Showing posts with label CORRUPTION IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label CORRUPTION IN TANZANIA. Show all posts

12 Sept 2012

Iliwahi kuripotiwa kuwa Mkurugenzi wa Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu, aliipinga Tume iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt Emmanuel Nchimbi kuchunguza mauaji ya mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, marehemu Daudi Mwangosi.Moja ya sababu alizotoa Lissu ni Tume hiyo kuwa chini ya uenyekiti wa Jaji Mstaafu Stephen Ihema,ambaye alimtuhumu kuwa na rekodi ya utendaji kazi yenye walakini.

Katika pitapita yangu mtandaoni, nimekutana na habari inayomhusu Jaji Mstaafu Ihema, ambapo alikuwa mjumbe wa Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu vya Uwindaji wa Kitalii, na sasa kamati hiyo imevunjwa kutokana na kulalamikiwa mno kwa vitendo vya rushwa miongoni mwa wajumbe.

Binafsi nimeguswa sana na habari hii hasa kwa vile inahusu tuhuma za rushwa kwa kamati iliyokuwa inamjumuisha Jaji Mstaafu Ihema.Sasa tukiamini kuwa Jaji Ihema ameshindwa jukumu la ujumbe tu kwenye tume hiyo ya ushauri,kwanini tumwamini kwenye uenyekiti wa kamati ya uchunguzi wa kifo cha marehemu Mwangosi?

Wakati ninawapongeza wanahabari waliojitokeza jana kuifahamisha bayana Serikali ya Rais Jakaya Kikwete  kuwa wanalaani vikali mauaji ya mwanahabari mwenzao yaliyofanywa na jeshi la polisi,ningependa kushauri kuwepo upinzani zaidi dhidi ya Tume hii ambayo kuna kila dalili kwamba itaishia kuwa kiini-macho tu.Awali,hofu yangu kuhusu Tume hiyo ilielemea zaidi Watanzania wameshashuhudia utitiri wa tume ambazo mara nyingi ripoti zake zimeishia kufungiwa maandazi na vitafunwa vingine badala ya kuwekwa hadharani//hatua kuchukuliwa.Wengi wetu tunakumbuka kuhusu tume ya milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto.Hadi leo hakuna kilichoelezwa kuhusu ripoti ya tume hiyo...and life goes on.

Je wewe ni mdau wa habari? Unapenda kuona uchunguzi wa kifo cha marehemu Mwangosi unafanywa independently na watu wasio na harufu ya utendaji kazi wenye walakini?Basi ungana na wanahabari kupiga kelele dhidi ya tume hiyo ya kisanii

6 Aug 2010

SERIKALI ya Awamu ya Nne imeendelea kukumbwa na jinamizi la matumizi mabaya ya fedha za umma (ufisadi), baada ya kubainika kuwa imetumia sh trilioni 1.7 kwa kipindi cha mwaka 2008/2009 bila maelezo ya kina.

Uchambuzi huo ni ule uliotolewa na Shirika lisilo la kiserikali la ‘Agenda Participation 2000’ juu ya ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyotolewa hivi karibuni, umethibitisha kuwepo kwa ufisadi mkubwa wa fedha za walipa kodi.

Uchambuzi wa ripoti hiyo ya CAG kwa mwaka 2008/2009, umeonyesha ufisadi wa kutisha serikalini kwa kiasi cha sh trilioni 1.7 uliofanyika ndani ya mwaka huo.

“Jumla ya fedha za serikali ambazo ama zilitumiwa vibaya au wahusika wameshindwa kutoa maelezo ya kuridhisha jinsi fedha hizo zilivyotumiwa inafikia shilingi trilioni 1.7. Kwa kweli fedha hizi ni nyingi sana…”, ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya shirika hilo.

Kiasi hicho kilichofujwa ni sawa na fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya bajeti ya Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi na ile ya Miundombinu katika mwaka huo wa fedha.

Kiasi hicho pia ni sawa na mara mbili ya fedha zilizokuwa zimetengwa mwaka huo kwa ajili ya Wizara ya Afya ambayo ilipata sh bilioni 589 na mara nne ya kiasi kilichokuwa kimetengwa kwa ajili ya Wizara za Kilimo na Maji, ambazo zilitengewa shilingi bilioni 379 na shilingi bilioni 309 katika mwaka wa bajeti wa 2008/2009.

Kwa ujumla, ufisadi huo unahusisha makadirio ya fedha zilizotumiwa vibaya katika eneo la manunuzi yasiyo ya kawaida ya sh bilioni 12.8, masuala ambayo hayakushughulikiwa tangu kaguzi zilizopita sh bilioni 95.7 na misamaha ya kodi ya sh bilioni 752. 3.

Maeneo mengine ni udhaifu katika ulipaji wa mishahara uliofuja sh bilioni 3. 078, masuala yahusuyo malipo ya marupurupu sh milioni 395.8, ukiukwaji katika ununuzi wa magari wa sh bilioni 4. 018, pamoja na kiasi cha sh bilioni 203.2 zilizotumiwa vibaya au kupotea katika serikali za mitaa.

Katika ufisadi huo, Wizara ya Maliasili na Utalii ndiyo imetajwa kama mfano wa kusikitisha wa wizara zilizotumia vibaya fedha za umma.

Sehemu ya ufisadi uliofanyika ndani ya wizara hiyo inahusisha ubadhirifu wa sh milioni 12 zilizolipwa kama mishahara zaidi ya viwango halali vya mishahara ya wafanyakazi na sh milioni 53 zilizolipwa bila kutolewa viambatanisho vya kuhalalisha malipo hayo.

Sh milioni 445 pia zilitumika kulipa wastaafu, marehemu na wafanyakazi walioachishwa kazi, fedha ambazo walengwa hawakujitokeza kulipwa lakini hazikurudishwa hazina.

“Jambo jingine la kusikitisha ni kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii ilishindwa kueleza yalipo mapato ya jumla ya shilingi bilioni 19.6,” ilisema sehemu ya uchambuzi huo wa Agenda Participation ikirejea ripoti ya CAG.

Mbali na wizara hiyo ya Maliasili na Utalii, wizara, idara au taasisi nyingine za umma zilizopata taarifa mbaya za fedha kutoka kwa CAG ni Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Jeshi la Polisi na Ofisi ya Makamu wa Rais.

Nayo Serikali ya Norway imeendelea kudai kurudishiwa sh bilioni 2.6 zilizotumiwa vibaya na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Hata hivyo, katika taarifa ya bajeti ya wizara hiyo ya mwaka huu wa fedha, wizara hiyo ilisema kuwa ingeilipa Serikali ya Norway fedha hizo.

