Showing posts with label EPA. Show all posts
Showing posts with label EPA. Show all posts

6 Mar 2014

Wakati haijafahamika nani aliyelipwa mabilioni ya shilingi yaliyokuwa kwenye akaunti ya Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kutokana na mvutano baina ya Tanesco na Kampuni ya IPTL, imebainika kuwa Bunge liliwahi kuagiza fedha hizo zisichukuliwe mpaka mitambo ya IPTL itakapokuwa chini ya Tanesco mwakani.
Hiyo imo katika taarifa ya iliyokuwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2007.
Hata hivyo, Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alithibitisha jana kuchotwa kwa Dola za Marekani 122 Milioni (Sh195.2 bilioni) katika akaunti hiyo, lakini akakataa kutaja nani hasa aliyelipwa.
Mkataba wa miaka 20 baina ya IPTL na Tanesco ulisainiwa mwaka 1995 na ulitakiwa kuisha 2015 na mitambo hiyo kuwa mali ya Tanesco.
Hata hivyo, ukiwa umebaki mwaka mmoja kumalizika, imebainika kuwa mitambo hiyo imeuzwa kwa Kampuni ya Pan African Power, ambayo inatarajiwa kuingia mkataba mwingine na Tanesco ili iwauzie umeme.
Ndulu alisema fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo ni Dola za Marekani 22 milioni na Sh161 bilioni za Tanzania ambazo zote kwa pamoja ndizo zilizofikisha jumla ya Sh195.2 bilioni.
Vyanzo vingine vilitoa takwimu mbili tofauti, kimoja kikisema kiasi cha fedha hizo kilifikia Dola za Marekani 270 milioni na kingine Dola 250 milioni. Kuhusu nani mwenye mamlaka ya kutoa fedha hizo, Profesa Ndulu alisema kwa mujibu wa mkataba wa kufunguliwa kwa akaunti ya fedha hizo, ni Wizara ya Nishati na Madini pamoja na IPTL.
“Hakuna mtu mwingine anayeweza kuidhinisha kutolewa kwa fedha hizo zaidi ya hao, kwa hiyo hao ndiyo waliosaini kutolewa kwa hizo fedha na taratibu zote zilifuatwa,” alisema Profesa Ndulu.
Alipoulizwa ni nani aliyelipwa fedha hizo, Profesa Ndulu alisema IPTL ndiyo iliyokuwa na mamlaka ya kusema ni nani alipwe na ilifanya hivyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alipoulizwa juu ya fedha hizo alisema: “Kwa kawaida huwa nina majibu mafupi sana, lakini kwa kuwa mmeamua kuandika uongo, endeleeni, siwezi kukujibu chochote wasiliana na hao IPTL wakujibu.”
Hata hivyo, haikuwa rahisi kumpata kiongozi wa IPTL kuzungumzia suala hilo kwa kuwa tayari kampuni hiyo ni mufilisi.
Msimamo wa Bunge
Ripoti ya POAC inasema Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) aliorodhesha matatizo ya mkataba kati ya Tanesco na IPTL na kuangalia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mipango ya kununua mitambo hiyo na kuibadilisha iwe inatumia gesi badala ya mafuta mazito.
“Mgogoro uliopo hivi sasa kati ya Tanesco na IPTL unahusu kiwango cha malipo ya uwekezaji yaani capacity charges ambacho IPTL walikuwa wanalipwa na Tanesco. Kwa mujibu wa mkataba huo, capacity charge inapaswa kukokotolewa kwa kuzingatia mtaji wa asilimia 30 na mkopo wa asilimia 22.31.
Baada ya uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa, ilikubalika kuwa mtaji uliowekezwa uwe ni Dola za Marekani 36 milioni.
Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa Tanesco iligundulika kuwa IPTL haikuwekeza fedha hizo, bali Sh50,000,” inasema ripoti hiyo.
Ilisema kuwa, mpaka kufikia Mei 2008, Tanesco ilikuwa imeilipa IPTL Sh221 bilioni tangu ilipoanza uzalishaji umeme Januari 2002.
Kamati iliagiza: “Wanasheria wa Tanesco na Serikali watumie ushahidi wote uliopo kuhakikisha kuwa kiwango cha fedha kilichopo kwenye akaunti maalumu (Escrow) ndicho hichohicho kitumike kumaliza madeni yaliyopo na vilevile kufanyia marekebisho mitambo hiyo ili itumie gesi,” inasema taarifa hiyo.
Pendekezo hilo lilipitishwa na Bunge huku POAC ikitoa maelekezo kwa Gavana Ndulu kuwa fedha zilizopo Escrow zisitumike kwa namna yoyote ile bila mitambo ya IPTL kuwa ya umma na kubadilishwa na kutumia gesi asilia.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa POAC, ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe alisema ameshtushwa na taarifa za kutolewa kwa fedha hizo kinyemela.
“Tunaitaka Serikali kutoa taarifa kama kweli hizo fedha zimetolewa, kwa sasa siwezi kutoa msimamo wetu kwa kuwa hatujakaa kama kamati, tunatarajia kuitisha kikao cha dharura Dodoma kuzungumzia suala hili,” alisema Zitto.
 CHANZO: Mwananchi


12 Dec 2010



Majuzi kulifanyika uzinduzi wa kitabu kinachoelezea wasifu wa Rais Jakaya Kikwete.Tukio hilo linaelekea kuwa na uzito wa kipekee kwani baadhi ya picha zilionyesha sehemu kubwa ya familia ya mkuu huyo wa nchi ilihudhuria uzinduzi huo.Sina hakika kuhusu kilichomo kwenye kitabu hicho lakini yayumkinika kuamini kuwa laiti wasifu huo ungegusia masuala kama "Wanamtandao na mchango wao katika ushindi wa Kikwete 2005",au "Uswahiba kati ya Kikwete,Lowassa na Rostam Aziz na jinsi unavochangia kufilisika kwa Tanzania", au "wasifu wa wateuliwa mbalimbali wa Kikwete na namna wanavyohusiana nae",nk isingekuwa rahisi kwa Rais Kikwete kujitokeza kwenye uzinduzi huo.

Mwandishi wa kitabu hicho ni Profesa Julius Nyang'oro.Wakati mwingine najiuliza kama baadhi ya maprofesa wa aina hii wameishiwa na mada za muhimu kwa jamii na badala yake wanageukia kujikomba kwa watawala kwa kuandika wasifu mithili ya pambio.Unaweza kunilaumu kwa kutoa tuhuma kabla sijasoma kilichomo katika kitabu hicho.Hata hivyo,huhitaji upeo wa juu kubashiri yaliyomo katika kitabu hicho,maana laiti ingekuwa ni wasifu wa Kikwete huyu ambaye utawala wake umetuzalishia msamiati wa "ufisadi",sambamba na kugubikwa na ishu za Kagoda,EPA,Dowans,Richmond na uzururaji njeya nchi,basi si mkulu huyo wala wanafamilia yake wangetia mguu kwenye uzinduzi huo.

Sasa sijui Profesa Nyang'oro kajaza nini kwenye wasifu huo!Mamia ya ahadi za Kikwete na kisha kuichambua moja baada ya nyingine ( kwa mtizamo chanya usiomuudhi mtawala) au ni hadithi za namna Jakaya alivyozaliwa katika familia ya kawaida,akajiendeleza pasipo makeke,akashika hatamu za uongozi lakini akiendelea kuwa "mtu wa watu" na hatimaye akapata urais ( bila kutaja mchango wa wanamtandao) na ameendelea kuwa mwenye upendo na upole sio kwa walalahoi pekee bali hata mafisadi.

