22 Apr 2009



KWA MFANO KATINA GAZETI LA SANI KUNA HABARI KWAMBA MWANANCHI MMOJA ALIYEPANDA MBEGU ZENYE THAMANI YA SHS MILIONI 20 "AMEPARALAIZI" (AMEPOOZA)UPANDE MMOJA WA MWILI WAKE BAADA YA HABARI KUWA HUENDA MBEGU YAKE HIYO IKAWA "IMEOZA ARDHINI".....KIBAYA ZAIDI NI KWAMBA MBEGU HIZO (SHS MILIONI 20) ZILIKUWA NI FEDHA ZA URITHI WA FAMILIA,NA "MPANDA MBEGU" HUYU ALITUMIA TU NAFASI YAKE KAMA MWEKA HAZINA WA FUNGU HILO AKIAMINI MBEGU ZINGEZAA FAIDA NA KISHA ANGEREJESHA KIWANGO HICHO......




Captured Somali pirates,like Abduwali Abdukhadir Muse (pictured above,smiling as he arrives on the U.S soil) are most likely to seek for asylum in the U.S. upon completion of their jail terms.Compared to the current situation in Somalia,life in a U.S. prison could most probably be perceived as a once-in-lifetime-luxury many Somalis could only imagine.Couldn't this encourage even more pirate attacks in the future?



May be that's why the captured pirate is all smiles....

1 When presidents get invited to the annual Gridiron Dinner for a night of political skits among the Washington press corps, they always go. Not this one, who became the first sitting President politely to decline.

2 We have had lots of canine companions on the rugs of the Oval Office, but Obama's is the first first whose name, Bo, is also his master's initials. Better still, Portuguese water dogs come with fine Democrat credentials – Senator Ted Kennedy has litters of them

3 Americans have become accustomed to knowing that the so-called "enemy combatants" were being held at a safe distance – at Guantanamo Bay. But BO comes into office and instantly declares he will close it within a year.

4 Never mind the Bush policy of hostility to Iran, BO has been making tentative overtures, asking Tehran to cooperate on Afghanistan and edging towards face-to-face talks on its nuclear programme without preconditions.

5 In his first formal press conference, BO took a question from a correspondent of The Huffington Post, the political blog site. In this White House, old journalism must compete with new journalism.

6 As soon as the first cherry buds were bursting in Washington, Michelle Obama, accompanied by local school children, was breaking sod for the First Family's organic vegetable patch.

7 America is no longer shrugging its shoulders at the drug cartel violence shaking Mexico. BO and Secretary of State Hillary Clinton acknowledged that the US is fueling the problem, supplying guns and consuming the drugs.

8 The Beast. The new first limousine – a Cadillac with more armour than your average tank and bullet-proof windows – has already prowled the streets of London, Strasbourg, Prague and Istanbul. And Pennsylvania Avenue on Inauguration Day.

9 Rush Limbaugh is the conservative blowhard on the radio who millions of Americans long ago learned to love or hate. But now his visibility, ratings and influence have soared. Some even tag him the unofficial head of the Republican opposition.

10 When Nato fed live footage of Barack and Michelle arriving for a dinner hosted by Angela Merkel into a packed press room, scores of normally cynical reporters rose to their feet to clap...CONTINUE

SOURCE: The Independent


21 Apr 2009

Shule ya Sekondari ya kutwa ya Marambo yenye wanafunzi 253 ya kidato cha Kwanza hadi cha Nne , iliyopo Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi ina mwalimu mmoja. Mkuu wa shule hiyo, Saidi Mbutuka ndiye pekee aliye shuleni hapo anayelazimika kushika nyadhifa zote.

Mbutuka aliliambia gazeti hili kuwa hali hiyo inatishia mustakabali wa elimu kwa wanafunzi shuleni hapo kwa kukosa elimu inayostahili. ''Mimi ndiye mkuu wa shule, ndiye mwalimu wa zamu, mwalimu wa taaluma, kila siku za kazi natakiwa kuingia katika madarasa yote manne, kwa siku ninakuwa na vipindi zaidi ya 10'', alisema.

