22 Oct 2008


HII ya Yanga haijapata kutokea kwenye historia ya soka ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Ndio kauli nyepesi unayoweza kuitumia kama ukipata nafasi ya kupita karibu na kambi ya Yanga jijini Dar es Salaam.

Yanga imeweka kambi kwenye Hoteli ya Lamada Ilala, jijini Dar es Salaam chini ya ulinzi mkali wa askari ambao haujapata kutokea kwa timu yoyote ya Tanzania pengine tangu Ligi Kuu Bara ianzishwe.

Ulinzi huo ambao wachezaji wa Yanga wamesema kwamba hawajapata kuuona, unadaiwa kuwekwa na mdhamini mkuu wa klabu hiyo, Yusufu Manji kutokana na kikosi hicho kukabiliwa na pambano gumu dhidi ya Simba Jumapili kwenye Uwanja Mkuu wa Tanzania jijini Dar es Salaam.

Walinzi hao wengine wakiwa na silaha ambao wametapakaa kila kona mpaka kwenye korido za kwenda vyumbani, walimwagwa hotelini hapo juzi Jumapili jioni wakati mechi baina ya Yanga na Polisi Dodoma ikiendelea kwenye Uwanja wa Taifa. Yanga ilishinda 3-1.

"Tuliporudi tu ile jioni tukashangaa mazingira yamebadilika ghafla, kila kona ina walinzi na wengine wamebeba silaha na wengine wana virungu pamoja na baadhi ya wanachama ambao walikuwa wanapitapita huku na huko kutulinda," alidokeza mchezaji mmoja.

"Sijapata kuiona hali hii, mpaka wachezaji tunashangaa kwa jinsi walinzi walivyomwagwa huku nje wapo kama 12, kwenye korido za vyumbani wapo na kwenye ngazi za kushukia pia wapo.

"Huruhusiwi kutoka nje ya geti na hata ukikaa nje mazungumzo yako yanafuatiliwa kila hatua, yaani mpaka wageni wanaoingia wanaulizwa maswali kama ni mtu mwenye chumba chake lazima waende mpaka chumbani wakahakikishe kama kweli ana chumba.

"Sisi wenyewe wakati unatoka chumbani unaulizwa unakwenda wapi, ukitoka nje kwenye ngazi unawakuta pia hawa walinzi wanafanana na wale wa ile kampuni inayolinda kule ofisni kwa Manji."

Mchezaji mwingine alisema; "Huku ni mitutu tu kila upande bwana, hata kama unaenda nje kununua vocha au kitu chochote kuna walinzi.

"Kwa jinsi palivyo huku utafikiri tunacheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika tena na Real Madrid, ni kasheshe tupu ndugu yangu lakini ndio soka," alisema mchezaji mwingine.

Mwanaspoti ilipojiri kwenye kambi ya timu hiyo jana, askari hao walicharuka mithili ya mbogo wenye njaa na hawakutaka kusikiliza chochote.

"Unakwenda wapi? Wewe ni mteja hapa au unakwenda kuwaona wachezaji wa Yanga?" Walisema walinzi hao wakiwazuia waandishi wa Mwanaspoti kuingia ndani ya hoteli hiyo.

"Huwezi kuingia humu hotelini mpaka upate kibali cha Yanga, wasiliana na mwenyekiti au meneja wa timu," alisema askari mmoja wa kampuni ya Group 7 Security aliyekuwa ameshika rungu.

"Ondokeni eneo hili haraka, usije ukatusababishia matatizo makubwa au tukakufanya chochote baadaye ikawa matatizo, ondoka bwana kwa usalama wako," alisema mlinzi mwingine aliyekuwa amekunja sura.

Waandishi wa Mwanaspoti wamekuwa wakienda mara kwa mara katika hoteli hiyo kufanya mahojiano na wachezaji wa timu hiyo, lakini kila kitu sasa kimebadilika na mawasiliano pekee yaliyobaki ni kwa njia ya simu.