Huenda wasifu huo pia ukagusia udaktari wa falsafa (wa heshima) wa Rais Kikwete.Inawezekana atapomaliza miaka yake 10 hapo 2015 (na kama hatafanya mbinu za kutaka aongezewe muda madarakani) ataweka historia nyingine ( on top ya ile ya kumpiku Vasco da Gama kwa safari) ambapo atakuwa kiongozi pekee aliyezawadiwa shahada nyingi za uzamifu kuliko mwingine duniani.Sijui mpaka sasa ana PhD ngapi,ila nakumbuka ile ya Uturuki,nyingine sijui ya Uganda kama sio Kenya,hii ya juzijuzi Dodoma na Muhimbili nao wamemzawadi shahada ya Afya ya Jamii.


Na kwa vile utawala wa Kikwete umetawaliwa na usanii wa namna flani,yayumkinika kuhisi kuwa hizo PhDs zinatolewa baada ya wahusika "kupigwa somo" au "kupewa kilicho chao".Ungeweza kuhisi kuwa ilikuwa hivyo hata Profesa Nyang'oro,lakini "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni" hapo itakuwa mtu tu kaamua kujikomba.

Na kama ilivyozoeleka,wanahabari wetu (pamoja na baadhi ya mabloga) walichokumbuka ni picha za tukio na maelezo ya picha hizo (captions) tu,utadhani kwa kuangalia picha hizo msomaji atapata summary ya jumla ya kilichomo katika kitabu hicho.Hapa "simpigi mtu dongo" ila natoa changamoto kwa wenzetu mliobobea kwenye picha,mkumbuke kuwa picha pekee si habari kamili.Hivyo,inapowezekana mtupatie habari zaidi ya picha husika.Ni ushauri tu,tena wa bure buleshi.

Nakumbuka mwaka 2005 kulikuwa na kitabu cha wasifu wa Kikwete.Nahisi hapa katikati kuna waliojipendekeza na kuja na wasifu mwingine.Sasa tuna wasifu huu "mpya" kutoka kwa Profesa Nyang'oro na huenda hapo 2015 kutakuwa na wasifu mwingine wa "miaka 10 ya mafanikio ya kihistoria chini ya utawala wa Jakaya Kikwete".Mtu mmoja wasifu kibao!

Enewei,hiyo ndio Tanzania yetu.Na ukiwa na kiongozi mpenda sifa basi wajanja hawachelewi kumpamba kwa sifa hii au ile.Na kwa vile hawagusii yale yatakayomfanya mtawala atambue kuwa "hajafunga zipu" basi kwa upande mmoja watoa sifa hao wanapata wanachotegemea kupata (sifa,hela,kupiga picha na rais,kualikwa ikulu,na pengine kuzawadiwa U-DC) na kiongozi mpenda sifa anaendelea kuamini yeye ni chaguo la Mungu ndio maana sifa zinaendelea kumiminika kumhusu yeye.

26 Aug 2010

Rostam Aziz
Katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005,mfanyabiashara controversial Rostam Aziz alitumia raslimali zake nyingi kuhakikisha mgombea wa nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,anashinda kwa gharama yoyote ile.Na kutokana na utajiri mkubwa alionao pamoja na mbinu zake mbalimbali,mchango wake ulimsaidia sana Kikwete kuingia Ikulu,na sasa ni Rais wetu anayeomba tena ridhaa ya kutuongoza kwa miaka mitano ijayo.

Kati ya mwaka 2005 (baada ya Kikwete kuingia Ikulu) na sasa,Rostam ameibuka kuwa kiumbe mwenye nguvu za kutisha sio tu ndani ya CCM bali kwenye siasa za Tanzania kwa ujumla.Lakini kubwa zaidi katika kipindi hicho ni kwa mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi na Kikwete na serikali yake kushindwa kuwaridhisha Watanzania kwamba "hamkumbatii swahiba wake huyo".Haihitaji kurejea namna Rostam alivyohusishwa na ufisadi wa EPA (Kagoda) na ujambazi wa Richmond.
Jakaya Kikwete

Mwaka 2010,yaani mwaka huu,Rostam anaelekea kurejea tena ulingoni japo si kwa wazi sana.Ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuhusika kwa mfanyabiashara huyo katika kampeni za Kikwete.Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Rostam vimekuwa vikiendesha kampeni ya chuki dhidi ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa,mwanasiasa anayeonekana kuwa  tishio kwa mfanyabiashara huyo na vitendo vyake dhidi ya maslahi ya taifa.
Magazeti yanayomilikiwa na Rostam

Na kama hilo la vyombo vya habari vya Rostam kumuandama Dkt Slaa halitoi mwangaza wa kutosha basi taarifa kwamba mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Habari Corporation (inayomilikiwa na Rostam),Muhingo Rweyemamu,anatajwa kuwa mratibu wa kampeni za Kikwete.Itakumbukwa kuwa mwaka 2005,waliokuwa waandishi waandamizi wa Habari Corporation,Salva Rweyemamu na Dokta Gideon Shoo walitumika sana kwenye kampeni hizo.Baada ya kuingia Ikulu,Kikwete "alimzawadia" Salva ukurugenzi wa habari wa Ikulu,nafasi anayoshikilia hadi sasa.
Muhingo Rweyemamu

Kama alivyo Salva,Muhingo anasifika kwa uwezo wake wa hali ya juu wa kujenga hoja.Kwa bahati mbaya au makusudi,uwezo huo pia unatumika ipasavyo kutengeneza fitna.Wengi watakumbuka namna Dokta Salim Ahmed Salim,mmoja wa wana-CCM waliokuwa wanawania kuchuana na Kikwete,alivyoundiwa zengwe kubwa na kumhusisha na kundi la Hizbu la huko Zanzibar.Inaelekea kuwa mbinu hizohizo zimeanza kutumika dhidi ya Dokta Slaa,na kuna kila sababu ya kuamini kuwa kuna mengi yatakayoibuliwa dhidi yake.
Salva Rweyemamu  (kushoto) na Gideon Shoo

Yayumkinika kuamini kuwa waandishi wa habari wanaotumiwa kumchafua Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanafanya hivyo kwa minajili ya "kupeleka mkono kinywani".Kubwa zaidi ni sapoti ya Rostam kwa Kikwete.Wakati mwaka 2005 alijibidiisha ili kufanikisha maslahi yake binafsi ya kibiashara (na amenufaika kweli-kwa kuangalia ishu za Kagoda na Richmond/Dowans) safari hii Rostam anahaha kumzuia Dokta Slaa kwa vile anafahamu fika kwamba laiti mwanasiasa huyo wa Chadema anayesifika kwa msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi akiingia Ikulu,zama za mafisadi kutumia jeuri yao ya fedha "kuendesha serikali kwa remote control" itakuwa imefikia kikomo.

Kwahiyo,Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanapaswa kuelewa kuwa safari hii Rostam ana "special mission" ya kuhakikisha "survival (kusalimika) yake.Atatumia kila raslimali aliyonayo kuhakikisha Dokta Slaa haingii Ikulu.Anafanya hivyo akifahamu wazi kuwa rais yeyote mwenye kujali maslahi ya nchi yake "atamkalia kooni" mfanyabisahara huyo na washirika wake.

Hata hivyo,kwa vile si fedha za Rostam au wanahabari wake zitakazopiga kura kwenye uchaguzi mkuu,bali mimi na wewe pamoja na kila Mtanzania aliyechoshwa kuona nchi yetu ikigeuzwa "shamba la bibi",ni muhimu kwa wapiga kura kusema HAPANA.Tusitoe fursa kwa watu wenye maslahi binafsi kuipeleka nchi yetu kwenye maangamizi.Na ni muhimu zaidi kutambua kuwa baadhi ya watu hao wana utata wa kutosha tu kuhusu asili ya mahali walipozaliwa.Hiyo inamaanisha kuwa "wakishaiingiza Tanzania kwenye mtaro",watakuwa na sehemu ya kukimbilia.