“Taarifa ya CAG pia inaonyesha utendaji usioridhisha katika nyanja ya mikopo iliyokuwa ikisimamiwa na taasisi za serikali kwa ajili ya wajasiriamali wadogo wadogo miongoni mwa wanawake na vijana nchini.

“Kwa mfano jumla ya sh milioni 355 zinazodaiwa kutolewa kwa wajasiriamali wanawake na vijana hazikuonyeshwa jinsi zilivyotumika. Taarifa za fedha kutoka halmashauri 41 hazikupatikana,” ilieleza taarifa hiyo.

Mashirika ya umma na mamlaka kama vile Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Shirika la Bima la Taifa (NIC), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Shirika la Taifa la Umeme (TANESCO), Mamlaka ya Bandari (TPA) na Mfuko wa Hifadhi wa Serikali za Mitaa (LAPF) ni maeneo mengine ya upotevu mkubwa wa fedha.

Kwa mfano, ilithibitishwa kuwa jumla ya sh bilioni 58 zilizokuwa zimetolewa kama mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2006, mpaka sasa hakuna uhakika wa kulipwa kwa fedha hizo ambazo zilitolewa dhamana na serikali.

“Kinachowasikitisha wengi ni kwanini serikali bado inashindwa kuziba mianya ya baadhi ya maofisa wake kuendelea kutafuna fedha za umma,” umehitimisha muhtasari wa wachambuzi wa wanaharakati hao.


5 Aug 2010

SHIRIKA la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limesema rushwa iliyojitokeza katika mchakato wa kura za maoni za CCM, ni hatari kwa mustakabali wa taifa.

Kufuatia hali hiyo shirika hilo limewataka Watanzania hasa vijana, kutokubali kununuliwa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
“Katika vitu vya kushangaza ni jinsi wagombea ubunge na udiwani wa CCM walivyokuwa wakishindana kutoa rushwa ili wachaguliwe na wananchi,” alisema Meneja Mradi wa Kusaidia Uchaguzi wa UNDP, Oskar Lehner.

Lehner alisema hayo jana jijini Dar es Salaam katika kongamano la siku mbili lililowakutanisha zaidi ya vijana 140 kutoka mashirika mbalimbali yasiyokuwa ya kiserikali na wale wa vyuo vikuu.

Kwa mujibu wa Lehner, uuzaji wa shahada za kupigia kura katika uchaguzi, ni sawa na kuuza malengo ya baadaye katika maisha ya watu hivyo ni vyema Watanzania wakafahamu kwamba mustakabali wa maendeleo ya nchi upo katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.

UNDP inatoa kauli hiyo baada ya vyombo mbalimbali vya habari kuripoti rushwa katika mchakato mzima wa kura za maoni za CCM kuwapata wabunge na madiwani watakaogombea katika uchaguzi ujao.

“Angalieni jinsi matendo ya rushwa yalivyoripotiwa katika mchakato wa kampeni na upigaji kura za maoni ya kuchagua mgombea ubunge na udiwani wa CCM," alisema na kuongeza.

“Wananachi na hasa vijana mjihadhari na kujiepusha na rushwa katika uchaguzi, eleweni kuwa, kuuza shahada yako ya kupigia kura, ni sawa na kuuza malengo ya baadaye katika maisha yako,"

“Mafanikio na maendeleo ya baadaye ya nchi, yapo katika mikono yenu hasa katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.”

CHANZO: Mwananchi

29 Jul 2010

TANZANIA imetajwa katika ripoti ya Kipimo cha Hali ya Rushwa Afrika Mashariki (EABI), kuwa na taasisi zinazoongoza kwa rushwa kwa nchi za Afrika Mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mratibu wa sekretarieti ya Jukwaa la Wazi (TRAFO), Kaiza Buberwa, alisema kuwa utafiti huo ulifanywa kwa kushirikisha sampuli 10,469 na watu 3,231 walihojiwa kwa Tanzania.

Alisema kuwa katika utafiti huo uliofanyika chini ya wataalamu wa nchi husika, ulifanyika Febrauari na Machi ambapo nchi za Kenya, Burundi, Tanzania, Rwanda na Uganda zilihusishwa.


. Buberwa alisema taasisi zinazoongoza kwa rushwa katika Afrika Mashariki ni Jeshi la Polisi, Mahakama, Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa, Wakala ya Usajili wa Vifo na Vizazi (RITA), Magereza, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi katika kutoa huduma kwa wananchi, sambamba na ajira.


Alisema kuongoza kwa taasisi hizo ni kutokana na sampuli hiyo ya watu hao, ambao walizitaja taasisi zilizokithiri kwa rushwa wakati wa kupata huduma za kijamii.

Buberwa alisema kwa kuongoza kwa rushwa katika idara nyeti za serikali kwa Afrika Mashariki, Jeshi la Polisi limechukua nafasi ya tano kwa asilimia 65.1 na Mahakama kuwa nafasi ya 10 kwa asilimia 56.4 katika utoaji wa huduma katika misingi ya rushwa.

Aidha, alisema kuwa katika ripoti hiyo haisemi Tanzania hakuna rushwa wala rushwa kidogo, ripoti inasema kwamba ni kwa kuzingatia idadi ya matukio ya vitendo vya rushwa katika idara kadhaa za umma wakati wa kutoa huduma kwa wananchi ikilinganishwa na nchi za Burundi, Kenya, Uganda na Rwanda.

Buberwa alisema kuwa baadhi ya Watanzania asilimia 85.8 wanaamini kuwa hali ya rushwa Tanzania ni mbaya, wakati asilimia 40.6 wanaamini serikali hatimizi wajibu wake katika kuondoa rushwa na kuimarisha utawala bora.

Alisema taasisi nyingine zinazofuata katika rushwa kwa utoaji wa huduma kwa jamii ni Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa (JKT) asilimia 74.2, Wakala ya Usajili wa Vifo na Vizazi (RITA), asilimia 66.2, Magereza asilimia 61.9, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) asilimia 46.8, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi asilimia 47.9.

CHANZO: Tanzania Daima

.

21 Jun 2010

Zaidi ya shilingi bilioni 150 zimefisadiwa kutoka katika Mfuko wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi,na hiyo ni kwa mwaka juzi (2008) pekee. Kiasi hicho kinajumuisha shilingi bilioni 71.2 zilizotengwa katika mwaka wa fedha 2007/8 lakini hazifika mahala zilipokusudiwa.Utafiti unachofuatilia mwenendo wa matumizi ya fedha za umma-PETS (Public Expenditure Tracking Survey)kinaonyesha kuwa takriban shilingi bilioni 47 zinatafunwa kila mwaka kwa udanganyifu wa malipo hewa katika sekta ya elimu.