Yanga ambayo imekuwa ikinyanyaswa na Simba kwenye Ligi Kuu Bara kwa takribani miaka saba sasa, inaonekana kujizatiti na kutaka kulipiza kisasi na hasa kutokana na hali kutokuwa shwari ndani ya Simba.

Viongozi wa Yanga wameapa kufanya mauaji makubwa Jumapili kwa madai kuwa dalili za kuimaliza Simba zilianza mwishoni mwa wiki wakati Toto wenye urafiki na Yanga walipoifunga Simba mabao 4-1

CHANZO: Mwanaspoti

Daniel Mjema na Ally Sonda
Siku saba zikiwa zimebaki kabla ya kile kinachoelezwa kuwa ni kiama cha mafisadi kutimia, mwananchi mmoja mkazi wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, jana alichomoza na kumuhoji Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhusu ukimya wa serikali katika kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi.

Hali hiyo ilijitokeza jana nje ya jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rombo wakati waziri mkuu aliposimama kwa muda kuwasalimia wananchi waliokuwa wamefurika nje ya ofisi hizo kwa lengo la kumuona.

Wakati waziri mkuu aliporuhusu maswali machache ndipo mwananchi mmoja alipomhoji Waziri Pinda akimuuliza kwa nini wanawaacha bila kuwashughulikia mafisadi hadi Bunge lilipoamua kuchukua jukumu hilo.

Mwananchi huyo, ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, alitaka serikali itunge sheria kali ya kuwashughulikia mafisadi.

Mbali na kumhoji Waziri Mkuu kuhusu ukimya huo wa serikali katika kuwashughulikia mafisadi, pia alitaka uteuzi wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) na makanda wa mikoa, uthibitishwe na Bunge.

Alisema kuwa hiyo itakuwa rahisi kwa chombo hicho cha wawakilishi wa wananchi kuweza kuwawajibisha viongozi watakaothibitika kujihusisha na vitendo vya ufisadi.

Akijibu swali hilo na mengine, Waziri Pinda alisema suala la ufisadi linapaswa kupigwa vita kuanzia ngazi ya familia kwa sababu viongozi wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu wanatoka katika familia.

Waziri Mkuu alisema hali sasa imebadilika na kwamba suala la kuwachukulia hatua mafisadi lazima lifuate taratibu na sheria za nchi, ikiwamo kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria.

Suala la kutochukuliwa hatua kwa mafisadi limekuwa mdomoni mwa watu wengi baada ya Rais Jakaya Kikwete kulieleza Bunge la Muungano kuwa watu waliochota Sh133 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) warejeshe fedha hizo ifikapo Oktoba 31, la sivyo wafikishwe mahakamani Novemba mosi.

Kauli hiyo ilionekana kama kuwapa ahueni mafisadi hao kuwa iwapo watarejesha fedha hizo ambazo zilichotwa kati ya mwaka 2005/06, hawatachukuliwa hatua zozote.

Kauli hiyo ilifanya watu kuwa na maoni tofauti, wengi wakihoji sababu za serikali kuwapa ahueni watu waliochota mamilioni ya fedha na wengine wakitaka wezi hao watajwe majina yao, lakini serikali imekuwa ikisema kuwa imeshachukua hatua, ikiwa ni pamoja na kuzuia akaunti zao na kushikilia mali zao.

Hadi sasa serikali inadai kuwa mafisadi hao wamesharejesha kiasi cha Sh61 bilioni, lakini haijataja waliokwisha rejesha fedha hizo wala wale ambao hawajarejesha, ikisema kuwa kufanya hivyo kutaharibu mikakati yao.

Akianza ziara yake mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete alikumbana na umati wa watu waliozuia msafara wake maeneo ya Mwanjelwa na wengi wakipiga kelele kutaja neno mafisadi, huku wakihoji maisha bora na ajira.