KILA MTANZANIA MWENYE KUITAKIA MEMA NCHI YETU ANAPASWA KUPAMBANA NA WAHUNI WA KISIASA WANAOTAKA KUTUWEKEA MADARAKANI VIONGOZI WANAOWAMUDU NA HIVYO KUENDELEA KUTUFISADI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ILIYOPITA.


INAWEZEKANA,TIMIZA WAJIBU WAKO

14 Jun 2009


Majuzi,Watanzania wametahadharishwa kuhusu athari za mdodoro wa uchumi wa dunia na madhara yake kwa nchi yetu.Kadhalika,bajeti ya mwaka ujao wa fedha imeandaliwa kwa kuzingatia tahadhari hiyo huku kukitangazwa mpango wa kuchochea uchumi (economic stimulus plan).

Hata hivyo,kama nilivyojadili HAPA,uwezekano wa bajeti na stimulus plan hiyo kufanikiwa,sambamba na umuhimu wa tahadhari iliyotolewa,utategemea zaidi hatua kali na za makusudi dhidi ya ufisadi na mafisadi.Yayumkinika kubashiri kwamba pamoja na imani kwamba mipango hiyo inalenga kulinusuru taifa,wanaufaika wakubwa wanweza kuwa mafisadi wanaojua vema namna ya kubuni mikakati ya ulaji huku wakiwa hawana hofu ya kuchukuliwa hatua yoyote kutokana na siasa za kulindana na kishkaji.

Hebu soma kwanza habari ifuatayo,kisha tujadili kidogo mwishoni.

Wingu zito fedha za EPA
• Chegeni: Zimekwenda kusikojulikana

na Mwandishi Wetu

UTATA umegubika mahali zilipo na matumizi ya fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoshiriki katika wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akilihutubia Bunge mjini Dodoma Agosti mwaka jana, alibainisha fedha hizo zilizorejeshwa na baadhi ya kampuni si mali ya serikali lakini zitawekwa kwenye akaunti maalumu kabla ya kupelekwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa ajili ya kufungua dirisha dogo la kuwakopesha wakulima wakati nchi ikielekea katika mchakato wa kuanzisha Benki ya Kilimo.

Ingawa Rais Kikwete na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, kwa nyakati tofauti walieleza kuwapo kwa fedha hizo katika akaunti maalumu, taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema hadi sasa fedha hizo hazijaingia katika Benki ya TIB, licha ya kuwapo kwa taarifa kuwa fedha hizo zimetumika kununulia mbolea iliyotolewa kwa mfumo wa vocha kwa baadhi ya wakulima hapa nchini.

Chanzo kimoja cha habari kilichomo ndani ya TIB kimedai fedha hizo wamekuwa wakizisikia kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari kutoka kwa wanasiasa, ambao wamekuwa wakijinadi kuwa fedha hizo zitatumika kunyanyua kilimo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

Chanzo hicho kilibainisha kuwa hadi sasa dirisha la kilimo lililosemwa bado halijaanza kufanya kazi iliyotarajiwa, ingawa maneno ya watu mbalimbali yamekuwa yakibainisha kuanza kazi kwake ambako kungetarajiwa kuwasaidia wakulima kupata mikopo ya muda mrefu, baada ya kuikosa fursa hiyo kwa kipindi kirefu kutokana na kutokopeshwa na taasisi za fedha za hapa nchini.

“Haya mambo huwa tunayasoma, kuyasikia na kuyaona kwenye hivyo vyombo vyenu vya habari, lakini kwenye makaratasi hali ni tofauti, sasa sijui niseme siasa inatawala au muda bado haujafika,” kilisema chanzo hicho.

Tanzania Daima Jumapili, ilifanya juhudi za kumtafuta Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Peter Noni, ambaye ameteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete, lakini Ofisa Mwanadamizi wa Mambo ya Uhusiano wa benki hiyo,Catherine Magambo, alisema mkurugenzi wake hawezi kutoa ufafanuzi hivi sasa, kwa kuwa ameanza kazi siku si nyingi na ni busara akapewa wiki moja ili aweze kujipanga.

Catherine, alipotakiwa kueleza kama ana taarifa zozote za kutokuwapo kwa fedha zilizoahidiwa na rais kupelekwa katika benki hiyo, alisema anachokifahamu ni kile kilichoelezwa wakati fulani na Mkurugenzi aliyestaafu, William Mlaki, kuwa hawajapokea fedha hizo na kama kungekuwa na mabadiliko vyombo vya habari vingejua kama walivyofanya hapo awali.

“Nyinyi Tanzania Daima Jumapili, habari kama hii unayoniuliza au unayotaka mkurugenzi wangu akujibu, najuakwamba hakuna kitu ambacho kimebadilika lakini kama mnataka habari zaidi msubiri mkurugenzi mpya azoee ofisi kwa muda wa wiki, halafu ndipo uje kumuuliza maswali yako,” alisema Magambo.

Pia alibainisha kuwa hajaona mabadiliko yoyote juu ya ahadi iliyotolewa pia na Rais Kikwete ya kutoa kiasi cha sh bilioni 15 kwa ajili ya kuendeleza benki hiyo ili iweze kutoa mikopo kwa wakulima.

“Jamani maswali yenu mbona yamezidi, si nimewaambia hakuna mabadiliko na hayo maswali yenu msubirini mkuu? Mbona mnanibana kwa mambo nisiyo na uwezo wa kutoa majibu? Kwani kila ofisi ina utaratibu wake,” alisema Magambo.

Wakati fedha hizo zikionekana kugubikwa na utata, baadhi ya watu wamekuwa wakiiona hatua ya serikali kutangaza kurejeshwa kwa fedha hizo ni kiini macho au zimetumika katika matumizi mengine badala ya kupelekwa katika kilimo kama ilivyoahidiwa, kwa kuwa viwanda vingi vya mbolea kwa mwaka huuvimejikuta vikishindwa kujiendesha baada ya kuzalisha bidhaa hiyo na kukosa wanunuaji.

Dhana hiyo inachagizwa na baadhi ya wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia kutokupata mbolea hiyo, licha ya serikali kutangaza kutenga fungula fedha kwa ajili ya kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima ili kukuza kilimo na kuleta mapinduzi ya kijani.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa na wanasiasa mbalimbali wa hapa nchini walikuwa wakihusisha wizi huo wa fedha na mkakati maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwaagiza baadhi ya makada wake na wanachama wakwapue fedha hizo kwa ajili ya matumizi ya kampeni za uchaguzimkuu wa mwaka 2005 uliokiwezesha chama hicho kuibuka na ushindi wa ‘kishindo.’

Hisia hizo zilipata nguvu baada ya kuwapo tetesi kuwa kampuni iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ya Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, inadaiwa kumilikiwa na baadhi ya vigogo wa chama hicho, jambo lililochangia ugumu wa kukamatwa kwa wamiliki wa kampuni hiyo ambayo inaaminika ndiyo iliyosuka mpango wa uchotaji wa fedha hizo.

Tuhuma hizo mara kadhaa zimekuwa zikikanushwa na viongozi waandamizi wa chama hicho, akiwamo Katibu Mkuu wake, YusufMakamba, ambaye aliweka bayana kuwa CCM haijamtuma mwanachama wake afanye wizi huo na kama kuna mwanachama amehusika na wizi huo apewe lawama hizo binafsi na si chama.