Ripoti inayoonyesha ufisadi huo,ambayo ni ya kina zaidi kuliko zilizotangulia,ilikabidhiwa kwa serikali tangu mwezi April mwaka jana.

Gazeti la Citizen limepata nakala ya ripoti hiyo ambayo inaonyesha kwa kiasi gani udhibiti hafifu wa mifumo ya fedha za umma unavyochangia kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.

Serikali iliamua kuagiza utafiti huo kwa shule za msingi na sekondari Tanzania Bara ili kubaini kama kutanuka kwa miundombinu ya elimu na kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na shule kunaendana na kuongezeka kwa raslimali zinazotengwa.

Kadhalika,ilitaka kufahamu kama raslimali zinafika kwa watoa huduma,hususan shule, na kwa kiwango gani mipango ya utanuzi imetekelezwa pasipo kuathiri kiwango cha ubora wa elimu kwa kuzingatia kipimo cha matokeo ya wanafunzi.

Taasisi zilizoshirikishwa katika kipimo hicho ni pamoja na Wizara za Elimu na Mafunzo,Fedha na Mipango ya Uchumi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa),Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,na Shirika la Taifa la Takwimu (TBS).Kadhalika,wawakilishi wa vikundi vya kiraia na wahisani walihusishwa.

Kwa majibu wa matokeo ya utafiti huo,wakati kwa miaka kadhaa sasa serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya elimu kutoka shilingi bilioni 701.1 mwaka 2005/6 hadi kufikia shilingi trilioni 1.43 mwaka 2008/9 na shilingi trilioni 2.045 kwa mwaka 2010/11,raslimali kwa elimu ya msingi zimekuwa zikishuka kutoka asilimia 55.8 zilizotengwa miaka mitano iliyopita hadi asilimia 46.6 mwaka juzi.

Fedha kwa ajili ya ujezi wa madarasa,nyumba za walimu,vyoo na miundombinu mingine pia zimekuwa zikishuka kwa kasi.Wakati wastani wa fedha zilizotengwa zilikuwa wastani wa shilingi bilioni 109 katika awamu ya kwanza ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (PEPD)kutoka mwaka 2002 hadi 2006,kiwango hicho katika mwaka wa fedha 2010/11 kimeshuka hadi kufikia shilingi bilioni 14 tu katika awamu ya pili ya PEPD kuanzia mwaka 2007 hadi 2011.

Na athari ni za hapo kwa hapo na za kina.Kwa mujibu wa takwimu,wakati madarasa 10,771 yalijengwa miaka saba iliyopita,idadi hiyo imepungua hadi kufikia 1,263 katika mwaka 2008.Hiyo ni mbali ya ukweli kwamba uwiano kati ya wanafunzi na uwezo wa darasa ulikuwa 1:78 kwa mwaka huo ni takrban maradufu ya uwiano stahili wa darasa moja kwa wanafunzi 40 (1:40)

Pia Utafiti huo ulibaini kuwa wakati shilingi bilioni 544.2 zilitolewa kwa manispaa kama mtaji na misaada ya kawaida kwa sekta ya elimu katika mwaka wa fedha 2008,kiwango halisi kilichopokelewa kilikuwa shilingi bilioni 473 na kuacha pengo la shilingi bilioni 71.2

Kadhalika,utafiti huo unaonyesha kuwa mamlaka 66 kati ya 131 zilizohusishwa katika utafiti huo zilielekeza shilingi bilioni 28.9 kwenye matumizi mengineyo badala ya minajili ya elimu kama ilivyokusudiwa.

Mwaka 2008,serikali iliwapangia vituo walimu wapya 1271 katika maeneo ya vijijini lakini ni asilimia 35 tu (walimu 444) walioripoti maeneo hayo.Lakini,wakati jiji la Dar es Salaam lilipangiwa walimu 182 tu,mamlaka husika ziliajiri walimu 441.

Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la The Citizen



6 Mar 2010


CCM kinara wa rushwa

Yahya Charahani

WAKATI vita dhidi ya ufisadi ikionekana kupoteza mwelekeo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoongoza kwa rushwa nchini, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Matokeo ya utafiti huo, unaojulikana kama 'Mapambano ya Rushwa kwenye Serikali za Mitaa' ambazo unalenga ngazi za vitongoji, vijiji, mitaa na kata', yalitangazwa jana jijini Dar es Salaam na mtafiti kiongozi wa jopo la utafiti, Profesa Suleyman Ngware wa Taasisi ya Taaluma na Maendeleo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IDS).

Watafiti wengine waliokuwapo katika jopo hilo ni pamoja na Peter Tumaini-Mungu, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IDS), Anthony Kiberiti wa Takukuru na Stephen Ndaki wa Takukuru.Kwa mujibu wa utafiti huo, CCM inaongoza katika kujihusisha na vitendo vya rushwa kwenye uchaguzi kwa kuzoa asilimia 49.5, ikifuatiwa na Chadema 7.0, CUF 2.7, NCCR 0.5 na TLP iliyoambulia asilimia 0.5.

Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa CCM, ambayo ilitingishwa na vita dhidi ya ufisadi iliyoendeshwa kijasiri na kikundi cha wabunge kabla ya jitihada hizo kupunguzwa kasi, imetambulika kama chama kilichoamka zaidi katika mapambano na rushwa baada ya kujinyakulia asilimia 45.1, ikifuatiwa na Chadema kilicho na asilimia 16.0 na CUF yenye asilimia 6.8.

Ngware aliwaambia wadau mbalimbali kutoka Tamisemi, baadhi ya wakurugenzi wa miji, manispaa na jiji, mameya, wenyeviti wa halmashauri, Tume ya Uchaguzi ya Taifa, wanaharakati, wanasiasa na wanahabari jana kuwa utafiti huo uliofanyika kwa miezi sita, kati ya Mei na Novemba 2009, ulihusisha katika 41 zilizo kwenye wilaya 11 zilizo ndani ya mikoa saba.

Alisema kuwa jumla ya watu 380 walihojiwa (233 wakiwa wanaume na 167 wanawake) kutoka kada mbalimbali za jamii, wakiwamo wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, maafisa wa Tamisemi, makamanda wa Takukuru, mameya na wenyeviti wa halmashauri za wilaya.

Wengine ni wakurugenzi wa halmashauri, viongozi wa dini, wanasheria, madiwani, viongozi wa vyama, wabunge, wanaharakati, wakuu wa shule na wananchi wa kawaida.

Alitaja mikoa hiyo kuwa ni Arusha, Dar es Salaam, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, Dodoma, na Tanga.