Mapema wiki hii, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilisema kuwa kitaifungulia serikali mashtaka ya kuwalinda mafisadi iwapo haitawafikisha mahakamani wale wote wanaohusika na tuhuma za uchotaji wa mabilioni hayo ya fedha.

Kashfa ya wizi wa fedha hizo ilibainika wakati kampuni ya Ernst and Young ilipopewa kazi ya kukagua mahesabu ya Benki Kuu (BoT) ya kipindi cha mwaka 2005/06. Kampuni hiyo iligundua kuwepo na malipo ya kasi ya mamilioni ya fedha kwa wafanyabiashara wa ndani katika kipindi hicho na hivyo kutoa ripoti iliyofichua wizi huo.

Fedha hizo, zilizohamishiwa kwenye akaunti hiyo maalum BoT kutoka NBC, ni zile zilizokuwa zikilipwa na wafanyabiashara wa ndani ambao walinunua bidhaa kutoka makampuni ya nje kwa dhamana ya serikali, ambayo ilikuwa inakabiliwa na uhaba mkubwa wa fedha za kigeni.

Akijibu swali la upungufu wa mbolea ya ruzuku, Waziri Pinda alikiri kwamba mbolea hiyo haitoshelezi mahitaji, hivyo akawashauri wakulima wajiunge na vyama vya akiba na mikopo ili waweze kupata mikopo.

Baadaye waziri mkuu alizindua awamu ya tatu ya mradi wa maji unaosimamiwa na kampuni ya Kiliwater ambao baada ya kukamilika utagharimu zaidi ya Sh10 bilioni.

Aliwataka wananchi kuutunza mradi huo dhidi ya hujuma zozote huku akiiagiza Bodi ya Wakurugenzi kuhakikisha wanaifanyia matengenezo ya mara kwa mara miundo mbinu yake ili iwe endelevu.

Katika ziara hiyo ya siku tano mkoani Kilimanjaro, waziri mkuu anafuatana na viongozi mbalimbali wa serikali, akiwemo Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Cyrill Chami.

Wengine ni mkewe, Tunu Pinda, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mohamed Babu na Mwenyekiti wa CCM mkoani Kilimanjaro, Vicky Nsilo Swai na watendaji wengine wa serikali na mashirika ya umma.

Wakati huohuo, ziara ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambayo leo inaingia Siku ya tatu mkoani Kilimanjaro, imegeuka msumari wa moto kwa vijana wa mji wa Moshi ambao wengi wao wanashikiliwa na polisi baada ya msako mkali uliofanywa jana.

Taarifa zilizoifikia Mwananchi jana, zimedai kuwa vijana wengi waliokamatwa ni wafanyabiashara ndogondogo (machinga) kwenye maeneo ya sokoni, Mtaa wa Kiusa ambako Waziri Pinda amepangiwa kuhutubia wananchi leo jioni.

Haikufahamika haraka kiini cha polisi kuendesha operesheni hiyo kali ambayo imesababisha vijana wengi kushindwa kumuona Waziri Pinda jana, lakini taarifa zisizo rasmi zimedai kuwa huenda vyombo vya ulinzi na usalama vina hofu na yale yaliyomkumba Rais Jakaya Kikwete mkoani Mbeya.

"Hivi sasa watu waliokata tamaa ni wengi…….hii kamatakamata inayofanywa na polisi leo (jana) ni kuweka mambo sawa ujio wa Waziri Mkuu, Pinda, bila hivyo yapo majitu yanaweza kumzomea," alisema kiongozi mmoja wa dini.

Mwananchi ilipotembelea mitaa ambayo polisi wanasemekana kufanya msako huo ilielezwa kuwa, baadhi ya vijana waliokamatwa walikuwa wakifanya biashara zao za kujiajiri zikiwemo za kuuza vocha za simu.

