliuawa katika matukio mawili tofauti, sita kati yao wakiuawa katika kijiji cha Mloda baada ya kufuatiliwa na polisi. Habari zinasema kuwa polisi waliwafuatilia kwa madai kuwa walikuwa wamepora fedha na vitu mbalimbali kutoka kwa abiria kwenye Barabara ya Dodoma-Mtera.

Polisi iliripoti kuwa watu hao, ambao walikutwa katika kijiji cha Mloda, waliuawa na wananchi wa kijiji hicho, lakini wanakijiji walikanusha kuhusika na tukio hilo, jambo lililozua maswali mengi miongoni mwa wananchi.

Tukio lingine lilitokea wilayani Mpwapwa mkoni Dodoma Aprili mwaka huu wakati watu wawili waliodaiwa kuwa ni majambazi, waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi.

Katika matukio mengine yaliyotokea jijini Dar es Salaam, polisi walituhumiwa kuwaua Zakayo Mwapi ambaye ni mkazi wa Kimara, Rashid Tuga (Gongo la Mboto) na Thomas Mwingira ambaye ni mkazi wa Yombo Bwawani.

Katika tukio la Mei 24 mwaka huu lililotokea eneo la Kimara Stop Over, Zakayo Mwapi, 24, aliyekuwa dereva teksi aliuawa kwa kupigwa risasi na ofisa wa polisi wa kikosi cha askari wa dharura. Kijana huyo alitii amri ya polisi waliovalia kiraia ya kumtaka asimamishe gari, lakini akakataa kushusha vioo, jambo lililomfanya askari huyo amfyatulie risasi na kumuua.

Tukio hilo lilitokea wakati polisi hao wakifuatilia majambazi waliohusika katika matukio mawili ya kupora kwa kutumia silaha katika eneo hilo.

Watu walioshuhudia tukio hilo walisema baada ya mahojiano ya muda mrefu na dereva huyo, walisikia mlio mkubwa ambao ulitumika kuvunja kioo cha gari na baadaye mlio wa bunduki kabla ya polisi hao kuita gari na kuupakia mwili wa kijana huyo.

Jijini Arusha watu watatu waliuawa katika matukio matatu tofauti likiwemo la mfanyabiashara Ramadhani Mussa ambaye aliuawa baada ya kupata mateso makali kutoka kwa polisi hao. Watu wengine ni Shadrack Motika, 22, na Ewald Mtui, 36, ambao waliuawa kwa kupigwa risasi wakidaiwa kuwa ni majambazi.

Tume iliyoundwa na mkuu wa mkoa kuchunguza tukio hilo ilibaini kuwa watu hao waliuawa kimakosa na hawakuwa majambazi.

Matukio mengine ni yale yaliyotokea mkoani Mara ambapo watu watatu waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi Februari 18 na Mei 7. Iranda Matoka, 26, na Abbas Adek, 23, waliuawa kwa kupigwa risasi Mei 7, wakati Jacob Waibina aliuawa kwa risasi Februari 18.

Katika tukio la Mei 7 mwaka huu watu hao waliuawa wakati polisi walipokabiliana na wakazi wa kijiji cha Moharango walioandamana kwenda kituo cha polisi Utegi, wakitaka kuachiwa huru kwa wazee wanne wa mila. 



Wazee hao waliojulikana kwa majina ya Kahanga Mwando, Odila Runyola, Saba Kahanga na Wasaga Mganga, walikamatwa kwa madai ya kutishia kumroga na kumuua mkazi wa kijiji hicho, Joseph Ngondi. 


Kwenye mji wa Tunduma mkoani Mbeya, kulitokea machafuko Juni 28 wakati wananchi walipovamia kituo cha polisi kwa kuwa askari walimuua mfanyabiashara Frank Mwachembe kwa tuhuma za ujambazi.

Baada ya tukio hilo jeshi la polisi liliunda tume ya kuchunguza tukio hilo kabla ya kuukabidhi mwili wa marehemu kwa ndugu zake ambao waliuzika kijijini kwao Imezu mkoani Mbeya.

Tukio lingine ni lile lililotokea Julai 14 ambapo polisi walidaiwa kumkamata na kumpiga Lucas Mwaipopo na kusababisha kifo chake.

Kutokana na tukio hilo wananchi zaidi ya 300 wilayani Kyela walivamia kituo cha polisi kwa lengo la kuwateka askari waliohusika na tukio hilo. Askari watatu na wananchi 15 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na kuhusika kwenye vurugu hizo zilizosababisha watu watatu kulazwa hospitali kwa kujeruhiwa na risasi.


Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba hakutaka kuzungumzia wimbi hilo la mauaji ya raia wasio na hatia na badala yake akamtaka mwandishi aongee na msemaji wa Jeshi la Polisi, Abdallah Msika ambaye aliomba aandikiwe maswali ili aandae majibu.

“Kwa sasa nipo safarini Mbeya ambako tumekuja kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Usalama. Wewe niandikie maswali halafu uniletea ofisini Jumanne na nitayajibu,” alisema Msika.

Katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka rais kuingilia kati suala hilo akidai litapoteza imani kati ya chombo hicho na wananchi.

Alisema ili kuhakikisha suala hilo linakomeshwa, rais anatakiwa aingilie kati na kuhakikisha tume zilizoundwa kuchunguza matukio ya polisi kuua raia wasio na hatia zinawekwa hadharani na wahusika wanachukuliwa hatua.

Alisema vitendo hivyo ambavyo vimeshamiri hapa nchini ni hatari kwa usalama wa taifa kwa kuwa kama vitaachwa viendelee vitawakatisha tamaa wananchi na kuwafanya kufuatilia haki zao wao wenyewe.

Habari hii imeandaliwa na Geofrey Nyang’oro Hussein Kauli na Mussa Mkama.

CHANZO: Mwananchi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.