"Utafiti huu tumeufanya katika ngazi ya chini kabisa, ambayo ni pamoja na kata, vijiji na wilaya. Umewajumuisha watu wa rika zote ambao tulikuwa tukiwauliza maswali mbalimbali kuhusu rushwa," alisema Profesa Ngware.

"Lengo la utafiti huu ni kuweka msingi wa majadiliano baina ya wananchi na serikali kwa sababu njia hii pekee ndio inaweza kuleta majadiliano na siku zote majadiliano ni mwanzo wa kutatua matatizo."

Kwa mujibu wa Profesa Ngware, wananchi wanatambua uwapo wa Takukuru na mapambano yake dhidi ya rushwa kwa asilimia 79.5, ikifuatiwa na polisi asilimia 31.1, Tume ya Uchaguzi asilimia 18.6, Mamlaka za mikoa na manispaa asilimia 12.4 na waangalizi wa uchaguzi asilimia 7.5, lakini hawaridhiki na ufanisi wao katika mapambano na rushwa.

Alifafanua kuwa lengo kuu la utafiti huo lilikuwa kujifunza hali ya rushwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2009. Kiwango cha tatizo hilo, mbinu zitumiwazo kutenda kosa hilo, wahusika wakuu, mitazamo ya wananchi kuhusu suala la uongozi na rushwa na mbinu na mikakati inayofaa kutekelezwa kupambana na janga hilo.

Kuhusu swali lililouliza kama uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2004 ulikuwa huru na wa haki, asilimia ya jumla ilionyesha 63 kuwa ulikuwa huru na wa haki huku asilimia nyingine 24.7 zilizosalia zikionyesha kuwa haukuwa huru wala wa hali na asilimia nyingine 11.8 hazikujibiwa.

Hata hivyo kwa mkoa mmoja mmoja, Tanga imeongoza kwa asilimia za kukubali kuwa ulikuwa huru na wa haki kwa asilimia 79.2, Manyara (74.3), Morogoro (73.1), Kilimanjaro (72.4), Dodoma (56.0), Arusha (51.4) na Dar es Salaam ikishika nafasi ya mwisho kwa kupata sifuri.

Kwenye utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na viongozi wa serikali za mitaa katika uchaguzi wa mwaka 2004 maoni ya wananchi kutoka ngazi mbalimbali yalionyesha kuwa asilimia 67.5 hazikutekelezwa na asilimia 32.5 ndiyo waliokubali kuwa ahadi hizo zilitekelezeka.

"Utafiti huu unaonyesha wazi kuwa rushwa bado ipo na imeanzia katika ngazi za chini kabisa. Kutokana na ukweli huo moja ya mapendekezo yetu ni kuitaka serikali kuanzisha kitengo maalumu cha kupambana na rushwa wakati wa uchaguzi," alisema.

Pia alipendekeza kuongezwa nguvu zaidi kwa mapambano ya rushwa na si kutegemea Takukuru peke yao kwani utafiti umeonyesha kuwa uwapo wa sheria pekee siyo suluhisho la mapambano dhidi ya rushwa.

Pia alitaka kuwapo kwa kamati maalumu za vijiji kwa ajili ya kupambana na rushwa na kwamba watu wengi walioulizwa walisema kuwa chanzo cha rushwa ni kutotekelezwa kwa sheria zilizopo.

Alisema kuwa asilimia kubwa ya watu waliokuwa wakiulizwa chanzo cha rushwa katika maeneo yao walieleza kuwa inachangiwa zaidi na ubinafsi na ulafi.

Alisisitiza kuwa moja ya umuhimu wa utafiti huo ni kuwafanya wadau mbalimbali nchini na nje ya nchi kujua nini kinafanyika mara baada ya kutoa misaada kwa ajili ya maendeleo ya sekta mbalimbali.

Alieleza kuwa asilimia 37.6 ya watu waliohojiwa walionyesha kujua maana ya rushwa wakiihusisha na fedha, ngono au chochote kinachowanywa kwa malengo binafsi huku asilimia 24.8 wakiitambua kama utoaji wa vitu vyovyote visivyokuwa halali.

Akizungumza wakati akifungua warsha ya utangazaji wa matokeo ya uchaguzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea alisema wamefanya utafiti huo ili kubaini nini vyanzo vya rushwa na mbinu zitumiwazo kutenda kosa hilo ili iweze kuwasaidia wadau mbalimbali wakiwamo serikali, vyama vya siasa na hata Takukuru kukabiliana nayo.

Pia alisema utafiti huo umefanyika kwa lengo la kuondokana na kufanya kazi kwa hisia na kuondokana na utamaduni wa kulaumu bila ya kuwapo taarifa sahihi ambazo mara nyingi hutokana na utafiti.

CHANZO: Mwananchi

16 Jun 2009

Miongoni mwa nukuu muhimu kuhusisna na Mwenyekiti Mao wa China ni hii: usiseme kitu kama hujakitafiti (tafsiri yangu isiyo rasmi kwenye usemi no research,no right to speak).Sasa sijui tumweleweje huyu Sekulu MUSTAFA MKULO anapodai kwamba kuna baadhi ya taasisi za dini zimekuwa zikitumia vibaya misamaha ya kodi,lakini hakuweza kutaja angalau jina la taasisi moja.Hizi ni dalili za ubabaishaji na uoga.Uoga huo wa kutaja hadharani watumishi wa Mungu wanaotuhumiwa kuvunja sheria unasababishwa na mtoa tuhuma kutokuwa mkamilifu.Ni mithili ya mama anayechelea kutaja madhambi ya bintie kwa kuwa naye yumo katika mchezo huohuo.



Kama kuna wachunga kondoo wa Bwana walikuwa wakitumia misamaha ya kodi vibaya lakini hawakuchukuliwa hatua,inamaanisha chombo kinachoitwa Mamlaka ya Mapato kiko kwenye usingizi wa pono.Kwanini wahusika hawakuchukuliwa hatua?Au kulikuwa na utatu usio mtakatifu wa vigogo serikalini,wafadhili ughaubuni na watumishi wa Mungu?

Hata kama tukiafikiana na maelezo za Mheshimiwa Mkulo kuhusu hako kamchezo kasikopendeza ,ni dhahiri kwamba vitendo vya watenda dhambi hao wachache havimaanishi kuwa dhehebu lote analotoka mtenda dhambi nalo lina makosa.Kuwepo kwa viongozi kadhaa wa dini ambao wamekuwa wakitumia vibaya misamaha ya kodi hakumaanishi kwamba mantiki nzima ya mpango huo imepoteza maana.