''Hatukatai Polisi kufanya kazi zao, lakini misako hii isiwaonee vijana kwa kuwa siyo kila kijana ni mwizi au mkorofi……..mimi nadhani Polisi wanatumika kujenga chuki kati ya serikali na wananchi na kitendo hiki ni hatari kwa amani ya nchi,'' alisema mfanyabiashara wa Soko Kuu la mjini Moshi.

Alipohojiwa kuhusu kamatakamata hiyo, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ramadhani Baruti alisema operesheni hiyo haikufanywa kwa ajili ya ujio wa Waziri Pinda, bali ni ya kawaida na kwamba baada ya uchunguzi wapo watakaofikishwa mahakamani.

CHANZO: Mwananchi


Viongozi wa dini waonya nchi inaelekaa pabaya
*Washauri Rais apunguze safari za nje

Na Waandishi Wetu

VIONGOZI wa dini wamesema kukithiri kwa migomo, maandamano, vitendo vya kikatili, na migogoro kati ya serikali na watumishi wa umma ni ishara tosha kwamba, mambo hayako sawa nchini.

Wakizungumza na Mwananchi nyakati tofauti jana, viongozi hao walisema hali hiyo inaipeleka nchi pabaya na kuitaka serikali kutafuta suluhisho la matatizo hayo haraka iwezekanavyo.

Walisema kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya ahadi zisizotekelezeka na kwamba njia pekee ni kuyashughulikia madai hayo ya wananchi.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Kanisa la Katoliki jijini Dar es Salaam, Mhashamu Methodius Kilaini alisema, iwapo hali hiyo haitashughulikiwa mapema itasababisha hali kuwa mbaya zaidi nchini.

Kauli hiyo imeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ramadhan Sanze aliyesema kuwa, ili kuondoa mitafaruku iliyopo nchini serikali lazima iwe tayari kuwajibika kwa jamii kisheria, kisiasa.

Aliishauri serikali kuyashirikisha makundi mbalimbali ya kijamii na kisiasa katika kupanga na kubuni sera mbalimbali kiutawala na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Sanze alimwomba Rais Jakaya Kikwete kupunguza safari za nje na hasa Marekani, akidai kuwa nchi hiyo si marafiki wazuri kwa ustawi wa taifa la Tanzania.

“Sidhani kama rais safari hizi za Marekani anapanga mwenyewe au anapangiwa, kama anapangiwa basi itifaki hii sio nzuri, hivyo tunamwomba apunguze safari za huko,” alisema Sheikh Sanze.

Alifafanua kuwa, ni vema kwa sasa rais akabakia nchini kuwatumikia Watanzania na kutuliza mitafaruku iliyopo badala ya kusafiri safiri tu huku nchi ikiwa inateketea kwa kuzongwa na migogoro ya kijamii.

Sheikh Sanze alionya kuwa, ikiwa hali itaendelea kama ilivyo sasa bila hatua madhubuti kuchukuliwa, basi kwa mara ya kwanza historia inaweza kubadilika kwa kuwa na rais wa kipindi kimoja.

Awali, Askofu Kilaini alisema ingawa tatizo la migomo linaonekana kuwa ni la miaka mingi, lakini ishara ya sasa inatia mashaka kwani serikali imekuwa ikitoa ahadi nyingi kwa wananchi na mambo machache tu ndiyo yanatekelezwa

“Hatuwezi tukasema kuwa mambo haya yanayoendelea kujiri ni ishara ya kukua kwa demokrasia, bali inatubidi tufahamu kuwa, serikali isipotekeleza ahadi zake kwa wananchi tutaendelea kushuhudia vitendo hivi kila mara.

Alisema uchumi wa dunia unapotikiswa, nchi zinazoendela ndizo zinazoathirika zaidi, hivyo ni vema serikali kupitia wizara zake ikatafuta mbinu zaidi za kuhakikisha kuwa suala la mfumuko wa bei unadhibitiwa ili mwananchi wa kawaida aweze kumudu maisha.

