Showing posts with label NEW HAMPSHIRE. Show all posts
Showing posts with label NEW HAMPSHIRE. Show all posts

16 Jan 2008


Wiki iliyopita ilitawaliwa na surprises mbili:huko New Hampshire,Marekani,Hillary Clinton aliibuka mshindi kwenye primaries za chama cha Democrats,kinyume kabisa na utabiri wa awali wa waendesha kura za maoni na wachambuzi wa siasa za nchi hiyo.Na huko nyumbani,ugavana wa Daudi Balali ulitenguliwa.Wakati ili kuelewa nini kinaweza kuwa chanzo cha tofauti kati ya utabiri (kwamba Hillary angeshindwa) na matokeo (ambapo mwanamama huyo alishinda) kunahitaji upeo wa namna flani kuhusu siasa za Marekani na tabia ya chaguzi katika nchi hiyo (kwa mfano phenomenon kama Bradley effect),utenguzi wa ugavana wa Balali haukuhitaji hata short course ya uchambuzi wa siasa kubaini kwamba he had to go,pengine mapema zaidi ya wiki iliyopita.

Makala yangu ndani ya gazeti la Raia Mwema wiki hii inazungumzia surprises hizo mbili.Inakwenda mbali zaidi kwa kuhoji iwapo ufisadi uliopelekea Balali kupoteza unga wake ulihusisha mtu mmoja pekee.Kadhalika,inahitimisha kwamba kufanikiwa kwa ufisadi huo ni failure kwa TAKUKURU na jeshi la Polisi,taasisi ambazo kimsingi zilipaswa kuchukua hatua mapema kuzuia na/au kupunguza uhalifu huo.

Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya Raia Mwema,bingirika na makala hiyo hapa.

9 Jan 2008


Baada ya Barack Obama kuibuka kidedea huko Iowa,kuna wengi walioanza kuamini kwamba sura mpya imefunguliwa katika siasa za Marekani.Mimi sikuwa mmoja wao,na ushahidi unapatikana kwenye makala zangu zilizopita kuhusu ushindi huo wa Obama.Katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema nimejaribu kuangalia namna imani na matumaini ya Obama yalivyomfikisha hapa alipo sasa.Napenda kusisitiza kwamba makala hiyo iliandaliwa kabla ya matokeo ya primaries huko New Hampshire ambapo Hillary Clinton ameibuka mshindi na kuwafanya baadhi ya wachambuzi wa siasa na waendesha kura za maoni "kulamba matapishi yao".

Nikipata muda mwafaka nitachambua kwa kirefu nini nachodhani kimechangia kugeuza upepo uliokuwa ukivuma kuelekea kwa Obama huko New Hampshire.Lakini kwa kifupi,nadhani waendesha kura za maoni waliokuwa wakimpa Obama nafasi kubwa ya ushindi huku wakitabiri kuwa Hillary ataanguka walisahau namna Bradley effect inavyoweza kuwazuga watu pindi panapokuwa mgombea Mweupe na Mweusi.Kwa kifupi kabisa,Bradley effect ni tabia katika chaguzi za Marekani  ambapo  wapiga kura watarajiwa ambao hawajafikia uamuzi watampa nani kura zao (undecided voters) hutoa mtizamo tofauti na namna watakavyopiga kura.Kimsingi,tabia hii huchochewa na ubaguzi wa rangi ambapo undecided voters Weupe huweza kudai kuwa hawajaamua wampe nani kura au kudai kuwa watampa kura mgombea Mweusi lakini huishia kumpa kura mgombea Mweupe.

Kama nilivyosema awali,makala yangu kwenye Raia Mwema inahusu namna imani inavyoweza kuyapa nguvu matumaini ili kufikia malengo flani.Nafasi ya Obama imetumiwa kama kielelezo tu cha namna imani mbalimbali huko nyumbani (kwa mfano,kwamba maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana) zinavyoshindwa kuleta matumaini yanayokusudiwa kutokana na ufisadi,uzembe na ubabaishaji.Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule katika gazeti la Raia Mwema,bingirika na makala yangu hapa.

Baada ya kusoma makala hii sio vibaya ukiburudika na warembo hawa wa Blu3 na kitu chao Hitaji


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.