Na lini utaratibu huu wa "akikosea mmoja basi wamekosea wote" ulianza?Mbona hapo Benki Kuu palipozaliwa ufisadi wa EPA na nduguye wa Maghorofa Pacha bado wahusika wameendelea "kupeta"?Kama Ballali ndio kinara cha wizi huo,kwanini basi wasaidizi wake (ikiwa ni pamoja na huyu gavana wa sasa) wameachwa kuendelea na kazi?Je Liyumba anapotuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za Maghorofa Pacha,kwanini basi menejimenti yote ya Benki Kuu nayo isipandishwe kizimbani kwa vile,kwamujibu wa Mkulo,akikosea mmoja basi wamekosea wote!Mbona Mattaka kalikoroga ATCL kapelekwa NIC,Peter Noni anahusishwa na EPA kapewa ulaji TIB,Mzee wa Vijisenti na mabilioni yake visiwani Jersey bado yuko kwenye kamati ya maadili ya chama tawala!

Kwa madhambi haya,dnio maana hutosikia yeyote akidiriki kutaja jina la kiongozi wa dini anayetuhumiwa kufuja misamaha ya kodi (kama yupo).Mtu asiye msafi hawezi kuonyesha uchafu wa mwenzie.

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.

1 Jun 2009


NIMEMALIZA KUSOMA RIWAYA YA KWANZA YA MATUKIO YA KWELI (NON-FICTION) KWA MTUNZI MAHIRI WA RIWAYA ULIMWENGUNI,JOHN GRISHAM.BINAFSI,GRISHAM NA SIDNEY SHELDON NDIO WALIOJAZA KIJIMAKTABA CHANGU CHA VITABU MBALIMBALI.NILIANZA KUSOMA RIWAYA ZA LUGHA YA KIINGEREZA NILIPOKUWA SHULE YA MSINGI,NA SHUKRANI ZIMWENDEE BABA MZEE CHAHALI KWA KUTUSIMULIA WANAWE YALIYOMO KWENYE RIWAYA YA JAMES HADLEY CHASE YA COME EASY GO EASY,KISHA NIKAJITUTUMUA KUISOMA MWENYEWE NA KUFANIKIWA KUELEWA.TANGU MUDA HUO,MIE NA NOVELS TUMEKUWA DAM DAM.KWA UJUMLA MIONGONI MWA INTERESTS ZANGU NI PAMOJA NA KUSOMA VITABU PAMOJA NA UANDISHI BUNIFU (CREATIVE WRITING).

RIWAYA HIYO YA GRISHAM INAITWA THE INNOCENT MAN.PASIPO KUINGIA KWA UNDANI ZAIDI,INAHUSU SHERIA INAPOKWENDA MRAMA.MWAKA 1982 YALITOKEA MAUAJI YA BINTI AITWAYE DEBRA CARTER KATIKA MJI MDOGO WA ADA,PONTOTOC COUNTY JIMBONI OKLAHOMA POLISI WAKASUASUA KUMPATA MUUAJI,"KESI IKABAMBIKWA" KWA RON WILLIAMSON (MHUSIKA MKUU KATIKA STORI HIYO) AMBAYE KIMSINGI ALIKUWA NA MATATIZO YA AKILI,HALI AMBAYO ILIPELEKEA "AKIRI KUWA MUUAJI" LAKINI KATIKA SIMULIZI YA NDOTO ALIYOOTA USIKU MMOJA.RAFIKI YAKE WA KARIBU,DENNIS FRITZ NAE AKAFANYWA MTUHUMIWA NAMBARI MBILI,KWA VILE TU "RAMLI YA POLISI" (KAMA HIYO ILIYOPIGWA KWENYE
AJALI YA MWAKYEMBE) ILIONYESHA KUWA ISINGEKUWA RAHISI KWA MAUAJI HUSIKA KUFANYWA NA MTU MMOJA.HATIMAYE,RON ALIHUKUMIWA KIFO NA KUPELEKWA DEATH ROW NA DENIIS ALIHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA.KUSALIMIKA KWA "WAUAJI HAO" NI TEKNOLOJIA YA D.N.A AMBAYO ILIONYESHA KUWA HAWAKUHUSIKA NA MAUAJI HAYO.

SI LENGO LANGU KUWASIMULIA SIMULIZI KUTOKA KWENYE RIWAYA BALI THE INNOCENT MAN IMENIFANYA NIJIULIZE KUHUSU HUKUMU YA KWENDA JELA MIAKA 11 ALIYOPEWA ALIYEKUWA HAKIMU WA MAHAKAMA YA WILAYA YA TEMEKE,
JAMILA NZOTA.MWANAMAMA HUYO ALIKUTWA NA HATIA YA KOSA LA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA YA SHILINGI LAKI 7 (AWALI ALIDAI MLUNGULA WA SHS MILIONI 4).

HAKI IMETENDEKA.LAKINI KWA UPANDE FLANI INAWEZEKANA HAKI HAIJAONEKANA KUTENDEKA,SI KWA HAKIMU NZOTA BALI WALE ALIOWAHI KUWAHUKUMU WAKATI WA UTAWALA WAKE.HIVI HAKUNA UWEZEKANA KWAMBA TUKIO LILOPELEKEA HAKIMU HUYO KUKAMATWA NA MLOLONGO WA MATUKIO KADHAA KATIKA MAISHA YA UHAKIMU WA JAMILA?MAANA WASWAHILI WANAPOSEMA ZA MWIZI NI 40 WANAMAANISHA PIA KUWA MWIZI ANAENDELEA NA WIZI WAKE HADI ITAPOJIRI HIYO 40

KATIKA MANTIKI HIYOHIYO,KUKAMATWA KWA HAKIMU HUYO KULIKUWA NI SAWA NA 40 YA "WIZI" WAKE,LAKINI PIA KULIASHIRIA MWISHO WA SHUGHULI ILIYOANZA AT A CERTAIN POINT OF TIME.MIMI NA WEWE HATUJUI NI LINI LAKINI YAYUMKINIKA KUAMINI KUWA KUNA HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA HAKIMU HUYO AMBAZO ZILIKUWA INFLUENCED NA "MCHEZO" WAKE WA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA.HAPA KUNA MAWILI:KUNA WALITOA RUSHWA ILI WASIKUTWE NA HATIA KATIKA HUKUMU ZA HAKIMU NZOTA,NA KUNA WALIOHUKUMIWA KWENDA JELA LICHA YA KUWA HAWANA HATIA LAKINI WALISHINDWA KUTOA RUSHWA KWA HAKIMU HUYO.