Alisema watu wanapochoka, na kukata tamaa na serikali yao, hutafuta njia nyingine kujinasua na matatizo yanayowakabili.

“ Ukizingatia kuwa suala la maandamano au migomo ni haki za msingi za wafanyakazi, hivyo kama serikali inataka kupunguza masuala haya ni vema ikabeba gharama na siyo kukwepa,” alisema Askofu Kilaini na kuongeza:

“Ninawaomba wananchi wenzangu watafute madai yao kwa kufanya mazungumzo na si kushiriki kwenye vurugu na migomo na pia serikali inapaswa kuwajibika kwa ahadi zake na si kuwayumbisha Watanzania.”

Hata hivyo, Askofu Kilaini alipoulizwa kwamba alishawahi kutamka kuwa Rais Jakaya Kikwete ni chaguo la Mungu na hivi sasa ana maoni gani, alisema kuwa kiongozi yeyote anayechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi ni chaguo la Mungu.

“Ni vema nikaeleweka kuwa maandiko ya Mungu yanasema uongozi na mamlaka yote hutoka kwa Mungu, hivyo basi rais aliyechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi wenyewe ndilo chaguo la Mungu na sisi tutaendelea kuwa na msimamo huo,” alisema Askofu Kilaini.

Alisema pamoja na kwamba Rais Kikwete ni chaguo la Mungu, anahitaji kusaidiwa katika kutekeleza sera na kutimiza ahadi zote zilizoahidiwa katika serikali yake, kwa sababu viongozi wengine wakimwachia na kushughulikia zaidi maisha yao binafsi, hakuna jambo litakalotekelezeka.

Aliwataka mawaziri na watendaji wengine serikalini wakawa mstari wa mbele kumshauri Rais mambo mema na si kumpotosha ili aweze kutekeleza.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Salum Fereji na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), Padri Charles Kitima walisema jana kwenye semina ya waandishi wa habari toka mikoa mbalimbali nchini inaendelea katika Hoteli ya Isamo mkoani hapa kuwa sera na sheria na madini vimetungwa kwa masilahi ya watu wachache walafi ambao wanajali masilahi yao na hivyo lazima vibadilishwe sambamba na mikataba yote ambayo makampuni ya wawekezaji yameingia katika uchimbaji wa madini hapa nchini.

Sheikh Ferej alisema ni lazima serikali kuamka kwa kuwa sasa nchi inaelekea pabaya kutokana na rasilimali muhimu kama madini kuachiwa watu toka nje ya nchi kuwaacha Watanzania kuendelea kuisha katika umaskini uliotopea.

"Ndugu zangu, sisi kama viongozi wa dini tulitembelea maeneo ya migodi yote, kule hali ni mbaya Watanzania wanaishi maisha ya dhiki, wamefukuzwa katika maeneo yao na watu toka nje ya nchi ndio wananufaika na madini haya kwa kupeleka kwao," alisema Sheikh Fereji.

Alisema wao kama viongozi wa dini wamebaini serikali imefanya makosa katika kuingia mikataba na wawekezaji toka nje ya nchi kwa sababu Watanzania hawanufaiki na madini hayo ambayo miaka michache ijayo yatakuwa yamekwisha na kuacha mashimo.

Naye Padri Kitima alisema bila serikali kufanyika marekebisho sheria na sera za madini Tanzania itaendelea kuwa maskini na siku zijazo yanaweza kukatokea mapigano kama ilivyo katika nchi nyingine barani Afrika ambapo kulikuwa na madini.

Alisema mikataba mingi ya wawekezaji ni mibaya na inatakiwa irekebishwe, lakini inavyoonekana hakuna wa kubadilisha hadi vyombo vya habari na wananchi washikamane na kudai mikataba hiyo ivunjwe au kurekebishwa.