Naye Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni, katikati ya wiki alinukuliwa na vyombo vya habari mjini Dodoma akisema kuwa fedha za EPA zinaonekana kwenda sehemu zisizoonekana kirahisi kwa wananchi, ingekuwabusara kama zingetumika katika ujenzi wa barabara ambayo ingepewa jina la EPA, ili kila
mwananchi aweze kuamini kinachosemwa na viongozi wa serikali.

Alisema mazingira ya fedha hizo tangu awali yalionyesha utata, hivyo ingekuwa busara hata matumizi yake yakafanyika bila kuwapo kwa usiri, ili kuondoa fikra potofu kuwa hakuna fedha iliyorejeshwa.

“Hizi fedha za EPA mimi nafikiri zingetumika kujengea barabara na tukaziita barabara za EPA, ili yeyote anayetaka kuzusha lake ashindwe kufanya hivyo au tumuonyeshe vithibitisho,” alisema Chegeni.

Alisema sekta ya kilimo ni pana na hata fedha zinazotumbukizwa huko ni lazima ziandaliwe mipango mizuri na mapema ili ziweze kufikia walengwa na zilete tija inayotakiwa kuliko inavyoonekana sasa ambapo serikali inasema imetoa mbolea ya ruzuku kwa wingi, lakini wakulima wanalalamika kutoipata mbolea hiyo kwa kiwango kinachohitajika.

Wizi wa fedha za EPA ulibainika baada ya Kampuni ya ukaguzi ya kimatifa ya Ernst &Young kubaini wizi wa sh bilioni 133, ambapo baada ya uchunguzi huo, Rais Kikwete aliamua kumfukuza kazi aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Daudi Ballali na kuagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi kwa maofisa wa benki hiyo ili kufikishwa mbele ya vyombo vyasheria.


CHANZO: Tanzania Daima.

Katika mazingira kama haya,itakuwa kosa kweli kuyamkinisha kwamba hiyo stimulus plan inaweza kuishia kutengeneza dili ya kuifanya EPA ionekane "cha mtoto"?

Halafu,habari hiyo hapo juu ina kitu kingine cha ziada,nacho ni kuhusu PETER NONI.Huyu jamaa anahusishwa kwa karibu na skandali la EPA.Awali wasiwasi wangu ulikuwa kwenye kuteuliwa kwake kuwa Mkurugenzi wa TIB.Kilichonifumbua macho katika habari hii ni ukweli kwamba marejesho ya fedha za EPA yalipangwa kupelekwa TIB.You see the connection?NONI anahusishwa na ishu ya EPA kwa wadhifa aliokuwa nao BoT.Sasa anapokwenda TIB ambako tunaambiwa ndiko zitakapopelekwa marejesho ya fedha za EPA ni mithili ya "kula denge" kuelekea lilipo fungu hilo.

Ndio Tanzania yetu hiyo!

24 Mar 2009


NAKUOMBA SOMA HABARI MBILI ZIFUATAZO KISHA TUJADILI DHANA YA KULAZIMISHA UWAJIBIKAJI.KWA KIFUPI,KATIKA HABARI YA KWANZA,PAMOJA NA MAMBO MENGINE,DR SLAA ANAONYESHA KUWA CHADEMA INA USHAHIDI WA KUTOSHA KUIHUSISHA CCM NA WIZI WA EPA.KATIKA HABARI YA PILI,MWANASHERIA TINDU LISSU ANAMTAKA MKUU WA MKOA WA SINGIDA,MHESHIMIWA KONE,AOMBE RADHI HADHARANI KUTOKANA NA MADAI KUWA ALIWATUKANA HADHARANI BAADHI YA WANANCHI ANAOWAONGOZA.MJADALA UTAKAOFUATA BAADA YA HABARI HIZO UNAANGALIA MANTIKI YA DR SLAA NA CHADEMA KUENDELEA KUTUELEZA KWAMBA WANA USHAHIDI WA KUTOSHA UNAOIHUSISHA CCM NA UFISADI WA EPA,LAKINI KIONGOZI HUYO NA CHAMA CHAKE WAMEKUWA KANA KWAMBA WANATINGISHA KIBERITI VILE...KWA MAANA KWAMBA KAMA USHAHIDI UPO,KWANINI WASIFUNGUE KESI MAHAKAMANI KWA NIABA YA WANANCHI BADALA YA KUENDELEA KUDAI USHAHIDI TUNAO,USHAHIDI UPO...IRONICALLY,TINDU LISSU,MWANASHERIA ANAYEWATETEA BAADHI YA WAKAZI WA SINGIDA DHIDI YA MH. KONE,SIO TU NI MWANASHERIA WA CHADEMA BALI PIA NI MIONGONI MWA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO.

ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA

Chama tawala chaambiwa kuacha kutisha wananchi kuhusu ufisadi

Na Mussa Juma, Same.

KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka katibu mwenezi wa CCM, John Chiligati, kuacha vitisho dhidi ya upinzani, akisema kuwa wataendelea kufichua ufisadi uliotanda kwenye chama hicho tawala.

Chiligati alivionya vyama vya upinzani kuwa visitumie ufisadi kama ngazi ya kujipatia umaarufu, huku akionya kuwa kuendelea kuishutumu CCM kunaweza kuhatarisha amani kwa sababu kama watu milioni nne watachukia (akimaanisha wana-CCM), hakutakuwa na amani.

Lakini Dk Slaa, mmoja wa wabunge ambao wamesimama imara katika kufichua na kupiga vita ufisadi, alisema hakuna ubishi kuwa CCM imeingia madarakani kwa kuchotewa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na kama kinapinga, basi kiende mahakamani. Kauli hiyo ilitolewa jana na Dk Slaa wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Hedaru na Makayanya wilayani Same na baadaye kukutana na waandishi wa habari.

Dk Slaa alisema Chadema ina ushahidi wa maandishi jinsi CCM ilivyokuwa inachotewa fedha za EPA kupitia kampuni ya Kagoda, hivyo kama inaona inapakwa matope, inaweza kwenda mahakamani kulalamika na sio kutoa vitisho kupitia vyombo vya habari.

“Tunamshangaa sana Chiligati na tunamuomba aache vitisho. Tunao ushahidi hadi muhtasari wa kikao kilichoongozwa na rais mstaafu kikielezea jinsi walivyokuwa wanajichotea fedha za EPA na pia ujumbe mfupi kutoka kwa katibu mkuu wa CCM kwenda Benki Kuu kuomba fedha hizo. Sasa wanaposema hawahusiki na EPA tunawashangaa,” alisema Dk Slaa.

CHANZO: Mwananchi
HABARI YA PILI :


RC atakiwa kuwaomba radhi wananchi

na Deogratius Temba

MKUU wa Mkoa wa Singida, Vincent Parseko Kone, ametakiwa kuitisha mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kisasida, Wilaya ya Singida na kuomba radhi kwa wanachi na mwenyekiti wa kijiji hicho, kwa kuwatukana hadharani na kuwalipa fidia ya sh milioni moja.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa kijiji hicho, Ramadhani Mwankumbi, kutoa taarifa kuwa anakusudia kumfikisha mkuu huyo wa mkoa mahakamani kutokana na kumtukana hadharani wakati akiwa katika mkutano wa hadhara kijijini hapo.