SISHANGAI KWANINI HABARI YA KIFUNGO CHA HAKIMU HUYO IMESHASAHAULIKA.NDIO TANZANIA YETU HIYO.LICHA YA AMANI NA TULIVU,TUNASIFIKA PIA KWA USAHALIFU HATA KATIKA MAMBO YANAYOWEZA KUWA NA MADHARA MAKUBWA MBELENI.TUNGETARAJI VIKUNDI VYA UTETEZI WA HAKI ZA BINADAMU AU TAASISI ZA KISHERIA ZISHIKILIE BANGO KUHUSU MAPITIO (REVIEWS) YA HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA HAKIMU HUYO.LAKINI KATIKA UTAMADUNI WA LAISSEZ FAIRE,NDIO "IMETOKA HIYO" KAMA WASEMAVYO WATOTO WA MJINI (ILA SINA HAKIKA KAMA MSEMO HUU BADO UNATUMIKA AS KISWAHILI KINAKUA KWA KASI YA TSUNAMI).

NI UTAMADUNI HUU WA "BORA LIENDE" UNAOIMARISHA UNYONGE WA WATANZANIA NA KUDUMISHA ULAFI WA MAFISADI KATIKA KILA NYANJA.NI UTAMADUNI HUU TUTAKAOUSHUHUDIA TENA MWAKA KESHO WAKATI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI AMBAPO WABABAISHAJI WALEWALE WALIOAHIDI BAKULI ZA MAZIWA NA ASALI HAPO 2005 (LAKINI WAKAISHIA KUTUMWAGIA UJI WA MWAROBAINI NA SHUBIRI) WATAKUJA TENA NA AHADI ZILEZILE,ILA ZIKINOGESHWA NA UONGO KUWA TUMEJIPANGA VYA KUTOSHA.BADALA YA BAKULI ZENYE MAZIWA NA ASILI TUMEAMUA KUWAJENGEA MABWAWA KABISA YATAKAYOKUWA YAKITIRIRIKA MAZIWA NA ASALI 24/7.WATAKAPOULIZWA KWANINI AWALI WALIAHIDI HIVYO NA BADALA YAKE WAKATOA MWAROBAINI NA SHUBIRI,WATAJIBU KISIASA KUWA MCHAKATO WA UTEKELEZAJI ENDELEVU WA BLAH BLAH BLAH NDIO ULIPELEKEA HIVYO LAKINI SASA KILA KITU KIKO TAYARI...TUPENI KURA ZENU ILI MFAIDI UHONDO KWENYE ARDHI YA MAZIWA NA ASALI....NA WATAPEWA.

TUMEROGWA?

17 May 2009

How a deported `EPA mogul` enjoys Dar`s life

His dodgy deals cost the government $100million in 1994, but he is today walking and living freely in Dar es Salaam despite the Parliamentary recommendations that he should be arrested and prosecuted immediately.

The man who in 1994 set up and then stole from the debt buy-back programme that is now known as the External Payment Arrears (EPA) account has been living in the country for the last five years despite being declared a prohibited immigrant.

Vidyadhar G. Chavda, an Indian citizen, first came to Tanzania in 1978 without a penny to his name, according to his own words quoted in a 1994 parliamentary report, but after years of working here as an architect he moved into the finance services industry and orchestrated a number of very lucrative, very shoddy deals.

Chavda approached the government with his idea for the creation of the Debt Conversion Programme (DCP) - which sought to reduce the country’s outstanding debts by selling them off to third parties at discounted prices - the deal that cost the country Sh50bn/- ($100m at that time prevailing exchange rate) in taxpayer money from the programme.

“I came to this country without a single penny, a beggar…but I came with a brain worth millions of dollars supported by education and exposure,” Chavda said after the news of his multibillion-shilling scandal broke in 1994.

“The DCP funds were brought totally by my idea and efforts,” he said at the time. “What I have done is beyond the sphere of understanding Parliament…it is a purely financial issue which nobody is capable of grasping.”

To repair the economic damage caused by his sleazy deals, the Central Bank of Tanzania (BoT) was forced to print billions of shillings in 1994.

After his scandal was thoroughly investigated by the Parliamentary Committee chaired by Edward Oyombe Ayila, Chavda was finally deported in 1996, though he was not charged with any wrongdoing.

Despite being deported, Chavda had already caused a strong political rift within the ruling party, and then-minister for home affairs Augustine Mrema resigned because he disagreed with the way the scandal was handled.

In its recommendations, the Parliamentary Committee advised Chavda’s immediate arrest and prosecution for fraud, violation of the Foreign Exchange Act of 1992 and giving false statements contrary to section 122, 309 and 346 of the country’s penal code.

The Committee further recommended that legal action be taken against all traders and lawyers who conspired with Chavda for economic sabotage, and it urged the concerned authorities to cancel the business licenses for those who collaborated with him, including Subhash Patel.

Surprisingly only one recommendation was implemented - to revoke Chavda’s residence permit and deport him - essentially letting him and his partner off the hook.

He is now back in Tanzania where he has been living in the Masaki suburb of Dar es Salaam for the last five years, according to reliable details obtained by The Guardian on Sunday this week.

How he played the game
Having managed to shake the Parliamentary Committee that was formed to investigate him, Chavda carefully planned his comeback in 1997 just three years after he was deported.

On March 18, 1997, Chavda, acting through his lawyers Mkono & Company, asked the High Court of Tanzania to issue a Witness Summons to allow him to testify on August 5 of that year in a pending civil case brought by his wife against him, Civil Case No 130 of 1993.

His wife, an Indian citizen who had continued living in Tanzania legally after Chavda was deported, was suing him over a family financial dispute.

On April 1, 1997, the High Court wrote to the Director of Immigration seeking clarification on the legal position of Chavda’s status once he arrived in the country to testify.

As such, the Director of Immigration informed Mkono & Company on September 25, 1997, that Chavda had been given a visa for 30 days to allow him to enter the country only to testify in court.

Later findings from the court show, however, that during that 30-day period, the civil case was not scheduled for a hearing and Chavda’s claims that he needed to appear in court lacked grounds. His visa expired and he left the country, but with the intention to come back yet again.

Having identified a loophole in the system that could be exploited, Chavda planned a comeback in January 2002 centred on another ‘necessary’ appearance in court.

Chavda again had his lawyers - this time from the firm Gomba & Tadayo - write to the High Court requesting a Witness Summons to testify in Civil Case No 74 of 1996, a separate civil case filed by the National Bank of Commerce against him for an alleged 800m/- in outstanding loan repayments.

He was again allowed to enter the country after being given Entry Visa No 0000695 dated March 4, 2002. Chavda should have left within 28 days of the visa’s issuance, but he had stayed almost a year until the Director of Immigration caught on and ordered him to leave the country immediately.