Aliongeza, ''kwa hali hiyo hata kama ningekuwa mwalimu mzuri, kuna kila sababu ya kutilia mashaka na ubora wa elimu, mimi ni mwalimu wa masomo ya Sanaa, lakini nalazimika kufundisha Sayansi,'' alisema Mbutuka.

Alifafanua kuwa tatizo hilo limejitokeza mwaka huu baada ya walimu wanne waliokuwa shuleni hapo kwenda kusoma. 'Tunao wanafunzi wa kidato cha Nne ambao wanahitaji wafanye mtihani wa kuhitimu elimu yao, hivi tujiulize nini watavuna wanafunzi hawa kwa kufundishwa na mwalimu mmoja ambaye pia ndiyo nguzo kwa wanafunzi wa vidato vingine,'' alihoji.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo, akiondoka kwenda mjini hulazimika kuwatawanya wanafunzi au kuwaacha chini ya uangalizi wa wanafunzi wenzao ambao ni viongozi.
Mbutuka alibainisha kuwa pamoja na tatizo hilo shule hiyo inakabiliwa na tatizo sugu la mdondoko wa wanafunzi unaotokana na wanafunzi hao kukimbilia katika machimbo ya madini ya Miruwi, Nachianji na Mituguru yaliyopo jirani na shule hiyo.

Alisema mwaka 2006, wanafunzi 53 waliripoti shuleni hapo hata hivyo waliobakia ni 31, wakati mwaka 2007 wanafunzi walioripoti walikuwa 111 waliopo 73. Mwaka 2008 wanafunzi 80 waliripoti na waliopo ni 50. Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Nachingwea, Bakari Mussa, alikiri kuwapo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa halmashauri inashindwa kuwahamishia walimu shuleni hapo kutoka shule zingine ili kupunguza ukubwa wa tatizo kutokana na kukosa fedha za uhamisho.

''Kuna waraka wa serikali unaomtaka mwajiri kutomhamisha mtumishi yeyote bila kumlipa stahiki zake, kwa sababu halmashauri haina pesa tunashindwa namna ya kuiisaidia shule hiyo, lakini uwapo wa tatizo hilo sote tunautambua'' alisema Mussa.

CHANZO:Habarileo


HALAFU 2010 CCM WATAKUJA KUTUIMBIA MAFANIKIO KATIKA SEKTA YA ELIMU,NA KUDAI WAPEWE TENA MUDA WA KUIPELEKA NCHI YETU WANAKUJUA WAO.MIAKA ZAIDI YA 40 BAADA YA UHURU BADO TUNAKUWA NA SHULE YENYE MWALIMU MMOJA?WATETEZI WATASEMA SIE MASIKINI.MASIKINI GANI ANAYEWALIPA WABUNGE ZAIDI YA 300 SHS MILIONI 7 KWA MWEZI?MASIKINI GANI ALIEIBIWA BILIONI 40 NA KAGODA LAKINI ANAMWONEA AIBU HATA KUMTAJA HADHARANI?






Baraza la Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) limepitisha uamuzi wa kuishirikisha Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhakiki vyeti vya wote wanaoomba kuwania nafasi za kisiasa ili sifa zao kielimu zitambulike.

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya, aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, TCU imewasiliana na NEC kwa barua, ili utaratibu huo uanze kutumika katika uchaguzi mkuu ujao mwakani.

Nkunya alitoa taarifa hiyo wakati akizungumzia maonyesho ya vyuo vikuu yaliyoandaliwa na TCU yatakayoanza kesho hadi Aprili 24, mwaka huu. “Baraza letu limepitisha uamuzi ili watu wanaotaka kugombea nafasi za kisiasa, vyeti vyao vihakikiwe, ili akipita sifa ijulikane rasmi kama ni daktari basi awe daktari na si daktari feki,” alisema Profesa Nkunya.

Hatua hiyo ya tume inatokana na kilichoelezwa na Nkunya kuwa ni kukithiri kwa vyuo na vyeti bandia nchini, jambo ambalo alisema wamejipanga kulivalia njuga kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha Tanzania haiangamii kitaalamu na kitaaluma.

Alisema orodha ya vyuo visivyotambulika vya nje ambavyo Watanzania wengi wakiwamo mawaziri na wabunge wamesoma, ni ya kweli na kwamba kama kuna mtu anahisi kuonewa ruhusa kwenda mahakamani...ENDELEA

CHANZO: Habarileo.

