29 Jan 2009

MWANZONI NILIPOONA KATUNI HII SIKUELEWA INAMAANISHA NINI.LAKINI BAADA YA KUSOMA KATI YA MISTARI (READING BETWEEN THE LINES) NIKAKUMBUKA SIMULIZI KUHUSU MUUNGWANA FLANI (ANAYEHUSISHWA NA UFISADI WA TWINI TAWAZ ZA BoT) KWAMBA ALIKUWA MKARIMU SANA KWA BAADHI YA AKINADADA WAREMBO NA WENYE MAJINA KIASI KWAMBA HAKUSITA "KUMUIGA" OPRA KWA KUGAWA MAGARI BURE (OFKOZ,TOFAUTI NI KWAMBA OPRA ALITOA ZAWADI ZISIZO NA MASHARTI WAKATI MHESHIMIWA ALIKUWA AKIGAWA "GARI NYEKUNDU" KWA MASHARTI YANAYOFANANISHWA NA "ADHABU YA KIFO").


HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO KISHA TUIJADILI PAMOJA

MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Emmanuel ole Naiko, amesema neno ufisadi linawatisha wawekezaji, hivyo kuwataka wananchi kulitumia kwa umakini huku
wakiweka uzalendo mbele.

Alisema wakati taratibu za kupambana na rushwa zikiendelea, kipaumbele kielekezwe kwenye uchumi na maendeleo kwa ujumla ili kulikwamua taifa, kwani kiwango cha rushwa kilichopo si kama kilichopo katika nchi zilizoendelea.

Naiko alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima, yaliyofanyika katika ofisi za TIC, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo alisema hakuna shaka kwamba rushwa na uwekezaji, haviendi pamoja lakini ni vema suala hili likachukuliwa kwa umakini na kutanguliza uzalendo kwa masilahi ya taifa.

“Tunatakiwa tuwe na uzalendo pale penye sifa mbaya, tulichukulie kwa umakini ili tusiendelee kulijengea sifa mbaya taifa letu. Tuziache taratibu na sheria zetu zifanye kazi, ikiwemo kuwapeleka mahakamani watuhumiwa,” alisema.

Alisema Tanzania haiongozi kwa rushwa lakini inaonekana hivyo kutokana na msimamo wa serikali kuweka wazi masuala ya rushwa. Akitolea mfano wa meya aliyeuza kiti cha useneta huko Illinois, nchini Marekani, Ole Naiko alisema hali hiyo inaashiria ni kwa jinsi gani kulivyo na rushwa katika nchi tajiri kuliko zile maskini.

“Sisi tuna rushwa ndogo ndogo, hatuwezi kuongoza kwa rushwa, nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa. Kwanza tuna taasisi za kupambana na rushwa na tunayaweka haya masuala wazi, wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao
zionekane mbaya,” alisisitiza. Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi aliwataka Watanzania kulifikiria taifa lao wakati likipambana na rushwa na kusisitiza kuwa wananchi wajadili jinsi ya kuliletea taifa maendeleo.

Akizungumzia mafanikio ya mkutano wa Sullivan uliofanyika mwaka jana, alisema huandaliwa kwa lengo la kuwaunganisha Wamarekani na Waafrika katika kujadili mustakabali wa jinsi ya kuondokana na hali ya umaskini inayowakabili.

Pamoja na hilo, alikiri kwamba mafanikio yameonekana hasa kwa wawekezaji wa Kimarekani, kwani mkutano huo umeifanya Marekani itoke nafasi ya nane hadi ya nne kwa uwekezaji nchini, ikifuatiwa na nchi za Uingereza, Afrika Kusini na Kenya.

Kuhusu safari za Rais Jakaya Kikwete nchini Marekani, Naiko alisema zimewawezesha Wamarekani kuifahamu vema Tanzania, hivyo kuvutika kuwekeza zaidi. Alisema kwa sasa kituo chake kina mpango mahususi wa kutumia balozi zake katika kuitangaza Tanzania, ikiwa ni pamoja na kuweka balozi zake katika nchi zenye uwezo wa kuwekeza nchini.


HIVI KIPI CHA BUSARA ZAIDI: KUTOPIGA KELELE KUHUSU UFISADI KWA VILE WAKIFANYA HIVYO WATAWATISHA WAWEKEZAJI AU KUPIGA KELELE KWA NGUVU ILI MAFISADI WATOKOMEE NA KISHA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI WENGI ZAIDI? HIVI HUYU OLE NAIKO ANATAKA KUJIFANYA HAELEWI KWAMBA MASLAHI YA MTANZANIA YANA UMHIMU ZAIDI KULIKO HAO WAWEKEZAJI (AMBAO MIONGONI MWAO NI MAFISADI VILEVILE)?