Kwa mujibu wa barua aliyoandikiwa jana, Mkuu wa mkoa huyo, kutoka kwa Kampuni ya uwakili ya M/S TUNDU A.M. LISSU Advocates, yenye kumbukumbu namba TAML/SDG/RSM/KSSD/09/01, na kusaniwa na wakili wa kujitegemea Tindu Lissu, ilieleza Februari 24, mwaka huu, mkuu huyo wa mkoa alienda katika kijiji hicho na kutumia cheo chake kwa lengo alilodai kuwa ni kukagua mradi wa kilimo cha umwagiliaji. Badala ya kutembelea mradi huo, kama alivyodai, aliomba kumwona Mwenyekiti wa Kijiji Mwankumbi, na kuanza kumfokea mbele ya wanakijiji wenzake, viongozi wa mkoa na wananchi wengine wengi kwa madai kuwa ameshirikiana na mtu mwingine aitwaye, Josephat Isango, kumchafulia jina lake.

“Mteja wetu alipoomba nafasi ya kujieleza juu ya tuhuma ulizokuwa unamrushia ulikataa na badala yake ulianza kumtukana matusi mazito, baada ya kumtukana ukaondoka na kurudi Singida,” ilieleza sehemu ya barua hiyo. Pia barua hiyo ilieleza kisheria maneno hayo, ambayo yalitolewa na mkuu huyo wa mkoa ni kosa na ni kashfa dhidi ya mteja wao, na yamemdhalilisha, kumnyanyasa, kumvunjia heshima aliyokuwa nayo mbele ya wanakijiji waliomchagua na kumpa dhamana.

“Maagizo kutoka kwa mteja wetu ni kukutaka wewe Parseko Kone, utembelee tena Kijiji cha Kisasida na kuitisha mkutano wa hadhara wa wanakijiji wote na uwaombe radhi hadharani kwa maneno ambayo sisi tutakuelekeza.

“Aidha, tunakuagiza ufanye ziara ya mkutano huo wa kuomba radhi ndani ya siku 14, kutokea leo (jana), pia mteja wetu anadai umlipe sh milioni moja kama gharama za ufuatiliaji kwetu,” ilieleza barua hiyo.

Lissu, alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa, endapo atashindwa kufanya hivyo, au kupuuza kutekeleza matakwa yao watamfungulia kesi ya madai katika mahakama watakayoichagua wao. Aliongeza pia kama Kone atashindwa kutekeleza madai yao, hawatasita kumdai fidia zaidi ya fedha na nafuu nyinginezo za kisheria dhidi yao.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Kone alizungumza na Tanzania Daima, alikanusha tuhuma hizo zinazomkabili na kudai kuwa alikwenda katika kijiji hicho kukagua mradi wa umwagiliaji na hakumtukana kiongozi yeyote.

MLOLONGO WA KULALAMIKA,KUTOA VITISHO AU HATA KULIA HAUWEZI KUKOMESHA UFISADI AU KUWAKUMBUSHA WAJIBU BAADHI YA VIONGOZI WANAOJIONA MIUNGU WATU.DR SLAA NA CHADEMA WAMEKUWA WAKITUAMINISHA KWAMBA CCM INAHUSIKA MOJA KWA MOJA KATIKA KUFANIKISHA UJAMBAZI WA EPA.JAPO NAFAHAMU KUWA HUKUMU YA UMMA INA MADHARA ZAIDI YA HUKUMU YA MAHAKAMA ZA KISHERIA,SOTE TUNAJUA NAMNA HUKUMU YA UMMA INAVYOWEZA KUPINDISHWA NA ZAWADI ZA KHANGA,FLANI,KILO YA SUKARI,NK KAMA VIVUTIO WAKATI WA UCHAGUZI.

NGOJA NIFAFANUE KAMA HUJANIELEWA VIZURI.YAYUMKINIKA KUAMINI KUWA CHADEMA INAPOITUHUMU CCM KWENYE MIKUTANO YA HADHARA KWAMBA CHAMA HICHO TAWALA KINA MAHUSIANO NA UFISADI/MAFISADI INATARAJIWA KUWA WANANCHI WATATOA HUKUMU DHIDI YA CCM (HUKUMU YA UMMA) WAKATI WA UCHAGUZI.HILO LINAWEZEKANA KATIKA MFUMO HURU WA DEMOKRASIA,NA MIFANO HAI NI NAMNA HUKUMU YA UMMA ILIVYOFANYA KAZI KATIKA CHAGUZI HUKO HISPANIA MWAKA 2004 NA MAREKANI MWAKA JANA.KATIKA CHAGUZI ZINAZOFANYIKA KATIKA MAZINGIRA YA DEMOKRASIA HURU,HASIRA ZA WAPIGA KURA (AU KURIDHISHWA KWAO) NI MIONGONI MWA MAMBO MUHIMU KATIKA KU-DETERMINE MATOKEO YA UCHAUZI HUSIKA.

SASA SOTE TUNAJUA MAZINGIRA YA CHAGUZI NYINGI ZA "DUNIA YA TATU".KANUNI ISIYO RASMI KUHUSU CHAGUZI ZETU INADAI KWAMBA CHAMA TAWALA HAKIWEZI KUSHINDWA UCHAGUZI.KIKISHINDWA BASI AIDHA KILIZEMBEA KUTUMIA MBINU ZAKE ZA AWALI ZA KUBAKI MADARAKANI AU KILIPIGIWA KURA ZA CHUKI NA WAFUASI WAKE AU KULITOKEA MPASUKO NDANI YA CHAMA TAWALA AMBAO ULIZAA MAKUNDI MAWILI YENYE TAKRIBAN NGUVU SAWA,KILA MOJA LIKIFAHAMU MBINU SAFI NA CHFU ZA KUSHINDA CHAGUZI,NK.WAPO WANAOAMINI KUWA HATA KANU YA MOI HAKIKUSHINDWA UCHAGUZI WA 2002 KWA VILE WAPIGA KURA WALIKUWA WAMEICHOKA (WHICH WAS TRUE i.e. kweli walikuwa wameichoka) BALI NI UTEUZI MBOVU WA MGOMBEA UHURU KENYATA.

VINGI VYA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA TATU HUSHIKILIA DOLA KWA MAANA HALISI YA KUSHIKILIA,YAANI WANAITUMIA IPASAVYO KUHAKIKISHA UTAWALA UNAENDELEA MILELE.HAKUNA DHAMBI KWA CHAMA KUWA MADARAKANI MUDA MREFU AS LONG AS KINAWAHUDUMIA WANANCHI IPASAVYO.KWA BAHATI MBAYA,U-KING'ANG'ANIZI WA BAADHI YA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA DUNIA YA TATU HAUTOKANI NA MAPENZI YAO KWA NCHI AU WANANCHI BALI HOFU YA KUADHIBIWA KWA MADHAMBI YALIYOWAFANYWA WAKATI VYAMA HIVYO VIKIWA MADARAKANI.KADRI MADHAMBI YANAVYOZIDI KUONGEZEKA NDIVYO KADRI VYAMA HIVYO VINAVYOZIDIWA NA HOFU YA NINI KITATOKEA PINDI VIKITOLEWA MADARAKANI,NA MATOKEO YAKE NI KUTUMIA KILA NJIA KUHAKIKISHA VINATAWALA MILELE.NA KWA VINASHIKILIA DOLA,HILO LINAKUWA SIO JAMBO GUMU.