According to details in our possession, Chavda then filed Miscellaneous Civil Case No 60 of 2003 asking the court to force the immigration department to grant him a visa so that he could testify in the two civil cases facing him.

On March 11, 2004, the High Court issued its ruling in Chavda’s favour, ordering the Director of Immigration to issue a two-year visa to the deportee.

One senior immigration official in Dar es Salaam told The Guardian on Sunday this week that the decision to grant Chavda the visa was both illogical and indefensible.

“The law is very clear; he should be outside the country and is only allowed to come once needed or summoned by the court,” said the official, who asked for anonymity on the grounds that he is not the department’s official spokesperson.

“A hearing can’t take two years, it is just one or a few weeks as long as the pending cases are civil cases.”

Chavda’s two-year visa expired in April 2006, but again neither of the two cases had been heard, and not even preliminary hearings had been held for either of them.

Following of the expiry of his visa, the office of the Attorney General wrote a letter on May 6, 2006, directing the Director of Immigration to act accordingly.

“Since the ruling date was March 11, 2004 then the time for stay in Tanzania has elapsed, and given the fact that Chavda didn’t appeal against the decision, now act according to the law on this issue,” reads part of the letter signed by D.L Chidowu on behalf of the AG.

Despite the AG’s letter, the immigration department has still not taken any action against Chavda.

In a May 25, 2007, letter to Professor Abdullah Safari of Safari Law Chambers - Chavda’s newest lawyer - the AG’s office wrote that it seemed the ministry of home affairs had flipped its position on the matter and was complicit in allowing Chavda to remain in the country.

“The issue of Chavda has taxed much this office. We as advocates of the government and chief legal advisers did our best to defend the position of the government in court to declare Chavda a prohibited immigrant…however it is now clear that the parent ministry [home affairs] has changed its previous position,” reads part of the letter signed by P. J Ngwembe on behalf of the AG.

When asked on Friday why Chavda was still being allowed to remain in Tanzania, Minister for Home Affairs Lawrence Masha was deliberately vague.

“It’s the government that has decided that he should stay in the country because he is still needed,” Masha told The Guardian on Sunday.

The minister would not elaborate on why Chavda was ‘needed’ in the country when he was no longer involved in any currently pending civil cases.

The minister’s response is a curious departure from what his boss, Prime Minister Mizengo Pinda, told Parliament on April 30 this year, in response to a question asked by Kigoma North MP Zitto Kabwe.

The Prime Minister said he wasn’t aware whether Chavda was still in the country, but he promised to thoroughly investigate on which grounds the Asian tycoon was allowed to stay in Tanzania if he were.

The senior immigration official said this ‘confusion’ among top-ranking government officials speaks to the deliberate obfuscation and questionable protection surrounding Chavda and his status in the country.

“This is a man who was supposed to be arrested and charged with criminal offences but surprisingly he is today a free man enjoying the protection of some government officials and a group of Asian traders,” the senior immigration official said.

SOURCE:
Guardian on Sunday

17 Apr 2009


A total of US$30 million (over 36bn/-) given to Tanzania as aid by the Norwegian government in the past 12 years may have been squandered through corruption and mismanagement, an independent report has revealed.

The just-released Anti-corruption Resource Centre Report entitled `Does Aid work?`, which considers the challenges to aid effectiveness in major natural resources programmes, says half of the US$60 million did not make it to the primary targets and ended up lost.

The report is authored by Erik Jansen, a senior advisor at NORAD Evaluation Department.

A former programme officer at the Norwegian Embassy in Tanzania quotes in the report an evaluation by independent consultants in 2006 as having established these facts.

``Those who have control over the natural resources are in a powerful position and usually have easy access to money... Tanzania has not been successful in managing its natural resources in a sustainable and equitable manner, nor has the country been able to achieve significant economic growth in its utilisation of these resources,`` notes the report.

Norway financed the Management of Natural Resources Programme (MNRP) in Tanzania from 1994 to 2006 and the report names the Natural Resources and Tourism ministry as being in charge of managing the forestry, fisheries and wildlife resources.

``The Ministry had three separate divisions, each dealing with one of these resources. MNRP had projects in the forestry, fisheries, and wildlife sectors that were closely connected to these three divisions of the Ministry. In all of the three sectors there has been pervasive corruption during the last decades. Management and staff in the Ministry, together with politicians and people from the local population, have plundered the resources and exploited the resources in a way that is not sustainable. Often this has been in collaboration with foreign investors,`` writes Jansen.

The example is given of assistance from the Kuwait Fund for Arab Economic Development, the OPEC Fund for International Development, and the Saudi Fund for Development, which resulted in one of the largest bridges in Africa. It was built over the Rufiji River in 2003.

``The bridge led straight into a natural forest of about 20,000 square kilometres that had remained fairly unexploited until then. A comprehensive study conducted after the completion of the bridge showed extensive illegal exploitation of the forest,`` says the report.

It adds: ``Logs worth tens of million of US dollars were exported illegally to China and other countries in Asia. Taxes and royalties were paid for only four per cent of the forests that were harvested.``

According to the study, illegal logging cost Tanzania about US$ 52 million of its potential revenue annually.

The reports further notes that corrupt politicians and representatives of the fisheries and wildlife sectors allowed these resources to be plundered by national and international companies, provided they themselves obtained a share of the resultant profit.

``Both in the fisheries and wildlife sectors, licences are allocated to investors at a price that is only a fraction of the market price. Corrupt representatives of the Government earn huge amounts of money that should have gone into the Treasury,`` the report states.

``The development partners in Dar es Salaam recently notified the Government that the fees which the Government received from the wildlife sector were minimal. The Government only charged US$ 8,000 for hunting blocks that had a much higher market value.

``The Government accepted the complaint by the development partners and increased the fees to US$ 40,000 for each block. However, many of the politicians and ministers who controlled these hunting blocks complained that the increased fees would lower their profit and therefore demanded that fees should remain at the old levels,`` it adds.

Some 150 trawlers from EU member countries and the Far East operating within Tanzania`s Exclusive Economic Zone in the Indian Ocean are said to have been paying a paltry US$18,000 annually to obtain a licence. But on a good day of fishing, the trawlers are able to catch fish of the same value.

The report says that, if the Government had charged market value for these licences, the Treasury could have collected US$20 million annually for the trawlers` licences.

``It is also well known that the export of Nile perch from Lake Victoria has been underreported for many years in order to avoid taxation. There is much money to be earned by government officials and politicians who contribute to increased export of natural resources without it being taxed,`` it adds.

