17 Dec 2008


Videos tu.tv
INTRO (T.I.):Life is an interesting journey; you never know where itll take you. Peaks and valleys, twists and turns, you can get the surprise of your life. Sometimes on the way to where you going you might think, this is the worst time in my life.But you know what, at the end of the road through all the adversity, if you can get where you wanted to be, you remember whatever dont kill you make you stronger, and all of the adversity was worth it. On your way to the top youll do anything. But how do you get your life back when you get there yeah thats my dilemma

A web developer has made thousands of dollars from George Bush after registering the lapsed domain name for his presidential library. 

George Huger bought the domain GeorgeWBushLibrary.com for just $10 (£6.60) after the web developers for the library website failed to renew it.

He then sold the domain back to the Bush family and their contractors for a whopping $35,000 (£23,000) - a 3,500% return on his investment.

GeorgeWBushLibrary.com is the official website for the presidential library of Mr Bush, located on the campus of Southern Methodist University in Dallas, Texas.

Jonathan Robinson, chief operating officer at domain registrar NetNames said opportunist speculators are so quick to pounce, "that brands, businesses and even former presidents can be at risk".

But internet and domain law expert Adam Taylor, principal at Adlex Solicitors, says there were several other options available.

He said: "It surprises me that they paid the $35,000 on the face of it. There are a whole range of options here."

Mr Taylor said the usual course in a case like this is to seek recovery of the domain name through arbitration under the "uniform domain name dispute resolution policy".

This protects rights owners where domain names have been registered and used in bad faith.

Court is also a possibility if it could be proven Mr Huger was misrepresenting himself as connected with the library, if he infringed a registered trade mark or if he broke the US laws on cybersquatting.

Mr Taylor added: "It looks to me as though there's a possibility the web development company paid it off their own back, perhaps out of embarrassment.

SOURCE: Sky News

16 Dec 2008



Chati ya Muntadhar al Zaid,mwandishi aliyemtupia viatu Rais Bush imepanda ghafla.Tayari charity organization moja huko Libya imetangaza kutoa tuzo kwa mwandishi huyo.

15 Dec 2008

Hii ni kwa mujibu wa mujibu wa Jamii Forums.For developing stories FUATILIA HAPA.

He had been hunted, kidnapped, and told he was filming his own execution. But CNN correspondent Michael Ware had no plans to leave Iraq. Now, it won’t leave him...CLICK HERE FOR THE FULL STORY.


14 Dec 2008

Makamu Wa Pili wa Rais wa TFF,"Ustaadh" Ramadhan Nassib (mbele kulia) akishangilia baada ya kushinda nafasi hiyo dhidi ya mpinzani wake Damas Ndumbaro katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo jijini Dar.Ila Ustaadh,mbona TFF sasa iko chini ya Yanga tupu?Tenga alikuwa Pan (mtoto wa Yanga),Nyamlani ni Yanga na wewe ndio kama vile.....just kidding!Big up,man.You made it.At least jamaa kadhaa wanaweza kusema "tuna mshkaji TFF...!!!".Picha na habari  kwa hisani ya MICHUZI

13 Dec 2008

Watanzania wengi wanapenda habari.Na siku hizi vyombo vya habari viko vya kumwaga.Hata hivyo,upatikanaji wa habari za uhakika bado ni tatizo.Kwanza,wanahabari wengi wa huko nyumbani wanapendelea zaidi kuripoti habari badala ya kuleta habari iliyochunguzwa.Leo hii ukitoka ughaibuni na vizawadi viwili vitatu kisha ukaitisha press conference na kudai unataka kuanzisha mradi flani,kesho yake habari hizo zitaripotiwa kama ulivyotaka.Na kama hiyo press conference itaambatana na makulaji na vinywaji basi si ajabu habari hiyo ikawa ukurasa wa kwanza.Of course,kuna exceptions kwenye magazeti kama This Day,Kulikoni,Raia Mwema,Mwanahalisi na mengine machache.