TAMKO ZURI LAKINI LINALOSTAHILI UMAKINI KATIKA KULIAMINI.HAWA TCU WAKATI WANAZUNGUMZIA UCHAGUZI WA 2010,WANATAKA KUTUMBIA HAWAKUWEPO 2005?AU WATAPATA NGUVU HIYO 2010?JE KAMA SASA WANASHINDWA KUWASHUGHULIKIA HAO "MADAKTARI WA FALSAFA" WALIOKWAA SHAHADA ZAO MTANDAONI TUTAAMINI VIPI KUWA WATAWEZA HIYO 2010?
TATIZO LA NCHI YETU SIO SHERIA,KWANI ZIMEKUWEPO TANGU TUNAKABIDHIWA UHURU NA MKOLONI.TATIZO NI UTEKELEZAJI WA SHERIA HIZO.KUNA MBUNGE ALIKUWA NA TUHUMA ZA KUFOJI ELIMU (SIO YA CHUO KIKUU) BALI YA SEKONDARI.CHA AJABU HADI LEO "ANAPETA".JE HII HAILETI USHAWISHI KWA VIHIYO WENGINE KUJARIBU BAHATI ZAO?

TATIZO LA PILI LA NCHI YETU SIO SHERIA BALI UTEKELEZAJI WAKE UNAOELEMEA ZAIDI AINA YA MKOSAJI.YALEYALE YA ANAEIBA KUKU KWA NJAA KUITWA MWIZI LAKINI ANAYEFUJA MABILIONI ANAOTWA M-BADHIRIFU (NA SANASANA BADALA YA KWENDA JELA ATAHAMISHWA KITUO CHA KAZI).KUNA SHERIA KWA AJILI YA VIGOGO (KAMA AKINA CHEYO WANAOUA KWENYE AJALI LAKINI WANAUNDIWA TUME BADALA YA SHERIA KUCHUKUA MKONDO WAKE) NA SHERIA NYINGINE NI KWA AJILI YA MAKABWELA.


SAKATA la mgodi wa Kiwira kufikishwa bungeni, limeendelea kugubikwa na wingu zito, kutokana na ratiba za bunge kutoonyesha kama serikali itatoa ripoti.

Mgodi wa Kiwira, ambao unamuhusisha Rais wa Serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati, Daniel Yona umejaa utata kutokana na madai kuwa kampuni ya Tan Power Resources Limited iliununua kwa Sh70 milioni badala ya thamani yake halisi ya Sh4 bilioni.

Hadi sasa serikali haijatoa ufafanuzi wowote kuhusu utata huo licha ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuahidi katika mkutano wa 13 wa bunge kwamba,ingetoa taarifa bungeni.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alisema tu kwa kifupi "vuta subira".

Iwapo serikali haitatoa ripoti hiyo katika mkutano unaoendelea itakuwa ni mara ya tatu kupigwa tarehe suala hilo.

Katika mkutano wa 13, wakati mjadala wa mgodi wa Kiwira na Meremeta ukiwa umepamba moto, Pinda alisema serikali ilikuwa ikiandaa taarifa lakini akasema ni bora asulubiwe kuliko kutaja wamiliki wa Meremeta kwa maelezo kuwa inahusu usalama wa taifa.

Lakini, hadi mkutano huo unamalizika hakukuwa na ripoti yoyote ya serikali na hata ulivyokuja mkutano wa 14 hakukuwa na ripoti kama hiyo.

Tayari ratiba ya bunge imetoka na kuonyesha kwamba, hoja nzito inayotarajiwa kutikisa bunge hadi sasa ni ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambayo imepangwa kuwasilishwa bungeni Aprili

20 Apr 2009



Mie adhabu zangu HUKO O'level zilikuwa kwenye namba (HISABATI) ambayo kwa miujiza mikubwa nillibuka na D (japo ilikuwa dhaifu mno,na chupchup iwe F) na FIZIKIA ambayo sikuwa na ujanja nayo na nikaambulia F.

