Showing posts with label YUSUF MANJI. Show all posts
Showing posts with label YUSUF MANJI. Show all posts

16 May 2011



Yanga wampa uchifu Manji 
Sunday, 15 May 2011 20:54

Clara Alponce
WAZEE wa klabu ya Yanga jana walimkabidhi Mkuki, Ngao na Kigoda kama alama ya cheo cha uchifu kwa aliyekuwa mfadhili wao Yussuf Manji.Manji alikabidhiwa heshima hiyo na kamati ya wazee ya muafaka wa Yanga chini ya kiongozi wake Mzee Yahaya Akilimali.

Akizungumza kwenye hafla hiyo mama Shadia Karume alisema Manji amejifunza mengi Yanga na amerejea rasmi kwa ajili ya kufanya kazi ya kuijenga Yanga mpya.Mama Karume alisema," Manji anatakiwa kujua hasira, jazba hazifai namtaka asahau yote yaliyopita."

Mama Karume aliongeza kuwa kuna watu wengi waliofanya mambo makubwa na mazuri Yanga huko nyuma na Manji ni moja wao."Mume wangu ndiye aliyejenga jengo la Yanga hapa Dar es Salaam, lakini angejisikia vibaya kama lingeachwa na kuharibika bila ya kufanyiwa ukarabati kama aliousimamia Manji,"alisema Mama Karume ambaye pia alimtaka Manji kujenga jengo lingine la Yanga huko Zanzibar kwa sababu uwanja umeshapatikana.

Tukio hilo lilishuhudiwa na viongozi wa serikali akiwemo Jamal Rwambo, Mbunge Mussa Zungu, Mudhihir Mudhihir pamoja na wachezaji wa Yanga huku burudani ikitolewa na bendi za Msondo, Sikinde na Tanzanite

CHANZO: Mwananchi.

28 Apr 2009

NKWAZI MHANGO
St John’s NL, Canada


AT last names are openly named! When Hon. Harrison Mwakyembe named Rostam Aziz as a suspect behind Kagoda profligacy, many scratched their heads. Some thought it was just politics. Others said: there must be something truly fishy. Others thought the government would wake up and bring him to book. Mwakyembe is a lawyer and an MP who knows what he is doing.

Before long, Reginald Mengi, the Executive Chairman of IPP, massively and openly weighed in with more damning allegations. He minced no words. He averred: Rostam, Yusuf Manji, Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel) who is facing EPA charges, Tanil Somaiya, and Subash Patel are the most corrupt people in Tanzania.

Today I’ll specifically look at two -Rostam and Manji. They’ve been stealing thunder when it comes to corruption save the government has pretended not to hear or see!
No doubt. The two are CCM bigwigs just like Mengi himself.

What makes things worse is the fact that the duo has been mentioned, though not openly, in almost all multi-million scams. I still remember how Manji was alleged to have swindled wananchi’s money, thanks to his business connections with NSSF. Though this was swept under the carpet, we still have more questions than answers.

Manji also tried hand in politics when he vied for Kigamboni Constituency backed by Yusuf Makamba - CCM’s secretary general who is said to have thick but suspicious bond with the duo.

As for Rostam, it’s an open secret. �He has been cowering before allegations connecting him with EPA theft thanks to being the mind behind Kagoda. Refer to the recent revelations by Bhyidinka Michael Sanze, a lawyer who presided over EPA authorization by Benjamin Mkapa - former president engrossed in many scams.

Also Rostam was linked with Richmond, thanks to his Caspian Company’s address being used by Richmond. He too was named by Ibrahim Msabaha as PM Edward Lowassa’s Arab in Richmond scam.

What damns so as to create doubts is the fact that, the duo, despite being mentioned in many scandals, still has much influence in CCM. They are awarded many lucrative tenders and other projects. They, too, are CCM’s financiers or donors. And this is the reason that forced the Father of the Nation Mwl. Julius Nyerere to sarcastically aver that CCM has been taken by corrupt business people. Who can step in Nyerere’s shoes.
Given that the government has been dragging feet in dealing with the buggers behind Kagoda, now it is aware who those buggers are. Will it go on keeping mum and acting indifferently as it sits on the same.

Silence is gold. But sometimes, it is admission of guilt. When Rostam was confronted by the media to shed light onto Mengi’s allegations, he’s quoted as thus. ’’Mengi is full of jealousy, hatred and what not. There is no way I can help him except to pray God and ignore all, for it is enough a punishment for him. Due to how I was brought up, I cannot quarrel with an old man.’’

Do such gimmicks address the allegations really. Let’s call shorts to white washing and be serious especially when allegations are damningly serious like these.

Though it can be lightly and wrongly perceived as racism and hatred for Mengi to name five Tanzanians of Asian decent as the most corrupt in the country, there is truth in this. Why should it be racism or hatred to aver they are corrupt but not when it comes to owning our economy Why not when they’re given tenders and other preferential treatments.

As Rostam once said that those alleging he is corrupt are labouring under racism, petty jealousy and hatred, but again, is it racism really or corruption.

Suspects should mount reasonable defence in lieu of taking camouflage under the colour of their skin. For example, if someone says Indians own a big chunk of national housing, will this be referred to as racism? If one avers that Indians own over 75% of commerce in the country, will it be branded hatred. If one avers that Indian and Chinese illegal immigrants and hawkers are favoured by authorities, will this be jealousy.

Indians own almost every lucrative business. And now they’ve already penetrated into politics, thanks to rotten takrima law. They live in government houses whilst its workers make do on the outskirts of the city. They’ve remained holier than us since they were brought in by colonialists.

We well know. Indian business moguls are almost behind every stinking lucrative government tender. Refer to the radar, presidential jet purchase, NSSF, Richmond, EPA and what not.

Many will wonder why. It is simple. Corrupt government officials prefer to do dirty business with Indians. They can not divulge their secrets. They’re easy to intimidate and repatriate when things go wrong as it happened in Chavda scam. So indigenous ’fisadis’ are left out of the big picture.

And if you look at whom Tanzania prefers to award citizenship to, you’ll find that Indians outsmart others. They still do the same- being middlemen-the job for which colonialists brought them. When white colonialists left and black ones took over, the role of Indians remained the same almost everywhere in Africa. Go to Kenya, Malawi, South Africa and elsewhere. Indians are still doing the same job-weakening the indigenous for the good of corrupt rulers.

So to avert wasting time, if Kikwete could take a leaf from Mengi, our war on corruption would make more sense than it is today when it is but white washing.

In other words, corruption in Tanzania is like ’mduara’ dance. It’s conspiracy between venal rulers and their corrupt guests. It’s time to rally behind Mengi to see to it that those ’fisadis’ are not harming him. Shall they, Mtikila’s gabacholi era will be latched onto. And the government must stop its indifference. The ’isadis’ it has been asking for are now given pro bono.
FOR MORE,VISIT HIM AT freethinking unabii

24 Apr 2009

Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.
>
Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo." Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.>
"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

CHANZO:Mwananchi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.