Tatizo la pili katika upitakanaji wa habari liko katika mafungu mawili.Kwanza,japo magazeti ni mengi,wenye uwezo wa kununua bado si wengi sana.Bei ya wastani ya gazeti ni shilingi 400.Ukizingatia ugumu wa maisha,ni vigumu kutoa kiasi hicho kwa gazeti ambalo ukishasoma linakuwa halina matumizi mengine ya muhimu.Pili,upatikanaji wa habari kwa njia ya runinga na redio bado ni mgumu katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.Nilipokuwa Ifakara hivi karibuni,nilibaini kwamba ili uweze kukamata matangazo ya vituo vyote vya televisheni ni lazima uwe na "ungo".Sasa unaweza ku-imagine ni watu wangapi wenye uwezo wa kumudu gharama za kununua na ku-install satellite dish.

Pamoja na "chengachenga" za hapa na pale,redio imeendelea kuwa tegemeo la wengi hasa vijijini.Na ukipta hapa na pale utakuta wazee wetu nyakati za jioni wakisikiliza matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC au Deutsche Welle.Na kupitia matangazo hayo ndipo mzee wangu mmoja niliyeongea nae kwa simu jioni ya leo alipata habari kwamba kuna wawekezaji kadhaa "walioingizwa mkenge" na tapeli mmoja,Bernard Madoff,katika kile kinachofahamika kama Ponzi Scheme.Mzee huyo aliniuliza inakuwaje "wazungu" wenye uelewa mkubwa wa mambo waliweza kuhadaika na kushiriki "upatu" huo?Sikua na jibu kwa vile habari yenyewe ilikuwa bado ngeni kwangu.Kama mwenzangu nawe hujaipata,BONYEZA HAPA kuisoma kwa undani.

The crisis in Somalia is getting worse as a force of Islamic militants, led by a hardline wing known as al-Shabab, seizes more territory, threatening the fragile transitional government. The Ethiopian troops that are backing the government are likely to leave the country soon, and experts warn this may lead to the government's collapse and the potential of Somalia becoming a safe haven for terrorists.

"They're expanding their reach,"said Jeniffer  Cooke,head of the Africa program at the Center for Strategic and International Studies in Washington. "They've seized a number of key port towns - Merka, Kismayo - and are really driving the chaos that is engulfing Mogadishu at this point."

There has been no real central Somali government since 1991. Only U.S. aid and the presence of Ethiopian troops who invaded in 2006 have kept the current transitional government in Mogadishu from collapse.

Although Ethiopia has announced it would pull out of Somalia by the end of the year, the government has hinted it could delay the move. Still, a withdrawal could prompt African Union peacekeepers to follow suit. 


U.S. State Department spokesman Sean McCormack says Washington is trying to avert a collapse in Somalia. "We're trying to work through the international system, that is trying to find a way that you can have a responsible international force in Somalia to help provide some security and therefore some stability," McCormack said. "And allow some of these weaker institutions to start to take hold in a positive way."

The concern in Washington is that if the militant al-Shabab takes control of Somalia the country could become a launching ground for terrorists.

Joint Chiefs of Staff Chairman Admiral Michael Mullen spoke about the danger at a news conference Wednesday."I am concerned about the potential for a safe haven in Somalia as I am in Yemen. I try to pay a lot of attention to the evolution of potential safe havens, these two in particular and specifically to the one in Somalia," Mullen said. "So, I'm extremely concerned about that."

The United States considers the multi-clan al-Shabab a terrorist group. 

It practices a harsh form of Islamic law as seen in this recent video of a beheading released by the militants. Its propaganda videos, and its terror tactics have led some to believe the group may have ties to al-Qaida. 

"Whether or not the links are direct, we don't know," Cooke stated. "There have been former al-Qaida operatives within Mogadishu responsible for the bombings in Dar Es Salaam and in Kenya in 1998, but certainly there's a potential there, a very strong potential for increasing support and linkage with al-Qaida."

Cooke and other experts say the prospect of further violence and a deepening humanitarian crisis in Somalia could become a major problem for the incoming Obama administration. 

SOURCE: VoA

Kwenye uchambuzi makini,vitu kama laana,nuksi au bahati mbaya huwa havileti maana yoyote.Lakini katika maisha yetu kijamii tunafahamu kuwa jambo likiandamwa na kutofanikiwa linaweza kuhusishwa na laana au bahati mbaya.Na kama kuna sekta ambayo imekuwa ikiandamwa na matatizo kwa muda mrefu huko nyumbani basi ni usafiri.