MASLAHI YA TAIFA YATALINDWA TU ENDAPO KELELE DHIDI YA MAFISADI ZITAENDELEA KWA NGUVU KUBWA NA KUWASHIRIKISHA WATU KAMA OLE NAIKO NA WALA SIO KWA KUONGEA CHINICHINI KWA KUHOFIA KUWATISHA WAWEKEZAJI.HIVI MAFISADI WAKISHAIFILISI TANZANIA HAO WAWEKEZAJI WATAKUJA KUWEKEZA KWENYE NINI?

TUANGALIE KWA MTIZAMO MWINGINE.HIVI SI KWELI KWAMBA NI VITENDO VYA UFISADI,NA SIO KELELE ZA WANANCHI KUHUSU MATENDO YAO,YANAYOCHAFUA SIFA YA TANZANIA NA HIVYO KUWATISHA WAWEKEZAJI?HUYU JAMAA VIPI?LAKINI SIMSAHNGAI SANA KWA VILE ALISHAWAHI KUCHEMKA HUKO NYUMA ALIPOHUSISHWA NA TUHUMA ZA MATAPELI WA RICHMOND NA AKAKIMBILIA KUDAI KWAMBA ANAFANYIWA HIVYO (KUHUSISHWA) KWA VILE YEYE NI MTU WA MONDULI (KAMA LOWASSA).
MFANO WAKE KWAMBA GAVANA (NA SIO MEYA KAMA ALIVYODAI) WA ILLINOIS,ROD BLAGOJEVICH,KUKABILIWA NA TUHUMA ZA "KUUZA KITI" CHA USENETA INAASHIRIA KUWA RUSHWA NI KUBWA KATIKA NCHI TAJIRI KULIKO MASIKINI UNASHINDWA KUZINGATIA UKWELI KWAMBA RUSHWA NI RUSHWA,IWE MAREKANI AU TANZANIA,TENA PENGINE RUSHWA KATIKA NCHI TAJIRI INAWEZA KUWA NA ATHARI NDOGO KULINGANISHA NA NCHI ZA MASIKINI KWA VILE ANGALAU WENZETU WANA MECHANISM KADHAA ZINAZOWEZA KUM-BANA MTU ALIYEPATA MADARAKA KWA NJIA YA RUSHWA.LA MUHIMU HAPO SIO GAVANA HUYO KUWA KISHIRIO KWAMBA RUSHWA IPO MAREKANI BALI NAMNA WENZETU WANAVYOJITAHIDI KUPAMBANA NAYO.SIJUI SIE TUNA AKINA BLAGO WANGAPI...KUBWA ZAIDI NI KILE WAINGEREZA WANACHOSEMA TWO WRONGS DO NOT MAKE A RIGHT.KUWEPO KWA RUSHWA MAREKANI,AU KWINGINEKO KOKOTE KULE HAKUWEZI KUHALALISHA RUSHWA WALA KUWA SABABU YA SIE KUPUNGUZA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA ETI KWA VILE TU "MBONA HATA KWA WENZETU IPO"!

WAKATI OLE NAIKO ANASEMA (NAMNUKUU) "Sisi tuna rushwa ndogo ndogo....nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa....wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao zionekane mbaya..." INAELEKEA ANASAHAU KWAMBA HIYO ANAYOITA RUSHWA NDOGO NDOGO (SIJUI KAPATA WAPI KIPIMO CHA KUJUA RUSHWA KUBWA NA NDOGO) INA MADHARA MAKUBWA SANA KWA NCHI MASIKINI KAMA AMBAVYO HIZO RUSHWA KUBWA ZINAVYOWEZA KUWA NA MADHARA KATIKA NCHI TAJIRI.HALAFU MBAONA ANAJICHANGANYA ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI "ZINAZOONGOZA KWA RUSHWA" (KWA MUJIBU WAKE) HAZIWEZI KUWEKA RUSHWA HADHARANI KWA VILE HAZITAKI ZIONEKANE MBAYA LAKINI HAPO HAPO AMETOA MFANO WA HUYO GAVANA WA ILLINOIS!?JE WANGEKUWA HAWATAKI HAYO YAONEKANE YEYE OLE NAIKO NA SIE TULIO NJE YA MAREKANI TUNGEJUAJE?