KWAHIYO,KAMA DR SLAA,CHADEMA NA WENGINEO WANADHANI KELELE KUWA CCM INAHUSIKA KATIKA WIZI WA EPA ZITAFANIKISHA KUPATIKANA KWA HUKUMU YA UMMA KATIKA UCHAGUZI WA 2010 AU BAADAYE,THEY REALLY NEED TO THINK AGAIN.KUFANYA HIVYO NI SAWA NA KUTARAJI KUWA HUYO RC ANAYETUHUMIWA KUWATUKANA WANANCHI ANGEAMUA YEYE MWENYEWE KWA HIARI YAKE KUOMBA RADHI BADALA YA KULAZIMISHWA KUFANYA HIVYO (KAMA ANAVYOTAKIWA NA WAKILI LISSU).NAMNA PEKEE YA CHADEMA,ET AL WANAWEZA KUFANIKIWA KATIKA TUHUMA ZAO DHIDI YA CCM NI KWENDA MAHAKAMANI WAKIWA NA USHAHIDI WANAODAI KUWA NAO.

KUITAKA CCM IENDE MAHAKAMANI (INAPOTUHUMIWA KUWA NA UHUSIANO NA MAFISADI) NI SAWA NA KUMTAKA MTU UNAYEMTUHUMU KUTEMBEA NA MKEO/MUMEO (KUTEGEMEA JINSI YAKO MSOMAJI) AENDE POLISI/MAHAKAMANI.....KWA KIFUPI,ATAENDELEA KUKUIBIA NA HATOTIA MGUU POLISI/MAHAKAMANI.COMMON SENSE INATUELEZA KUWA MWENYE TUHUMA NDIO ANAYEPASWA KUWA NA UHARAKA WA KUZIDHIBITISHA AU KUWA NA DHAMIRA YA KUZITOKOMEZA KABISA.MTUHUMIWA ANAWEZA KUWA NA UHARAKA HUO IWAPO ANAONA ZINAMCHAFULIA JINA.LAKINI WHAT IF TUHUMA DHIDI YA MTUHUMIWA NI ZA KWELI?BADO TUTATEGEMEA MTUHUMIWA AJIEPELEKE KWENYE HUKUMU YAKE?

NAHISI CHADEMA WANACHELEA KWENDA MAHAKAMANI SIO KWA VILE WANAHOFIA KUTOPATA HAKI BALI WANAZITUMIA TUHUMA HIZO KUWA MTAJI WA KISIASA.NA-HYPOTHESIZE KUWA CHAMA HICHO KITAZITUMIA TUHUMA HIZO KWENYE KAMPENI ZAKE ZA UCHAGUZI MKUU WA 2010 KIKIAMINI KUWA ZITAKISAIDIA KUPATA USHINDI KWA HUKUMU YA UMMA DHIDI YA CCM.JAPO LOLOTE LINAWEZEKANA KATIKA SIASA,NA MBINU HIYO YA CHADEMA INAWEZA KUFANIKIWA,WAZOEFU WA SIASA WANAWEZA KUAFIKIANA NAMI KWENYE HYPOTHESIS YANGU YA PILI KUWA MKAKATI HUO HAUTOFANIKIWA.KINACHONIPELEKA KUAMINI HIVYO NI UZOEFU KUHUSU NAMNA CCM INAVYOELEWA UDHAIFU WA MPIGA KURA WA KITANZANIA,FAIDA ZA KILOJISTIKI ZINAZOELEMEA UPANDE WA CHAMA TAWALA,MILKI NA SAPOTI YA DOLA BILA KUSAHAU "MBINU CHAFU."

UCHAGUZI MKUU WA 2010 UNAWEZA KABISA KUPITA NA CCM KUIBUKA KIDEDEA HUKU CHADEMA IKIWA "IMEDODEWA" NA USHAHIDI WAKE DHIDI YA CCM.HILO SIO BAO LA KISIGINO BALI NI MITHILI YA KIBAKA KUKUPORA KISHA ANAKUPIGIA KELELE KUWA WEWE NDIO MWIZI....(AND WE ALL VERY WELL KNOW MOB JUSTICE HUKO NYUMBANI ZILIVYO...WATU WAKISKIA UKELELE WA MWIZI,MWIZI HAWAULIZI ILIKUWAJE.NI KIPIGO TU....PASIPO KUJUA KUWA WANAYEMPIGA NDIO ALOPORWA NA KIBAKA).

2 Mar 2009

UAMUZI WA SERIKALI KUHUSU KURA YA MAONI DHIDI YA WAUAJI WA ALBINO-ULIOTANGAZWA NA RAIS JK KWENYE HOTUBA YAKE YA MWISHO WA MWEZI FEBRUARI- UMEPOKELEWA KWA HISIA TOFAUTI NA BAADHI YA WANANCHI KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI NAMBARI 2 HAPO CHINI.KWA MTAZAMO WANGU,NADHANI WANANCHI WANA KILA SABABU YA KUHOJI UAMUZI HUO WA SERIKALI HASA KWA VILE IMEKUWA NI KAMA DESTURI KWA NCHI YETU KUTANGAZA HATUA KALI ZA KISIASA AMBAZO HUISHIA KUBAKI HISTORIA TU PASIPO MAFANIKIO.WENGI TUNAKUMBUKA KUHUSU DEADLINE WALIYOPEWA WALA RUSHWA MWANZONI MWA MWAKA 2006 NA ORODHA YA MAJINA YA WANAOJIHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA ILIYOKABIDHIWA KWA (ALIYEKUWA )WAZIRI BAKARI MWAPACHU....LAKINI HADI LEO HAKUNA HATUA YOYOTE ILIYOCHUKULIWA.KWANZA SOMA HABARI HUSIKA KISHA TUJADILI ZAIDI:

Kikwete:Wanaoua albinokuanza kutajwa kwa kura
mwezi huu

Claud Mshana

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.

Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.

"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."

Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa. Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.

"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.

"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema......
CHANZO: Mwananchi

NA IFUATAYO NI HABARI KUHUSU REACTION YA BAADHI YA WANANCHI JIJINI DAR ES AALAAM KUHUSIANA NA UAMUZI HUO WA KURA YA MAONI KUWATAMBUA WAUAJI WA MAALBINO.


Dar wataka serikali iweke wazi chanzo cha mauaji ya
albino


Na Boniface Meena

WANANCHI wa Mkoa wa Dar es Salaam wameiomba serikali itafute na kuewaleza chanzo cha mauaji ya albino, badala ya kuendelea kutoa kauli za kisiasa wakati hali inaendelea kuwa mbaya.

Pia wamesema hawadhani kama upigaji kura kuhusu mauaji hayo kama utasaidia kwa kuwa hata kesi za waliokamatwa kwa kuhusishwa na mauaji hayo hazijasikika. Mbali na hilo wameitaka serikali kuanzisha mahakama maalum kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji hayo ili waweze kujua maamuzi yanayotolewa na mahakama. Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Kihato wananchi hao walidai serikali inaoneka kutokuwa makini na suala hilo kwa kuwa hakuna hata kesi moja ya mauaji ya albino iliyotolewa hukumu hadi hivi sasa.

Mbunge wa kuteuliwa, Al-Shaimar Kweiger alidai kuwa kuna mtandao mkubwa wa matajiri unaohusika na mauaji hayo ambao alisema hadhani kama unaweza kuishinda serikali katika kupambana nao. "Hili suala limeshazungumziwa sana, tumezunguka na Waziri Mkuu sehemu nyingi, lakini hawakomi nadhani kuna mtandao mkubwa wa watu wenye fedha uko nyuma ya jambo hili," alisema Kweiger.

Josephat Torner ambaye ni mwanaharkati wa kupinga mauaji ya albino alisema suala hilo linaonekana kuwa la kisiasa kwa kuwa hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuwasaisdia wahanga wa mauaji hayo. "Tunataka kujua serikali imefikia wapi tangu suala hili lilipotangazwa kuwa ni la kitaifa," alihoji Torner. Torner ambaye ni albino alisema hawadhani kama upigaji kura utasaidia, kwani wanaona kama ni mchezo wa kisiasa hivyop wangependa kujua wako katika hali gani hivi sasa kuhusu mauaji hayo.