Ukiangalia usafiri kuanzia kwenye cities hadi vijijini utabaini kwamba kadri unavyozidi kwenda chini (city ikiwa juu na kijiji chini) ndivyo matatizo yanavyozidi kuongezeka.Matatizo ya daladala jijini Dar ni "cha mtoto" ukilinganisha na namna ya kufika sehemu iitwayo Tanganyika Masagati (sijui kama ushawahi kuisikia).
Na hata hapo Dar,kero ya usafiri inazidi kuongezeka kadri unavyoelekea kwenye vitongoji vya jiji hilo.Ushawahi kufika Pemba Mnazi?Mara kwa mara tunasikia mipango mipya ya kuboresha usafiri,hasa jijini Dar.Tulisikia kuwa vipanya vingekuwa phased out lakini wajuzi wa mambo walishajua kuwa hilo ni changa la macho kwa vile wamiliki wengi wa vipanya hivyo ndio haohao wanaotuzuga kwenye media kuwa vipanya ni kero.Wanajuaje kero za vipanya ilhali wao wanazungushwa na ma-VX au Vogue yao yenye viyoyozi?
Tukiachana na usafiri wa barabara,wa majini ndio wa roho mkononi zaidi.Na hapa sizungumzii meli au boti pekee.Angalia pale Kigamboni!Au kama unadhani pale ndio kiboko cha matatizo basi jaribu kwenda kivuko cha Mto Kilombero!Nilipokuwa huko hivi karibuni nilihabarishwa kwamba kivuko kipya kilichotarajiwa kutatua kero katika eneo hilo kiliishia kusomwa na maji.Kisa?Bila shaka fisadi flani kanunua kivuko mtumba.Kama kawaida,hakuna aliyewajibika hadi leo.

Hapo feri jijini Dar nako ni ngonjera kila siku.Mara sijui kuna daraja litajengwa,mara sijui kuna nini kitafanyika.Kama kawaida yetu,tunasubiri litokee janga flani kisha ndio mabwana mipango wetu waje na mipango mipya ya kujali maisha yetu.Vivuko vingi huko nyumbani ni sawa majeneza yanayoelea.Hakuna la muhimu tulilojifunza kutokana na janga la Mv Bukoba,na sijui hata kama policy makers wetu wanakumbuka janga hilo.
Usafiri wa reli ndio balaa.Zamani za kale,ukiwa ndani ya treni ya Tazara ungeweza kujiskia kama uko kwenye treni ya nchi zilizoendelea.Siku hizo tulikuwa tunasafiri na watalii kibao.Si unajua reli ya Tazara inakatiza katika hifadhi ya Selous,kwahiyo kwa wenzetu wanaotafuta vivutio safari hiyo ilikuwa ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja:kufikishwa waendako na kupata uhondo wa wanyama mbugani.Hivi sasa Tazara iko dhoful khal,inakaribia kukata kauli.Mara ya mwisho niliposafiri kwa Tazara,jamaa mmoja Mzambia alinieleza bayana kuwa wanasubiri tu kifo cha shirika hilo.
Huko Reli ya Kati ndio habari mbaya zaidi.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtu anayejiita mwekezaji kuwa anapewa fedha na serikali kulipa mishahara ya watumishi?Huyu ni m-babaishaji tu.Watu pekee wanaofahamu sababu za kwanini hadi leo TRL bado iko mikononi kwa wababaishaji hao wa kidosi ni Watanzania wenzetu wachache wanaoendela kuamini kwamba ipo siku TRL itasisima na kujiendesha yenyewe.Wajuzi wa mambo wanaiona TRL kama kipofu anayetafuta sindano kwenye chumba chenye kiza totoro,huku sindano hiyo ikiwa haipo humo!