Padri Kitima alisema katika mazingira ya sasa angependa yafanyike mabadiliko makubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kabla ya mwaka 2010 na kuwa na kundi la wafuasi wa Nyerere ambao watatetea rasilimali za nchi hii.

"Mimi binafsi kwa hali ilivyo ningependa CCM igawanyike najua kuna watu wazuri ndani ya CCM, lakini wanashindwa kuifanya nchi hii kuwa mikononi mwa Watanzania badala yake kundi la watu wabinafsi ndilo lina nguvu na hata katika kambi ya upinzani kuna matatizo makubwa ya ubinafsi na kuwepo viongozi wasio na sifa," alisema Padri Kitima.

Alisema nchi imepoteza agenda muhimu alizoziacha hayati Mwalimu Julius Nyerere alipounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sasa ubinafsi umetawala hadi kutishia kuvunja Muungano.

CHANZO: Mwananchi


Na Hilary Komba 

WATANZANIA Bara hawawezi kulazimika kuingia Zanzibar kwa pasipoti kutokana na sheria ya uraia kukataza utaratibu huo ndani ya Jamhuri moja. 

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Naibu Kamishina wa Uhamiaji, Wizara ya Mambo ya Ndani Bw. Abdi Ijimbo, wakati akizungumza na Majira kuhusu hoja zilizoripotiwa na vyombo vya habari hivi karibuni, vikiwanukuu baadhi ya watu wakisema ni vyema Watanzania Bara waingie Zanzibar kwa pasipoti. 

Bw. Ijimbo alisema sheria za Uhamiaji zinaruhusu Mtanzania anayetaka kutoka nje ya nchi kuwa na pasipoti, ili ajulikane kuwa ni Mtanzania aliyefuata taratibu ambazo zipo duniani kote. 

"Hadi sasa Serikali haina sababu ya kuanzisha pasipoti kuingia Zanzibar, kwa vile hakuna sheria inayosema hivyo na Zanzibar ipo katika Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, ndiyo maana hata huko nyuma hati ya kuingilia Zanzibar ilifutwa," alisema. 

Bw. Ijimbo aliongeza kuwa katika Serikali ya Awamu ya Pili, Watanzania Bara walikuwa wanaingia Zanzibar kwa hati ambayo ilikuwa pia haina hadhi ya pasipoti, bali ulikuwa ni utaratibu fulani tu uliowekwa na baadaye kuonekana hauna sababu ya kuendelea kuwapo. 

Alisema anashangaa kuona baadhi ya Watanzania wanazungumzia jambo hilo ndani ya nchi zilizoungana na kuwa kwenye Jamhuri ya Muungano. 

Nayo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imesisitiza kwamba vitambulisho vinavyotolewa vya Mzanzibari mkazi ni kwa wale tu wanaoishi visiwani humo, anaripoti Ali Suleiman. 

SMZ imesema Watanzania kutoka Bara wataweza kutambuliwa kwa vitambulisho hivyo, baada ya kutimiza masharti yaliyopo. 

Imesema vitambulisho hivyo havina malengo ya kisiasa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kwamba ni mikakati ya CCM kushinda katika uchaguzi mkuu ujao. 

Akitoa juzi majumuisho ya mjadala wa sera ya vitambulisho vya Mzanzibari, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali Zanzibar, Bw. Suleiman Othman Nyanga, alisema Zanzibar haiwezi kutoa vitambulisho vya uraia kwani yenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Serikali ya Muungano. 

Alisema sera iliyoandaliwa ni ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na si ya vitambulisho vya Mzanzibari. 

“Mheshimiwa Spika ni vyema kutambua kuwa hii sera ni ya vitambulisho vya Mzanzibari kwa sababu michango mingi iliyotolewa, imezungumzia suala la Mzanzibari, lakini hapa tunasema ni sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi kwa sababu Mzanzibari tunayetaka kumpa kitambulisho ni yule ambaye anakaa Zanzibar,” alisema Waziri huyo. 