The Natural Resources and Tourism ministry is viewed as being in a special position in the government set-up because of its opportunity to generate its own resources from taxes, fees and royalties. It also receives allocations from the Treasury.

``It is difficult to estimate how much money the Ministry transfers to the Treasury and how much disappears due to corruption. With all the potential income from natural resources, the Government of Tanzania should have been able to manage its own natural resources without depending on funds from development partners,`` notes the report further.

A report from the World Bank enforces this view, saying: ``Because of policy failures, Tanzania’s natural resource endowments are not harnessed in an optimal way to achieve both economic growth and poverty reduction. On the contrary, owing to weak governance regimes in revenue-generating sectors, resources are offered below market price to the benefit of a few powerful winners and the loss of the majority of the rural population.``

It adds: ``Yet these natural resources provide substantive potential for income to communities in the rural areas. The weakness in governance regimes in forestry, wildlife and fisheries include primarily the lack of transparency and accountability in issuing rights to extract resources and accrue revenues from them, inequitable sharing of benefits with communities, and monitoring and surveillance of stocks.

``In all four principal sectors providing natural capital in the growth equation – forestry, wildlife, fisheries, and mining – royalties are set arbitrarily and do not reflect scarcity. Royalties are hence not used as a policy instrument of intertemporal resource pricing and sustained yield management (Pfliegner 2008).``

The World Bank report stresses that the problem is not lack of legal acts and instruments, policies, strategies and plans that explains the mismanagement and corruption in the natural resources sector but lack of the political will to follow up on the adopted instruments.

``The Government of Tanzania has a complicated relationship to its task of managing the natural resources. On the one hand the government has, with the support of its development partners, spent much time and resources in developing legal acts, policies, strategies, national plans, and sector strategies for its forestry, fisheries, and wildlife resources which are compatible with those of the international community.

No doubt many government officials in Tanzania do their utmost to comply with and follow up these adopted plans and strategies.`

``On the other hand, there are also many government officials and politicians who undermine the policies they themselves have been central in having Parliament adopt.

Many of these politicians and government officials have held high positions in the Ministry. These leaders can force honest government officials to adopt corrupt practices,`` it adds.

Published as part of the project named `Corruption in Natural Resource Management`, the paper suggests a more sophisticated approach to budget and programme support.

``If we are to improve and understand the relationships between a plan and the reality, it is important that we are open and share experiences made in development aid.

It is therefore a good thing that the political leadership in the Ministry of Foreign Affairs and Norad welcomes a broader and more open debate on development aid,`` writes Jansen.

Renewable natural resources in Tanzania play an important role both for the population in rural areas of the country and for the economy as a whole.

Of Tanzania`s total population of about 40 million people, 75 per cent live in rural areas.

Most of the rural population has access to forestry, fish and/or wildlife resources.

It is estimated that on average 40 per cent of the income in rural households comes from one of these three natural resources.

Agriculture is the main economic sector in the rural areas but most people living off the land use simple technology and land productivity is very low.

Efforts to improve the agricultural sector are slow and income and food from forests, fisheries and wildlife will for many years continue to play an important role for the rural population.

Natural resources are important at the national level too. Timber from the forests is important for economic activities in the country and it is also a major source of foreign exchange.

The country also receives substantial foreign exchange from the export of Nile perch from Lake Victoria and shellfish from the coastal areas. Wildlife brings income from tourism and hunting licences.

Traditionally, local people have used their own rules of management for the various natural resources they have found of interest. But this has changed during the last few decades.

A new set of actors, very often foreign investors, have discovered the value of Tanzania`s natural resources and stiff competition for scarce natural resources has changed the constellation among the actors.

SOURCE: Ippmedia

29 Mar 2009

SHAHIDI katika kesi ya kuomba na kupokea rushwa ya sh 600,000 inayomkabili Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mbelekese, wilayani Iramba, Singida, Iddi Mughenyi, juzi alipata kipigo kutoka kwa mwanasheria wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwenye viwanja vya Mahakama ya Wilaya ya Iramba, kwa madai kuwa alimgeuka katika ushahidi alioutoa mahakamani hapo.

Mtuhumiwa alipata kipigo kutoka kwa mwanasheria huyo aliyetambulika kwa jina moja la Mchumi, kwa madai kwamba alimgeuka katika ushahidi aliuotoa mahakamani hapo.

Tukio hilo la aina yake limedaiwa kutokea muda mfupi baada ya Mughenyi kutoa ushahidi katika kesi namba 14/2009 inayomkabili ofisa mtendaji huyo.

Akizungumza kwa njia za simu kutoka Iramba, mmoja wa watumishi wa mahakama hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina, alisema kuwa kuna kila dalili kuwa ushahidi uliotolewa na shahidi huyo haukumridhisha mwanasheria Mchumi, kwa madai kwamba ulikuwa kinyume cha walivyokubaliana.

“Idd Mughenyi ni shahidi wa upande wa TAKUKURU kwenye kesi hiyo ambayo Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mbelekese anatuhumiwa kuomba na kupokea rushwa, lakini juzi aliposimama kizimbani aliikana taasisi hiyo, kitendo ambacho kinawezekana kilimuudhi mwanasheria huyo ambaye ndiye alikuwa mwendesha mashtaka katika kesi hiyo,” alifafanua mtumishi huyo wa mahakama.

Aidha, mtumishi huyo alisema baada ya kesi hiyo kuahirishwa na kutoka nje ya mahakama, ndipo Mchumi alipomweka chini ya ulinzi shahidi huyo na kumtaka apande kwenye gari ili waende ofisi za TAKUKURU Wilaya ya Iramba.

Alisema kutokana na shahidi huyo kugoma kupanda gari kwa madai ya kutofahamu kosa, ndipo mwanasheria huyo alipoanza kumpiga makofi hadi kumuumiza kwenye jicho la upande wa kushoto na kumchania shati.

Alibainisha tukio hilo lilishuhudiwa na baadhi ya mahakimu, na kuongeza kuwa waliwaamru askari kwenda kuamua ugomvi huo, kisha kuwapeleka kituo cha polisi.


RUSHWA NI RUSHWA,IWE NDOGO AU KUBWA.LAKINI INGEPENDEZA ZAIDI KUONA TAKUKURU IKITUMIA MISULI MINGI KWENYE RUSHWA KUBWA NA UFISADI SAMBAMBA NA HIZO RUSHWA NDOGO.MAPAPA WA KAGODA NA RICHMOND (achana na yule Mdosi aliyepandishwa kizimbani) BADO WANAPETA URAIANI SAMBAMBA NA MAFISADI WA RADA.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.