HALAFU ARGUEMENTS ZA HUYU MHESHIMIWA ZINAWEZA KUWA NA MADHARA KULIKO HICHO ANACHOJARIBU KUTUELEZA.HIVI TUMWELEWEJE ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI ZINAONGOZA KWA RUSHWA,HALAFU WAWEKEZAJI ANAOTAKA TUSIWATISHE KWA NENO UFISADI WANATOKA KWENYE NCHI HIZOHIZO ANAZODAI ZINAONGOZA KWA RUSHWA!!!!ANATAKA TUSIWATISHE ILI WAJE KUENDELEZA RUSHWA TANZANIA?

HOJA YENYE UZITO NI KWAMBA UFISADI SIO TU UNAATHIRI SEKTA YA UWEKEZAJI BALI PIA UNAATHIRI TAIFA LENYEWE AMBALO TUNATAKA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI HAO.KWA MWENYE BUSARA ZA KUTOSHA HOJA YA MSINGI NI KUZIDISHA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI NA WALA SIO HOFU KWAMBA NENO MAFISADI LITAWATISHA WAWEKEZAJI.JINGINE LA MUHIMU NI KILE ALICHOSEMA MWENYEKITI MAO KWAMBA NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK.KUTUHUMU MATAIFA TAJIRI KUWA YANAONGOZA KWA RUSHWA PASIPO KUTOA TAKWIMU ZA KUSAPOTI HOJA HIYO,SIO TU INAWEZA KUWACHUKIZA HAO WAWEKEZAJI KWA VILE WANAWEZA KUDAI WANATUHUMIWA PASIPO SUPPORTING EVIDENCE,BALI PIA KUNAMPUNGUZIA CREDIBILITY MTOA HOJA HASA IKIZINGATIWA KUWA ENEO ANALOZUNGUMZIA NDILO ALILOKABIDHIWA DHAMANA NA TAIFA KULISIMAMIA KWA UMAKINI.

28 Jan 2009


Iceland is set to appoint the world's first openly gay woman as interim prime minister - a former flight attendant who rose through the political ranks to become a cabinet minister...CONTINUE

27 Jan 2009

Kujichua,punyeto,puli,nk.Majina ni mengi kuhusu tendo hili ambalo inaaminika kuwa "faraja binafsi miongoni mwa wapweke wengi" japo huzungumziwa hadharani kwa nadra mno.Sasa wanasayansi wanadai kwamba kujichua (masturbation) kunaweza kuwa kinga dhidi ya kansa ya kibofu (prostate cancer) kwa walio na umri wa miaka 50 na zaidi.Jenga picha...unamkuta mzee wa miaka hamsini na kadhaa "anapata kinga na sabuni yake mkononi..."Au inagundulika kwamba kisa cha kila Revola inayoachwa bafuni kupotea kimiujiza ni baba mwenye nyumba "kuitumia kama kinga ya kansa"....Enewei,BONYEZA HAPA kusoma habari kamili.


Lakini wakati nyeto inaelekea kuwa habari njema kwa wazee,wanasayansi wanadai kwamba "ngono binafsi" kwa vijana wenye kati ya miaka 20-30 inaweza kupelekea kansa hiyohiyo ya kibofu.

Picha kwa hisani ya BongoPicha.JAPO KANUNI MUHIMU KATIKA SHERIA INATAMKA BAYANA KUWA MTUHUMIWA ANABAKI KUWA MTUHUMIWA HADI ATAPOTIWA HATIANI,LAKINI YAYUMKINIKA KUHISI KWAMBA HUKO MITAANI ISHU YA HUYU MHESHIMIWA LIUMBA ISHATOLEWA HUKUMU ZAMANI HIZO...NA WALA HAIHUSIANI NA HIZO GHOROFA PACHA ZA BENKI KUU.NAAMINI WANAOFATILIA VIMBWANGA VYA VIGOGO WATAKUWA WANAELEWA NAZUNGUMZIA NINI.KWA HABARI KAMILI KUHUSU KILICHOMPANDISHA KIZIMBANI LIUMBA BONYEZA HAPA.

26 Jan 2009


Gavana wa zamani wa "Benki Kuu" ya Marekani,Allan Greenspan
Rais Mstaafu wa Marekani,George W Bush
Rais Mstaafu wa Marekani,Bill Clinton

Waziri Mkuu wa Uingereza,Gordon Brown
Bonyeza HAPA kwa orodha kamili na maelezo.

25 Jan 2009


Hatimaye katika kukabiliana na wimbi la mauaji ya albino,Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameagiza leseni za waganga wa jadi wote zifutwe.Majuzi,Pinda alikaririwa akiagiza wananchi kuchukua sheria mkononi kwa kuwaua "wauaji wa maalbino".Hatua zote mbili zinaweza kutofanikiwa kwa vile inaelekea kana kwamba zimechukuliwa pasipo kufanyiwa utafiti wa kina.