Waziri Nyanga alisisitiza, kwamba vitambulisho hivyo hatapewa Mzanzibari anayekaa nje ya visiwa hata kama anakaa Dar es Salaam, lakini ikiwa si mkazi, hatakuwa na halali ya kupata kitambulisho hicho, ambacho ni kwa ajili ya Wazanzibari wanaoishi Unguja na Pemba. 

“Tunayemsema sisi hapa ni Mzanzibari mkazi ndiye tutakayempa kitambulisho, kama anakaa Dar es Salaam maadam si mkazi yeye hahusiki na kitambulisho hiki cha sera hii, ambayo tunataka kuipitisha,” alisema. 

Waziri huyo alisema SMZ haitatoa vitambulisho vya uraia kwa sababu suala hilo ni la Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hata Rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Amaan Karume alitoa vitambulisho vya uraia kwa Zanzibar. 

“Wakati huo vitambulisho kweli vilitolewa na viliitwa pasi ya uraia iliyotolewa wakati huo na kwa kuwa kuna neno uraia, na uraia kwa Tanzania ni mmoja, kwa hivyo vitambulisho hivyo kama utavitazama vitakuwa vimeandikwa pasi ya uraia na vimeandikwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Zanzibar ... haikuwa pasi ya uraia ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,” alisema. 

Alisema watakaopaswa kupewa vitambulisho ni wale walioamua kuwa wakazi wa Zanzibar, ambao watakuwa na makazi yao ya kudumu na watakuwa wanahitaji huduma za kila siku za Serikali ambao takwimu zao zitasaidia kupanga mipango ya maendeleo ya visiwa vya Unguja na Pemba. 

Hata hivyo, Waziri Nyanga alisema Mzanzibari yeyote anayeishi nje ya Zanzibar anapoamua kurudi Zanzibar, basi ana haki ya kuomba kitambulisho na atapewa baada ya kuthibitisha kuwa na sifa zinazohitajika. 

“Kwa hiyo akiweza kuthibitisha sifa zilizotajwa, atapewa vitambulisho ingawa wengine walitoa maoni kwamba vielezwe kuwa ni vitambulisho vya uraia kwa kuwa suala la uraia ni la Jamhuri ya Muungano na hakuna raia wa Zanzibar, kwa hiyo vitambulisho hivi vitakuwa bado ni vya Mzanzibari mkazi na si vitambulisho vya uraia wa Zanzibar," alisema. 

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha sera ya vitambulisho vya ukazi vya Zanzibar, hatua ambayo itasaidia kuweka kumbukumbu na kusaidia takwimu za nchi katika maendeleo.

CHANZO: Majira

21 Oct 2008

Albino Girl Killed For Witchcraft
Tuesday, October 21 02:52 pm
Sky News
A gang murdered and mutilated a 10-year-old albino girl in Tanzania - because they wanted to sell her body parts to witch doctors. Skip related content

Esther Charles was killed in Shilela in the western region of the African country on Sunday.

She died just hours after President Jakaya Kikwete called for a crackdown on gangs, saying the killing of albinos has "stained the country's good image".

At least 26 other albinos, mostly women and children, have been killed in different parts of the east African country over the past year.

Albinos lack melanin pigment in the skin, eyes and hair, which protects from the sun's ultraviolet rays.

But witch doctors believe they have magical powers to bring fortune, and discrimination against albinos is rife across sub-Saharan Africa.

In 2007, police in Tanzania reported several cases of people digging up the bodies of children to remove organs, in many cases the genitals and eyes, to make potions used in rituals.

Shilela councillor Joseph Manyara told a rally organised by the Tanzania Albino Society (TAS): "It is utterly stupid for some people to believe that albinos have magic powers and their parts can make them rich.

"People should be provided with education to understand that it is only through hard working that they can prosper in life and not through selling albinos' body parts."

Police said they have arrested 47 people suspected to be involved in the killings this year.