Christopher Andendekisye ambaye ni Mkurugenzi wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania (Shivyawata) alisema, kama serikali haitakuwa makini na mauaji hayo yanaweza kuendelea kwa muda mrefu kwa kuwa chanzo chake bado hakijajulikana. "Itabidi tuwe na wiki maalum au mahakama maalumu kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji haya na kama haiwezekani tuambiwe chanzo ni nini," alisema Andendekisye. Maria Chale ambaye ni albino alidai kuwa inaonekana serikali mpaka sasa haijui chanzo kitu ambacho kinatia wasiwasi kama zoezi hilo litafanikiwa.

Steven pascal ambaye ni katibu wa Albino muungano Investiment Trust(Amit), alisema ni bora jeshi (JWTZ) watumike kuwaska wanaohusika na mauaji hayo. "Ni bora Jeshi lihusishwe kwani hawa jamaa (wanajeshi) akipigwa mwenzao mmoja kijiji kizima kinazingira mpaka wapatikane wahusuka," alisema Pascal. Wananchi hao walisemas hayo jana wakitoa maoni yao mbele ya DC Kihato ambaye alikutana nao kuwaeleza juu ya uzinduzi wa upigaji kura za maoni dhidi ya mauaji ya albino utakaofanyika jijini Dar es Salaam Machi 5, mwaka huu.

Akijibu baadhi ya maoni yaliyotolewa na wananchi hao, Kihato ni kweli serikali haijatatua tatizo hilo kama wananchi wanavyotaka lakini inajitahidi kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa, ndiyo maana wameitisha kura ya maoni.


CHANZO: Mwananchi

KATIKA HABARI YA KWANZA,KUNA MANENO NIMEYAONYESHA KWA RANGI NYEKUNDU KWA SABABU MAALUMU.PAMOJA NA NIA NZURI YA SERIKALI KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MAUAJI YA MAALBINO,WAZO LA KURA YA MAONI LINAWEZA LISIWE NA MAFANIKO YANAYOKUSUDIWA.KWANZA,KAMA MANENO YENYE RANGI NYEKUNDU YANAVYOONYESHA "...Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa..." KUTANUA WIGO WA WALENGWA KUNALIFANYA ZOEZI HILO KUWA PANA ZAIDI ILHALI MAANDALIZI YAKIWA DUNI.ZAIDI,IWAPO KWELI DHAMIRA NI KUWASAKA WAUAJI WA MAALBINO,KUNA HAJA GANI KUINGIZA HABARI ZA WAUZA MADAYA YA KULEVYA,KWA MFANO,AMBAO HUKO NYUMA TULISHAAMBIWA KUWA ORODHA YAO ILIKABIDHIWA KWA WAZIRI MWAPACHU NAE AKADAI KUWA AMEIKABIDHI KWA RAIS?

JINGINE AMBALO LINAHITAJI TAFAKURI NI UTATA KATIKA KAULI ZA VIONGOZI WETU.RAIS ANASEMA ALITOA AGIZO MWEZI DESEMBA,LAKINI TUNAKUMBUKA KAULI ZA WAZIRI MKUU HAPO KATIKATI KWAMBA WAUAJI WA MAALBINO NAO WAUAWE (JAPO BAADAYE ALIOMBA MSAMAHA KWA MACHOZI HUKO BUNGENI)....INA MAANA AGIZO LA DESEMBA LILIPUUZWA NA KUBADILISHWA KUWA "JINO KWA JINO" KABLA HALIJAFUTWA KUFUATIA KELELE ZA WADAU KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA?

NA KAMA AGIZO LILITOLEWA DISEMBA,KWANINI BASI ICHUKUE MIEZI MITATU MIZIMA KUTOA UAMUZI HUU AMBAO KWA HAKIKA UNAHITAJI MAANDALIZI MAZURI NA YA KUTOSHA (HUSUSAN UHAMASISHAJI)?JE WIKI MBILI ZINATOSHA ?RAIS ANASEMA "...maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu...zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."ARE WE ARE WE REALLY SERIOUS?KURA YA MAONI WIKI MOJA BAADA YA UZINDUZI!?JE MAANDALIZI YANAYODAIWA KUKAMILIKA HAYAKUPASWA KUJUMUISHA UHAMASISHAJI WA WANANCHI?PASIPO UMAKINI,ZOEZI HILI LITAISHIA KUTUNISHA POSHO ZA WAHUSIKA NA WAUAJI WA MAALBINO,WAUZA UNGA NA MAJAMBAZI WAKAENDELEA "KUPETA."

SWALI JINGINE LA MSINGI NI KUHUSU MATOKEO YA KURA HIYO YA MAONI.HIVI KWA MFANO BLOGU HII IKIPIGIWA KURA NYINGI KUWA NDIO SPONSOR WA WAUAJI WA MAALBINO (GOD FORBID),NINI KINAFUATA?MHUSIKA ATAKAMATWA NA KUHOJIWA KWA VILE KURA NYINGI ZIMESEMA HIVYO?MHUSIKA ATATAKIWA AJIELEZE KWANINI WANANCHI WENGI WAMEMPIGIA KURA "ZA CHUKI"?AU WAPELELEZI WATAINGIA UWANJANI KUANZA UCHUNGUZI?VIPI ILE TASK FORCE ILIYOUNDWA HUKO NYUMA?

KWA NCHI INAYOHESHIMU UTAWALA WA SHERIA INATARAJIWA KUWA MATOKEO YA KURA HIYO HAYATACHUKULIWA KUWA NDIO HUKUMU DHIDI YA WATAJWA.HIYO ITAMAANISHA KUFANYIA UCHUNGUZI MAJINA YA WALIOPATA KURA NYINGI.KISHA UCHUNGUZI UTAPOKAMILIKA NA USHAHIDI WA KUTOSHA KUPATIKANA NDIPO ZIANZE HATUA ZA KISHERIA KWA VILE,KWA MUJIBU WA SHERIA, NI MAHAKAMA PEKEE (NA SIO MATOKEO YA KURA YA MAONI) INAYOWEZA KUMTIA MTUHUMIWA HATIANI AU KUMWACHIA HURU.

MWISHO,NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA NAMNA UTAMADUNI WA RUSHWA UNAVYOATHIRI MWENENDO WA MAISHA YA MTANZANIA KILA SIKU.HIVI KAMA BAADHI YA WAHESHIMIWA WANAWEZA KUNUNUA KURA ILI WATUWAKILISHE HUKO BUNGENI,KWA MFANO,ITASHINDIKANA VIPI KWA MATAJIRI WANAOFADHILI MAUAJI YA MAALBINO KUNUNUA KURA "ZA KUPENDWA" NA WAPIGA KURA?VIPI IWAPO MATOKEO YA KURA YATAONYESHA MAJINA YA BAADHI YA WAHUSIKA WA KAMPUNI YA KAGODA?HAKUTAKUWA NA KIGUGUGMIZI KAMA KILICHOPO KWENYE UFISADI WA KAMPUNI HIYO KWENYE FEDHA ZA EPA?

NA VIPI IWAPO WANYONGE WATAPIGIWA KURA ZA CHUKI?

MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU.KWA HAKIKA DHAMIRA KUHUSU KURA YA MAONI NI NZURI LAKINI WASIWASI WANGU MKUBWA NI KATIKA UTEKELEZAJI WAKE.NA KAMA WALIVYOSEMA BAADHI YA WAKAZI WA DAR KATIKA STORI NAMBA 2,MAFANIKIO KATIKA HARAKATI ZA KUKOMESHA MAUAJI YA ALBINO YANAHITAJI JITIHADA ZA ZAIDI YA KAULI ZA KISIASA.

7 Dec 2008


UTATA wa zilipo fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoiba fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), umeendelea kuigubika nchi, baada ya kubainika kuwa fedha hizo hazijaingizwa kwenye mfuko ulioelekezwa na Rais Jakaya Kikwete wakati akilihutubia Bunge, Agosti 21 mwaka huu.

Fedha hizo ambazo ni zaidi ya sh bilioni 70, zilitakiwa ziende Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB), ambapo zingefunguliwa dirisha maalumu, lenye jukumu la kutoa mikopo kwa wakulima ambao kwa miaka mingi wamekosa fursa hiyo.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili, umebaini kuwa fedha hizo zimehifadhiwa katika akaunti maalumu ambayo mpaka hivi sasa maelezo yake bado yamegubikwa na utata, kwa sababu kila ofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi aliyeulizwa juu ya akaunti hiyo, ameshindwa kutoa jibu linaloeleweka.

Tangu awali baadhi ya watu walionyesha wasiwasi wao kuhusu urejeshaji wa fedha hizo kama ni kweli zimerejeshwa au ilikuwa mbinu ya kisiasa ya serikali kutaka kuzima joto la wananchi, wapinzani na wahisani waliotaka fedha hizo zirejeshwe na watuhumiwa wafikishwe katika mikono ya sheria.

Watu hao waliweka wazi msimamo wao kuwa fedha hizo hazikurejeshwa bali ilikuwa ni janja ya serikali ili waweze kupata misaada kutoka kwa wafadhili ambao awali walitishia kutochangia bajeti ya serikali mpaka majibu sahihi na hatua za wizi wa EPA zichukuliwe.

Shinikizo hilo inadaiwa ndilo lililomfanya Rais Jakaya Kikwete kuamua kutengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali, pamoja na kuunda timu ya uchunguzi chini ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, baada ya mkaguzi wa nje, Ernst & Young, kuthibitisha kuwapo kwa wizi katika akaunti hiyo, unaofikia kiasi cha sh bilioni 133.

Mkurugenzi wa Benki ya Rasilimali (TIB), William Mlaki, hivi karibuni alikaririwa na vyombo vya habari kuwa fedha hizo hadi sasa hawajazipokea.

Alisema inawezekana serikali inajiandaa kuwapelekea fedha hizo ambazo Rais Jakaya Kikwete alishaweka wazi dhamira ya serikali yake kuzipeleka TIB ili ziwasaidie wakulima.

“Mpaka sasa fedha za EPA, bado hazijaingia kwetu na si jukumu letu kuulizia fedha hizo zitakuja lini, kazi yetu ni kuzipokea na kuratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wakulima,” alikaririwa Mlaki.

Kauli hiyo ya Mlaki, inazidisha utata kuhusu ukweli wa urejeshaji wa fedha za EPA ambazo uchotwaji wake unahusishwa na matumizi ya uchaguzi mkuu uliopita.

Inadaiwa kuwa mbinu za kuchota fedha hizo, zilifanywa na viongozi wa juu wa Serikali ya Awamu ya Tatu kwa kushirikiana na mwanasiasa na mfanyabiashara maarufu nchini ili zikisaidie Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu uliopita.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, tena kwa nyakati tofauti, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha, Amos Makala, wamekanusha chama chao kuhusishwa na wizi huo.

Mfanyabiashara huyo ndiye anayeaminika alikuwa mmiliki halali wa Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited iliyochota sh bilioni 40, lakini hadi hivi sasa hajafikishwa mahakamani au kutajwa mbele ya umma.

Kutotajwa kwa mfanyabiashara huyo kunatokana na ukweli kuwa ndiye anayejua siri yote ya Kagoda na viongozi waliomuagiza kuzichota fedha hizo na hata matumizi yake pamoja na kujua nani kapata kiasi gani na kwa kazi gani.

Kwa hali ilivyo, Kagoda ndiyo kampuni inayoonekana kuitikisa nchi kama wamiliki wake watatajwa na kufikishwa mahakamani, kwani hawatakubali kushitakiwa peke yao bila kuwataja viongozi waliowatuma kufanya wizi huo.

Hali hiyo ndiyo iliyomfanya aliyekuwa Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji, kutoa ufafanuzi kwa umma kuwa fedha zilizochotwa zilitumika kwa mambo ya usalama na si ufisadi kama ambavyo baadhi ya wanasiasa, akiwemo Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, walivyokuwa wakisema.

Msumari wa moto juu ya utata wa urejeshwaji wa fedha za EPA na ufisadi hivi karibuni ulishindiliwa na mfanyabiashara maarufu nchini na mwachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jafar Sabodo, ambaye alisema serikali inafanya mchezo wa kuigiza na haina nia thabiti ya kutatua matatizo ya rushwa.

Sabodo ambaye ni rafiki wa karibu wa marehemu Mwalimu Nyerere na mfadhili wa mfuko wa taasisi ya Mwalimu Nyerere na CCM, alifikia hatua ya kusema yuko tayari kukisaidia chama chochote cha upinzani katika uchaguzi ujao, kuiangusha CCM madarakani, kwa madai kuwa imeshindwa kuondoa tatizo la rushwa nchini.

Wachambuzi wa masula ya siasa wanadai kupandishwa mahakamani kwa mawaziri wawili ya serikali iliyopita Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona ((Nishati na Madini), ni mpango wa kuwasahaulisha wananchi juu ya mwenendo wa kesi ya EPA, hasa kuendelea kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wengine.

Mpango huo uliasisiwa kutokana na joto la wananchi kutaka wamiliki wa Kampuni ya Kagoda inayohusishwa na wafanyabiashara, wanasiasa maarufu na wakongwe nchini, kuzidi kushika kasi kiasi cha kumfanya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuweka bayana kuwa joto hilo likizidi, wamiliki wake watajulikana.

Wadadisi hao wanaendelea kubainisha kuwa mpango huo kwa kiasi fulani, umefanikiwa, kwani watu walihamisha macho na masikio yao kutoka EPA na kuhamia kwa Yona na Mramba, ambao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salam kwa kosa la kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya sh bilioni 11.7, kwa kutoa misamaha ya kodi kiholela katika sekta ya madini.

Wakati wingu zito likiwa limetanda kuhusu mahali zilipo fedha za EPA, kuna tetesi kwamba fedha hizo ndizo zilizotumika kulipa madai ya walimu ambao miezi miwili iliyopita walitishia kugoma nchi nzima kushinikiza kulipwa fedha zao za malimbikizo zinazofikia sh bilioni 16.


27 Feb 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UNAFIKI: Ule wa Profesa Mwandosya kuitaka Dawasco isiwataje hadharani mawaziri wanaodaiwa maji na Mamlaka hiyo;ule wa Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Arusha kutumia neno la Bwana kuwapiga vijembe wanamwandama Lowassa,na ule wa "mabilioni ya EPA yanayorejeshwa kwa kasi."Makala hiyo imeanza kwa stori za hapa na pale,mambo ya muziki wa kufokafoka na albamu ya Jay-Z ya American Gangster ilivyosahau matatizo ya Black Americans.Stori hizo ni zinaunganishwa katika namna ile ile ya conversational style,napenda sana makala iwe mithili ya kupiga stori na msomaji,iwe kijiweni,kwenye pub,au hata barazani.Pamoja na habari na makala zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.