Kuruhusu wananchi wafanye "jino kwa jino" dhidi ya wanaoua maalbino kunaweza kulipeleka Taifa mahala pabaya.Taasisi pekee yenye mamlaka ya kuhukumu ni mahakama zetu,na hizo ndio zinazoweza kuhakiki makosa halasi tofauti na majungu,chuki,visasi,nk na haki inatarajiwa kuwa imetendeka pindi hukumu itapokuwa ya kifo au mshtakiwa kuachiwa huru kulingana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani.Hilo haliwezekani katika "mahakama za jino kwa jino mitaani".Si ajabu watu waliokosana kwa sababu zao binafsi wakishia kupigana mapanga kwa kisingizio cha "kudhibiti mauaji ya maalbino".Ikumbukwe kuwa ni rahisi kuruhusu uvunjifu wa sheria lakini ni zaidi ya vigumu kurejesha heshima na utiifu kwa sheria.


Tuje kwa hili la kufuta leseni za waganga wa jadi.Je amri hii inamaanisha ni marufuku kwa mtu yeyote kujihusisha na uganga wa jadi au...?Sijaelewa vizuri hapo lakini nahisi inamaanisha hivyo kwani katika hali ya kawaida,kufanya shughuli inayohitaji leseni pasipo kuwa na leseni husika ni uvunjifu wa sheria.Swali la kwanza,hivi ni waganga wa jadi wangapi wenye leseni (tukiachana na hao Maprofesa wanaojitangaza kwenye magazeti kuwa wanatibu ukimwi,wanawezesha kufaulu pasipo kusoma,na miujiza mingine)?Nauliza hivyo kwani haitaleta mnaana yoyote kumfutia mtu leseni ambayo hajawahi kuwa nayo hata siku moja.Swali la pili,je utekelezaji wa amri hiyo utasimamiwa vipi?Polisi watazungukia mganga mmoja hadi mwingine nchi nzima kuhakikisha kuwa hafanyi uganga?
Swali la tatu,je tumefikia hatua ya kufanya maamuzi kwa kigezo cha "samaki mmoja akioza basi wote wameoza"?Nauliza hivyo kwani tafsiri ya moja kwa moja ya kuwafutia leseni masangoma ni kwamba wao ndio wahusika muhimu katika suala la mauaji ya maalbino.Hii "overgeneralization" inatoka wapi?Mbona wale wazembe wa Muhimbili walipompasua kichwa mgonjwa wa goti na wa goti akapasuliwa kichwa walioadhibiwa ni madaktari husika tu na sio kada nzima ya madaktari hapo Muhimbili au nchi nzima?Au mbona ilipobainika kwamba kuna uhuni umefanyika pale BoT kwenye ishu ya EPA,aliyefukuzwa kazi ni Ballali pekee na wengine wameendelea kuwa madarakani hadi leo?Au mbona aliyekuwa balozi wetu huko Italy alipokumbwa na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma haikupelekea kutimua mabalozi wote?Sasa iweje "uhuni" wa baadhi ya waganga wa jadi upelekee hukumu kwa wote wanaohusika kwenye taaluma hiyo (na yayumkinika kusema kuwa wengi wao-hususan vijijini-ni waadilifu katika kazi yao)?


Naomba nisisitize kwamba hapa simaanishi two wrongs make a right.Hapana,najaribu kuangalia approaches za nyuma katika kukabiliana na matatizo mbalimbali na namna zinavyokinzanna na hii ya ku-revoke leseni za waganga wa jadi.


Kwa wanaofahamu umuhimu wa tiba asili katika jamii husasan katika kipindi hiki cha uchangiaji wa gharama kwenye public health facilities,ni dhahiri hatua ya kuwafutia leseni waganga wote wa jadi itaathiri Watanzania wengi wanaotegemea huduma hizo (aidha kutokana na imani,nature ya maradhi yao au uwezo duni katika kumudu gharama za huduma za afya hospitalini).


Japo ni muhimu sana kutafuta ufumbuzi wa haraka kukomesha mauaji dhidi ya maalbino,ni muhimu zaidi kutumia common sense and viable approaches kuliko hatua ambazo pamoja na nia zake nzuri zinaweza kutuletea matatizo zaidi.Tukirihusu sheria zivunjwe kwa kuruhusu kuua wanaoua maalbino (badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vya dola) basi tusishangae pindi baadhi ya wananchi watakapoamua kuchukua sheria mkononi dhidi ya mafisadi,kwa mfano,badala ya kusubiri kesi zilizoko mahakamani,ripoti za tume,nk

23 Jan 2009



CLICK HERE for more on this story.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.