But TAS chairman Ernest Kimaya blasted authorities over the speed at which the murders were solved.

He said: "We are yet to witness any convictions and incidents of the murder of albinos are on the rise."

There are about 150,000 albinos in the country, and more than 8,000 of them are registered with the TAS.

Some families kill albino babies upon birth, Tanzanian authorities say.

And authorities in Kenya and Burundi, where albino killings have also been reported in recent months, have started to give added protection.

Some reports say albino skin is prized in the Democratic Republic of Congo, another troubled African nation where superstition is high.

SOURCE: Sky News


BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamepinga sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na kusema suala hilo linafanywa zaidi kisiasa na kutaka kurudishwa kwa hati ya kusafiri kati ya Tanzania Bara na Zanzibar ambayo iliondoshwa mwaka 1995. 

Hayo yalisemwa jana na Waziri Kivuli Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Bw. Abdalla Juma, wakati akisoma maoni ya kambi ya upinzani katika suala la sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi. 

Alisema haiwezekani Wazanzibari kuitwa wakazi katika nchi yao na kuongeza kwamba vitambulisho hivyo havifai. 

"Vitambulisho hivi kwa kweli havifai, sera hii haifai isipitishwe, kwa sababu inaonekana wazi kuwadhalilisha Wazanzibari katika nchi yao," alisema Bw. Abdalla. 

Wajumbe wengine wa Baraza walitaka kurudishwa kwa utaratibu wa zamani wa kuwapo hati za usafiri wakati wa kuingia katika visiwa vya Unguja na Pemba. 

Mwakilishi wa Magomeni, Bw. Salmin Awadh, alitaka kurudishwa kwa hati za usafiri na kusema kuondoshwa kwake kwa kiasi kikubwa kumesababisha kasi ya ujambazi na uhalifu. 

"Tunataka kurudishwa kwa hati za usafiri kati ya Zanzibar na Tanzania Bara...tunataka kuwepo kwa udhibiti katika eneo la bandari pamoja na uwanja wa ndege'alisema Awadh. 

awadh alisema sera ya vitambulisho vya uzanzibari ukazi lengo lake ni ulinzi kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba na kuweza kuwatambuwa hasa Wazanzibari na wageni. 

mwakilishi wa viti maalumu kutoka katika chama cha wananchi CUF Zakia Omar naye alitaka kurudishwa kwa utaratibu huo ambao alisema ulisaidia sana kudhibiti vitendo vya uhalifu. 

alisema kuondoshwa kwa hati za kusafiria kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kiasi kikubwa kumerudisha wimbi la vitendo vya uhalifu. 

hati ya kusafiri kati ya Tazania Bara na Zanzibar pasipoti iliondolewa katika miaka ya 1995,baada ya kubainika kuwepo kwa vikwazo vya usafiri katika nchi moja ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na kuonekana kwenda kinyume na katiba
.

CHANZO: Majira

20 Oct 2008


Now you will need a passport to buy a mobile phone under 'Big Brother' style scheme

Anyone buying a mobile phone could be forced to produce their passport as part of the plan for a huge surveillance database. 

Security chiefs want a national register of all 72million mobile phone users in the UK to help track terror plots or crime networks. 

Customers can currently buy prepaid mobile phones with cash, without providing personal details. 

There are some 40 million prepaid and unregistered mobile phones in Britain. 

Opponents claim determined terrorists or criminals will find it easy to sidestep the database by using foreign-registered mobile or satellite phones. 

The phone database will form part of a surveillance system proposed in the Communications Data Bill, unveiled by Home Secretary Jacqui Smith last week. 

It includes plans to log and store details of every phone call, email, text message and internet visit in Britain - including websites such as Facebook and eBay. 

A spokesman for Information Commissioner Richard Thomas said: 'We would expect that this information would be included in the database proposed in the draft Bill.'

SOURCE: Daily Mail

19 Oct 2008






CLICK HERE to read the story

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.