Kitu pekee kitachowakimbiza Wahindi hao ni janga.Kwanza tukubaliane kwamba kama wangekuwa hawapati faida katika huduma yao mbovu wasingeendelea kuwepo hadi leo.Si unawajua Wahindi linapokuja suala la faida?Yes,janga ndio itawakimbiza wadosi hao.Mungu aepushe janga hilo lakini likitokea la kutokea na kisha tukaishia kumlaumu Mungu,atatuadhibu vikali.Hawa wababaishaji hawajafanya matengenezo ya reli,wanasafirisha abiria kwenye mabehewa ambayo hata ng'ombe hawastahili kupanda,na ratiba zao ni za bahati nasibu.Yayumkinika kuhitimisha kuwa mazingira hayo ni sawa na a catastophy in the making.And once that happens,God forbid,hawa jamaa wataingia mitini just like wawekezaji wababsiahji wengine wanavyotukimbia baada ya kuukamua uchumi wetu.Na huwezi kuwalaumu kwani hata mwenye nyumba ambaye anaacha mboga yake jikoni pasipo kuhofia nyau,hawezi kuwalaumu paka wakikwiba mboga hiyo kukidhi njaa zao!

Hatuwezi kuuzungumzia usafiri wa anga pasipo kutaja AIR TANZANIA.Uongozi mmoja umeupisha mwingine one times too much,nembo zimebadilishwa mara lukuki,mgogoro mmoja umeupisha mwingine,lawama za wasafiri ndio usiseme!Hivi Waethiopia ni wachawi kwa namna walivyoweza kuifanya Ethiopian Airlines kuwa moja ya mashirika ya ndege ya mfano barani Afrika?Vipi kuhusu watani zetu na Kenyan Airways yao?Sisi tunashindwa nini?Hivi kuna ugumu gani wa kukodi ndege,kutoa huduma ya kuridhisha,kutumia itakayopatikana kununua ndege zaidi na kisha kutanua safari katika maeneo mbalimbali duniani?
Tatizo kubwa la Air Tanzania,or whatever its current name is,ni ufisadi.Na chanzo cha ufisadi huo ni hao wanaofanya teuzi pasipo kuzingatia rekodi.Hivi hawa viongozi wa sasa wa ATC wana sifa stahili za kulitoa shirika ICU na kulirejesha angani?Majuzi David Mattaka aliruka kimanga alipoulizwa iwapo ndege za shirika hilo zimepigwa stop kutoa huduma (kutoa non-existent huduma?) kabla ya kukiri muda mfupi baadaye kwamba habari hiyo ni ya kweli.Hivi background ya mtu huyu inaleta matumaini yoyote ya kufufuka kwa ATC?Na hapo sizungumzii maisha yake binafsi (hapa sio mahala pake).

Sababu kubwa ya nuksi,mikosi na bahati mbaya zinazoiandama sekta ya usafiri huko nyumbani ni uksefu wa uzalendo.Hilo linaanzia kwa hao wanaofanya uteuzi wa kuongoza taasisi zinazotoa huduma za usafiri wa angani,majini,barabara na reli.Pia uteuzi usiozingatia rekodi kwenye mamlaka zinazosimamia sekta hiyo ni tatizo jingine la msingi.Takriban maeneo yote yaliyoguswa katika uchambuzi huu yana Waziri,Naibu Waziri,Katibu Mkuu,Naibu Katibu Mkuu,Mkurugenzi Wizarani na Mkurugenzi shirikani,mameneja lukuki,Wenyeviti na wajumbe wa bodi ambao vikao vyao ni about posho tu na sio maendeleo ya shirika husika,na mlolongo mwingine wa watendaji.Sasa hapo inahitajika domino effect top to down.Waziri akiweka mbele uzalendo na uwajibikaji hao wote chini yake watatimiza majukumu yao.Lini tutapata Waziri ambaye ataapa kuwa lazima AIR TANZANIA itarudi hewani,TRC itafufuka kutoka katika wafu,TAZARA itapata uhai mpya,vivuko vinakuwa na maana ya vivuko,na hatua nyingine nyingi.Na isiishie kuapa tu kwani waheshimiwa wneig tu huapa lakini huishia kufisadi nchi na viapo vyao.

Uzalendo ni kuweka maslahi ya nchi mbele badala ya maslahi binafsi,Uzalendo ni kuchagua watu wenye sifa na uwezo na sio ku-recycle watendaji wenye sifa zisizostahili personally na professionally.It can be done,if wenzetu wakiamua ku-play their part....au just kusema YES WE CAN!

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.