18 Apr 2009


Na Leon Bahati

SAKATA la Halmashauri ya Karatu, kugomea kulipia malazi ya Makamu wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein na ujumbe wake limechukuwa sura mpya, baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Celina Kombani kuunga mkono uamuzi wa halmashauri ni sahihi.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Kombani alisema halmashauri za wilaya haziwajibiki kuchangia ziara za mawaziri, rais au makamu wake, wanapotembelea katika maeneo yao.

Kombani alibainisha kuwa kama ingekuwa utaratibu huo upo, halmashauri nyingi zingefilisika hasa ambazo mawaziri wanatoka, kwa sababu wana utaratibu maalumu wa kutembelea zaidi ya mara tano kwenye maeneo yao, kwa mwaka.

"Kwa mfano kwa mwaka mimi hufanya ziara mara sita katika wilaya yangu ya Ulanga (Morogoro). Tukisema wanigharamie basi ingefilisika pamoja na halmashauri nyingine ambazo zina mawaziri," alisema Kombani ambaye ni Mbunge wa Ulanga Mashariki.

Akielezea kuhusu taratibu za matumizi ya fedha kwenye halmashauri, alisema kwa kawaida matumizi yote hupitishwa kwenye vikao vya madiwani.

Alibainisha kuwa gharama za msafara wa rais, makamu wa rais na mawaziri hugharamiwa na serikali kuu, kulingana na taratibu zilizowekwa.

"Ndiyo maana rais anapokuwa kwenye ziara huenda na vyakula vyake," alisema Kombani lakini akafahamisha kuwa halmashauri zinaweza kutenga fungu kwa ajili ya kuuandalia ugeni kwenye maeneo yao chakula cha jioni.

Iwapo halmashauri itaamua kufanya hivyo, alisema kuwa ni lazima fungu hilo liwe limepitishwa na halmashauri kupitia vikao vyake halali na si mkurugenzi na watendaji wake.

Alipoulizwa juu ya adhabu ya kiongozi wa halmashauri atakayetoa fedha pasipokufuata taratibu; alisema kila halmashauri ina taratibu zake za kuwajadili viongozi au maofisa waliokiuka taratibu na kuwachukulia hatua.

Suala la Halmashauri ya Karatu, kugomea kulipia malazi ya Makamu wa Rais pamoja na ujumbe wake liliripotiwa na gazeti la Mwananchi Jumatano iliyopita likionyesha kuwa Mkuu wa wilaya hiyo, Mathew Sedoyeka alimjia juu na kumtaka aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Majid Myao, aandike barua ya kujieleza kwanini alikataa kutoa fedha za kulipia ziara ya makamu wa rais wilayani humo.

Sedoyeka hakufurahishwa na kitendo cha halmashauri hiyo kugoma kulipa kiasi cha Sh2 milioni ambazo ni malipo ya kulala siku moja pamoja na chakula kwa ujumbe huo wa makamu wa rais, katika hoteli ya Bougain Villea ya mjini Karatu.

Kwenye barua ya kujieleza iliyoandikwa Machi 3, 2009 yenye kumbukumbu namba kdc/ded/cv.3/1/121, Myao amejitetea kuwa uamuzi wa kutolipiwa ziara hiyo, umetokana na kamati ya fedha ya madiwani kukataa kuidhinisha fedha hizo.

Alisema kutokana na kutoidhinishwa malipo hayo, aliona angekiuka Sheria namba tisa ya mwaka 1982 ambayo inahusu masuala ya matumizi ya fedha za halmashauri na maamuzi ya kamati ya fedha.

“Kama mimi ningetoa malipo hayo ni wazi ningekiuka sheria za serikali za mitaa hasa ikizingatiwa madiwani katika kikao chao halali ndio waligomea,” alieleza Myao.

Akizungumzia sakata hilo, Mbunge wa Jimbo la Karatu, Dk Willibrod Slaa alisema alichofanya ofisa huyo wa serikali ilikuwa halali kwa sababu walikuwa hawana bajeti ya malipo hayo.

Dk Slaa alitoa wito kwa serikali kutomuadhibu mtendaji yoyote wa halmashauri hiyo kutokana na uamuzi uliochukuliwa, ambao ulizingatia maadili ya kazi na utekelezaji wa utawala bora.
CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.